Mezali
5 Kila mutu mwenye kiburi katika moyo ni chukizo kwa Yehova.+
Ukuwe hakika kwamba* hatakosa kupewa azabu.
6 Kwa upendo mushikamanifu na uaminifu, kosa linafunikwa,+
Na kwa kumuogopa Yehova mutu anajiepusha na ubaya.+
10 Uamuzi wenye kuongozwa na roho* unapaswa kuwa kwenye midomo ya mufalme;+
Hapaswe hata kidogo kusaliti haki.+
11 Mizani* na vipimo vyenye kuwa sawa vinatoka kwa Yehova;
Majiwe yote ya kupimia yenye kuwa katika mufuko ni kazi yake.+
12 Matendo maovu yanachukiza wafalme,+
Kwa maana kiti cha ufalme kinafanywa kuwa imara kabisa kupitia haki.+
13 Maneno ya haki yanafurahisha wafalme.
Wanapenda mutu mwenye anasema kweli.+
15 Katika mwangaza wa uso wa mufalme kuko uzima;
Kukubaliwa naye ni kama wingu la mvua wakati wa kipindi cha mvua ya mwisho.+
16 Ni muzuri sana kupata hekima kuliko zahabu!+
Inafaa kuchagua uelewaji kuliko kuchagua feza.+
17 Barabara kubwa ya watu wanyoofu inaepuka mambo ya mubaya.
Kila mutu mwenye analinda njia yake analinda uzima wake.*+
19 Ni muzuri zaidi kuwa munyenyekevu* kati ya wapole+
Kuliko kupata sehemu ya vitu vyenye watu wenye majivuno walichukua katika vita.
20 Mutu mwenye anaonyesha ufahamu katika jambo atapata mafanikio,*
Na mwenye furaha ni ule mwenye anamutegemea Yehova.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa wenye kuwa nao,
Lakini wapumbavu wanapewa nizamu kwa upumbavu wao wenyewe.
25 Kuko njia yenye inaonekana kuwa sawa mbele ya macho ya mutu,
Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+
27 Mutu mwenye hana mafaa yoyote anachimbua mambo ya mubaya;+
Na maneno yake ni kama moto wenye kuunguza.+
29 Mutu mwenye jeuri anashawishi jirani yake
Na kumuongoza katika njia ya mubaya.
30 Anafinya jicho lake wakati anafanya mipango yenye kuumiza.
Anakaza midomo yake pamoja wakati anafanya jambo lenye kuumiza.