KUTOKA
1 Basi haya ndiyo majina ya wana wa Israeli wenye waliingia Misri pamoja na Yakobo, kila mwanaume mwenye alikuja pamoja na nyumba yake:+ 2 Rubeni, Simeoni, Lawi, na Yuda;+ 3 Isakari, Zabuloni, na Benyamini; 4 Dani na Naftali, Gadi na Asheri.+ 5 Na wale wote wenye walizaliwa* na Yakobo* walikuwa watu* makumi saba (70), lakini tayari Yosefu alikuwa Misri.+ 6 Mwishowe Yosefu akakufa,+ na pia ndugu zake wote na kizazi hicho chote. 7 Na Waisraeli* wakazaa na kuanza kuongezeka sana, na wakaendelea kuongezeka na kuwa wenye nguvu zaidi kwa namna yenye haikukuwa ya kawaida; na hivyo wakajaa katika inchi.+
8 Kisha wakati fulani kukatokea mufalme mupya juu ya Misri, mwenye hakumujua Yosefu. 9 Kwa hiyo akaambia watu wake: “Muangalie! Watu wa Israeli ni wengi sana na wako na nguvu sana kuliko sisi.+ 10 Tuwatendee kwa werevu. Kama hatufanye vile, wataendelea kuongezeka, na kama vita inatokea, wataungana na maadui wetu na watapigana na sisi na kuondoka katika inchi.”
11 Kwa hiyo wakaweka juu yao wakubwa wa kazi ya kulazimishwa* ili kuwakandamiza kwa kazi ya nguvu,+ na wakamujengea Farao miji ya kuwekea vitu, ni kusema, Pitomu na Raamsesi.+ 12 Lakini kadiri waliendelea kuwakandamiza, ni vile waliendelea kuongezeka na ni vile waliendelea kuenea kila mahali, kwa hiyo Wamisri wakaogopa na kuchukizwa sana kwa sababu ya Waisraeli.+ 13 Basi Wamisri wakaweka Waisraeli katika utumwa mukali.+ 14 Wakafanya maisha yao kuwa machungu kwa kazi ya nguvu, kadiri waliendelea kufanya kazi na saruji* ya udongo na matofali na kila namna ya kazi ya utumwa katika mashamba. Ndiyo, waliwatesa sana katika hali za nguvu za kila namna ya utumwa.+
15 Kisha wakati fulani mufalme wa Misri akazungumuza na wanamuke Waebrania wa kuzalisha wenye waliitwa Shifra na Pua: 16 na akawaambia: “Wakati munasaidia wanamuke Waebrania kuzaa+ na munawaona kwenye kiti cha kuzalia, kama ni mutoto mwanaume munapaswa kumuua; lakini kama ni mutoto mwanamuke, anapaswa kuishi.” 17 Lakini, wanamuke hao wa kuzalisha walimuogopa Mungu wa kweli, na hawakufanya jambo lenye mufalme wa Misri aliwaambia. Kuliko kufanya vile, walikuwa wanaacha watoto wanaume waishi.+ 18 Kisha wakati fulani mufalme wa Misri akaita wanamuke hao wa kuzalisha na kuwaambia: “Sababu gani mumeacha watoto wanaume waishi?” 19 Wanamuke hao wa kuzalisha wakamuambia Farao: “Wanamuke Waebrania hawako kama wanamuke Wamisri. Wako na nguvu; mbele mwanamuke wa kuzalisha afike karibu nao, wanakuwa tayari wamezaa.”
20 Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wanamuke hao wa kuzalisha, na watu wakaendelea kuongezeka na kuwa wenye nguvu sana. 21 Na kwa sababu wanamuke hao wa kuzalisha walimuogopa Mungu wa kweli, kisha wakati fulani Mungu akawapatia familia. 22 Mwishowe Farao akatoa amri kwa watu wake wote: “Munapaswa kutupa katika Muto Nile kila mutoto mwanaume wa Waebrania mwenye anazaliwa, lakini munapaswa kuacha kila mutoto mwanamuke aishi.”+
2 Karibu wakati huo, mwanaume fulani wa nyumba ya Lawi alimuoa binti ya Lawi.+ 2 Na mwanamuke huyo akakuwa na mimba na akazaa mwana. Wakati aliona namna mwana huyo alikuwa mwenye sura na umbo ya muzuri, akamuficha kwa miezi tatu (3).+ 3 Wakati hakuweza tena kuendelea kumuficha,+ alikamata kitunga cha* mafunjo* na kukipakaa kabulimbo na bereu* na akatia mutoto huyo ndani yake na kutia kile kitunga kati ya matete pembeni ya Muto Nile. 4 Lakini dada ya mutoto huyo+ akasimama mbali kidogo ili aone mambo yenye yatamupata mutoto huyo.
5 Wakati binti ya Farao alishuka kuenda kuoga katika Muto Nile, watumishi wake wanamuke walikuwa wanatembea-tembea pembeni ya Muto Nile. Na binti ya Farao akaona kile kitunga katikati ya matete. Mara moja akamutuma mutumwa wake mwanamuke aende kukileta.+ 6 Wakati alifungua kile kitunga, akaona ule mutoto, na ule mutoto mwanaume alikuwa analia. Akamusikilia huruma, lakini akasema: “Huyu ni mumoja wa watoto wa Waebrania.” 7 Kisha dada ya mutoto huyo akamuambia binti ya Farao: “Je, niende kukuitia mwanamuke mwenye kunyonyesha kati ya Waebrania ili akunyonyeshee mutoto huyu?” 8 Binti ya Farao akamuambia: “Uende!” Mara moja huyo kijana mwanamuke akaenda kumuita mama ya mutoto huyo.+ 9 Kisha binti ya Farao akamuambia mama huyo: “Chukua mutoto huyu uninyonyeshee yeye, na mimi nitakulipa.” Kwa hiyo mwanamuke huyo akamuchukua mutoto huyo na kumunyonyesha. 10 Wakati mutoto huyo alikomaa, akamupeleka kwa binti ya Farao, na akakuwa mwana wake.+ Akamupatia jina Musa* na kusema: “Ni kwa sababu nimemutosha ndani ya maji.”+
11 Sasa katika siku hizo, kisha Musa kuwa mutu muzima,* alitoka na kuenda kwa ndugu zake ili kuona mizigo yenye walikuwa wanabeba,+ na akaona Mumisri fulani mwenye alikuwa anamupiga Mwebrania fulani, mumoja wa ndugu zake. 12 Kwa hiyo Musa akaangalia huku na huku, na wakati aliona hakuna mutu karibu, akamuua ule Mumisri na akamuficha katika muchanga.+
13 Lakini alitoka tena siku yenye ilifuata, na kulikuwa wanaume wawili Waebrania wenye walikuwa wanapigana. Kwa hiyo akamuambia ule mwenye alikuwa na kosa: “Sababu gani unamupiga mwenzako?”+ 14 Akasema: “Ni nani alikuweka kuwa mukubwa na muamuzi juu yetu? Je, unataka kuniua kama vile ulimuua ule Mumisri?”+ Basi Musa akaogopa na kusema: “Hakika jambo hilo limejulikana!”
15 Kisha Farao akasikia habari hiyo, naye akajaribu kumuua Musa; lakini Musa akamukimbia Farao na kuenda kuishi katika inchi ya Midiani,+ na akakaa pembeni ya kisima. 16 Sasa kuhani wa Midiani+ alikuwa na mabinti saba (7), nao wakakuja kushota maji na kujaza vyombo vya kuwekea maji ya kunywa ya wanyama wa kundi la baba yao. 17 Lakini kama kawaida, wachungaji wakakuja na kufukuza mabinti hao. Basi Musa akasimama na kusaidia* wanamuke hao na akanywesha kundi lao. 18 Wakati walifika kwa baba yao Reueli,*+ mara moja akasema: “Namna gani mumerudia mbio sana leo?” 19 Wakajibu: “Mumisri fulani+ alituokoa katika mikono ya wachungaji, na hata alitushotea maji na kunywesha kundi letu.” 20 Akaambia mabinti wake: “Lakini iko* wapi? Sababu gani muliacha mwanaume huyo nyuma? Mumuite, ili akule chakula pamoja na sisi.” 21 Kisha mambo hayo Musa akakubali kuishi pamoja na mwanaume huyo, na akamupatia Musa binti yake Sipora+ ili akuwe bibi yake. 22 Kisha wakati fulani Sipora akamuzaa mwana, na Musa akamupatia jina Gershomu,*+ kwa sababu alisema: “Nimekuwa mukaaji mugeni katika inchi ya kigeni.”+
23 Kisha wakati murefu, mufalme wa Misri akakufa,+ lakini Waisraeli wakaendelea kulia kwa maumivu kwa sababu ya utumwa na kutoa sauti za malalamiko, na kilio chao cha kuomba musaada kikaendelea kupanda mupaka kwa Mungu wa kweli.+ 24 Mwishowe Mungu akasikia kilio chao cha maumivu,+ na Mungu akakumbuka agano lenye alifanya pamoja na Abrahamu, Isaka, na Yakobo.+ 25 Kwa hiyo Mungu akakaza uangalifu wake juu ya Waisraeli; na Mungu akaona hali yao.
3 Musa akakuwa muchungaji wa kundi la Yetro, baba-mukwe wake,+ kuhani wa Midiani. Wakati alikuwa anaongoza kundi kuelekea upande wa mangaribi wa jangwa, mwishowe akafika kwenye mulima wa Mungu wa kweli, kule Horebu.+ 2 Kisha malaika wa Yehova akamutokea katika mwali wa moto katikati ya muti mudogo wa miiba.+ Wakati Musa aliendelea kuangalia, akaona kwamba ule muti mudogo wa miiba ulikuwa unawaka moto, lakini ule muti mudogo wa miiba haukukuwa unateketea. 3 Kwa hiyo Musa akasema: “Niende karibu zaidi ili nichunguze jambo hili la ajabu kusudi nione sababu gani ule muti mudogo wa miiba hauteketee.” 4 Wakati Yehova aliona kwamba Musa anaenda karibu zaidi ili kuangalia, Mungu akamuita kutoka katikati ya ule muti mudogo wa miiba na kusema: “Musa! Musa!” naye akasema: “Mimi huyu.” 5 Kisha Mungu akasema: “Usikaribie. Vua viatu vyako kwenye miguu yako, kwa sababu mahali unasimama ni udongo mutakatifu.”
6 Akaendelea kusema: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu,+ Mungu wa Isaka,+ na Mungu wa Yakobo.”+ Kisha Musa akaficha uso wake, kwa sababu aliogopa kumuangalia Mungu wa kweli. 7 Yehova akaongeza kusema: “Kwa kweli nimeona mateso ya watu wangu wenye wako Misri, na nimesikia kilio chao kwa sababu ya wale wenye kuwalazimisha kufanya kazi; ninajua muzuri maumivu yenye wako nayo.+ 8 Nitashuka ili kuwakomboa katika mukono wa Wamisri+ na kuwatosha katika inchi hiyo na kuwaleta kwenye inchi ya muzuri na kubwa, inchi yenye kutiririka maziwa na asali,+ eneo la Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.+ 9 Sasa angalia! Kilio cha watu wa Israeli kimenifikia, na nimeona pia namna Wamisri wanawakandamiza kwa ukali.+ 10 Sasa kuja, nitakutuma kwa Farao, na wewe utatosha watu wangu Waisraeli katika Misri.”+
11 Lakini, Musa akamuambia Mungu wa kweli: “Mimi niko nani ili niende kwa Farao na kutosha Waisraeli katika Misri?” 12 Basi Mungu akasema: “Nitakuwa pamoja na wewe,+ na hii ndiyo alama yenye itaonyesha kwamba ni mimi nilikutuma: Kisha wewe kutosha watu katika Misri, ninyi mutamutumikia* Mungu wa kweli kwenye mulima huu.”+
13 Lakini Musa akamuambia Mungu wa kweli: “Tuseme ninaenda kwa Waisraeli na kuwaambia, ‘Mungu wa mababu zenu amenituma kwenu,’ nao wakiniambia, ‘Jina lake ni nani?’+ Nitawaambia nini?” 14 Kwa hiyo Mungu akamuambia Musa: “Nitakuwa Kile Ninachagua* Kuwa.”*+ Na akaongeza kusema: “Utaambia Waisraeli hivi: ‘Nitakuwa amenituma kwenu.’”+ 15 Kisha Mungu akamuambia Musa tena:
“Utaambia Waisraeli hivi: ‘Yehova Mungu wa mababu zenu, Mungu wa Abrahamu,+ Mungu wa Isaka,+ na Mungu wa Yakobo,+ amenituma kwenu.’ Hilo ndilo jina langu milele,+ na ni vile ninapaswa kukumbukwa kutoka kizazi mupaka kizazi. 16 Sasa, uende ukusanye wazee wa Israeli na kuwaambia, ‘Yehova Mungu wa mababu zenu amenitokea, Mungu wa Abrahamu, Isaka, na Yakobo, na alisema: “Hakika nimewakazia uangalifu+ na nimeona mambo yenye wanawatendea katika Misri. 17 Kwa hiyo ninasema, nitawatosha katika mateso+ yenye munapata katika mikono ya Wamisri na nitawapeleka katika inchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori,+ Waperizi, Wahivi, na Wayebusi,+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali.”’+
18 “Hakika watasikiliza sauti yako,+ na utaenda, wewe pamoja na wazee wa Israeli, kwa mufalme wa Misri, na mutamuambia, ‘Yehova Mungu wa Waebrania+ amezungumuza na sisi. Kwa hiyo, tafazali, acha tufanye safari ya siku tatu (3) katika jangwa ili tumutolee Yehova Mungu wetu zabihu.’+ 19 Lakini mimi mwenyewe ninajua muzuri kwamba mufalme wa Misri hatawapatia ruhusa ya kuenda kama halazimishwe na mukono wenye nguvu.+ 20 Kwa hiyo nitanyoosha mukono wangu na kupiga Misri kwa matendo yangu yote ya ajabu yenye nitafanya katika inchi hiyo, na kisha atawaruhusu muende.+ 21 Na nitafanya watu hawa wakubaliwe mbele ya macho ya Wamisri, na wakati mutaondoka, hamutaenda mikono wazi.+ 22 Kila mwanamuke anapaswa kumuomba jirani yake na mwanamuke mwenye kukaa katika nyumba yake vitu vya feza na vya zahabu na pia nguo, na mutavivalisha watoto wenu wanaume na watoto wenu wanamuke, na mutanyanganya vitu vya Wamisri.”+
4 Hata hivyo, Musa akajibu: “Lakini tuseme hawaniamini na hawasikilize sauti yangu,+ kwa maana watasema, ‘Yehova hakukutokea.’” 2 Kisha Yehova akamuambia: “Uko na nini katika mukono wako?” Akajibu: “Fimbo.” 3 Akasema: “Uitupe chini.” Kwa hiyo akaitupa chini, na ikakuwa nyoka;+ na Musa akamukimbia ule nyoka. 4 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Nyoosha mukono wako umukamate kwenye mukia.” Kwa hiyo akanyoosha mukono wake na kumukamata, na nyoka huyo akakuwa fimbo katika mukono wake. 5 Kisha Mungu akasema: “Ni vile ili waamini kama Yehova Mungu wa mababu zao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo,+ amekutokea.”+
6 Tena Yehova akamuambia: “Tafazali, tia mukono wako ndani ya mukunjo wa juu wa nguo yako.” Kwa hiyo akatia mukono wake ndani ya mukunjo wa nguo yake. Wakati aliutosha ndani, angalia, mukono wake ulikuwa umepigwa na ukoma kama teluji!*+ 7 Kisha Mungu akasema: “Rudisha mukono wako ndani ya mukunjo wa juu wa nguo yako.” Kwa hiyo akarudisha mukono wake ndani ya nguo yake. Wakati aliutosha ndani ya nguo yake, ulirudia tena kama sehemu zingine za mwili wake! 8 Mungu akasema: “Kama hawatakuamini ao kama hawatakazia uangalifu alama ya kwanza, basi hakika wataamini alama yenye kufuata.+ 9 Lakini, hata kama hawataamini zile alama mbili na hata kama watakataa kusikiliza sauti yako, utakamata maji katika Muto Nile na kuyamwanga kwenye inchi kavu, na maji hayo yenye utakamata katika Muto Nile yatakuwa damu kwenye inchi kavu.”+
10 Sasa Musa akamuambia Yehova: “Unisamehe, Ee Yehova, lakini siko musemaji muzuri, ikuwe zamani ao tangu wakati ulianza kuzungumuza na mutumishi wako, kwa maana niko muzito wa kusema* na ulimi wangu ni muzito.”+ 11 Yehova akamuambia: “Ni nani alifanya kinywa kwa ajili ya mwanadamu, ao ni nani anafanya mutu kuwa bubu, kiziwi, mwenye kuona muzuri, ao kipofu? Je, haiko mimi Yehova? 12 Kwa hiyo uende sasa, na nitakuwa pamoja na wewe wakati utakuwa unazungumuza,* na nitakufundisha jambo lenye unapaswa kusema.”+ 13 Lakini akasema: “Unisamehe, Yehova, tafazali tuma mutu yeyote mwenye unataka kutuma.” 14 Basi kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Musa, na akasema: “Namna gani kuhusu ndugu yako Haruni+ ule Mulawi? Ninajua kama anaweza kuzungumuza muzuri sana. Na sasa anakuja ili kukutana na wewe. Wakati atakuona, moyo wake utafurahi.+ 15 Kwa hiyo unapaswa kuzungumuza naye na kuweka maneno katika kinywa chake,+ na nitakuwa pamoja na wewe na pamoja naye wakati unazungumuza,+ na nitawafundisha mambo yenye mutafanya. 16 Atazungumuza na watu kwa ajili yako, na atakuwa musemaji wako, na wewe utakuwa kama Mungu kwake.*+ 17 Na utakamata fimbo hii katika mukono wako na kuitumia ili kufanya zile alama.”+
18 Kwa hiyo Musa akarudia kwa Yetro baba-mukwe wake+ na kumuambia: “Tafazali, ninataka kuenda na kurudia kwa ndugu zangu wenye wako Misri ili nione kama wangali wazima.” Yetro akamuambia Musa: “Uende kwa amani.” 19 Kisha Yehova akamuambia Musa kule Midiani: “Uende, urudie Misri, kwa sababu watu wote wenye walikuwa wanatafuta kukuua* wamekufa.”+
20 Basi Musa akamuchukua bibi yake na wana wake na kuwapandisha juu ya punda, na akaanza safari ya kurudia katika inchi ya Misri. Pia, Musa akakamata ile fimbo ya Mungu wa kweli katika mukono wake. 21 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Wakati utakuwa umerudia Misri, hakikisha kwamba unafanya mbele ya Farao miujiza yote yenye nimekupatia uwezo wa kufanya.+ Lakini nitaacha moyo wa Farao ukuwe mugumu,+ naye hataruhusu watu wangu waende.+ 22 Unapaswa kumuambia Farao, ‘Yehova anasema hivi: “Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.+ 23 Ninakuambia, Ruhusu mwana wangu aende ili aweze kunitumikia. Lakini kama unakataa kumuruhusu aende, nitaua mwana wako, muzaliwa wako wa kwanza.”’”+
24 Sasa katika barabara, mahali pa kulala, Yehova+ akakutana naye na alikuwa anatafuta kumuua.+ 25 Mwishowe Sipora+ akakamata jiwe ngumu* na kutahiri mwana wake na Sipora akafanya govi* la mwana huyo liguse miguu yake na akasema: “Ni kwa sababu wewe uko bwana-arusi wa damu kwangu.” 26 Kwa hiyo Mungu akamuacha aende. Wakati huo Sipora akasema, “bwana-arusi wa damu,” kwa sababu ya kutahiri.
27 Kisha Yehova akamuambia Haruni: “Uende katika jangwa ili ukutane na Musa.”+ Kwa hiyo akaenda na kukutana naye kwenye mulima wa Mungu wa kweli+ na akamusalimia kwa kumubusu. 28 Na Musa akamuambia Haruni maneno yote ya Yehova, mwenye alikuwa amemutuma,+ na alama zote zenye Mungu alikuwa amemuamuru kufanya.+ 29 Kisha Musa na Haruni wakaenda na wakakusanya wazee wote wa Waisraeli.+ 30 Haruni akawaambia maneno yote yenye Yehova alikuwa amemuambia Musa, naye akafanya zile alama+ mbele ya watu. 31 Kwa hiyo watu wakaamini.+ Wakati walisikia kwamba Yehova alikuwa ameelekezea Waisraeli uangalifu wake+ na kwamba alikuwa ameona mateso yao,+ wakainama na kushusha uso chini.
5 Kisha, Musa na Haruni wakaingia na kumuambia Farao: “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Ruhusu watu wangu waende kunifanyia sikukuu katika jangwa.’” 2 Lakini Farao akasema: “Yehova ni nani,+ ili nitii sauti yake kwa kuruhusu Israeli waende?+ Simujue Yehova hata kidogo, na tena, sitaruhusu Israeli waende.”+ 3 Lakini wakasema: “Mungu wa Waebrania amezungumuza na sisi. Tafazali, tunataka kufanya safari ya siku tatu (3) katika jangwa na kumutolea Yehova Mungu wetu zabihu;+ kama hatufanye vile, atatupiga kwa ugonjwa ao kwa upanga.” 4 Mufalme wa Misri akawajibu: “Musa na Haruni, sababu gani muko munatosha watu katika kazi yao? Murudie kwenye kazi yenu!”*+ 5 Kisha Farao akasema: “Muangalie namna watu wa inchi hii ni wengi, na munataka kuwafanya waache kufanya kazi yao!”
6 Siku ileile, Farao akawaamuru hivi wasimamizi wa kazi na wakubwa wa wafanyakazi: 7 “Hamupaswe tena kupatia watu hawa nyasi ili kutengeneza matofali.+ Muwaache waende kujitafutia nyasi wao wenyewe. 8 Lakini munapaswa kuwalazimisha watengeneze hesabu ileile ya matofali kama vile walifanya zamani. Musiwapunguzie hesabu hiyo, kwa sababu wameanza kuregea.* Ndiyo sababu wanalia, na kusema, ‘Tunataka kuenda, tunataka kumutolea Mungu wetu zabihu!’ 9 Muwatumikishe vikali, na muwapatie kazi nyingi ili wasisikilize maneno ya uongo.”
10 Kwa hiyo wasimamizi wa kazi+ na wakubwa wa wafanyakazi wakaenda na kuambia watu: “Farao anasema hivi: ‘Sitawapatia tena nyasi. 11 Muende mujitafutie nyasi yenu ninyi wenyewe kila mahali kwenye munaweza kuipata, lakini kazi yenu haitapunguzwa hata kidogo.’” 12 Basi watu wakasambaa kila mahali katika inchi ya Misri ili kukusanya majani ya kukauka pa nafasi ya nyasi. 13 Na wasimamizi wa kazi wakaendelea kuwaambia hivi: “Kila mutu anapaswa kumaliza kazi yake kila siku, kama vile wakati walikuwa wanawapatia nyasi.” 14 Pia, wakubwa wa wafanyakazi wa Waisraeli, wenye wasimamizi wa kazi wa Farao walikuwa wameweka juu ya Waisraeli, walipigwa.+ Wasimamizi wa kazi waliwauliza: “Sababu gani hamukueneza hesabu ya matofali yenye mulikuwa munafanya? Ilikuwa vile jana na leo.”
15 Kwa hiyo wakubwa wa wafanyakazi wa Waisraeli wakaingia na kutoa malalamiko yao kwa Farao, kwa kusema: “Sababu gani unatutendea hivi sisi watumishi wako? 16 Sisi watumishi wako, hawatupatie tena nyasi, lakini wanaendelea kutuambia, ‘Mutengeneze matofali!’ Watumishi wako wanapigwa, lakini kosa ni la watu wako mwenyewe.” 17 Lakini Farao akasema: “Mumeanza kuregea,* mumeanza kuregea!*+ Ndiyo sababu munasema, ‘Tunataka kuenda, tunataka kumutolea Yehova zabihu.’+ 18 Sasa muende, murudie kwenye kazi! Hamutapewa nyasi yoyote, lakini munapaswa kuendelea kutengeneza hesabu ileile ya matofali.”
19 Kwa hiyo wakubwa wa wafanyakazi wa Waisraeli wakaona kwamba wako katika shida kubwa kwa sababu ya amri hii: “Hamupaswe kupunguza hata kidogo hesabu ya matofali yenye munapaswa kutengeneza kila siku.” 20 Kisha mambo hayo wakakutana na Musa na Haruni, wenye walikuwa wanasimama pale ili kukutana nao wakati walikuwa wanatoka kwa Farao. 21 Mara moja wakawaambia: “Yehova awaangalie ninyi na kuwahukumu, kwa sababu mumefanya Farao na watumishi wake watuzarau* na mumeweka upanga katika mikono yao ili watuue.”+ 22 Kisha Musa akageuka kumuelekea Yehova na kusema: “Yehova, sababu gani umetesa watu hawa? Sababu gani umenituma? 23 Tangu wakati niliingia mbele ya Farao ili kuzungumuza kwa jina lako,+ amewatendea mubaya sana watu hawa,+ na hakika haujaokoa watu wako.”+
6 Kwa hiyo Yehova akamuambia Musa: “Sasa utaona mambo yenye nitamutendea Farao.+ Mukono wenye nguvu utamulazimisha aruhusu watu wangu waende, na mukono wenye nguvu utamulazimisha awafukuze mutoke katika inchi yake.”+
2 Kisha Mungu akamuambia Musa: “Mimi ni Yehova. 3 Nilikuwa ninamutokea Abrahamu, Isaka, na Yakobo kama Mungu Mweza-Yote,+ lakini kuhusu jina langu Yehova+ sikujitambulisha kwao.+ 4 Pia, nilifanya agano pamoja nao ili kuwapatia inchi ya Kanaani, inchi yenye waliishi ndani yake kama wageni.+ 5 Sasa mimi mwenyewe nimesikia kilio cha maumivu cha watu wa Israeli, wenye Wamisri wako wanafanya kuwa watumwa, na ninakumbuka agano langu.+
6 “Kwa hiyo uambie Waisraeli: ‘Mimi ni Yehova, na nitawatosha chini ya mizigo ya Wamisri na kuwaokoa katika utumwa wao,+ na nitawakomboa kwa mukono wenye kunyooshwa* na kwa hukumu kubwa.+ 7 Na nitawachukua kuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu,+ na hakika mutajua kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu mwenye anawatosha chini ya mizigo ya Misri. 8 Na nitawaingiza katika inchi yenye niliapa kwa kiapo* kwamba nitamupatia Abrahamu, Isaka, na Yakobo; na nitawapatia inchi hiyo ikuwe uriti wenu.+ Mimi ni Yehova.’”+
9 Kisha wakati fulani Musa akapatia Waisraeli ujumbe huo, lakini hawakumusikiliza Musa kwa sababu walikuwa wamevunjika moyo na kwa sababu ya utumwa mugumu.+
10 Kisha Yehova akasema na Musa, na kumuambia: 11 “Ingia na umuambie Farao, mufalme wa Misri, kwamba anapaswa kuruhusu Waisraeli waondoke katika inchi yake.” 12 Lakini Musa akamujibu Yehova: “Angalia! Waisraeli hawakunisikiliza;+ namna gani Farao atanisikiliza, mimi mwenye kuwa muzito wa kusema?”*+ 13 Lakini Yehova akamuambia tena Musa na Haruni amri za kupatia Waisraeli na Farao, mufalme wa Misri, ili kutosha Waisraeli katika inchi ya Misri.
14 Hawa ndio vichwa vya nyumba za baba zao: Wana wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli,+ walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi.+ Ni hizo zilikuwa familia za Rubeni.
15 Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli, mwana wa mwanamuke Mukanaani.+ Ni hizo zilikuwa familia za Simeoni.
16 Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi,+ kulingana na vizazi vya familia zao: Gershoni, Kohati, na Merari.+ Lawi aliishi miaka mia moja makumi tatu na saba (137).
17 Wana wa Gershoni walikuwa Libni na Shimei, kulingana na familia zao.+
18 Wana wa Kohati walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli.+ Kohati aliishi miaka mia moja makumi tatu na tatu (133).
19 Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi.
Ni hizo zilikuwa familia za Walawi, kulingana na vizazi vya familia zao.+
20 Sasa Amramu alimuchukua Yokebedi, dada ya baba yake, akuwe bibi yake.+ Yokebedi akamuzalia Haruni na Musa.+ Amramu aliishi miaka mia moja makumi tatu na saba (137).
21 Wana wa Ishari walikuwa Kora,+ Nefegi, na Zikri.
22 Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elsafani,+ na Sitri.
23 Sasa Haruni akamuchukua Elisheba, binti ya Aminadabu, dada ya Nashoni,+ akuwe bibi yake. Akamuzalia Nadabu, Abihu, Eleazari, na Itamari.+
24 Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elkana, na Abiasafu.+ Ni hizo zilikuwa familia za Wakora.+
25 Eleazari+ mwana wa Haruni, alichukua mumoja wa mabinti wa Putieli akuwe bibi yake. Akamuzalia Finehasi.+
Hao ndio vichwa vya jamaa za upande wa baba za Walawi, kulingana na familia zao.+
26 Huyu ndiye Haruni na Musa wenye Yehova aliambia: “Mutoshe watu wa Israeli katika inchi ya Misri, vikundi-vikundi.”*+ 27 Ni wao walisema na Farao, mufalme wa Misri, atoshe watu wa Israeli katika Misri. Ilikuwa huyu Musa na huyu Haruni.+
28 Katika siku hiyo wakati Yehova alisema na Musa katika inchi ya Misri, 29 Yehova akamuambia Musa: “Mimi ni Yehova. Umuambie Farao, mufalme wa Misri, kila jambo lenye ninakuambia.” 30 Kisha Musa akasema mbele ya Yehova: “Angalia! Niko muzito wa kusema,* kwa hiyo namna gani Farao atanisikiliza?”+
7 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Angalia, nimekufanya kuwa kama Mungu* kwa Farao, na Haruni ndugu yako atakuwa nabii wako.+ 2 Utarudilia mambo yote yenye nitakuamuru, na Haruni ndugu yako atazungumuza na Farao, na Farao ataruhusu Waisraeli watoke katika inchi yake. 3 Lakini mimi, nitaacha moyo wa Farao ukuwe mugumu,+ na nitafanya alama na miujiza mingi katika inchi ya Misri.+ 4 Lakini Farao hatawasikiliza, na nitaweka mukono wangu juu ya Misri na kutosha vikundi vyangu,* watu wangu, Waisraeli, katika inchi ya Misri kwa matendo makubwa ya hukumu.+ 5 Na hakika Wamisri watajua kwamba mimi ni Yehova+ wakati nitanyoosha mukono wangu juu ya Misri na kutosha Waisraeli kati yao.” 6 Musa na Haruni wakafanya mambo yenye Yehova alikuwa amewaamuru; ni vile walifanya kabisa. 7 Musa alikuwa na miaka makumi munane (80) na Haruni alikuwa na miaka makumi munane na tatu (83) wakati walizungumuza na Farao.+
8 Yehova akamuambia Musa na Haruni: 9 “Kama Farao anawaambia, ‘Mufanye muujiza,’ umuambie Haruni, ‘Kamata fimbo yako, uitupe chini mbele ya Farao.’ Itageuka kuwa nyoka mukubwa.”+ 10 Kwa hiyo Musa na Haruni wakaingia kwa Farao na kufanya kama vile Yehova alikuwa ameamuru. Haruni akatupa chini fimbo yake mbele ya Farao na watumishi wake, nayo ikageuka kuwa nyoka mukubwa. 11 Lakini, Farao akaita watu wenye hekima na walozi, na makuhani wenye kufanya uchawi wa Misri+ wao pia wakafanya muujiza uleule kwa uchawi wao.+ 12 Kila mumoja wao akatupa chini fimbo yake, na fimbo hizo zikageuka kuwa nyoka wakubwa; lakini fimbo ya Haruni ikameza fimbo zao. 13 Lakini, moyo wa Farao ukaendelea kuwa mugumu,+ na hakuwasikiliza, kama vile Yehova alikuwa amesema.
14 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Moyo wa Farao uko mugumu.+ Amekataa kuruhusu watu wangu waende. 15 Uende kukutana na Farao asubui. Angalia! Anatoka ili kuenda kwenye maji! Na unapaswa kusimama ili kukutana naye pembeni ya Muto Nile; na ubebe katika mukono wako ile fimbo yenye iligeuka kuwa nyoka.+ 16 Na unapaswa kumuambia, ‘Yehova Mungu wa Waebrania amenituma kwako,+ na anasema: “Ruhusu watu wangu waende ili waweze kunitumikia katika jangwa,” lakini mupaka sasa haujatii. 17 Yehova anasema hivi: “Kwa jambo hili utajua kwamba mimi ni Yehova.+ Angalia, ninapiga maji yenye kuwa katika Muto Nile kwa fimbo hii, na yatageuka kuwa damu. 18 Na samaki wenye kuwa katika Muto Nile watakufa, na Muto Nile utanuka, na Wamisri hawataweza kunywa maji ya Muto Nile.”’”
19 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Ambia Haruni, ‘Kamata fimbo yako na unyooshe mukono wako juu ya maji yote ya Misri,+ juu ya mito yake, juu ya mifereji yake,* juu ya tingitingi zake,+ na juu ya viziwa vyao vyote vya maji, ili yageuke kuwa damu.’ Kutakuwa damu katika inchi yote ya Misri, hata katika vyombo vya mbao na vya majiwe.” 20 Mara moja Musa na Haruni wakafanya kama vile Yehova alikuwa ameamuru. Haruni akainua fimbo na kupiga maji ya Muto Nile mbele ya Farao na watumishi wake, na maji yote yenye yalikuwa katika muto yakageuka kuwa damu.+ 21 Na samaki wenye walikuwa katika muto wakakufa,+ na muto ukaanza kunuka, na Wamisri hawakuweza kunywa maji ya Muto Nile,+ na damu ilikuwa katika inchi yote ya Misri.
22 Lakini makuhani wenye kufanya uchawi wa Misri wakafanya jambo lilelile kwa ufundi wao wa siri,+ kwa hiyo moyo wa Farao ukaendelea kuwa mugumu, na hakuwasikiliza, kama vile Yehova alikuwa amesema.+ 23 Kisha Farao akarudia kwenye nyumba yake, na tena hakuweka jambo hilo katika moyo wake. 24 Kwa hiyo Wamisri wote walikuwa wanachimba kuzunguka Muto Nile pande zote ili kutafuta maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya Muto Nile. 25 Na siku saba (7) zikapita kisha Yehova kupiga Muto Nile.
8 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Ingia kwa Farao na umuambie, ‘Yehova anasema hivi: “Ruhusu watu wangu waende ili waweze kunitumikia.+ 2 Kama unaendelea kukataa kuwaruhusu waende, nitaleta pigo la vyura katika inchi yako yote.+ 3 Na Muto Nile utajaa vyura, nao wataingia ndani ya nyumba yako, ndani ya chumba chako cha kulala, kwenye kitanda chako, ndani ya nyumba za watumishi wako na juu ya watu wako, ndani ya majiko yenu, na ndani ya vyombo vyenu vya kufinyangia unga.*+ 4 Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako, na juu ya watumishi wako wote.”’”
5 Kisha wakati fulani Yehova akamuambia Musa: “Ambia Haruni, ‘Nyoosha mukono wako pamoja na fimbo yako juu ya mito, mifereji ya Muto Nile, na tingitingi, na ufanye vyura wakuje juu ya inchi ya Misri.’” 6 Kwa hiyo Haruni akanyoosha mukono wake juu ya maji ya Misri, na vyura wakaanza kuja na kufunika inchi ya Misri. 7 Lakini, makuhani wenye kufanya uchawi wakafanya jambo lilelile kwa ufundi wao wa siri, na wakafanya vyura wakuje juu ya inchi ya Misri.+ 8 Kisha Farao akaita Musa na Haruni na kusema: “Mumulilie Yehova anitoshee mimi na watu wangu vyura hawa,+ kwa maana ninataka kuruhusu watu waende ili waweze kumutolea Yehova zabihu.” 9 Kisha Musa akamuambia Farao: “Ni wewe utaniambia wakati wenye ninapaswa kumulilia Mungu ili vyura watoke kwako, kwa watumishi wako, kwa watu wako, na nyumba zenu. Watabakia tu katika Muto Nile.” 10 Basi Farao akasema: “Kesho.” Kwa hiyo Musa akasema: “Itakuwa kama vile unasema ili ujue kwamba hakuna mutu mwingine mwenye kuwa kama Yehova Mungu wetu.+ 11 Vyura watatoka kwako, katika nyumba zenu, kwa watumishi wako, na kwa watu wako. Watabakia tu katika Muto Nile.”+
12 Kwa hiyo Musa na Haruni wakatoka mbele ya Farao, na Musa akamulilia Yehova kuhusu vyura wenye Mungu alikuwa ameleta juu ya Farao.+ 13 Kisha Yehova akafanya kama vile Musa alimuomba, na vyura wakaanza kufa ndani ya nyumba, viwanja, na mashamba. 14 Watu wakakusanya vyura hao marundo marundo, na inchi ikaanza kunuka. 15 Wakati Farao aliona kwamba hali imekuwa muzuri, akafanya moyo wake ukuwe mugumu,+ na akakataa kuwasikiliza, kama vile Yehova alikuwa amesema.
16 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Ambia Haruni, ‘Nyoosha fimbo yako na upige mavumbi ya dunia, na yatakuwa imbu katika inchi yote ya Misri.’” 17 Nao wakafanya vile. Haruni akanyoosha mukono wake pamoja na fimbo yake na kupiga mavumbi ya dunia, na imbu wakakuja juu ya watu na wanyama. Mavumbi yote ya dunia yakageuka kuwa imbu katika inchi yote ya Misri.+ 18 Makuhani wenye kufanya uchawi wakajaribu kufanya jambo lilelile na kutokeza imbu kwa ufundi wao wa siri,+ lakini hawakuweza. Na imbu wakakuja juu ya watu na wanyama. 19 Kwa hiyo makuhani wenye kufanya uchawi wakamuambia Farao: “Ni kidole cha Mungu!”+ Lakini moyo wa Farao ukaendelea kuwa mugumu, na hakuwasikiliza, kama vile Yehova alikuwa amesema.
20 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Amuka asubui sana na usimame mbele ya Farao. Angalia! Anatoka ili aende kwenye maji! Na unapaswa kumuambia, ‘Yehova anasema hivi: “Ruhusu watu wangu waende ili waweze kunitumikia. 21 Lakini kama hauruhusu watu wangu waende, nitatuma mainzi* juu yako, juu ya watumishi wako, na juu ya watu na ndani ya nyumba zenu; na nyumba za Misri zitajaa mainzi, nao wataingia katika nyumba zenu; na nyumba za Misri zitajaa mainzi, na hata watafunika udongo wenye wao* wanasimama juu yake. 22 Siku hiyo nitaweka pembeni inchi ya Gosheni, mahali kwenye watu wangu wanaishi. Hakuna mainzi wenye watapatikana kule,+ na kwa jambo hilo utajua kwamba mimi, Yehova, niko katika inchi hii.+ 23 Na nitafanya kukuwe tofauti kati ya watu wangu na watu wako. Kesho alama hii itatokea.”’”
24 Na Yehova akafanya vile; na makundi makubwa ya mainzi yakaanza kushambulia nyumba ya Farao na nyumba za watumishi wake na inchi yote ya Misri.+ Inchi ikaharibiwa na mainzi hayo.+ 25 Mwishowe, Farao akaita Musa na Haruni na kusema: “Muende, mumutolee Mungu wenu zabihu katika inchi.” 26 Lakini Musa akasema: “Haiko muzuri kufanya vile, kwa sababu zabihu zenye tutamutolea Yehova Mungu wetu zitachukiza Wamisri.+ Kama tunatoa zabihu zenye kuchukiza Wamisri mbele ya macho yao, je, hawatatupiga majiwe? 27 Tutafanya safari ya siku tatu (3) katika jangwa, na kule tutamutolea Yehova Mungu wetu zabihu, kama vile alituambia.”+
28 Sasa Farao akasema: “Nitawaruhusu muende ili mumutolee Yehova Mungu wenu zabihu katika jangwa. Lakini tu, musiende mbali sana. Muniombee.”+ 29 Kisha Musa akasema: “Sasa ninatoka mbele yako, na nitamulilia Yehova, na mainzi watatoka kwa Farao, kwa watumishi wake, na kwa watu wake kesho. Lakini Farao anapaswa kuacha kutuchezea* kwa kukataa kuruhusu watu waende kumutolea Yehova zabihu.”+ 30 Basi Musa akatoka mbele ya Farao na akamulilia Yehova.+ 31 Kwa hiyo Yehova akafanya kama vile Musa alisema, na mainzi wakatoka kwa Farao, kwa watumishi wake, na kwa watu wake. Hakuna hata inzi mumoja mwenye alibakia. 32 Lakini, Farao akafanya tena moyo wake kuwa mugumu na hakuruhusu watu waende.
9 Kwa hiyo Yehova akamuambia Musa: “Ingia kwa Farao na umuambie, ‘Yehova Mungu wa Waebrania anasema hivi: “Ruhusu watu wangu waende ili waweze kunitumikia.+ 2 Lakini kama unakataa kuwaruhusu waende na ukiendelea kuwazuia, 3 angalia! mukono wa Yehova+ utakuja juu ya mifugo yenye kuwa katika eneo la mashamba. Kutakuwa pigo kali juu ya farasi, punda, ngamia, mifugo, na makundi.+ 4 Na hakika Yehova atafanya kukuwe tofauti kati ya mifugo ya Israeli na mifugo ya Misri, na hakuna munyama wa Waisraeli mwenye atakufa.”’”+ 5 Tena, Yehova akaweka wakati wa kufanya vile, na kusema: “Kesho Yehova atafanya jambo hilo katika inchi.”
6 Na Yehova akafanya vile siku yenye ilifuata, na kila aina ya mifugo ya Misri ikaanza kufa,+ lakini hakuna munyama yeyote kati ya mifugo ya Israeli mwenye alikufa. 7 Wakati Farao aliuliza watu, angalia! hakuna munyama hata mumoja kati ya mifugo ya Israeli mwenye alikuwa amekufa. Lakini, moyo wa Farao ukaendelea kuwa mugumu, na hakuruhusu watu waende.+
8 Kisha Yehova akaambia Musa na Haruni: “Mujaze majivu meusi ya tanuru katika mikono yenu mbili, na Musa anapaswa kuyatupa katika hewa mbele ya Farao. 9 Na yatageuka kuwa mavumbi laini juu ya inchi yote ya Misri, na yatageuka kuwa majipu yenye usaha kwenye miili ya watu na wanyama katika inchi yote ya Misri.”
10 Kwa hiyo wakakamata majivu meusi ya tanuru na kusimama mbele ya Farao, na Musa akayatupa katika hewa, na yakageuka kuwa majipu yenye usaha na yenye kupasuka kwenye miili ya watu na wanyama. 11 Makuhani wenye kufanya uchawi hawakuweza kusimama mbele ya Musa kwa sababu ya majipu, kwa maana majipu hayo yalikuwa yametokea juu ya makuhani wenye kufanya uchawi na juu ya Wamisri wote.+ 12 Lakini Yehova akaacha moyo wa Farao ukuwe mugumu, na hakuwasikiliza, kama vile Yehova alikuwa amemuambia Musa.+
13 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Amuka asubui sana na usimame mbele ya Farao, na umuambie, ‘Yehova Mungu wa Waebrania anasema hivi: “Ruhusu watu wangu waende ili waweze kunitumikia. 14 Kwa maana wakati huu ninatuma mapigo yangu ili kupiga moyo wako, watumishi wako, na watu wako, kusudi uweze kujua kwamba hakuna mwenye kuwa kama mimi katika dunia yote.+ 15 Kwa maana kufikia sasa ningekuwa nimenyoosha mukono wangu ili kukupiga wewe na watu wako kwa pigo kali, na ungekuwa umeondolewa* juu ya dunia. 16 Lakini nimekuacha uendelee kuishi kwa sababu hii: ili nikuonyeshe nguvu zangu na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.+ 17 Je, ungali unajiendesha kwa kiburi kwa kukataa kuruhusu watu wangu waende? 18 Kesho, wakati kama huu, nitaleta mvua kubwa sana ya majiwe yenye hakuna siku imetokea katika inchi ya Misri tangu wakati musingi wake uliwekwa mupaka sasa. 19 Kwa hiyo, ambia watu watoshe mifugo yako yote na vitu vyako vyote vyenye kuwa katika eneo la mashamba na kuvileta mahali salama. Kila mutu na kila munyama mwenye atapatikana katika eneo la mashamba na mwenye hataletwa katika nyumba atakufa wakati mvua ya majiwe itaanguka juu yao.”’”
20 Kila mutu kati ya watumishi wa Farao mwenye aliogopa neno la Yehova akaleta haraka watumishi wake mwenyewe na mifugo yake katika nyumba, 21 lakini kila mutu mwenye hakuweka katika moyo wake neno la Yehova aliacha watumishi wake na mifugo yake katika eneo la mashamba.
22 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Nyoosha mukono wako kuelekea mbinguni, ili mvua ya majiwe ianguke juu ya inchi yote ya Misri,+ juu ya watu na wanyama na juu ya mimea yote ya mashamba katika inchi ya Misri.”+ 23 Kwa hiyo Musa akanyoosha fimbo yake kuelekea mbinguni, na Yehova akatuma mingurumo ya radi na mvua ya majiwe, na moto* ukashuka juu ya dunia, na Yehova akaendelea kufanya mvua ya majiwe inyeshe juu ya inchi ya Misri. 24 Kulikuwa mvua ya majiwe, na moto ulikuwa unawaka katikati ya mvua hiyo ya majiwe. Mvua hiyo ya majiwe ilikuwa kubwa sana; hakuna siku mvua ya majiwe kama hiyo ilikuwa imenyesha katika inchi tangu wakati Misri ilikuwa taifa.+ 25 Mvua hiyo ya majiwe ilipiga kila kitu katika eneo lote la mashamba la inchi ya Misri, kuanzia mutu mupaka munyama, na ilipiga mimea yote na kuvunja-vunja miti yote ya mashamba.+ 26 Ni katika inchi ya Gosheni tu, mahali Waisraeli walikuwa, ndio mvua hiyo ya majiwe haikukuwa.+
27 Kwa hiyo Farao akatuma watu ili Musa na Haruni waletwe na akawaambia: “Mara hii nimefanya zambi. Yehova ni mwenye haki, lakini mimi na watu wangu tumekosea. 28 Mumulilie Yehova ili mingurumo ya radi na mvua hii ya majiwe ya Mungu imalizike. Kisha nitakuwa tayari kuwaruhusu muende, na hamutaendelea kukaa hapa.” 29 Kwa hiyo Musa akamuambia: “Wakati tu nitatoka katika muji, nitanyoosha mikono yangu mbele ya Yehova. Mingurumo ya radi itamalizika na mvua ya majiwe haitaendelea tena, ili uweze kujua kwamba dunia ni ya Yehova.+ 30 Lakini kuhusu wewe na watumishi wako, tayari ninajua kwamba hata wakati huo, hamutamuogopa Yehova Mungu.”
31 Sasa mimea ya kitani na mimea ya shayiri ilikuwa imepigwa, kwa sababu mimea ya shayiri ilikuwa na masuke na mimea ya kitani ilikuwa imetoa matumba ya maua. 32 Lakini ngano na ngano ya kusemeti haikupigwa kwa sababu ilikuwa haijakomaa.* 33 Sasa Musa akatoka katika muji mbele ya Farao na akanyoosha mikono yake mbele ya Yehova na mingurumo ya radi na mvua ya majiwe ikaisha na mvua ikaacha kumwangika juu ya dunia.+ 34 Wakati Farao aliona kwamba mvua, mvua ya majiwe, na mingurumo ya radi vimeisha, akatenda zambi tena na akafanya moyo wake ukuwe mugumu,+ yeye pamoja na watumishi wake. 35 Na moyo wa Farao ukaendelea kuwa mugumu, na hakuruhusu Waisraeli waende, kama vile Yehova alikuwa amemuambia Musa.+
10 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Ingia kwa Farao, kwa sababu nimeacha moyo wake na mioyo ya watumishi wake ikuwe migumu,+ ili nionyeshe alama zangu hizi mbele yake,+ 2 na ili muweze kuelezea wana wenu na wajukuu wenu namna nilitendea Misri kwa ukali na alama zenye nilifanya kati yao;+ na hakika mutajua kwamba mimi ni Yehova.”
3 Kwa hiyo Musa na Haruni wakaingia kwa Farao na kumuambia: “Yehova Mungu wa Waebrania anasema hivi: ‘Utakataa kujinyenyekeza kwangu mupaka wakati gani?+ Ruhusu watu wangu waende ili waweze kunitumikia. 4 Kwa maana kama unaendelea kukataa kuruhusu watu wangu waende, angalia, kesho nitaleta nzige ndani ya mipaka yako. 5 Na nzige watafunika uso wa dunia, na haitawezekana kuona udongo. Watakula kila kitu chenye kilibakia kisha mvua ya majiwe na chenye kiliachwa kwa ajili yenu, na watakula miti yenu yote yenye kuota katika eneo la mashamba.+ 6 Watajaa ndani ya nyumba zako, ndani ya nyumba za watumishi wako wote, na ndani ya nyumba zote za Misri kwa kadiri yenye baba zako na mababu zako hawajapata kuona tangu wakati walikuwa katika inchi hii mupaka leo.’”+ Kisha akatoka mbele ya Farao.
7 Kisha watumishi wa Farao wakamuambia: “Mutu huyu ataendelea kuwa hatari kwetu* mupaka wakati gani? Ruhusu Waisraeli waende ili waweze kumutumikia Yehova Mungu wao. Je, hauone kwamba Misri imeangamia?” 8 Kwa hiyo Musa na Haruni wakarudishwa kwa Farao, naye akawaambia: “Muende, mumutumikie Yehova Mungu wenu. Lakini ni nani kabisa wataenda?” 9 Kisha Musa akasema: “Tutaenda pamoja na vijana wetu, wazee wetu, watoto wetu wanaume, na watoto wetu wanamuke, kondoo zetu, na ngombe zetu,+ kwa maana tutamufanyia Yehova sikukuu.”+ 10 Farao akawaambia: “Kama nitawaruhusu ninyi na watoto wenu muende, basi Yehova iko* kabisa pamoja na ninyi!+ Ni wazi kwamba muko na nia ya kufanya jambo fulani la mubaya. 11 Hapana! Ni wanaume wenu tu ndio wanaweza kuenda na kumutumikia Yehova, kwa sababu ni kile muliomba.” Kwa hiyo wakafukuzwa mbele ya Farao.
12 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Nyoosha mukono wako juu ya inchi ya Misri ili nzige wakuje juu ya inchi ya Misri na kula mimea yote ya inchi, kila kitu chenye majiwe ya mvua yaliacha.” 13 Mara moja Musa akanyoosha fimbo yake juu ya inchi ya Misri, na Yehova akafanya upepo wa mashariki uvume juu ya inchi muchana wote na usiku wote. Wakati asubui ilifika, upepo huo wa mashariki ukaleta nzige. 14 Na nzige hao wakakuja juu ya inchi yote ya Misri na wakashuka juu ya eneo lote la Misri.+ Hali ilikuwa mubaya sana,+ na hakuna siku kulikuwa kumetokea nzige wengi sana hivyo, na hakuna siku kungekuwa tena nzige wengi kama hao. 15 Walifunika uso wa inchi yote, na inchi ikakuwa na giza kwa sababu yao, nao wakakula mimea yote ya inchi na matunda yote ya miti yenye majiwe ya mvua yalikuwa yameacha; hakuna majani yenye yalibakia juu ya miti wala juu ya mimea ya mashamba yenye yalibakia katika inchi yote ya Misri.
16 Kwa hiyo Farao akaita haraka Musa na Haruni na kusema: “Nimetenda zambi juu ya Yehova Mungu wenu na juu yenu. 17 Sasa, tafazali, musamehe zambi yangu mara hii moja tu, na mumulilie Yehova Mungu wenu ili anitoshee pigo hili lenye kuleta kifo.” 18 Kwa hiyo akatoka* mbele ya Farao na kumulilia Yehova.+ 19 Kisha Yehova akageuza upepo huo, nao ukaanza kuvuma kwa nguvu kuelekea mangaribi, nao ukapeperusha nzige hao na kuwapeleka katika Bahari Nyekundu. Hakuna hata nzige mumoja mwenye alibakia katika eneo lote la Misri. 20 Lakini, Yehova akaacha moyo wa Farao ukuwe mugumu,+ na hakuruhusu Waisraeli waende.
21 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Nyoosha mukono wako kuelekea mbinguni ili kukuwe giza juu ya inchi ya Misri, giza nzito lenye linaweza kuguswa.” 22 Mara moja Musa akanyoosha mukono wake kuelekea mbinguni, na kukakuwa giza nzito katika inchi yote ya Misri kwa siku tatu (3).+ 23 Hakuna mwenye alikuwa anaona mwingine, na hakuna mwenye alitoka mahali alikuwa kwa siku tatu (3); lakini Waisraeli wote walikuwa na mwangaza katika makao yao.+ 24 Kisha Farao akaita Musa na kusema: “Muende, mumutumikie Yehova.+ Ni kondoo zenu na ngombe zenu tu ndio watabakia. Hata watoto wenu wanaweza kuenda pamoja na ninyi.” 25 Lakini Musa akasema: “Wewe mwenyewe pia utatupatia* zabihu na matoleo ya kuteketezwa, na tutayatolea Yehova Mungu wetu.+ 26 Mifugo yetu itaenda pia pamoja na sisi. Hakuna munyama mwenye atabakia,* kwa sababu tutatumia wanyama fulani kati yao ili kumuabudu Yehova Mungu wetu, na hatujue kile tutatoa ili kumuabudu Yehova mupaka wakati tutafika kule.” 27 Kwa hiyo Yehova akaacha moyo wa Farao ukuwe mugumu, na hakukubali kuwaruhusu waende.+ 28 Farao akamuambia: “Toka mbele ya macho yangu! Usipime kutafuta kuona uso wangu tena, kwa maana siku yenye utaona uso wangu, utakufa.” 29 Kwa hiyo Musa akasema: “Kama vile umesema, sitatafuta kuona uso wako tena.”
11 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Nitaleta pigo moja zaidi juu ya Farao na Misri. Kisha pigo hilo atawaruhusu mutoke hapa.+ Wakati atawaruhusu muende, atawafukuza kabisa mutoke hapa.+ 2 Sasa ambia watu kwamba wanaume wote na wanamuke wanapaswa kuomba majirani wao vitu vya feza na zahabu.”+ 3 Na Yehova akafanya watu wakubaliwe mbele ya macho ya Wamisri. Tena, Musa mwenyewe alifikia kuwa mutu mwenye kuheshimiwa sana katika inchi ya Misri kati ya watumishi wa Farao na kati ya watu.
4 Kisha Musa akasema: “Yehova anasema hivi: ‘Karibu katikati ya usiku nitapita katikati ya Misri,+ 5 na kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri atakufa,+ kuanzia muzaliwa wa kwanza wa Farao mwenye kukaa kwenye kiti chake cha ufalme mupaka muzaliwa wa kwanza wa mutumwa mwanamuke mwenye kufanya kazi juu ya jiwe la kusagia la mukono, na kila muzaliwa wa kwanza wa mifugo.+ 6 Kutakuwa kilio kikubwa katika inchi yote ya Misri, kilio chenye hakuna siku kimekwisha kutokea na hakuna siku kitapata kutokea tena.+ 7 Lakini hakuna hata imbwa mumoja mwenye atafokea* Waisraeli, ikuwe watu ao mifugo yao, ili muweze kujua kwamba Yehova anaweza kufanya kukuwe tofauti kati ya Wamisri na Waisraeli.’”+ 8 Na watumishi wako wote hakika watakuja mbele yangu na kuinamisha uso mupaka chini mbele yangu, na kusema, ‘Uende, wewe pamoja na watu wote wenye kukufuata.’+ Na kisha mambo hayo nitaondoka.” Basi akatoka mbele ya Farao akiwa amewaka kasirani.
9 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Farao hatakusikiliza,+ ili miujiza yangu iongezeke katika inchi ya Misri.”+ 10 Musa na Haruni walifanya miujiza hiyo yote mbele ya Farao,+ lakini Yehova aliacha moyo wa Farao ukuwe mugumu, na hivyo Farao hakuruhusu Waisraeli watoke katika inchi yake.+
12 Sasa Yehova akamuambia Musa na Haruni katika inchi ya Misri: 2 “Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu. Utakuwa mwezi wa kwanza wa mwaka kwenu.+ 3 Museme na mukusanyiko wote wa Israeli, na kuwaambia: ‘Siku ya kumi (10) ya mwezi huu, kila mumoja wao anapaswa kujikamatia kondoo mumoja+ kwa ajili ya nyumba ya baba yake, kondoo mumoja kwa kila nyumba. 4 Lakini kama watu wa nyumba hiyo wako kidogo na hivyo hawawezi kumaliza kondoo mumoja, watamugawanya katika nyumba yao pamoja na jirani yao* wa karibu kulingana na hesabu ya watu.* Wakati mutafanya hesabu ya watu, mukadirie kiasi cha nyama ya kondoo chenye kila mutu atakula. 5 Kondoo anapaswa kuwa bila kasoro,+ kondoo-dume wa mwaka mumoja. Munaweza kumuchagua kati ya wana-kondoo dume ao kati ya mbuzi. 6 Munapaswa kumuchunga mupaka siku ya kumi na ine (14) ya mwezi huu,+ na kutaniko lote la mukusanyiko wa Israeli linapaswa kumuchinja mangaribi wakati giza linaanza.*+ 7 Wanapaswa kukamata sehemu fulani ya damu na kuipakaa kwenye miimo mbili ya mulango na kwenye sehemu ya juu ya mulango wa nyumba yenye watakulia ndani munyama huyo.+
8 “‘Wanapaswa kula nyama hiyo usiku huo.+ Wataichoma juu ya moto na kuikula pamoja na mikate yenye haina chachu+ na mboga chungu za majani.+ 9 Musikule nyama hiyo ikiwa mubichi ao ikiwa imetokoteshwa, lakini muichome juu ya moto, kichwa chake pamoja na miguu yake na sehemu zake za ndani. 10 Musiache nyama yoyote mupaka asubui, lakini nyama yoyote yenye itabakia munapaswa kuiteketeza kwa moto.+ 11 Na mutaikula hivi: mutakuwa mumejifunga mikaba* yenu,* mutakuwa mumevaa viatu kwenye miguu yenu, na mutakuwa na fimbo zenu katika mikono yenu; na mutaikula haraka-haraka. Ni Pasaka ya Yehova. 12 Kwa maana nitapita katikati ya inchi ya Misri usiku huo na kuua kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri, kuanzia mwanadamu mupaka munyama;+ na nitaleta hukumu juu ya miungu yote ya Misri.+ Mimi ni Yehova. 13 Ile damu itakuwa alama juu ya nyumba zenye muko ndani yake; na nitaona damu hiyo na kupita juu yenu, na pigo halitakuja juu yenu ili kuwaharibu wakati nitapiga inchi ya Misri.+
14 “‘Munapaswa kukumbuka siku hiyo, na katika siku hiyo munapaswa kumufanyia Yehova sikukuu katika vizazi vyenu vyote. Munapaswa kuifanya kwa sababu ni sheria ya kudumu. 15 Mutakula mikate yenye haina chachu kwa siku saba (7).+ Ndiyo, siku ya kwanza mutaondoa katika nyumba zenu unga wenye ulifinyangwa na wenye kuwa na chachu, kwa sababu mutu mwenye atakula kitu chenye kuwa na chachu kuanzia siku ya kwanza mupaka siku ya saba, mutu huyo anapaswa* kuondolewa* katika Israeli. 16 Siku ya kwanza mutafanya mukusanyiko mutakatifu, na siku ya saba (7) mutafanya mukusanyiko mwingine mutakatifu. Hakuna kazi yenye inapaswa kufanywa siku hizo.+ Isipokuwa tu kile chenye kila mutu* iko* na lazima ya kula, ni kile tu kinaweza kutayarishwa kwa ajili yenu.
17 “‘Katika siku hiyo munapaswa kufanya Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu,+ kwa sababu siku hiyo, nitatosha makundi yenu makubwa* katika inchi ya Misri. Na munapaswa kushika siku hiyo katika vizazi vyenu vyote kwa kuwa ni sheria ya kudumu. 18 Katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na ine (14) ya mwezi huo, mangaribi, mutakula mikate yenye haina chachu mupaka siku ya makumi mbili na moja (21) ya mwezi huo, mangaribi.+ 19 Hakuna unga wenye kufinyangwa na wenye kuwa na chachu wenye unapaswa kupatikana katika nyumba zenu kwa muda wa siku saba (7), kwa sababu kila mutu mwenye anakula kitu chenye kuwa na chachu, akuwe mugeni ao mwenyeji wa inchi,+ mutu huyo anapaswa* kuondolewa* katikati ya mukusanyiko wa Israeli.+ 20 Hamupaswe kula kitu chochote chenye kuwa na chachu. Katika nyumba zenu zote, munapaswa kula mikate yenye haina chachu.”
21 Mara moja Musa akaita wazee wote wa Israeli+ na kuwaambia: “Muende muchague wanyama wadogo* kwa ajili ya kila moja ya familia zenu, na muchinje zabihu ya Pasaka. 22 Kisha mutachovya majani ya hisopo katika damu yenye kuwa ndani ya beseni na kuipakaa kwenye sehemu ya juu ya mulango na kwenye miimo yake mbili; na mutu yeyote asitoke inje ya nyumba yake mupaka asubui. 23 Kisha wakati Yehova atapita ili kupiga Wamisri na kuona damu kwenye sehemu ya juu ya mulango na kwenye miimo mbili ya mulango, hakika Yehova atapita juu ya ule mulango, na hataruhusu pigo la kifo* liingie katika nyumba zenu.+
24 “Munapaswa kukumbuka tukio hili kwa kuwa ni sharti la kudumu kwa ajili yenu na kwa ajili ya wana wenu.+ 25 Na wakati mutaingia katika inchi yenye Yehova atawapatia kama vile amesema, munapaswa kuendelea kukumbuka tukio hilo.+ 26 Na wakati wana wenu watawauliza, ‘Sababu gani munafanya sikukuu hii?’+ 27 mutawaambia, ‘Ni zabihu ya Pasaka kwa ajili ya Yehova, mwenye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika Misri wakati alipiga Wamisri, lakini aliacha nyumba zetu.’”
Kisha watu wakainama na kushusha uso chini. 28 Kwa hiyo Waisraeli wakaenda na kufanya kama vile Yehova alikuwa ameamuru Musa na Haruni.+ Ni vile walifanya kabisa.
29 Kwa hiyo katikati ya usiku, Yehova akapiga na kuua kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri,+ kuanzia muzaliwa wa kwanza wa Farao mwenye alikuwa anakaa kwenye kiti chake cha ufalme mupaka muzaliwa wa kwanza wa mutu mwenye alitekwa mwenye alikuwa katika gereza,* na kila muzaliwa wa kwanza wa wanyama.+ 30 Farao akaamuka usiku huo pamoja na watumishi wake wote na Wamisri wengine wote, na kulikuwa kilio kikubwa kati ya Wamisri, kwa sababu hapakukuwa nyumba yenye haikukuwa na mutu mwenye kufa.+ 31 Mara moja akaita Musa na Haruni+ usiku na kusema: “Musimame, mutoke kati ya watu wangu, ninyi na Waisraeli wengine. Muende na mumutumikie Yehova, kama vile mumesema.+ 32 Mukamate pia makundi yenu na mifugo yenu na muende, kama vile mumesema.+ Lakini munapaswa pia kunibariki.”
33 Na Wamisri wakaanza kuambia watu watoke haraka+ katika inchi, “kwa sababu,” walisema, “ni kama vile sisi wote tumekufa!”+ 34 Kwa hiyo watu wakabeba unga wao wenye ulikuwa umefinyangwa mbele hawajaweka ndani chachu, na pia wakabeba vyombo vyao vya kufinyangia unga,* wakavifunga kwa nguo zao na kuvibeba kwenye mabega yao. 35 Waisraeli wakafanya kama vile Musa alikuwa amewaambia na wakaomba Wamisri vitu vya feza na zahabu na pia nguo.+ 36 Yehova akafanya Waisraeli wakubaliwe mbele ya macho ya Wamisri, na hivyo Wamisri wakawapatia kile chenye waliomba, na Waisraeli wakanyanganya vitu vya Wamisri.+
37 Kisha Waisraeli wakatoka Ramesesi+ na kuenda Sukoti,+ wanaume karibu elfu mia sita (600 000) wenye kutembea kwa miguu, bila kuhesabu watoto.+ 38 Na kikundi kikubwa cha watu wenye kuchangamana*+ walienda pia pamoja nao, na pia makundi na mifugo, mifugo mingi sana. 39 Wakaanza kupika mikate ya muviringo yenye haikukuwa na chachu kwa kutumia unga wenye walitosha Misri. Unga huo haukukuwa na chachu kwa sababu walifukuzwa haraka kutoka Misri na hawakukuwa wametayarisha chakula chochote kwa ajili ya safari.+
40 Na muda wenye Waisraeli walikuwa wamekaa katika inchi ya Misri+ ilikuwa miaka mia ine makumi tatu (430).+ 41 Wakati miaka hiyo mia ine makumi tatu (430) ilimalizika, siku ileile, vikundi vyote* vya Yehova vikatoka katika inchi ya Misri. 42 Ni usiku wenye Waisraeli watakumbuka namna Yehova aliwatosha katika inchi ya Misri. Usiku huo unapaswa kukumbukwa na watu wote wa Israeli katika vizazi vyao vyote ili kuonyesha heshima kwa Yehova.+
43 Kisha Yehova akaambia Musa na Haruni, “Hii ndiyo sheria ya Pasaka: Hakuna mugeni mwenye ataikula.+ 44 Lakini kama mutu iko* na mutumwa mwenye alinunuliwa kwa feza, unapaswa kumutahiri.+ Ni kisha kufanya vile tu ndio anaweza kuikula. 45 Muhamiaji na mufanyakazi wa kulipwa hataikula. 46 Itakuliwa ndani ya nyumba moja tu. Hamupaswe kupeleka nyama yoyote inje ya nyumba hiyo, na hamupaswe kuvunja mufupa wowote wa munyama huyo.+ 47 Mukusanyiko wote wa Israeli utafanya Pasaka. 48 Kama mugeni fulani mwenye kukaa pamoja na wewe anataka kumufanyia Yehova Pasaka, kila mwanaume wa nyumba yake anapaswa kutahiriwa. Kisha anaweza kukaribia ili kufanya sikukuu ya Pasaka, na atakuwa kama mwenyeji wa inchi. Lakini mwanaume mwenye hatahiriwe hapaswe kula chakula cha Pasaka.+ 49 Sheria moja itatumika kwa ajili ya mwenyeji na kwa ajili ya mugeni mwenye kuishi kati yenu.”+
50 Kwa hiyo Waisraeli wote wakafanya kama vile Yehova alikuwa ameamuru Musa na Haruni. Ni vile walifanya kabisa. 51 Katika siku hiyohiyo, Yehova alitosha Waisraeli pamoja na vikundi vyao* katika inchi ya Misri.
13 Yehova akazungumuza tena na Musa, na kusema: 2 “Nitakasie* kila muzaliwa wa kwanza mwanaume* kati ya Waisraeli. Muzaliwa wa kwanza mwanaume, wa mwanadamu na wa munyama ni wangu.”+
3 Kisha Musa akaambia watu: “Mukumbuke siku hii yenye mulitoka Misri,+ katika nyumba ya utumwa, kwa sababu kwa mukono wenye nguvu Yehova aliwatosha hapa.+ Kwa hiyo musikule kitu chochote chenye kuwa na chachu. 4 Munaondoka leo, katika mwezi wa Abibu.*+ 5 Wakati Yehova atakuwa amewaingiza katika inchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi, na Wayebusi,+ inchi yenye aliapia mababu zenu kwamba atawapatia,+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali,+ basi mutafanya sikukuu hii katika mwezi huu. 6 Mutakula mikate yenye haina chachu kwa siku saba (7),+ na katika siku ya saba, kutakuwa sikukuu kwa ajili ya Yehova. 7 Mikate yenye haina chachu itakuliwa kwa siku hizo saba (7);+ na kitu chochote chenye kuwa na chachu hakipaswe kupatikana kwako,+ na unga wowote wenye kufinyangwa na wenye kuwa na chachu haupaswe kupatikana katika eneo* lako lote. 8 Na unapaswa kumuambia mwana wako katika siku hiyo, ‘Ni kwa sababu ya mambo yenye Yehova alinifanyia wakati nilitoka katika inchi ya Misri.’+ 9 Na hii itakuwa alama kwenye mukono wako na ukumbusho* kwenye paji la uso wako,*+ ili sheria ya Yehova ikuwe katika kinywa chako, kwa maana Yehova alikutosha katika Misri kwa mukono wenye nguvu. 10 Unapaswa kushika sheria hii kila mwaka kwa wakati wake wenye uliwekwa.+
11 “Wakati Yehova atakuingiza katika inchi ya Wakanaani, yenye alikuapia wewe na mababu zako kwamba atakupatia,+ 12 unapaswa kumupatia Yehova kila muzaliwa wa kwanza mwanaume,* na pia kila muzaliwa wa kwanza wa kiume wa mifugo yako. Wazaliwa hao wa kiume ni wa Yehova.+ 13 Kila muzaliwa wa kwanza wa punda utamukomboa na kondoo; na kama haumukomboe, basi utamuvunja shingo. Na kila muzaliwa wa kwanza mwanaume wa wana wako utamukomboa.+
14 “Kama siku moja mwana wako anakuuliza, ‘Hii maana yake nini?’ basi utamuambia, ‘Kwa mukono wenye nguvu Yehova alitutosha Misri, katika nyumba ya utumwa.+ 15 Wakati Farao alikataa kwa kichwa-nguvu kuturuhusu tuende,+ Yehova aliua kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri, kuanzia muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu mupaka muzaliwa wa kwanza wa munyama.+ Ndiyo sababu ninamutolea Yehova wazaliwa wote wa kwanza wa kiume* kuwa zabihu, na ninakomboa kila muzaliwa wa kwanza kati ya wana wangu.’ 16 Hiyo itakuwa alama kwenye mukono wako na utepe wa kichwa kwenye paji la uso wako,*+ kwa sababu Yehova alitutosha Misri kwa mukono wenye nguvu.”
17 Sasa wakati Farao aliwaruhusu Waisraeli waende, Mungu hakuwapitisha katika inchi ya Wafilisti, hata kama njia hiyo ilikuwa ya karibu. Kwa maana Mungu alisema: “Watu hawa wanaweza kubadilisha nia yao na kurudia Misri kama vita inawatokea.” 18 Kwa hiyo Mungu akafanya watu wazunguke kupitia njia ya jangwa la Bahari Nyekundu.+ Lakini Waisraeli walitoka katika inchi ya Misri wakiwa wamejipanga kwa ajili ya vita. 19 Pia Musa alibeba mifupa ya Yosefu, kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli kwa uzito: “Mungu hatakosa kuelekeza uangalifu wake juu yenu, na munapaswa kutosha mifupa yangu hapa na kuenda nayo.”+ 20 Wakatoka Sukoti na kupiga kambi Etamu, pembeni-pembeni ya jangwa.
21 Sasa Yehova alikuwa anaenda mbele yao muchana katika nguzo ya wingu ili awaongoze katika njia,+ na wakati wa usiku katika nguzo ya moto ili awaangazie katika njia, kusudi waweze kusafiri muchana na usiku.+ 22 Ile nguzo ya wingu haikukuwa inatoka mbele ya watu wakati wa muchana, wala ile nguzo ya moto wakati wa usiku.+
14 Sasa Yehova akamuambia Musa: 2 “Ambia Waisraeli kwamba wanapaswa kurudia nyuma na kupiga kambi mbele ya Pihahiroti, katikati ya Migdoli na bahari, kuangaliana na Baal-sefoni.+ Mutapiga kambi mbele ya mahali pale karibu na bahari. 3 Kisha Farao atasema kuhusu Waisraeli, ‘Wanatanga-tanga kwa sababu wamevurugika katika inchi. Jangwa limewafungia ndani wasiweze kutoka.’ 4 Nitaacha moyo wa Farao ukuwe mugumu,+ na atawafuatilia, na mimi nitajitukuza kupitia Farao na jeshi lake lote;+ na hakika Wamisri watajua kwamba mimi ni Yehova.”+ Basi ni vile Waisraeli walifanya.
5 Kisha wakati fulani mufalme wa Misri akaambiwa kwamba watu wamekimbia. Mara moja moyo wa Farao na wa watumishi wake ukabadilika kuhusu watu hao,+ na wakasema: “Sababu gani tumefanya jambo hili na kuruhusu Israeli waache kututumikia kama watumwa?” 6 Kwa hiyo akatayarisha magari yake ya vita, na akaenda pamoja na watu wake.+ 7 Akakamata magari mia sita (600) yenye yalikuwa ya pekee na magari mengine yote ya Misri, na kila gari lilikuwa na wapiganaji-vita. 8 Kwa hiyo Yehova akaacha moyo wa Farao mufalme wa Misri ukuwe mugumu, na Farao akafuatilia Waisraeli, wakati Waisraeli walikuwa wanatoka katika inchi bila woga.*+ 9 Wamisri wakawafuatilia,+ na farasi wote wa magari ya Farao na maaskari wake wapanda-farasi na jeshi lake wakawafikia Waisraeli wakati walikuwa wanapiga kambi pembeni ya bahari, karibu na Pihahiroti, mbele ya Baal-sefoni.
10 Wakati Farao alikaribia, Waisraeli wakainua macho yao na kuona Wamisri wanawafuatilia. Waisraeli wakaogopa sana na wakaanza kumulilia Yehova.+ 11 Wakamuambia Musa: “Je, ni kwa sababu hakuna makaburi katika Misri ndiyo sababu umetuleta hapa ili tukufe katika jangwa?+ Ni jambo gani hili umetutendea kwa kututosha Misri? 12 Je, haiko jambo hili tulikuambia kule Misri wakati tulisema, ‘Utuache tutumikie Wamisri’? Kwa maana ni muzuri zaidi kwa upande wetu tutumikie Wamisri kuliko kufa katika jangwa.”+ 13 Kisha Musa akaambia watu: “Musiogope.+ Musimame imara na muone wokovu wenye Yehova atafanya kwa ajili yenu leo.+ Kwa maana Wamisri wenye munaona leo, hamutawaonaka tena.+ 14 Yehova mwenyewe atawapigania ninyi,+ na ninyi mutakaa kimya.”
15 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Sababu gani unaendelea kunililia? Ambia Waisraeli wavunje kambi. 16 Sasa wewe, inua fimbo yako na unyooshe mukono wako juu ya bahari na uitenganishe, ili Waisraeli wapite katikati ya bahari juu ya inchi kavu. 17 Lakini mimi, nitaacha mioyo ya Wamisri ikuwe migumu, ili Wamisri waingie ndani nyuma ya Waisraeli; katika njia hiyo nitajitukuza kupitia Farao na jeshi lake lote, magari yake ya vita, na maaskari wake wapanda-farasi.+ 18 Na hakika Wamisri watajua kwamba mimi ni Yehova wakati nitajitukuza kupitia Farao, magari yake ya vita, na maaskari wake wapanda-farasi.”+
19 Kisha malaika wa Mungu wa kweli+ mwenye alikuwa anaenda mbele ya kambi ya Israeli akaondoka na kuenda nyuma yao, na nguzo ya wingu yenye ilikuwa mbele yao ikaenda nyuma na ikasimama nyuma yao.+ 20 Basi nguzo hiyo ikasimama kati ya kambi ya Wamisri na kambi ya Israeli.+ Kwenye upande mumoja, nguzo hiyo ilikuwa wingu lenye giza. Kwenye upande mwingine, nguzo hiyo ilikuwa inaangaza usiku.+ Kwa hiyo kambi hii haikukaribia ile kambi ingine usiku wote.
21 Sasa Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari;+ na Yehova akasukuma bahari nyuma usiku wote kwa upepo wenye nguvu wa mashariki, akageuza bonde la bahari kuwa inchi kavu,+ na maji yakagawanyika.+ 22 Kwa hiyo Waisraeli wakapita katikati ya bahari juu ya inchi kavu,+ na maji yalifanyiza ukuta kwenye upande wao wa kuume na kwenye upande wao wa kushoto.+ 23 Wamisri wakawafuatilia, na farasi wote wa Farao, magari yake ya vita, na maaskari wake wapanda-farasi wakaanza kuingia nyuma ya Waisraeli katikati ya bahari.+ 24 Wakati wa kesha la asubui,* Yehova akaangalia kambi ya Wamisri kutoka ndani ya ile nguzo ya moto na wingu,+ naye akatia muvurugo katika kambi ya Wamisri. 25 Akaendelea kuondoa magurudumu* kwenye magari yao na kwa hiyo walikuwa wanayaendesha kwa shida, na Wamisri wakasema: “Tukimbie ili tusikaribie hata kidogo Israeli, kwa sababu Yehova anapigana na Wamisri kwa ajili ya Israeli.”+
26 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Nyoosha mukono wako juu ya bahari ili maji yarudie na kufunika Wamisri, magari yao ya vita, na maaskari wao wapanda-farasi.” 27 Mara moja Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari, na kadiri asubui ilifika, bahari ikarudia katika hali yake ya kawaida. Wakati Wamisri walikuwa wanakimbia bahari, Yehova akakunguta Wamisri katikati ya bahari.+ 28 Maji yakarudia na kufunika magari ya vita na maaskari wapanda-farasi, na jeshi lote la Farao lenye lilikuwa limeingia ndani ya bahari nyuma ya Waisraeli.+ Hakuna hata mumoja kati ya Wamisri mwenye aliokoka.+
29 Lakini Waisraeli wakatembea juu ya inchi kavu katika bonde la bahari,+ na maji yalifanyiza ukuta kwenye upande wao wa kuume na kwenye upande wao wa kushoto.+ 30 Hivyo Yehova akaokoa Israeli siku hiyo katika mukono wa Wamisri,+ na Israeli wakaona maiti za Wamisri pembeni ya bahari. 31 Pia Israeli wakaona uwezo mukubwa* wenye Yehova alitumia juu ya Wamisri, na watu wakaanza kumuogopa Yehova na kumuamini Yehova na Musa mutumishi wake.+
15 Wakati huo Musa na Waisraeli wakamuimbia Yehova wimbo huu:+
“Nimuimbie Yehova, kwa maana ametukuzwa sana.+
Farasi na mupandaji wake amewatupa katika bahari.+
2 Nguvu zangu na uwezo wangu ni Yah,* kwa maana amekuwa wokovu wangu.+
Huyu ndiye Mungu wangu, na nitamusifu;+ Mungu wa baba yangu,+ na nitamutukuza.+
3 Yehova ni mupiganaji-vita mwenye nguvu.+ Yehova ni jina lake.+
4 Ametupa magari ya Farao na jeshi lake katika bahari,+
Na wapiganaji-vita wake wenye nguvu zaidi wamezama katika Bahari Nyekundu.+
5 Maji yenye mawimbi makubwa yaliwafunika; walishuka kama jiwe katika sehemu za chini kabisa.+
6 Mukono wako wa kuume, Ee Yehova, uko na nguvu nyingi;+
Mukono wako wa kuume, Ee Yehova, unaweza kumuvunja-vunja adui.
7 Katika wingi wa ukubwa wako unaweza kuangusha chini wale wenye kusimama ili kukupinga;+
Unatuma kasirani yako yenye kuwaka, inawateketeza kama majani yenye kukauka.
8 Kwa pumuzi ya matundu ya pua yako maji yalijikusanya pamoja;
Yalisimama imara, yalizuia mafuriko yasiteremuke;
Maji yenye mawimbi makubwa yaligandamana katika moyo wa bahari.
9 Adui alisema, ‘Nitafuatilia! Nitafikia!
Nitagawanya vitu vyenye vinachukuliwa katika vita mupaka nitosheke!*
Nitachomoa upanga wangu! Mukono wangu utawanyenyekeza!’+
10 Ulipuliza kwa pumuzi yako, bahari ikawafunika;+
Walizama kama risasi katika maji makubwa.
11 Ni nani kati ya miungu mwenye kuwa kama wewe, Ee Yehova?+
Ni nani mwenye kuwa kama wewe, mwenye kujionyesha kuwa mwenye nguvu katika utakatifu?+
Mwenye anapaswa kuogopwa kwa kumuimbia nyimbo za sifa, Mwenye anatenda mambo ya ajabu.+
12 Ulinyoosha mukono wako wa kuume, na dunia ikawameza.+
13 Kwa upendo wako mushikamanifu umeongoza watu wenye ulikomboa;+
Kwa nguvu zako utawaongoza kwenye makao yako matakatifu.
15 Wakati huo mashehe* wa Edomu wataogopa sana,
Wakaaji wote wa Kanaani watavunjika moyo.+
16 Woga na hofu vitaanguka juu yao.+
Kwa sababu ya mukono wako wenye nguvu watabakia bila kutikisika kama jiwe
Mupaka watu wako wapite, Ee Yehova,
17 Utawaleta na kuwapanda katika mulima wa uriti wako,+
Mahali kwenye kulifanywa imara kwenye ulijitayarishia ili ukae pale, Ee Yehova,
Patakatifu, Ee Yehova, kwenye mikono yako imejenga.
18 Yehova atatawala akiwa mufalme milele na milele.+
19 Wakati farasi za Farao pamoja na magari yake ya vita na maaskari wake wapanda-farasi waliingia katika bahari,+
Basi Yehova alirudisha maji ya bahari juu yao,+
Lakini watu wa Israeli walitembea juu ya inchi kavu katikati ya bahari.”+
20 Kisha Miriamu nabii mwanamuke, dada ya Haruni, akakamata ngoma ya kidogo* katika mukono wake, na wanamuke wote wakamufuata wakiwa na ngoma za kidogo* na walikuwa wanacheza dansi. 21 Miriamu alikuwa anaimba hivi kwa kuitikia wanaume:
“Mumuimbie Yehova, kwa maana ametukuzwa sana.+
Farasi na mupandaji wake amewatupa katika bahari.”+
22 Kisha wakati fulani Musa akaongoza Israeli kutoka kwenye Bahari Nyekundu, na wakaenda kwenye jangwa la Shuri na kusafiri kwa siku tatu (3) katika jangwa, lakini hawakupata maji. 23 Wakafika Mara,*+ lakini hawakuweza kunywa maji ya Mara kwa sababu yalikuwa machungu. Ndiyo sababu aliita mahali pale Mara. 24 Kwa hiyo watu wakaanza kumunungunikia Musa,+ kwa kusema: “Tutakunywa nini?” 25 Musa akamulilia Yehova,+ na Yehova akamuongoza kwenye muti fulani. Wakati alitupa muti huo ndani ya maji hayo, maji hayo yakakuwa matamu.
Pale Mungu akawawekea sharti na musingi wa hukumu, na pale akawatia katika jaribu.+ 26 Mungu akasema: “Kama utasikiliza kabisa sauti ya Yehova Mungu wako na kufanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya macho yake na kusikiliza kwa uangalifu amri zake na kushika masharti yake yote,+ sitakuletea magonjwa yenye nilileta juu ya Wamisri,+ kwa sababu mimi, Yehova, niko nakuponyesha.”+
27 Kisha wakafika Elimu, mahali kwenye kulikuwa chemchemi kumi na mbili (12) na miti ya mitende makumi saba (70). Kwa hiyo wakapiga kambi pale pembeni ya maji.
16 Kisha kutoka Elimu, mwishowe mukusanyiko wote wa Waisraeli ukafika katika jangwa la Sini,+ katikati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano (15) ya mwezi wa pili kisha kutoka katika inchi ya Misri.
2 Kisha mukusanyiko wote wa Waisraeli ukaanza kumunungunikia Musa na Haruni katika jangwa.+ 3 Waisraeli waliendelea kuwaambia: “Ingekuwa muzuri kama tungekufa katika mukono wa Yehova katika inchi ya Misri wakati tulikuwa tunakaa pembeni ya vyungu vya nyama,+ wakati tulikuwa tunakula na kushiba mikate. Sasa mumetuleta katika jangwa hili ili kuua kutaniko hili lote kwa njaa.”+
4 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Angalia, nitawanyeshea mukate kutoka mbinguni,+ na kila mutu ataenda kukusanya kiasi chake kila siku,+ ili niwajaribu nione kama watatembea katika sheria yangu ao hapana.+ 5 Lakini siku ya sita (6)+ wakati watatayarisha kile chenye walikusanya, kitakuwa mara mbili ya kiasi chenye wanaokota kila siku ya zile siku zingine.”+
6 Kwa hiyo Musa na Haruni wakaambia Waisraeli wote: “Mangaribi mutajua hakika kwamba Yehova ndiye aliwatosha ninyi katika inchi ya Misri.+ 7 Asubui mutaona utukufu wa Yehova, kwa sababu amesikia manunguniko yenu juu ya Yehova. Sisi ni nani ili mutunungunikie?” 8 Musa akaendelea kusema: “Wakati Yehova atawapatia nyama ya kula mangaribi, na asubui mukate ili mukule na kushiba, mutatambua kwamba Yehova amesikia manunguniko yenu juu yake. Lakini sisi ni nani? Hamutunungunikie sisi, lakini munamunungunikia Yehova.”+
9 Kisha Musa akamuambia Haruni: “Ambia mukusanyiko wote wa Waisraeli, ‘Mukuje karibu mbele ya Yehova, kwa sababu amesikia manunguniko yenu.’”+ 10 Wakati tu Haruni alimaliza kuzungumuza na mukusanyiko wote wa Waisraeli, wakageuka na kuangalia jangwa, na angalia! utukufu wa Yehova ulionekana katika lile wingu.+
11 Yehova akaendelea kuzungumuza na Musa, na kusema: 12 “Nimesikia manunguniko ya Waisraeli.+ Waambie: ‘Mangaribi wakati giza linaanza* mutakula nyama, na asubui mutashiba mukate,+ na mutajua hakika kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+
13 Basi mangaribi hiyo ndege wenye kuitwa kware wakakuja na kufunika kambi,+ na asubui umande ulifunika udongo kuzunguka kambi pande zote. 14 Wakati umande huo uligeuka kuwa muvuke, kulikuwa kitu fulani laini, chenye chembechembe juu ya uso wa jangwa,+ kitu laini kama barafu nyembamba juu ya udongo. 15 Wakati Waisraeli walikiona, wakaanza kuambiana: “Hii ni nini?” kwa maana hawakujua kilikuwa kitu gani. Musa akawaambia: “Ni mukate wenye Yehova amewapatia ukuwe chakula.+ 16 Yehova ameamuru hivi: ‘Kila mutu anapaswa kukusanya kiasi chenye anaweza kula. Munapaswa kukamata kipimo kimoja cha omeri*+ kwa ajili ya kila mutu kulingana na hesabu ya watu wenye kila mumoja wenu iko* nao katika hema yake.’” 17 Waisraeli wakaanza kufanya vile; wakakikusanya, wengine walikusanya kingi na wengine walikusanya kidogo. 18 Wakati walikuwa wanapima kwa omeri, ule mwenye alikuwa amekusanya kingi hakukuwa na kingi zaidi na ule mwenye alikuwa amekusanya kidogo hakupungukiwa.+ Kila mumoja alikusanya kiasi chenye aliweza kula.
19 Kisha Musa akawaambia: “Mutu asiache chochote mupaka asubui.”+ 20 Lakini hawakumusikiliza Musa. Wakati watu waliacha sehemu fulani mupaka asubui, kilitokeza minyoo na kilinuka, na Musa akawakasirikia. 21 Walikuwa wanakiokota kila asubui, kila mutu kulingana na kile angeweza kula. Wakati jua lilikuwa kali, kiliyeyuka.
22 Siku ya sita (6), waliokota mara mbili kiasi cha mukate,+ vipimo mbili vya omeri kwa ajili ya kila mutu. Kwa hiyo wakubwa wote wa mukusanyiko wakaenda na kumuambia Musa jambo hilo. 23 Basi Musa akawaambia: “Ni vile Yehova alisema. Kesho kutakuwa pumuziko kamili,* sabato takatifu kwa ajili ya Yehova.+ Mupike kile munaweza kupika, mutokoteshe kile munaweza kutokotesha;+ kisha muweke kile kitabakia na mukichunge mupaka asubui.” 24 Kwa hiyo wakakiweka mupaka asubui, kama vile Musa alikuwa ameamuru, na hakikunuka wala funza hawakukuwa* ndani yake. 25 Kisha Musa akasema: “Mukikule leo, kwa sababu leo ni sabato kwa ajili ya Yehova. Leo hamutakipata juu ya udongo. 26 Mutakiokota kwa siku sita (6), lakini siku ya saba (7) ni Sabato,+ hakitakuwa.” 27 Lakini, watu fulani walienda ili kukiokota katika siku ya saba (7), lakini hawakupata kitu.
28 Kwa hiyo Yehova akamuambia Musa: “Mutakataa kushika amri zangu na sheria zangu mupaka wakati gani?+ 29 Mukumbuke kwamba Yehova amewapatia Sabato.+ Ndiyo sababu siku ya sita (6) anawapatia mukate wa siku mbili. Kila mutu anapaswa kubakia kwenye iko;* mutu asitoke mahali pake siku ya saba (7).” 30 Kwa hiyo watu wakafanya Sabato* siku ya saba (7).+
31 Nyumba ya Israeli ikaita mukate huo “mana.”* Ulikuwa mweupe kama mbegu za mugiligilani, na utamu wake ulikuwa kama wa keki zenye kuwa tambarare* na zenye kuwa na asali.+ 32 Kisha Musa akasema: “Yehova ameamuru hivi: ‘Mujaze kipimo kimoja cha omeri ili kikuwe kitu cha kuweka katika vizazi vyenu vyote,+ ili wapate kuona mukate wenye niliwakulisha katika jangwa wakati nilikuwa ninawatosha katika inchi ya Misri.’” 33 Kwa hiyo Musa akamuambia Haruni: “Kamata mutungi mumoja na utie ndani kipimo kimoja cha omeri ya mana na uiweke mbele ya Yehova kuwa kitu cha kuwekwa katika vizazi vyenu vyote.”+ 34 Kama vile Yehova alimuamuru Musa, Haruni akaiweka mbele ya Ushuhuda+ ili ichungwe. 35 Waisraeli walikula mana miaka makumi ine (40),+ mupaka wakati walifika katika inchi yenye kuikaliwa na watu.+ Walikula mana mupaka wakati walifika kwenye mupaka wa inchi ya Kanaani.+ 36 Omeri ni sehemu moja ya kumi (1/10) ya kipimo cha efa.*
17 Mukusanyiko wote wa Waisraeli ukaondoka katika jangwa la Sini+ hatua kwa hatua kama vile Yehova aliagiza,+ na wakapiga kambi Refidimu.+ Lakini mahali pale hapakukuwa maji yenye watu wangekunywa.
2 Kwa hiyo watu wakaanza kugombana na Musa+ na kusema: “Tupatie maji ya kunywa!” Lakini Musa akawaambia: “Sababu gani munagombana na mimi? Sababu gani munaendelea kumujaribu Yehova?”+ 3 Lakini pale watu walikuwa na kiu sana ya maji, na wakaendelea kumunungunikia Musa+ na kusema: “Sababu gani umetutosha Misri ili kutuua na kiu sisi na wana wetu na mifugo yetu?” 4 Mwishowe Musa akamulilia Yehova akisema: “Nifanye nini na watu hawa? Kisha wakati kidogo tu watanipiga majiwe!”
5 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Pita mbele ya watu, na uende pamoja na wazee fulani wa Israeli na ukamate fimbo yako yenye ulitumia kupiga Muto Nile.+ Uibebe katika mukono wako na uendelee kutembea. 6 Angalia! Nitasimama mbele yako juu ya mwamba kule Horebu. Utapiga mwamba huo, na maji yatatoka ndani yake, na watu watakunywa maji hayo.”+ Musa akafanya vile mbele ya wazee wa Israeli. 7 Kwa hiyo akaita mahali pale Masa*+ na Meriba,*+ kwa sababu ya ugomvi wa Waisraeli na kwa sababu walimujaribu Yehova+ kwa kusema: “Je, Yehova iko* katikati yetu ao hapana?”
8 Kisha Waamaleki+ wakakuja na kupigana na Israeli kule Refidimu.+ 9 Basi Musa akamuambia Yoshua:+ “Tuchagulie wanaume na uende kupigana na Waamaleki. Kesho nitasimama kwenye kichwa cha kilima, nitakuwa na fimbo ya Mungu wa kweli katika mukono wangu.” 10 Kisha Yoshua akafanya kama vile Musa alimuambia,+ na akapigana na Waamaleki. Na Musa, Haruni, na Huru+ wakapanda mupaka kwenye kichwa cha kilima.
11 Wakati wote wenye Musa aliinua mikono yake, Waisraeli walishinda, lakini wakati tu alishusha mikono yake, Waamaleki walishinda. 12 Wakati mikono ya Musa ilichoka, wakakamata jiwe na kuliweka chini yake, naye akakaa juu ya jiwe hilo. Kisha Haruni na Huru wakashika mikono yake na kuitegemeza, mumoja kila upande, kwa hiyo mikono ya Musa ikabakia imara mupaka wakati jua lilishuka. 13 Basi Yoshua akamushinda Amaleki na watu wake kwa upanga.+
14 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Andika mambo haya katika kitabu ili yakumbukwe na uyaseme tena kwa Yoshua: ‘Nitafuta kabisa Amaleki chini ya mbingu, naye hatakumbukwa tena.’”+ 15 Kisha Musa akajenga mazabahu na akaipatia jina Yehova-nisi,* 16 na akasema: “Kwa sababu mukono wa Amaleki umepigana na kiti cha ufalme cha Yah,+ Yehova atapigana na Amaleki kutoka kizazi mupaka kizazi.”+
18 Sasa Yetro kuhani wa Midiani, baba-mukwe wa Musa,+ akasikia mambo yote yenye Mungu alikuwa amemufanyia Musa na watu wake Israeli, namna Yehova alikuwa ametosha Israeli katika Misri.+ 2 Yetro, baba-mukwe wa Musa, alikuwa amekubali Sipora bibi ya Musa aishi pamoja naye, wakati Sipora alirudishwa kwa Yetro, 3 pamoja na wana wake wawili.+ Mumoja aliitwa Gershomu,*+ kwa sababu Musa alisema, “Nimekuwa mukaaji mugeni katika inchi ya kigeni,” 4 na ule mwingine aliitwa Eliezeri,* kwa sababu Musa alisema, “Mungu wa baba yangu ni musaidizi wangu, mwenye aliniokoa kutokana na upanga wa Farao.”+
5 Kwa hiyo Yetro, baba-mukwe wa Musa, pamoja na wana wa Musa na bibi yake, wakaenda kumuona Musa katika jangwa mahali alikuwa amepiga kambi kwenye mulima wa Mungu wa kweli.+ 6 Kisha akatuma ujumbe huu kwa Musa: “Mimi, baba-mukwe wako Yetro,+ niko nakuja kukuona pamoja na bibi yako na wana wako wawili.” 7 Mara moja Musa akaenda kumupokea baba-mukwe wake, na akainama na kumubusu. Kila mumoja wao akauliza hali ya mwingine, na kisha wakaingia katika hema.
8 Musa akamuelezea baba-mukwe wake mambo yote yenye Yehova alikuwa amemutendea Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli,+ magumu yote yenye walipata wakati walikuwa katika safari,+ na namna Yehova aliwaokoa. 9 Yetro akafurahi kusikia mambo yote ya muzuri yenye Yehova alikuwa amefanyia Israeli kwa kuwaokoa kutoka Misri.* 10 Kisha Yetro akasema: “Yehova asifiwe, yeye mwenye aliwaokoa kutoka Misri na kutoka kwa Farao, na mwenye aliokoa watu kutoka katika mukono wa Misri. 11 Sasa ninajua kwamba Yehova ni mukubwa kuliko miungu mingine yote,+ kwa sababu ya mambo yenye alifanyia wale wenye kutendea watu wake kwa kiburi.” 12 Kisha Yetro, baba-mukwe wa Musa, akaleta toleo la kuteketezwa na zabihu kwa ajili ya Mungu, na Haruni na wazee wote wa Israeli wakakuja kula chakula pamoja na baba-mukwe wa Musa mbele ya Mungu wa kweli.
13 Siku yenye ilifuata, Musa akakaa kama kawaida ili kuhukumu watu, na watu wakaendelea kusimama mbele ya Musa tangu asubui mupaka mangaribi. 14 Wakati baba-mukwe wa Musa aliona mambo yote yenye Musa alikuwa anafanya kwa ajili ya watu, akasema: “Ni jambo gani hili lenye unafanya kwa ajili ya watu? Sababu gani unakaa hapa peke yako na watu hawa wamesimama mbele yako tangu asubui mupaka mangaribi?” 15 Musa akamuambia baba-mukwe wake: “Ni kwa sababu watu wanaendelea kuja kwangu ili kuuliza habari kutoka kwa Mungu. 16 Wakati kesi fulani ya hukumu inatokea, inaletwa kwangu na ninapaswa kuhukumu kati ya mutu na mwenzake, na ninawajulisha maamuzi ya Mungu wa kweli na sheria zake.”+
17 Baba-mukwe wa Musa akamuambia: “Jambo lenye unafanya haliko muzuri. 18 Hakika utachoka, wewe pamoja na watu hawa wenye kuwa pamoja na wewe, kwa sababu huu ni muzigo muzito sana na hauwezi kuubeba wewe peke yako. 19 Sasa unisikilize, nitakupatia shauri, na Mungu atakuwa pamoja na wewe.+ Wewe utakuwa mwakilishi wa watu mbele ya Mungu wa kweli,+ na utaleta kesi za hukumu mbele ya Mungu wa kweli.+ 20 Unapaswa kuwafundisha masharti na sheria+ na kuwaonyesha njia yenye wanapaswa kutembea ndani yake na kazi yenye wanapaswa kufanya. 21 Lakini unapaswa kuchagua kati ya watu, wanaume wenye uwezo,+ wenye kumuogopa Mungu, wanaume wenye kutumainika wenye kuchukia faida yenye haiko ya haki,+ na uwaweke juu ya watu ili wakuwe wakubwa wa maelfu, wakubwa wa mamia, wakubwa wa makumi tano, na wakubwa wa makumi.+ 22 Watahukumu watu wakati kesi za hukumu zinatokea,* na watakuletea kila kesi ya hukumu yenye kuwa ngumu,+ lakini wataamua kila kesi ya hukumu ya kidogo. Fanya mambo yakuwe mepesi kwako kwa kufanya wabebe muzigo huo pamoja na wewe.+ 23 Kama unafanya vile, na ikuwe ni vile Mungu anakuamuru, utaweza kuvumilia muzigo huo, na kila mutu atarudia kwake akiwa mwenye kutosheka.”
24 Mara moja Musa akamusikiliza baba-mukwe wake na akafanya mambo yote yenye alisema. 25 Musa akachagua wanaume wenye uwezo katikati ya Israeli wote na akawaweka wakuwe vichwa juu ya watu, wakubwa wa maelfu, wakubwa wa mamia, wakubwa wa makumi tano, na wakubwa wa makumi. 26 Kwa hiyo walihukumu watu wakati kulitokea kesi za hukumu. Walikuwa wanamuletea Musa kesi ya hukumu yenye kuwa ngumu,+ lakini kila kesi ya hukumu ya kidogo walikuwa wanaiamua wao wenyewe. 27 Kisha mambo hayo Musa akamusindikiza baba-mukwe wake,+ na baba-mukwe wake akarudia katika inchi yake.
19 Katika mwezi wa tatu (3) kisha Waisraeli kutoka katika inchi ya Misri, siku ileile, wakafika katika jangwa la Sinai. 2 Waliondoka Refidimu+ na wakafika katika jangwa la Sinai na kupiga kambi katika jangwa. Israeli walipiga kambi kule mbele ya mulima.+
3 Kisha Musa akapanda kwa Mungu wa kweli, na Yehova akamuita kutoka katika mulima,+ na kusema: “Ni hivi utaambia nyumba ya Yakobo na kuambia Waisraeli, 4 ‘Mumejionea wenyewe mambo yenye nilitendea Wamisri,+ ili niwabebe juu ya mabawa ya tai na kuwaleta kwangu.+ 5 Na sasa kama mutatii kabisa sauti yangu na kushika agano langu, hakika mutakuwa mali yangu ya pekee* kati ya vikundi vyote vya watu,+ kwa sababu dunia yote ni yangu.+ 6 Mutakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’+ Hayo ndiyo maneno yenye utawaambia Waisraeli.”
7 Kwa hiyo Musa akaenda na kuita wazee wa watu na akawaambia maneno hayo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru.+ 8 Kisha watu wote wakajibu kwa pamoja: “Mambo yote yenye Yehova amesema, tuko tayari kuyafanya.”+ Mara moja Musa akamupelekea Yehova jibu la watu. 9 Na Yehova akamuambia Musa: “Angalia! Nitakuja kwako katika wingu lenye giza, ili watu wasikie wakati ninazungumuza na wewe na ili wakuamini wewe pia sikuzote.” Kisha Musa akamuambia Yehova mambo yenye watu walisema.
10 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Uende mahali watu wako na uwatakase leo na kesho, na wanapaswa kufua nguo zao. 11 Na wanapaswa kuwa tayari kwa ajili ya siku ya tatu (3), kwa sababu katika siku ya tatu Yehova atashuka juu ya Mulima Sinai mbele ya macho ya watu wote. 12 Unapaswa kuwekea watu mipaka kuzunguka mulima huo pande zote na uwaambie, ‘Mufanye angalisho ili musipande kwenye mulima wala kugusa mupaka wake. Mutu yeyote mwenye atagusa mulima hakika atauawa. 13 Mukono wowote usimuguse mutu huyo, lakini atapigwa kwa majiwe ao kutobolewa na silaha.* Ikuwe munyama ao mwanadamu, hataishi.’+ Lakini watu wanaweza kupanda kwenye mulima wakati wanasikia sauti ya pembe ya kondoo.”+
14 Kisha Musa akashuka kutoka kwenye mulima na kuenda mahali watu walikuwa, na akaanza kutakasa watu, na watu wakafua nguo zao.+ 15 Akaambia watu: “Mujitayarishe kwa ajili ya siku ya tatu (3). Musifanye ngono.”*
16 Siku ya tatu (3) asubui, kulikuwa mungurumo na umeme wa radi, na kulikuwa wingu nzito+ kwenye mulima na sauti kubwa sana ya baragumu, na watu wote katika kambi wakaanza kutetemeka.+ 17 Basi Musa akapeleka watu inje ya kambi ili wakutane na Mungu wa kweli, na watu wakasimama kwenye sehemu ya chini ya mulima. 18 Mulima Sinai ulitoa moshi kila mahali, kwa sababu Yehova alishuka juu yake katika moto;+ na moshi huo ulikuwa unapanda kama moshi wa tanuru, na mulima wote ulitetemeka kwa nguvu.+ 19 Wakati sauti ya baragumu iliendelea kuongezeka zaidi na zaidi, Musa akasema, na sauti ya Mungu wa kweli ikamujibu.
20 Kwa hiyo Yehova akashuka juu ya Mulima Sinai kwenye kichwa cha mulima. Kisha Yehova akamuita Musa apande kwenye kichwa cha mulima, na Musa akapanda.+ 21 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Shuka chini na uonye watu wasijaribu kuvuka mipaka kwa nguvu ili kumuangalia Yehova, wakifanya vile wengi wao watakufa. 22 Na makuhani wenye wanamukaribia Yehova kwa ukawaida wajitakase, ili Yehova asiwapige.”*+ 23 Kisha Musa akamuambia Yehova: “Watu hawawezi kupanda kwenye Mulima Sinai kwa sababu tayari ulituonya, kwa kusema, ‘Weka mipaka kuzunguka mulima huu, na uutakase.’”+ 24 Lakini, Yehova akamuambia: “Uende, ushuke, na upande tena, wewe na Haruni, lakini usiache makuhani na watu wavuke mipaka kwa nguvu ili kuja kwa Yehova, kusudi asiwapige.”+ 25 Kwa hiyo Musa akashuka mupaka mahali watu walikuwa na akawaambia.
20 Kisha Mungu akasema maneno haya yote:+
2 “Mimi ni Yehova Mungu wako, mwenye alikutosha katika inchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.+ 3 Haupaswe kuwa na miungu mingine isipokuwa mimi.*+
4 “Haupaswe kujifanyia sanamu ya kuchongwa wala umbo* ya kitu fulani chenye kuwa juu mbinguni wala chenye kuwa hapa chini juu ya dunia wala chenye kuwa ndani ya maji chini ya dunia.+ 5 Haupaswe kuviinamia wala kushawishiwa kuvitumikia,+ kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu,+ mwenye analeta azabu juu ya wana kwa sababu ya kosa la baba zao, juu ya kizazi cha tatu (3) na juu ya kizazi cha ine (4) cha wale wenye kunichukia, 6 lakini ninaonyesha upendo mushikamanifu kwa kizazi cha elfu (1 000) cha watu wenye kunipenda na kushika amri zangu.+
7 “Haupaswe kutumia jina la Yehova Mungu wako kwa njia yenye haifae,+ kwa maana Yehova hatakosa kumupatia azabu mutu mwenye anatumia jina Lake kwa njia yenye haifae.+
8 “Kumbuka siku ya Sabato na uione kuwa takatifu.+ 9 Utatumika na kufanya kazi zako zote kwa siku sita (6),+ 10 lakini siku ya saba (7) ni sabato kwa ajili ya Yehova Mungu wako. Haupaswe kufanya kazi yoyote, wewe, wala mutoto wako mwanaume, wala mutoto wako mwanamuke, wala mutumwa wako mwanaume, wala mutumwa wako mwanamuke, wala munyama wako wa kufugwa, wala mukaaji mugeni mwenye kuwa ndani ya makao yako.*+ 11 Kwa maana katika siku sita (6) Yehova alifanya mbingu na dunia, bahari, na vyote vyenye kuwa ndani, na alianza kupumuzika katika siku ya saba (7).+ Ndiyo sababu Yehova alibariki siku ya Sabato na kuifanya kuwa takatifu.
12 “Heshimia baba yako na mama yako,+ ili uishi wakati murefu katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia.+
13 “Haupaswe kuua.+
14 “Haupaswe kufanya uzinifu.+
15 “Haupaswe kuiba.+
16 “Haupaswe kutoa ushahidi wa uongo juu ya mwenzako.+
17 “Haupaswe kutamani nyumba ya mwenzako. Haupaswe kutamani bibi ya mwenzako,+ wala mutumwa wake mwanaume, wala mutumwa wake mwanamuke, wala ngombe-dume wake, wala punda wake, wala kitu chochote cha mwenzako.”+
18 Sasa watu wote waliona umeme wa radi na ule mungurumo, sauti ya baragumu, na mulima wenye ulikuwa unatoa moshi; na wakati waliona mambo hayo wakatetemeka na kusimama mbali.+ 19 Kwa hiyo wakamuambia Musa: “Wewe useme na sisi, na sisi tutakusikiliza, lakini Mungu asiseme na sisi, ili tusikufe.”+ 20 Kwa hiyo Musa akaambia watu: “Musiogope, kwa sababu Mungu wa kweli amekuja ili kuwajaribu,+ ili muendelee kumuogopa kusudi musitende zambi.”+ 21 Kwa hiyo watu wakaendelea kusimama mbali, lakini Musa akaenda karibu na lile wingu la mweusi mahali Mungu wa kweli alikuwa.+
22 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Ni hivi utaambia Waisraeli, ‘Mumejionea ninyi wenyewe kwamba nimezungumuza na ninyi kutoka mbinguni.+ 23 Hamupaswe kufanya miungu ya feza pembeni yangu, na hamupaswe kujifanyia miungu ya zahabu.+ 24 Utanifanyia mazabahu ya udongo, na juu yake utanitolea matoleo yako ya kuteketezwa, zabihu zako za ushirika,* kundi lako, na mifugo yako. Kila mahali kwenye nitafanya jina langu likumbukwe,+ nitakuja kwako na nitakubariki. 25 Kama unanifanyia mazabahu ya majiwe, usiijenge na majiwe yenye yalikatwa kwa vifaa vya kukata navyo.*+ Kwa maana kama unatumia kifaa cha kukata vitu juu ya mazabahu hiyo, utaichafua. 26 Na haupaswe kupanda kwenye mazabahu yangu kwa kutumia ngazi za kupandia, ili sehemu zako za siri* zisifunuliwe juu ya mazabahu hiyo.’
21 “Haya ndiyo maamuzi ya hukumu yenye utawaambia:+
2 “Kama unanunua mutumwa Mwebrania,+ atafanya kazi ya utumwa kwa miaka sita (6), lakini mwaka wa saba (7), atawekwa huru bila kulipa kitu.+ 3 Kama alikuja peke yake, ataondoka peke yake. Kama iko* na bibi, basi bibi yake anapaswa kuondoka pamoja naye. 4 Kama bwana wa mutumwa huyo anamupatia bibi, na bibi huyo anamuzalia watoto wanaume ao watoto wanamuke, bibi huyo na watoto wake watakuwa mali ya bwana wa mutumwa huyo, na mutumwa huyo ataondoka peke yake.+ 5 Lakini kama mutumwa huyo anasema hivi kwa mukazo: ‘Ninamupenda bwana wangu, bibi yangu, na wana wangu; sitaki kuwekwa huru,’+ 6 bwana wa mutumwa huyo atamuleta mbele ya Mungu wa kweli. Kisha bwana huyo atamuleta kwenye mulango ao kwenye mwimo wa mulango, na bwana wa mutumwa huyo atatoboa sikio la mutumwa huyo kwa sindano, naye atakuwa mutumwa wa bwana wake maisha yake yote.
7 “Kama mutu anamuuzisha binti yake akuwe mutumwa, binti huyo hatawekwa huru kama vile mutumwa mwanaume anawekwa huru. 8 Kama bwana wa mutumwa huyo mwanamuke hamufurahie na hamuchague kuwa suria* wake lakini anamufanya anunuliwe na mutu mwingine,* bwana huyo hatakuwa na haki ya kumuuzisha kwa wageni, kwa sababu amemusaliti mutumwa huyo. 9 Kama anamuchagua akuwe bibi ya mwana wake, anapaswa kumupatia haki zenye binti yake anastahili. 10 Kama anajichukulia bibi mwingine, chakula, nguo, na haki ya ndoa ya bibi yake wa kwanza havitapunguzwa.+ 11 Kama hamupatie hayo mambo tatu (3), basi mutumwa huyo mwanamuke ataondoka na kuwa huru bila kulipa feza yoyote.
12 “Mutu yeyote mwenye anamupiga mutu na kumuua anapaswa kuuawa.+ 13 Lakini kama anamuua bila kukusudia na Mungu wa kweli anaruhusu jambo hilo litokee, nitakuchagulia mahali kwenye anaweza kukimbilia.+ 14 Kama mutu anamukasirikia sana mwenzake na kumuua kwa makusudi,+ mutu huyo anapaswa kufa hata kama inaomba kumutosha kwenye mazabahu yangu.+ 15 Mutu mwenye anamupiga baba yake ao mama yake anapaswa kuuawa.+
16 “Kama mutu yeyote anamukamata mutu mwingine kinguvu+ na kumuuzisha ao anapatikana amemushika mutu huyo,+ anapaswa kuuawa.+
17 “Mutu yeyote mwenye anamulaani baba yake ao mama yake anapaswa kuuawa.+
18 “Ni hivi mambo yatakuwa kama watu wanagombana na kama mumoja wao anamupiga mwenzake kwa jiwe ao ngumi* na hakufe lakini haweze kutoka kwenye kitanda chake: 19 Kama anaweza kusimama na kutembea inje kwa kutumia fimbo, basi ule mwenye alimupiga hatapewa azabu. Atamulipa tu kwa ajili ya wakati wenye alipoteza bila kufanya kazi mupaka akuwe amepona kabisa.
20 “Kama mutu anamupiga kwa fimbo mutumwa wake mwanaume ao mutumwa wake mwanamuke na mutumwa huyo anakufa kwa mukono wake, mutu huyo mwenye amekufa anapaswa kulipiziwa kisasi.+ 21 Lakini, kama mutumwa huyo anaendelea kuishi kwa siku moja ao siku mbili, hatalipiziwa kisasi, kwa sababu yeye ni mutu mwenye bwana wake alimununua kwa feza.
22 “Kama watu wanapigana na wanamuumiza mwanamuke mwenye mimba naye anazaa mbele ya wakati wake*+ lakini hakutokee kifo,* ule mwenye alimuumiza anapaswa kulipa amande* yenye bwana ya bibi huyo atamuomba; na anapaswa kulipa amande hiyo kupitia waamuzi.+ 23 Lakini kama kifo kinatokea, basi unapaswa kutoa uzima kwa uzima,*+ 24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mukono kwa mukono, muguu kwa muguu,+ 25 alama ya moto kwa alama ya moto, kidonda kwa kidonda, pigo kwa pigo.
26 “Kama mutu anapiga jicho la mutumwa wake mwanaume ao jicho la mutumwa wake mwanamuke na kuliharibu, atamuacha mutumwa huyo aende huru kwa sababu ya jicho lake.+ 27 Na kama anangoa jino la mutumwa wake mwanaume ao jino la mutumwa wake mwanamuke, atamuacha mutumwa huyo aende huru kwa sababu ya jino lake.
28 “Kama ngombe-dume anamupiga kwa pembe mwanaume ao mwanamuke na mutu huyo anakufa, ngombe-dume huyo anapaswa kupigwa majiwe mupaka akufe+ na nyama yake haitakuliwa; lakini mwenye ngombe-dume huyo hatapewa azabu. 29 Lakini kama ngombe-dume alizoea kupiga watu kwa pembe na mwenye ngombe huyo alionywa lakini hakumufunga na ngombe-dume huyo aliua mwanaume ao mwanamuke, ngombe atapigwa majiwe na mwenye ngombe-dume huyo atauawa pia. 30 Kama anaombwa kulipa ukombozi,* anapaswa kutoa kila kitu chenye ataombwa ili akomboe uzima wake.* 31 Kama ngombe-dume anamupiga kwa pembe mutoto mwanaume ao mutoto mwanamuke, mwenye ngombe-dume huyo atatendewa kulingana na uamuzi huu wa hukumu. 32 Kama ngombe-dume huyo anamupiga kwa pembe mutumwa mwanaume ao mutumwa mwanamuke, mwenye ngombe-dume huyo atamulipa bwana wa mutumwa huyo shekeli makumi tatu (30),* na ngombe huyo atapigwa majiwe mupaka akufe.
33 “Kama mutu anafunua shimo ao anachimba shimo lakini halifunike na ngombe-dume ao punda anaangukia ndani, 34 mwenye shimo hilo atalipa.+ Atamulipa mwenye munyama huyo, na munyama mwenye alikufa atakuwa wake. 35 Kama ngombe-dume wa mutu fulani anaumiza ngombe-dume wa mutu mwingine na ngombe-dume huyo anakufa, basi wanapaswa kuuzisha ngombe-dume mwenye kuwa muzima na kugawanya bei yenye ililipwa wakati aliuzishwa; na wanapaswa pia kugawanya ule munyama mwenye alikufa. 36 Lakini kama ilikuwa inajulikana kwamba ngombe-dume alikuwa anazoea kupiga kwa pembe lakini mwenye ngombe-dume huyo hakukuwa anamufunga, anapaswa kulipa ngombe-dume kwa ngombe-dume, na ngombe-dume mwenye alikufa atakuwa wake.
22 “Kama mutu anaiba ngombe-dume ao kondoo na kumuchinja ao kumuuzisha, atalipa ngombe-dume tano (5) kwa ajili ya ngombe-dume huyo na kondoo ine (4) kwa ajili ya kondoo huyo.+
2 (“Kama mwizi+ anapatikana akivunja nyumba na kisha anapigwa na kufa, hakuna hatia ya damu kwa ajili yake. 3 Lakini kama jambo hilo linafanyika kisha jua kutokea, kutakuwa hatia ya damu kwa ajili yake.)
“Mwizi huyo anapaswa kulipa. Kama hana kitu cha kulipa, basi anapaswa kuuzishwa ili alipie vitu vyenye aliiba. 4 Kama mwizi huyo anapatikana na munyama mwenye aliiba na munyama huyo hajakufa, ikuwe ngombe-dume, punda, ao kondoo, atalipa mara mbili.
5 “Kama mutu anapeleka wanyama wake ili wakule majani katika shamba ao katika shamba la mizabibu na anawaacha wakule majani katika shamba la mutu mwingine, atalipa kwa vitu vya muzuri zaidi vya shamba lake mwenyewe ao vitu vya muzuri zaidi vya shamba lake la mizabibu.
6 “Kama moto unaanza kuwaka na kisha unaenea katika miti midogo-midogo ya miiba na unateketeza mafungu ya nafaka kwa moto ao mimea ya nafaka yenye kusimama ao shamba, mutu mwenye aliwasha moto huo anapaswa kulipa kwa sababu ya vitu vyenye viliteketea.
7 “Kama mutu anamupatia mwenzake feza ao vitu ili aviweke na vitu hivyo vinaibwa katika nyumba ya huyo mwenzake, kama mwizi anapatikana, mwizi huyo anapaswa kulipa mara mbili.+ 8 Kama mwizi hapatikane, mwenye nyumba hiyo anapaswa kuletwa mbele ya Mungu wa kweli+ ili kuhakikisha kama alitia mukono wake juu ya vitu vya mwenzake. 9 Katika kesi zote za hukumu za mutu kushitakiwa kuwa na mali yenye haiko yake, kama ni ngombe-dume, punda, kondoo, nguo, ao kitu chochote chenye kilipotea chenye mutu anaweza kusema, ‘Hiki ni changu!’ wote wawili wataleta kesi yao ya hukumu mbele ya Mungu wa kweli.+ Mutu mwenye Mungu atasema kwamba iko* na kosa atamulipa mwenzake mara mbili.+
10 “Kama mutu anapatia mwenzake punda ao ngombe-dume ao kondoo ao munyama yeyote wa kufugwa ili amuchunge, na kisha munyama huyo anakufa ao anaumia mubaya sana ao anachukuliwa bila mutu yeyote kuona, 11 kiapo kitafanywa kati yao mbele ya Yehova, kwamba hakuweka mukono wake juu ya mali ya mwenzake; na mwenye munyama huyo anapaswa kukubali kiapo hicho. Ule mutu mwingine hatalipa kitu.+ 12 Lakini kama munyama huyo aliibwa akiwa kwake, atamulipa mwenye munyama huyo. 13 Kama munyama huyo alipasuliwa na munyama wa pori, atamuleta ili akuwe ushuhuda. Hatalipa kwa sababu ya kitu chenye kilipasuliwa na munyama wa pori.
14 “Lakini kama mutu anaazima munyama na munyama huyo anaumia mubaya sana ao anakufa wakati mwenye munyama huyo haiko, mutu mwenye aliazima munyama huyo anapaswa kulipa. 15 Kama mwenye munyama huyo iko,* mwenye alikodi hatalipa. Kama munyama huyo alikodishwa kwa feza, feza hizo zenye zililipwa ili kumukodisha ndio itakuwa malipo yake.
16 “Kama mwanaume anamutongoza bikira mwenye hajachumbiwa na kisha analala naye, anapaswa kulipa mali ya kuoa ili bikira huyo akuwe bibi yake.+ 17 Kama baba yake anakataa kabisa kupatia mwanaume huyo binti yake, mwanaume huyo atalipa feza zenye kulingana na mali ya kuoa nayo.
18 “Haupaswe kuacha mwanamuke mulozi aishi.+
19 “Mutu yeyote mwenye analala na munyama anapaswa kabisa kuuawa.+
20 “Mutu yeyote mwenye anatoa zabihu kwa miungu mingine isipokuwa kwa Yehova peke yake anapaswa kuharibiwa.+
21 “Haupaswe kumutendea mubaya mukaaji mugeni wala kumukandamiza,+ kwa sababu mulikuwa wakaaji wageni katika inchi ya Misri.+
22 “Hamupaswe kumutesa mujane wala mutoto mwenye hana baba.*+ 23 Kama munamutesa kwa njia yoyote, naye ananililia, hakika nitasikia kilio chake;+ 24 na kasirani yangu itawaka, na mimi nitawaua kwa upanga, na bibi zenu watakuwa wajane, na watoto wenu watakuwa bila baba.
25 “Kama unamukopesha feza maskini yeyote* katikati ya watu wangu, mutu mwenye kuishi pamoja na wewe, haupaswe kumutendea kama mutu mwenye kufanya kazi ya kukopesha watu feza. Haupaswe kumulipisha faida.+
26 “Kama unakamata nguo ya mwenzako kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo,+ unapaswa kumurudishia nguo hiyo mbele ya jua kushuka. 27 Kwa sababu hiyo ndiyo nguo peke yake yenye iko* nayo, nguo yake ya kufunika mwili wake;* atajifunika nini?+ Wakati atanililia, hakika nitasikia, kwa sababu mimi niko mwenye huruma.*+
28 “Haupaswe kumulaani* Mungu+ wala kumulaani mukubwa* kati ya watu wako.+
29 “Haupaswe kusita kufanya matoleo yenye kutokana na mazao yako mengi na vitu vyenye kujaa sana katika vikamulio vyako.*+ Utanipatia muzaliwa wa kwanza wa wana wako.+ 30 Ni hivi unapaswa kufanya kuhusu ngombe-dume wako na kondoo wako:+ Atakaa na mama yake kwa siku saba (7). Siku ya munane (8), utanipatia yeye.+
31 “Munapaswa kuwa watu watakatifu mbele yangu,+ na hamupaswe kula nyama ya kitu chochote katika eneo la mashamba chenye kilipasuliwa na munyama wa pori.+ Munapaswa kutupia imbwa nyama hiyo.
23 “Haupaswe kueneza habari za uongo.+ Usishirikiane na mutu muovu kwa kutoa ushahidi wenye utaumiza wengine.+ 2 Haupaswe kufuata watu wengi ili kutenda maovu, na haupaswe kupotosha haki kwa kutoa ushahidi ili kuunga mukono watu wengi.* 3 Haupaswe kuonyesha upendeleo katika mabishano ya mutu maskini.+
4 “Kama unakutana na ngombe-dume ao punda wa adui yako mwenye amepotea, unapaswa kumurudisha kwake.+ 5 Kama punda wa mutu mwenye anakuchukia ameanguka chini ya muzigo wake, haupaswe kujifanya kama haumuone punda huyo na kuenda. Unapaswa kumusaidia kufungua munyama huyo.+
6 “Haupaswe kupotosha hukumu ya maskini kati yenu katika kesi yake ya kuhukumu.+
7 “Ujiepushe na mashitaka ya* uongo, na usimuue mutu mwenye hana kosa na mwenye haki, kwa maana sitamutangaza mutu muovu kuwa mwenye haki.*+
8 “Haupaswe kukubali rushwa,* kwa maana rushwa* inapofusha wenye hekima na inaweza kupotosha maneno ya wenye haki.+
9 “Haupaswe kumukandamiza mukaaji mugeni. Munajua namna mutu anajisikia wakati iko* mukaaji mugeni,* kwa sababu mulikuwa wakaaji wageni katika inchi ya Misri.+
10 “Kwa miaka sita (6) utapanda mbegu katika shamba lako na kuvuna mazao yake.+ 11 Lakini mwaka wa saba (7) utaliacha bila kulilima na utaliacha lipumuzike, na maskini wenye kuwa kati ya watu wako watakula chakula cha shamba hilo, na kile wataacha, kitakuliwa na wanyama wa pori. Ni vile utafanyia shamba lako la mizabibu na shamba lako la mizeituni.
12 “Utafanya kazi zako kwa siku sita (6); lakini siku ya saba (7), utaacha kufanya kazi zako, ili ngombe-dume wako na punda wako wapumuzike na mwana wa mutumwa wako mwanamuke na mukaaji mugeni wapate nguvu mupya.+
13 “Munapaswa kuwa waangalifu ili kufanya mambo yote yenye nimewaambia,+ na hamupaswe kutaja majina ya miungu mingine; hayapaswe kusikika kwenye midomo yenu.*+
14 “Mara tatu (3) kwa mwaka utanifanyia sikukuu.+ 15 Utafanya Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu.+ Utakula mikate yenye haina chachu kwa siku saba (7), kama vile nimekuamuru, kwa wakati wenye uliwekwa katika mwezi wa Abibu,*+ kwa maana kwa wakati huo ulitoka Misri. Mutu yeyote asionekane mbele yangu mikono wazi.+ 16 Pia, utafanya Sikukuu ya Mavuno* ya matunda ya kwanza yenye kukomaa ya kazi zako, na ya vitu vyenye unapanda katika mashamba;+ na Sikukuu ya Kukusanya* kwenye mwisho wa mwaka, wakati unakusanya katika shamba mazao ya kazi zako.+ 17 Mara tatu (3) kwa mwaka wanaume wako wote wanapaswa kuonekana mbele ya Bwana wa kweli, Yehova.+
18 “Haupaswe kutoa damu ya zabihu yangu pamoja na kila kitu chenye kuwa na chachu. Na zabihu za mafuta zenye zinatolewa kwenye sikukuu zangu hazipaswe kuachwa usiku wote mupaka asubui.
19 “Utaleta katika nyumba ya Yehova Mungu wako matunda ya kwanza ya muzuri zaidi yenye kukomaa ya udongo wako.+
“Haupaswe kutokotesha mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.+
20 “Ninamutuma malaika mbele yenu+ ili akulinde katika safari na kukuingiza mahali kwenye nimetayarisha.+ 21 Umusikilize, na utii sauti yake. Usimuasi, kwa maana hatasamehe makosa yako,+ kwa sababu jina langu liko ndani yake. 22 Lakini, kama unatii kabisa sauti yake na kufanya mambo yote yenye ninasema, nitaonyesha maadui wako uadui na nitapinga wale wenye kukupinga. 23 Kwa maana malaika wangu ataenda mbele yako na atakupeleka kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi, na Wayebusi, na mimi nitawaharibu.+ 24 Haupaswe kuinamia miungu yao wala kushawishiwa kuitumikia, na haupaswe kuiga matendo yao.+ Lakini, unapaswa kuharibu sanamu zao na kuvunja-vunja nguzo zao takatifu.+ 25 Munapaswa kumutumikia Yehova Mungu wenu,+ naye atabariki mukate wako na maji yako.+ Nitaondoa magonjwa kati yako.+ 26 Mimba ya wanamuke katika inchi yako haitaharibika wala hawatakuwa tasa,+ na nitakupatia maisha ya murefu.*
27 “Nitatuma woga wangu mbele yako,+ na nitavuruga watu wote wenye utakutana nao, na nitafanya maadui wako wote washindwe na kukimbia.+ 28 Nitatuma hisia ya kuvunjika moyo* mbele yako,+ na itawakimbiza Wahivi, Wakanaani, na Wahiti mbele yako.+ 29 Sitawafukuza watoke mbele yako katika mwaka mumoja, ili inchi isikuwe ukiwa na ili wanyama wa pori wasiongezeke na kukushambulia.+ 30 Nitawafukuza hatua kwa hatua watoke mbele yako, mupaka uzae na kuongezeka na kuriti ile inchi.+
31 “Nitaweka mupaka wako kuanzia Bahari Nyekundu kufikia bahari ya Wafilisti na kuanzia jangwa kufikia ule Muto;*+ kwa maana nitatia wakaaji wa inchi hiyo katika mukono wako, na utawafukuza watoke mbele yako.+ 32 Haupaswe kufanya agano pamoja nao wala pamoja na miungu yao.+ 33 Hawapaswe kuishi katika inchi yako, ili wasikufanye unitendee zambi. Kama unatumikia miungu yao, hakika jambo hilo litakuwa mutego kwako.”+
24 Kisha akamuambia Musa: “Panda uende kwa Yehova, wewe na Haruni, Nadabu na Abihu,+ na wazee makumi saba (70) wa Israeli, na muiname mukiwa mbali. 2 Ni Musa peke yake atamukaribia Yehova; lakini wale wengine hawapaswe kukaribia, na watu hawapaswe kupanda pamoja naye.”+
3 Kisha Musa akakuja na kuambia watu maneno yote ya Yehova na maamuzi yote ya hukumu,+ na watu wote wakajibu kwa sauti moja: “Maneno yote yenye Yehova amesema, tuko tayari kuyafanya.”+ 4 Kwa hiyo Musa akaandika maneno yote ya Yehova.+ Kisha akaamuka asubui sana na kujenga kwenye sehemu ya chini ya mulima huo mazabahu na nguzo kumi na mbili (12) kulingana na hesabu ya makabila kumi na mbili ya Israeli. 5 Kisha akatuma vijana Waisraeli, nao wakatoa matoleo ya kuteketezwa na wakatoa ngombe-dume kuwa zabihu za ushirika+ kwa Yehova. 6 Kisha Musa akakamata nusu ya damu na kuitia katika mabakuli, na ile nusu ingine ya damu akainyunyiza* juu ya mazabahu. 7 Halafu akakamata kitabu cha agano na kukisomea watu kwa sauti kubwa.+ Na watu wakasema: “Mambo yote yenye Yehova amesema tuko tayari kuyafanya, na tutatii.”+ 8 Kwa hiyo Musa akakamata damu akainyunyiza* juu ya watu+ na kusema: “Hii ndiyo damu ya agano lenye Yehova amefanya pamoja na ninyi kupatana na maneno hayo yote.”+
9 Musa na Haruni, Nadabu na Abihu, na wazee makumi saba (70) wa Israeli wakapanda kwenye mulima, 10 na wakamuona Mungu wa Israeli.+ Chini ya miguu yake kulikuwa kitu chenye kufanana sakafu* ya yakuti, na ilikuwa safi kama mbingu zenyewe.+ 11 Naye hakuumiza wanaume hao wenye kuheshimiwa sana wa Israeli,+ na walipata maono ya Mungu wa kweli na walikula na kunywa.
12 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Panda ukuje kwangu kwenye mulima na ubakie kule. Nitakupatia mabamba ya majiwe yenye kuwa na sheria na amri zenye nitaandika ili kuwafundisha.”+ 13 Kwa hiyo Musa na Yoshua mutumishi wake wakasimama,+ na Musa akapanda kwenye mulima wa Mungu wa kweli.+ 14 Lakini alikuwa ameambia wale wazee: “Mutungojee hapa mupaka wakati tutarudia.+ Haruni na Huru+ wako pamoja na ninyi. Kila mutu mwenye kuwa na kesi ya hukumu aende kuwaona.”+ 15 Kisha Musa akapanda kwenye mulima na wakati huo wingu lilikuwa linafunika mulima.+
16 Utukufu wa Yehova+ uliendelea kukaa juu ya Mulima Sinai,+ na wingu likafunika mulima huo kwa siku sita (6). Siku ya saba (7) akamuita Musa kutoka katikati ya lile wingu. 17 Kwa Waisraeli wenye walikuwa wanaangalia, utukufu wa Yehova ulionekana kama moto wenye kuteketeza kwenye kichwa cha mulima. 18 Kisha Musa akaingia ndani ya wingu na kupanda kwenye mulima.+ Na Musa akakaa kwenye mulima siku makumi ine (40), muchana na usiku.+
25 Kisha Yehova akamuambia Musa: 2 “Ambia watu wa Israeli wanifanyie muchango; munapaswa kukusanya muchango wangu kutoka kwa kila mutu mwenye moyo wake unamuchochea.+ 3 Huu ndio muchango wenye utapokea kutoka kwao: zahabu,+ feza,+ shaba,+ 4 uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau,* kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa,* kitani kizuri, manyoya ya mbuzi, 5 ngozi za kondoo-dume zenye kutiwa rangi nyekundu, ngozi za sili,* mbao za muti wa mugunga,*+ 6 mafuta kwa ajili ya taa,+ zeri kwa ajili ya mafuta ya kutia mafuta+ na kwa ajili ya uvumba wenye marashi,+ 7 na majiwe ya shohamu na majiwe mengine ya kuweka kwenye efodi+ na kifuko cha kifua.+ 8 Watanifanyia patakatifu, na mimi nitakaa kati yao.+ 9 Mutaifanya, tabenakulo na vyombo vyake vyote, kwa kufuata kabisa na mufano wenye ninakuonyesha.+
10 “Watafanya sanduku la mbao za muti wa mugunga* lenye urefu wa mikono mbili na nusu* na upana wa mukono mumoja na nusu na urefu kuenda juu wa mukono mumoja na nusu.+ 11 Kisha utafunika sanduku hilo kwa zahabu safi.+ Utalifunika ndani na inje, na utatengeneza ukingo wa zahabu kulizunguka pande zote.+ 12 Na utalitengenezea pete ine (4) za zahabu na kuzifunga juu ya miguu yake ine, pete mbili upande mumoja na pete mbili upande wa pili. 13 Na utatengeneza fito za muti wa mugunga* na kuzifunika zahabu.+ 14 Utapitisha fito hizo ndani ya zile pete zenye kuwa kwenye pande za Sanduku ili kubeba Sanduku hilo. 15 Fito hizo za miti zitabakia ndani ya pete za Sanduku; hazipaswe kuondolewa kwenye Sanduku.+ 16 Utaweka ndani ya Sanduku hilo Ushuhuda wenye nitakupatia.+
17 “Utatengeneza kifuniko cha zahabu safi chenye urefu wa mikono mbili na nusu na upana wa mukono mumoja na nusu.+ 18 Utatengeneza makerubi wawili wa zahabu; utawatengeneza kwa kutumia nyundo* juu ya miisho mbili ya kifuniko hicho.+ 19 Tengeneza makerubi juu ya miisho mbili, kerubi mumoja kwenye kila mwisho wa kifuniko. 20 Makerubi hao watanyoosha mabawa yao mbili kuelekea juu, na kufunika kifuniko kwa kivuli cha mabawa yao,+ na wataangaliana. Nyuso za makerubi hao zitakuwa zenye kuangalia kifuniko. 21 Utaweka kifuniko hicho+ juu ya Sanduku, na ndani ya Sanduku utaweka Ushuhuda wenye nitakupatia. 22 Nitakutokea pale na nitazungumuza na wewe kutoka juu ya kifuniko hicho.+ Kutoka katikati ya hao makerubi wawili wenye kuwa juu ya sanduku la Ushuhuda, nitakujulisha amri zote zenye nitapatia Waisraeli.
23 “Pia utatengeneza meza+ ya mbao za muti wa mugunga* yenye urefu wa mikono mbili na upana wa mukono mumoja na urefu kuenda juu wa mukono mumoja na nusu.+ 24 Utaifunika kwa zahabu safi na utatengeneza ukingo wa zahabu kuizunguka. 25 Utatengeneza mupaka wenye kuinuka wenye upana wa kiganja kimoja* cha mukono kuizunguka na ukingo wa zahabu kuzunguka mupaka huo. 26 Utaitengenezea pete ine (4) za zahabu na kuzitia kwenye pembe ine, mahali kila muguu wa miguu hiyo ine ulikuwa umeunganishwa. 27 Pete hizo zitakuwa karibu na mupaka huo wenye kuinuka ili fito za kubebea meza hiyo zipitishwe ndani ya pete hizo. 28 Utatengeneza fito za muti wa mugunga* na kuzifunika kwa zahabu na watu watazitumia ili kubebea meza hiyo.
29 “Pia utatengeneza sahani zake, vikombe vyake, na mitungi yake na mabakuli yenye watatumia ili kumwanga matoleo ya kinywaji. Utatengeneza vyombo hivyo kwa zahabu safi.+ 30 Na utatia mikate ya wonyesho juu ya meza hiyo ili ikuwe mbele yangu kila wakati.+
31 “Utatengeneza kinara cha taa+ kwa zahabu safi. Kinara hicho cha taa kitatengenezwa kwa kutumia nyundo.* Sehemu yake ya chini, shina lake, matawi yake, vikombe vyake, mafundo yake, na maua yake yatakuwa kitu kimoja.+ 32 Na matawi sita (6) yatatoka kwenye pande zote za kinara hicho na kupanda juu, matawi tatu (3) yatatoka upande mumoja na matawi tatu yatatoka upande mwingine. 33 Vikombe tatu (3) vyenye umbo ya maua ya muti wa lozi vitakuwa kwenye kila moja la matawi, pamoja na mafundo na maua yenye kufuatana, na vikombe tatu vyenye umbo ya maua ya muti wa lozi kwenye matawi mengine, pamoja na mafundo na maua yenye kufuatana. Ni vile matawi hayo sita (6) yatatoka katika shina la kinara hicho na kupanda juu. 34 Kwenye shina la kinara hicho cha taa kuko vikombe ine (4) vyenye umbo ya maua ya muti wa lozi, pamoja na mafundo yake na maua yake yenye kufuatana. 35 Kutakuwa fundo moja chini ya matawi mbili ya kwanza yenye kutoka kwenye shina na kupanda juu na kutakuwa fundo moja chini ya matawi mbili yenye kufuata na fundo moja chini ya matawi mbili yenye kufuata, kwa ajili ya matawi sita (6) yenye kutoka kwenye shina na kupanda juu. 36 Mafundo na matawi na kinara chote cha taa vinapaswa kuwa kitu kimoja cha zahabu safi, chenye kilitengenezwa kwa kutumia nyundo.*+ 37 Utatengeneza taa saba (7) kwa ajili ya kinara hicho, na wakati taa hizo zinawashwa zitaangazia nafasi yenye kuwa mbele ya kinara hicho.+ 38 Vifaa vyake vya kushikia tambi* na vyetezo vyake vitatengenezwa kwa zahabu safi.+ 39 Kinara hicho pamoja na vyombo vyake vyote vitatengenezwa kwa talanta moja* ya zahabu safi. 40 Uhakikishe kwamba unatengeneza vitu hivyo kulingana na mufano wavyo wenye ulionyeshwa kwenye mulima.+
26 “Utatengeneza tabenakulo+ kwa vitambaa kumi (10) vya hema vya kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, na kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa. Utashona kwa uzi michoro+ ya makerubi+ kwenye vitambaa hivyo vya hema. 2 Kila kitambaa cha hema kitakuwa na urefu wa mikono* makumi mbili na munane (28) na upana wa mikono ine (4). Vitambaa vyote vya hema vitakuwa na kipimo kilekile.+ 3 Vitambaa tano (5) vya hema vitaunganishwa pamoja na kuwa muunganisho mumoja, na vile vitambaa tano vingine vitaunganishwa pamoja na muunganisho mumoja. 4 Utatengeneza viviringo vya uzi ya rangi ya bluu kwenye upindo wa kitambaa kimoja cha hema chenye kuwa kwenye mwisho wa kile kitambaa kimoja kirefu, na utafanya vilevile kwenye upindo wa inje kabisa wa kile kitambaa kingine mahali kwenye vitaunganishwa. 5 Utatengeneza viviringo makumi tano (50) vya uzi kwenye kitambaa kimoja cha hema na viviringo vingine makumi tano vya uzi kwenye upindo wa kile kitambaa kingine cha hema ili viviringo hivyo vya uzi viangaliane mahali kwenye vitaunganishwa. 6 Utatengeneza vifungo makumi tano (50) vya zahabu na kuunganisha pamoja vitambaa hivyo vya hema kwa kutumia vifungo hivyo, na tabenakulo itakuwa hema moja.+
7 “Pia utatengeneza vitambaa vya manyoya ya mbuzi+ kwa ajili ya hema yenye kuwa juu ya tabenakulo. Utatengeneza vitambaa kumi na moja (11) vya hema.+ 8 Kila kitambaa cha hema kitakuwa na urefu wa mikono makumi tatu (30) na upana wa mikono ine (4). Vitambaa vyote kumi na moja (11) vya hema vitakuwa na kipimo kilekile. 9 Utaunganisha pamoja vitambaa tano (5) vya hema na utaunganisha pamoja vitambaa vingine sita (6) vya hema, na kitambaa cha sita cha hema utakikunja upande wa mbele wa hema. 10 Na utatengeneza viviringo makumi tano (50) vya uzi kwenye upindo wa kitambaa kimoja cha hema, kitambaa cha inje kabisa cha ule muunganisho mumoja, na viviringo makumi tano vya uzi kwenye upindo wa kitambaa kingine cha hema, mahali kwenye vitaunganishwa. 11 Na utatengeneza vifungo makumi tano (50) vya shaba na kuingiza vifungo hivyo katika viviringo hivyo vya uzi na kuunganisha hema pamoja, na hema hiyo itakuwa kitu kimoja. 12 Sehemu yenye kubakia ya vitambaa vya hema itaninginia. Nusu yenye kubakia ya kitambaa cha hema itaninginia upande wa nyuma wa tabenakulo. 13 Sehemu yenye kubakia katika urefu wa vitambaa hivyo vya hema itaninginia pande zote za tabenakulo kwa urefu wa mukono mumoja kila upande, ili kufunika tabenakulo hiyo.
14 “Utatengeneza pia kifuniko cha hema kwa kutumia ngozi za kondoo-dume zenye kutiwa rangi nyekundu na juu yake kifuniko cha ngozi za sili.*+
15 “Utatengeneza kadre za mbao+ za muti wa mugunga* zenye kuwa wima kwa ajili ya tabenakulo hiyo.+ 16 Kila kadre ya mbao itakuwa na urefu wa mikono kumi (10) na upana wa mukono mumoja na nusu. 17 Kila kadre ya mbao itakuwa na ndimi* mbili zenye kuunganishwa pamoja. Ni vile utatengeneza kadre zote za mbao za tabenakulo. 18 Utatengeneza kadre makumi mbili (20) za mbao kwa ajili ya upande wa kusini wa tabenakulo, kuelekea kusini.
19 “Utatengeneza vikalio makumi ine (40) vya feza+ chini ya zile kadre makumi mbili (20) za mbao: vikalio mbili chini ya kadre moja ya mbao kwa ajili ya ndimi zake mbili na vikalio mbili chini ya kila kadre ya mbao yenye kufuata kwa ajili ya ndimi zake mbili.+ 20 Kwa ajili ya upande mwingine wa tabenakulo, upande wa kaskazini, tengeneza kadre makumi mbili (20) za mbao 21 pamoja na vikalio vyake makumi ine (40) vya feza, vikalio mbili chini ya kadre moja ya mbao na vikalio mbili chini ya kila kadre ya mbao yenye kufuata. 22 Kwa ajili ya sehemu ya nyuma ya tabenakulo kuelekea upande wa mangaribi, utatengeneza kadre sita (6) za mbao.+ 23 Utatengeneza kadre mbili za mbao ili zikuwe nguzo* mbili za pembe upande wa nyuma wa tabenakulo. 24 Kadre hizo za mbao zitakuwa mbili-mbili kuanzia chini mupaka juu, mupaka kwenye pete ya kwanza. Ni vile itafanywa kwa ajili ya zote mbili, na kadre hizo za mbao zitafanyiza nguzo mbili za pembe. 25 Na kutakuwa kadre munane (8) za mbao na vikalio vyake kumi na sita (16) vya feza, vikalio mbili chini ya kadre moja ya mbao na vikalio mbili chini ya kila kadre ya mbao yenye kufuata.
26 “Utatengeneza fito za muti wa mugunga,* fito tano (5) kwa ajili ya kadre za mbao za upande mumoja wa tabenakulo,+ 27 na fito tano (5) kwa ajili ya kadre za mbao za upande mwingine wa tabenakulo, na fito tano kwa ajili ya kadre za mbao za tabenakulo kuelekea upande wa mangaribi, kwa ajili ya sehemu ya nyuma. 28 Ufito wenye kupita katikati ya kadre za mbao utatoka mwisho mumoja mupaka mwisho mwingine.
29 “Utafunika kadre hizo za mbao kwa zahabu,+ na utatengeneza pete za kadre hizo za mbao kwa zahabu ili zishikilie fito hizo, na utafunika fito hizo kwa zahabu. 30 Unapaswa kusimamisha tabenakulo kulingana na plani yenye ulionyeshwa kwenye mulima.+
31 “Utatengeneza pazia+ la uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa. Utashona kwa uzi michoro ya makerubi kwenye pazia hilo. 32 Utaninginiza pazia hilo kwenye nguzo ine (4) za muti wa mugunga* zenye kufunikwa kwa zahabu. Kulabu* zake zitakuwa za zahabu. Nguzo hizo zitakaa juu ya vikalio ine vya feza. 33 Utaninginiza pazia hilo chini ya vifungo na kuleta sanduku la Ushuhuda+ pale ndani ya pazia. Pazia hilo litatenganisha Patakatifu+ na Patakatifu Zaidi.+ 34 Unapaswa kutia kile kifuniko juu ya sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu Zaidi.
35 “Utaweka ile meza inje ya pazia, na kinara cha taa+ kitaangaliana na meza hiyo upande wa kusini wa tabenakulo; na utaweka ile meza upande wa kaskazini. 36 Utatengeneza kitambaa cha kuficha* kwa ajili ya muingilio wa hema kwa kutumia uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa na kufumwa pamoja.+ 37 Utatengeneza nguzo tano (5) za muti wa mugunga* kwa ajili ya kitambaa cha kuficha* na utazifunika kwa zahabu. Kulabu* zake zitakuwa za zahabu, na utazitengenezea vikalio tano vya shaba.
27 “Utatengeneza mazabahu kwa kutumia mbao za muti wa mugunga;*+ itakuwa na urefu wa mikono* tano (5) na upana wa mikono tano. Mazabahu hiyo itakuwa na pande ine (4) zenye kuwa sawasawa,* na urefu wake kuenda juu utakuwa mikono tatu (3).+ 2 Utatengeneza pembe+ kwenye kona zake ine (4); pembe hizo zitakuwa sehemu ya mazabahu, na utafunika mazabahu hiyo kwa shaba.+ 3 Utatengeneza mbeketi za kuondolea majivu* ya mazabahu, na pia vipao,* mabakuli, kanya,* na vyetezo; na utatengeneza vyombo vyote vya mazabahu kwa shaba.+ 4 Utatengeneza kayungio kwa ajili ya mazabahu, chombo cha fito za shaba, na kwenye chombo hicho utatengeneza pete ine (4) za shaba kwenye kona zake ine. 5 Utaingiza chombo hicho chini ya mupaka wa mazabahu, na chombo hicho kitaingia kufikia katikati ya mazabahu. 6 Utatengeneza fito za muti wa mugunga* kwa ajili ya mazabahu na kuzifunika kwa shaba. 7 Fito hizo zitaingizwa ndani ya zile pete ili fito hizo zikuwe kwenye pande mbili za mazabahu wakati inabebwa.+ 8 Utatengeneza mazabahu hiyo kama sanduku la mbao lenye kuwa wazi. Inapaswa kutengenezwa kama vile Yeye alikuonyesha kwenye mulima.+
9 “Utatengeneza kiwanja+ cha tabenakulo. Kwa ajili ya upande wa kusini, kuelekea kusini, kiwanja hicho kitakuwa na mapazia yenye kuninginia ya kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa; yatakuwa na urefu wa mikono mia moja (100) upande mumoja.+ 10 Kiwanja hicho kitakuwa na nguzo makumi mbili (20) na vikalio makumi mbili vya shaba. Kulabu* za nguzo hizo na vibanio* vyake vitakuwa vya feza. 11 Mapazia yenye kuninginia ya upande wa kaskazini yatakuwa pia na urefu wa mikono mia moja (100), pamoja na nguzo zake makumi mbili (20) na vikalio vyake makumi mbili vya shaba, lakini kulabu* za nguzo hizo na vibanio* vyake vitakuwa vya feza. 12 Kwenye upande wa mangaribi kutakuwa mapazia yenye kuninginia ya mikono makumi tano (50) kwa ajili ya upana wa kiwanja, na nguzo kumi (10) na vikalio kumi. 13 Upana wa kiwanja kwenye upande wa mashariki kuelekea mahali jua linatokea utakuwa wa mikono makumi tano (50). 14 Kutakuwa mapazia yenye kuninginia yenye urefu wa mikono kumi na tano (15) kwenye upande mumoja, pamoja na nguzo tatu (3) na vikalio tatu.+ 15 Na kwenye upande mwingine, kutakuwa mapazia yenye kuninginia ya mikono kumi na tano (15), pamoja na nguzo tatu (3) na vikalio tatu.
16 “Muingilio wa kiwanja utakuwa na kitambaa cha kuficha* chenye urefu wa mikono makumi mbili (20) chenye kutengenezwa kwa uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa na kufumwa pamoja,+ na nguzo ine (4) na vikalio vyake ine.+ 17 Nguzo zote zenye kuzunguka kiwanja hicho zitakuwa na viunganishi vya feza na kulabu* za feza, lakini vikalio vya nguzo hizo vitakuwa vya shaba.+ 18 Kiwanja hicho kitakuwa na urefu wa mikono mia moja (100),+ upana wa mikono makumi tano (50), na urefu kuenda juu wa mikono tano (5), na kitatengenezwa kwa kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa, na kitakuwa na vikalio vya shaba. 19 Vyombo na vitu vyote vyenye vitatumiwa katika utumishi wa tabenakulo, pamoja na misumari yote ya hema na misumari yote ya kiwanja, vitakuwa vya shaba.+
20 “Utaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni zenye zilipondwa kwa ajili ya mwangaza, ili taa ziendelee kuwaka kila wakati.+ 21 Katika hema ya mukutano, inje ya pazia lenye kuwa karibu na Ushuhuda,+ Haruni na wana wake watafanya mipango ili taa hizo ziendelee kuwaka kuanzia mangaribi mupaka asubui mbele ya Yehova.+ Hiyo ni sheria ya kudumu yenye Waisraeli wanapaswa kushika katika vizazi vyao vyote.+
28 “Utamuita Haruni ndugu yako kutoka kati ya Waisraeli, pamoja na wana wake, ili anitumikie akiwa kuhani+—Haruni,+ pamoja na Nadabu na Abihu,+ Eleazari na Itamari,+ wana wa Haruni.+ 2 Utamutengenezea Haruni ndugu yako nguo takatifu, kwa ajili ya utukufu na uzuri.+ 3 Utaambia wale wote wenye kuwa mafundi,* wenye nimejaza roho ya hekima,+ nao watatengeneza nguo za Haruni ili kumutakasa, kusudi anitumikie akiwa kuhani.
4 “Hizi ndizo nguo zenye watatengeneza: kifuko cha kifua,+ efodi,+ koti yenye haina mikono,+ kanzu yenye miraba-miraba, kilemba,+ na kitambaa cha kujifunga kiuno;+ watamutengenezea Haruni ndugu yako na wana wake nguo hizo takatifu, ili anitumikie akiwa kuhani. 5 Wafanyakazi hao wenye ufundi watatumia zahabu, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri.
6 “Watatengeneza efodi ya zahabu, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa, na michoro ya uzi inapaswa kushonewa juu yake.+ 7 Efodi itakuwa na vipande mbili vya nguo vya mabega vyenye vitaunganishwa kwenye miisho yake mbili. 8 Mukaba* wenye kusukwa,+ wenye kufungwa kwenye efodi ili kuishikilia muzuri mahali pake, utatengenezwa kwa vitu hivyohivyo: zahabu, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa.
9 “Utakamata majiwe mbili ya shohamu+ na kuchonga juu yake majina ya wana wa Israeli,+ 10 majina sita (6) juu ya jiwe moja na majina mengine sita juu ya jiwe lingine, kulingana na miaka yao ya kuzaliwa. 11 Muchonga-majiwe atachonga majina ya wana wa Israeli kwenye majiwe hayo mbili kama vile mutu anachonga muhuri.+ Kisha majiwe hayo yatatiwa katika vikalio vya zahabu. 12 Utaweka majiwe hayo mbili juu ya vipande vya nguo vya mabega vya efodi ili yakuwe majiwe ya ukumbusho kwa wana wa Israeli,+ na Haruni anapaswa kubeba majina yao mbele ya Yehova kwenye vipande mbili vya nguo vya mabega yake ili kuwa ukumbusho. 13 Utatengeneza vikalio vya zahabu 14 na minyororo mbili ya zahabu safi yenye kusukwa-sukwa kama kamba,+ na utafunga minyororo hiyo kwenye vikalio hivyo.+
15 “Utamuagiza fundi wa kushonea michoro kwenye nguo atengeneze kifuko cha kifua cha hukumu.+ Kinapaswa kutengenezwa kama efodi kwa kutumia zahabu, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa.+ 16 Kifuko hicho kinapaswa kuwa na pande ine (4) zenye kuwa sawasawa* wakati kinakunjwa mara mbili, urefu wa shubiri moja* na upana wa shubiri moja. 17 Unapaswa kuweka kwenye kifuko hicho majiwe yenye kupangwa katika mistari ine (4). Mustari wa kwanza utakuwa na zabarijadi, topazi, na zumaridi. 18 Mustari wa pili utakuwa na feruzi, yakuti, na yaspi. 19 Mustari wa tatu (3) utakuwa na jiwe la leshemi,* akiki, na ametisti. 20 Mustari wa ine (4) utakuwa na krisolito, shohamu, na yashefi. Majiwe hayo yatawekwa ndani ya vikalio vya zahabu. 21 Majiwe hayo yatalingana na majina kumi na mbili (12) ya wana wa Israeli. Kila jiwe litachongwa kama vile muhuri, kila jina litawakilisha moja la makabila kumi na mbili.
22 “Utatengeneza kwenye kifuko cha kifua minyororo yenye kusukwa-sukwa, kama kamba za zahabu safi.+ 23 Utatengenezea kifuko cha kifua pete mbili za zahabu na kufungia pete hizo mbili kwenye miisho mbili ya kifuko cha kifua. 24 Utapitisha zile kamba mbili za zahabu katika pete mbili zenye kuwa kwenye miisho ya kifuko cha kifua. 25 Utapitisha miisho mbili ya zile kamba mbili katika vile vikalio mbili, na unapaswa kufungia miisho hiyo kwenye vile vipande vya nguo vya mabega vya efodi, kwenye sehemu ya mbele. 26 Utatengeneza pete mbili za zahabu na kuziweka kwenye miisho mbili juu ya ukingo wa ndani wa kifuko cha kifua, kuelekeana na efodi.+ 27 Utatengeneza pete zingine mbili za zahabu upande wa mbele wa efodi, chini ya vipande mbili vya nguo vya mabega vya efodi, karibu na mahali kwenye inaunganishwa, juu ya mukaba* wenye kusukwa wa efodi.+ 28 Kifuko cha kifua kitabakia mahali pake kupitia kamba ya rangi ya bluu, itafungia pete zake kwenye pete za efodi. Hiyo itafanya kifuko cha kifua kibakie mahali pake kwenye efodi, juu ya mukaba* wenye kusukwa.
29 “Haruni atabeba majina ya wana wa Israeli juu ya moyo wake kwenye kile kifuko cha kifua cha hukumu wakati anaingia Patakatifu ili ikuwe ukumbusho wa kila wakati mbele ya Yehova. 30 Utaweka Urimu na Tumimu*+ ndani ya kifuko cha kifua cha hukumu, na zinapaswa kuwa juu ya moyo wa Haruni wakati anaingia mbele ya Yehova, na Haruni anapaswa kubeba vitu hivyo vya kufanyia hukumu kwa ajili ya Waisraeli kila wakati juu ya moyo wake mbele ya Yehova.
31 “Utatengeneza koti ya efodi yenye haina mikono kwa uzi ya rangi ya bluu peke yake.+ 32 Kutakuwa nafasi yenye kuwa wazi upande wa juu* katikati ya koti hiyo. Nafasi hiyo yenye kuwa wazi itakuwa na ukingo wenye kusukwa kuizunguka pande zote wenye utafanywa na musukaji wa nguo. Itakuwa kama vile nafasi yenye kuwa wazi ya koti ya chuma, ili isipasuke. 33 Kuzunguka upindo wake wote wa chini pande zote, utatengeneza makomamanga ya uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kutia kengele za zahabu katikati ya makomamanga hayo. 34 Utatia kengele ya zahabu kisha komamanga moja, kengele ya zahabu kisha komamanga moja, pande zote kuzunguka upindo wa chini wa koti yenye haina mikono. 35 Haruni anapaswa kuivaa ili afanye utumishi, na sauti yenye kutoka kwenye koti hiyo inapaswa kusikika wakati anaingia ndani ya patakatifu mbele ya Yehova na wakati anatoka inje, kusudi asikufe.+
36 “Utatengeneza bamba lenye kungaa la zahabu safi na kuchora juu yake kama vile mutu anachora kwenye muhuri: ‘Utakatifu ni wa Yehova.’+ 37 Utafunga bamba hilo kwenye kilemba+ kwa kamba ya rangi ya bluu; litakuwa kila wakati kwenye upande wa mbele wa kilemba. 38 Na bamba hilo litakuwa kwenye paji la uso wa Haruni, na Haruni atachukua hatia wakati mutu fulani anatenda kosa juu ya vitu vitakatifu,+ vyenye Waisraeli wanatakasa wakati wanavitoa kuwa zawadi takatifu. Bamba hilo litabakia kwenye paji la uso wake ili Waisraeli wapate kukubaliwa mbele ya Yehova.
39 “Utasuka kanzu ya kitani kizuri yenye miraba-miraba, utatengeneza kilemba cha kitani kizuri, na kitambaa cha kujifunga kiuno chenye kusukwa.+
40 “Pia utatengenezea wana wa Haruni kanzu, vitambaa vya kujifunga kiuno, na kitu cha kuvaa kwenye kichwa,+ kwa ajili ya utukufu na uzuri.+ 41 Utavalisha Haruni ndugu yako na wana wake, na utawatia mafuta+ na kuwaweka katika madaraka* yao+ na kuwatakasa, nao watanitumikia wakiwa makuhani. 42 Pia uwatengenezee kapitula* za kitani ili kufunika uchi wao.+ Kapitula hizo zitaanzia kwenye kiuno mupaka kwenye mapaja. 43 Haruni na wana wake wanapaswa kuzivaa wakati wanaingia katika hema ya mukutano ao wakati wanakaribia mazabahu ili kufanya utumishi katika mahali patakatifu, kusudi wasikuwe na hatia na kufa. Ni sheria ya kudumu kwa ajili yake na uzao wake* kisha yeye.
29 “Ni hivi utafanya ili kuwatakasa kusudi wanitumikie wakiwa makuhani: Kamata ngombe-dume mudogo, kondoo-dume wawili wenye hawana kasoro,+ 2 mikate yenye haina chachu, mikate ya muviringo yenye haina chachu na yenye kuchangwa na mafuta, na mikate myembamba yenye haina chachu na yenye imepakaliwa mafuta.+ Utaifanya kwa unga laini wa ngano 3 na kuitia ndani ya kitunga, na utaitoa ikiwa ndani ya kitunga,+ pamoja na ule ngombe-dume na wale kondoo-dume wawili.
4 “Utaleta Haruni na wana wake kwenye muingilio wa hema ya mukutano+ na utawanawisha na maji.+ 5 Kisha utakamata zile nguo+ na kumuvalisha Haruni ile kanzu, ile koti ya efodi yenye haina mikono, ile efodi, na kile kifuko cha kifua, na utafunga kwa kukaza ule mukaba* wenye kusukwa wa efodi kuzunguka kiuno chake.+ 6 Utaweka kile kilemba juu ya kichwa chake na kuweka ile alama takatifu ya kuwekwa pembeni kwa ajili ya kusudi la pekee* kwenye kilemba;+ 7 na utakamata mafuta ya kutia mafuta+ na kuyamwanga juu ya kichwa chake na kumutia mafuta.+
8 “Kisha utaleta wana wake na kuwavalisha zile kanzu+ 9 na utafunga kuzunguka viuno vya Haruni na pia wana wake vitambaa vya kujifunga kiuno, na utawavalisha kitu chao cha kuvaa kwenye kichwa; na ukuhani utakuwa wao, na hiyo itakuwa sheria ya kudumu.+ Ni vile utaweka Haruni na wana wake katika madaraka yao ili watumikie wakiwa makuhani.*+
10 “Sasa utaleta ule ngombe-dume mbele ya hema ya mukutano, na Haruni na wana wake watatia mikono yao juu ya kichwa cha ule ngombe-dume.+ 11 Uchinje ule ngombe-dume mbele ya Yehova, kwenye muingilio wa hema ya mukutano.+ 12 Kamata sehemu fulani ya damu ya ule ngombe-dume kwa kidole chako na kuitia kwenye pembe za mazabahu,+ na umwange damu yote yenye inabakia chini ya mazabahu.+ 13 Kisha ukamate mafuta yote+ yenye kufunika matumbotumbo, mafuta yenye kuwa juu ya maini, na zile figo mbili na mafuta yenye kuwa juu yake, na uchome vitu hivyo ili vitoe moshi juu ya mazabahu.+ 14 Lakini nyama ya ule ngombe-dume na ngozi yake na mavi yake utaviteketeza kwa moto inje ya kambi. Ni toleo la zambi.
15 “Kisha utakamata kondoo-dume mumoja, na Haruni na wana wake watatia mikono yao juu ya kichwa cha ule kondoo-dume.+ 16 Uchinje ule kondoo na ukamate damu yake na kuinyunyiza* kwenye pande zote za mazabahu.+ 17 Kata ule kondoo vipande-vipande, na usafishe matumbotumbo yake+ na miguu yake, na upange vipande hivyo pamoja na kichwa chake. 18 Unapaswa kuchoma kondoo yote muzima, ili itoe moshi kwenye mazabahu. Ni toleo la kuteketezwa kwa ajili ya Yehova, harufu ya muzuri.*+ Ni toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.
19 “Kisha utakamata ule kondoo-dume mwingine, na Haruni na wana wake watatia mikono yao juu ya kichwa cha ule kondoo-dume.+ 20 Uchinje ule kondoo na ukamate sehemu fulani ya damu yake na kuitia kwenye sehemu ya chini ya sikio la kuume la Haruni na kwenye sehemu ya chini ya sikio la kuume la wana wake na kwenye kidole kikubwa cha mukono wao wa kuume na kwenye kidole kikubwa cha muguu wao wa kuume, na unyunyize* damu pande zote za mazabahu. 21 Kisha ukamate sehemu fulani ya damu yenye kuwa kwenye mazabahu na sehemu fulani ya mafuta ya kutia mafuta+ na uyanyunyize* juu ya Haruni na juu ya nguo zake na juu ya wana wake na juu ya nguo zao, ili akuwe mutakatifu yeye na nguo zake na wana wake na nguo zao.+
22 “Kisha tosha mafuta ya ule kondoo-dume, mukia wenye mafuta, mafuta yenye kufunika matumbotumbo, mafuta yenye kuwa juu ya maini, zile figo mbili na mafuta yenye kuwa juu yake,+ na muguu wa kuume, kwa maana huyo ni kondoo-dume wa kuwaweka katika madaraka.+ 23 Kamata pia mukate wa muviringo na mukate wa muviringo wenye ulimwangiwa mafuta na mukate mwembamba katika kile kitunga cha mikate yenye haina chachu chenye kuwa mbele ya Yehova. 24 Unapaswa kutia vitu hivyo vyote katika mikono ya Haruni na katika mikono ya wana wake, na utavitikisa mbele na nyuma vikiwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova. 25 Kisha utavikamata kutoka katika mikono yao na kuviteketeza kwa moto juu ya mazabahu, juu ya toleo la kuteketezwa, ili vikuwe harufu ya muzuri* mbele ya Yehova. Ni toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.
26 “Kisha kamata kifua cha kondoo-dume wa kuwaweka katika madaraka yao,+ mwenye anatolewa kwa ajili ya Haruni, na ukitikise mbele na nyuma kikiwa toleo la kutikiswa mbele ya Yehova, na kifua hicho kitakuwa fungu lako. 27 Utatakasa kile kifua cha toleo la kutikiswa na ule muguu wa fungu takatifu wenye ulitikiswa na wenye uliondolewa kwenye ule kondoo-dume wa kuwaweka katika madaraka yao,+ mwenye alitolewa kwa ajili ya Haruni na wana wake. 28 Vitu hivyo vitakuwa vya Haruni na wana wake kulingana na sharti la kudumu lenye Waisraeli walipaswa kushika, kwa sababu vitu hivyo ni fungu takatifu, na vitakuwa fungu takatifu lenye litatolewa na Waisraeli.+ Ni fungu lao takatifu kwa ajili ya Yehova kutoka katika zabihu zao za ushirika.+
29 “Nguo takatifu+ za Haruni zitatumiwa na wana wake+ kisha yeye wakati watatiwa mafuta na kuwekwa kuwa makuhani. 30 Kuhani mwenye kutoka kati ya wana wake mwenye atakamata nafasi yake na mwenye ataingia katika hema ya mukutano ili kufanya utumishi katika mahali patakatifu atavaa nguo hizo kwa siku saba (7).+
31 “Utakamata ule kondoo-dume wa kumuweka katika madaraka na kutokotesha nyama yake katika mahali patakatifu.+ 32 Haruni na wana wake watakula+ nyama ya ule kondoo-dume na mikate yenye kuwa katika kitunga kwenye muingilio wa hema ya mukutano. 33 Watakula vitu vyenye vilitumiwa ili kufunika zambi wakati waliwekwa kuwa makuhani na wakati walitakaswa. Lakini mutu mwenye haruhusiwe* hapaswe kula vitu hivyo, kwa maana ni vitu vitakatifu.+ 34 Kama nyama yoyote ya zabihu ya kumuweka katika madaraka na mukate wowote unabakia mupaka asubui, utaviteketeza kwa moto.+ Vitu hivyo havipaswe kukuliwa, kwa sababu ni vitu vitakatifu.
35 “Ni vile utamufanyia Haruni na wana wake, kulingana na yote yenye nimekuamuru. Utatumia siku saba (7) ili kuwaweka kuwa makuhani.*+ 36 Utatoa ngombe-dume kuwa toleo la zambi kila siku kwa ajili ya kufunika zambi, na utatakasa mazabahu kutokana na zambi kwa kufunika zambi kwa ajili ya mazabahu hiyo, na utaitia mafuta ili kuitakasa.+ 37 Utatumia siku saba (7) ili kufunika zambi kwa ajili ya mazabahu, na unapaswa kuitakasa ili ikuwe mazabahu takatifu sana.+ Mutu yeyote mwenye atagusa mazabahu hiyo anapaswa kuwa mutakatifu.
38 “Hivi ndivyo vitu vyenye utatoa kwenye mazabahu: wana-kondoo dume wawili wenye kuwa na mwaka mumoja kila siku, kwa kuendelea.+ 39 Toa mwana-kondoo dume mumoja asubui na ule mwana-kondoo dume mwingine mangaribi wakati giza linaanza.*+ 40 Sehemu moja ya kumi (1/10) ya kipimo cha efa* ya unga muzuri wenye kuchanganywa na sehemu moja ya ine (1/4) ya hini* ya mafuta yenye kupondwa, na toleo la kinywaji la sehemu moja ya ine (1/4) ya hini ya divai, vitatolewa pamoja na mwana-kondoo dume wa kwanza. 41 Utatoa mwana-kondoo dume wa pili mangaribi wakati giza linaanza,* pamoja na matoleo ya nafaka na kinywaji kama yale ya asubui. Utamutoa ili akuwe harufu ya muzuri,* toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto. 42 Litakuwa toleo la kuteketezwa lenye litatolewa kwa ukawaida katika vizazi vyenu vyote kwenye muingilio wa hema ya mukutano mbele ya Yehova, mahali kwenye nitawatokea ili kuzungumuza na ninyi pale.+
43 “Nitatokea Waisraeli pale, na mahali pale patatakaswa na utukufu wangu.+ 44 Nitatakasa hema ya mukutano na mazabahu, na nitatakasa Haruni na wana wake+ ili wanitumikie wakiwa makuhani. 45 Nitakaa kati ya watu wa Israeli, na nitakuwa Mungu wao.+ 46 Na hakika watajua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao, mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri ili nikae kati yao.+ Mimi ni Yehova Mungu wao.
30 “Utatengeneza mazabahu ili ikuwe mahali pa kuchomea uvumba;+ utaitengeneza na mbao za muti wa mugunga.*+ 2 Itakuwa na pande ine (4) zenye kuwa sawasawa;* itakuwa na urefu wa mukono mumoja,* upana wa mukono mumoja, na urefu wake kuenda juu mikono mbili. Pembe zake zitakuwa sehemu moja pamoja na mazabahu hiyo.+ 3 Utaifunika kwa zahabu safi: sehemu yake ya juu, kuizunguka pande zake zote, na pembe zake; na utatengeneza ukingo wa zahabu kuizunguka. 4 Pia, utaitengenezea pete mbili za zahabu chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili zenye kuelekeana, na pete hizo zitashikilia fito za kubebea mazabahu. 5 Tengeneza fito za muti wa mugunga* na kuzifunika kwa zahabu. 6 Utaiweka mbele ya pazia lenye kuwa karibu na sanduku la Ushuhuda,+ mbele ya kifuniko chenye kuwa juu ya Ushuhuda, mahali kwenye nitakutokea.+
7 “Haruni+ atachoma uvumba wenye marashi+ juu ya mazabahu hiyo,+ na kuufanya utoe moshi juu ya mazabahu wakati anashugulikia zile taa+ kila asubui. 8 Pia, wakati Haruni anawasha zile taa mangaribi mbele ya giza kuanza,* atachoma uvumba. Ni toleo la uvumba lenye linatolewa kwa ukawaida mbele ya Yehova katika vizazi vyenu vyote. 9 Hamupaswe kutoa juu yake uvumba wenye hauruhusiwe+ ao kutoa juu yake toleo la kuteketezwa ao toleo la nafaka, na hamupaswe kumwanga juu yake toleo la kinywaji. 10 Haruni anapaswa kufunika zambi juu ya pembe za mazabahu hiyo mara moja kwa mwaka.+ Kwa kutumia sehemu fulani ya damu ya toleo la zambi la kufunika zambi,+ atafunika zambi kwa ajili ya mazabahu hiyo mara moja kwa mwaka katika vizazi vyenu vyote. Ni mazabahu takatifu sana kwa ajili ya Yehova.”
11 Kisha Yehova akamuambia Musa: 12 “Kila mara wakati unaandikisha na kuhesabia wana wa Israeli,+ kila mumoja wao anapaswa kumupatia Yehova bei ya ukombozi kwa ajili ya uzima wake* wakati anaandikishwa. Watafanya vile ili wasipatwe na pigo lolote wakati wanaandikishwa. 13 Wote wenye kuandikishwa watatoa nusu ya shekeli* kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.*+ Gera* makumi mbili (20) ni sawa na shekeli moja. Nusu shekeli ni muchango kwa ajili ya Yehova.+ 14 Kila mutu mwenye kuandikishwa mwenye kuwa na miaka makumi mbili (20) na zaidi atatoa muchango wa Yehova.+ 15 Tajiri asitoe zaidi na maskini asitoe chini ya nusu shekeli* kuwa muchango kwa ajili ya Yehova ili kufunika zambi kwa ajili ya uzima wenu.* 16 Utakamata feza za kufunika zambi kutoka kwa Waisraeli na kuzitoa kwa ajili ya utumishi wa hema ya mukutano, ili zikuwe kumbukumbu mbele ya Yehova kwa ajili ya Waisraeli, ili zifunike zambi kwa ajili ya uzima wenu.”*
17 Yehova akazungumuza tena na Musa, na kusema: 18 “Tengeneza beseni ya kunawia ya shaba pamoja na kitu cha kuweka beseni juu yake;+ kisha uitie katikati ya hema ya mukutano na mazabahu na utie maji ndani ya beseni hiyo.+ 19 Haruni na wana wake watanawa mikono yao na miguu yao pale.+ 20 Wakati wanaingia katika hema ya mukutano ao wakati wanaenda karibu na mazabahu ili kufanya utumishi na kutoa matoleo ya moto na moshi kwa ajili ya Yehova, watanawa kwa maji kusudi wasikufe. 21 Wanapaswa kunawa mikono na miguu ili wasikufe, na hiyo itakuwa sharti la kudumu kwa ajili yao, kwa ajili ya Haruni na uzao wake, katika vizazi vyao vyote.”+
22 Yehova akaendelea kumuambia Musa: 23 “Kisha, kamata marashi ya muzuri sana: vipimo mia tano (500) vya manemane yenye kuganda, vipimo mia mbili makumi tano (250) vya mudalasini wenye harufu ya muzuri, vipimo mia mbili makumi tano vya kane yenye harufu ya muzuri, 24 na vipimo mia tano (500) vya kida, yenye kupimwa kwa shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,*+ pamoja na hini moja* ya mafuta ya zeituni. 25 Kisha utengeneze mafuta matakatifu ya kutia mafuta kutokana na vitu hivyo; vinapaswa kuchanganywa muzuri.*+ Yatakuwa mafuta matakatifu ya kutia mafuta.
26 “Utayatumia ili kutia mafuta hema ya mukutano+ na sanduku la Ushuhuda, 27 na pia meza na vyombo vyake vyote, kinara cha taa na vyombo vyake, mazabahu ya uvumba, 28 mazabahu ya toleo la kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na ile beseni pamoja na kitu cha kuweka beseni juu yake. 29 Unapaswa kuvitakasa ili vikuwe vitakatifu sana.+ Kila mutu mwenye anavigusa anapaswa kuwa mutakatifu.+ 30 Na utamutia mafuta Haruni+ na wana wake+ na utawatakasa ili wanitumikie wakiwa makuhani.+
31 “Utasema na Waisraeli, na kuwaambia, ‘Mafuta haya ya kutia mafuta yataendelea kuwa matakatifu kwangu katika vizazi vyenu.+ 32 Hayapaswe kupakwa kwenye ngozi ya mwanadamu, na ninyi hamupaswe kutengeneza kitu chochote chenye kuwa na muchanganyiko kama huo. Ni mafuta matakatifu. Yataendelea kuwa kitu kitakatifu kwenu. 33 Mutu yeyote mwenye anatengeneza mafuta yenye marashi kama hayo na kupakaa sehemu fulani ya mafuta hayo juu ya mutu mwenye haruhusiwe* anapaswa kuondolewa* katikati ya watu wangu.’”+
34 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Kamata vipimo vyenye kulingana vya marashi haya:+ matone ya natafi, shekeleti, kelbena yenye marashi, na ubani safi. 35 Uvifanye kuwa uvumba;+ muchanganyiko wa manukato unapaswa kuchanganywa muzuri,* kutiwa chumvi,+ kuwa safi, na unapaswa kuwa kitu kitakatifu. 36 Utaponda sehemu fulani ya vitu hivyo ili vikuwe unga laini na kutia sehemu fulani ya unga huo mbele ya Ushuhuda katika hema ya mukutano, mahali kwenye nitakutokea. Vitu hivyo vinapaswa kuwa vitakatifu sana kwenu. 37 Hamupaswe kutumia muchanganyiko huo ili kutengeneza uvumba kwa ajili ya matumizi yenu.+ Munapaswa kuuona kuwa kitu kitakatifu kwa ajili ya Yehova. 38 Kila mutu mwenye atatengeneza uvumba kama huo ili afurahie harufu yake anapaswa kuondolewa* katikati ya watu wake.”
31 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Angalia, nimemuchagua* Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda.+ 3 Nitamujaza roho ya Mungu, ili kumupatia hekima, uelewaji, na ujuzi wa kila namna ya ufundi, 4 ili atengeneze vyombo vya ufundi, ili afanye kazi ya zahabu, feza, na shaba, 5 ili achonge majiwe na kuyaweka katika vikalio vyake,+ na kutengeneza vitu vya mbao vya kila namna.+ 6 Pia, nimemuchagua Oholiabu+ mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani ili amusaidie, na ninatia hekima katika moyo wa wote wenye kuwa na ufundi,* ili watengeneze kila kitu chenye nilikuamuru:+ 7 hema ya mukutano,+ sanduku la Ushuhuda+ na kifuniko+ chenye kuwa juu yake, vifaa vyote vya hema, 8 meza+ na vyombo vyake, kinara cha taa cha zahabu safi na vyombo vyake vyote,+ mazabahu ya uvumba,+ 9 mazabahu ya toleo la kuteketezwa+ na vyombo vyake vyote, beseni na kitu cha kuweka beseni juu yake,+ 10 nguo zenye kusukwa muzuri, nguo takatifu za Haruni kuhani, nguo za wana wake ili watumikie wakiwa makuhani,+ 11 mafuta ya kutia mafuta, na uvumba wenye marashi kwa ajili ya patakatifu.+ Watafanya kila kitu chenye nimekuamuru.”
12 Yehova akaendelea kumuambia Musa: 13 “Sema na Waisraeli na kuwaambia, ‘Zaidi sana, mutashika sabato zangu,+ kwa maana ni alama kati yangu na ninyi katika vizazi vyenu ili mujue kwamba mimi, Yehova, ninawatakasa ninyi. 14 Munapaswa kushika Sabato, kwa maana ni kitu kitakatifu kwenu.+ Kila mutu mwenye ataichafua anapaswa kuuawa. Kama mutu yeyote anafanya kazi siku hiyo, basi mutu huyo anapaswa* kuondolewa* kati ya watu wake.+ 15 Kazi inaweza kufanywa kwa siku sita (6), lakini siku ya saba (7) ni sabato ya pumuziko kamili.+ Ni kitu kitakatifu kwa Yehova. Mutu yeyote mwenye atafanya kazi siku ya Sabato anapaswa kuuawa. 16 Waisraeli wanapaswa kushika Sabato; wanapaswa kushika Sabato katika vizazi vyao vyote. Ni agano la kudumu. 17 Ni alama ya kudumu kati yangu na watu wa Israeli,+ kwa sababu katika siku sita (6) Yehova alifanya mbingu na dunia na katika siku ya saba (7) alipumuzika na kustarehe.’”+
18 Sasa wakati tu alimaliza kuzungumuza naye kwenye Mulima Sinai, akamupatia Musa mabamba mbili ya Ushuhuda,+ mabamba ya majiwe yenye yaliandikwa na kidole cha Mungu.+
32 Wakati huo, watu wakaona kwamba Musa alikawia kushuka kutoka kwenye mulima.+ Kwa hiyo watu wakakusanyika kumuzunguka Haruni na kumuambia: “Simama, ututengenezee mungu mwenye ataenda mbele yetu,+ kwa sababu hatujue kile kimemufikia huyu Musa, ule mutu mwenye alitutosha katika inchi ya Misri.” 2 Basi Haruni akawaambia: “Mutoshe mahereni ya masikio+ ya zahabu kwenye masikio ya bibi zenu, ya watoto wenu wanaume, na ya watoto wenu wanamuke na muniletee.” 3 Kwa hiyo watu wote wakaanza kutosha mahereni ya masikio ya zahabu zenye zilikuwa kwenye masikio yao na kuzileta kwa Haruni. 4 Kisha akakamata zahabu kutoka kwao, na akatengeneza nayo sanamu* ya kitoto-dume cha ngombe kwa kutumia kifaa cha kuchongea.+ Watu wakaanza kusema: “Huyu ndiye Mungu wako, Ee Israeli, mwenye alikuongoza kutoka katika inchi ya Misri.”+
5 Wakati Haruni aliona jambo hilo, akajenga mazabahu mbele ya sanamu hiyo. Kisha akasema hivi kwa sauti kubwa: “Kesho kutakuwa sikukuu kwa ajili ya Yehova.” 6 Kwa hiyo wakaamuka asubui sana siku yenye ilifuata na kuanza kutoa matoleo ya kuteketezwa na zabihu za ushirika. Kisha mambo hayo watu wakakaa ili kula na kunywa. Kisha wakasimama ili kujifurahisha.+
7 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Uende, ushuke, kwa sababu watu wako, wenye uliongoza kutoka katika inchi ya Misri, wamejipotosha.+ 8 Wamegeuka haraka na kuacha njia yenye niliwaamuru wafuate.+ Wamejifanyia sanamu* ya kitoto-dume cha ngombe, na wanaendelea kuiinamia na kuitolea zabihu na kusema, ‘Huyu ndiye Mungu wako, Ee Israeli, mwenye alikuongoza kutoka katika inchi ya Misri.’” 9 Yehova akaendelea kumuambia Musa: “Nimeona kwamba watu wako kichwa-nguvu.*+ 10 Kwa hiyo sasa niache, niwaharibu kwa kasirani yangu yenye kuwaka, na uache nikufanye wewe kuwa taifa kubwa pa nafasi yao.”+
11 Kisha Musa akamulilia* Yehova Mungu wake+ na kusema: “Ee Yehova, sababu gani ugeuzie kasirani yako yenye kuwaka juu ya watu wako kisha kuwatosha katika inchi ya Misri kwa nguvu kubwa na kwa mukono wenye nguvu?+ 12 Sababu gani Wamisri waseme, ‘Alikuwa na nia mubaya wakati aliwatosha Misri. Alitaka kuwaua katika milima na kuwaangamiza wasikuwe tena juu ya uso wa dunia’?+ Acha kasirani yako yenye kuwaka na ubadilishe nia* kuhusu uamuzi wako wa kuleta musiba huu juu ya watu wako. 13 Kumbuka watumishi wako Abrahamu, Isaka, na Israeli, wenye uliapia kwa jina lako mwenyewe na kusema, ‘Nitafanya uzao wenu ukuwe mwingi* kama nyota za mbinguni,+ na nitapatia uzao wenu* inchi yote hii yenye niliwaahidi, ili waikamate kuwa uriti wa kudumu.’”+
14 Kwa hiyo Yehova akabadilisha nia yake* kuhusu musiba wenye alikuwa amesema kwamba ataleta juu ya watu wake.+
15 Kisha Musa akageuka na kushuka kutoka kwenye mulima akiwa amebeba yale mabamba mbili ya Ushuhuda+ katika mukono wake.+ Mabamba hayo yalikuwa yameandikwa pande zote mbili; yalikuwa yameandikwa upande wa mbele na upande wa nyuma. 16 Mabamba hayo yalitengenezwa na Mungu, na maandishi yenye yalichongwa juu ya mabamba hayo yalikuwa maandishi ya Mungu.+ 17 Wakati Yoshua alianza kusikia makelele ya watu wenye walikuwa wanasema kwa sauti kubwa, akamuambia Musa: “Kuko makelele ya vita katika kambi.” 18 Lakini Musa akasema:
“Haiko makelele ya nyimbo za ushindi,*
Na haiko makelele ya vilio vya kushindwa;
Ninasikia makelele ya nyimbo za namna ingine.”
19 Wakati tu Musa alifika karibu na kambi na kuona ile sanamu ya kitoto-dume cha ngombe+ na dansi, kasirani yake ikaanza kuwaka, na akatupa chini yale mabamba mbili yenye yalikuwa katika mikono yake na akayavunja-vunja chini ya mulima.+ 20 Akakamata ile sanamu ya kitoto-dume cha ngombe yenye walikuwa wametengeneza na akaiteketeza kwa moto na kuiponda-ponda na kuifanya kuwa ungaunga;+ kisha akasambaza ungaunga huo juu ya maji na akalazimisha Waisraeli kunywa maji hayo.+ 21 Na Musa akamuambia Haruni: “Watu hawa walikufanya nini hivi kwamba umeleta zambi kubwa juu yao?” 22 Haruni akajibu: “Usikasirike, bwana wangu. Unajua muzuri kwamba watu hawa wako na muelekeo wa kutenda maovu.+ 23 Kwa hiyo waliniambia, ‘Ututengenezee mungu mwenye ataenda mbele yetu, kwa sababu hatujue kile kimemufikia huyu Musa, ule mutu mwenye alitutosha katika inchi ya Misri.’+ 24 Kwa hiyo niliwaambia, ‘Kila mutu mwenye iko* na zahabu aitoshe na kunipatia.’ Kisha nikaitupa ndani ya moto na hii sanamu ya kitoto-dume cha ngombe ikatokea.”
25 Musa akaona kwamba watu walikosa kujizuia, kwa sababu Haruni alikuwa amewaacha wakose kujizuia, na hivyo wakajizaraulisha mbele ya wapinzani wao. 26 Kisha Musa akasimama katika mulango mukubwa wa kambi na kusema: “Ni nani iko* upande wa Yehova? Akuje hapa kwenye niko!”+ Na Walawi wote wakakusanyika kumuzunguka. 27 Halafu Musa akawaambia: “Yehova Mungu wa Israeli amesema, ‘Kila mumoja wenu ajifunge upanga wake na kupita katika kambi yote, kutoka mulango mukubwa mupaka mulango mukubwa, amuue ndugu yake, jirani yake, na rafiki yake.’”+ 28 Walawi wakafanya kama vile Musa alisema. Kwa hiyo watu karibu elfu tatu (3 000) wakauawa siku hiyo. 29 Kisha Musa akasema: “Mujitakase leo kwa ajili ya Yehova, kwa sababu kila mumoja wenu amemushambulia mwana wake mwenyewe na ndugu yake mwenyewe;+ leo atawapatia baraka.”+
30 Siku yenye ilifuata, Musa akaambia watu: “Mulitenda zambi kubwa sana, na sasa nitapanda kuenda kwa Yehova ili nione kama ninaweza kufunika zambi yenu.”+ 31 Kwa hiyo Musa akarudia kwa Yehova na kusema: “Watu hawa wametenda zambi kubwa sana! Walijitengenezea mungu wa zahabu!+ 32 Lakini sasa ukipenda, samehe zambi yao;+ kama haiko vile, tafazali, unifute katika kitabu chako chenye umeandika.”+ 33 Hata hivyo, Yehova akamuambia Musa: “Kila mutu mwenye amenitendea zambi, nitamufuta katika kitabu changu. 34 Uende sasa, uongoze watu hao mupaka mahali kwenye nimekuambia. Angalia! Malaika wangu ataenda mbele yako,+ na siku hiyo yenye nitaomba hesabu itolewe, nitaleta azabu juu yao kwa sababu ya zambi yao.” 35 Kisha Yehova akaanza kuletea watu pigo kwa sababu walikuwa wametengeneza sanamu ya kitoto-dume cha ngombe, yenye Haruni alikuwa ametengeneza.
33 Yehova akaendelea kumuambia Musa: “Utoke hapa pamoja na watu wenye uliongoza kutoka katika inchi ya Misri. Muende katika inchi yenye nilimuapia Abrahamu, Isaka, na Yakobo, na kusema, ‘Nitaipatia uzao wako.’*+ 2 Nitatuma malaika mbele yako+ na nitafukuza Wakanaani, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.+ 3 Mupande kuenda kwenye inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+ Lakini mimi sitaenda katikati yenu, kwa sababu ninyi ni watu wenye kuwa kichwa-nguvu,*+ na ninaweza kuwaharibu katika njia.”+
4 Wakati watu walisikia maneno hayo makali, wakaanza kuomboleza, na hakuna mutu katikati yao mwenye alivaa mapambo yake. 5 Yehova akamuambia Musa: “Ambia Waisraeli, ‘Ninyi ni watu wenye kuwa kichwa-nguvu.*+ Ninaweza kuja mara moja katikati yenu na kuwaharibu.+ Sasa musivae mapambo yenu wakati ninafikiria jambo lenye nitawatendea.’” 6 Kwa hiyo kuanzia Mulima Horebu na kuendelea, Waisraeli hawakuvaa* mapambo yao.
7 Sasa Musa akakamata hema yake na kuisimamisha inje ya kambi, mbali kidogo na kambi, na akaiita hema ya mukutano. Kila mutu mwenye alitafuta muongozo wa Yehova+ alikuwa anaenda kwenye hema ya mukutano, yenye ilikuwa inje ya kambi. 8 Wakati tu Musa alikuwa anatoka ili aende kwenye hema hiyo, watu wote walikuwa wanainuka na kusimama kwenye muingilio wa mahema yao, na walikuwa wanamuangalia Musa mupaka wakati aliingia ndani ya hema hiyo. 9 Wakati tu Musa alikuwa anaingia ndani ya hema hiyo, ile nguzo ya wingu+ ilikuwa inashuka chini na kusimama kwenye muingilio wa hema hiyo wakati Mungu alikuwa anaongea na Musa.+ 10 Wakati watu wote waliona nguzo hiyo ya wingu ikisimama kwenye muingilio wa ile hema, kila mumoja wao alisimama na kuinama kwenye muingilio wa hema yake. 11 Yehova alikuwa anazungumuza na Musa uso kwa uso,+ kama vile mwanadamu anazungumuza na mwanadamu mwingine. Wakati Musa alirudia katika kambi, Yoshua+ mwana wa Nuni, mwenye alikuwa muhudumu na mutumishi wake,+ hakukuwa anatoka katika hema.
12 Sasa Musa akamuambia Yehova: “Angalia, unaniambia, ‘Ongoza watu hawa,’ lakini haujaniambia ni nani mwenye utatuma pamoja na mimi. Tena, umeniambia, ‘Ninakujua kwa jina* na pia umekubaliwa mbele ya macho yangu.’ 13 Tafazali, kama nimekubaliwa mbele ya macho yako, nijulishe njia zako,+ ili nikujue wewe na niendelee kukubaliwa mbele ya macho yako. Pia, kumbuka kwamba taifa hili ni watu wako.”+ 14 Kwa hiyo akasema: “Mimi mwenyewe nitaenda* pamoja na wewe,+ na nitakupatia pumuziko.”+ 15 Kisha Musa akamuambia: “Kama wewe mwenyewe* hauende pamoja na sisi, usitutoshe mahali hapa. 16 Itajulikana namna gani kwamba nimekubaliwa mbele ya macho yako, mimi na watu wako? Je, haitajulikana kama unaenda pamoja na sisi,+ ili mimi na watu wako tufanywe kuwa tofauti na watu wengine wenye kuwa juu ya uso wa dunia?”+
17 Yehova akaendelea kumuambia Musa: “Nitafanya pia jambo hilo lenye unaomba, kwa sababu umekubaliwa mbele ya macho yangu na ninakujua wewe kwa jina.” 18 Kisha Musa akamuambia: “Tafazali unionyeshe utukufu wako.” 19 Lakini akasema: “Nitapitisha wema wangu wote mbele ya uso wako, na nitatangaza jina la Yehova mbele yako;+ na nitamuonyesha wema ule mwenye ninaonyesha wema, na nitamuonyesha rehema ule mwenye ninataka kumuonyesha rehema.”+ 20 Lakini akaongeza: “Hauwezi kuona uso wangu, kwa sababu hakuna mwanadamu mwenye anaweza kuniona na kuishi.”
21 Yehova akaendelea kusema: “Angalia, kuko nafasi hapa karibu na mimi. Simama juu ya mwamba. 22 Wakati utukufu wangu utakuwa unapita, nitakutia katika shimo la mwamba, na nitakulinda kwa mukono wangu mupaka wakati nitakuwa nimepita. 23 Kisha nitatosha mukono wangu, na wewe utaona mugongo wangu. Lakini uso wangu hautaonekana.”+
34 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Ujichongee mabamba mbili ya majiwe kama yale ya kwanza,+ na nitaandika kwenye mabamba hayo maneno yenye yalikuwa kwenye yale mabamba ya kwanza,+ yenye ulivunja-vunja.+ 2 Ujitayarishe kwa ajili ya asubui, kwa sababu asubui utapanda Mulima Sinai na kusimama mbele yangu kule kwenye kichwa cha mulima.+ 3 Lakini mutu yeyote asipande pamoja na wewe, na mutu mwingine yeyote asionekane mahali popote juu ya mulima. Hata makundi ao mifugo isikule majani mbele ya mulima huo.”+
4 Kwa hiyo Musa akachonga mabamba mbili ya majiwe kama yale ya kwanza na akaamuka asubui sana na kupanda kwenye Mulima Sinai, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru, na alibeba yale mabamba mbili ya majiwe katika mukono wake. 5 Kisha Yehova akashuka+ katika wingu na akasimama pamoja naye kule na akatangaza jina la Yehova.+ 6 Yehova alipita mbele yake akitangaza: “Yehova, Yehova, Mungu mwenye rehema+ na huruma,*+ hakasirike haraka+ na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu*+ na kweli,*+ 7 mwenye kuonyesha upendo mushikamanifu kwa maelfu,+ mwenye kusamehe kosa na uovu na zambi,+ lakini hatakosa hata kidogo kupatia azabu wenye kosa,+ mwenye kuleta azabu juu ya wana na wajukuu kwa sababu ya kosa la baba zao, juu ya kizazi cha tatu (3) na juu ya kizazi cha ine (4).”+
8 Musa akafanya haraka kuinama na kushusha uso mupaka chini. 9 Kisha akasema: “Kama sasa nimekubaliwa mbele ya macho yako, Ee Yehova, basi tafazali, Yehova, uende pamoja na sisi na ukuwe katikati yetu,+ hata kama sisi tuko watu wenye kuwa kichwa-nguvu,*+ na usamehe kosa letu na zambi yetu,+ na utuchukue kuwa mali yako.” 10 Naye akasema: “Angalia, ninafanya agano: Nitafanya mbele ya watu wako wote mambo ya ajabu yenye sijapata kufanya katika dunia yote wala katika mataifa yote,+ na watu wote wenye munaishi kati yao wataona kazi za Yehova, kwa sababu nitafanya jambo lenye kuogopesha sana kwa ajili yenu.+
11 “Sikiliza kwa uangalifu mambo yenye ninakuamuru leo.+ Angalia, ninafukuza Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi kutoka mbele yako.+ 12 Ukuwe muangalifu ili usifanye agano pamoja na wakaaji wa inchi yenye unaenda ndani yake,+ ili agano hilo lisikuwe mutego kati yako.+ 13 Lakini mutabomoa mazabahu zao, mutavunja nguzo zao takatifu, na kukata miti yao mitakatifu.*+ 14 Hamupaswe kuinamia mungu mwingine,+ kwa sababu Yehova anajulikana kuwa* Mungu mwenye kutaka watu washikamane na yeye tu.* Ndiyo, yeye ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu.+ 15 Ukuwe muangalifu ili usifanye agano pamoja na wakaaji wa inchi, kwa maana wakati wanafanya ukahaba na miungu yao na kuitolea zabihu,+ mutu fulani atakualika na utakula sehemu ya zabihu yake.+ 16 Kisha hakika utachukua wamoja kati ya watoto wao wanamuke kwa ajili ya watoto wako wanaume,+ na watoto wao wanamuke watafanya ukahaba na miungu yao na watashawishi watoto wako wanaume wafanye ukahaba na miungu yao.+
17 “Haupaswe kutengeneza sanamu za miungu ya metali yenye kuyeyushwa.+
18 “Utafanya Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu.+ Utakula mikate yenye haina chachu, kama vile nimekuamuru; utafanya vile siku saba (7) kwa wakati wenye uliwekwa katika mwezi wa Abibu,*+ kwa sababu ulitoka Misri katika mwezi wa Abibu.
19 “Kila muzaliwa wa kwanza wa kiume ni wangu,*+ kutia ndani mifugo yako yote, ikuwe ngombe-dume wa kwanza ao kondoo.+ 20 Muzaliwa wa kwanza wa punda utamukomboa na kondoo. Lakini kama haumukomboe, basi utamuvunja shingo. Utakomboa kila muzaliwa wa kwanza wa wana wako.+ Mutu yeyote asionekane mbele yangu mikono wazi.
21 “Utafanya kazi kwa siku sita (6), lakini siku ya saba (7) utapumuzika.*+ Hata wakati wa kulima na wakati wa kuvuna, utapumuzika.
22 “Na utafanya Sikukuu ya Majuma kwa kutumia matunda ya kwanza yenye kukomaa ya mavuno ya ngano, na Sikukuu ya Kukusanya* katika mwisho wa mwaka.+
23 “Mara tatu (3) kwa mwaka, wanaume wako wote wanapaswa kuonekana mbele ya Bwana wa kweli, Yehova, Mungu wa Israeli.+ 24 Kwa maana nitafukuza mataifa mbele yako,+ na nitapanua eneo lako, na hakuna mutu mwenye atatamani inchi yako wakati utakuwa unapanda ili kuona uso wa Yehova Mungu wako mara tatu (3) kwa mwaka.
25 “Haupaswe kutoa damu ya zabihu yangu pamoja na kila kitu chenye kuwa na chachu.+ Zabihu ya sikukuu ya Pasaka haipaswe kuwekwa usiku wote mupaka asubui.+
26 “Matunda ya kwanza ya muzuri zaidi yenye kukomaa ya udongo wako utayaleta kwenye nyumba ya Yehova Mungu wako.+
“Haupaswe kutokotesha mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.”+
27 Yehova akaendelea kumuambia Musa: “Unapaswa kuandika maneno haya,+ kwa sababu kwa musingi wa maneno haya, ninafanya agano pamoja na wewe na pamoja na Israeli.”+ 28 Na Musa akabakia kule pamoja na Yehova kwa siku makumi ine (40), muchana na usiku. Hakukula mukate na hakukunywa maji.+ Na aliandika kwenye yale mabamba maneno ya agano hilo, zile Amri Kumi.*+
29 Kisha Musa akashuka kutoka kwenye Mulima Sinai, na yale mabamba mbili ya Ushuhuda yalikuwa katika mukono wake.+ Wakati alishuka kutoka kwenye mulima, Musa hakujua kwamba ngozi ya uso wake ilikuwa inatoa miali kwa sababu alikuwa amezungumuza na Mungu. 30 Wakati Haruni na Waisraeli wote walimuona Musa, waliona kwamba ngozi ya uso wake ilikuwa inatoa miali na waliogopa kumukaribia.+
31 Lakini Musa akawaita, kwa hiyo Haruni na wakubwa wote wa mukusanyiko wakamukaribia, na Musa akazungumuza nao. 32 Kisha Waisraeli wote wakaenda karibu naye, na akawapatia amri zote zenye Yehova alimupatia kwenye Mulima Sinai.+ 33 Wakati Musa alikuwa anamaliza kuzungumuza nao, alikuwa anaweka kitambaa juu ya uso wake.+ 34 Lakini wakati Musa alikuwa anaingia mbele ya Yehova ili kuzungumuza naye, alikuwa anatosha kile kitambaa mupaka wakati angetoka inje.+ Kisha kutoka inje alijulisha Waisraeli amri zenye alikuwa amepokea.+ 35 Na Waisraeli waliona kwamba ngozi ya uso wa Musa ilitoa miali; basi Musa alirudisha tena kitambaa kwenye uso wake mupaka wakati aliingia ili kuzungumuza na Mungu.*+
35 Kisha wakati fulani Musa akakusanya mukusanyiko wote wa Waisraeli na kuwaambia: “Haya ndiyo mambo yenye Yehova ameamuru yafanywe:+ 2 Kazi inaweza kufanywa kwa siku sita (6), lakini siku ya saba (7) itakuwa kitu kitakatifu kwa ajili yenu, sabato ya pumuziko kamili kwa ajili ya Yehova.+ Mutu yeyote mwenye atafanya kazi siku hiyo atauawa.+ 3 Hamupaswe kuwasha moto katika makao yenu yoyote katika siku ya Sabato.”
4 Kisha Musa akaambia mukusanyiko wote wa Waisraeli: “Yehova ameamuru hivi: 5 ‘Mumufanyie Yehova muchango kutoka katikati yenu.+ Kila mutu mwenye kuwa na moyo wa kupenda+ amuletee Yehova muchango: zahabu, feza, shaba, 6 uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, kitani kizuri, manyoya ya mbuzi,+ 7 ngozi za kondoo-dume zenye kutiwa rangi nyekundu, ngozi za sili,* mbao za muti wa mugunga,* 8 mafuta kwa ajili ya taa, zeri kwa ajili ya mafuta ya kutia mafuta na kwa ajili ya uvumba wenye marashi,+ 9 majiwe ya shohamu, na majiwe mengine ya kuweka kwenye efodi+ na kifuko cha kifua.+
10 “‘Watu wote wenye kujua ufundi*+ kati yenu wakuje na watengeneze kila kitu chenye Yehova ameamuru, 11 ni kusema, tabenakulo na hema yake na kifuniko chake, vifungo vyake na kadre zake za mbao, fito zake, nguzo zake, na vikalio vyake; 12 Sanduku+ na fito zake,+ kifuniko,+ na pazia+ kwa ajili ya kitambaa cha kuficha; 13 meza+ na fito zake na vyombo vyake vyote na mikate ya wonyesho;+ 14 kinara cha taa+ kwa ajili ya mwangaza na vyombo vyake na taa zake na mafuta ya kuangazia;+ 15 mazabahu ya uvumba+ na fito zake; mafuta ya kutia mafuta na uvumba wenye marashi;+ kitambaa cha kuficha cha* muingilio wa tabenakulo; 16 mazabahu ya toleo la kuteketezwa+ na kayungio yake ya shaba, fito zake na vyombo vyake vyote; beseni na kitu cha kuweka beseni juu yake;+ 17 mapazia yenye kuninginia ya kiwanja,+ nguzo zake na vikalio vyake; kitambaa cha kuficha cha* muingilio wa kiwanja; 18 misumari ya hema ya tabenakulo na misumari ya hema ya kiwanja na kamba zake;+ 19 nguo zenye kusukwa muzuri+ kwa ajili ya kufanya utumishi katika patakatifu, nguo takatifu za Haruni+ kuhani, na nguo za wana wake ili watumikie wakiwa makuhani.’”
20 Kwa hiyo mukusanyiko wote wa Waisraeli ukatoka mbele ya Musa. 21 Kisha kila mutu mwenye moyo wake ulimusukuma+ na kila mutu mwenye roho yake ilimuchochea, akakuja na kumuletea Yehova muchango wake ili utumiwe kwa ajili ya hema ya mukutano, kwa ajili ya utumishi wake wote, na kwa ajili ya nguo takatifu. 22 Wakaendelea kuja, wanaume pamoja na wanamuke, kila mutu mwenye moyo wa kupenda, akaleta mapambo ya kuvaliwa juu ya nguo, mahereni ya masikio, pete za vidole, na vitu vingine vya kujipamba, na pia vitu vya zahabu vya kila namna. Wote wakamuletea Yehova matoleo yao* ya zahabu.+ 23 Na wale wote wenye walikuwa na uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, kitani kizuri, manyoya ya mbuzi, ngozi za kondoo-dume zenye kutiwa rangi nyekundu, na ngozi za sili* wakavileta. 24 Wale wote wenye walitoa feza na shaba wakaleta muchango wa Yehova, na wale wote wenye walikuwa na mbao za muti wa mugunga* za kutumiwa katika kazi yoyote wakazileta.
25 Wanamuke wote wenye walikuwa na ufundi+ wakasuka kwa mikono yao, na wakaleta vitu vyenye walisuka: uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri. 26 Na wanamuke wote wenye walikuwa na ufundi na wenye mioyo yao ilisukuma wakasuka manyoya ya mbuzi.
27 Na wakubwa wakaleta majiwe ya shohamu na majiwe mengine ya kuweka kwenye efodi na kifuko cha kifua,+ 28 na zeri na mafuta kwa ajili ya kuangazia na kwa ajili ya mafuta ya kutia mafuta+ na kwa ajili ya uvumba wenye marashi.+ 29 Wanaume na wanamuke wote wenye mioyo yao ilisukuma wakaleta kitu fulani kwa ajili ya kazi yenye Yehova, kupitia Musa, aliamuru ifanywe; Waisraeli walimuletea Yehova vitu hivyo kama toleo la kujipendea.+
30 Kisha Musa akaambia Waisraeli: “Muangalie, Yehova amemuchagua Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda.+ 31 Amemujaza roho ya Mungu, ili kumupatia hekima, uelewaji, na ujuzi wa kila namna ya ufundi 32 ili atengeneze vyombo vya ufundi, ili afanye kazi ya zahabu, feza, na shaba, 33 ili achonge majiwe na kuyaweka katika vikalio vyake, na kutengeneza vitu vya mbao vya kila namna. 34 Na ameweka uwezo wa kufundisha katika moyo wa Bezaleli na pia katika moyo wa Oholiabu+ mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani. 35 Amewajaza ufundi+ wa* kufanya kazi zote za ufundi, kushona kwa uzi michoro juu ya nguo, na kusuka kwa kutumia uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri, na kazi yote ya musukaji wa nguo. Wanaume hao watafanya kazi za kila namna na kutayarisha michoro na kufikiria namna kila kitu kitatengenezwa.
36 “Bezaleli atafanya kazi pamoja na Oholiabu na kila mutu mwenye kuwa na ufundi* mwenye Yehova amepatia hekima na uelewaji ili kujua namna ya kufanya kazi yote ya utumishi mutakatifu kama vile Yehova ameamuru.”+
2 Kisha Musa akaita Bezaleli na Oholiabu na kila mutu mwenye ufundi mwenye Yehova alikuwa ameweka hekima katika moyo wake,+ kila mutu mwenye moyo wake ulimusukuma ili ajitolee kufanya kazi.+ 3 Kisha wakakamata kutoka kwa Musa michango yote+ yenye Waisraeli walikuwa wameleta kwa ajili ya kazi ya utumishi mutakatifu. Lakini, watu waliendelea kuleta matoleo ya kujipendea, asubui baada ya asubui.
4 Wakati walianza kufanya kazi takatifu, wafanyakazi wote wenye walikuwa na ufundi walikuja, mumoja kisha mwingine, 5 na walikuwa wanamuambia Musa: “Watu wanaleta vitu vingi kuliko vile vinaombwa kwa ajili ya kazi yenye Yehova ameamuru ifanywe.” 6 Kwa hiyo Musa akaamuru kwamba tangazo litolewe katika kambi yote, kwa kusema: “Wanaume na wanamuke, musilete vitu vingine tena kwa ajili ya muchango mutakatifu.” Basi watu wakazuiwa ili wasilete tena kitu kingine. 7 Vitu hivyo vilikuwa vyenye kuenea kwa ajili ya kazi yote yenye ilipaswa kufanywa, na vilikuwa vingi sana.
8 Kwa hiyo wafanyakazi wote wenye walikuwa na ufundi+ wakatengeneza tabenakulo+ ya vitambaa kumi (10) vya kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, na kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa; akashona* kwa uzi michoro ya makerubi juu ya vitambaa hivyo.+ 9 Kila kitambaa cha hema kilikuwa na urefu wa mikono* makumi mbili na munane (28) na upana wa mikono ine (4). Vitambaa vyote vilikuwa na kipimo kilekile. 10 Kisha akaunganisha pamoja vile vitambaa tano (5) vya hema, na vile vitambaa vingine tano akaviunganisha pamoja. 11 Kisha akatengeneza viviringo vya uzi ya rangi ya bluu kwenye upindo wa kitambaa kimoja cha hema mahali kingeunganishwa. Na akafanya vilevile kwenye upindo wa kitambaa cha inje kabisa cha hema mahali palepale kwenye kingeunganishwa. 12 Akatengeneza viviringo makumi tano (50) vya uzi kwenye kitambaa kimoja cha hema na viviringo makumi tano vya uzi kwenye upindo mwingine wa kitambaa mahali kingeunganishwa ili viviringo vya uzi viangaliane. 13 Mwishowe, akatengeneza vifungo makumi tano (50) vya zahabu na akaunganisha vitambaa vya hema pamoja kwa kutumia vifungo hivyo, kwa hiyo tabenakulo ikakuwa hema moja.
14 Kisha akatengeneza vitambaa vya hema vya manyoya ya mbuzi kwa ajili ya hema yenye kuwa juu ya tabenakulo. Akatengeneza vitambaa kumi na moja (11) vya hema.+ 15 Kila kitambaa cha hema kilikuwa na urefu wa mikono makumi tatu (30) na upana wa mikono ine (4). Vitambaa vyote kumi na moja (11) vya hema vilikuwa na kipimo kilekile. 16 Kisha akaunganisha pamoja vitambaa tano (5) vya hema, na akaunganisha pamoja vile vitambaa vingine sita (6) vya hema. 17 Halafu akatengeneza viviringo makumi tano (50) vya uzi kwenye upindo wa inje kabisa wa kitambaa cha hema mahali kinaunganishwa, na akatengeneza viviringo makumi tano vya uzi kwenye upindo wa kitambaa kingine cha hema chenye kuunganishwa nacho. 18 Na akatengeneza vifungo makumi tano (50) vya shaba vya kuunganisha hema pamoja kusudi ikuwe kitu kimoja.
19 Akatengeneza kifuniko cha hema kwa kutumia ngozi za kondoo-dume zenye kutiwa rangi nyekundu na kifuniko cha ngozi za sili* cha kuweka juu ya hema.+
20 Kisha akatengeneza kwa ajili ya tabenakulo kadre za mbao za muti wa mugunga,*+ zenye zilisimama wima.+ 21 Kila kadre ya mbao ilikuwa na urefu wa mikono kumi (10) na upana wa mukono mumoja na nusu. 22 Kila kadre ya mbao ilikuwa na ndimi* mbili zenye kuunganishwa pamoja. Ni vile alitengeneza kadre zote za mbao za tabenakulo. 23 Kwa hiyo akatengeneza kadre za mbao kwa ajili ya upande wa kusini wa tabenakulo, kadre makumi mbili (20) za mbao, kuelekea kusini. 24 Kisha akatengeneza vikalio makumi ine (40) vya feza ili kuwekwa chini ya zile kadre makumi mbili (20) za mbao, vikalio mbili chini ya kadre moja ya mbao kwa ajili ya ndimi zake mbili na vikalio mbili chini ya kila kadre ya mbao yenye kufuata kwa ajili ya ndimi zake mbili.+ 25 Kwa ajili ya upande mwingine wa tabenakulo, upande wa kaskazini, akatengeneza kadre makumi mbili (20) za mbao 26 na vikalio vyake makumi ine (40) vya feza, vikalio mbili chini ya kadre moja ya mbao na vikalio mbili chini ya kila moja ya zile kadre zingine za mbao.
27 Kwa ajili ya sehemu ya nyuma ya tabenakulo kuelekea upande wa mangaribi, akatengeneza kadre sita (6) za mbao.+ 28 Akatengeneza kadre mbili za mbao ili zikuwe nguzo mbili za pembe za tabenakulo kwenye pembe za nyuma. 29 Nguzo hizo zilikuwa mbili-mbili kuanzia chini mupaka juu, mupaka kwenye pete ya kwanza. Ni vile alitengeneza zile nguzo mbili za pembe. 30 Kwa hiyo zilifikia hesabu ya kadre munane (8) za mbao pamoja na vikalio vyake kumi na sita (16) vya feza, vikalio mbili chini ya kila kadre ya mbao.
31 Kisha akatengeneza fito za muti wa mugunga,* fito tano (5) kwa ajili ya kadre za mbao za upande mumoja wa tabenakulo+ 32 na fito tano (5) kwa ajili ya kadre za mbao za upande mwingine wa tabenakulo na fito tano kwa ajili ya kadre za mbao za tabenakulo kwa ajili ya sehemu ya nyuma kuelekea upande wa mangaribi. 33 Akatengeneza ufito wa katikati ili upite katikati ya zile kadre za mbao kuanzia mwisho mumoja mupaka mwisho mwingine. 34 Akafunika zile kadre za mbao kwa zahabu, na akatengeneza pete za zahabu za kadre hizo za mbao ili zishikilie fito hizo, na akafunika fito hizo kwa zahabu.+
35 Kisha akatengeneza pazia+ la uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa. Akashona kwa uzi michoro ya makerubi+ kwenye pazia hilo.+ 36 Kisha akaitengenezea nguzo ine (4) za muti wa mugunga* na kuzifunika kwa zahabu, akatengeneza pia kulabu* za zahabu na vikalio ine vya feza kwa ajili ya nguzo hizo. 37 Tena akatengeneza kitambaa cha kuficha* kwa ajili ya muingilio wa hema kwa kutumia uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa na kufumwa pamoja,+ 38 na pia nguzo zake tano (5) na kulabu* zake. Akafunika kwa zahabu sehemu za juu za nguzo hizo pamoja na vibanio* vyake, lakini vikalio vyake tano vilikuwa vya shaba.
37 Kisha Bezaleli+ akatengeneza sanduku+ la mbao za muti wa mugunga.* Lilikuwa na urefu wa mikono* mbili na nusu na upana wa mukono mumoja na nusu na urefu kuenda juu wa mukono mumoja na nusu.+ 2 Akalifunika ndani na inje kwa zahabu safi na akatengeneza ukingo wa zahabu kulizunguka.+ 3 Kisha akalitengenezea pete ine (4) za zahabu, za kuweka juu ya miguu yake ine, pete mbili upande wake mumoja na pete mbili upande wake mwingine. 4 Tena akatengeneza fito za muti wa mugunga* na kuzifunika kwa zahabu.+ 5 Halafu akapitisha fito hizo ndani ya zile pete zenye kuwa kwenye pande za Sanduku ili zitumiwe kubebea Sanduku hilo.+
6 Akatengeneza kifuniko cha zahabu safi.+ Kilikuwa na urefu wa mikono mbili na nusu na upana wa mukono mumoja na nusu.+ 7 Kisha akatengeneza makerubi wawili+ wa zahabu kwa kutumia nyundo* kwenye miisho mbili ya kifuniko hicho.+ 8 Kerubi moja alikuwa kwenye mwisho mumoja, na ule kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine wa kifuniko. Alitengeneza makerubi hao kwenye miisho mbili ya kifuniko. 9 Makerubi hao walinyoosha mabawa yao kuelekea juu, na walifunika kifuniko kwa kivuli cha mabawa yao.+ Walielekeana, na nyuso zao zilikuwa zenye kuangalia kifuniko.+
10 Kisha akatengeneza meza ya mbao za muti wa mugunga.*+ Ilikuwa na urefu wa mikono mbili, upana wa mukono mumoja, na urefu kuenda juu wa mukono mumoja na nusu.+ 11 Na akaifunika kwa zahabu safi na akatengeneza ukingo wa zahabu kuizunguka. 12 Kisha akatengeneza mupaka wenye kuinuka wenye upana wa kiganja kimoja* cha mukono kuizunguka na ukingo wa zahabu kuzunguka mupaka huo. 13 Tena, akaitengenezea pete ine (4) za zahabu na kutia pete hizo kwenye pembe ine mahali kila muguu wa miguu hiyo ine ulikuwa umeunganishwa. 14 Pete hizo zilikuwa karibu na ule mupaka wenye kuinuka, zilishikilia fito za kubebea meza hiyo. 15 Kisha akatengeneza fito za muti wa mugunga* na kuzifunika kwa zahabu ili zitumiwe kubebea meza hiyo. 16 Kisha akatengeneza kwa kutumia zahabu safi vyombo vya kutia juu ya meza—sahani zake, vikombe vyake, na mabakuli yake na mitungi yake ili vyombo hivyo vitumiwe kumwanga matoleo ya kinywaji.+
17 Kisha akatengeneza kinara cha taa+ kwa kutumia zahabu safi. Alitengeneza kinara hicho cha taa kwa kutumia nyundo.* Sehemu yake ya chini, shina lake, vikombe vyake, mafundo yake, na maua yake yalikuwa kitu kimoja.+ 18 Matawi sita (6) yalitoka kwenye shina lake na kupanda juu, matawi tatu (3) ya kinara hicho yalitoka upande wake mumoja na matawi tatu yalitoka upande wake mwingine. 19 Vikombe tatu (3) vyenye umbo ya maua ya muti wa lozi vilikuwa kwenye kila moja la matawi, pamoja na mafundo na maua yenye kufuatana, na vikombe tatu vyenye umbo ya maua ya muti wa lozi vilikuwa kwenye matawi mengine, pamoja na mafundo na maua yenye kufuatana. Ni vile ilifanywa kuhusu matawi sita (6) yenye yalitoka kwenye shina la kinara cha taa na kupanda juu. 20 Na kwenye shina la kinara cha taa kulikuwa vikombe ine (4) vyenye umbo ya maua ya muti wa lozi, pamoja na mafundo na maua yenye kufuatana. 21 Kulikuwa fundo moja chini ya matawi mbili ya kwanza yenye kutoka kwenye shina na kupanda juu na kulikuwa fundo moja chini ya matawi mbili yenye kufuata na fundo moja chini ya matawi mbili yenye kufuata, kwa ajili ya matawi sita (6) yenye kutoka kwenye shina la kinara cha taa na kupanda juu. 22 Mafundo na matawi na kinara chote cha taa vilitengenezwa ili kuwa kitu kimoja cha zahabu safi, chenye kilitengenezwa kwa kutumia nyundo.* 23 Kisha akatengeneza taa zake saba (7)+ na vifaa vyake vya kushikia tambi* na vyetezo vyake kwa kutumia zahabu safi. 24 Alitengeneza kinara hicho, pamoja na vyombo vyake vyote kwa kutumia talanta moja* ya zahabu safi.
25 Sasa akatengeneza mazabahu ya uvumba+ kwa kutumia mbao za muti wa mugunga.* Ilikuwa na pande ine (4) zenye kuwa sawasawa,* urefu wa mukono mumoja, upana wa mukono mumoja, na urefu kuenda juu wa mikono mbili. Pembe zake zilikuwa sehemu moja pamoja na mazabahu hiyo.+ 26 Aliifunika kwa zahabu safi, sehemu yake ya juu na kuizunguka pande zote na pembe zake, na alitengeneza ukingo wa zahabu kuizunguka. 27 Akaitengenezea pete mbili za zahabu chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili zenye kuelekeana ili zishikilie fito za kubebea mazabahu. 28 Kisha akatengeneza fito za muti wa mugunga* na kuzifunika kwa zahabu. 29 Alitengeneza pia mafuta matakatifu ya kutia mafuta+ na uvumba safi, wenye marashi,+ wenye kuchanganywa muzuri.*
38 Akatengeneza mazabahu ya toleo la kuteketezwa kwa kutumia mbao za muti wa mugunga.* Ilikuwa na pande ine (4) zenye kuwa sawasawa,* urefu wa mikono* tano (5), upana wa mikono tano, na urefu kuenda juu wa mikono tatu (3).+ 2 Kisha akatengeneza pembe zake kwenye kona zake ine (4). Pembe hizo zilikuwa sehemu moja pamoja na mazabahu hiyo. Na akaifunika kwa shaba.+ 3 Kisha mambo hayo akatengeneza vyombo vya mazabahu, mbeketi, vipao,* mabakuli, kanya,* na vyetezo. Alitengeneza vyombo hivyo vyote kwa kutumia shaba. 4 Pia, alitengeneza kayungio kwa ajili ya mazabahu, chombo cha fito za shaba, chini ya ukingo wa mazabahu, kiliingia kufikia katikati ya mazabahu. 5 Alitengeneza pete ine (4) kwenye kona ine karibu na hiyo kayungio ya shaba, ili zishikilie fito. 6 Kisha akatengeneza fito za muti wa mugunga* na akazifunika kwa shaba. 7 Akaingiza fito hizo katika zile pete zenye kuwa kwenye pande za mazabahu ili zitumiwe kubebea mazabahu hiyo. Akatengeneza mazabahu hiyo kama sanduku la mbao lenye kuwa wazi.
8 Kisha akatengeneza beseni ya shaba+ na kitu cha shaba cha kuweka beseni juu yake; alitumia vioo* vya wanamuke wenye walipangwa muzuri ili kutumikia kwenye muingilio wa hema ya mukutano.
9 Kisha akatengeneza kiwanja.+ Kwa ajili ya upande wa kusini wa kiwanja hicho, kuelekea kusini, alitengeneza mapazia yenye kuninginia ya kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa, yenye urefu wa mikono mia moja (100).+ 10 Kulikuwa nguzo makumi mbili (20) na vikalio makumi mbili vya shaba, na kulabu* za nguzo hizo na vibanio* vyake vilikuwa vya feza. 11 Pia, upande wa kaskazini, kulikuwa mapazia yenye kuninginia yenye urefu wa mikono mia moja (100). Nguzo zake makumi mbili (20) na vikalio vyake makumi mbili vilikuwa vya shaba. Lakini kulabu* za nguzo hizo na vibanio* vyake vilikuwa vya feza. 12 Lakini kuhusu upande wa mangaribi, mapazia yenye kuninginia yalikuwa na urefu wa mikono makumi tano (50). Kulikuwa nguzo kumi (10) na vikalio kumi, na kulabu* za nguzo na vibanio* vyake vilikuwa vya feza. 13 Upana wa upande wa mashariki, kuelekea mahali jua linatokea, ulikuwa mikono makumi tano (50). 14 Kulikuwa mapazia yenye kuninginia yenye urefu wa mikono kumi na tano (15) kwenye sehemu moja, pamoja na nguzo tatu (3) na vikalio tatu. 15 Na kwenye sehemu ingine yenye kuwa kwenye upande mwingine wa muingilio wa kiwanja, kulikuwa mapazia yenye kuninginia yenye urefu wa mikono kumi na tano (15), pamoja na nguzo tatu (3) na vikalio tatu. 16 Mapazia yote yenye kuninginia kuzunguka kiwanja hicho yalikuwa ya kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa. 17 Vikalio vya nguzo vilikuwa vya shaba, kulabu* za nguzo hizo na vibanio* vyake vilikuwa vya feza, sehemu za juu zilifunikwa kwa feza, na kulikuwa viunganishi vya feza kwa ajili ya nguzo zote za kiwanja hicho.+
18 Kitambaa cha kuficha cha* muingilio wa kiwanja kilisukwa na uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa. Kilikuwa na urefu wa mikono makumi mbili (20) na urefu kuenda juu wa mikono tano (5), sawa na urefu kuenda juu wa mapazia ya kiwanja.+ 19 Nguzo zake ine (4) na vikalio vyake ine vilikuwa vya shaba. Kulabu* zake na vibanio* vyake vilikuwa vya feza, na sehemu za juu za nguzo hizo zilifunikwa na feza. 20 Misumari yote ya hema ya tabenakulo na kuzunguka kiwanja ilikuwa ya shaba.+
21 Hii ni hesabu ya vitu vyenye vilitumiwa kutengeneza tabenakulo, tabenakulo ya Ushuhuda,+ hesabu yenye ilitayarishwa kwa amri ya Musa, na lilikuwa daraka la Walawi+ kuitayarisha chini ya uongozi wa Itamari+ mwana wa Haruni kuhani. 22 Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda alifanya mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru Musa. 23 Alikuwa pamoja na Oholiabu+ mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, mwenye alikuwa fundi na mushonaji wa michoro juu ya nguo na musukaji wa uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri.
24 Zahabu yote yenye ilitumiwa kwa ajili ya kazi yote ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa zahabu ya toleo la kutikiswa,+ talanta* makumi mbili na kenda (29) na shekeli* mia saba makumi tatu (730) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.* 25 Na feza ya watu wa mukusanyiko wenye waliandikishwa ilikuwa talanta mia moja (100) na shekeli elfu moja mia saba makumi saba na tano (1 775) kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.* 26 Nusu shekeli yenye ilitolewa na kila mutu ilikuwa nusu shekeli kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu,* ilitolewa na kila mwanaume mwenye alikuwa kati ya wale wenye waliandikishwa kuanzia miaka makumi mbili (20) na zaidi,+ wote walikuwa elfu mia sita na tatu na mia tano makumi tano (603 550).+
27 Kazi ya kutengeneza vikalio vya mahali patakatifu na vikalio vya pazia ilifanywa kwa kutumia talanta mia moja (100); vikalio mia moja vilifanywa kwa kutumia talanta mia moja, talanta moja kwa kila kikalio.+ 28 Kwa kutumia shekeli elfu moja mia saba makumi saba na tano (1 775), alitengeneza kulabu* za nguzo na kufunika sehemu zake za juu na kuziunganisha pamoja.
29 Shaba ya toleo* ilikuwa talanta makumi saba (70) na shekeli elfu mbili mia ine (2 400). 30 Alitumia shaba hiyo ili kutengeneza vikalio vya muingilio wa hema ya mukutano, mazabahu ya shaba na kayungio yake ya shaba, vyombo vyote vya mazabahu, 31 vikalio kuzunguka kiwanja, vikalio vya muingilio wa kiwanja, na misumari yote ya hema ya tabenakulo na misumari yote ya hema+ kuzunguka kiwanja.
39 Kwa kutumia ile uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, na kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa,+ walitengeneza nguo zenye kusukwa muzuri kwa ajili ya kufanya utumishi katika patakatifu. Walimutengenezea Haruni nguo takatifu,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
2 Alitengeneza efodi+ ya zahabu, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa. 3 Walipiga-piga mabamba ya zahabu kwa kutumia nyundo* ili yakuwe mabamba membamba, na aliyakata yakakuwa nyuzi za kuchanganya na uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri, na michoro ya uzi ilishonewa juu yake. 4 Waliitengenezea vipande vya nguo vya mabega vyenye viliunganishwa kwenye miisho yake mbili. 5 Mukaba* wenye kusukwa, wenye ulifungwa kwenye efodi ili kuishikilia muzuri mahali pake,+ ulitengenezwa na vitu hivyohivyo, ulitengenezwa na zahabu, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
6 Kisha wakatia majiwe ya shohamu katika vikalio vya zahabu, na wakachonga majina ya wana wa Israeli kwenye majiwe hayo, kama vile mutu anachonga muhuri.+ 7 Akaweka majiwe hayo kwenye vipande vya nguo vya mabega vya efodi ili yakuwe majiwe ya ukumbusho kwa wana wa Israeli,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa. 8 Kisha akatengeneza kifuko cha kifua+ kwa kutumia ufundi wa mutu mwenye kushonea michoro juu ya nguo, alikitengeneza kama efodi kwa kutumia zahabu, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa.+ 9 Kifuko hicho kilikuwa na pande ine (4) zenye kuwa sawasawa* wakati kilikunjwa mara mbili. Walitengeneza kifuko cha kifua, chenye, wakati kilikunjwa mara mbili, kilikuwa na urefu na upana wa shubiri moja.* 10 Wakaweka kwenye kifuko hicho majiwe yenye kupangwa katika mistari ine (4). Mustari wa kwanza ulikuwa na zabarijadi, topazi, na zumaridi. 11 Mustari wa pili ulikuwa na feruzi, yakuti, na yaspi. 12 Mustari wa tatu (3) ulikuwa na jiwe la leshemi,* akiki, na ametisti. 13 Mustari wa ine (4) ulikuwa na krisolito, shohamu, na yashefi. Majiwe hayo yaliwekwa ndani ya vikalio vya zahabu. 14 Majiwe hayo yalilingana na majina kumi na mbili (12) ya wana wa Israeli, na kila jina lilichongwa kama vile muhuri, na kila jina liliwakilisha moja la makabila kumi na mbili.
15 Kisha wakatengeneza kwenye kifuko cha kifua minyororo yenye kusukwa-sukwa, kama kamba za zahabu safi.+ 16 Na wakatengeneza vikalio mbili vya zahabu na pete mbili za zahabu na kuzifungia kwenye pembe mbili za kifuko cha kifua. 17 Kisha wakapitisha zile kamba mbili za zahabu katika pete mbili zenye zilikuwa kwenye pembe za kifuko cha kifua. 18 Kisha wakapitisha miisho mbili ya zile kamba mbili katika vile vikalio mbili na wakaifungia kwenye vile vipande vya nguo vya mabega kwenye sehemu ya mbele ya efodi. 19 Kisha wakatengeneza pete mbili za zahabu na kuzitia kwenye miisho mbili juu ya ukingo wa ndani wa kifuko cha kifua, kuelekeana na efodi.+ 20 Kisha wakatengeneza pete zingine mbili za zahabu na wakazitia upande wa mbele wa efodi, chini ya vipande mbili vya nguo vya mabega, karibu na mahali kwenye inaunganishwa, juu ya mukaba* wenye kusukwa wa efodi. 21 Mwishowe, wakafunga kifuko cha kifua na kamba ya rangi ya bluu kuanzia pete zake mupaka kwenye pete za efodi, ili kifuko cha kifua kibakie mahali pake kwenye efodi, juu ya mukaba* wenye kusukwa, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
22 Kisha akatengeneza koti ya efodi yenye haina mikono, ilisukwa na musukaji wa nguo, yote ilisukwa na uzi ya rangi ya bluu.+ 23 Nafasi yenye kuwa wazi ya koti yenye haina mikono ilikuwa katikati ya koti hiyo, kama vile nafasi yenye kuwa wazi ya koti ya chuma. Nafasi yake yenye kuwa wazi ilikuwa na ukingo kuizunguka, ili isipasuke. 24 Kisha wakatengeneza kwenye upindo wa ile koti yenye haina mikono makomamanga ya uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, na kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa; vyote vilisukwa-sukwa pamoja. 25 Na walitengeneza kengele za zahabu safi na kuzitia katikati ya makomamanga pande zote kuzunguka upindo wa ile koti yenye haina mikono, katikati ya makomamanga; 26 walitia kengele kisha komamanga moja, kengele kisha komamanga moja, pande zote kuzunguka upindo wa chini wa koti yenye haina mikono, yenye ilitumiwa ili kufanya utumishi, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
27 Na walitengeneza kanzu za kitani kizuri, zilisukwa na fundi wa chombo cha kusukia nguo, kwa ajili ya Haruni na wana wake,+ 28 na kilemba+ cha kitani kizuri, kitu cha kupamba cha kuvaa kwenye kichwa cha kitani kizuri,+ kapitula*+ za kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa, 29 na kitambaa cha kujifunga kiuno chenye kutengenezwa na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, na kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
30 Mwishowe, walitengeneza bamba lenye kungaa, ile alama takatifu ya kuwekwa pembeni kwa ajili ya kusudi la pekee,* kwa kutumia zahabu safi na kuchora juu yake kama vile mutu anachora kwenye muhuri: “Utakatifu ni wa Yehova.”+ 31 Wakafunga kwenye bamba hilo kamba yenye ilitengenezwa na uzi ya rangi ya bluu ili kulitia kwenye kilemba, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
32 Kwa hiyo kazi yote ya tabenakulo, lile hema ya mukutano, ikamalizika, na Waisraeli walifanya kila jambo lenye Yehova alikuwa amemuamuru Musa.+ Ni vile walifanya kabisa.
33 Kisha wakamuletea Musa tabenakulo,+ ile hema+ pamoja na vifaa vyake vyote: vifungo vyake,+ kadre zake za mbao,+ fito zake+ na nguzo zake, na vikalio vyake;+ 34 kifuniko chake cha ngozi za kondoo-dume zenye zilitiwa rangi nyekundu,+ kifuniko chake cha ngozi za sili,* na pazia kwa ajili ya kitambaa cha kuficha;+ 35 sanduku la Ushuhuda pamoja na fito zake+ na kifuniko chake;+ 36 meza, vyombo vyake vyote+ na mikate ya wonyesho; 37 kinara cha taa cha zahabu safi, taa zake,+ musururu wa taa, na vyombo vyake vyote+ na mafuta ya kuangazia;+ 38 mazabahu+ ya zahabu, mafuta ya kutia mafuta,+ uvumba wenye marashi,+ kitambaa cha kuficha*+ kwa ajili ya muingilio wa hema; 39 mazabahu ya shaba+ na kayungio yake ya shaba, fito zake,+ vyombo vyake vyote,+ beseni na kitu cha kuweka beseni juu yake;+ 40 mapazia yenye kuninginia ya kiwanja, nguzo zake na vikalio vyake,+ kitambaa cha kuficha*+ kwa ajili ya muingilio wa kiwanja, kamba za hema na misumari ya hema+ na vyombo vyote kwa ajili ya utumishi wa tabenakulo, kwa ajili ya hema ya mukutano; 41 nguo zenye kusukwa muzuri kwa ajili ya kufanya utumishi katika patakatifu, nguo takatifu kwa ajili ya Haruni kuhani,+ na nguo za wana wake ili kutumikia wakiwa makuhani.
42 Waisraeli walifanya kazi hiyo yote kulingana na mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru Musa.+ 43 Wakati Musa alichunguza kazi yao yote, aliona kwamba walikuwa wameifanya kama vile Yehova alikuwa ameamuru; na Musa akawabariki.
40 Kisha Yehova akamuambia Musa: 2 “Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, utasimamisha tabenakulo, ile hema ya mukutano.+ 3 Weka sanduku la Ushuhuda ndani yake,+ na kuficha sanduku hilo kwa pazia.+ 4 Utaingiza ndani meza+ na kupanga vyombo vyake juu yake na utaingiza ndani kinara cha taa+ na kuwasha taa zake.+ 5 Kisha utatia mazabahu ya zahabu kwa ajili ya uvumba+ mbele ya sanduku la Ushuhuda na utatia kitambaa cha kuficha* kwa ajili ya muingilio wa tabenakulo mahali pake.+
6 “Utatia mazabahu ya toleo la kuteketezwa+ mbele ya muingilio wa tabenakulo, ile hema ya mukutano, 7 na utatia beseni katikati ya hema ya mukutano na mazabahu na kutia maji ndani ya beseni hiyo.+ 8 Kisha utafanya kiwanja+ kuzunguka hema hiyo na utatia kitambaa cha kuficha*+ kwa ajili ya muingilio wa kiwanja. 9 Halafu utakamata mafuta ya kutia mafuta+ na kutia tabenakulo mafuta na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake,+ na utaitakasa pamoja na vyombo vyake vyote, na itakuwa kitu kitakatifu. 10 Utatia mafuta mazabahu ya toleo la kuteketezwa pamoja na vyombo vyake vyote na kutakasa mazabahu hiyo, na itakuwa mazabahu takatifu sana.+ 11 Na utatia mafuta beseni na kitu cha kuweka beseni juu yake na kuitakasa.
12 “Kisha utamuleta Haruni na wana wake karibu na muingilio wa hema ya mukutano, na kuwanawisha na maji.+ 13 Na utamuvalisha Haruni zile nguo takatifu+ na kumutia mafuta+ na kumutakasa, na atanitumikia akiwa kuhani. 14 Kisha utaleta wana wake karibu, na kuwavalisha kanzu.+ 15 Utawatia mafuta kama vile ulimutia mafuta baba yao,+ ili wanitumikie wakiwa makuhani, na kwa sababu wametiwa mafuta, ukuhani utaendelea kuwa wao sikuzote katika vizazi vyao vyote.”+
16 Musa alifanya kulingana na mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuamuru.+ Ni vile alifanya kabisa.
17 Katika mwezi wa kwanza, mwaka wa pili, siku ya kwanza ya mwezi, tabenakulo ilisimamishwa.+ 18 Wakati Musa alisimamisha tabenakulo, aliweka chini vikalio vyake,+ alisimamisha kadre zake za mbao,+ aliweka fito zake,+ na kusimamisha nguzo zake. 19 Akatandika ile hema+ juu ya tabenakulo na akaweka kifuniko+ cha hema juu yake, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
20 Kisha akakamata Ushuhuda+ na akautia ndani ya Sanduku+ na akatia fito+ kwenye Sanduku na kuweka kifuniko+ juu ya Sanduku hilo.+ 21 Akaingiza Sanduku ndani ya tabenakulo na akatia pazia+ la kitambaa cha kuficha mahali pake na kuficha sanduku la Ushuhuda,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
22 Kisha akatia meza+ ndani ya hema ya mukutano upande wa kaskazini wa tabenakulo inje ya pazia, 23 na akapanga juu yake ule mustari wa mikate+ mbele ya Yehova, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
24 Akatia kile kinara cha taa+ ndani ya hema ya mukutano mbele ya meza hiyo, upande wa kusini wa tabenakulo. 25 Akawasha zile taa+ mbele ya Yehova, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
26 Kisha akatia ile mazabahu ya zahabu+ ndani ya hema ya mukutano mbele ya lile pazia, 27 ili kufanya uvumba wenye marashi+ utoe moshi juu yake,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
28 Kisha akatia kitambaa cha kuficha*+ kwa ajili ya muingilio wa tabenakulo mahali pake.
29 Akatia mazabahu ya toleo la kuteketezwa+ kwenye muingilio wa tabenakulo, ile hema ya mukutano, ili atoe juu yake toleo la kuteketezwa+ na toleo la nafaka, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
30 Kisha akatia beseni katikati ya hema ya mukutano na mazabahu na kutia maji ya kunawa ndani ya beseni hiyo.+ 31 Musa na Haruni na wana wake walinawa mikono yao na miguu yao pale. 32 Kila mara wakati waliingia katika hema ya mukutano ao kukaribia mazabahu, walinawa,+ kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
33 Mwishowe akafanya kiwanja+ kuzunguka tabenakulo na ile mazabahu na akaweka kitambaa cha kuficha* kwa ajili ya muingilio wa kiwanja.+
Kwa hiyo Musa akamaliza kazi yote. 34 Na wingu likaanza kufunika hema ya mukutano, na utukufu wa Yehova ukajaa katika tabenakulo.+ 35 Musa hakuweza kuingia ndani ya hema ya mukutano kwa sababu wingu liliendelea kukaa juu yake, na utukufu wa Yehova ulijaa katika tabenakulo.+
36 Na wakati wingu liliinuka kutoka juu ya tabenakulo, Waisraeli walikuwa wanavunja kambi katika hatua zote za safari yao.+ 37 Lakini, wakati wingu lilikosa kuinuka, hawakuvunja kambi mupaka siku liliinuka.+ 38 Kwa maana wingu la Yehova lilikuwa juu ya tabenakulo wakati wa muchana, na moto uliendelea kukaa juu ya tabenakulo wakati wa usiku mbele ya macho ya nyumba yote ya Israeli katika hatua zote za safari yao.+
Ao “nafsi zote zenye zilizaliwa.”
Tnn., “zenye zilitoka katika paja la Yakobo.”
Ao “nafsi.”
Tnn., “wana wa Israeli.”
Ao “wakaweka wasimamizi wa kazi.”
Ao “mortier.”
Ao “safina ya; sanduku ya.”
Ao “papyrus.” Angalia Maana ya Maneno.
Bereu ni kabulimbo nzito.
Maana yake “Mwenye Alitoshwa,” ni kusema, mwenye aliokolewa kutoka kwenye maji.
Ao “kadiri Musa aliendelea kuwa na nguvu.”
Ao “kutetea.”
Ni kusema, Yetro.
Ao “eko.”
Maana yake “Mukaaji Mugeni Kule.”
Ao “mutamuabudu.”
Ao “Ninataka.”
Ao “Nitakuwa Kile Nitakuwa.” Angalia Nyongeza A4.
Ao “neige.”
Tnn., “kinywa changu ni kizito.”
Tnn., “nitakuwa pamoja na kinywa chako.”
Ao “utakuwa mwakilishi wa Mungu kwake.”
Ao “wanatafuta nafsi yako.”
Ao “kisu cha jiwe ngumu.”
Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.
Ao “mizigo yenu.”
Ao “ni wavivu.”
Ao “Muko wavivu.”
Ao “muko wavivu.”
Ao “mumefanya tunuke mubaya mbele ya Farao na watumishi wake.”
Ao “wenye nguvu.”
Tnn., “niliinua mukono wangu.”
Tnn., “sijatahiriwa midomo?”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Tnn., “sijatahiriwa midomo.”
Tnn., “nimekufanya Mungu.”
Tnn., “majeshi yangu.”
Ni kusema, mifereji ya Muto Nile.
Ao “mabakuli yenu.”
Aina ya mainzi wenye kuuma watu na wanyama.
Ni kusema, Wamisri.
Ao “kufanya muchezo.”
Ao “umefutwa.”
Pengine ni umeme wa radi wenye nguvu.
Ao “kipindi chake kilikuwa kimechelewa kufika.”
Tnn., “kuwa mutego kwetu.”
Ao “eko.”
Pengine ni Musa.
Ao “utatusaidia tupate.”
Tnn., “kwato yoyote yenye itabakia.” Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.
Tnn., “atanoa ulimi wake juu ya.”
Ao “yeye na jirani yake.”
Ao “nafsi.”
Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”
Ao “mishipi.”
Tnn., “mutakuwa mumefunga viuno vyenu.”
Ao “nafsi hiyo inapaswa.”
Ao “kuuawa kutoka.”
Ao “nafsi.”
Ao “eko.”
Tnn., “majeshi.”
Ao “nafsi hiyo inapaswa.”
Ao “kuuawa kutoka.”
Ni kusema, wana-kondoo ao wana-mbuzi.
Tnn., “uharibifu.”
Tnn., “nyumba ya tangi.”
Ao “mabakuli yao.”
Ni kusema, kikundi kikubwa cha watu wenye kuchangamana, wenye hawakukuwa Waisraeli, kutia ndani Wamisri.
Tnn., “majeshi yote.”
Ao “eko.”
Tnn., “majeshi.”
Ao “Niwekee pembeni.”
Tnn., “kila muzaliwa wa kwanza mwenye kufungua tumbo la uzazi.”
Angalia Nyongeza B15.
Tnn., “mipaka.”
Ao “kikumbusho.”
Tnn., “katikati ya macho yako.”
Tnn., “kila mwenye kufungua tumbo la uzazi.”
Tnn., “kila kitu chenye kufungua tumbo la uzazi.”
Tnn., “katikati ya macho yako.”
Tnn., “wakiwa na mukono wenye kuinuliwa.”
Ni kusema, karibu saa 8 ya usiku (2:00) mupaka saa 12 ya asubui (6:00).
Ao “mipeto; pneus.”
Tnn., “mukono.”
“Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “nafsi yangu itosheke.”
Tnn., “maumivu ya kuzaa.”
Shehe alikuwa mukubwa wa kabila.
Ao “viongozi wenye kutawala kwa nguvu.”
Ao “tari.”
Ao “matari.”
Maana yake “Uchungu.”
Tnn., “Katikati ya zile mangaribi mbili.”
Karibu litre 2.2 (vibaba 2). Angalia Nyongeza B14.
Ao “eko.”
Ao “sabato.”
Ao “mivunyu haikukuwa.”
Ao “eko.”
Ao “wakapumuzika.”
Pengine inatokana na neno la Kiebrania lenye kumaanisha “Hii ni nini?”
Ao “bapa.”
Efa moja ilikuwa sawa na litre 22 (vibaba 20). Angalia Nyongeza B14.
Maana yake “Kujaribu; Jaribu.”
Maana yake “Ugomvi.”
Ao “eko.”
Maana yake “Yehova Ni Nguzo Yangu ya Alama.”
Maana yake “Mukaaji Mugeni Kule.”
Maana yake “Mungu Wangu Ni Musaidizi.”
Tnn., “katika mukono wa Misri.”
Tnn., “kila wakati.”
Ao “mali yangu yenye ninapendezwa nayo sana.”
Pengine angetobolewa kwa mushale.
Tnn., “Musimukaribie mwanamuke.”
Tnn., “asiwalipukie.”
Ao “tofauti na mimi.” Tnn., “zidi ya uso wangu.”
Ao “mufano.”
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Ao “matoleo yako ya amani.”
Ao “majiwe yenye kuchongwa.”
Tnn., “uchi wako.”
Ao “eko.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “akombolewe.”
Ao pengine, “kifaa.”
Tnn., “na watoto wake watoke.”
Ao “haumizwe sana.”
Ao “faini.”
Ao “nafsi kwa nafsi.”
Ao “kulipia hasara ya kitu chenye kiliharibiwa.”
Ao “nafsi yake.”
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “yatima.”
Ao “mutu yeyote mwenye kuteseka.”
Ao “eko.”
Tnn., “ngozi yake.”
Ao “neema.”
Ao “kumutukana.”
Ao “mutawala.”
Ni kusema, vikamulio vya mafuta na vikamulio vya divai.
Ni kusema, ushahidi wenye kupendwa na watu wengi.
Tnn., “neno la.”
Ao “sitamutangaza kuwa hana kosa.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “eko.”
Ao “munajua maisha (nafsi) ya mukaaji mugeni.”
Tnn., “kinywa chenu.”
Angalia Nyongeza B15.
Inaitwa pia Sikukuu ya Majuma, ao Pentekoste.
Inaitwa pia Sikukuu ya Vibanda (Tabenakulo).
Ao “nitafanya siku zako zikuwe nyingi.”
Ao pengine, “wasiwasi; woga mukubwa.”
Ni kusema, Efrati.
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “pavement.”
Ao “manyoya ya kondoo yenye kutiwa rangi ya zambarau.”
Ao “kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa ya kidudu chenye kuitwa kochinili.”
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “mushita.”
Ao “mushita.”
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Ao “mushita.”
Ao “hama, marteau.”
Ao “mushita.”
Karibu santimetre 7.4 (inchi 2.9). Angalia Nyongeza B14.
Ao “mushita.”
Ao “hama, marteau.”
Ao “hama, marteau.”
Ao “koleo zake.”
Talanta moja ilikuwa sawa na kilograme 34.2 (aunsi troi 1.101). Angalia Nyongeza B14.
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “mushita.”
Ao “mihimili.”
Ao “mihimili.”
Ao “mushita.”
Ao “mushita.”
Ao “Crochets.”
Ao “pazia.”
Ao “mushita.”
Ao “pazia.”
Ao “Crochets.”
Ao “mushita.”
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Ao “muraba; carré.”
Ao “majivu yenye mafuta,” ni kusema, majivu yenye kujaa mafuta ya zabihu.
Ao “sepetu; bêches.”
Ao “nyuma.”
Ao “mushita.”
Ao “Crochets.”
Ao “pete” za kushika pamoja.
Ao “crochets.”
Ao “pete” za kushika pamoja.
Ao “pazia.”
Ao “crochets.”
Tnn., “wenye kuwa na moyo wa hekima.”
Ao “Mushipi.”
Ao “muraba; carré.”
Karibu santimetre 22 (inchi 8.75). Angalia Nyongeza B14.
Jiwe la samani lenye halijulikane muzuri kabisa, pengine ni jiwe la kaharabu, hayasinti, ao opali.
Ao “mushipi.”
Ao “mushipi.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “ili kupitishia kichwa.”
Tnn., “na kujaza mikono.”
Ao “nguo za ndani.”
Tnn., “mbegu yake.”
Ao “mushipi.”
Ao “taji takatifu.”
Tnn., “utajaza mukono wa Haruni na mukono wa wana wake.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”
Tnn., “mugeni,” ni kusema, mutu mwenye haiko wa familia ya Haruni.
Tnn., “kuwajaza mukono wao.”
Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”
Efa moja ilikuwa sawa na litre 22 (vibaba 20). Angalia Nyongeza B14.
Hini moja ilikuwa sawa na litre 3.67 (painti 7.75). Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”
Ao “ya kutuliza.” Tnn., “ya kupumuzisha.”
Ao “mushita.”
Ao “muraba; carré.”
Mukono mumoja ulikuwa na urefu wa santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Ao “mushita.”
Tnn., “katikati ya zile mangaribi mbili.”
Ao “nafsi yake.”
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0. 367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “shekeli takatifu.”
Gera moja ilikuwa sawa na grame 0.57 (aunsi troi 0.01835). Angalia Nyongeza B14.
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0. 367). Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “kwa ajili ya nafsi zenu.”
Ao “nafsi zenu.”
Ao “shekeli takatifu.”
Hini moja ilikuwa sawa na litre 3.67 (painti 7.75). Angalia Nyongeza B14.
Ao “kama vile mutengenezaji wa mafuta yenye marashi anafanya.”
Tnn., “mugeni,” ni kusema, mutu mwenye haiko wa familia ya Haruni.
Ao “kuuawa kutoka.”
Ao “kama vile mutengenezaji wa mafuta yenye marashi anafanya.”
Ao “kuuawa kutoka.”
Tnn., “nimemuita kwa jina.”
Tnn., “wenye moyo wa hekima.”
Ao “nafsi hiyo inapaswa.”
Ao “kuuawa kutoka.”
Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”
Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”
Ao “ni wenye shingo ngumu.”
Tnn., “akatuliza uso wa.”
Ao “usikitike.”
Tnn., “mbegu yenu ikuwe nyingi.”
Tnn., “mbegu yenu.”
Ao “akasikitika.”
Ao “tendo lenye nguvu.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Tnn., “mbegu yako.”
Tnn., “wenye shingo ngumu.”
Tnn., “wenye shingo ngumu.”
Tnn., “walivua.”
Ao “Nimekuchagua.”
Tnn., “Uso wangu utaenda.”
Tnn., “Kama uso wako.”
Ao “mwenye neema.”
Ao “fazili nyingi zenye upendo.”
Ao “uaminifu.”
Tnn., “wenye shingo ngumu.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “Yehova, jina lake ni.”
Ao “mwenye havumilie ushindani.”
Angalia Nyongeza B15.
Tnn., “Kila kitu chenye kufungua tumbo la uzazi ni changu.”
Ao “utashika sabato.”
Inaitwa pia Sikukuu ya Vibanda (Tabenakulo).
Tnn., “Maneno Kumi.”
Tnn., “naye.”
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “mushita.”
Ao “wenye moyo wa hekima.”
Ao “pazia la.”
Ao “pazia la.”
Ao “matoleo yao ya kutikiswa.”
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “mushita.”
Ao “hekima ya moyo ili.”
Ao “mwenye moyo wa hekima.”
Inaonekana ni Bezaleli.
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “mushita.”
Ao “mihimili.”
Ao “mushita.”
Ao “mushita.”
Ao “crochets.”
Ao “pazia.”
Ao “crochets.”
Ao “pete” za kushika pamoja.
Ao “mushita.”
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Ao “mushita.”
Ao “hama, marteau.”
Ao “mushita.”
Karibu santimetre 7.4 (inchi 2.9). Angalia Nyongeza B14.
Ao “mushita.”
Ao “hama, marteau.”
Ao “hama, marteau.”
Ao “koleo zake.”
Talanta moja ilikuwa sawa na kilograme 34.2 (aunsi troi 1.101). Angalia Nyongeza B14.
Ao “mushita.”
Ao “muraba; carré.”
Ao “mushita.”
Ao “kama vile mutengenezaji wa mafuta yenye marashi anafanya.”
Ao “mushita.”
Ao “muraba; carré.”
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Ao “sepetu; bêches.”
Ao “nyuma.”
Ao “mushita.”
Ni kusema, vioo vya metali yenye kungarishwa sana.
Ao “crochets.”
Ao “pete” za kushika pamoja.
Ao “crochets.”
Ao “pete” za kushika pamoja.
Ao “crochets.”
Ao “pete” za kushika pamoja.
Ao “crochets.”
Ao “pete” za kushika pamoja.
Ao “pazia la.”
Ao “Crochets.”
Ao “pete” za kushika pamoja.
Talanta moja ilikuwa sawa na kilograme 34.2 (aunsi troi 1.101). Angalia Nyongeza B14.
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “shekeli takatifu.”
Ao “shekeli takatifu.”
Ao “shekeli takatifu.”
Ao “crochets.”
Ao “toleo la kutikiswa.”
Ao “hama, marteau.”
Ao “Mushipi.”
Ao “muraba; carré.”
Karibu santimetre 22. Angalia Nyongeza B14.
Jiwe la samani lenye halijulikane muzuri kabisa, pengine ni jiwe la kaharabu, hayasinti, ao opali.
Ao “mushipi.”
Ao “mushipi.”
Ao “nguo za ndani.”
Ao “taji takatifu.”
Sili ni munyama fulani mwenye anaishi katika maji.
Ao “pazia.”
Ao “pazia.”
Ao “pazia.”
Ao “pazia.”
Ao “pazia.”
Ao “pazia.”