Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
6 Wakati huo Sulemani akasema: “Yehova alisema kwamba atakaa katika giza nzito.+ 2 Sasa nimekujengea nyumba yenye kuinuliwa, mahali kwenye kulifanywa imara ili ukae ndani milele.”+
3 Kisha mufalme akageuka na akaanza kubariki kutaniko lote la Israeli wakati kutaniko lote la Israeli lilikuwa limesimama.+ 4 Akasema: “Yehova Mungu wa Israeli asifiwe, yeye mwenye kwa kinywa chake mwenyewe alimuahidi baba yangu Daudi na kwa mikono yake mwenyewe ametimiza, kwa kusema, 5 ‘Kuanzia siku yenye nilitosha watu wangu katika inchi ya Misri, sikuchagua muji katika makabila yote ya Israeli ili kujenga ndani nyumba kusudi jina langu likae ndani,+ na sikuchagua mwanaume akuwe kiongozi juu ya watu wangu Israeli. 6 Lakini nimechagua Yerusalemu+ ili jina langu likae ndani, na nimemuchagua Daudi akuwe juu ya watu wangu Israeli.’+ 7 Na ilikuwa tamaa ya moyo wa baba yangu Daudi kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli.+ 8 Lakini Yehova akamuambia baba yangu Daudi, ‘Ilikuwa tamaa ya moyo wako kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu, na ulifanya muzuri kutamani jambo hilo katika moyo wako. 9 Hata hivyo, hautajenga nyumba hiyo, lakini mwana wako mwenye utazaa* ndiye atajenga nyumba hiyo kwa ajili ya jina langu.’+ 10 Yehova ametimiza ahadi yenye alitoa, kwa maana nimechukua nafasi ya baba yangu Daudi na ninakaa kwenye kiti cha ufalme cha Israeli,+ kama vile Yehova aliahidi.+ Nimejenga pia nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli, 11 na nimeweka mule lile Sanduku lenye ndani yake muko agano+ lenye Yehova alifanya pamoja na watu wa Israeli.”
12 Kisha akasimama mbele ya mazabahu ya Yehova mbele ya kutaniko lote la Israeli, na akanyoosha mikono yake.+ 13 (Kwa maana Sulemani alikuwa amejenga jukwaa la shaba na kuliweka katikati ya kiwanja.+ Lilikuwa na urefu wa mikono* tano [5], upana wa mikono tano, na urefu kuenda juu wa mikono tatu [3]; na akasimama juu yake.) Na akapiga magoti mbele ya kutaniko lote la Israeli na akanyoosha mikono yake kuelekea mbinguni,+ 14 na akasema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe mbinguni ao duniani, mwenye anashika agano na kuonyesha upendo mushikamanifu kwa watumishi wako wenye wanatembea mbele yako kwa moyo wao wote.+ 15 Umetimiza ahadi yenye ulimutolea mutumishi wako Daudi baba yangu.+ Ulitoa ahadi hiyo kwa kinywa chako mwenyewe, na siku hii umeitimiza kwa mukono wako mwenyewe.+ 16 Na sasa, Ee Yehova Mungu wa Israeli, timiza ahadi yenye ulimutolea mutumishi wako Daudi baba yangu wakati ulisema: ‘Hakutakosa hata kidogo mwanaume wa uzao wako mbele yangu ili kukaa kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wana wako wanakuwa waangalifu kuhusu njia yao kwa kutembea katika sheria yangu,+ kama vile umetembea mbele yangu.’+ 17 Na sasa, Ee Yehova Mungu wa Israeli, acha ahadi yenye ulimutolea mutumishi wako Daudi ikuwe yenye kutegemeka.
18 “Lakini je, kweli Mungu atakaa pamoja na wanadamu katika dunia?+ Angalia! Mbingu, ndiyo, mbingu za mbingu, haziwezi kukuenea;+ namna gani basi nyumba hii yenye nimejenga!+ 19 Sasa kaza uangalifu kwenye sala ya mutumishi wako na ombi lake la kuomba rehema, Ee Yehova Mungu wangu, na usikilize kilio cha kuomba musaada na sala yenye mutumishi wako anasali mbele yako. 20 Macho yako yafunguliwe kuelekea nyumba hii muchana na usiku, kuelekea mahali kwenye ulisema kwamba utaweka jina lako,+ ili kusikiliza sala yenye mutumishi wako anasali kuelekea mahali hapa. 21 Na usikilize maombi ya mutumishi wako ya kuomba musaada na maombi ya watu wako Israeli wakati wanasali kuelekea mahali hapa,+ na usikie ukiwa katika makao yako, kutoka mbinguni;+ ndiyo, usikie na usamehe.+
22 “Kama mwanadamu anamutendea mwanadamu mwenzake zambi na anaapishwa* na anakubali kubeba matokeo ya kiapo hicho,* na wakati iko* chini ya kiapo* anakuja mbele ya mazabahu yako katika nyumba hii,+ 23 basi usikie kutoka mbinguni na utende na uhukumu watumishi wako kwa kulipa muovu na kuleta mambo yenye alifanya juu ya kichwa chake mwenyewe+ na kwa kumutangaza mwenye haki kuwa hana kosa* na kwa kumupatia zawabu kulingana na haki yake.+
24 “Na kama watu wako Israeli wanashindwa mbele ya adui kwa sababu waliendelea kukutendea zambi,+ na wanarudia na wanatukuza jina lako+ na kusali+ na kukuomba ili wapate kukubaliwa mbele yako katika nyumba hii,+ 25 basi usikie kutoka mbinguni+ na usamehe zambi ya watu wako Israeli na uwarudishe katika inchi yenye uliwapatia wao na mababu zao.+
26 “Wakati mbingu zinafungwa na hakuna mvua+ kwa sababu waliendelea kukutendea zambi,+ na wanasali kuelekea mahali hapa na wanatukuza jina lako na wanageuka na kuacha zambi yao kwa sababu uliwanyenyekeza,*+ 27 basi usikie kutoka mbinguni na usamehe zambi ya watumishi wako, ya watu wako Israeli, kwa maana utawafundisha juu ya njia ya muzuri yenye wanapaswa kutembea ndani;+ na ulete mvua+ juu ya inchi yako yenye ulipatia watu wako kuwa uriti.
28 “Kama njaa inatokea katika inchi,+ ao ugonjwa wa kuambukiza,+ ugonjwa wenye kukausha mimea, kuvu,+ nzige wenye kupatikana kwa wingi, ao nzige wenye kula sana*+ ao kama maadui wao wanawazunguka kwa ajili ya vita katika muji wowote wa inchi*+ ao kama kunatokea aina ingine yoyote ya pigo ao ya ugonjwa,+ 29 sala yoyote,+ ombi lolote la kuomba rehema+ lenye linaweza kutolewa na mutu yeyote ao na watu wako wote Israeli (kwa maana kila mumoja anajua pigo lake mwenyewe na maumivu yake mwenyewe)+ wakati wananyoosha mikono yao kuelekea nyumba hii,+ 30 basi usikie kutoka mbinguni, makao yako,+ na usamehe;+ na upatie zawabu kila mumoja kulingana na njia zake zote, kwa maana unajua moyo wake (wewe peke yako unajua kwa kweli moyo wa mwanadamu),+ 31 ili wakuogope kwa kutembea katika njia zako sikuzote zenye wanaishi katika inchi yenye ulipatia mababu zetu.
32 “Pia kuhusu mugeni mwenye haiko sehemu ya watu wako Israeli na mwenye anakuja kutoka inchi ya mbali kwa sababu ya jina lako* kubwa+ na mukono wako wenye nguvu na mukono wako wenye kunyooshwa, na anakuja na kusali kuelekea nyumba hii,+ 33 basi usikilize kutoka mbinguni, makao yako, na ufanye mambo yote yenye mugeni huyo anakuomba, ili vikundi vyote vya watu katika dunia vijue jina lako+ na vikuogope, kama vile watu wako Israeli wanafanya, na ili wajue kwamba jina lako limeitwa juu ya nyumba hii yenye nimejenga.
34 “Kama watu wako wanaenda katika vita ili kupigana na maadui wao katika njia yenye unawatuma+ na wanasali+ kwako kuelekea muji huu wenye umechagua na kuelekea nyumba yenye nimejenga kwa ajili ya jina lako,+ 35 basi usikie kutoka mbinguni sala yao na ombi lao la kuomba rehema na ufanye hukumu kwa ajili yao.+
36 “Kama wanakutendea zambi (kwa maana hakuna mwanadamu mwenye hafanyake zambi),+ na unawakasirikia sana na kuwaacha katika mikono ya adui, na wenye waliwakamata wanawapeleka wakiwa wametekwa katika inchi fulani, mbali ao karibu,+ 37 na wanarudiwa na fahamu zao katika inchi kwenye walipelekwa wakiwa wametekwa, na wanarudia kwako na kukuomba uwaonyeshe rehema katika inchi kwenye walitekwa, wakisema, ‘Tumetenda zambi na tumefanya makosa; tumetenda kwa uovu,’+ 38 na wanarudia kwako kwa moyo wao wote+ na kwa nafsi* yao yote katika inchi ya utekwa wao+ kwenye walipelekwa wakiwa wametekwa, na wanasali kuelekea inchi yao yenye ulipatia mababu zao na muji wenye umechagua+ na nyumba yenye nimejenga kwa ajili ya jina lako, 39 basi usikie kutoka mbinguni, makao yako, sala yao na ombi lao la kuomba rehema, na ufanye hukumu kwa ajili yao+ na usamehe watu wako wenye wamekutendea zambi.
40 “Sasa, Ee Mungu wangu, tafazali, macho yako yafunguliwe na masikio yako yasikilize kwa uangalifu sala yenye inatolewa* mahali hapa.+ 41 Na sasa panda, Ee Yehova Mungu, uingie mahali pako pa kupumuzikia,+ wewe pamoja na Sanduku la nguvu zako. Makuhani wako, Ee Yehova Mungu, wavalishwe wokovu, na washikamanifu wako wafurahi katika wema wako.+ 42 Ee Yehova Mungu, usikatae* mutiwa-mafuta wako.+ Ukumbuke upendo wako mushikamanifu kwa Daudi mutumishi wako.”+