Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 1 Wathesalonike 1:1-5:28
  • Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike

Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike

1 Paulo na Silvano+ na Timotheo+ kwa kutaniko la Wathesalonike katika muungano+ na Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo:

Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani.+

2 Sikuzote sisi humshukuru Mungu tunapowataja ninyi nyote katika sala zetu,+ 3 kwa maana daima sisi hukumbuka akilini kazi yenu ya uaminifu+ na kazi yenu ya jasho yenye upendo na uvumilivu wenu kwa sababu ya tumaini+ lenu katika Bwana wetu Yesu Kristo mbele za Mungu wetu na Baba. 4 Kwa maana tunajua, akina ndugu mnaopendwa na Mungu, kuchaguliwa kwenu naye,+ 5 kwa sababu habari njema tunayohubiri haikutokea katikati yenu kwa maneno peke yake bali pia kwa nguvu+ na kwa roho takatifu na usadikisho+ wenye nguvu, kama vile mnavyojua namna ya watu ambao sisi tulikuwa kwenu kwa ajili yenu;+ 6 nanyi mkawa waigaji+ wetu na wa Bwana,+ kwa kuwa mlilipokea neno chini ya dhiki+ nyingi pamoja na shangwe ya roho takatifu,+ 7 hivi kwamba mkawa kielelezo kwa waamini wote katika Makedonia na katika Akaya.

8 Ukweli ni kwamba, si kwamba neno la Yehova+ kutoka kwenu limevuma tu katika Makedonia na Akaya, bali pia kila mahali imani yenu+ kwa Mungu imeenea kotekote,+ hivi kwamba hatuhitaji kusema lolote. 9 Kwa maana wao wenyewe wanaendelea kutoa habari kuhusu namna tulivyoingia kwanza katikati yenu na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkatoka kwenye sanamu+ zenu ili mmtumikie Mungu aliye hai+ na wa kweli,+ 10 na kumngojea+ Mwana wake kutoka mbinguni,+ ambaye yeye alimfufua kutoka kwa wafu,+ yaani, Yesu, anayetukomboa sisi kutoka kwenye ghadhabu inayokuja.+

2 Kwa hakika, ninyi wenyewe mnajua, akina ndugu, jinsi ambavyo ziara+ yetu kwenu haikuwa bila matokeo,+ 2 bali jinsi, baada ya sisi kuwa tumeteseka+ kwanza na kutendewa kwa dharau+ (kama mnavyojua) katika Filipi,+ tulijipa ujasiri kwa njia ya Mungu wetu ili kuwaambia+ ninyi habari njema ya Mungu kwa kupambana sana. 3 Kwa maana himizo ambalo tunatoa halitokani na kosa au kutokana na uchafu+ au na udanganyifu, 4 bali, kama vile tumethibitishwa na Mungu kuwa tunafaa kukabidhiwa+ habari njema, hivyo sisi tunasema, kama wenye kupendeza,+ si wanadamu, bali Mungu, anayeithibitisha mioyo yetu.+

5 Kwa kweli, hakuna wakati wowote ambao sisi tumetokea ama tukiwa na maneno laini,+ (kama mnavyojua) au tukiwa na unafiki+ kwa ajili ya tamaa,+ Mungu ni shahidi! 6 Wala hatutafuti utukufu kutoka kwa wanadamu,+ hapana, ama kutoka kwenu ninyi au kutoka kwa wengine, ingawa tungeweza kuwa mzigo wenye gharama+ tukiwa mitume wa Kristo. 7 Kinyume cha hilo, tulikuwa wapole katikati yenu, kama mama mwenye kunyonyesha anavyowatunza+ kwa upendo watoto wake mwenyewe. 8 Kwa hiyo, tukiwa na upendo mwororo kwa ajili yenu,+ tulipendezwa vema kuwapa ninyi, si habari njema ya Mungu tu, bali pia nafsi zetu wenyewe,+ kwa sababu ninyi mlikuwa wapendwa+ kwetu.

9 Hakika mnakumbuka akilini, akina ndugu, kazi yetu ya jasho na kutaabika. Ilikuwa kwa kufanya kazi+ usiku na mchana, ili tusimtwike yeyote kati yenu mzigo wenye gharama,+ kwamba tuliwahubiria ninyi habari njema ya Mungu. 10 Ninyi ni mashahidi, na Mungu pia, kuhusu tulivyokuwa washikamanifu na waadilifu na wasiolaumika+ kwenu ninyi waamini. 11 Kwa kupatana na hilo mnajua vema jinsi, kama baba+ anavyowatendea watoto wake, tulivyoendelea kumhimiza+ kila mmoja wenu, na kuwafariji na kuwatolea ninyi ushahidi, 12 ili kwamba mwendelee kutembea+ kwa kumstahili Mungu anayewaita+ ninyi kwenye ufalme+ na utukufu wake.

13 Kwa kweli, ndiyo sababu sisi tunamshukuru Mungu pia bila kuacha,+ kwa sababu mlipolipokea neno la Mungu,+ ambalo mlilisikia kutoka kwetu, mlilikubali, si kama neno la wanadamu,+ bali, kama vile lilivyo kwa kweli, kama neno la Mungu, ambalo pia linafanya kazi ndani yenu waamini.+ 14 Kwa maana ninyi mlikuwa waigaji, akina ndugu, wa makutaniko ya Mungu yaliyo katika Yudea katika muungano na Kristo Yesu, kwa sababu ninyi pia mlianza kuteseka+ mikononi mwa wananchi wenzenu wenyewe mambo yaleyale kama yale ambayo wao pia wanateseka mikononi mwa Wayahudi, 15 waliomuua hata Bwana Yesu+ na manabii+ na kututesa sisi.+ Zaidi ya hayo, wao hawampendezi Mungu, bali wako kinyume cha faida za wanadamu wote, 16 wanapojaribu kutuzuia+ tusiseme na watu wa mataifa ili hawa waokolewe,+ matokeo yakiwa kwamba sikuzote wao hukijaza kabisa kipimo+ cha dhambi zao. Lakini ghadhabu yake mwishowe imekuja juu yao.+

17 Na kwa habari yetu wenyewe, akina ndugu, tulipoachwa mayatima bila ninyi kwa wakati mfupi tu, kimwili, si katika moyo, tulijitahidi zaidi kuliko ilivyo kawaida ili kuona nyuso zenu tukiwa na tamaa kubwa.+ 18 Kwa sababu hiyo tulitaka kuja kwenu, ndiyo, mimi Paulo, mara ya kwanza na pia mara ya pili, lakini Shetani aliizuia njia yetu. 19 Kwa maana ni nini tumaini letu au shangwe au taji+ la furaha—je, kwa kweli si ninyi?—mbele ya Bwana wetu Yesu wakati wa kuwapo kwake?+ 20 Ninyi hakika ni utukufu na shangwe yetu.

3 Kwa sababu hiyo, wakati hatukuweza kuvumilia hilo tena, tuliona vema kuachwa peke yetu katika Athene;+ 2 nasi tukamtuma Timotheo,+ ndugu yetu na mhudumu wa Mungu katika habari njema+ juu ya Kristo, kusudi awaimarishe ninyi na kuwafariji kwa ajili ya imani yenu, 3 ili yeyote asiyumbishwe na dhiki hizi.+ Kwa maana ninyi wenyewe mnajua tumewekewa jambo hili.+ 4 Kwa kweli, pia, wakati tulipokuwa pamoja nanyi, tulikuwa tukiwaambia kimbele+ kwamba tulikusudiwa kupatwa na dhiki,+ kama vile ambavyo imetukia pia na kama mnavyojua.+ 5 Hiyo ndiyo sababu, kwa kweli, wakati sikuweza kuvumilia hilo tena, nilimtuma mtu ili nijue juu ya uaminifu wenu,+ kama labda kwa njia fulani yule Mjaribu+ alikuwa amewajaribu ninyi, na kazi yetu ya jasho ikawa ya bure.+

6 Lakini Timotheo amekuja sasa hivi kutoka kwenu+ na kutupa sisi habari njema juu ya uaminifu na upendo wenu,+ na kwamba mnaendelea kutukumbuka vema sikuzote, mkitamani sana kutuona kwa njia ileile, kwa kweli, kama vile sisi pia tunavyotamani kuwaona ninyi.+ 7 Hiyo ndiyo sababu, akina ndugu, tumefarijiwa+ juu yenu ninyi katika uhitaji wetu wote na dhiki kupitia uaminifu mnaoonyesha,+ 8 kwa sababu sasa sisi tunaishi ikiwa ninyi mnasimama imara katika Bwana.+ 9 Kwa maana ni shukrani gani tunazoweza kumtolea Mungu kuhusu ninyi ili ziwe malipo ya shangwe yote tunayoshangilia+ kwa ajili yenu mbele za Mungu wetu, 10 huku usiku na mchana tukiomba dua+ ambazo ni zaidi kuliko zile za kawaida ili tuone nyuso zenu na kutimiza mambo yanayokosekana juu ya imani yenu?+

11 Sasa Mungu na Baba yetu mwenyewe na Bwana wetu Yesu+ na waifanikishe njia yetu kuja kwenu. 12 Zaidi ya hayo, Bwana na awafanye ninyi mwongezeke,+ ndiyo, awafanye ninyi mzidi, katika upendo+ kwa mtu na mwenzake na kwa wote, kama vile sisi pia tunavyowatendea ninyi; 13 kusudi afanye mioyo yenu kuwa imara, isiyolaumika+ katika utakatifu mbele za Mungu na Baba yetu wakati wa kuwapo+ kwa Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.+

4 Mwishowe, akina ndugu, tunawaomba ninyi na kuwahimiza kwa njia ya Bwana Yesu, kama vile mlivyopokea mafundisho kutoka kwetu kuhusu mnavyopaswa kutembea+ na kumpendeza Mungu, kwa kweli kama vile mnavyotembea, kwamba mwendelee kufanya hivyo kwa ukamili zaidi.+ 2 Kwa maana mnajua maagizo+ tuliyowapa ninyi kupitia Bwana Yesu.

3 Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba mtakaswe,+ kwamba mjiepushe na uasherati;+ 4 kwamba kila mmoja wenu ajue jinsi ya kukiweza chombo chake+ mwenyewe katika utakaso+ na heshima, 5 si katika hamu yenye tamaa ya ngono+ kama ile waliyo nayo pia mataifa+ wale wasiomjua Mungu;+ 6 kwamba yeyote asifikie hatua ya kudhuru na kuziingilia haki za ndugu yake katika jambo hilo,+ kwa sababu Yehova ndiye anayelipiza adhabu kwa ajili ya mambo yote haya,+ kama vile tulivyowaambia ninyi kimbele na pia tukawapa ushahidi kamili.+ 7 Kwa maana Mungu alituita sisi bila kuruhusu nafasi ya uchafu, bali kuhusiana na utakaso.+ 8 Kwa hiyo, basi, mtu anayepuuza+ hampuuzi mwanadamu, bali Mungu,+ anayeitia roho yake takatifu+ ndani yenu.

9 Hata hivyo, kuhusu upendo wa kindugu,+ hamhitaji sisi tuwe tukiwaandikia ninyi, kwa maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu+ kupendana;+ 10 na, kwa kweli, mnafanya hivyo kwa ndugu wote katika Makedonia yote. Lakini tunawahimiza ninyi, akina ndugu, mwendelee kufanya hivyo kwa kipimo kamili zaidi, 11 na kufanya iwe shabaha yenu kuishi kwa utulivu+ na kukazia akili mambo yenu wenyewe+ na kufanya kazi kwa mikono yenu,+ kama vile tulivyowaagiza ninyi; 12 ili muwe mkijiendesha kwa adabu+ kuhusiana na watu walio nje+ na msiwe mkihitaji kitu chochote.+

13 Zaidi ya hayo, akina ndugu, hatutaki mkose kujua kuhusu wale walalao usingizi+ katika kifo; ili msiwe na huzuni kama wale watu wengine wasio na tumaini.+ 14 Kwa maana ikiwa imani yetu ni kwamba Yesu alikufa na kufufuliwa tena,+ vivyo hivyo pia, wale ambao wamelala usingizi katika kifo kupitia Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.+ 15 Kwa maana tunawaambia hivi kwa neno la Yehova,+ kwamba sisi tulio hai ambao tutabaki mpaka kuwapo kwa Bwana+ hatutawatangulia kwa vyovyote wale ambao wamelala usingizi katika kifo; 16 kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni+ akiwa na mwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mkuu+ na kwa tarumbeta+ ya Mungu, na wale walio wafu katika muungano na Kristo watafufuliwa kwanza.+ 17 Baadaye sisi tulio hai tuliobaki tutanyakuliwa,+ pamoja nao,+ katika mawingu+ ili kukutana+ na Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana sikuzote.+ 18 Kwa hiyo endeleeni kufarijiana kwa maneno hayo.

5 Sasa kwa habari ya nyakati na majira,+ akina ndugu, hamhitaji kuandikiwa kitu. 2 Kwa maana ninyi wenyewe mnajua vema kabisa kwamba siku ya Yehova+ inakuja sawasawa kabisa kama mwizi usiku.+ 3 Wakati watakapokuwa wakisema:+ “Amani+ na usalama!” ndipo uharibifu+ wa ghafula utakapokuwa juu yao mara moja kama vile maumivu ya taabu juu ya mwanamke mwenye mimba;+ nao hawataponyoka hata kidogo.+ 4 Lakini ninyi, akina ndugu, hamko gizani,+ hivi kwamba siku hiyo iwafikie ninyi kama vile ambavyo ingewafikia wezi,+ 5 kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru+ na wana wa mchana.+ Sisi si wa usiku wala si wa giza.+

6 Kwa hiyo, basi, na tusiendelee kulala usingizi+ kama wengine,+ bali na tukae macho+ na kutunza akili zetu.+ 7 Kwa maana wale wanaolala usingizi+ wana desturi ya kulala usingizi usiku,+ na kwa kawaida wale wanaolewa, hulewa usiku. 8 Lakini kwa habari yetu sisi tulio wa mchana, na tutunze akili zetu na kuvaa bamba la kifuani+ la imani+ na upendo na lile tumaini la wokovu+ kama kofia ya chuma;+ 9 kwa sababu Mungu hakutuweka sisi tupate ghadhabu,+ bali tujipatie wokovu+ kupitia Bwana wetu Yesu Kristo.+ 10 Yeye alikufa kwa ajili yetu,+ ili, kama tunakaa macho au kama tumelala usingizi, tuishi pamoja naye.+ 11 Kwa hiyo endeleeni kufarijiana na kujengana,+ kama vile mnavyofanya.+

12 Sasa tunawaomba ninyi, akina ndugu, mwatilie maanani wale wanaofanya kazi kwa bidii kati yenu na kuwasimamia+ ninyi katika Bwana na kuwaonya ninyi; 13 na kuwafikiria kwa njia inayozidi ile ya kawaida katika upendo kwa sababu ya kazi yao.+ Iweni wenye kufanya amani mtu na mwenzake.+ 14 Kwa upande mwingine, tunawahimiza ninyi, akina ndugu, mwaonye wale wasio na utaratibu,+ semeni kwa kuzifariji nafsi zilizohuzunika,+ tegemezeni walio dhaifu, iweni wenye ustahimilivu+ kuelekea wote. 15 Angalieni kwamba mtu asimlipe mwingine yeyote ubaya kwa ubaya,+ bali sikuzote fuatilieni yaliyo mema kuelekea mtu na mwenzake na kwa wengine wote.+

16 Shangilieni sikuzote.+ 17 Salini bila kuacha.+ 18 Kuhusiana na kila jambo toeni shukrani.+ Kwa maana hayo ndiyo mapenzi ya Mungu katika muungano na Kristo Yesu kwa habari yenu. 19 Msiuzime moto wa roho.+ 20 Msiyatendee kwa dharau maneno ya unabii.+ 21 Hakikisheni mambo yote;+ shikeni sana yaliyo mazuri.+ 22 Jiepusheni na kila namna ya uovu.+

23 Yule Mungu wa amani+ na awatakase ninyi kikamilifu.+ Na vikiwa timamu katika kila jambo, roho na nafsi na mwili wenu akina ndugu na vihifadhiwe kwa namna isiyo na lawama wakati wa kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo.+ 24 Yeye anayewaita ninyi ni mwaminifu, naye atafanya hilo pia.

25 Akina ndugu, endeleeni kusali kwa ajili yetu.+

26 Mwasalimu ndugu wote kwa busu takatifu.+

27 Nawaweka ninyi chini ya wajibu mzito kwa Bwana ili barua hii isomewe ndugu wote.+

28 Fadhili zisizostahiliwa+ za Bwana wetu Yesu Kristo na ziwe pamoja nanyi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki