Mezali
28 Waovu wanakimbia hata kama hakuna mwenye anawafuatilia,
2 Wakati kuko kosa* katika inchi, inchi inakuwa na mukubwa mumoja kisha mwingine,+
Lakini kwa musaada wa mutu mwenye utambuzi na ujuzi, mukubwa* atadumu wakati murefu.+
3 Mutu maskini mwenye anapunja mutu wa hali ya chini+
Ni kama mvua yenye inaharibu chakula chote.
4 Wale wenye kuacha sheria wanasifu mutu muovu,
Lakini wale wenye kushika sheria wanawakasirikia.+
6 Maskini mwenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu wake ni muzuri zaidi
Kuliko tajiri mwenye njia zake zimepotoka.+
7 Mwana mwenye uelewaji anashika sheria,
Lakini rafiki ya walafi analetea baba yake haya.+
8 Mwenye anaongeza mali yake kwa faida+ na faida ya juu sana
Anaikusanyia ule mwenye anaonyesha maskini wema.+
9 Mwenye anakataa kusikiliza sheria
—Hata sala yake inachukiza.+
10 Mwenye anapoteza watu wanyoofu ili wafuate njia ya uovu ataanguka katika shimo lake mwenyewe,+
Lakini wenye hawana lawama watariti mambo ya muzuri.+
11 Tajiri anajiona mwenyewe kuwa mwenye hekima,+
Lakini mutu maskini mwenye utambuzi anaweza kumuchunguza kwa undani.+
12 Wakati wenye haki wanashinda, kunakuwa utukufu mwingi,
Lakini wakati waovu wanapata mamlaka, watu wanajificha.+
13 Mwenye anafunika makosa yake hatafanikiwa,+
Lakini kila mutu mwenye anayaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+
14 Mwenye furaha ni mutu mwenye kuwa muangalifu sikuzote,*
Lakini kila mutu mwenye anafanya moyo wake kuwa mugumu ataanguka katika musiba.+
15 Kama simba mwenye kunguruma na dubu mwenye kushambulia
Ni vile pia mutawala muovu mwenye anatawala juu ya watu wenye hawana uwezo.+
16 Kiongozi mwenye hana utambuzi anatumia mubaya mamlaka yake,+
Lakini mutu mwenye anachukia faida yenye haiko ya haki atarefusha maisha yake.+
17 Mutu mwenye kulemewa na hatia ya damu kwa sababu ya kuondoa uzima wa mutu* ataendelea kukimbia mupaka katika kaburi.*+
Mutu yeyote asimusaidie.
18 Mwenye anatembea bila kosa ataokolewa,+
Lakini ule mwenye njia zake zimepotoka ataanguka bila kutazamia.+
19 Mwenye analima udongo wake atakuwa na mikate mingi,
Lakini mwenye anafuatilia vitu vyenye havina mafaa yoyote atakuwa maskini sana.+
20 Mutu muaminifu atapata baraka nyingi,+
Lakini mwenye anaharakisha kupata utajiri hatakosa kuwa na hatia.+
21 Haiko muzuri kuonyesha upendeleo;+
Lakini mutu anaweza kukosea kwa sababu ya kipande cha mukate.
22 Mutu mwenye wivu* anajikaza sana kupata mali,
Lakini hajue kwamba umaskini utamupata.
23 Kila mutu mwenye anakaripia mwingine+ atafikia kukubaliwa zaidi+
Kuliko mutu mwenye anasifu-sifu kwa ulimi wake.
24 Kila mutu mwenye anaiba vitu vya baba yake na vya mama yake na kusema, “Haiko kosa,”+
Ni rafiki ya mutu mwenye analeta uharibifu.+
25 Mutu mwenye pupa anachochea* mugawanyiko,
Lakini kila mutu mwenye anamutegemea Yehova atapata mafanikio.*+
26 Kila mutu mwenye anategemea moyo wake mwenyewe ni mujinga,+
Lakini ule mwenye anatembea kwa hekima ataponyoka.+
27 Kila mutu mwenye anapatia maskini hatakosa kitu,+
Lakini ule mwenye anawafungia macho atapata laana nyingi.
28 Wakati waovu wanapata mamlaka, mutu anajificha,
Lakini wakati wanaangamia, wenye haki wanaongezeka.+