Zaburi
Muziki wa Asafu.+
50 Mungu wa miungu, Yehova,+ amesema;
Anaita dunia
Kutoka mahali jua linatokea mupaka mahali linashukia.*
2 Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu anaangaza.
3 Mungu wetu atakuja na hawezi kubakia kimya.+
5 “Munikusanyie washikamanifu wangu,
Wale wenye kufanya agano pamoja na mimi kupitia zabihu.”+
6 Mbingu zinatangaza haki yake,
Kwa maana Mungu mwenyewe ni Muamuzi.+ (Sela)
7 “Munisikilize, Enyi watu wangu, na mimi nitasema;
Israeli, nitatoa ushahidi juu yako.+
Mimi ni Mungu, Mungu wako.+
8 Sikukaripie kwa sababu ya zabihu zako,
Wala kwa sababu ya matoleo yako mazima ya kuteketezwa yenye kuwa mbele yangu kila wakati.+
10 Kwa maana kila munyama wa pori ni wangu,+
Hata wanyama wenye kuwa juu ya milima elfu moja (1 000).
11 Ninajua kila ndege wa milima;+
Wanyama wa pori wenye hawana hesabu ni wangu.
12 Kama ningekuwa na njaa, singekuambia,
Kwa maana inchi yenye kuzaa na kila kitu chenye kuwa ndani ni changu.+
13 Je, nitakula nyama ya ngombe-dume
Na kunywa damu ya mbuzi?+
14 Toa shukrani zikiwa zabihu yako kwa Mungu,+
Na utimize naziri zako kwa Mwenye Kuwa Juu Zaidi;+
15 Uniitie wakati wa taabu.+
Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.”+
16 Lakini Mungu atamuambia muovu:
19 Unatumia kinywa chako kueneza mambo ya mubaya,
Na udanganyifu umeshikamana na ulimi wako.+
21 Wakati ulifanya mambo hayo, nilibakia kimya,
Kwa hiyo ukafikiri kwamba nitakuwa tu kama wewe.
Lakini sasa nitakukaripia,
Na nitakushitaki.+
22 Tafazali, mufikirie jambo hili, ninyi wenye kumusahau Mungu,+
Ili nisiwapasue vipande-vipande bila mutu wa kuwaokoa.