Zaburi
Ya Daudi.
103 Acha nimusifu* Yehova;
Acha kila kitu chenye kuwa ndani yangu kisifu jina lake takatifu.
3 Anasamehe makosa yako yote+
Na anaponyesha magonjwa yako yote;+
4 Anaokoa uzima wako kutoka katika shimo*+
Na anakuvalisha taji la upendo wake mushikamanifu na rehema.+
5 Anakushibisha kwa vitu vya muzuri+ maisha yako yote,
Na hivyo ujana wako unafanywa upya kama ule wa tai.+
11 Kwa maana kama vile mbingu ziko juu kuliko dunia,
Ni vile upendo wake mushikamanifu uko mwingi kuelekea wale wenye kumuogopa.+
12 Kama vile mahali jua linatokea kuko mbali sana na mahali jua linashukia,
Ni vile ametia zambi zetu mbali sana na sisi.+
13 Kama vile baba anaonyesha wana wake rehema,
Ni vile Yehova ameonyesha rehema wale wenye kumuogopa.+
15 Kuhusu mwanadamu mwenye anaweza kufa, siku zake ziko kama za majani;+
Anachanuka kama ua la shamba.+
16 Lakini wakati upepo unavuma, haliko tena,
Kama vile halijapata kuwa pale.*
17 Lakini upendo mushikamanifu wa Yehova ni wa umilele wote*
Kuelekea wale wenye kumuogopa,+
Na haki yake kuelekea watoto wa watoto wao,+
18 Kuelekea wale wenye kushika agano lake+
Na wale wenye kuwa waangalifu ili kushika maagizo yake.
19 Yehova amefanya kiti chake cha ufalme kikuwe imara kabisa mbinguni;+
Na ufalme wake unatawala juu ya kila kitu.+
22 Mumusifu Yehova, kazi zake zote,
Mahali pote penye anatawala.*
Nafsi yangu yote imusifu Yehova.