Zaburi
Sala ya Daudi.
2 Linda uzima wangu,* kwa maana niko mushikamanifu.+
Okoa mutumishi wako mwenye anakutegemea,
Kwa maana wewe ni Mungu wangu.+
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova, uko mwema+ na uko tayari kusamehe;+
Uko na upendo mwingi mushikamanifu kwa ajili ya wale wote wenye wanakuitia.+
6 Ee Yehova, sikiliza sala yangu;
Na usikilize vilio vyangu vya kuomba musaada.+
8 Hakuna mutu yeyote mwenye kuwa kama wewe kati ya miungu, Ee Yehova,+
Hakuna kazi zenye kuwa kama kazi zako.+
11 Unifundishe, Ee Yehova, kuhusu njia yako.+
Nitatembea katika kweli yako.+
Unganisha moyo wangu* ili niogope jina lako.+
12 Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote,+
Na nitatukuza jina lako milele,
13 Kwa maana upendo wako mushikamanifu ni mwingi kunielekea,
Na umeokoa uzima wangu* katika sehemu za chini kabisa za Kaburi.*+
14 Ee Mungu, watu wenye kimbelembele wanasimama ili kunishambulia;+
Kikundi cha wanaume wenye hawana huruma kinatafuta kuondoa uzima wangu,*
15 Lakini wewe, Ee Yehova, uko Mungu mwenye rehema na huruma,*
Haukasirike haraka na uko mwenye upendo mwingi mushikamanifu na uaminifu.*+
16 Geuka kunielekea na unionyeshe wema.+
Patia mutumishi wako nguvu zako,+
Na umuokoe mwana wa mutumwa wako mwanamuke.
17 Unionyeshe alama ya* wema wako,
Ili wale wenye kunichukia waione na kupatishwa haya.
Kwa maana wewe, Ee Yehova, uko musaidizi wangu na mufariji wangu.