Zaburi
Wa Daudi.
א [Aleph]
2 Watanyauka haraka kama majani+
Na kusinyaa kama majani yaliyochipuka ya kijani kibichi.
ב [Beth]
4 Pata furaha tele* katika Yehova,
Naye atatosheleza tamaa za moyo wako.
ג [Gimel]
6 Ataufanya uadilifu wako ung’ae kama mapambazuko,
Na haki yako kama jua la adhuhuri.
ד [Daleth]
Usikasirishwe na mtu
Anayefanikiwa kutekeleza njama zake.+
ה [He]
ו [Waw]
10 Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawatakuwepo tena;+
Utapaangalia mahali walipokuwa,
Nao hawatakuwepo.+
ז [Zayin]
12 Mtu mwovu hupanga njama dhidi ya mwadilifu;+
Humsagia meno yake.
13 Lakini Yehova atamcheka,
Kwa maana Anajua kwamba siku yake itakuja.+
ח [Heth]
14 Waovu huchomoa panga zao na kuzikunja* pinde zao
Ili kumwangusha chini aliyekandamizwa na pia maskini,
Ili kuwachinja wale ambao njia yao imenyooka.
15 Lakini upanga wao utauchoma moyo wao wenyewe;+
Pinde zao zitavunjwa.
ט [Teth]
16 Kidogo alicho nacho mwadilifu ni bora
Kuliko wingi wa vitu walivyo navyo watu wengi waovu.+
17 Kwa maana mikono ya waovu itavunjwa,
Lakini Yehova atawategemeza waadilifu.
י [Yod]
19 Hawataaibishwa wakati wa msiba;
Wakati wa njaa kali watakuwa na chakula tele.
כ [Kaph]
20 Lakini waovu wataangamia;+
Maadui wa Yehova watatoweka kama malisho bora kabisa;
Watatoweka kama moshi.
ל [Lamed]
22 Wale Anaowabariki wataimiliki dunia,
Lakini wale Anaowalaani wataangamizwa.+
מ [Mem]
24 Hata akianguka, hataangushwa chini kabisa,+
נ [Nun]
25 Nilikuwa kijana lakini sasa nimezeeka,
Lakini sijamwona mtu yeyote mwadilifu akiwa ameachwa,+
26 Sikuzote anakopesha bila faida,+
Na watoto wake watapata baraka.
ס [Samekh]
27 Acha uovu, utende mema,+
Nawe utaishi milele.
28 Kwa maana Yehova anapenda haki,
Naye hatawaacha washikamanifu wake.+
ע [Ayin]
פ [Pe]
צ [Tsade]
32 Mwovu humtazama mwadilifu,
Akitafuta kumuua.
ק [Qoph]
34 Mtumaini Yehova na ufuate njia yake,
Naye atakukweza uimiliki dunia.
Waovu watakapoangamizwa,+ utaona jambo hilo.+
ר [Resh]
35 Nimemwona mtu mkatili, mwovu
Akisambaa kama mti wenye majani mengi katika udongo wake wa asili.+
ש [Shin]
37 Mwangalie mtu asiye na lawama,*
Na uendelee kumwangalia mnyoofu,+
Kwa maana wakati ujao wa mtu huyo utakuwa na amani.+
38 Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa;
Wakati ujao wa watu waovu utakomeshwa.+
ת [Taw]
40 Yehova atawasaidia na kuwaokoa.+
Atawanusuru kutoka kwa waovu na kuwaokoa,
Kwa sababu wanamkimbilia yeye.+