Isaya
1 Maono yenye Isaya*+ mwana wa Amozi aliona kuhusu Yuda na Yerusalemu katika siku za Uzia,+ Yotamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda:+
3 Ngombe-dume anajua muzuri mwenye alimununua,
Na punda anajua chombo cha kukulishia wanyama cha bwana wake;
Watu wangu mwenyewe hawajiendeshe kwa uelewaji.”
4 Ole wake taifa lenye zambi,+
Watu wenye kulemewa na kosa,
Uzao wa watu waovu, watoto wenye kupotoka!
5 Ni wapi mutapigwa tena kwa sababu munaongeza kwenye uasi wenu?+
Kichwa chote ni kigonjwa,
Na moyo wote ni mugonjwa.+
6 Kuanzia kikanyangio cha muguu mupaka kwenye kichwa, hakuna kitu chenye afya ya muzuri.
Kuko vidonda na michubuko na vidonda vyenye kuwa wazi
—Havijatunzwa* wala kufungwa wala kulainishwa kwa mafuta.+
7 Inchi yenu iko ukiwa.
Miji yenu imeteketezwa kwa moto.
Wageni wanakula inchi yenu mbele yenu.+
Ni kama eneo lenye limeachwa lenye limepinduliwa na wageni.+
8 Binti ya Sayuni ameachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu,
Kama nyumba ya kidogo katika shamba la matango,
Kama muji wenye umezungukwa kwa ajili ya vita.+
9 Kama Yehova wa majeshi hangetuachia waokokaji kidogo,
Tungekuwa kama Sodoma,
Na tungefanana na Gomora.+
10 Musikie neno la Yehova, ninyi madikteta* wa Sodoma.+
Mukazie uangalifu sheria ya* Mungu wetu, ninyi watu wa Gomora.+
11 “Zabihu zenu nyingi ziko na faida gani kwangu?”+ ni vile Yehova anasema.
“Nimechoka na matoleo yenu ya kuteketezwa ya kondoo-dume+ na mafuta ya wanyama wenye kukulishwa muzuri,+
Na sifurahie damu+ ya ngombe-dume wadogo+ na wana-kondoo na mbuzi.+
12 Wakati munakuja ili kuonekana mbele yangu,+
Ni nani amewaomba mufanye vile,
Mukanyange-kanyange viwanja vyangu?+
13 Musilete tena matoleo ya nafaka yenye hayana mafaa yoyote.
Uvumba wenu ni chukizo kwangu.+
Miezi mipya,+ sabato,+ kuita mikusanyiko+
—Siwezi kuvumilia matumizi ya nguvu za uchawi+ pamoja na mukusanyiko wenu mukubwa.
14 Nimechukia* miezi yenu mipya na sikukuu zenu.
Zimekuwa muzigo kwangu;
Nimechoka kuzibeba.
Muondoe matendo yenu maovu mbele ya macho yangu;
Muache kutenda mabaya.+
17 Mujifunze kutenda mema, mutafute haki,+
Murekebishe mukandamizaji,
Mutetee haki za mutoto mwenye hana baba,*
Na mutetee mashitaka ya mujane.”+
18 “Sasa, mukuje, tunyooshe mambo kati yetu,” ni vile Yehova anasema.+
“Hata kama zambi zenu ziko na rangi nyekundu yenye kungaa,
Zitafanywa kuwa nyeupe kama teluji;*+
Hata kama ziko nyekundu kama kitambaa chekundu,
Zitakuwa kama manyoya ya kondoo.
20 Lakini kama munakataa na munaasi,
Mutakuliwa na upanga,+
Kwa maana kinywa cha Yehova kimesema vile.”
21 Muji muaminifu+ umekuwa kahaba sana!+
23 Wakubwa wako ni wenye kichwa-nguvu na wanashirikiana na wezi.+
Kila mumoja wao anapenda rushwa* na anafuatilia zawadi.+
24 Kwa hiyo Bwana wa kweli, Yehova wa majeshi,
Mwenye Nguvu wa Israeli, anasema:
“Aha! Nitaondoa wapinzani wangu,
Na nitalipiza kisasi juu ya maadui wangu.+
25 Nitageuza mukono wangu ili kukupinga,
Nitayeyusha takataka yako kama kwa sabuni,
Na nitaondoa uchafu wako wote.+
Kisha hilo wewe utaitwa Muji wa Haki, Muji Muaminifu.+
29 Kwa maana watasikia haya kwa sababu ya miti yenye nguvu yenye mulitamani,+
Na mutapata haya kwa sababu ya mabustani* yenye mulichagua.+