Isaya
14 Kwa maana Yehova atamuonyesha Yakobo rehema,+ na atachagua tena Israeli.+ Atawafanya wakae* katika inchi yao,+ na wakaaji wageni watajiunga nao na watashikamana na nyumba ya Yakobo.+ 2 Na vikundi vya watu vitawakamata na kuwaleta mahali pao wenyewe, na nyumba ya Israeli itawariti kuwa watumishi wanaume na watumishi wanamuke+ katika inchi ya Yehova; na watakamata mateka wale wenye walikuwa wanawashika wakiwa wametekwa, na watatiisha wale wenye walikuwa wanawalazimisha kufanya kazi.*
3 Siku yenye Yehova atakupatia pumuziko kutokana na maumivu yako na kutokana na musukosuko wako na kutokana na utumwa mugumu wenye ulilazimishwa kufanya,+ 4 utarudilia-rudilia mezali hii* juu ya mufalme wa Babiloni:
“Namna ule mwenye alilazimisha wengine kufanya kazi* amefikia mwisho wake!
Namna ukandamizaji umeisha!+
5 Yehova amevunja fimbo ya waovu,
Fimbo ya watawala,+
6 Ule mwenye kupiga vikundi vya watu kwa hasira, mapigo yenye kuendelea,+
Ule mwenye kutiisha mataifa kwa kasirani, kwa mateso bila kuacha.+
7 Dunia yote imepumuzika sasa, haina usumbufu.
Watu wanatoa sauti za furaha.+
8 Hata miti ya miberoshi inafurahi sana kwa sababu yako,
Pamoja na miti ya mierezi ya Lebanoni.
Inasema, ‘Tangu wakati ulianguka,
Hakuna mukataji wa miti mwenye anapanda ili kutukata.’
Kwa sababu yako, linaamusha wale wenye hawana uwezo katika kifo,
Viongozi wote wa dunia* wenye kukandamiza watu.
Linafanya wafalme wote wa mataifa wasimame kutoka kwenye viti vyao vya ufalme.
10 Wote wanaanza kusema na kukuambia,
‘Je, wewe pia umekuwa muzaifu kama sisi?
Je, umekuwa kama sisi?
Funza* wametandikwa chini yako kama kitanda,
Na umefunikwa na minyoo.’
Namna umekatwa ukaangushwa katika dunia,
Wewe mwenye ulishinda mataifa!+
13 Ulisema katika moyo wako, ‘Nitapanda juu mbinguni.+
Nitainua kiti changu cha ufalme juu ya nyota za Mungu,+
Na nitakaa juu ya mulima wa mukutano,
Katika sehemu za mbali zaidi za kaskazini.+
14 Nitaenda juu ya sehemu za juu za mawingu;
Nitajifananisha na Mwenye Kuwa Juu Zaidi.’
16 Wale wenye kukuona watakuangalia sana;
Watakuchunguza kwa uangalifu, na kusema,
‘Je, huyu ndiye ule mutu mwenye alikuwa anatikisa dunia,
Mwenye alitetemesha falme,+
17 Mwenye alifanya dunia yenye kuikaliwa na watu ikuwe kama jangwa
Na kupindua miji yake,+
Mwenye alikataa kuruhusu wafungwa wake waende kwao?’+
18 Wafalme wengine wote wa mataifa,
Ndiyo, wote, wamelala katika utukufu,
Kila mumoja katika kaburi lake* mwenyewe.
19 Lakini wewe, umetupwa pasipo kaburi,
Kama chipukizi* lenye kuchukiwa sana,
Ukiwa umevalishwa watu wenye waliuawa kwa kutobolewa kwa upanga,
Wenye wanashuka kwenye majiwe ya shimo,
Kama muzoga wenye unakanyangiwa chini kwa miguu.
Uzao wa watenda maovu hautatajwa tena.
21 Mutayarishe ubao wa kuchinjia wana wake
Kwa sababu ya hatia ya mababu zao,
Ili wasisimame na kutawala dunia
Na kujaza miji yao katika inchi.”
22 “Nitasimama ili kupigana nao,”+ ni vile Yehova wa majeshi anasema.
“Na nitafuta katika Babiloni jina na mabaki na wazao na watoto,”+ ni vile Yehova anasema.
23 “Na nitafanya muji huo kuwa makao ya nungunungu na eneo la tingitingi, na nitaufagia kwa ufagio wa uharibifu,”+ ni vile Yehova wa majeshi anasema.
24 Yehova wa majeshi ameapa:
“Kama vile nimekusudia, ni vile itatendeka,
Na kama vile nimeamua, ni vile itatimia.
Nira yake itaondolewa juu yao,
Na muzigo wake utaondolewa juu ya bega lao.”+
26 Hili ndilo jambo lenye limeamuliwa* juu ya dunia yote,
Na huu ndio mukono wenye umenyooshwa* juu ya mataifa yote.
Mukono wake umenyooshwa,
Na ni nani anaweza kuurudisha nyuma?+
28 Katika mwaka wenye Mufalme Ahazi alikufa,+ tangazo hili lilitolewa:
29 “Usishangilie, Ufilisti, mutu yeyote kati yenu,
Kwa sababu tu fimbo ya ule mwenye kuwapiga imevunjwa.
Kwa maana kwenye muzizi wa nyoka+ kutatoka nyoka mwenye sumu,+
Na uzao wake utakuwa nyoka wa moto mwenye kuruka.*
30 Wakati wazaliwa wa kwanza wa watu wa hali ya chini watakuwa wanakula,
Na wakati maskini watakuwa wanalala katika usalama,
Nitaua muzizi wako kwa njaa kali,
Na kile kitabakia kwako kitauawa.+
31 Omboleza, Ee mulango mukubwa! Lia kwa sauti kubwa, Ee muji!
Ninyi wote mutavunjika moyo, Ee Ufilisti!
Kwa maana moshi unakuja kutoka kaskazini,
Na katika vikundi vyake vya maaskari hakuna wenye kutawanyika.”
32 Namna gani watajibu wajumbe wa taifa lile?
Kwamba Yehova ameweka musingi wa Sayuni,+
Na kwamba watu wa hali ya chini kati ya watu wake watakimbilia ndani yake.