Mezali
21 Moyo wa mufalme ni kama mito midogo ya maji katika mukono wa Yehova.+
Anauongoza mahali popote kwenye anapenda.+
2 Njia zote za mwanadamu zinaonekana kuwa sawa mbele ya macho yake,+
3 Kufanya mambo yenye kuwa sawa na ya haki
Kunamupendeza Yehova zaidi kuliko zabihu.+
4 Macho yenye kiburi na moyo wenye majivuno
—Taa yenye inaongoza waovu ni zambi.+
5 Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio,*+
Lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.+
6 Kupata hazina kupitia ulimi wenye kusema uongo
7 Jeuri ya waovu itawaharibu,+
Kwa maana wanakataa kutenda haki.
8 Njia ya mutu mwenye hatia ni yenye kujikunja-kunja,
Lakini matendo ya mutu safi ni yenye kunyooka.+
9 Ni muzuri zaidi kuishi kwenye pembe ya sehemu ya juu ya nyumba
11 Wakati mwenye zihaka anapewa azabu, mwenye hana uzoefu anakuwa na hekima zaidi,
Na wakati mutu mwenye hekima anapata ufahamu, anapata ujuzi.*+
12 Mwenye Haki anachunguza nyumba ya muovu;
Anapindua waovu na kuwaharibu.+
13 Kila mutu mwenye anafunga sikio lake ili asisikie kilio cha mutu wa hali ya chini
Yeye mwenyewe ataita naye hatajibiwa.+
14 Zawadi yenye kutolewa kwa uficho inatuliza hasira,+
15 Mwenye haki anafurahia kutenda kwa haki,+
Lakini ni jambo la mubaya sana kwa wale wenye kutenda uovu.
16 Mutu mwenye anakengeuka na kuacha njia ya ufahamu
Atapumuzika katika kikundi cha wale wenye hawana uwezo katika kifo.+
18 Muovu ni bei ya ukombozi kwa ajili ya mwenye haki,
Na mudanganyifu atakamatwa pa nafasi ya watu wanyoofu.+
19 Ni muzuri zaidi kuishi katika jangwa
Kuliko kuishi na bibi mugomvi* na mwenye kukasirika-kasirika.+
20 Hazina yenye samani na mafuta vinapatikana katika nyumba ya mwenye hekima,+
Lakini mutu mujinga atatumia mubaya* vitu vyenye iko* navyo.+
22 Mutu mwenye hekima anaweza kupanda katika* muji wa watu wenye nguvu
Na kupunguza nguvu zenye wanategemea.+
24 Mutu mwenye kimbelembele, mwenye kujisifu-sifu, ni vile unamuita
Mutu mwenye kutenda kwa kimbelembele bila kujali.+
25 Kile mutu muvivu anatamani sana kitamuua,
Kwa maana mikono yake inakataa kufanya kazi.+
26 Anatamani sana kwa pupa muchana wote,
Lakini mwenye haki anatoa, haime wengine kitu.+
27 Zabihu ya muovu inachukiza.+
Namna gani wakati anaitoa na nia yenye uovu!*
28 Shahidi mwenye kusema uongo ataangamia,+
Lakini mutu mwenye anasikiliza atatoa ushuhuda kwa mafanikio.*
30 Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumupinga Yehova.+