HOSEA
1 Neno la Yehova lililomjia Hosea* mwana wa Beeri katika siku za Uzia,+ Yothamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda,+ na katika siku za Yeroboamu+ mwana wa Yoashi,+ mfalme wa Israeli. 2 Yehova alipoanza kusema neno lake kupitia Hosea, Yehova alimwambia hivi Hosea: “Nenda, muoe mwanamke kahaba* na uzae watoto wa ukahaba,* kwa sababu nchi imeacha kabisa kumfuata Yehova kwa sababu ya ukahaba.”*+
3 Basi akaenda na kumwoa Gomeri binti ya Diblaimu, na Gomeri akapata mimba na kumzalia mwana.
4 Kisha Yehova akamwambia Hosea: “Mpe mwana huyo jina Yezreeli,* kwa sababu baada ya muda mfupi tu nitaifanya nyumba ya Yehu+ iwajibike kwa sababu ya matendo ya umwagaji wa damu ya Yezreeli, nami nitaukomesha utawala wa wafalme wa Israeli.+ 5 Siku hiyo nitavunja upinde wa Israeli katika Bonde la* Yezreeli.”
6 Gomeri akapata mimba tena na kuzaa binti. Mungu akamwambia Hosea: “Mpe binti huyo jina Lo-ruhama,* kwa maana sitaionyesha tena rehema+ nyumba ya Israeli, kwa sababu kwa hakika nitawafukuza.+ 7 Lakini nitaionyesha rehema nyumba ya Yuda,+ nami nitawaokoa kwa nguvu za Yehova Mungu wao;+ sitawaokoa kwa upinde au kwa upanga au kwa vita au kwa farasi au kwa wapanda farasi.”+
8 Baada ya kumwachisha Lo-ruhama kunyonya, Gomeri alipata mimba na kuzaa mwana. 9 Kisha Mungu akasema: “Mpe mwana huyo jina Lo-ami,* kwa sababu ninyi si watu wangu nami sitakuwa Mungu wenu.
10 “Na Waisraeli* watakuwa wengi kama chembe za mchanga wa bahari, ambao hauwezi kupimwa wala kuhesabiwa.+ Na mahali ambapo Mungu aliwaambia, ‘Ninyi si watu wangu,’+ atawaita, ‘Wana wa Mungu aliye hai.’+ 11 Na watu wa Yuda na wa Israeli watakusanywa pamoja ili wawe na umoja+ nao watajichagulia kiongozi mmoja na kupanda kutoka nchini, kwa maana siku ya Yezreeli itakuwa kuu.+
2 “Waambieni ndugu zenu, ‘Ninyi ni watu wangu!’*+
Na dada zenu, ‘Enyi wanawake mlioonyeshwa rehema!’*+
Anapaswa kuacha ukahaba*
Na uzinzi kutoka kati ya matiti yake,
3 La sivyo nitamvua nguo abaki uchi kama alivyozaliwa,
Nitamfanya awe kama nyika,
Nitamfanya awe nchi isiyo na maji,
Na kusababisha afe kwa kiu.
5 Kwa maana mama yao amefanya ukahaba.*+
Aliyewachukua mimba ametenda kwa aibu,+ kwa kuwa alisema,
‘Nitawafuatia wapenzi wangu,+
Wanaonipa mkate wangu* na maji yangu,
Sufu yangu na kitani changu, mafuta yangu na kinywaji changu.’
6 Basi nitaziba njia yako kwa uzio wa miiba;
Nami nitajenga ukuta wa mawe ili kumzuia,
Ili asiweze kupata njia za kutokea.
Kisha atasema, ‘Nitarudi kwa mume wangu wa kwanza,+
Kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi wakati huo kuliko sasa.’+
8 Hakutambua kwamba mimi ndiye niliyempa nafaka,+ divai mpya, na mafuta,
Na mimi ndiye niliyempa fedha nyingi
Na dhahabu, waliyotumia kumtumikia Baali.+
9 ‘Kwa hiyo, nitarudi na kuchukua nafaka yangu itakapokomaa
Na divai yangu mpya katika majira yake,+
Nami nitampokonya sufu yangu na kitani changu kilichokusudiwa kufunika uchi wake.
10 Naam, nitafunua sehemu zake za siri ili wapenzi wake wazione waziwazi,
Na hakuna mtu yeyote atakayemwokoa kutoka mikononi mwangu.+
11 Nitakomesha shangwe yake yote,
Sherehe zake,+ miezi yake mipya, sabato zake, na misimu yake yote ya sherehe.
12 Nami nitaharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo amesema hivi kuihusu:
“Haya ni malipo yangu, niliyopewa na wapenzi wangu”;
Nitaifanya iwe misitu,
Na wanyama wa mwituni wataila kwa pupa.
13 Nitamfanya awajibike kwa sababu ya siku alizotumia kutoa dhabihu kwa sanamu za Baali,+
Alipokuwa akijipamba kwa pete zake na mapambo yake na kuwafuatia wapenzi wake,
Na mimi ndiye aliyenisahau,’+ asema Yehova.
15 Nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu kuanzia wakati huo na kuendelea,+
Na Bonde la* Akori+ liwe lango la tumaini;
Atanijibu huko kama alivyofanya alipokuwa kijana,
Kama siku aliyotoka katika nchi ya Misri.+
18 Siku hiyo nitafanya agano na wanyama wa mwituni kwa ajili ya watu wangu,+
Pia na ndege wa angani na viumbe wa ardhini wanaotambaa;+
Nitaondoa upinde na upanga na vita nchini,+
19 Nitakuchumbia ili uwe wangu milele;
Nitakuchumbia kwa uadilifu na kwa haki,
Kwa upendo mshikamanifu na kwa rehema.+
21 ‘Siku hiyo nitajibu,’ asema Yehova,
‘Nitazijibu mbingu,
Nazo zitaijibu dunia;+
22 Nayo dunia itajibu nafaka na divai mpya na mafuta;
23 Nitampanda kama mbegu kwa ajili yangu duniani,+
Nami nitamwonyesha rehema yule ambaye hakuonyeshwa rehema;*
Nitawaambia wale ambao si watu wangu:* “Ninyi ni watu wangu,”+
Nao watasema: “Wewe ni Mungu wetu.”’”+
3 Kisha Yehova akaniambia: “Nenda tena, mpende mwanamke anayependwa na mwanamume mwingine na ambaye anafanya uzinzi,+ mpende kama Yehova anavyowapenda Waisraeli+ ingawa wanaabudu miungu mingine+ na kupenda keki za zabibu kavu.”*
2 Basi nikamnunua ili awe wangu kwa vipande 15 vya fedha na homeri moja na nusu* ya shayiri. 3 Kisha nikamwambia: “Utaendelea kuwa wangu kwa siku nyingi. Usifanye ukahaba,* na usifanye ngono na mwanamume mwingine, nami pia sitafanya ngono nawe.”
4 Kwa maana Waisraeli watakaa kwa muda mrefu* bila mfalme,+ bila mkuu, bila dhabihu, bila nguzo, na bila efodi+ na sanamu za terafimu.*+ 5 Baadaye Waisraeli watarudi na kumtafuta Yehova Mungu wao+ na Daudi mfalme wao,+ nao watamjia Yehova wakitetemeka na kutafuta wema wake katika kipindi cha mwisho cha zile siku.+
4 Lisikieni neno la Yehova, enyi Waisraeli,
Kwa maana Yehova ana kesi dhidi ya wakaaji wa nchi,+
Kwa sababu hakuna ukweli wala upendo mshikamanifu wala ujuzi kumhusu Mungu nchini.+
2 Viapo vya uwongo na udanganyifu+ na mauaji+
Na wizi na uzinzi+ umeenea sana,
Na tendo moja la umwagaji wa damu linafuata tendo lingine la umwagaji wa damu.+
3 Ndiyo sababu nchi itaomboleza+
Na kila mkaaji nchini atadhoofika;
Wanyama wa mwituni na ndege wa angani,
Hata samaki wa baharini, wataangamia.
4 “Hata hivyo, mtu yeyote asibishane nanyi wala kuwakaripia,+
Kwa maana watu wenu ni kama wale wanaobishana na kuhani.+
5 Basi mtajikwaa kweupe kabisa wakati wa mchana,
Na nabii atajikwaa pamoja nanyi, kana kwamba ni usiku.
Nami nitamnyamazisha* mama yenu.
6 Watu wangu watanyamazishwa,* kwa sababu hawana ujuzi.
Kwa sababu mmekataa ujuzi,+
Nitawakataa pia msinitumikie mkiwa makuhani wangu;
Na kwa sababu mmesahau sheria* ya Mungu wenu,+
Mimi mwenyewe nitawasahau wana wenu.
7 Kadiri walivyoongezeka,* ndivyo walivyozidi kunitendea dhambi.+
Nitabadili utukufu wao uwe aibu.*
8 Wanajilisha dhambi ya watu wangu,
Nao wana pupa ya kuona watu wangu wakikosea.
9 Yatakayowapata watu ndiyo yatakayompata kuhani;
Nitawafanya wawajibike kwa sababu ya njia zao,
Nami nitawaletea matokeo ya matendo yao.+
10 Watakula lakini hawatashiba.+
12 Watu wangu hutafuta ushauri kutoka kwa sanamu zao za miti,
Wakifanya mambo wanayoambiwa na fimbo yao;*
Kwa sababu roho ya ukahaba* huwapotosha,
Na kwa ukahaba* wao wanakataa kujinyenyekeza kwa Mungu wao.
13 Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima,+
Na juu ya vilima wanafukiza moshi wa dhabihu,
Chini ya mialoni na milubna na kila mti mkubwa,+
Kwa sababu vivuli vyake ni vizuri.
Ndiyo sababu mabinti wenu wanafanya ukahaba*
Na mabinti wakwe zenu wanafanya uzinzi.
14 Sitawafanya mabinti wenu wawajibike kwa sababu ya ukahaba* wao,
Wala mabinti wakwe zenu kwa sababu ya uzinzi wao.
Kwa maana wanaume huwatafuta makahaba
Nao hutoa dhabihu pamoja na makahaba wa hekaluni;
Watu kama hao wasio na uelewaji+ wataangamia.
16 Waisraeli wamekuwa wakaidi kama ng’ombe mkaidi.+
Je, sasa Yehova atawachunga kama mwanakondoo dume malishoni?*
17 Waefraimu wameshikamana na sanamu.+
Waacheni!
Na watawala wao* hupenda sana aibu.+
5 “Sikieni jambo hili, enyi makuhani,+
Sikiliza kwa makini, Ee nyumba ya Israeli,
Sikiliza, Ee nyumba ya mfalme,
Kwa maana hukumu inawahusu ninyi;
Kwa sababu ninyi ni mtego kwa Mispa
Na wavu uliotandazwa juu ya Tabori.+
3 Ninawajua Waefraimu,
Na Waisraeli hawajafichika mbele zangu.
4 Shughuli zao haziwaruhusu wamrudie Mungu wao,
Kwa sababu kuna roho ya ukahaba* miongoni mwao;+
Nao hawamtambui Yehova.
5 Kiburi cha Waisraeli kimetoa ushahidi dhidi yao;*+
Waisraeli na Waefraimu wamejikwaa katika kosa lao,
Na watu wa Yuda wamejikwaa pamoja nao.+
6 Walienda kumtafuta Yehova wakiwa na kundi lao la kondoo na kundi lao la ng’ombe,
Lakini hawakuweza kumpata.
Alikuwa amejitenga mbali nao.+
Sasa mwezi mmoja utawanyafua* pamoja na mafungu* yao.
8 Pigeni pembe+ huko Gibea, tarumbeta huko Rama!+
Pigeni kelele za vita huko Beth-aveni+—tunawafuata, enyi Wabenjamini!
9 Enyi Waefraimu, mtakuwa kitu cha kutisha katika siku ya adhabu.+
Nimetangaza jambo ambalo hakika litatukia miongoni mwa makabila ya Israeli.
10 Wakuu wa Yuda ni kama wale wanaosogeza mpaka.+
Nitawamwagia ghadhabu yangu kama maji.
13 Waefraimu walipoona ugonjwa wao, na watu wa Yuda kidonda chao,
Waefraimu walienda Ashuru+ na kutuma wajumbe kwa mfalme mkuu.
Lakini hakuweza kuwaponya,
Wala hakuweza kuponya kidonda chenu.
Mimi mwenyewe nitawararua vipandevipande na kwenda zangu;+
Nitawabeba na kwenda nao, na hakuna yeyote atakayewaokoa.+
15 Nitaenda na kurudi mahali pangu mpaka watakapolipia hatia yao,
Watakapokuwa wakiteseka, watanitafuta.”+
Alitupiga, lakini atafunga majeraha yetu.
2 Atatuhuisha baada ya siku mbili.
Siku ya tatu atatuinua,
Nasi tutaishi mbele zake.
3 Tutamjua, tutajitahidi kumjua Yehova.
Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko;
Atakuja kwetu kama mvua kubwa,
Kama mvua ya masika inayolowesha dunia.”
4 “Niwafanyie nini, enyi Waefraimu?
Niwafanyie nini, enyi watu wa Yuda,
Kwa maana upendo wenu mshikamanifu ni kama ukungu wa asubuhi,
Kama umande unaotoweka haraka.
Na hukumu zangu dhidi yenu zitang’aa kama mwangaza.+
6 Kwa maana ninapendezwa na upendo mshikamanifu,* si dhabihu,
Na kumjua Mungu, badala ya dhabihu nzima za kuteketezwa.+
7 Lakini wao, kama wanadamu tu, wamevunja agano.+
Wamenisaliti katika nchi yao.
9 Magenge ya makuhani ni kama makundi ya wavamizi yanayomvizia mtu.
Wanawaua watu barabarani kule Shekemu,+
Kwa maana mwenendo wao ni wa aibu.
10 Nimeona jambo la kuchukiza sana katika nyumba ya Israeli.
11 Zaidi ya hayo, enyi watu wa Yuda, wakati wa mavuno umetengwa kwa ajili yenu,
Nitakapowakusanya watu wangu waliotekwa.”+
Kwa maana wamezoea udanganyifu;+
Wezi huvunja na kuingia ndani na makundi ya wavamizi hushambulia nje.+
2 Lakini hawasemi moyoni mwao kwamba mimi nitakumbuka uovu wao wote.+
Sasa wamezungukwa kabisa na shughuli zao;
Ziko mbele kabisa ya uso wangu.
3 Wanamfanya mfalme ashangilie kwa uovu wao,
Na wakuu kwa udanganyifu wao.
4 Wote ni wazinzi,
Wanawaka kama jiko lililowashwa moto na mwokaji,
Ambaye huacha kuchochea moto baada ya kukanda unga na kuuacha uumuke.
Amewanyooshea mkono wadhihaki.
6 Kwa maana wanakaribia kwa mioyo inayowaka kama jiko.*
Mwokaji hulala usiku kucha;
Asubuhi jiko huwaka kama miali ya moto.
8 Waefraimu huchangamana na mataifa.+
Waefraimu ni kama keki ya mviringo ambayo haijaokwa upande mmoja.
9 Wageni wamenyonya nguvu zao,+ lakini hawajui.
Na mvi zimejaa kichwani, lakini hawana habari.
10 Kiburi cha Waisraeli kimetoa ushahidi dhidi yao,+
Lakini hawajamrudia Yehova Mungu wao,+
Wala hawajamtafuta licha ya hayo yote.
11 Waefraimu ni kama njiwa mjinga, asiye na akili.*+
Wameomba msaada Misri;+ wameenda Ashuru.+
12 Popote waendapo, nitatandaza wavu wangu juu yao.
Nitawaangusha kama ndege wa angani.
Nitawatia nidhamu kulingana na onyo ambalo kusanyiko lao lilipewa.+
13 Ole wao, kwa sababu wamenikimbia!
Wataangamia, kwa maana wameniasi!
Nilikuwa tayari kuwakomboa, lakini wamesema uwongo dhidi yangu.+
Walijikatakata kwa sababu ya nafaka na divai yao mpya;
Wananigeuka.
15 Ingawa niliwatia nidhamu na kuimarisha mikono yao,
Wananipinga, wakipanga njama ya kutenda uovu.
16 Walibadili njia yao, lakini hawakufuata chochote kilichokwezwa;*
Walikuwa wasiotegemeka kama upinde uliolegea.+
Wakuu wao wataangamizwa kwa upanga kwa sababu ya ndimi zao za ukaidi.
Kwa sababu hiyo watadhihakiwa katika nchi ya Misri.”+
Adui anakuja kama tai kuivamia nyumba ya Yehova,+
2 Wananililia wakisema, ‘Mungu wetu, sisi, Waisraeli, tunakujua!’+
Adui na awafuatie.
4 Wamejichagulia wafalme, lakini bila kibali changu.
Wamejichagulia wakuu, lakini sikuwatambua.
5 Ndama wenu amekataliwa, enyi watu wa Samaria.+
Hasira yangu inawaka dhidi yao.+
Wataendelea mpaka lini kushindwa kuwa bila hatia?*
6 Kwa maana ndama huyu ametoka Israeli.
Fundi ndiye aliyemtengeneza, si Mungu;
Ndama wa Samaria atavunjwa na kubaki vipandevipande.
Hakuna bua linalozaa nafaka iliyokomaa;+
Bua lolote linalochipuka halitokezi unga.
Unga wowote wanaopata, utamezwa na wageni.+
Sasa watakuwa miongoni mwa mataifa,+
Kama chombo ambacho hakitakikani.
9 Kwa maana wamepanda kwenda Ashuru,+ kama punda mwitu aliye peke yake.
Waefraimu wamekodi wapenzi.+
10 Ingawa wanawakodi kutoka miongoni mwa mataifa,
Sasa mimi nitawazingira;
Wataanza kuteseka+ kwa sababu ya mzigo waliotwikwa na mfalme na wakuu.
11 Kwa maana Waefraimu wamezidisha madhabahu ili watende dhambi.+
Zikawa madhabahu walizotumia kutenda dhambi.+
Sasa nitakumbuka kosa lao na kuwaadhibu kwa sababu ya dhambi zao.+
14 Waisraeli wamemsahau Muumba wao+ na kujenga mahekalu,+
Na watu wa Yuda wamezidisha majiji yenye ngome.+
Lakini nitashusha moto kwenye majiji yao,
Nao utateketeza minara iliyo katika kila jiji.”+
Kwa maana kwa ukahaba* wenu mmetangatanga na kumwacha Mungu wenu.+
Mmependa malipo ya kahaba katika kila kiwanja cha kupuria nafaka.+
3 Hawataendelea kukaa katika nchi ya Yehova;+
Badala yake, Waefraimu watarudi Misri,
Nao watakula vitu visivyo safi kule Ashuru.+
Dhabihu hizo ni kama mkate wa maombolezo;
Wote wanaoula watajichafua.
Kwa maana mkate wao ni wao peke yao;*
Hautaletwa katika nyumba ya Yehova.
6 Kwa maana tazama! watalazimika kukimbia kwa sababu ya maangamizi.+
Misri itawakusanya pamoja,+ na Memfisi itawazika.+
Upupu utamiliki vitu vyao vya fedha vyenye thamani,
Na vichaka vya miiba vitakuwa katika mahema yao.
Nabii wao atakuwa mjinga, na mtu anayeongozwa na roho atashikwa na wazimu;
Kwa sababu makosa yenu ni mengi, uhasama dhidi yenu ni mkubwa.”
8 Mlinzi+ wa Efraimu alikuwa na Mungu wangu.+
Lakini sasa njia zote za manabii wake+ ni kama mitego ya mwindaji wa ndege;
Kuna uhasama katika nyumba ya Mungu wake.
9 Wamezama ndani sana katika maangamizi, kama ilivyokuwa kule Gibea.+
Atakumbuka kosa lao na kuwaadhibu kwa sababu ya dhambi zao.+
10 “Niliwapata Waisraeli kama zabibu nyikani.+
Kama matunda ya kwanza ya tini niliwaona mababu zenu.
Lakini walienda kwa Baali wa Peori;+
Walijiweka wakfu kwa kile kitu cha aibu,*+
Wakawa chukizo kama kitu walichokipenda.
11 Utukufu wa Waefraimu unaruka mbali kama ndege;
Hakuna kuzaa, hakuna mimba, na hakuna kushika mimba.+
13 Waefraimu, waliopandwa malishoni, walikuwa kama Tiro kwangu;+
Sasa lazima Waefraimu wawalete wana wao ili wachinjwe.”
15 “Walifanya uovu wao wote kule Gilgali,+ kwa maana nilianza kuwachukia huko.
Nitawafukuza katika nyumba yangu kwa sababu ya matendo yao maovu.+
Sitawapenda tena;+
Wakuu wao wote ni wakaidi.
16 Waefraimu wataangushwa chini.+
Mzizi wao utakauka, nao hawatazaa tunda lolote.
Hata wakizaa, nitawaua wazao wao wanaowapenda.”
10 “Waisraeli ni mzabibu ulioharibika* unaozaa matunda.+
Kadiri matunda yao yanavyoongezeka, ndivyo wanavyozidisha madhabahu zao;+
Kadiri nchi yao inavyozaa vizuri, ndivyo fahari ya nguzo zao takatifu inavyozidi kuongezeka.+
Kuna yule atakayebomoa madhabahu zao na kuharibu nguzo zao.
3 Watasema, ‘Hatuna mfalme,+ kwa sababu hatujamwogopa Yehova.
Na mfalme atatufanyia nini?’
4 Wanasema maneno matupu, wanatoa viapo vya uwongo,+ na kufanya maagano;
Basi maamuzi wanayofanya ni kama magugu yenye sumu kwenye mitaro iliyo shambani.+
5 Wakaaji wa Samaria wataogopa kwa sababu ya sanamu ya ndama ya Beth-aveni.+
Watu wake wataiombolezea,
Na pia makuhani wa mungu huyo wa kigeni waliokuwa wakiishangilia pamoja na utukufu wake,
Kwa maana itachukuliwa na kupelekwa uhamishoni.
6 Itapelekwa Ashuru kama zawadi kwa mfalme mkuu.+
Waefraimu wataaibishwa,
Na Waisraeli wataaibika kwa sababu ya ushauri waliofuata.+
7 Watu wa Samaria na mfalme wao hakika wataangamizwa,*+
Kama kijiti kilichokwanyuliwa kinachoelea juu ya maji.
8 Mahali pa juu pa Beth-aveni,+ dhambi ya Waisraeli,+ pataharibiwa kabisa.+
Miiba na michongoma itamea juu ya madhabahu zao.+
Watu wataiambia milima, ‘Tufunikeni!’
Na vilima, ‘Tuangukieni!’+
9 Enyi Waisraeli, mmetenda dhambi tangu kule Gibea.+
Nao wanaendelea kutenda dhambi huko.
Vita havikuwaangamiza kabisa wana wa ukosefu wa uadilifu kule Gibea.
10 Pia nitawatia nidhamu wakati ninaopenda.
Na mataifa yatakusanyika dhidi yao,
Makosa yao mawili yatakapofungiliwa juu yao.*
11 Waefraimu walikuwa kama ndama jike aliyezoezwa aliyependa kupura,
Basi niliihurumia shingo yake nzuri.
Sasa nitamfanya mtu fulani apande juu ya Waefraimu na kuwaendesha.*+
Watu wa Yuda watalima; watu wa Yakobo watamlimia.
12 Jipandieni mbegu kwa uadilifu na mvune upendo mshikamanifu.
Jilimieni shamba linalofaa kwa kilimo+
Maadamu wakati upo wa kumtafuta Yehova,+
Mpaka atakapokuja na kuwafundisha uadilifu.+
13 Lakini mmelima uovu,
Mmevuna ukosefu wa uadilifu,+
Nanyi mmekula matunda ya udanganyifu;
Kwa sababu mmetumaini njia yenu wenyewe,
Mmewatumaini mashujaa wenu wengi.
14 Fujo itatokea dhidi ya watu wenu,
Na majiji yenu yenye ngome yataharibiwa yote,+
Kama Shalmani alivyoharibu kabisa nyumba ya Arbeli,
Katika siku ya vita, akina mama walipondwapondwa pamoja na watoto wao.
15 Hivyo ndivyo mtakavyotendewa, enyi wakaaji wa Betheli,+ kwa sababu ya uovu wenu uliozidi.
Kwa hakika mfalme wa Israeli ataangamizwa* wakati wa mapambazuko.”+
3 Lakini mimi ndiye niliyewafundisha Waefraimu kutembea,+ nikawabeba mikononi mwangu;+
Lakini hawakutambua kwamba niliwaponya.
4 Niliendelea kuwavuta kwa kamba za wanadamu,* kwa kamba za upendo;+
Nami nilikuwa kwao kama mtu anayeinua nira kutoka kwenye mataya yao,
Na kwa upole nikamletea kila mmoja wao chakula.
6 Na upanga utavuma dhidi ya majiji yao+
Na kuharibu makomeo yao na kuwanyafua kwa sababu ya njama zao.+
7 Watu wangu wana mwelekeo wa kutokuwa waaminifu kwangu.+
Ingawa waliwaita wapande juu,* hakuna yeyote anayeinuka.
8 Enyi Waefraimu, kwa nini niwaache?+
Enyi Waisraeli, kwa nini niwatie mikononi mwa maadui wenu?
Kwa nini niwatendee kama Adma?
Kwa nini niwafanye kama Seboiimu?+
Moyo wangu umebadilika;
Na pia nimechochewa kuwahurumia.+
9 Sitamwaga hasira yangu inayowaka.
Sitawaangamiza tena Waefraimu,+
Kwa maana mimi ni Mungu, mimi si mwanadamu,
Mtakatifu aliye miongoni mwenu;
Nami sitawashambulia kwa hasira.
10 Watatembea wakimfuata Yehova, naye atanguruma kama simba;+
Atakaponguruma, wanawe watakuja wakitetemeka kutoka magharibi.+
Lakini watu wa Yuda bado wanazunguka huku na huku* pamoja na Mungu,
Nao ni waaminifu kwangu mimi, niliye Mtakatifu Zaidi.”+
12 “Waefraimu wanakula upepo.
Wanaukimbiza upepo wa mashariki siku nzima.
Wanazidisha uwongo na ukatili.
Wanafanya agano na Ashuru+ na kupeleka mafuta Misri.+
2 Yehova ana kesi dhidi ya watu wa Yuda;+
Atawafanya wazao wa Yakobo wawajibike kulingana na njia zao,
Naye atawalipa kulingana na matendo yao.+
4 Aliendelea kushindana na malaika na kumshinda.
Alilia na kumsihi apate kibali chake.”+
Alimkuta Yakobo kule Betheli, na huko akazungumza nasi,+
Dumisheni upendo mshikamanifu na haki,+
Na sikuzote mumtumaini Mungu wenu.
Na katika kazi zetu zote za jasho, hawatapata kosa au dhambi yoyote.’
9 Lakini mimi ni Yehova Mungu wenu kuanzia* mlipokuwa nchini Misri.+
Nitawafanya mkae tena katika mahema
Kama ilivyokuwa katika siku za kipindi kilichoamriwa.*
11 Kule Gileadi watu wametenda kwa udanganyifu*+ na uwongo.
Huko Gilgali wametoa dhabihu za ng’ombe dume,+
Na madhabahu zao ni kama marundo ya mawe katika mitaro iliyo shambani.+
12 Yakobo alikimbilia eneo* la Aramu;*+
Israeli+ alitumikia huko ili apate mke,+
Na ili apate mke, alichunga kondoo.+
14 Waefraimu wamemchukiza sana Mungu;+
Wataendelea kuwa na hatia ya damu;
Bwana wao atawaadhibu kwa sababu ya kumwaibisha.”+
Lakini wakawa na hatia kuhusiana na Baali,+ nao wakafa.
2 Sasa wanazidisha dhambi yao
Na kutengeneza sanamu za madini* kwa fedha yao;+
Wanatengeneza sanamu kwa ustadi, hizo zote ni kazi za mafundi.
Wanasema hivi mbele ya sanamu hizo: ‘Watu wanaotoa dhabihu na wabusu ndama hawa.’+
3 Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi,
Kama umande unaotoweka mapema,
Kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba kutoka kwenye uwanja wa kupuria,
Na kama moshi unaotoka katika bomba la moshi paani.
4 Lakini mimi ni Yehova Mungu wenu kuanzia* mlipokuwa nchini Misri;+
Hamkumjua Mungu mwingine yeyote isipokuwa mimi,
Na hakuna mwokozi mwingine yeyote ila mimi.+
5 Niliwajua mlipokuwa nyikani,+ katika nchi yenye ukame.
Na kwa hiyo wakanisahau.+
Na huko nitawanyafua kama simba;
Mnyama wa mwituni atawararua vipandevipande.
9 Atawaangamiza, enyi Waisraeli,
Kwa sababu mmenigeuka, mmemgeuka msaidizi wenu.
10 Yuko wapi sasa mfalme wenu ili awaokoe katika majiji yenu yote,+
Na watawala* wenu ambao mlisema kuwahusu,
‘Tupe mfalme na wakuu’?+
13 Watashikwa na uchungu wa kuzaa.
Lakini wao ni mtoto asiye na hekima;
Hatoki tumboni wakati wa kuzaliwa ufikapo.
Ewe Kifo, yako wapi maumivu yako makali?*+
Ewe Kaburi, yako wapi maangamizi yako?+
Macho yangu yatazuiwa yasione huruma.
15 Hata wakisitawi kati ya matete,
Upepo wa mashariki utakuja, upepo wa Yehova,
Utakuja kutoka jangwani, kukausha kisima chao na chemchemi yao.
Huyo atapora hazina ya vitu vyao vyote vyenye thamani.+
16 Watu wa Samaria watahesabiwa kuwa na hatia,+ kwa sababu wamemwasi Mungu wao.+
2 Mrudieni Yehova kwa maneno haya,
Mwambieni, ‘Tusamehe kosa letu+ na ukubali yaliyo mema,
Nasi tutatoa sifa ya midomo yetu+ kama vile ambavyo tungetoa ng’ombe dume wachanga.*
Hatutapanda farasi,+
Na hatutaziambia tena kazi za mikono yetu, “Ee Mungu wetu!”
Kwa sababu ni wewe unayemwonyesha yatima rehema.’+
4 Nitauponya ukosefu wao wa uaminifu.+
5 Nitakuwa kama umande kwa Waisraeli;
Watachanua kama yungiyungi
Nao wataipenyeza chini mizizi yao kama miti ya Lebanoni.
7 Watakaa tena chini ya kivuli chake.
Watapanda nafaka na kutokeza matumba kama mzabibu.+
Umaarufu* wao utakuwa kama wa divai ya Lebanoni.
8 Waefraimu watasema, ‘Tunahitaji tena sanamu za nini?’+
Nitawajibu na kuwalinda.+
Nitakuwa kama mberoshi unaositawi.
Mtapata matunda yenu kutoka kwangu.”
9 Ni nani aliye na hekima? Na aelewe mambo haya.
Ni nani aliye na busara? Na ayajue mambo hayo.
Kwa maana njia za Yehova zimenyooka,+
Na waadilifu watatembea katika njia hizo;
Lakini watenda dhambi watajikwaa humo.
Ufupisho wa jina Hoshaya, linalomaanisha “Aliyeokolewa na Yah; Yah Ameokoa.”
Au “malaya.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Maana yake “Mungu Atapanda Mbegu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Maana yake “Hajaonyeshwa Rehema.”
Maana yake “Si Watu Wangu.”
Yaani, wana wa Israeli.
Angalia maelezo ya chini ya Hosea 1:9.
Angalia maelezo ya chini ya Hosea 1:6.
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Au “chakula changu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Au “Baali Wangu.”
Au, “waishi.”
Maana yake “Mungu Atapanda Mbegu.”
Angalia maelezo ya chini ya Hosea 1:6.
Angalia maelezo ya chini ya Hosea 1:9.
Yaani, keki zilizotumiwa katika ibada ya uwongo.
Homeri ni kipimo sawa na lita 220. Angalia Nyongeza B14.
Au “umalaya.”
Tnn., “siku nyingi.”
Au “miungu ya familia; sanamu.”
Tnn., “nitamwangamiza.”
Tnn., “wataangamizwa.”
Au “mafundisho.”
Yaani, makuhani.
Au labda, “Wameniaibisha badala ya kunitukuza.”
Au “Watakuwa waasherati kupindukia; Watafanya umalaya.”
Au “Umalaya.”
Tnn., “Huondoa moyo.”
Au “fimbo yao ya ubashiri.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Au “umalaya.”
Tnn., “mahali penye nafasi ya kutosha.”
Au “Pombe yao ya ngano.”
Au “Wanafanya uasherati kupindukia; Wanafanya ukahaba.”
Tnn., “ngao zao.”
Au “utawafagilia mbali.”
Au “waasi.”
Au “wamejitumbukiza kabisa.”
Au “nitawatia nidhamu.”
Au “mmefanya uasherati; mmefanya umalaya.”
Au “umalaya.”
Tnn., “mbele za uso wao.”
Au labda, “Watanyafuliwa katika mwezi mmoja.”
Au “mashamba yao.”
Aina fulani ya wadudu waharibifu.
Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”
Tnn., “uso wangu.”
Au “rehema.”
Au labda, “Mioyo yao ni kama jiko wanapokaribia kwa hila.”
Tnn., “waamuzi.”
Tnn., “asiye na moyo.”
Yaani, hawakufuata ibada iliyokwezwa.
Au “kushindwa kuwa safi?”
Au “mafundisho.”
Au labda, “Watarudi.”
Au “umalaya.”
Au “ni wa nafsi yao wenyewe.”
Au “karamu yenu iliyoamriwa.”
Au “mungu wa aibu.”
Au “yaliyonyauka.”
Au labda, “unaoenea.”
Au “hila; udanganyifu.”
Tnn., “watanyamazishwa.”
Yaani, watakapobeba adhabu yao kama nira.
Au “kuwafunga nira.”
Tnn., “atanyamazishwa.”
Yaani, manabii na watu wengine waliotumwa kuwafundisha Waisraeli.
Au “kamba za fadhili,” kama zile zinazotumiwa na mzazi.
Yaani, kwenye ibada iliyokwezwa.
Tnn., “nitafanya wakae katika nyumba zao.”
Au “wanatembea.”
Au “anakumbukwa kwa jina hilo.”
Au “tangu.”
Au labda, “sherehe.”
Au “wametenda uchawi; mazingaombwe.”
Tnn., “shamba.”
Au “Siria.”
Tnn., “za kuyeyushwa.”
Au “tangu.”
Tnn., “chumba cha moyo wao.”
Tnn., “waamuzi.”
Au “limehifadhiwa.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “iko wapi michomo yako?”
Tnn., “nasi tutakutolea ng’ombe dume wachanga wa midomo yetu.”
Tnn., “Ukumbusho.”