Zaburi
Kwa kiongozi. Wa Daudi mtumishi wa Yehova, aliyemwambia Yehova maneno ya wimbo huu siku ambayo Yehova alimwokoa kutoka mikononi mwa maadui wake wote na kutoka mikononi mwa Sauli. Alisema:+
18 Ninakupenda, Ee Yehova, nguvu zangu.+
2 Yehova ni jabali langu na ngome yangu na Mwokozi wangu.+
Mungu wangu ni mwamba wangu,+ ninayemkimbilia,
Ngao yangu na pembe* yangu ya wokovu,* kimbilio langu salama.*+
3 Ninamlilia Yehova, anayestahili kusifiwa,
Nami nitaokolewa kutoka kwa maadui wangu.+
6 Katika taabu yangu nilimwita Yehova,
Niliendelea kumlilia Mungu wangu anisaidie.
Akiwa katika hekalu lake aliisikia sauti yangu,+
Na kilio changu cha kumwomba msaada kilifika masikioni mwake.+
7 Kisha dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika;+
Misingi ya milima ikasukasuka
Nayo ikatikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
8 Moshi ulipanda kutoka katika mianzi ya pua yake,
Na moto unaoteketeza kabisa ukatoka kinywani mwake;+
Makaa ya mawe yanayowaka moto mkali yakatoka kwake.
10 Alipanda juu ya kerubi, akaja akiruka.+
Akashuka chini kwa ghafla juu ya mabawa ya kiumbe wa roho.*+
12 Kutoka katika mwangaza ulio mbele zake
Mvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto yakapasua mawingu.
13 Kisha Yehova akaanza kunguruma mbinguni;+
Aliye Juu Zaidi aliifanya sauti yake isikike+
Kwa mvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto.
15 Sakafu za vijito zikaonekana;*+
Misingi ya nchi ikafunuliwa kwa kemeo lako, Ee Yehova,
Kwa mlipuko wa pumzi kutoka katika mianzi ya pua yako.+
16 Aliunyoosha mkono wake kutoka juu;
Alinishika na kunivuta kutoka katika maji yenye kina.+
17 Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+
Kutoka kwa wale wanaonichukia, waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.+
18 Walinikabili katika siku ya msiba wangu,+
Lakini Yehova alikuwa tegemeo langu.
20 Yehova hunithawabisha kulingana na uadilifu wangu;+
21 Kwa maana nimezishika njia za Yehova,
Nami sijamwacha kwa uovu Mungu wangu.
22 Hukumu zake zote ziko mbele yangu;
Sitazipuuza sheria zake.
25 Kwa mtu mshikamanifu unatenda kwa ushikamanifu;+
Kwa mtu asiye na lawama unatenda bila lawama;+
26 Kwa walio safi unajidhihirisha mwenyewe kuwa safi,+
Lakini kwa waliopotoka unajidhihirisha mwenyewe kuwa mwenye busara.+
28 Kwa maana ni wewe unayeiwasha taa yangu, Ee Yehova,
Mungu wangu ambaye hulifanya giza langu liangaze.+
29 Kwa msaada wako ninaweza kukabiliana na kundi la wavamizi;+
Kwa nguvu za Mungu ninaweza kuupanda ukuta.+
Yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia.+
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu ila Yehova?+
Na ni nani aliye mwamba isipokuwa Mungu wetu?+
33 Huifanya miguu yangu iwe kama ya paa;
Hunifanya nisimame mahali palipo juu.+
34 Huizoeza mikono yangu kupigana vita;
Mikono yangu inaweza kuukunja upinde wa shaba.
35 Wewe hunipa ngao yako ya wokovu,+
Mkono wako wa kuume hunitegemeza,*
Na unyenyekevu wako hunifanya niwe mkuu.+
37 Nitawafuatia maadui wangu na kuwapita;
Sitarudi mpaka watakapoangamizwa kabisa.
38 Nitawaponda wasiweze kuinuka;+
Wataanguka chini ya miguu yangu.
39 Utanipa nguvu kwa ajili ya vita;
Utawafanya maadui wangu waanguke chini yangu.+
41 Wanalilia msaada, lakini hakuna mtu wa kuwaokoa;
Hata wanamlilia Yehova, lakini yeye hawajibu.
42 Nitawaponda wawe laini kama mavumbi katika upepo;
Nitawatupa nje kama matope barabarani.
43 Utaniokoa kutoka kwa watu wanaotafuta makosa.+
Utaniweka kuwa kiongozi wa mataifa.+
Watu ambao siwajui watanitumikia.+
44 Watanitii watakaposikia fununu tu;
Wageni watakuja wakijikunyata mbele zangu.+
45 Wageni watakosa ujasiri;*
Watakuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
46 Yehova yuko hai! Mwamba wangu na asifiwe!+
Mungu wa wokovu wangu na akwezwe.+
47 Mungu wa kweli hunilipizia kisasi;+
Huyatiisha mataifa chini yangu.
48 Yeye huniokoa kutoka kwa maadui wangu wenye hasira;
Unaniinua juu ya wale wanaonishambulia;+
Unaniokoa kutoka kwa mtu mkatili.
49 Ndiyo sababu nitakutukuza wewe miongoni mwa mataifa, Ee Yehova,+