Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yohana 12
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yohana—Yaliyomo

      • Maria ammiminia Yesu mafuta miguuni (1-11)

      • Yesu aingia kwa kishindo (12-19)

      • Yesu atabiri kifo chake (20-37)

      • Ukosefu wa imani wa Wayahudi watimiza unabii (38-43)

      • Yesu alikuja kuuokoa ulimwengu (44-50)

Yohana 12:1

Marejeo

  • +Yoh 11:1, 43

Yohana 12:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wameketi mezani.”

Marejeo

  • +Lu 10:40

Yohana 12:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, ratili ya Kiroma, karibu gramu 327. Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Mt 26:6-10; Mk 14:3-6

Yohana 12:4

Marejeo

  • +Mt 26:47; Mk 14:10; Lu 22:48; Yoh 13:29; Mdo 1:16

Yohana 12:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza B14.

Yohana 12:7

Marejeo

  • +Mt 26:12; Mk 14:8; Yoh 19:40

Yohana 12:8

Marejeo

  • +Kum 15:11
  • +Mt 26:11; Mk 14:7

Yohana 12:9

Marejeo

  • +Yoh 11:43, 44

Yohana 12:11

Marejeo

  • +Yoh 7:31; 11:44, 45

Yohana 12:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Marejeo

  • +Zb 118:25, 26
  • +Mt 21:8, 9; Mk 11:8, 9; Yoh 1:49

Yohana 12:14

Marejeo

  • +Mt 21:7; Mk 11:7; Lu 19:35

Yohana 12:15

Marejeo

  • +1Fa 1:33, 34; Isa 62:11; Zek 9:9; Mt 21:5

Yohana 12:16

Marejeo

  • +Yoh 7:39
  • +Lu 24:45; Yoh 14:26

Yohana 12:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kwenye kaburi la ukumbusho.”

Marejeo

  • +Yoh 11:1, 43
  • +Mt 21:15; Lu 19:37

Yohana 12:19

Marejeo

  • +Yoh 11:48

Yohana 12:21

Marejeo

  • +Yoh 1:44

Yohana 12:23

Marejeo

  • +Yoh 13:31, 32; 17:1

Yohana 12:24

Marejeo

  • +Mt 16:21; Ro 14:9; 1Ko 15:36

Yohana 12:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “anayeipenda sana nafsi yake.”

  • *

    Au “anayeichukia nafsi yake.”

Marejeo

  • +Ufu 12:11
  • +Mt 16:25; Mk 8:35; Lu 9:24

Yohana 12:26

Marejeo

  • +Yoh 14:3; 17:24; 1Th 4:17

Yohana 12:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yangu inataabika.”

Marejeo

  • +Mt 26:38; Mk 14:34
  • +Lu 12:50; 22:41, 42; Ebr 5:7

Yohana 12:28

Marejeo

  • +Mt 3:17; 17:5; Mk 1:11; 9:7; Lu 3:22; 9:35; 2Pe 1:17
  • +Yoh 17:1

Yohana 12:31

Marejeo

  • +Yoh 14:30; 16:11; Mdo 26:17, 18; 2Ko 4:3, 4; Efe 2:1, 2; 1Yo 5:19
  • +Lu 10:18; Ufu 12:9

Yohana 12:32

Marejeo

  • +Yoh 8:28

Yohana 12:33

Marejeo

  • +Mdo 5:30

Yohana 12:34

Marejeo

  • +Zb 89:35, 36; 110:4; Isa 9:7
  • +Yoh 3:14

Yohana 12:35

Marejeo

  • +Yoh 11:10

Yohana 12:36

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “onyesheni imani.”

Marejeo

  • +Efe 5:8

Yohana 12:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

  • *

    Au “ujumbe wetu?”

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Marejeo

  • +Ro 10:16
  • +Isa 53:1

Yohana 12:40

Marejeo

  • +Isa 6:10; Mt 13:14; Mk 4:11, 12; Mdo 28:27

Yohana 12:41

Marejeo

  • +Isa 6:1, 8

Yohana 12:42

Marejeo

  • +Yoh 19:38
  • +Yoh 9:22; 16:2

Yohana 12:43

Marejeo

  • +Yoh 5:44

Yohana 12:44

Marejeo

  • +Mt 10:40; Mk 9:37

Yohana 12:45

Marejeo

  • +Yoh 14:9

Yohana 12:46

Marejeo

  • +Yoh 3:19; 8:12; 9:5
  • +Yoh 12:35

Yohana 12:47

Marejeo

  • +Yoh 3:16, 17

Yohana 12:49

Marejeo

  • +Yoh 8:38; 14:10

Yohana 12:50

Marejeo

  • +Yoh 6:40
  • +Yoh 3:34

Jumla

Yoh. 12:1Yoh 11:1, 43
Yoh. 12:2Lu 10:40
Yoh. 12:3Mt 26:6-10; Mk 14:3-6
Yoh. 12:4Mt 26:47; Mk 14:10; Lu 22:48; Yoh 13:29; Mdo 1:16
Yoh. 12:7Mt 26:12; Mk 14:8; Yoh 19:40
Yoh. 12:8Kum 15:11
Yoh. 12:8Mt 26:11; Mk 14:7
Yoh. 12:9Yoh 11:43, 44
Yoh. 12:11Yoh 7:31; 11:44, 45
Yoh. 12:13Zb 118:25, 26
Yoh. 12:13Mt 21:8, 9; Mk 11:8, 9; Yoh 1:49
Yoh. 12:14Mt 21:7; Mk 11:7; Lu 19:35
Yoh. 12:151Fa 1:33, 34; Isa 62:11; Zek 9:9; Mt 21:5
Yoh. 12:16Yoh 7:39
Yoh. 12:16Lu 24:45; Yoh 14:26
Yoh. 12:17Yoh 11:1, 43
Yoh. 12:17Mt 21:15; Lu 19:37
Yoh. 12:19Yoh 11:48
Yoh. 12:21Yoh 1:44
Yoh. 12:23Yoh 13:31, 32; 17:1
Yoh. 12:24Mt 16:21; Ro 14:9; 1Ko 15:36
Yoh. 12:25Ufu 12:11
Yoh. 12:25Mt 16:25; Mk 8:35; Lu 9:24
Yoh. 12:26Yoh 14:3; 17:24; 1Th 4:17
Yoh. 12:27Mt 26:38; Mk 14:34
Yoh. 12:27Lu 12:50; 22:41, 42; Ebr 5:7
Yoh. 12:28Mt 3:17; 17:5; Mk 1:11; 9:7; Lu 3:22; 9:35; 2Pe 1:17
Yoh. 12:28Yoh 17:1
Yoh. 12:31Yoh 14:30; 16:11; Mdo 26:17, 18; 2Ko 4:3, 4; Efe 2:1, 2; 1Yo 5:19
Yoh. 12:31Lu 10:18; Ufu 12:9
Yoh. 12:32Yoh 8:28
Yoh. 12:33Mdo 5:30
Yoh. 12:34Zb 89:35, 36; 110:4; Isa 9:7
Yoh. 12:34Yoh 3:14
Yoh. 12:35Yoh 11:10
Yoh. 12:36Efe 5:8
Yoh. 12:38Ro 10:16
Yoh. 12:38Isa 53:1
Yoh. 12:40Isa 6:10; Mt 13:14; Mk 4:11, 12; Mdo 28:27
Yoh. 12:41Isa 6:1, 8
Yoh. 12:42Yoh 19:38
Yoh. 12:42Yoh 9:22; 16:2
Yoh. 12:43Yoh 5:44
Yoh. 12:44Mt 10:40; Mk 9:37
Yoh. 12:45Yoh 14:9
Yoh. 12:46Yoh 3:19; 8:12; 9:5
Yoh. 12:46Yoh 12:35
Yoh. 12:47Yoh 3:16, 17
Yoh. 12:49Yoh 8:38; 14:10
Yoh. 12:50Yoh 6:40
Yoh. 12:50Yoh 3:34
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
  • 44
  • 45
  • 46
  • 47
  • 48
  • 49
  • 50
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yohana 12:1-50

Kulingana na Yohana

12 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu akafika Bethania, alikoishi Lazaro+ ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka kwa wafu. 2 Basi, wakamwandalia mlo wa jioni huko, na Martha alikuwa akiwahudumia,+ lakini Lazaro alikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wakila* pamoja na Yesu. 3 Kisha Maria akachukua ratili* moja ya mafuta yenye marashi, nardo halisi, ghali sana, akammiminia Yesu miguuni na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba ikajaa harufu ya mafuta yenye marashi.+ 4 Lakini Yuda Iskariote,+ mmoja wa wanafunzi wake aliyekuwa karibu kumsaliti akasema: 5 “Kwa nini mafuta haya yenye marashi hayangeuzwa kwa dinari* 300 na maskini wapewe pesa hizo?” 6 Hakusema hivyo kwa sababu aliwahangaikia maskini, bali kwa sababu alikuwa mwizi, naye ndiye aliyetunza sanduku la pesa na alikuwa akiiba pesa zilizowekwa humo. 7 Kisha Yesu akawaambia: “Mwacheni afanye hivyo kwa ajili ya matayarisho ya siku ya mazishi yangu.+ 8 Kwa maana maskini mnao sikuzote,+ lakini mimi hamtakuwa nami sikuzote.”+

9 Wakati huohuo, umati mkubwa wa Wayahudi ukajua kwamba alikuwa huko, nao ukaja, si kwa sababu ya Yesu tu, bali pia ili kumwona Lazaro aliyekuwa amefufuliwa kutoka kwa wafu.+ 10 Sasa wakuu wa makuhani wakapanga njama ili kumuua Lazaro pia, 11 kwa kuwa Wayahudi wengi walikuwa wakienda huko na kumwamini Yesu kwa sababu ya Lazaro.+

12 Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye sherehe, ukasikia kwamba Yesu alikuwa akija Yerusalemu. 13 Basi wakachukua matawi ya mitende na kutoka nje kwenda kumlaki, nao wakaanza kusema kwa sauti kubwa: “Tunaomba umwokoe! Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova,*+ Mfalme wa Israeli!”+ 14 Yesu alipompata mwanapunda, akaketi juu yake,+ kama ilivyoandikwa: 15 “Usiogope binti ya Sayuni. Tazama! Mfalme wako anakuja, akiwa ameketi juu ya mwanapunda.”+ 16 Mwanzoni, wanafunzi wake hawakuelewa mambo hayo, lakini Yesu alipotukuzwa,+ wakakumbuka kwamba mambo hayo yalikuwa yameandikwa kumhusu na kwamba walimtendea mambo hayo.+

17 Umati uliokuwa pamoja naye alipomwita Lazaro kutoka kaburini*+ na kumfufua kutoka kwa wafu ukaendelea kutoa ushahidi.+ 18 Kwa sababu hiyo pia, umati ukaenda kumlaki kwa sababu ulisikia alikuwa amefanya muujiza huo. 19 Basi Mafarisayo wakaambiana: “Mnaona, hamjafaulu hata kidogo. Tazama! Ulimwengu wote umemfuata.”+

20 Sasa kulikuwa na baadhi ya Wagiriki miongoni mwa wale waliokuja kuabudu kwenye sherehe. 21 Basi, wakamjia Filipo+ aliyetoka Bethsaida ya Galilaya, wakaanza kumwomba: “Bwana, tunataka kumwona Yesu.” 22 Filipo akaenda kumwambia Andrea, kisha wote wawili wakaja na kumwambia Yesu.

23 Lakini Yesu akawajibu: “Saa imefika ya Mwana wa binadamu kutukuzwa.+ 24 Kwa kweli ninawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka kwenye udongo na kufa, hubaki ikiwa mbegu moja tu; lakini ikifa,+ huzaa matunda mengi. 25 Yeyote anayeupenda sana uhai wake* huuangamiza, lakini yeyote anayeuchukia uhai wake*+ katika ulimwengu huu ataulinda kwa ajili ya uzima wa milele.+ 26 Ikiwa yeyote anataka kunihudumia, basi anifuate na mahali nilipo ndipo mhudumu wangu atakapokuwa pia.+ Ikiwa yeyote anataka kunihudumia, Baba atamheshimu. 27 Sasa ninataabika,*+ nami niseme nini? Baba, niokoe kutoka katika saa hii.+ Hata hivyo, ndiyo sababu nimekuja kwenye saa hii. 28 Baba, litukuze jina lako.” Ndipo sauti+ ikasikika kutoka mbinguni ikisema: “Nimelitukuza nami nitalitukuza tena.”+

29 Umati uliokuwa umesimama hapo ulisikia sauti hiyo ukaanza kusema kumekuwa na mngurumo. Nao wengine wakasema: “Malaika ameongea naye.” 30 Yesu akajibu: “Sauti hii imesikika, si kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu. 31 Sasa ulimwengu huu unahukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu+ huu atatupwa nje.+ 32 Na bado mimi, nikiinuliwa kutoka duniani,+ nitawavuta watu wa namna zote kwangu.” 33 Kwa kweli alisema hivyo ili kuonyesha ni kifo cha aina gani alikuwa karibu kufa.+ 34 Kisha umati ukamwambia: “Tulisikia kutoka katika Sheria kwamba Kristo hudumu milele.+ Kwa nini unasema kwamba lazima Mwana wa binadamu ainuliwe?+ Huyo Mwana wa binadamu ni nani?” 35 Basi Yesu akawaambia: “Nuru itakuwa miongoni mwenu kwa muda kidogo zaidi. Tembeeni wakati bado mna nuru, ili giza lisiwazidi nguvu; yeyote anayetembea katika giza hajui anakoenda.+ 36 Wakati mna nuru, iweni na imani* katika nuru ili muwe wana wa nuru.”+

Yesu alisema mambo hayo, kisha akaenda kujificha mbali nao. 37 Ingawa alikuwa amefanya ishara nyingi sana mbele yao, hawakuwa wakimwamini, 38 ili maneno haya aliyosema nabii Isaya yatimizwe: “Yehova,* ni nani ambaye ameamini jambo alilosikia kutoka kwetu?*+ Na mkono wa Yehova,* umefunuliwa kwa nani?”+ 39 Wao hawakuamini kwa sababu pia Isaya alisema: 40 “Ameyapofusha macho yao naye ameifanya mioyo yao iwe migumu, ili wasione kwa macho yao na kuelewa kwa mioyo yao na kugeuka nami niwaponye.”+ 41 Isaya alisema mambo haya kwa sababu aliona utukufu wake, naye alisema kumhusu.+ 42 Hata hivyo, watawala wengi kwa kweli walimwamini,+ lakini hawakumkiri kwa sababu waliwaogopa Mafarisayo, ili wasifukuzwe katika sinagogi;+ 43 kwa maana waliupenda utukufu wa wanadamu kuliko utukufu wa Mungu.+

44 Hata hivyo, Yesu akasema kwa sauti kubwa: “Yeyote anayeniamini, haniamini mimi tu bali pia Yule aliyenituma;+ 45 na yeyote anayeniona mimi anamwona pia Yule aliyenituma.+ 46 Nimekuja nikiwa nuru ulimwenguni,+ ili kila mtu anayeniamini asibaki gizani.+ 47 Lakini ikiwa yeyote anasikia maneno yangu na hayashiki, simhukumu; kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.+ 48 Yeyote anayenipuuza na hapokei maneno yangu, ana wa kumhukumu. Neno ambalo nimesema ndilo litakalomhukumu katika siku ya mwisho. 49 Kwa maana sijasema kwa uamuzi wangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma amenipa amri kuhusu jambo la kutangaza na la kusema.+ 50 Pia, ninajua kwamba amri yake inamaanisha uzima wa milele.+ Kwa hiyo, mambo ninayosema, ninasema kama Baba alivyoniambia.”+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki