Zaburi
א [Aleph]
3 Hawatendi uovu wowote;
Wanatembea katika njia zake.+
4 Umeamuru
Kwamba maagizo yako yafuatwe kwa uangalifu.+
6 Ndipo sitaaibishwa+
Ninapokazia uangalifu amri zako zote.
7 Nitakusifu kwa moyo mnyoofu
Ninapojifunza hukumu zako za uadilifu.
8 Nitayashika masharti yako.
Kamwe usiniache kabisa.
ב [Beth]
9 Kijana anaweza kuisafishaje njia yake?
Kwa kujilinda kulingana na neno lako.+
10 Ninakutafuta kwa moyo wangu wote.
Usiache nikengeuke kutoka katika amri zako.+
12 Na usifiwe, Ee Yehova;
Nifundishe masharti yako.
13 Kwa midomo yangu ninatangaza
Hukumu zote ulizonena.
16 Ninazipenda sana sheria zako.
Sitalisahau neno lako.+
ג [Gimel]
17 Nitendee kwa fadhili mimi mtumishi wako,
Ili niishi na kulishika neno lako.+
18 Yafumbue macho yangu ili nione wazi
Mambo yanayostaajabisha katika sheria yako.
19 Mimi ni mgeni tu nchini.+
Usinifiche amri zako.
20 Ninapondeka* kwa kutamani sana
Hukumu zako nyakati zote.
21 Unawakemea wenye kimbelembele,
Watu waliolaaniwa wanaokengeuka kutoka katika amri zako.+
22 Niondolee* dhihaka na dharau,
Kwa maana nimeshika vikumbusho vyako.
23 Hata wakuu wanapoketi pamoja na kusema mambo mabaya kunihusu,
Mimi mtumishi wako ninatafakari* masharti yako.
ד [Daleth]
25 Ninalala kifudifudi mavumbini.+
Nihifadhi hai kulingana na neno lako.+
26 Nilikwambia kuhusu njia zangu, nawe ukanijibu;
Nifundishe masharti yako.+
28 Nimekosa usingizi kwa sababu ya huzuni.
Nitie nguvu kulingana na neno lako.
29 Niondolee njia ya udanganyifu,+
Na unionyeshe kibali kwa kunipa sheria yako.
30 Nimechagua njia ya uaminifu.+
Ninatambua kwamba hukumu zako zinafaa.
31 Ninashikamana na vikumbusho vyako.+
Ee Yehova, usiache nikatishwe tamaa.*+
32 Nitaifuata kwa bidii* njia ya amri zako
Kwa sababu wewe huufanya moyo wangu uwe na nafasi kwa ajili yake.*
ה [He]
34 Nipe uelewaji,
Ili niweze kushika sheria yako
Na kuitii kwa moyo wangu wote.
37 Yageuzie mbali macho yangu yasitazame mambo yasiyofaa;+
Nihifadhi hai katika njia yako.
39 Niondolee aibu ninayoogopa sana,
Kwa maana hukumu zako ni njema.+
40 Tazama jinsi ninavyoyatamani sana maagizo yako!
Nihifadhi hai katika uadilifu wako.
ו [Waw]
41 Acha nijionee upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova,+
Wokovu wako kulingana na ahadi yako;*+
42 Kisha nitamjibu yule anayenidhihaki,
Kwa maana ninalitumaini neno lako.
43 Usiondoe kabisa neno la kweli kutoka kinywani mwangu,
Kwa maana nimetumaini* hukumu yako.
44 Nitaishika sheria yako daima,
Milele na milele.+
46 Nitaongea kuhusu vikumbusho vyako mbele ya wafalme,
Nami sitaaibika.+
47 Ninazipenda sana amri zako,
Naam, ninazipenda.+
48 Nitainua mikono yangu kuelekea amri zako, ambazo ninazipenda,+
ז [Zayin]
50 Hilo ndilo faraja yangu katika mateso yangu,+
Kwa maana neno lako limenihifadhi hai.
51 Wenye kimbelembele wananidhihaki sana,
Lakini sikengeuki kutoka kwenye sheria yako.+
53 Nimeshikwa na hasira kali kwa sababu ya waovu,
Wanaoiacha sheria yako.+
54 Masharti yako ni nyimbo kwangu
Popote ninapoishi.*
55 Wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, Ee Yehova,+
Ili niweze kuishika sheria yako.
56 Nimezoea kufanya hivyo
Kwa sababu nimeyatii maagizo yako.
ח [Heth]
59 Nimezichunguza njia zangu,
Ili niirudishe miguu yangu kwenye vikumbusho vyako.+
60 Ninafanya haraka wala sikawii
Kuzishika amri zako.+
61 Kamba za waovu zinanizunguka,
Lakini siisahau sheria yako.+
62 Katikati ya usiku ninaamka ili kukushukuru+
Kwa sababu ya hukumu zako za uadilifu.
63 Mimi ni rafiki ya wote wanaokuogopa wewe
Na ya wale wanaoyatii maagizo yako.+
64 Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova, umeijaza dunia;+
Nifundishe masharti yako.
ט [Teth]
65 Umenitendea mema mimi mtumishi wako,
Ee Yehova, kulingana na neno lako.
66 Nifundishe busara na ujuzi,+
Kwa maana nimezitumaini amri zako.
68 Wewe ni mwema+ na kazi zako ni njema.
Nifundishe masharti yako.+
69 Wenye kimbelembele hunipaka uwongo,
Lakini ninayatii maagizo yako kwa moyo wangu wote.
71 Ni vema kwamba nimeteswa,+
Ili nijifunze masharti yako.
י [Yod]
73 Mikono yako iliniumba na kunifinyanga.
Nipe uelewaji,
Ili nijifunze amri zako.+
76 Tafadhali, upendo wako mshikamanifu+ na unifariji,
Kulingana na ahadi yako uliyonipa* mimi mtumishi wako.
78 Wenye kimbelembele na waaibishwe,
Kwa maana wananikosea bila sababu.*
Lakini nitayatafakari* maagizo yako.+
79 Acha wale wanaokuogopa warudi kwangu,
Wale wanaojua vikumbusho vyako.
כ [Kaph]
83 Kwa maana mimi ni kama kiriba cha ngozi kilichokaushwa na moshi,
Lakini siyasahau masharti yako.+
84 Mimi mtumishi wako nisubiri kwa siku ngapi?
Ni lini utakapowahukumu wale wanaonitesa?+
85 Wenye kimbelembele wananichimbia mashimo,
Wale wanaoasi sheria yako.
86 Amri zako zote zinategemeka.
Watu wananitesa bila sababu; nisaidie!+
87 Karibu waniangamize kutoka duniani,
Lakini sikuyaacha maagizo yako.
88 Nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu,
Ili nishike vikumbusho ulivyosema.
ל [Lamed]
89 Milele, Ee Yehova,
Neno lako litadumu mbinguni.+
90 Uaminifu wako umekuwepo kwa vizazi vyote.+
Umeiimarisha kabisa dunia, ili idumu.+
91 Kwa sababu ya hukumu zako zinadumu* mpaka leo,
Kwa maana zote ni watumishi wako.
92 Kama singeipenda sana sheria yako,
Ningekuwa nimeangamia katika mateso yangu.+
93 Sitayasahau kamwe maagizo yako,
Kwa sababu kupitia hayo umenihifadhi hai.+
95 Waovu wanasubiri kuniangamiza,
Lakini ninavikazia sana fikira vikumbusho vyako.
96 Nimeona mwisho wa ukamilifu wote,
Lakini amri yako haina mpaka.*
מ [Mem]
97 Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako!+
98 Amri yako hunifanya niwe na hekima kuliko maadui wangu,+
Kwa sababu ninayo milele.
100 Ninatenda kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,
Kwa sababu ninayatii maagizo yako.
101 Ninakataa kutembea kwenye njia yoyote ya uovu,+
Ili nishike neno lako.
102 Sigeuki kando kutoka katika hukumu zako,
Kwa maana umenifundisha.
103 Jinsi maneno yako yalivyo matamu kwenye kaakaa langu,
Kuliko asali kinywani mwangu!+
104 Kwa sababu ya maagizo yako ninatenda kwa uelewaji.+
Ndiyo sababu ninaichukia kila njia ya uwongo.+
נ [Nun]
105 Neno lako ni taa ya mguu wangu,
Na nuru ya njia yangu.+
106 Nimeweka kiapo, nami nitakitimiza,
Kwamba nitazishika hukumu zako za uadilifu.
107 Nimeteseka sana.+
Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na neno lako.+
108 Tafadhali yafurahie matoleo yangu ya hiari ya kukusifu,*+ Ee Yehova,
Na unifundishe hukumu zako.+
110 Waovu wamenitegea mtego,
Lakini sijakengeuka kutoka katika maagizo yako.+
111 Ninavichukua vikumbusho vyako kuwa mali yangu ya kudumu,*
Kwa maana hivyo ni shangwe ya moyo wangu.+
112 Nimeazimia* kuyatii masharti yako
Nyakati zote, mpaka mwisho.
ס [Samekh]
115 Kaeni mbali nami, enyi waovu,+
Ili nizishike amri za Mungu wangu.
118 Unawakataa wote wanaokengeuka kutoka katika masharti yako,+
Kwa maana ni waongo na wadanganyifu.
119 Unawatupilia mbali waovu wote walio duniani kana kwamba ni takataka.*+
Ndiyo sababu ninavipenda vikumbusho vyako.
120 Mwili wangu unatetemeka kwa sababu ya kukuhofu;
Ninaogopa hukumu zako.
ע [Ayin]
121 Nimetenda yaliyo ya haki na uadilifu.
Usiniache mikononi mwa wale wanaonikandamiza!
122 Nihakikishie hali njema mimi mtumishi wako;
Wenye kimbelembele wasinikandamize.
125 Mimi ni mtumishi wako; nipe uelewaji,+
Ili nijue vikumbusho vyako.
126 Wakati umefika wa Yehova kutenda,+
Kwa maana wameivunja sheria yako.
128 Kwa hiyo, ninayaona mafundisho* yote yanayotoka kwako kuwa yanafaa;+
Ninaichukia kila njia ya uwongo.+
פ [Pe]
129 Vikumbusho vyako ni vizuri sana.
Ndiyo sababu ninavishika.
134 Niokoe* kutoka kwa wanadamu wanaokandamiza,
Nami nitayatii maagizo yako.
136 Macho yangu yanatiririkwa na machozi
Kwa sababu watu hawatii sheria yako.+
צ [Tsade]
138 Vikumbusho unavyotoa ni vya uadilifu
Navyo vinategemeka kabisa.
139 Bidii yangu inanila,+
Kwa sababu maadui wangu wameyasahau maneno yako.
141 Mimi ni duni na mwenye kudharauliwa;+
Hata hivyo, sijayasahau maagizo yako.
143 Hata nikipatwa na taabu na shida,
Nitaendelea kuzipenda sana amri zako.
144 Uadilifu wa vikumbusho vyako ni wa milele.
Nipe uelewaji,+ ili niendelee kuishi.
ק [Qoph]
145 Ninakuita kwa moyo wangu wote. Nijibu, Ee Yehova.
Nitayashika masharti yako.
146 Ninakulilia wewe; niokoe!
Nitashika vikumbusho vyako.
149 Isikie sauti yangu kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+
Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na haki yako.
150 Watu wenye mwenendo wa aibu* hunikaribia;
Wako mbali sana na sheria yako.
152 Zamani za kale nilijifunza kuhusu vikumbusho vyako,
Ambavyo umeviweka vidumu milele.+
ר [Resh]
153 Yatazame mateso yangu na uniokoe,+
Kwa maana sijaisahau sheria yako.
155 Wokovu uko mbali sana na waovu,
Kwa maana hawajayatafuta masharti yako.+
156 Rehema zako ni nyingi, Ee Yehova.+
Nihifadhi hai kulingana na haki yako.
157 Wanaonitesa na pia maadui wangu ni wengi;+
Lakini sijakengeuka kutoka katika vikumbusho vyako.
158 Ninawatazama wenye hila kwa chuki kali,
Kwa sababu hawalishiki neno lako.+
159 Tazama jinsi ninavyoyapenda sana maagizo yako!
Ee Yehova, nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+
160 Kiini hasa cha neno lako ni kweli,+
Na hukumu zako zote za uadilifu zinadumu milele.
ש [Sin] au [Shin]
162 Ninashangilia kwa sababu ya neno lako+
Kama mtu anayepata nyara nyingi.
164 Mara saba kwa siku ninakusifu wewe
Kwa sababu ya hukumu zako za uadilifu.
166 Ninayatazamia matendo yako ya wokovu, Ee Yehova,
Nami ninazishika amri zako.
167 Ninavishika vikumbusho vyako,
Nami navipenda sana.+
168 Ninayatii maagizo yako na vikumbusho vyako,
Kwa maana unajua mambo yote ninayotenda.+
ת [Taw]
169 Kilio changu cha kuomba msaada na kikufikie wewe, Ee Yehova.+
Nifanye nielewe, kulingana na neno lako.+
170 Ombi langu la kutaka kibali na lifike mbele zako.
Niokoe, kama ulivyoahidi.*
171 Midomo yangu na ifurikwe na sifa,+
Kwa maana wewe hunifundisha masharti yako.
172 Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako,+
Kwa maana amri zako zote ni za uadilifu.
174 Ninautamani sana wokovu wako, Ee Yehova,
Nami ninaipenda sana sheria yako.+
175 Acha niishi ili nikusifu;+
Hukumu zako na ziwe msaada wangu.