Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bi12 Ezekieli 1:1-48:35
  • Ezekieli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ezekieli
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Ezekieli

Ezekieli

1 Basi ikawa kwamba katika mwaka wa 30, mwezi wa 4, siku ya 5 ya mwezi huo, nilipokuwa kati ya watu waliohamishwa+ kando ya mto Kebari,+ mbingu zilifunguka+ nami nikaanza kuona maono ya Mungu.+ 2 Katika siku ya tano ya mwezi huo, yaani, katika mwaka wa tano wa uhamisho wa mfalme Yehoyakini,+ 3 neno la Yehova likaja+ moja kwa moja kwa Ezekieli+ mwana wa Buzi kuhani katika nchi ya Wakaldayo+ kando ya mto Kebari, nao mkono wa Yehova ukawa juu yake mahali pale.+

4 Nami nikaanza kuona, na, tazama! kulikuwa na upepo wenye tufani+ ukija kutoka kaskazini, wingu kubwa sana+ na moto wenye kutetemeka,+ nalo lilikuwa linang’aa pande zote, na kutoka katikati yake kulikuwa na kitu kama mchanganyiko wa dhahabu na fedha, kutoka katikati ya moto.+ 5 Na kutoka katikati yake kulikuwa na mfano wa viumbe hai wanne,+ na hivi ndivyo walivyoonekana: walifanana na mtu wa udongo. 6 Na kila mmoja wao alikuwa na nyuso nne,+ na kila mmoja wao alikuwa na mabawa manne.+ 7 Na miguu yao ilikuwa miguu iliyonyooka, na wayo wa miguu yao ulikuwa kama wayo wa mguu wa ndama;+ nayo ilikuwa iking’aa kama mng’ao wa shaba iliyong’arishwa.+ 8 Na kulikuwako mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yao pande zote nne,+ na hao wanne walikuwa na nyuso zao na mabawa yao.+ 9 Mabawa yao yaliungana pamoja. Hawakugeuka walipokuwa wakienda; kila mmoja wao alikuwa akienda mbele moja kwa moja.+

10 Na mfano wa nyuso zao, hao wanne walikuwa na uso wa mwanadamu+ na uso wa simba+ upande wa kuume,+ na hao wanne walikuwa na uso wa ng’ombe-dume+ upande wa kushoto;+ hao wanne pia walikuwa na uso wa tai.+ 11 Hivyo ndivyo nyuso zao zilivyokuwa. Nayo mabawa+ yao yalikuwa yamenyooshwa nje kuelekea juu. Kila mmoja wao alikuwa na mawili yakiwa yameungana pamoja, na mawili yaliifunika miili yao.+

12 Na kila mmoja wao alikuwa akienda mbele moja kwa moja.+ Popote ambapo roho ilitaka kwenda, walienda.+ Hawakugeuka walipokuwa wakienda.+ 13 Na kuhusu mfano wa hao viumbe hai, kuonekana kwao kulikuwa kama makaa ya moto yanayowaka.+ Kitu kama kuonekana kwa mienge+ kilikuwa kikisonga mbele na nyuma katikati ya hao viumbe hai, nao moto ulikuwa mwangavu, na umeme ulikuwa ukitoka kati ya moto.+ 14 Na hao viumbe hai walionekana kama umeme katika kuondoka na kurudi kwao.+

15 Nilipoendelea kuwaona hao viumbe hai, tazama! kulikuwa na gurudumu moja duniani kando ya wale viumbe hai,+ kando ya zile nyuso nne za kila mmoja.+ 16 Na kuonekana kwa magurudumu+ hayo na muundo wake, kulikuwa kama mng’ao wa krisolito;+ nayo yote manne yalikuwa mfano mmoja. Na kuonekana kwake na muundo wake ni kama vile gurudumu linavyokuwa katikati ya gurudumu.+ 17 Yalipoenda yaliweza kwenda pande zote nne.+ Hayakugeuka upande mwingine yalipoenda.+ 18 Nayo mizingo yake, ilikuwa na kimo hivi kwamba yaliogopesha; nayo mizingo yake ilikuwa imejaa macho kuyazunguka yote manne pande zote.+ 19 Na wale viumbe hai walipoenda, yale magurudumu yalienda kando yao, na wale viumbe hai walipoinuliwa kutoka duniani, yale magurudumu yaliinuliwa.+ 20 Popote ambapo roho ilitaka kwenda, yalienda, roho ikitaka kwenda huko; nayo magurudumu yaliinuliwa juu karibu nao kando yao, kwa maana roho ya yule kiumbe hai ilikuwa katika magurudumu. 21 Walipoenda, hayo yalienda; na waliposimama tuli, nayo yalisimama tuli; na walipoinuliwa kutoka duniani, magurudumu yaliinuliwa juu karibu nao, kando yao, kwa maana roho ya yule kiumbe hai ilikuwa katika magurudumu.+

22 Na juu ya vichwa vya wale viumbe hai kulikuwa na mfano wa anga+ kama kumetameta kwa barafu yenye kutia woga, lililotanda juu ya vichwa vyao, upande wa juu.+ 23 Na chini ya anga hilo mabawa yao yalikuwa yamenyooka, moja kuelekea lingine. Kila mmoja alikuwa na mabawa mawili yakifunika upande huu na kila mmoja alikuwa na mawili yakifunika upande ule wa miili yao. 24 Nami nikasikia kishindo cha mabawa yao, kishindo kama kile cha maji mengi,+ kama kishindo cha Yule Mweza-Yote, walipoenda, kishindo cha fujo,+ kama kishindo cha kambi.+ Waliposimama tuli, walikuwa wakiyashusha chini mabawa yao.

25 Na kukawa na sauti juu ya anga lililokuwa juu ya kichwa chao. (Waliposimama tuli, walikuwa wakiyashusha chini mabawa yao.) 26 Na juu ya anga lililokuwa juu ya kichwa chao kulikuwa na kitu kinachoonekana kama jiwe la yakuti,+ mfano wa kiti cha ufalme.+ Na juu ya kile kitu chenye mfano wa kiti cha ufalme kulikuwa na mfano wa mtu anayeonekana kama mtu wa udongo juu yake,+ upande wa juu. 27 Nami nikaona kitu kama mng’ao wa mchanganyiko wa dhahabu na fedha,+ kinachoonekana kama moto kuzunguka pande zote za ndani,+ kuanzia kuonekana kwa kiuno chake kwenda juu; na kuanzia kuonekana kwa kiuno chake kwenda chini niliona kitu kinachoonekana kama moto, naye alikuwa na mwangaza kuzunguka pande zote. 28 Kulikuwa na kitu kinachoonekana kama upinde+ ambao hutokea katika wingu kubwa katika siku ya mvua. Hivyo ndivyo ulivyokuwa mwangaza uliozunguka pande zote. Kulikuwa ni kuonekana kwa mfano wa utukufu wa Yehova.+ Nilipouona, ndipo nikaanguka kifudifudi,+ nami nikaanza kusikia sauti ya mtu anayesema.

2 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu,+ simama kwa miguu yako ili niseme nawe.”+ 2 Na roho ikaanza kuingia ndani yangu mara tu aliposema nami,+ nayo mwishowe ikanifanya nisimame kwa miguu yangu ili nimsikie Yule anayesema nami.+

3 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, ninakutuma kwa wana wa Israeli,+ kwa mataifa yenye kuasi ambayo yameniasi.+ Hao wenyewe na mababu zao wamenitendea makosa mpaka siku hii ya leo.+ 4 Na wana wenye uso wa dharau+ na wenye moyo mgumu+—ninakutuma wewe kwao, nawe lazima utawaambia, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema.’ 5 Nao, ikiwa watasikia+ au watakataa+—kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi+—hakika watajua pia kwamba nabii alikuwako katikati yao.+

6 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, usiwaogope;+ wala maneno yao usiyaogope, kwa sababu kuna wakaidi+ na vitu vinavyokuwasha+ nawe unakaa katikati ya nge.+ Maneno yao usiyaogope,+ nawe usiingiwe na hofu+ kwa sababu ya nyuso zao, kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi.+ 7 Nawe utawaambia maneno yangu, bila kujali ikiwa watasikia au watakataa, kwa maana wao ni waasi.+

8 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, sikia ninalokuambia. Usiwe mwasi kama ile nyumba yenye kuasi.+ Fungua kinywa chako ule ninachokupa.”+

9 Nami nikaanza kuona, na, tazama! kulikuwa na mkono ulionyooshwa kunielekea,+ na, tazama! kitabu cha kukunjwa kilikuwa ndani yake.+ 10 Naye akakikunjua mbele yangu hatua kwa hatua, nacho kilikuwa kimeandikwa mbele na nyuma;+ nacho kilikuwa kimeandikwa nyimbo za huzuni na maombolezo na vilio.+

3 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, kula unachoona. Kula kitabu hiki cha kukunjwa,+ uende, ukaseme na nyumba ya Israeli.”

2 Kwa hiyo nikafungua kinywa changu, naye hatua kwa hatua akanilisha kile kitabu.+ 3 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, unapaswa kulisha tumbo lako, ili ujaze matumbo yako kwa kitabu hiki ninachokupa wewe.” Nami nikaanza kukila, nacho kikawa kitamu kama asali kinywani mwangu.+

4 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, nenda, uingie katikati ya nyumba+ ya Israeli, nawe lazima uwaambie maneno yangu. 5 Kwa maana hutumwi kwenda kwa watu wa lugha isiyoeleweka+ wala walio wazito wa ulimi+—kwa nyumba ya Israeli, 6 si kwa vikundi vya watu wengi sana wa lugha isiyoeleweka wala walio wazito wa ulimi, ambao maneno yao huwezi kuyasikia ukayafahamu.+ Ikiwa ningekutuma kwao, watu hao wangekusikiliza wewe.+ 7 Lakini nyumba ya Israeli, hawatataka kukusikiliza wewe, kwa maana hawataki kunisikiliza mimi;+ kwa sababu wote hao wa nyumba ya Israeli wana vichwa vigumu na mioyo migumu.+ 8 Tazama! Nimeufanya uso wako uwe mgumu+ kama nyuso zao na paji la uso wako liwe gumu kama mapaji ya nyuso zao.+ 9 Nimelifanya paji la uso wako kuwa kama almasi, gumu kuliko jiwe gumu.+ Usiwaogope,+ wala usiingiwe na hofu kwa sababu ya nyuso zao,+ kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi.”+

10 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, maneno yangu yote nitakayokuambia, yatie moyoni+ mwako na usikie kwa masikio yako mwenyewe. 11 Nawe uende, uingie katikati ya watu waliohamishwa,+ katikati ya wana wa watu wako, nawe utasema nao na kuwaambia, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema,’ bila kujali ikiwa watasikia au watakataa.”+

12 Nayo roho ikaniinua+ nami nikaanza kusikia nyuma yangu kishindo cha mvumo mkubwa:+ “Na ubarikiwe utukufu wa Yehova kutoka katika mahali pake.”+ 13 Na kulikuwa na kishindo cha mabawa ya wale viumbe hai yaliyokuwa yakigusana karibu karibu,+ na kishindo cha magurudumu karibu nao kando yao,+ na kishindo cha mvumo mkubwa. 14 Nayo roho ikaniinua+ na kunichukua, hivi kwamba nikaenda kwa uchungu katika ghadhabu ya roho yangu, na mkono wa Yehova juu yangu ulikuwa wenye nguvu.+ 15 Kwa hiyo nikaingia katikati ya watu waliohamishwa huko Tel-abibu, waliokuwa wakikaa+ kando ya mto Kebari,+ nami nikaanza kukaa mahali walipokuwa wakikaa; nami nikaendelea kukaa hapo kwa siku saba, nikiwa nimepigwa na bumbuazi katikati yao.+

16 Na ikawa kwamba mwishoni mwa siku saba neno la Yehova likanijia, na kusema:

17 “Mwana wa binadamu, nimekufanya kuwa mlinzi katika nyumba ya Israeli,+ nawe utasikia maneno kutoka katika kinywa changu nawe lazima utawapa maonyo kutoka kwangu.+ 18 Mimi ninapomwambia mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’+ na wewe usimwonye na kusema ili kumwonya mwovu aiache njia yake ya uovu ili kumhifadhi hai,+ yeye akiwa ni mwovu, katika kosa lake atakufa,+ lakini damu yake nitaidai kutoka katika mkono wako mwenyewe.+ 19 Lakini wewe, ikiwa umemwonya mwovu+ naye asigeuke na kuuacha uovu wake na njia yake ya uovu, yeye mwenyewe atakufa kwa sababu ya kosa lake;+ lakini wewe, utakuwa umeiokoa nafsi yako mwenyewe.+ 20 Na mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu+ wake naye kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki nami nilazimike kuweka kikwazo mbele yake,+ yeye mwenyewe atakufa kwa sababu hukumwonya. Kwa sababu ya dhambi yake atakufa,+ na matendo yake ya uadilifu aliyoyatenda hayatakumbukwa,+ lakini damu yake nitaidai kutoka katika mkono wako mwenyewe.+ 21 Na wewe, ikiwa umemwonya mtu mwadilifu kwamba mwadilifu huyo asitende dhambi, naye mwenyewe aepuke kutenda dhambi,+ hakika ataendelea kuishi kwa sababu alikuwa ameonywa,+ na wewe mwenyewe utakuwa umeiokoa nafsi yako mwenyewe.”+

22 Nao mkono wa Yehova ukawa juu yangu huko, naye akaniambia: “Ondoka, nenda kwenye nchi tambarare ya bondeni,+ na huko nitasema nawe.” 23 Basi nikaondoka na kwenda kwenye nchi tambarare ya bondeni, na, tazama! utukufu wa Yehova ulikuwa umesimama huko,+ kama utukufu niliouona kando ya mto Kebari,+ nami nikaanguka kifudifudi.+ 24 Ndipo roho ikaingia+ ndani yangu na kunifanya nisimame kwa miguu yangu,+ naye akaanza kusema nami na kuniambia:

“Nenda, jifungie ndani ya nyumba yako. 25 Na wewe, Ee mwana wa binadamu, tazama! hakika wataweka kamba juu yako nao watatumia kamba hizo kukufunga ili usiweze kwenda katikati yao.+ 26 Nami nitaufanya ulimi wako ushikamane na kaakaa la kinywa chako,+ nawe hakika utakuwa bubu,+ na kwao wewe hutakuwa mtu mwenye kutoa karipio,+ kwa sababu wao ni nyumba yenye kuasi.+ 27 Nami ninaposema nawe, nitakifungua kinywa chako, nawe utawaambia,+ ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema.’ Anayesikia na asikie,+ na anayekataa na akatae, kwa sababu wao ni nyumba yenye kuasi.+

4 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, jichukulie tofali, nawe utaliweka mbele yako na kuchonga jiji juu yake, yaani, Yerusalemu.+ 2 Nawe utalizingira+ na kujenga ukuta wa kulizingira+ na kuweka boma la kulizingira+ na kuweka kambi kulizunguka na kuweka mitambo ya kubomolea kulizunguka pande zote.+ 3 Na wewe, jichukulie kiokeo cha chuma, nawe utakiweka kuwa ukuta wa chuma kati yako na jiji hilo, nawe utaukaza uso wako juu yake, nalo litazingirwa, nawe utalizingira. Hiyo ni ishara kwa nyumba ya Israeli.+

4 “Na wewe, lalia upande wako wa kushoto, nawe utaweka kosa la nyumba ya Israeli juu yake.+ Kwa hesabu ya siku utakazolalia upande huo utalichukua kosa lao. 5 Na mimi mwenyewe nitakupa wewe miaka ya kosa lao+ kuwa hesabu ya siku 390,+ nawe utalichukua kosa la nyumba ya Israeli. 6 Nawe lazima utazitimiza.

“Kisha utalalia upande wako wa kuume mara ya pili, nawe utalichukua kosa la nyumba ya Yuda kwa siku 40.+ Nimekupa wewe siku moja kwa mwaka mmoja, siku moja kwa mwaka mmoja.+ 7 Nawe utaukaza uso wako kuelekea kuzingirwa kwa Yerusalemu,+ mkono wako ukiwa wazi, nawe utatoa unabii dhidi yake.

8 “Na, tazama! nitaweka kamba+ juu yako ili usijigeuze kutoka upande wako mmoja mpaka upande wako mwingine, mpaka utakapokuwa umezitimiza siku za kuzingira kwako.

9 “Na wewe, jichukulie ngano+ na shayiri na maharagwe mapana+ na dengu+ na mtama na kusemethi,+ nawe utavitia katika chombo kimoja na kuvifanya kuwa mkate kwa ajili yako, kwa hesabu ya siku unazolalia upande wako; siku 390 utaula.+ 10 Na chakula chako utakachokula kitakuwa kulingana na kipimo—shekeli 20 kwa siku.+ Mara kwa mara utakila.

11 “Na maji utayanywa kulingana na kipimo, sehemu ya sita ya hini. Mara kwa mara utakunywa.

12 “Na kama keki ya mviringo ya shayiri+ utaila; nayo, utaioka juu ya mashonde ya mavi+ ya wanadamu mbele ya macho yao.” 13 Na Yehova akaendelea kusema: “Hivyo ndivyo wana wa Israeli watakavyoula mkate wao ukiwa si safi+ katikati ya mataifa ambako nitawatawanya.”+

14 Nami nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tazama! Nafsi yangu haijatiwa unajisi;+ Sijala mnyama ambaye tayari amekufa wala mnyama aliyeraruliwa tangu ujana wangu,+ mpaka sasa, na nyama chafu haijaingia kinywani mwangu.”+

15 Basi akaniambia: “Tazama, nimekupa wewe mavi ya ng’ombe badala ya mashonde ya wanadamu, nawe utaufanya mkate wako juu yake.” 16 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, tazama, ninavunja fimbo ambazo mikate ya mviringo huning’inizwa,+ katika Yerusalemu, nao watalazimika kula mkate wao kulingana na kipimo na kwa hangaiko zito,+ nao watakunywa maji kulingana na kipimo na kwa tisho,+ 17 ili wapate kupungukiwa na mkate na maji nao watazamane kwa mshangao na kuoza kabisa katika kosa lao.+

5 “Na wewe, Ee Mwana wa binadamu, jichukulie upanga mkali. Utajichukulia ulio kama wembe wa kinyozi, nawe utaupitisha juu ya kichwa chako na juu ya ndevu zako,+ nawe utajichukulia mizani ya kupimia na kuzigawanya nywele hizo katika mafungu. 2 Sehemu ya tatu utaiteketeza katika moto katikati ya jiji mara tu zitakapotimia siku za kuzingira.+ Nawe utachukua sehemu nyingine ya tatu. Utaipiga kwa upanga kulizunguka jiji pande zote,+ nayo sehemu ya tatu ya mwisho utaitawanya kwenye upepo, nami nitauchomoa upanga nyuma yao.+

3 “Nawe utachukua hesabu ndogo katika hizo na kuzifunga katika pindo za nguo yako.+ 4 Na nyingine kati ya hizo utazichukua nawe utazitupa katikati ya moto na kuziteketeza katika moto. Kutoka kwa moto huo utatoka na kwenda katika nyumba yote ya Israeli.+

5 “Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Huyu ni Yerusalemu. Katikati ya mataifa nimemweka, kukiwa na nchi zinazomzunguka pande zote. 6 Naye alijiendesha kwa kuyaasi maamuzi yangu ya hukumu katika uovu kuliko mataifa,+ na kuziasi sheria zangu kuliko nchi zinazomzunguka pande zote, kwa maana waliyakataa maamuzi yangu ya hukumu, nao hawakutembea katika sheria zangu.’+

7 “Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Kwa sababu mlikuwa na fujo+ kuliko mataifa yanayowazunguka ninyi pande zote, hamkutembea katika sheria zangu na hamkufanya maamuzi yangu ya hukumu;+ bali mlifanya kulingana na maamuzi ya hukumu ya mataifa yanayowazunguka pande zote, sivyo?+ 8 kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Tazama niko dhidi yako, Ee jiji, naam mimi,+ nami nitayatenda katikati yako maamuzi ya hukumu machoni pa mataifa.+ 9 Nami nitafanya ndani yako jambo ambalo sijafanya na ambalo mfano wake sitafanya tena kwa sababu ya machukizo yenu yote.+

10 “ ‘ “Kwa hiyo akina baba wenyewe watakula wana katikati yako,+ na wana wenyewe watakula baba zao, nami nitatenda ndani yako matendo ya hukumu na kutawanya mabaki yako yote kuelekea kila upepo.” ’+

11 “ ‘Kwa hiyo kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘kwa hakika kwa sababu ni patakatifu pangu ulipopatia unajisi kwa machukizo+ yako yote na kwa vinyaa+ vyako vyote, mimi mwenyewe pia Ndiye nitakayekupunguza+ wewe nalo jicho langu halitakusikitikia+ na mimi mwenyewe sitakuhurumia.+ 12 Sehemu ya tatu yako—kwa tauni watakufa,+ na kwa njaa watafikia mwisho wao katikati yako.+ Na sehemu nyingine ya tatu—kwa upanga wataanguka kukuzunguka pande zote. Na sehemu ya tatu ya mwisho nitawatawanya hata kuelekea kila upepo,+ nami nitauchomoa upanga nyuma yao.+ 13 Na hasira yangu hakika itafikia mwisho+ wake nami nitaituliza ghadhabu yangu juu yao+ na kujifariji mwenyewe;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema katika kusisitiza kwangu kwamba watu wajitoe kikamili,+ nitakapomaliza ghadhabu yangu juu yao.

14 “ ‘Nami nitakufanya kuwa ukiwa na shutuma kati ya mataifa yanayokuzunguka pande zote mbele ya macho ya kila mpita-njia.+ 15 Nawe utakuwa shutuma+ na kitu cha kutukanwa,+ mfano wa kuonya+ na tisho kwa mataifa yanayokuzunguka pande zote, nitakapotenda ndani yako matendo ya hukumu katika hasira na katika ghadhabu na katika makaripio ya ghadhabu.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.

16 “ ‘Nitakapotuma ile mishale yenye madhara ya njaa juu yao,+ itakayokuwa ya uharibifu, mishale ambayo nitatuma ili kuwaharibu ninyi,+ hata njaa nitaiongeza juu yenu nami nitazivunja fimbo zenu ambazo mikate ya mviringo huning’inizwa kuzizunguka.+ 17 Nami nitatuma juu yenu njaa na wanyama-mwitu wenye kudhuru,+ nao watawaua watoto wenu, na tauni+ na damu+ zitapitia katikati yenu, nami nitauleta upanga juu yenu.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’”

6 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako kwenye milima ya Israeli na uitolee unabii.+ 3 Nawe utasema, ‘Enyi milima ya Israeli, sikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova:+ Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameiambia milima na vilima,+ vijito na mabonde: “Tazama mimi! Ninaleta upanga juu yenu, nami hakika nitaharibu mahali penu pa juu.+ 4 Na madhabahu zenu zitafanywa ukiwa+ na vinara vyenu vya uvumba vitavunjwa, nami nitawafanya waliouawa kati yenu waanguke mbele ya sanamu zenu za mavi.+ 5 Nami nitaiweka mizoga ya wana wa Israeli mbele ya sanamu zao za mavi, nami nitaitawanya mifupa yenu kuzunguka pande zote za madhabahu zenu.+ 6 Katika makao+ yenu yote majiji yataharibiwa+ na mahali pa juu patafanywa ukiwa, ili padumu katika uharibifu+ na madhabahu zenu zikae ukiwa na kuvunjwa+ nazo sanamu zenu za mavi zikomeshwe+ na vinara vyenu vya uvumba vikatwe+ na kazi zenu zifutiliwe mbali. 7 Naye aliyeuawa hakika ataanguka katikati yenu,+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+

8 “ ‘ “Na wakati hilo litakapotukia nitawaruhusu muwe na mabaki wale watakaouponyoka upanga kati ya mataifa, wakati mtakapotawanywa kati ya nchi mbalimbali.+ 9 Na walioponyoka kati yenu hakika watanikumbuka kati ya mataifa ambamo watakuwa wamechukuliwa mateka,+ kwa kuwa nimevunjika moyo kwa sababu ya moyo wao wenye kufanya uasherati ambao umegeuka na kuniacha+ na macho yao yanayozifuata sanamu zao za mavi katika uasherati;+ na nyuso zao hakika zitachukizwa na mambo mabaya ambayo wamefanya katika machukizo yao yote.+ 10 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova; sikusema+ kwa ubatili juu ya kuwatendea jambo hili lenye msiba.” ’+

11 “Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Piga makofi+ na kufanya vishindo kwa mguu wako, na kusema: “Ole wangu!” kwa sababu ya machukizo yote mabaya ya nyumba ya Israeli,+ kwa sababu wataanguka+ kwa upanga,+ kwa njaa+ na kwa tauni. 12 Yule aliye mbali,+ kwa tauni atakufa; na yule aliye karibu, kwa upanga ataanguka; naye yule aliyebaki na ambaye amelindwa, kwa njaa atakufa, nami nitaitimiza ghadhabu yangu juu yao.+ 13 Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ wakati ambapo waliouawa kati yao watakuwa katikati ya sanamu zao za mavi,+ kuzunguka pande zote za madhabahu zao,+ juu ya kila kilima kirefu,+ juu ya vilele vyote vya milima+ na chini ya kila mti wenye majani mengi+ na chini ya kila mti mkubwa wenye matawi mengi,+ mahali ambapo wametoa harufu yenye kutuliza kwa sanamu zao zote za mavi.+ 14 Nami nitaunyoosha mkono wangu juu yao+ na kuifanya nchi iwe mahame yenye ukiwa, kuwa ukiwa mbaya zaidi kuliko nyika inayoelekea Dibla, katika makao yao yote. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”

7 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Na wewe, Ee Mwana wa binadamu, hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameiambia nchi ya Israeli, ‘Mwisho, ule mwisho, umekuja juu ya miisho minne ya nchi.+ 3 Sasa mwisho uko juu yako,+ nami nitaipeleka hasira yangu juu yako, nami nitakuhukumu kulingana na njia zako+ na kuleta juu yako machukizo yako yote. 4 Na jicho langu halitakusikitikia, wala sitakuwa na huruma,+ kwa maana juu yako nitazileta njia zako mwenyewe, na katikati yako machukizo yako mwenyewe yatakuja kuwamo;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+

5 “Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Msiba, msiba wa pekee, tazama! unakuja.+ 6 Mwisho wenyewe lazima uje.+ Lazima ule mwisho uje; lazima huo uamke kwa ajili yako. Tazama! Unakuja.+ 7 Lazima shada likujie wewe, Ee mkaaji wa nchi, wakati utakuja, siku ile iko karibu.+ Kuna mvurugo, wala si kupaaza sauti kwa milima.

8 “ ‘Hivi karibuni nitaimwaga ghadhabu yangu juu yako,+ nami nitaitimiza hasira yangu juu yako,+ nami nitakuhukumu kulingana na njia zako+ na kuleta juu yako machukizo yako yote. 9 Jicho langu halitasikitika+ wala sitakuonea huruma.+ Kulingana na njia zako nitaleta juu yako, na machukizo yako mwenyewe yatakuja kuwa katikati yako;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova ninayewapiga.+

10 “ ‘Tazama! Ile siku! Tazama! Inakuja.+ Shada limetoka.+ Fimbo imechanua.+ Kimbelembele kimechipuka.+ 11 Jeuri yenyewe imesimama na kuwa fimbo ya uovu.+ Si kutoka kwao, wala kutoka kwa mali yao; na si kutoka kwao wenyewe, wala hamna ukuu wowote ndani yao. 12 Lazima wakati uje, siku ile lazima ifike. Mnunuzi na ashangilie;+ naye muuzaji asianze kuomboleza, kwa maana kuna hasira juu ya umati wake wote. 13 Kwa maana kwa kile kilichouzwa muuzaji mwenyewe hatakirudia, uhai wao ukiwa bado katikati ya walio hai; kwa maana maono ni ya umati wake wote. Hakuna atakayerudi, na kila mmoja wao hatakuwa na uhai wake mwenyewe kupitia kwa kosa lake mwenyewe.

14 “ ‘Wamepiga tarumbeta+ na kila mtu ametayarishwa, lakini hakuna anayeenda kwenye pigano, kwa sababu hasira yangu iko juu ya umati wake wote.+ 15 Upanga+ uko nje, na tauni na njaa zimo ndani.+ Yeyote aliye uwanjani, atakufa kwa upanga, na wowote walio jijini, njaa na tauni zitawameza.+ 16 Na watu wao walioponyoka hakika wataponyoka+ na kuwa kama njiwa wa mabondeni juu ya milima,+ ambao wote wanaomboleza, kila mmoja katika kosa lake mwenyewe. 17 Nayo mikono yote, inaendelea kulegea;+ nayo magoti yote yanaendelea kudondoka maji.+ 18 Nao wamejifunga nguo za magunia,+ na kutetemeka kumewafunika;+ na nyuso zote zina aibu+ na vichwa vyao vyote vina upara.+

19 “ ‘Katika barabara watatupa fedha yao wenyewe, na dhahabu yao wenyewe itakuwa chukizo. Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwakomboa katika siku ya ghadhabu ya Yehova.+ Nafsi zao hawatazishibisha, nayo matumbo yao hawatayajaza, kwa maana ni kikwazo kinachosababisha kosa lao.+ 20 Na pambo la mtu—mtu ameliweka kuwa sababu ya kiburi; na sanamu zao zenye kuchukiza,+ machukizo+ yao, wamezifanya kwa hilo. Ndiyo sababu nitalifanya hilo kuwa chukizo kwao.+ 21 Nami nitalitia mkononi mwa wageni walipore na kuwapa waovu wa dunia liwe nyara,+ nao hakika watalitia unajisi.

22 “ ‘Nami nitaugeuzia mbali uso wangu kutoka kwao,+ nao watapatia unajisi mahali pangu palipofichika, na wanyang’anyi wataingia ndani yake kwelikweli na kupatia unajisi.+

23 “ ‘Fanya mnyororo,+ kwa maana nchi yenyewe imejaa hukumu yenye madoa ya damu+ na jiji lenyewe limejaa jeuri.+ 24 Nami nitaingiza yaliyo mabaya kabisa kati ya mataifa,+ nayo hakika yatazimiliki nyumba zao,+ nami nitakikomesha kiburi cha wenye nguvu,+ na patakatifu pao patatiwa unajisi.+ 25 Kutakuwa na maumivu makali, nao hakika watatafuta amani lakini hakutakuwa na yoyote.+ 26 Shida itakuja juu ya shida,+ na kutakuwa na habari juu ya habari, na hakika watu watatafuta maono kutoka kwa nabii,+ na sheria yenyewe itaangamia kutoka kwa kuhani na shauri kutoka kwa wanaume wazee.+ 27 Mfalme mwenyewe ataomboleza;+ hata mkuu atajivika ukiwa,+ na mikono yenyewe ya watu wa nchi itasumbuka. Kulingana na njia yao nitatenda kuwaelekea wao,+ na kwa hukumu zao nitawahukumu wao;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”+

8 Na ikawa kwamba katika mwaka wa sita, katika mwezi wa sita, siku ya tano ya mwezi huo, nilikuwa nimeketi nyumbani mwangu nao wanaume wazee wa Yuda walikuwa wameketi mbele yangu,+ mkono wa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova uliponiangukia hapo.+ 2 Nami nikaanza kuona, na, tazama! mfano unaoonekana kama moto;+ kuanzia kuonekana kwa viuno vyake hata kuelekea chini kulikuwa na moto,+ na kuanzia kuonekana kwa viuno vyake hata kuelekea juu kulikuwa na kitu kama kuonekana kwa mng’ao, kama mng’ao wa mchanganyiko wa dhahabu na fedha.+ 3 Ndipo akanyoosha mfano wa mkono+ na kuniinua kwa kishungi cha nywele za kichwa changu, na roho+ ikanichukua katikati ya dunia na mbingu na kunileta Yerusalemu katika maono ya Mungu,+ kwenye mwingilio wa lango la ndani+ linaloelekea kaskazini, ambapo ni makao ya mfano wa wivu unaochochea wivu.+ 4 Na, tazama! utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa hapo,+ kama kuonekana nilikokuwa nimeona katika nchi tambarare ya bondeni.

5 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, tafadhali inua macho yako kuelekea upande wa kaskazini.” Kwa hiyo nikayainua macho yangu kuelekea upande wa kaskazini, na, tazama! kaskazini mwa lango la madhabahu kulikuwa na mfano huu wa wivu+ katika njia ya kuingilia. 6 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, je, unaona machukizo makubwa wanayofanya,+ mambo ambayo nyumba ya Israeli wananifanyia hapa ili mimi niwe mbali na patakatifu pangu?+ Na bado utaona tena machukizo makubwa.”

7 Basi akanileta kwenye mwingilio wa ua, nami nikaanza kuona, na, tazama! tundu fulani ukutani. 8 Sasa akaniambia: “Mwana wa binadamu, toboa, tafadhali, ukutani.”+ Nami nikatoboa ukutani hatua kwa hatua, na, tazama! kulikuwa na mwingilio fulani. 9 Naye akazidi kuniambia: “Ingia ndani uone machukizo mabaya wanayoyafanya hapa.”+ 10 Kwa hiyo nikaingia na kuanza kuona, na, tazama! kulikuwa na kila mfano+ wa vitu vyenye kutambaa na wanyama wenye kuchukiza,+ na sanamu zote za mavi za nyumba ya Israeli,+ michongo hiyo ikiwa juu ya ukuta kuuzunguka pande zote. 11 Na wanaume 70+ wazee wa nyumba ya Israeli, pamoja na Yaazania mwana wa Shafani+ akiwa amesimama kati yao, walikuwa wamesimama mbele ya hiyo, kila mmoja akiwa na chetezo chake mkononi mwake, na manukato ya wingu la uvumba yalikuwa yakipaa.+ 12 Naye akaniambia: “Je, umeona, Ee mwana wa binadamu, mambo ambayo wazee wa nyumba ya Israeli wanafanya katika giza,+ kila mmoja katika vyumba vya ndani vya sanamu yake ya kuchongwa? Kwa maana wanasema, ‘Yehova hatuoni.+ Yehova ameiacha nchi hii.’ ”

13 Naye akaendelea kuniambia: “Bado utaona tena machukizo makubwa wanayofanya.”+ 14 Kwa hiyo akanileta kwenye mwingilio wa lango la nyumba ya Yehova, linaloelekea kaskazini, na, tazama! wanawake walikuwa wameketi hapo, wakimlilia mungu Tamuzi.

15 Naye akazidi kuniambia: “Je, umeona hili, Ee mwana wa binadamu? Bado utaona tena machukizo+ makubwa yaliyo mabaya kuliko haya.” 16 Kwa hiyo akanileta katika ua wa ndani wa nyumba ya Yehova,+ na, tazama! kwenye mwingilio wa hekalu la Yehova, katikati ya ukumbi na madhabahu,+ kulikuwa na wanaume 25+ hivi migongo yao ikielekea hekalu la Yehova+ na nyuso zao zikielekea mashariki, nao walikuwa wameelekea mashariki, wakiliinamia jua.+

17 Naye akaendelea kuniambia: “Je, umeona hili, Ee mwana wa binadamu? Je, ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda kufanya machukizo ambayo wamefanya hapa, kwamba waijaze nchi jeuri+ na kwamba wanitie uchungu tena, na tazama, wananyoosha lile chipukizi kuelekea pua yangu? 18 Na mimi mwenyewe pia nitachukua hatua katika ghadhabu.+ Jicho langu halitasikitika, wala sitakuwa na huruma.+ Nao hakika wataita masikioni mwangu kwa sauti kubwa, lakini sitawasikia.”+

9 Naye akaita masikioni mwangu kwa sauti kubwa, na kusema: “Waleteni karibu wale wanaolikazia jiji fikira, kila mmoja wao akiwa na silaha yake mkononi mwake ili kuleta uharibifu!”

2 Na, tazama! kulikuwa na wanaume sita wakija kutoka upande wa lango la juu+ linaloelekea kaskazini, kila mmoja akiwa na silaha yake ya kuponda mkononi mwake; na kulikuwa na mwanamume mmoja kati yao aliyevaa kitani,+ akiwa na kidau cha wino kiunoni, nao wakaingia ndani na kusimama kando ya madhabahu ya shaba.+

3 Nao utukufu wa Mungu wa Israeli,+ uliondolewa juu ya makerubi+ ambao ulikuwa juu yao kwenye mlango wa nyumba hiyo,+ naye akaanza kumwita yule mwanamume aliyevaa kitani,+ ambaye alikuwa na kidau cha wino kiunoni. 4 Na Yehova akamwambia: “Pita katikati ya jiji, katikati ya Yerusalemu, nawe lazima utie alama kwenye mapaji ya uso ya watu wanaougua na kulia+ kwa sababu ya machukizo yote yanayofanywa katikati yake.”+

5 Naye akawaambia hawa wengine masikioni mwangu: “Piteni katikati ya jiji nyuma yake na kupiga. Jicho lenu lisisikitike, wala msiwe na huruma yoyote.+ 6 Mzee, kijana na bikira na mtoto mdogo na wanawake+ mtawaua kabisa—mtawaharibu. Lakini mtu yeyote ambaye ana ile alama msimkaribie,+ nanyi mnapaswa kuanzia patakatifu pangu.”+ Kwa hiyo wakaanza na wale wanaume wazee waliokuwa mbele ya nyumba.+ 7 Naye akazidi kuwaambia: “Itieni nyumba unajisi na kuzijaza nyua kwa wale waliouawa.+ Nendeni!” nao wakaenda na kupiga jijini.

8 Na ikawa kwamba, walipokuwa wakipiga nami nikiwa nimeachwa, nikaanguka kifudifudi,+ nikapaaza kilio, na kusema: “Ole+ wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Je, unawaharibu mabaki wote wa Israeli huku ukimwaga ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”+

9 Kwa hiyo akaniambia: “Kosa la nyumba ya Israeli na Yuda+ ni kubwa, kubwa sana,+ na nchi imejaa umwagaji wa damu+ nalo jiji limejaa upotovu;+ kwa maana wamesema, ‘Yehova ameiacha nchi hii,+ na Yehova haoni.’+ 10 Na mimi pia, jicho langu halitasikitika,+ wala sitaonyesha huruma.+ Hakika nitaileta njia yao juu ya kichwa chao wenyewe.”+

11 Na, tazama! yule mwanamume aliyevaa kitani, ambaye alikuwa na kidau cha wino kiunoni, akaleta neno, na kusema: “Nimefanya kama ulivyoniamuru.”+

10 Nami nikaendelea kuona, na, tazama! juu ya anga+ lililokuwa juu ya kichwa cha makerubi kulikuwa na kitu kama jiwe la yakuti,+ kilichoonekana kama mfano wa kiti cha ufalme,+ kikionekana juu yao. 2 Naye akamwambia yule mwanamume aliyevaa kitani,+ akasema: “Ingia katikati ya magurudumu yanayozunguka,+ upande wa ndani chini ya makerubi, ujaze mikono yako makaa+ ya moto kutoka katikati ya makerubi na kuyatupa juu ya jiji.”+ Kwa hiyo akaingia ndani mbele ya macho yangu.

3 Nao makerubi walikuwa wamesimama upande wa kuume wa nyumba wakati mwanamume huyo alipoingia, nalo wingu lilikuwa limeujaza ua wa ndani.+ 4 Na utukufu wa Yehova+ ukainuka juu kutoka kwa makerubi mpaka kwenye mlango wa nyumba, nayo nyumba hiyo ikajaa wingu+ hatua kwa hatua, na ua wenyewe ulikuwa umejaa wangavu wa utukufu wa Yehova. 5 Na sauti ya mabawa ya makerubi+ ikasikiwa katika ua wa nje, kama sauti ya Mungu Mweza-Yote wakati anaposema.+

6 Na ikawa kwamba, alipomwamuru yule mwanamume aliyevaa kitani, na kusema: “Chukua moto kutoka katikati ya magurudumu yanayozunguka, kutoka katikati ya makerubi,” akaingia na kusimama kando ya gurudumu. 7 Kisha kerubi yule akanyoosha mkono wake kutoka katikati ya makerubi mpaka kwenye moto+ uliokuwa katikati ya makerubi,+ akauchukua na kuutia kwenye mikono ya yule mwanamume aliyevaa kitani,+ naye akauchukua na kwenda nje. 8 Na kukaonekana katika makerubi hao mfano wa mkono wa mtu wa udongo chini ya mabawa yao.+

9 Nami nikaendelea kuona, na, tazama! kulikuwa na magurudumu manne kando ya makerubi, gurudumu moja kando ya kerubi mmoja na gurudumu moja kando ya kerubi mwingine,+ na kuonekana kwa magurudumu hayo kulikuwa kama mng’ao wa jiwe la krisolito. 10 Na kuonekana kwao, yote manne yalikuwa mfano mmoja, kama vile gurudumu linavyokuwa katikati ya gurudumu.+ 11 Yalipokuwa yakienda, yalikuwa yakienda pande zake nne. Hayakuwa yakigeuka yalipokuwa yakienda, kwa sababu mahali ambapo kichwa kingeelekea, yalienda huko. Hayakuwa yakigeuka yalipokuwa yakienda.+ 12 Na mwili wao wote na migongo yao na mikono yao na mabawa yao na magurudumu yalijaa macho kuzunguka pande zote.+ Hao wanne walikuwa na magurudumu yao. 13 Na kuhusu hayo magurudumu, yakaitwa masikioni mwangu, “Ee magurudumu yanayozunguka!”

14 Na kila mmoja wao alikuwa na nyuso nne.+ Uso wa kwanza ulikuwa uso wa kerubi, na uso wa pili ulikuwa uso wa mtu wa udongo,+ na wa tatu ulikuwa uso wa simba, na wa nne ulikuwa uso wa tai.+

15 Na makerubi hao walikuwa wakiinuka+—ni kiumbe hai kilekile nilichokuwa nimekiona kwenye mto Kebari+— 16 na makerubi hao walipoenda, magurudumu yale yalikuwa yakienda kando yao;+ na makerubi hao walipoyainua mabawa yao yawe juu ya dunia, magurudumu yale hayakuwa yakibadili mwelekeo, kutoka kando yao.+ 17 Wakati hawa waliposimama tuli, hayo yalisimama tuli; na wakati hawa walipoinuka,+ hayo yaliinuka pamoja nao, kwa maana roho ya kile kiumbe hai ilikuwa ndani yao.+

18 Nao utukufu+ wa Yehova ukatoka juu ya mlango wa nyumba na kusimama tuli juu ya makerubi.+ 19 Nao makerubi sasa wakainua mabawa yao na kuinuka kutoka duniani+ mbele ya macho yangu. Walipoenda, magurudumu yale pia yalikuwa karibu, kando yao; nao wakaanza kusimama katika mwingilio wa mashariki wa lango la nyumba ya Yehova, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao, kutoka juu.

20 Hiki ndicho kiumbe hai+ nilichokuwa nimeona chini ya Mungu wa Israeli kwenye mto Kebari,+ hivyo nikajua kwamba walikuwa makerubi. 21 Nao wale wanne, kila mmoja wao alikuwa na nyuso nne+ na kila mmoja alikuwa na mabawa manne, na mfano wa mikono ya mtu wa udongo ilikuwa chini ya mabawa yao. 22 Na mfano wa nyuso zao, zilikuwa nyuso zilezile ambazo mfano wake nilikuwa nimeuona kando ya mto Kebari.+ Kila mmoja wao alikuwa akienda mbele moja kwa moja.+

11 Na roho+ ikaniinua juu+ na kunileta kwenye lango la mashariki la nyumba ya Yehova linaloelekea mashariki,+ na, tazama! katika mwingilio wa lango kulikuwa na wanaume 25,+ nami nikamwona katikati yao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, wakuu wa watu.+ 2 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, hawa ndio wanaume wanaopanga hila ya madhara na kutoa mashauri mabaya juu ya jiji hili;+ 3 ambao wanasema, ‘Je, ujenzi wa nyumba haujakaribia?+ Yeye ni chungu cha kupikia chenye mdomo mpana,+ na sisi ni nyama.’

4 “Kwa hiyo toa unabii juu yao. Toa unabii, Ee mwana wa binadamu.”+

5 Ndipo roho ya Yehova ikaniangukia,+ naye akaendelea kuniambia: “Sema, ‘Hivi ndivyo Yehova amesema:+ “Ninyi mlisema jambo lililo sawa, Ee nyumba ya Israeli; na kuhusu mambo yanayokuja katika roho yenu, mimi mwenyewe nimeyajua.+ 6 Mmewafanya waliouawa kati yenu katika jiji hili kuwa wengi, nanyi mmezijaza barabara zake kwa watu waliouawa.” ’ ”+ 7 “Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Kuhusu wale waliouawa ambao ninyi mmewaweka katikati yake, wao ni nyama,+ na yeye ndiye chungu cha kupikia chenye mdomo mpana;+ na ninyi wenyewe mtatolewa katikati yake.’ ”+

8 “ ‘Ninyi mmeuogopa upanga,+ nami nitauleta upanga juu yenu,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ 9 ‘Nami hakika nitawatoa ninyi katikati yake na kuwatia mkononi mwa wageni+ na kutekeleza juu yenu matendo ya hukumu.+ 10 Kwa upanga mtaanguka.+ Katika mpaka wa Israeli+ nitawahukumu ninyi; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 11 Yeye mwenyewe hatakuwa kwenu chungu cha kupikia chenye mdomo mpana,+ nanyi wenyewe hamtakuwa nyama katikati yake. Katika mpaka wa Israeli nitawahukumu ninyi, 12 nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, kwa sababu hamkutembea katika masharti yangu na hamkuzitenda hukumu zangu,+ bali mmetenda kulingana na hukumu za mataifa yanayowazunguka.’ ”+

13 Na ikawa kwamba mara tu nilipotoa unabii Pelatia mwana wa Benaya mwenyewe akafa,+ nami nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kubwa+ na kusema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova!+ Je, utaangamiza mabaki ya Israeli?”+

14 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 15 “Mwana wa binadamu, kuhusu ndugu zako,+ ndugu zako, wanaume wanaohangaikia haki yako ya kukomboa, na nyumba yote ya Israeli, yote kabisa, ndio ambao wakaaji wa Yerusalemu wamewaambia, ‘Nendeni mbali kutoka kwa Yehova. Ni yetu; tumepewa nchi tuimiliki’;+ 16 kwa hiyo sema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Ijapokuwa nimewaweka mbali kabisa katikati ya mataifa, na ijapokuwa nimewatawanya katikati ya nchi+ hizo, hata hivyo nitakuwa patakatifu kwao kwa kitambo kidogo katikati ya nchi ambazo wameenda.” ’+

17 “Kwa hiyo sema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Pia nitawakusanya ninyi kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya ninyi kutoka katika nchi ambazo katikati yake mmetawanywa, nami nitawapa ninyi udongo wa Israeli.+ 18 Nao hakika watakuja huko na kuondoa machukizo yake yote na vinyaa vyake vyote kutoka ndani yake.+ 19 Nami nitawapa moyo mmoja,+ nami nitaweka roho mpya ndani yao;+ nami hakika nitauondoa ule moyo wa jiwe kutoka katika mwili+ wao na kuwapa moyo wa nyama,+ 20 ili watembee katika sheria zangu na kushika maamuzi yangu ya hukumu na kuyatenda;+ na ili wawe watu wangu kwelikweli+ na ili mimi mwenyewe niwe Mungu wao.” ’+

21 “ ‘ “Lakini kwa wale ambao moyo wao unatembea katika machukizo yao na vinyaa vyao,+ hakika nitaleta njia yao wenyewe juu ya vichwa vyao,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’ ”+

22 Na sasa wale makerubi+ wakayainua mabawa yao, na yale magurudumu yalikuwa karibu nao,+ nao utukufu+ wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao, kutoka juu.+ 23 Nao utukufu wa Yehova+ ukapaa kutoka juu katikati ya jiji na kuanza kusimama juu ya mlima+ ulio upande wa mashariki wa jiji hilo.+ 24 Na roho+ ikaniinua+ na mwishowe ikanileta Ukaldayo kwa watu waliohamishwa,+ katika maono kwa roho ya Mungu; na yale maono niliyokuwa nimeyaona yakapaa kutoka juu yangu. 25 Nami nikaanza kuwaambia watu waliohamishwa mambo yote ya Yehova ambayo alikuwa amenifanya niyaone.+

12 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, unakaa katikati ya nyumba yenye kuasi,+ ambao wana macho ya kuona lakini kwa kweli hawaoni,+ ambao wana masikio ya kusikia lakini kwa kweli hawasikii,+ kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi.+ 3 Na wewe, Ee mwana wa binadamu, jifanyie mizigo kwa ajili ya uhamisho nawe uende uhamishoni wakati wa mchana mbele ya macho yao, nawe utaenda uhamishoni kutoka mahali pako mpaka mahali pengine mbele ya macho yao. Labda wataona, ingawa wao ni nyumba yenye kuasi.+ 4 Nawe utatoa nje mizigo yako kama mizigo ya uhamisho wakati wa mchana mbele ya macho yao, na wewe mwenyewe utatoka nje wakati wa jioni mbele ya macho yao kama wale wanaotolewa ili kupelekwa uhamishoni.+

5 “Mbele ya macho yao, toboa njia yako ukutani, nawe utaitolea hapo.+ 6 Mbele ya macho yao utaibeba begani. Wakati wa giza utaitoa nje. Utaufunika uso wako usiione dunia, kwa sababu nimekufanya kuwa ishara+ kwa nyumba ya Israeli.”+

7 Nami nikafanya vile nilivyokuwa nimeamriwa.+ Mizigo yangu nikaitoa nje, kama vile mizigo ya kwenda uhamishoni, wakati wa mchana; na jioni nikatoboa njia yangu ukutani kwa mkono. Wakati wa giza nikaitoa nje. Nikaibeba juu ya bega langu, mbele ya macho yao.

8 Na neno la Yehova likaendelea kunijia asubuhi, na kusema: 9 “Mwana wa binadamu, je, wale wa nyumba ya Israeli, nyumba yenye kuasi,+ hawakukuambia, ‘Unafanya nini?’ 10 Waambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Kuhusu mkuu,+ kuna tangazo hili juu ya Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli walio katikati yao.” ’

11 “Sema, ‘Mimi ni ishara+ kwenu. Kama vile nilivyotenda, ndivyo watakavyotendewa. Wataenda uhamishoni, utekwani.+ 12 Na kuhusu mkuu aliye katikati yao, atabeba begani wakati wa giza na kutoka nje; watautoboa ukuta ili kuitolea hapo.+ Uso wake ataufunika ili asiione dunia kwa jicho lake mwenyewe.’ 13 Nami nitautandaza wavu wangu juu yake, naye atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia;+ nami nitampeleka Babiloni, mpaka nchi ya Wakaldayo,+ lakini hataiona; naye atakufa huko.+ 14 Na wote wanaomzunguka ili kumsaidia, na majeshi yake yote, nitawatawanya kuelekea kila upepo;+ na upanga nitauchomoa nyuma yao.+ 15 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapowatawanya katikati ya mataifa nami kwa kweli niwatawanye katikati ya nchi hizo.+ 16 Na kati yao nitaacha watu wachache waponyoke upanga,+ njaa na tauni, ili wayasimulie machukizo+ yao yote katikati ya mataifa ambamo wataingia ndani yake;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”

17 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 18 “Mwana wa binadamu, utakula mkate wako kwa kutetemeka, nawe utakunywa maji yako kwa kufadhaika na kwa kuhangaika.+ 19 Nawe utawaambia watu wa nchi, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amewaambia wakaaji wa Yerusalemu katika udongo wa Israeli:+ “Watakula mkate wao kwa hangaiko, nao watakunywa maji yao kwa tisho, ili kujaa kwa nchi yao kufanywe kuwa ukiwa+ kwa sababu ya jeuri ya wale wote wanaokaa ndani yake.+ 20 Nayo majiji yanayokaliwa yatakuwa ukiwa,+ na nchi yenyewe itakuwa mahame yenye ukiwa;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” ’ ”+

21 Nalo neno la Yehova likazidi kunijia, na kusema: 22 “Mwana wa binadamu, ni neno gani hili la kimethali mlilo nalo katika udongo wa Israeli,+ linalosema, ‘Siku zimerefushwa,+ na maono yote yameangamia’?+ 23 Kwa hiyo waambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Hakika nitalifanya neno hili la kimethali likome, nao hawatalisema tena kama methali katika Israeli.” ’+ Lakini waambie, ‘Siku zimekaribia,+ na jambo linalohusu maono yote.’ 24 Kwa maana hakutakuwako tena maono yoyote yasiyo na thamani+ wala uaguzi wenye nyuso mbili katikati ya nyumba ya Israeli.+ 25 ‘ “Kwa maana mimi mwenyewe, Yehova, nitasema neno nitakalosema, nalo litafanywa.+ Hakutakuwa na kucheleweshwa tena,+ kwa maana katika siku zenu,+ Ee nyumba yenye kuasi, nitasema neno na kulifanya hakika,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’ ”

26 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 27 “Mwana wa binadamu, tazama! Wale wa nyumba ya Israeli wanasema, ‘Maono anayoona ni ya siku nyingi zinazokuja, naye anatoa unabii kuhusu nyakati zilizo mbali.’+ 28 Kwa hiyo waambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “ ‘Hakutakuwa na kucheleweshwa tena kwa yoyote ya maneno yangu.+ Neno nitakalosema, litafanywa,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” ’ ”+

13 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, toa unabii kuwahusu manabii wa Israeli wanaotoa unabii,+ nawe utawaambia wale wanaotoa unabii kutoka moyoni mwao wenyewe,+ ‘Sikieni neno la Yehova.+ 3 Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Ole wao manabii wajinga,+ wanaoifuata roho yao wenyewe,+ wakati ambapo hakuna chochote ambacho wameona!+ 4 Kama mbweha katika mahali palipo ukiwa ndivyo manabii wako mwenyewe wamekuwa, Ee Israeli.+ 5 Hakika ninyi hamtaingia katika mapengo,+ wala hamtajenga ukuta wa mawe+ kwa ajili ya nyumba ya Israeli, ili kusimama vitani katika ile siku ya Yehova.”+ 6 “Wameona maono ya jambo lisilo la kweli na uaguzi wa uwongo,+ wale wanaosema, ‘Neno la Yehova ni,’ wakati ambapo Yehova mwenyewe hajawatuma, nao wamengoja neno litimie.+ 7 Je, ninyi hamkuona maono yasiyo ya kweli, na kusema uaguzi wa uwongo, mnaposema, ‘Neno la Yehova ni,’ wakati ambapo mimi mwenyewe sikusema lolote?” ’+

8 “ ‘Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “ ‘Kwa sababu ninyi mmesema mambo yasiyo ya kweli na kuona uwongo, kwa hiyo tazama mimi niko dhidi yenu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” 9 Na mkono wangu umekuwa dhidi ya manabii wanaoona mambo yasiyo ya kweli na wanaoagua uwongo.+ Katika kikundi cha rafiki wa karibu+ wa watu wangu hawataendelea kukaa, nao hawataandikwa katika kitabu cha kuandikisha cha nyumba ya Israeli,+ na katika udongo wa Israeli hawatakuja;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova,+ 10 kwa sababu, naam, kwa sababu wamewapotosha watu wangu, na kusema, “Kuna amani!” wakati hakuna amani,+ pia kuna mtu anayejenga ukuta wa kugawanya, lakini kwa ubatili+ kuna wale wanaoupiga lipu kwa chokaa.’+

11 “Waambie wale wanaopiga lipu kwa chokaa kwamba huo utaanguka. Mvua kubwa yenye kufurika hakika itakuja, na ninyi, enyi mawe ya mvua, mtaanguka, na mlipuko wa dhoruba utasababisha mpasuko.+ 12 Na, tazama! ukuta huo lazima utaanguka. Je, ninyi hamtaambiwa, ‘Uko wapi mpako ambao mliupiga lipu?’+

13 “Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Pia nitasababisha mlipuko wa dhoruba ulipuke katika ghadhabu yangu, na katika hasira yangu kutatukia mvua yenye kufurika, na katika ghadhabu kutakuwa na mawe ya mvua kwa ajili ya maangamizi.+ 14 Nami nitaubomoa ukuta ambao ninyi mmeupiga lipu kwa chokaa na kuuangusha chini, nao msingi wake utafunuliwa.+ Naye hakika ataanguka, nanyi mtafikia mwisho katikati yake; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+

15 “ ‘Nami nitaimalizia ghadhabu yangu juu ya ukuta huo na juu ya wale wanaoupiga lipu kwa chokaa, nami nitawaambia ninyi: “Ukuta hauko tena, na wale wanaoupiga lipu hawako tena,+ 16 manabii wa Israeli wanaotoa unabii kwa Yerusalemu na ambao wanamwonea maono ya amani,+ wakati hakuna amani,” ’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+

17 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, elekeza uso+ wako juu ya binti za watu wako wanaotenda kama manabii+ kutokana na moyo wao wenyewe,+ utoe unabii juu yao. 18 Nawe utasema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Ole wao wanawake wanaoshona pamoja tepe juu ya viwiko vyote vya mkono na kufanya ushungi juu ya kichwa cha kila ukubwa ili kuwinda nafsi!+ Je, nafsi ambazo ninyi wanawake mnawinda ni zile za watu wangu, nazo nafsi zenu ndizo mnazohifadhi hai? 19 Na je, mtanitia unajisi mimi kuelekea watu wangu kwa ajili ya makonzi ya shayiri na kwa ajili ya vipande vya mkate,+ ili kuziua nafsi zisizopaswa kufa+ na ili kuzihifadhi hai nafsi zisizopaswa kuishi kwa uwongo wenu mnaowaambia watu wangu, wanaousikia uwongo?” ’+

20 “Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Tazama, mimi niko dhidi ya tepe zenu ninyi wanawake, ambazo mnatumia kuwinda nafsi kana kwamba ni vitu vinavyoruka, nami nitazipasua kutoka mikononi mwenu na kuzifungulia nafsi mnazowinda, nafsi kana kwamba ni vitu vinavyoruka.+ 21 Nami nitapasua ushungi wenu na kuwakomboa watu wangu kutoka katika mkono wenu, nao hawatakuwa tena windo mkononi mwenu; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 22 Kwa sababu kupitia uwongo mnauhuzunisha moyo wa aliye mwadilifu,+ wakati mimi mwenyewe sikuwa nimemsababishia maumivu, na kwa kuifanya mikono ya aliye mwovu kuwa yenye nguvu+ hivi kwamba asigeuke na kuiacha njia yake mbaya ili kumhifadhi hai,+ 23 kwa hiyo ninyi wanawake hamtaendelea kuona maono yasiyo ya kweli,+ na uaguzi+ ninyi hamtaufanya+ tena;+ nami nitawakomboa watu wangu kutoka katika mkono wenu,+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”+

14 Na wanaume kati ya wazee wa Israeli wakanijia na kuketi mbele yangu.+ 2 Ndipo neno la Yehova likanijia, na kusema: 3 “Mwana wa binadamu, kuhusu wanaume hawa, wameleta sanamu zao za mavi juu ya mioyo yao, na kikwazo kinachosababisha kosa lao wamekiweka mbele ya nyuso zao.+ Je, watauliza hata kidogo juu yangu?+ 4 Basi sema nao, nawe utawaambia, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Mtu yeyote wa nyumba ya Israeli anayeleta sanamu zake za mavi+ juu ya moyo wake na ambaye anaweka kikwazo kinachosababisha kosa lake mbele ya uso wake na kumwendea nabii, mimi, Yehova, nitakubali kuletwa ili nimjibu katika habari hiyo kulingana na wingi wa sanamu zake za mavi,+ 5 kwa kusudi la kuikamata nyumba ya Israeli kwa moyo wao,+ kwa sababu wao wenyewe wamejiondoa kwangu kupitia kwa sanamu zao za mavi—zote hizo.” ’+

6 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Rudini, mgeuke na kuziacha sanamu zenu za mavi+ na mgeuze nyuso zenu kutoka kwa machukizo yenu yote;+ 7 kwa maana mtu yeyote kutoka katika nyumba ya Israeli au kutoka kati ya wakaaji wageni wanaokaa wakiwa wageni katika Israeli, anayejiondoa mwenyewe asinifuate+ na anayeleta sanamu zake za mavi juu ya moyo wake na kuweka kikwazo kinachosababisha kosa mbele ya uso wake na ambaye anamjia nabii ili kuuliza habari kwa ajili yake mwenyewe kupitia kwangu, mimi,+ Yehova, mimi mwenyewe ninakubali kumjibu. 8 Nami nitauelekeza uso wangu juu ya mtu huyo+ na kumweka awe ishara+ na maneno ya kimethali,+ nami nitamkatilia mbali kutoka katikati ya watu wangu;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” ’+

9 “ ‘Naye nabii, ikiwa atapumbazwa naye hakika aseme neno, mimi mwenyewe, Yehova, nimempumbaza nabii huyo;+ nami nitaunyoosha mkono wangu juu yake na kumwangamiza kutoka katikati ya watu wangu Israeli.+ 10 Nao lazima watalibeba kosa lao.+ Kosa la mwenye kuuliza litakuwa kama kosa la nabii,+ 11 ili wale wa nyumba ya Israeli wasiweze tena kutanga-tanga na kuacha kunifuata+ wala wasijichafue tena kwa makosa yao yote. Nao watakuwa watu wangu na mimi mwenyewe nitakuwa Mungu wao,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”+

12 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 13 “Mwana wa binadamu, kwa habari ya nchi, ikiwa itanitendea dhambi kwa kutenda kwa kukosa uaminifu,+ pia nitaunyoosha mkono wangu juu yake na kuivunjia fimbo ambazo mikate ya mviringo huning’inizwa,+ nami nitaleta njaa+ juu yake na kumkatilia mbali mtu wa udongo na mnyama wa kufugwa kutoka ndani yake.”+ 14 “ ‘Na kama watu hawa watatu wangekuwa katikati yake, Noa,+ Danieli+ na Ayubu,+ wao wenyewe kwa sababu ya uadilifu+ wao wangeikomboa nafsi yao,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”+

15 “ ‘Au nikipitisha wanyama-mwitu wenye kudhuru nchini+ nao wawaue watoto+ wenu nayo nchi iwe mahame yenye ukiwa bila mtu yeyote anayeipitia kwa sababu ya wanyama-mwitu,+ 16 kama watu hao watatu wangekuwa katikati yake, kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hawangekomboa wana wala mabinti; wao, wao wenyewe tu, ndio wangekombolewa nayo nchi ingekuwa mahame yenye ukiwa.’ ”+

17 “ ‘Au kama ningeuleta upanga juu ya nchi hiyo,+ nami niseme: “Upanga wenyewe upite katikati ya nchi,” nami nimkatilie mbali mtu wa udongo na mnyama wa kufugwa,+ 18 hata kama watu hawa watatu wangekuwa katikati yake,+ kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hawangekomboa wana wala mabinti, bali wao, wao wenyewe tu, ndio wangekombolewa.’ ”+

19 “ ‘Au kama ningeileta tauni juu ya nchi hiyo+ nami nimwage ghadhabu yangu juu yake pamoja na damu,+ ili kumkatilia mbali mtu wa udongo na mnyama wa kufugwa, 20 hata kama Noa,+ Danieli+ na Ayubu+ wangekuwa katikati yake,+ kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hawangekomboa mwana wala binti; wao wenyewe kwa sababu ya uadilifu wao wangeikomboa nafsi yao.’ ”+

21 “Kwa maana hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Hivyo, pia, ndivyo itakavyokuwa wakati kutakapokuwa na hukumu zangu nne zenye madhara+—upanga na njaa na mnyama-mwitu mwenye kudhuru na tauni+—nitakazoleta juu ya Yerusalemu ili kumkatilia mbali kutoka humo mtu wa udongo na mnyama wa kufugwa.+ 22 Lakini, tazama! jamii iliyoponyoka hakika itabaki ndani yake, wale wanaoletwa.+ Wana na mabinti, tazama! Wanawatokea ninyi, nanyi mtalazimika kuona njia yao na shughuli zao.+ Nanyi hakika mtafarijiwa juu ya msiba ambao nitakuwa nimeuleta juu ya Yerusalemu, naam, yote nitakayokuwa nimeleta juu yake.’ ”

23 “ ‘Na hakika wao watawafariji ninyi wakati ambapo mtaiona njia yao na shughuli zao; nanyi mtalazimika kujua kwamba sitakuwa nimetenda, bila sababu, yote hayo ambayo lazima nitatenda juu yake,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”+

15 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, mzabibu+ hutofautianaje na kila mti mwingine, hilo chipukizi, ambalo limekuja kuwa kati ya miti ya msituni? 3 Je, ufito huchukuliwa kutoka kwa huo ili kuutumia kufanyia kazi? Au watu huchukua kutoka kwa huo kijiti ili kuning’iniza aina yoyote ya chombo juu yake? 4 Tazama! Lazima utiwe motoni uwe kuni.+ Hakika moto huteketeza miisho yake yote miwili, na sehemu yake ya katikati huungua.+ Je, unafaa kwa kazi yoyote? 5 Tazama! Unapokuwa mzima, hautumiwi kwa kazi yoyote. Itakuwaje basi wakati ambapo moto umeuteketeza nao umeungua, je, kwa kweli unaweza kutumiwa tena kwa kazi zaidi!”+

6 “Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Kama vile mzabibu kati ya miti ya msituni, ambao nimeupa moto uwe kuni, ndivyo nimewatoa wakaaji wa Yerusalemu.+ 7 Nami nimeukaza uso wangu juu yao.+ Wametoka motoni, lakini moto wenyewe utawateketeza.+ Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, nitakapouelekeza uso wangu juu yao.’ ”+

8 “ ‘Nami nitaifanya nchi iwe mahame yenye ukiwa,+ kwa sababu wametenda kwa kukosa uaminifu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

16 Nalo neno la Yehova likazidi kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, julisha+ Yerusalemu machukizo yake.+ 3 Nawe utasema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameambia Yerusalemu: “Asili yako na kuzaliwa kwako ni katika nchi ya Mkanaani.+ Baba yako alikuwa Mwamori,+ na mama yako alikuwa Mhiti.+ 4 Na kuhusu kuzaliwa kwako, katika siku ya kuzaliwa+ kwako uzi wa kitovu chako haukuwa umekatwa, na katika maji hukuwa umeoshwa ili usafishwe, nawe hukuwa kamwe umepakwa chumvi, wala hukuwa umefungwa kwa nguo kamwe. 5 Hakuna jicho lililokusikitikia ili kukufanyia moja la mambo haya kwa kukuhurumia,+ bali ulitupwa kwenye uso wa uwanja kwa sababu nafsi yako ilichukiwa katika siku ya kuzaliwa kwako.

6 “ ‘ “Nami nilipita kando yako na kukuona ukitupatupa mateke katika damu yako, nami nikakuambia katika damu yako, ‘Endelea kuishi!’+ naam, kukuambia wewe katika damu yako, ‘Endelea kuishi!’ 7 Nilikufanya uwe umati mkubwa sana kama kuchipuka kwa shamba ili uwe mkubwa+ na kuwa mkuu na kuingia ndani ukiwa na pambo bora kabisa.+ Yale maziwa mawili yalikomaa kabisa, nywele zako mwenyewe zikakua sana, ulipokuwa uchi na tupu.” ’

8 “ ‘Nami nikaja nikipita kando yako nikakuona, na, tazama! wakati wako ulikuwa wakati wa maonyesho ya upendo.+ Kwa hiyo nikatandaza upindo wa nguo yangu juu yako+ na kuufunika utupu wako na kukutolea ahadi yenye kiapo na kuingia katika agano pamoja nawe,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘na kwa hiyo ukawa wangu.+ 9 Tena, nikakuosha kwa maji+ na kuiosha damu yako kutoka juu yako na kukupaka mafuta.+ 10 Nami nikakuvika vazi lililopambwa+ na kukuvika viatu vya ngozi ya sili+ na kukufunika kwa kitani bora+ na kukufunika kwa kitambaa cha bei. 11 Nami nikakupamba kwa mapambo na kuweka vikuku+ juu ya mikono yako na mkufu+ shingoni mwako. 12 Tena, nikaweka pete ya puani+ katika pua yako na vipuli katika masikio+ yako na taji zuri kichwani pako.+ 13 Nawe ukaendelea kujipamba kwa dhahabu na fedha, nayo mavazi yako yalikuwa kitani bora na kitambaa cha bei na vazi lililopambwa.+ Chakula chako kilikuwa unga laini na asali na mafuta,+ nawe ukawa mrembo, mrembo sana, na mwishowe ukastahili kwa ajili ya cheo cha kifalme.’ ”+

14 “ ‘Nalo jina lako likaanza kuenea kati ya mataifa kwa sababu ya urembo wako, kwa maana ulikuwa kamili kwa sababu ya fahari yangu niliyoiweka juu yako,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

15 “‘Lakini ulianza kuutegemea urembo wako+ nawe ukawa kahaba kwa sababu ya jina lako+ na kumimina matendo yako ya ukahaba kwa kila mpita-njia;+ ukawa wake. 16 Nawe ukachukua sehemu ya mavazi yako na kujifanyia mwenyewe mahali pa juu+ penye rangi mbalimbali nawe ukawa ukifanya ukahaba juu yake+—mambo hayo hayaingii, na hayapasi kutukia hivyo. 17 Nawe ukawa ukichukua vyombo vyako vyenye kupendeza kutoka katika dhahabu yangu na katika fedha yangu niliyokuwa nimekupa wewe+ nawe ukawa ukijifanyia mwenyewe sanamu za mwanamume+ na kufanya ukahaba nazo.+ 18 Nawe ukawa ukiyachukua mavazi yako yaliyopambwa na kuzifunika; na mafuta yangu na uvumba+ wangu ukawa ukiweka mbele yake. 19 Na mkate wangu niliokuwa nimekupa wewe—unga laini na mafuta na asali nilivyokuwa nimekulisha+—uliviweka viwe harufu yenye kutuliza+ mbele yake, na ikaendelea kutukia hivyo,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

20 “ ‘Nawe ulikuwa ukiwachukua wana na binti zako uliokuwa umenizalia,+ na ukawa ukiwatoa dhabihu kwao ili wamezwe+—je, matendo yako hayo ya ukahaba hayatoshi? 21 Nawe ukawa ukiwachinja wanangu,+ na kwa kuwafanya wapite katikati ya moto ukawa ukiwatolea hao.+ 22 Na katika machukizo yako yote na matendo yako ya ukahaba hukukumbuka siku za ujana wako ulipokuwa uchi na tupu; ulikuwa ukitupatupa mateke katika damu yako.+ 23 Kwa hiyo ikawa kwamba baada ya ubaya wako wote (“ole, ole wako,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova) 24 ulijijengea kilima na kujifanyia kilele katika kila kiwanja cha watu wote.+ 25 Katika kila kichwa cha njia ulikijenga kilele+ chako nawe ukaanza kuufanya urembo wako kuwa chukizo+ na kumpanulia miguu yako kila mpita-njia+ na kuzidisha matendo yako ya ukahaba.+ 26 Nawe ukafanya ukahaba na wana wa Misri,+ jirani zako wenye kiungo kikubwa,+ nawe ukaendelea kuufanya ukahaba wako uwe mwingi ili kunitia uchungu. 27 Na, tazama! hakika nitaunyoosha mkono wangu juu yako+ nami nitapunguza posho lako+ na kukutia katika tamaa ya nafsi+ ya wanawake wanaokuchukia,+ binti za Wafilisti,+ wanawake waliofedheheshwa kwa sababu ya njia yako kuhusiana na mwenendo mpotovu.+

28 “ ‘Nawe ukaendelea kufanya ukahaba na wana wa Ashuru kwa sababu hukutoshelezwa,+ nawe ukaendelea kufanya ukahaba pamoja nao, nawe hukutoshelezwa pia. 29 Kwa hiyo ukazidi kuufanya ukahaba wako uwe mwingi kuelekea nchi ya Kanaani,+ kuwaelekea Wakaldayo;+ na hata katika hilo hukutoshelezwa. 30 Lo! Jinsi nilivyojaa ghadhabu+ juu yako,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘kwa kufanya kwako mambo yote haya, kazi ya mwanamke,+ kahaba mwenye kutawala!+ 31 Ulipojenga kilima chako kwenye kichwa cha kila njia na kufanya kilele chako mwenyewe katika kila kiwanja cha watu wote, hata hivyo ukawa tofauti na kahaba kwa kudharau malipo. 32 Kuhusu mwanamke anayefanya uzinzi, yeye huwachukua wageni badala ya mume wake mwenyewe.+ 33 Watu wana desturi ya kuwapa zawadi makahaba wote,+ lakini wewe—wewe umewapa zawadi wote wanaokupenda kwa tamaa,+ nawe unawapa rushwa waingie kwako kutoka pande zote katika matendo+ yako ya ukahaba. 34 Na kukuhusu wewe jambo lililo kinyume linatukia tofauti na walivyo wanawake wengine katika matendo yako ya ukahaba, na hakuna ukahaba ambao umefanywa kama wa mtindo wako, naam, kwa wewe kutoa malipo wakati ambapo hakuna malipo uliyopewa, na kwa hiyo mambo yanatukia kinyume.’

35 “Kwa hiyo, Ee kahaba,+ lisikie neno la Yehova.+ 36 Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Kwa sababu uchu wako umemiminwa+ nazo sehemu zako za siri+ zimefunuliwa katika matendo yako ya ukahaba kuwaelekea wale wanaokupenda+ kwa tamaa na kuelekea sanamu zako zote za mavi zenye kuchukiza,+ hata kwa damu ya wana wako ambao ulizipa hizo,+ 37 kwa hiyo, tazama, ninawakusanya pamoja wote wanaokupenda kwa tamaa ambao ulikuwa mwenye kupendeza kwao na wale wote uliowapenda pamoja na wale wote uliowachukia, nami nitawakusanya hao pamoja juu yako kutoka pande zote na kuwafunulia sehemu zako za siri, nao wataziona sehemu zako zote za siri.+

38 “ ‘Nami nitakuhukumu kwa hukumu za wanawake wazinzi+ na wanawake wanaomwaga damu,+ nami nitakupa damu ya ghadhabu na wivu.+ 39 Nami nitakutia mkononi mwao, nao hakika watakibomoa kilima+ chako na vilele vyako hakika vitabomolewa,+ nao watakuvua mavazi+ yako na kuvichukua vyombo vyako vyenye urembo+ na kukuacha ukiwa uchi na tupu. 40 Nao wataleta kutaniko+ juu yako na kukupiga kwa mawe+ na kukuchinja kwa panga zao.+ 41 Nao wataziteketeza nyumba zako kwa moto+ na kufanya ndani yako matendo ya hukumu mbele ya macho ya wanawake wengi;+ nami nitakufanya uache kuwa kahaba,+ na pia hutatoa malipo yoyote tena. 42 Na ghadhabu yangu nitaituliza ndani yako,+ na wivu wangu utageukia mbali nawe;+ nami nitakaa kimya wala sitaendelea kuwa na uchungu tena.’

43 “ ‘Kwa sababu hukuzikumbuka siku za ujana wako+ nawe ulikuwa ukinisumbua kwa sababu ya mambo yote haya,+ hata hapa mimi pia, nitaiweka njia yako mwenyewe juu ya kichwa chako mwenyewe,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nawe hakika hutaendeleza mwenendo mpotovu wowote pamoja na machukizo yako yote.

44 “ ‘Tazama! Kila mtu anayetumia methali+ juu yako ataitumia methali, na kusema: “Kama mama ndivyo binti alivyo!”+ 45 Wewe ni binti ya mama yako,+ anayemchukia mume+ wake na wanawe. Na wewe ni dada ya dada zako, waliowachukia waume zao na wana wao. Mama yenu ninyi wanawake alikuwa Mhiti,+ na baba yenu alikuwa Mwamori.’ ”+

46 “ ‘Na dada yako mkubwa ni Samaria+ pamoja na miji yake ya kandokando,+ anayekaa upande wako wa kushoto, na dada yako aliye mdogo wako, anayekaa upande wako wa kuume, ni Sodoma+ pamoja na miji yake ya kandokando.+ 47 Nawe hukutembea katika njia zao, wala hukufanya kulingana na machukizo yao.+ Baada ya kitambo kidogo sana hata ulianza kutenda kwa uharibifu zaidi kuliko walivyofanya katika njia zako zote.+ 48 Kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘Sodoma dada yako, yeye pamoja na miji yake ya kandokando, hajatenda kulingana na uliyotenda, wewe na miji yako ya kandokando.+ 49 Tazama! Hili ndilo lililokuwa kosa la Sodoma dada yako: Yeye pamoja na miji yake ya kandokando+ walikuwa na kiburi,+ utoshelevu wa mkate+ na ukosefu wa wasiwasi+ wa kukaa bila usumbufu, naye hakuutia nguvu mkono wa mwenye kuteseka na aliye maskini.+ 50 Nao wakaendelea kuwa wenye majivuno+ na kuendeleza chukizo mbele zangu,+ na mwishowe mimi nikawaondoa, kama nilivyoona kuwa inafaa.+

51 “ ‘Naye Samaria,+ hajatenda dhambi hata kufikia nusu ya dhambi zako, lakini wewe uliendelea kuyafanya machukizo yako yawe mengi kuliko walivyotenda, hivi kwamba ukawafanya dada zako waonekane kuwa waadilifu kwa sababu ya machukizo yako yote uliyoyaendeleza.+ 52 Wewe pia, beba fedheha yako utakapolazimika kuwatetea dada zako. Kwa sababu ya dhambi zako ambazo ulitenda kwa njia yenye kuchukiza zaidi kuliko walivyotenda, wao ni waadilifu zaidi kuliko wewe.+ Na wewe pia, na upate aibu na kubeba fedheha yako kwa kuwa unawafanya dada zako waonekane kuwa waadilifu.’

53 “ ‘Nami nitawakusanya mateka wao,+ mateka wa Sodoma na wa miji yake ya kandokando, na mateka wa Samaria na wa miji yake ya kandokando; pia nitawakusanya mateka wako katikati yao,+ 54 ili uibebe fedheha yako;+ nawe utafedheheka kwa sababu ya yote ambayo umefanya, kwa kuwa uliwafariji.+ 55 Na dada zako wenyewe, Sodoma na miji yake ya kandokando, watarudi kwenye hali yao ya kwanza, na Samaria na miji yake ya kandokando watarudi kwenye hali yao ya kwanza, na wewe mwenyewe na miji yako ya kandokando mtarudi kwenye hali yenu ya kwanza.+ 56 Na Sodoma dada yako hakuwa kitu kinachostahili kusikiwa kutoka kinywani mwako katika siku ya fahari yako,+ 57 kabla ubaya wako mwenyewe haujafunuliwa,+ kama katika ule wakati wa shutuma ya binti za Siria+ na za wote waliomzunguka pande zote, binti za Wafilisti,+ wale wanaokutendea kwa dharau pande zote.+ 58 Mwenendo wako mpotovu+ na machukizo yako, wewe mwenyewe lazima uyabebe,’+ asema Yehova.”

59 “Kwa maana hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Mimi pia lazima nikutendee wewe kama vile ulivyotenda,+ kwa sababu ulikidharau kiapo kwa kuvunja agano langu.+ 60 Nami, mimi mwenyewe, nitalikumbuka agano langu pamoja nawe katika siku za ujana wako,+ nami nitakufanyia wewe agano lenye kudumu mpaka wakati usio na kipimo.+ 61 Nawe hakika utazikumbuka njia zako+ na kufedheheka unapowapokea dada zako, walio wakubwa wako na walio wadogo wako, nami hakika nitakupa wao wawe mabinti,+ lakini si kwa sababu ya agano lako.’+

62 “ ‘Na mimi, mimi mwenyewe, nitalifanya agano langu pamoja nawe;+ nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, 63 ili ukumbuke na kuona aibu+ nawe usije kamwe kuwa na sababu ya kufungua kinywa+ chako kwa sababu ya kufedheheka kwako, nitakapofanya upatanisho+ kwa ajili yako kwa sababu ya yote ambayo umetenda,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

17 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, tega kitendawili+ na utunge neno la kimethali kuelekea nyumba ya Israeli.+ 3 Nawe utasema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Tai mkubwa,+ mwenye mabawa makubwa,+ na manyoya marefu, aliyejaa manyoya, yaliyokuwa na rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni+ na kukichukua kilele+ cha mwerezi.+ 4 Aliking’oa kilele cha machipukizi yake machanga, akakileta mpaka nchi ya Kanaani;+ akakiweka katika jiji la wafanya-biashara. 5 Tena, akachukua sehemu ya mbegu ya nchi+ hiyo na kuiweka katika shamba la mbegu. Akaiweka kama mvinje kando ya maji mengi,+ kama mti wa mvinje. 6 Nayo ikaanza kuchipuka na hatua kwa hatua ikawa mzabibu wenye majani mengi na ulio mfupi,+ wenye mwelekeo wa kugeuza majani yake kuelekea ndani; nayo mizizi yake, hatua kwa hatua ikaja kuwa chini yake. Nao mwishowe ukawa mzabibu, ukazaa machipukizi na kutokeza matawi.+

7 “ ‘ “Na kukawa na tai mwingine mkubwa,+ mwenye mabawa makubwa, na mwenye manyoya makubwa,+ na, tazama! mzabibu huohuo ukasambaza mizizi yake kwa pupa kumwelekea.+ Nao ukamnyooshea majani yake ili ayanyweshe, mbali na eneo dogo la bustani mahali ulipopandwa.+ 8 Katika shamba zuri, kando ya maji mengi, tayari ulikuwa umepandikizwa,+ ili utokeze matawi na kuzaa matunda, uwe mzabibu mkubwa.” ’

9 “Sema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Je, huo utakuwa na mafanikio?+ Je, mtu fulani hataing’oa mizizi yake+ na kuyafanya matunda yake yawe na magamba? Na je, machipukizi yake yote yaliyokatwa hivi karibuni hayatakauka?+ Utakauka. Hautainuliwa kutoka mizizini mwake kwa mkono wenye nguvu wala kwa umati wa watu. 10 Na, tazama! ijapokuwa ulipandikizwa, je, utakuwa na mafanikio? Je, hautakauka kabisa, kama wakati ambapo upepo wa mashariki huugusa?+ Utakauka katika eneo dogo la bustani la chipukizi lake.” ’ ”+

11 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 12 “Iambie, tafadhali, nyumba yenye kuasi,+ ‘Je, ninyi kwa kweli hamjui maana ya mambo haya?’ Sema, ‘Tazama! Mfalme wa Babiloni alikuja Yerusalemu, akamchukua mfalme wake+ na wakuu wake na kuwaleta Babiloni kwa ajili yake.+ 13 Tena, alichukua mmoja wa uzao wa kifalme,+ akafanya agano naye na kumwingiza katika kiapo;+ na watu wa kwanza kabisa wa nchi akawachukua,+ 14 ili ufalme huo ushuke,+ usiweze kujiinua, ili kwa kushika agano lake uweze kusimama.+ 15 Lakini mwishowe alimwasi+ kwa kutuma wajumbe wake Misri, ili wampe farasi+ na umati wa watu. Je, atakuwa na mafanikio? Je, ataponyoka, yeye anayefanya mambo haya, na ambaye amevunja agano? Na je, kwa kweli ataponyoka?’+

16 “ ‘ “Kama ninavyoishi,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “mahali pa mfalme aliyemweka kuwa mfalme yule aliyekidharau kiapo+ chake na ambaye alilivunja agano lake, atakufa pamoja naye katikati ya Babiloni.+ 17 Na kwa jeshi kubwa na kwa kutaniko lenye watu wengi Farao hatamfanya apate mafanikio katika vita,+ kwa kujenga boma la kuzingira na kwa kujenga ukuta wa kuzingira, ili kukatilia mbali nafsi nyingi.+ 18 Naye amedharau kiapo kwa kuvunja agano,+ na, tazama! alikuwa ameutia mkono+ wake naye amefanya mambo yote hayo. Yeye hataponyoka.” ’+

19 “ ‘Kwa hiyo, hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Kama ninavyoishi, hakika kiapo changu ambacho amekidharau+ na agano langu ambalo amelivunja—nitamletea juu ya kichwa chake. 20 Nami nitautandaza wavu wangu juu yake, naye hakika atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia;+ nami nitamleta Babiloni na kujiweka katika hukumu pamoja naye huko kuhusiana na ukosefu wake wa uaminifu alionitendea.+ 21 Nao wakimbizi wake wote katika vikosi vyake vyote, wataanguka kwa upanga, nao wanaobaki watatawanywa kotekote kuelekea kila upepo.+ Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema hilo.” ’+

22 “ ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Mimi mwenyewe nitachukua pia na kuweka sehemu ya vilele vilivyo juu sana vya mierezi;+ kutoka juu ya vitawi vyake nitang’oa kitawi kichanga+ nami mwenyewe nitakipandikiza juu ya mlima mrefu na ulio juu sana.+ 23 Kwenye mlima wa kilele cha Israeli nitakipandikiza,+ nacho hakika kitazaa matawi na kutokeza matunda+ na kuwa mwerezi mkubwa.+ Na chini yake hakika watakaa ndege wote wenye mabawa ya kila aina; watakaa katika uvuli wa majani yake.+ 24 Na miti yote ya shambani italazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova,+ nimeushusha ule mti mrefu,+ nimeuweka juu ule mti mfupi,+ nimeukausha ule mti ambao ungali mbichi+ na kuufanya mti uliokauka uchipuke. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nimefanya+ hilo.” ’ ”

18 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Inamaanisha nini kwenu kwamba mnataja neno hili la kimethali kwenye udongo wa Israeli, na kusema, ‘Akina baba ndio wanaokula zabibu mbichi, lakini meno ya wana ndiyo yanayotiwa ukakasi’?+

3 “ ‘Kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hamtaendelea kuwa na sababu ya kulitaja neno hili la kimethali katika Israeli. 4 Tazama! Nafsi zote—ni zangu.+ Kama ilivyo nafsi+ ya baba ndivyo ilivyo nafsi ya mwana—ni zangu.+ Nafsi inayotenda dhambi+—hiyo yenyewe itakufa.+

5 “ ‘Na mtu, ikiwa ni mwadilifu naye ametenda haki na uadilifu;+ 6 naye hakula+ juu ya milima+ wala hakuyainua macho yake kuelekea sanamu za mavi za nyumba ya Israeli,+ wala hakumnajisi mke wa mwenzake+ wala hakumkaribia mwanamke aliye katika uchafu wake;+ 7 wala hakumtendea vibaya mtu yeyote;+ rehani aliyotwaa kwa ajili ya deni, alikuwa akiirudisha;+ hakuwa akinyakua chochote kwa unyang’anyi;+ mkate wake mwenyewe alikuwa akimpa mwenye njaa+ na alikuwa akimvika vazi aliye uchi;+ 8 naye hakuwa akitoa chochote apate faida+ wala hakuwa akichukua riba yoyote;+ naye alikuwa akiuepusha mkono wake na ukosefu wa haki;+ naye alikuwa akiitenda haki ya kweli kati ya mtu na mwenzake;+ 9 naye aliendelea kutembea katika amri zangu+ na aliyashika maamuzi yangu ya hukumu ili kutenda kweli,+ yeye ni mwadilifu.+ Hakika yeye ataendelea kuishi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

10 “ ‘Na ikiwa mtu amemzaa mwana ambaye ni mnyang’anyi,+ mmwagaji wa damu,+ ambaye amefanya jambo linalofanana na moja kati ya mambo hayo 11 (lakini yeye mwenyewe hajafanya lolote la mambo hayo); ikiwa yeye pia amekula juu ya milima,+ naye amemnajisi mke wa mwenzake;+ 12 naye amemtendea vibaya mtu mwenye kuteseka na aliye maskini;+ naye amenyakua vitu kwa unyang’anyi,+ naye hakuwa akirudisha kitu kilichowekwa rehani;+ naye aliyainua macho yake kuelekea sanamu za mavi,+ yeye amefanya chukizo.+ 13 Ametoa kwa riba,+ na amechukua faida,+ naye hakika hataendelea kuishi. Ameyafanya machukizo hayo yote.+ Hakika atauawa. Damu yake mwenyewe itakuwa juu yake.+

14 “ ‘Na, tazama! mtu amemzaa mwana, ambaye anaendelea kuona dhambi zote za baba yake ambazo amefanya, naye anaona lakini hafanyi mambo kama hayo.+ 15 Hajakula juu ya milima, naye hajayainua macho yake kuelekea sanamu za mavi za nyumba ya Israeli;+ hajamnajisi mke wa mwenzake;+ 16 wala hajamtendea vibaya+ mtu yeyote, hajachukua rehani+ yoyote, wala hajachukua chochote kwa unyang’anyi;+ yeye amempa mwenye njaa mkate wake mwenyewe,+ na amemvika vazi aliye uchi;+ 17 ameuepusha mkono wake na mwenye kuteseka; hajachukua riba+ wala faida+ yoyote; ameyafanya maamuzi yangu ya hukumu;+ ametembea katika amri zangu;+ yeye mwenyewe hatakufa kwa sababu ya kosa la baba yake.+ Hakika ataendelea kuishi.+ 18 Naye baba yake, kwa sababu alifanya unyang’anyi+ wa moja kwa moja, alinyakua kitu kwa kumnyang’anya ndugu,+ na lolote ambalo si zuri amelifanya katikati ya watu wake,+ tazama! basi lazima afe kwa ajili ya kosa lake.+

19 “ ‘Nanyi hakika mtasema: “Kwa nini mwana hawezi kuwa na hatia yoyote kwa sababu ya kosa la baba?”+ Sasa kwa habari ya mwana huyo, yeye ametenda haki na uadilifu,+ amezishika amri zangu zote naye anaendelea kuzitenda.+ Hakika ataendelea kuishi.+ 20 Nafsi inayotenda dhambi—hiyo yenyewe itakufa.+ Mwana hatakuwa na hatia yoyote kwa sababu ya kosa la baba, na baba hatakuwa na hatia yoyote kwa sababu ya kosa la mwana.+ Uadilifu wa mwadilifu utakuwa juu yake mwenyewe,+ nao uovu wa mwovu utakuwa juu yake mwenyewe.+

21 “ ‘Sasa kwa habari ya mwovu, ikiwa atageuka na kuziacha dhambi zake zote ambazo ametenda+ naye hakika ashike sheria zangu zote na kutenda haki na uadilifu,+ hakika yeye ataendelea kuishi. Hatakufa.+ 22 Makosa yake yote ambayo ametenda—hayo hayatakumbukwa juu yake.+ Ataendelea kuishi kwa uadilifu ambao ametenda.’+

23 “ ‘Je, ninapendezwa hata kidogo na kifo cha mtu mwovu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘bali kwamba ageuke na kuziacha njia zake, naye kwa kweli aendelee kuishi?’+

24 “ ‘Sasa, mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu wake naye kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki;+ kulingana na machukizo yote ambayo mwovu ametenda yeye anaendelea kutenda+ naye anaishi, hakuna lolote la matendo yake ya uadilifu ambayo ametenda litakalokumbukwa.+ Atakufa kwa sababu ya ukosefu wake wa uaminifu ambao ametenda na kwa sababu ya dhambi ambayo ametenda.+

25 “ ‘Nanyi hakika mtasema: “Njia ya Yehova si sawa.”+ Sikia, tafadhali, Ee nyumba ya Israeli. Je, njia yangu mwenyewe si sawa?+ Je, njia zenu ninyi sizo ambazo si sawa?+

26 “ ‘Mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu wake naye kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki+ na afe kutokana nao, atakufa kwa sababu ya kutenda kwa njia isiyo ya haki.+

27 “ ‘Na mwovu anapogeuka na kuuacha uovu wake ambao ameutenda naye atende haki na uadilifu,+ yeye ndiye atakayeihifadhi hai nafsi yake mwenyewe.+ 28 Anapoona+ na kugeuka na kuyaacha makosa yake yote ambayo ametenda,+ hakika yeye ataendelea kuishi. Hatakufa.+

29 “ ‘Nayo nyumba ya Israeli hakika itasema: “Njia ya Yehova si sawa.”+ Nazo njia zangu, je, si sawa, Ee nyumba ya Israeli?+ Je, njia zenu sizo ambazo si sawa?’+

30 “ ‘Kwa hiyo nitawahukumu ninyi kila mmoja kulingana na njia yake,+ Ee nyumba ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ ‘Geukeni, naam, geukeni na kuyaacha makosa yenu yote,+ na chochote kisiwe kwenu kikwazo kinachosababisha kosa.+ 31 Tupilieni mbali kutoka juu yenu makosa yenu yote mliyokosa+ na kujifanyia wenyewe moyo mpya+ na roho mpya,+ kwa maana kwa nini mfe,+ Ee nyumba ya Israeli?’

32 “ ‘Kwa maana sipendezwi na kifo cha mtu anayekufa,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Kwa hiyo geukeni, mwendelee kuishi.’ ”+

19 “Nawe, imba wimbo wa huzuni+ kuhusu wakuu wa Israeli,+ 2 nawe useme, ‘Mama yako alikuwa nini? Simba-jike kati ya simba.+ Alilala kati ya wana-simba wenye manyoya shingoni. Aliwalea watoto wake.

3 “ ‘Na hatua kwa hatua akamlea mmoja wa watoto wake.+ Akawa mwana-simba mwenye manyoya shingoni, naye akaanza kujifunza jinsi ya kurarua mawindo.+ Alimrarua hata mtu wa udongo. 4 Na mataifa yakaendelea kusikia juu yake. Akakamatwa katika shimo lao, nao wakamchukua kwa kulabu mpaka katika nchi ya Misri.+

5 “ ‘Mama huyo alipoona kwamba amengoja nalo tumaini lake lilikuwa limepotea, ndipo akachukua mwingine kati ya watoto wake.+ Akamweka kuwa mwana-simba mwenye manyoya shingoni. 6 Na huyo akaanza kutembea huku na huku katikati ya simba. Akawa mwana-simba mwenye manyoya shingoni. Naye hatua kwa hatua akajifunza jinsi ya kurarua mawindo.+ Akamrarua hata mtu wa udongo.+ 7 Naye akaijua minara ya makao yake, akayaharibu majiji yao,+ hivi kwamba nchi ikafanywa ukiwa naye akaijaza kwa sauti ya mngurumo wake.+ 8 Na mataifa kuzunguka pande zote kutoka katika wilaya za utawala wakaanza kujipanga dhidi yake+ na kuutandaza wavu wao juu yake.+ Akakamatwa katika shimo lao.+ 9 Mwishowe wakamweka katika tundu kwa kulabu na kumleta kwa mfalme wa Babiloni.+ Wakamleta kwa kutumia nyavu za kuwindia, ili sauti yake isisikiwe tena katika milima ya Israeli.+

10 “ ‘Mama yako+ alikuwa kama mzabibu katika damu yako,+ uliopandwa kando ya maji. Akawa mwenye kuzaa matunda na mwenye kujaa matawi kwa sababu ya maji mengi.+ 11 Nayo yakawa kwake fimbo zenye nguvu, zilizokusudiwa kuwa fimbo za enzi za watawala.+ Nacho kimo chake kikarefuka hatua kwa hatua katikati ya matawi, nao ukaonekana kwa sababu ya urefu wake, kwa sababu ya wingi wa majani yake.+ 12 Lakini mwishowe aling’olewa kwa ghadhabu.+ Akatupwa chini, na kulikuwa na upepo wa mashariki ulioyakausha matunda yake.+ Fimbo yake yenye nguvu ilikatwa nayo ikakauka.+ Moto wenyewe ukaiteketeza.+ 13 Na sasa amepandwa nyikani,+ katika nchi isiyo na maji na yenye kiu.+ 14 Na moto ukatoka katika fimbo yake.+ Ukateketeza machipukizi yake, matunda yake, na ndani yake akawa hana fimbo yoyote yenye nguvu, fimbo yoyote ya enzi ya kutawalia.+

“ ‘Huo ni wimbo wa huzuni, nao utakuwa wimbo wa huzuni.’ ”+

20 Ikawa kwamba katika mwaka wa saba, katika mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi huo, baadhi ya watu kati ya wazee wa Israeli wakaja kuuliza juu ya Yehova,+ nao wakaketi mbele yangu.+ 2 Ndipo neno la Yehova likanijia, na kusema: 3 “Mwana wa binadamu, sema na wanaume wazee wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Je, mnakuja kuuliza neno juu yangu?+ ‘Kama ninavyoishi, hamtauliza neno juu yangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” ’

4 “Je, utawahukumu? Je, utawahukumu, Ee mwana wa binadamu?+ Wajulishe machukizo ya mababu zao.+ 5 Nawe utawaambia, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Katika siku ile nilipochagua Israeli,+ pia niliuinua mkono+ wangu katika kiapo kwa uzao wa nyumba ya Yakobo+ na kujijulisha kwao katika nchi ya Misri.+ Naam, niliuinua mkono wangu katika kiapo kwao, na kusema, ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu.’+ 6 Katika siku hiyo niliuinua mkono+ katika kiapo kwao ili kuwatoa katika nchi ya Misri mpaka katika nchi niliyokuwa nimeipeleleza kwa ajili yao, yenye kutiririka maziwa na asali.+ Hiyo ilikuwa ni pambo la nchi zote.+ 7 Nami nikaendelea kuwaambia, ‘Tupilieni mbali, kila mmoja wenu, machukizo ya macho yake,+ nanyi msijitie unajisi kwa sanamu za mavi za Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’+

8 “ ‘ “Nao wakaanza kuniasi,+ wala hawakukubali kunisikiliza. Kila mmoja wao hakuyatupilia mbali machukizo ya macho yake, nazo sanamu zao za mavi za Misri hawakuziacha,+ hivi kwamba nikaahidi kumwaga ghadhabu yangu juu yao, ili kuitimiliza hasira yangu juu yao katikati ya nchi ya Misri.+ 9 Nami nikachukua hatua kwa ajili ya jina langu mwenyewe ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa ambayo walikuwa katikati yao,+ kwa sababu nilikuwa nimejijulisha kwao mbele ya macho yao kwa kuwatoa katika nchi ya Misri.+ 10 Kwa hiyo nikawatoa katika nchi ya Misri na kuwaingiza nyikani.+

11 “ ‘ “Nami nikawapa sheria+ zangu; nayo maamuzi yangu ya hukumu+ nikawajulisha, ili mtu ambaye huendelea kuyafanya aweze pia kuishi kwa hayo.+ 12 Nami nikawapa pia sabato zangu,+ ziwe ishara kati yangu nao,+ ili wajue kwamba mimi ni Yehova ninayewatakasa.

13 “ ‘ “Lakini wao, nyumba ya Israeli, waliniasi nyikani.+ Hawakutembea katika sheria+ zangu, nao wakayakataa maamuzi yangu ya hukumu,+ ambayo, mtu akiendelea kuyafanya, pia ataendelea kuishi kwa hayo.+ Nazo sabato zangu walizitia unajisi sana,+ hivi kwamba nikaahidi kumwaga ghadhabu yangu juu yao nyikani, ili kuwaangamiza.+ 14 Lakini nilitenda kwa ajili ya jina langu mwenyewe ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa, ambao nilikuwa nimewatoa mbele ya macho yao.+ 15 Na mimi mwenyewe pia nikawainulia mkono wangu katika kiapo nyikani,+ kwamba sitawaingiza katika nchi niliyokuwa nimeitoa, yenye kutiririka maziwa na asali,+ (hiyo ni pambo la nchi zote,)+ 16 kwa sababu walikataa maamuzi yangu mwenyewe ya hukumu; nazo sheria zangu, hawakutembea katika hizo, nazo sabato zangu walizitia unajisi, kwa sababu moyo wao ulikuwa ukifuatilia sanamu zao za mavi.+

17 “ ‘ “Nalo jicho langu likaanza kuwasikitikia ili kunizuia nisiwaharibu,+ nami sikuwaangamiza nyikani. 18 Nami nikawaambia wana wao nyikani,+ ‘Msitembee katika masharti ya mababu zenu,+ wala msizishike hukumu zao,+ wala msijitie unajisi kwa sanamu zao za mavi.+ 19 Mimi ni Yehova Mungu wenu.+ Tembeeni katika sheria+ zangu mwenyewe, na kuyashika maamuzi yangu mwenyewe ya hukumu+ na kuyafanya.+ 20 Na zitakaseni sabato zangu mwenyewe,+ nazo zitakuwa ishara kati yangu na ninyi, ili mjue kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’+

21 “ ‘ “Na hao wana wakaanza kuniasi.+ Hawakutembea katika sheria zangu, nayo maamuzi yangu ya hukumu hawakuendelea kuyashika kwa kuyafanya, ambayo, kama mtu akiendelea kuyafanya, ataendelea pia kuishi kwa hayo.+ Sabato zangu walizitia unajisi.+ Kwa hiyo nikaahidi kumwaga ghadhabu yangu juu yao, ili kuitimiliza hasira yangu juu yao nyikani.+ 22 Nami nikaurudisha mkono wangu+ na kutenda kwa ajili ya jina langu mwenyewe, ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa, ambao nilikuwa nimewatoa mbele ya macho yao.+ 23 Pia, mimi mwenyewe niliwainulia mkono wangu katika kiapo nyikani,+ ili kuwatawanya kati ya mataifa na kuwatawanya kati ya nchi mbalimbali,+ 24 kwa sababu hawakufanya maamuzi yangu mwenyewe ya hukumu+ nao walizikataa sheria zangu mwenyewe+ nao wakazitia unajisi sabato zangu mwenyewe,+ nayo macho yao yalizifuata sanamu za mavi za mababu zao.+ 25 Na mimi mwenyewe pia niliwaacha wawe na masharti ambayo hayakuwa mazuri na maamuzi ya hukumu ambayo hawangeweza kuendelea kuishi kulingana nayo.+ 26 Nami nikawa nikiwaacha watiwe unajisi kwa zawadi zao walipomfanya kila mtoto aliyelifungua tumbo la uzazi apite katikati ya moto,+ ili niwafanye ukiwa, ili wapate kujua kwamba mimi ni Yehova.” ’+

27 “Kwa hiyo sema na nyumba ya Israeli, Ee mwana wa binadamu, nawe utawaambia hivi,+ ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Hata katika habari hii, mababu zenu walisema vibaya juu yangu, kwa kunitendea kwa ukosefu wa uaminifu.+ 28 Nami nikawaleta katika nchi+ ambayo nilikuwa nimeuinua mkono wangu katika kiapo kwamba nitawapa wao.+ Walipoona kila kilima kilichoinuka+ na kila mti wenye matawi mengi, ndipo wakaanza kutoa dhabihu+ zao huko na kutolea huko matoleo yao yenye kuudhi, na kutolea huko harufu zao za kutuliza+ na kumimina huko matoleo yao ya kinywaji.+ 29 Kwa hiyo nikawaambia, ‘Mahali pa juu mnapokuja panamaanisha nini, hivi kwamba paitwe jina lake Mahali pa Juu mpaka leo hii?’ ” ’+

30 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Je, ninyi mnajitia unajisi katika njia za mababu zenu,+ na je, katika kufuatilia machukizo yao mnaingilia kufanya uasherati?+ 31 Na katika kuinua zawadi zenu kwa kuwafanya wana wenu wapite katikati ya moto,+ je, mnajitia unajisi kwa ajili ya sanamu zenu zote za mavi mpaka leo hii?+ Wakati huohuo je, mtauliza neno juu yangu, Ee nyumba ya Israeli?” ’+

“ ‘Kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘Hamtauliza juu yangu.+ 32 Na kile kinachoingia katika roho yenu+ hakika hakitatukia,+ kwa kuwa mnasema: “Na tuwe kama mataifa, kama familia za nchi mbalimbali,+ katika kuhudumia miti na mawe.” ’ ”+

33 “ ‘Kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitatawala nikiwa mfalme juu yenu kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa+ na kwa ghadhabu iliyomwagwa.+ 34 Nami nitawatoa kati ya vikundi vya watu, nami nitawakusanya pamoja kutoka katika nchi ambako mmetawanywa kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa na kwa ghadhabu iliyomwagwa.+ 35 Nami nitawaleta katika nyika ya vikundi vya watu+ na kujiweka katika hukumu pamoja nanyi huko uso kwa uso.+

36 “ ‘Kama vile nilivyojiweka mwenyewe katika hukumu pamoja na mababu zenu katika nyika ya nchi ya Misri,+ ndivyo nitakavyojiweka mwenyewe katika hukumu pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 37 ‘Nami nitawafanya mpite chini ya fimbo+ na kuwaingiza katika kifungo cha agano.+ 38 Nami nitasafishia mbali kutoka kwenu wale wanaoasi na wale wanaonikosea,+ kwa maana kutoka katika nchi ya makao yao ya kigeni nitawaleta, lakini hawatakuja kwenye udongo wa Israeli;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+

39 “Nanyi, Ee nyumba ya Israeli, hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Nendeni kila mmoja wenu akazitumikie sanamu zake mwenyewe za mavi.+ Na baadaye ikiwa hamnisikilizi, basi hamtaendelea kulitia unajisi jina langu takatifu kwa zawadi zenu na kwa sanamu zenu za mavi.’+

40 “ ‘Kwa maana katika mlima wangu mtakatifu, katika mlima wa kilele cha Israeli,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘huko ndiko wao, nyumba yote ya Israeli ikiwa nzima, itanitumikia, katika nchi ile.+ Nitafurahishwa nao huko, na huko nitaitaka michango yenu na matunda ya kwanza ya matoleo yenu katika vitu vyenu vyote vilivyo vitakatifu.+ 41 Kwa sababu ya harufu ya kutuliza nitafurahishwa nanyi,+ nitakapowatoa kati ya vikundi vya watu nami hakika niwakusanye pamoja kutoka katika nchi ambazo mmetawanywa,+ nami nitatakaswa ndani yenu mbele ya macho ya mataifa.’+

42 “ ‘Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ nitakapowaleta kwenye udongo wa Israeli,+ katika nchi ambayo niliuinua mkono wangu katika kiapo kwamba nitawapa mababu zenu. 43 Nanyi hakika mtakumbuka huko njia zenu na matendo yenu yote+ ambayo mlijitia unajisi kwa hayo,+ nanyi hakika mtajichukia mbele ya nyuso zenu wenyewe kwa sababu ya mambo yenu yote mabaya ambayo mliyatenda.+ 44 Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova+ nitakapochukua hatua kuhusiana nanyi kwa ajili ya jina langu,+ si kulingana na njia zenu mbaya au kulingana na matendo yenu yenye uharibifu,+ Ee nyumba ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

45 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 46 “Mwana wa binadamu, elekeza uso+ wako upande wa eneo la kusini na udondoshe+ maneno kuelekea kusini, na utoe unabii kwa msitu wa uwanja wa kusini. 47 Nawe utauambia msitu wa kusini, ‘Sikia neno la Yehova. Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Tazama, ninawasha moto juu yako,+ nao utateketeza ndani yako kila mti ambao ungali mbichi na kila mti uliokauka.+ Mwali huo wa moto unaowaka hautazimwa,+ na kwa huo nyuso zote zitateketezwa kutoka kusini mpaka kaskazini.+ 48 Na watu wote wenye mwili wataona kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimeuwasha moto, ili usipate kuzimwa.” ’ ”+

49 Nami nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Wanasema juu yangu, ‘Je, yeye hatungi maneno ya kimethali?’ ”+

21 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako Yerusalemu na udondoshe+ maneno kuelekea mahali patakatifu,+ na kutoa unabii juu ya udongo wa Israeli.+ 3 Nawe utauambia udongo wa Israeli, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama, niko juu yako,+ nami nitauchomoa upanga wangu katika ala+ yake na kumkatilia mbali kutoka kwako mwadilifu na mwovu.+ 4 Ili kwa kweli nimkatilie mbali kutoka kwako mwadilifu na mwovu, kwa hiyo upanga wangu utatoka katika ala yake uwe juu ya wote wenye mwili kutoka kusini mpaka kaskazini.+ 5 Nao wote wenye mwili watalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimeuchomoa upanga wangu kutoka katika ala yake.+ Hautarudi tena kamwe.” ’+

6 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, ugua kwa viuno vyenye kutikisika.+ Unapaswa kuugua kwa uchungu mbele ya macho yao.+ 7 Na itakuwa kwamba, ikiwa watakuambia ‘Kwa nini unaugua?’+ utasema, ‘Kwa sababu ya habari fulani.’+ Kwa maana hakika itakuja,+ na kila moyo utayeyuka+ na mikono yote itaanguka chini na kila roho itahuzunika na magoti yote yatadondoka maji.+ ‘Tazama! Hakika itakuja+ na kutokezwa,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

8 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 9 “Mwana wa binadamu, toa unabii, nawe useme, ‘Yehova amesema hivi: “Sema, ‘Upanga, upanga!+ Umenolewa,+ nao umesuguliwa pia. 10 Umenolewa ili kupanga uchinjaji; umesuguliwa ili upate kumetameta.’ ” ’ ”+

“Au je, tufurahi?”+

“ ‘Je, huo unaikataa fimbo ya enzi+ ya mwana wangu mwenyewe,+ kama unavyoukataa kila mti?+

11 “ ‘Na mtu huutoa usuguliwe, ili kuutumia kwa mkono. Huo—upanga umenolewa, na huo—huo umesuguliwa, ili kuutia mkononi mwa muuaji.+

12 “ ‘Paaza kilio na kupiga mayowe,+ Ee mwana wa binadamu, kwa maana huo wenyewe umekuja kuwa juu ya watu wangu;+ huo uko juu ya wakuu wote wa Israeli.+ Wale waliotupwa kwenye upanga wamekuwa pamoja na watu wangu.+ Kwa hiyo piga paja kofi.+ 13 Kwa maana uchunguzi umefanywa,+ na vipi juu yake ikiwa unaikataa fimbo ya enzi pia?+ Haitaendelea kuwapo,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

14 “Nawe, Ee mwana wa binadamu—toa unabii, na upige kiganja cha mkono juu ya kiganja cha mkono,+ na ‘Upanga!’ unapaswa kurudiwa mara tatu.+ Huo ni upanga wa waliouawa. Ni upanga wa mtu mkuu aliyeuawa, unaowazunguka.+ 15 Ili moyo uyeyuke+ na ili kuzidisha wale walioshindwa katika malango yao yote,+ nitafanya uchinjaji kwa upanga. Ole, huo umefanywa ili umetemete, umesuguliwa kwa ajili ya uchinjaji!+ 16 Jionyeshe kuwa na makali;+ nenda upande wa kuume! Jipange mahali pako; nenda upande wa kushoto! Popote ambapo uso wako unaelekezwa! 17 Na mimi mwenyewe pia nitapiga kiganja changu kimoja cha mkono juu ya kile kiganja changu kingine cha mkono,+ nami nitaituliza+ ghadhabu+ yangu. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.”

18 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 19 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, jipangie njia mbili ili upanga wa mfalme wa Babiloni uingie.+ Zote mbili zinapaswa kutoka katika nchi moja, na uchonge mkono wa ishara;+ uuchonge penye kichwa cha njia ya kwenda jijini. 20 Unapaswa kuweka njia ili upanga uingie ndani ya Raba+ la wana wa Amoni, na moja ndani ya Yuda, ndani ya Yerusalemu lenye ngome.+ 21 Kwa maana mfalme wa Babiloni alisimama tuli katika makutano ya njia, penye kichwa cha zile njia mbili, ili kufanya uaguzi.+ Ametikisa mishale. Ameuliza habari kwa kutumia terafimu;+ ametazama ndani ya ini. 22 Katika mkono wake wa kuume uaguzi ulikuwa kwa ajili ya Yerusalemu, ili kuweka mitambo ya kubomolea,+ kufungua kinywa cha mtu kwa ajili ya uchinjaji, kupaaza sauti ya king’ora,+ kuweka mitambo ya kubomolea juu ya malango, kujenga boma la kuzingira, kujenga ukuta wa kuzingira.+ 23 Na hilo limekuwa kwao kama uaguzi usio wa kweli machoni pao+—wale ambao wameapishwa kwa viapo kwao;+ naye analikumbuka kosa,+ ili wao wakamatwe.+

24 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu mlifanya kosa lenu likumbukwe kupitia kufunuliwa kwa ukosaji wenu, ili dhambi zenu zionekane kulingana na matendo yenu yote, kwa sababu ya ninyi kukumbukwa+ mtakamatwa kwa mkono.’+

25 “Na wewe, Ee mwenye majeraha kiasi cha kufisha, mkuu+ mwovu wa Israeli,+ ambaye siku yake imekuja katika wakati wa kosa la mwisho,+ 26 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kiondoe kilemba, na kulivua taji.+ Hili halitakuwa tena kama lilivyo.+ Kiinue kilicho chini,+ na ukishushe kilicho juu.+ 27 Nitaliharibu, nitaliharibu, nitaliharibu.+ Nalo hili pia, hakika hili halitakuwa la mtu yeyote mpaka atakapokuja yule aliye na haki ya kisheria,+ nami nitampa yeye.’+

28 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, toa unabii, nawe useme, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi kuhusu wana wa Amoni na kuhusu shutuma kutoka kwao.’ Nawe useme, ‘Upanga, upanga umechomolewa kwa ajili ya uchinjaji, umesuguliwa ili kuufanya uangamize, ili kumetameta,+ 29 kwa sababu ya wao kutazama kwa ajili yako jambo lisilo halisi, kwa sababu ya kukufanyia uaguzi wa uwongo,+ ili kukuweka juu ya shingo za waliochinjwa, watu waovu ambao siku yao imekuja katika wakati wa kosa la mwisho.+ 30 Urudishe huo katika ala yake. Katika mahali ulipoumbwa wewe, katika nchi ya asili yako,+ nitakuhukumu. 31 Nami nitamwaga shutuma zangu juu yako. Kwa moto wa ghadhabu yangu nitapuliza juu yako,+ nami nitakutia mkononi mwa watu wasiotumia akili, mafundi wa uharibifu.+ 32 Wewe utakuwa kuni kwa ajili ya moto.+ Damu yako mwenyewe itakuwa katikati ya nchi. Hutakumbukwa, kwa maana mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’ ”+

22 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, je, utahukumu,+ je, utahukumu lile jiji lenye hatia ya damu+ na kulifanya lijue machukizo yake yote?+ 3 Nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Ee jiji, linalomwaga damu+ katikati yake mpaka wakati wake ufike,+ na ambalo limefanya sanamu za mavi ndani yake ili kuwa lisilo safi,+ 4 umekuwa na hatia kwa damu yako ambayo umemwaga,+ na umekuwa usiye safi kwa sanamu zako za mavi ambazo umefanya.+ Nawe unazileta siku zako karibu, nawe utaifikia miaka yako. Ndiyo sababu lazima nikufanye kuwa kitu cha kushutumiwa kwa mataifa na cha kudhihakiwa katika nchi zote.+ 5 Nchi zilizo karibu nawe na zile zilizo mbali nawe zitakudhihaki, wewe uliye na jina lisilo safi, uliyejaa mvurugo.+ 6 Tazama! Wakuu+ wa Israeli wamekuwa ndani yako, kila mmoja akiwa amejitoa kwa mkono wake ili kumwaga damu.+ 7 Wamemtendea dharau baba na mama ndani yako.+ Wamemtendea mkaaji mgeni ndani yako kwa upunjaji.+ Wamewatendea vibaya mvulana asiye na baba na mjane ndani yako.” ’ ”+

8 “ ‘Umepadharau mahali pangu patakatifu, nazo sabato zangu umezitia unajisi.+ 9 Wachongezi wanaofanya hivyo waziwazi wamo ndani yako, kwa kusudi la kumwaga damu;+ nao wamekula juu ya milima ndani yako.+ Wameendeleza mwenendo mpotovu ndani yako.+ 10 Wameufunua uchi wa baba ndani yako;+ wamemfedhehesha mwanamke asiye safi katika hedhi yake ndani yako.+ 11 Na mwanamume amefanya chukizo pamoja na mke wa mwenzake, na mwanamume amemnajisi+ binti-mkwe wake mwenyewe kwa mwenendo mpotovu;+ na ndani yako mwanamume amemfedhehesha dada yake, binti ya baba yake mwenyewe.+ 12 Wamechukua rushwa ndani yako kwa kusudi la kumwaga damu.+ Umechukua faida na riba,+ nawe kwa ujeuri unaendelea kupata mapato+ ya wenzako kwa upunjaji,+ nawe umenisahau mimi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

13 “ ‘Na, tazama! Nimeupiga mkono wangu+ kwa sababu ya pato lisilo la haki ambalo umepata,+ na kwa sababu ya matendo yako ya kumwaga damu yaliyo katikati yako.+ 14 Je, moyo wako utaendelea kuvumilia+ au mikono yako kukupa nguvu katika siku ambayo nitatenda kukuelekea wewe?+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nitatenda.+ 15 Nami nitakutawanya wewe kati ya mataifa na kukutawanya kati ya nchi+ hizo, nami nitauharibu uchafu wako kutoka ndani yako.+ 16 Nawe hakika utatiwa unajisi ndani yako mwenyewe mbele ya macho ya mataifa, nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”+

17 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 18 “Mwana wa binadamu, kwangu mimi wale wa nyumba ya Israeli wamekuwa kama takataka.+ Wote ni shaba na bati na chuma na risasi katikati ya tanuru. Wamekuwa takataka nyingi, ile ya fedha.+

19 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu ninyi nyote mmekuwa kama takataka+ nyingi, kwa hiyo, tazama, ninawakusanya ninyi pamoja katikati ya Yerusalemu.+ 20 Kama kukusanya fedha na shaba na chuma+ na risasi na bati katikati ya tanuru, ili kupuliza+ juu yake kwa moto kusudi ziyeyuke,+ ndivyo nitakavyowakusanya wao pamoja katika hasira yangu na katika ghadhabu yangu, nami nitawapuliza na kuwayeyusha ninyi. 21 Nami nitawakusanya pamoja na kupuliza juu yenu kwa moto wa ghadhabu yangu,+ nanyi mtayeyushwa katikati yake.+ 22 Kama kuyeyushwa kwa fedha katikati ya tanuru, ndivyo ninyi mtakavyoyeyushwa katikati yake; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimemwaga ghadhabu yangu juu yenu.’ ”+

23 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 24 “Mwana wa binadamu, iambie hivi, ‘Wewe ni nchi isiyosafishwa, ambayo hainyeshewi wakati wa siku ya shutuma.+ 25 Katikati yake kuna hila ya manabii wake,+ kama simba anayenguruma, anayerarua mawindo.+ Kwa kweli wanairarua nafsi.+ Wanaendelea kuchukua hazina na vitu vyenye thamani.+ Wamewazidisha wajane wake katikati yake.+ 26 Makuhani wake wenyewe wameitendea jeuri sheria yangu,+ nao wanaendelea kutia unajisi mahali pangu patakatifu.+ Hawatofautishi kati ya kitu kitakatifu na cha kawaida,+ nao hawajafanya chochote kijulikane kati ya kitu kisicho safi na kilicho safi,+ nao wameyaficha macho+ yao yasione sabato zangu, nami ninatiwa unajisi katikati yao.+ 27 Wakuu wake walio katikati yake ni kama mbwa-mwitu wanaorarua mawindo katika kumwaga damu,+ katika kuangamiza nafsi kusudi wapate pato lisilo la haki.+ 28 Nao manabii wake wamewapigia lipu kwa kutumia chokaa,+ wakiona maono yasiyo halisi+ na kuagua uwongo+ kwa ajili yao, na kusema: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi,” wakati ambapo Yehova mwenyewe hajasema. 29 Watu wa nchi wenyewe wameendesha mbinu ya kupunja+ nao wamenyakua katika unyang’anyi,+ nao wamemtendea vibaya+ anayeteseka na aliye maskini, na kumpunja bila haki mkaaji mgeni.’+

30 “ ‘Nami nikaendelea kumtafuta mtu kati yao ambaye angekuwa akiurekebisha ukuta wa mawe+ na kusimama katika pengo+ mbele yangu kwa ajili ya nchi hiyo, ili mimi nisiiangamize;+ nami sikumpata yeyote. 31 Kwa hiyo nitamwaga shutuma+ zangu juu yao. Nitawaangamiza wao kwa moto wa ghadhabu yangu.+ Nitaileta njia yao juu ya kichwa chao wenyewe,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

23 Na neno la Yehova likanijia,+ na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, kulikuwa na wanawake wawili, binti za mama mmoja.+ 3 Nao wakaanza kufanya ukahaba katika Misri.+ Wakati wa ujana wao walifanya ukahaba.+ Huko maziwa yao yalifinywa-finywa,+ na huko walivibana vifua vya ubikira wao. 4 Nayo majina yao yalikuwa Ohola, yule mkubwa na Oholiba dada yake, nao wakaja kuwa wangu+ na kuanza kuzaa wana na mabinti.+ Nayo majina yao, Ohola ni Samaria,+ na Oholiba ni Yerusalemu.+

5 “Naye Ohola akaanza kufanya ukahaba,+ alipokuwa chini yangu, na kuendelea kuwa na uchu kuwaelekea wale wanaompenda kwa tamaa,+ kuwaelekea Waashuru,+ waliokuwa karibu, 6 magavana waliovaa mavazi ya bluu, na watawala-wasaidizi—wote wakiwa vijana wenye kupendeza, askari wenye kupanda farasi. 7 Naye akaendelea kuwagawia ukahaba wake, wote wakiwa wana bora wa Ashuru; na wale wote ambao alikuwa na uchu kuwaelekea—pamoja na sanamu zao za mavi—alijitia unajisi.+ 8 Na ukahaba wake uliotoka Misri hakuuacha, kwa maana walikuwa wamelala naye wakati wa ujana wake, nao ndio waliokuwa wamebana vifua vya ubikira wake nao waliendelea kumimina juu yake uasherati wao.+ 9 Kwa hiyo nilimtia mkononi mwa wale wanaompenda kwa tamaa,+ mkononi mwa wana wa Ashuru, ambao alikuwa na uchu kuwaelekea.+ 10 Hao ndio walioufunua uchi wake.+ Wakawachukua wanawe na binti zake,+ naye wakamuua kwa upanga. Akaja kuwa na sifa mbaya kwa wanawake, nao wakatekeleza matendo ya hukumu juu yake.

11 “Dada yake Oholiba alipoona jambo hilo,+ basi akatimiza tamaa yake ya kimwili kwa uharibifu mkubwa kuliko yeye, na ukahaba wake mwingi kuliko uasherati wa dada yake.+ 12 Akawa na uchu kuwaelekea wana wa Ashuru,+ magavana na watawala-wasaidizi waliokuwa karibu, waliovaa mavazi yenye kupendeza, askari wenye kupanda farasi—wote wakiwa vijana wenye kupendeza.+ 13 Nami nikaona jambo hilo, kwa sababu alikuwa amejitia unajisi, wote wawili walikuwa na njia moja.+ 14 Naye akazidi kuongezea matendo yake ya ukahaba alipowaona wanaume waliochongwa ukutani,+ sanamu+ za Wakaldayo zilizochongwa na kupakwa rangi nyekundu,+ 15 zilizofungwa mishipi+ katika viuno vyao, zikiwa na vilemba vinavyoning’inia katika vichwa vyao, wote wakiwa na sura ya mashujaa wa vita, wanaofanana na wana wa Babiloni, wakiwa ni wazaliwa wa nchi ya Wakaldayo. 16 Naye akaanza kuwa na uchu kuwaelekea alipoona kwa macho+ yake, naye akatuma wajumbe kwao katika Ukaldayo.+ 17 Nao wana wa Babiloni wakaendelea kumjia, kwenye kitanda cha wonyesho wa upendo, na kumtia unajisi kwa uasherati wao;+ nao wakaendelea kumtia unajisi, nayo nafsi yake ikaanza kugeukia mbali nao kwa kuchukizwa.

18 “Naye akaendelea kufunua matendo yake ya ukahaba na kufunua uchi wake,+ hivi kwamba nafsi yangu ikageukia mbali kwa kuchukizwa isiandamane naye, kama vile nafsi yangu ilivyogeukia mbali kwa kuchukizwa isiandamane na dada yake.+ 19 naye akaendelea kuzidisha matendo yake ya ukahaba+ kufikia hatua ya kurudisha kumbukumbu ya siku za ujana wake,+ wakati ambapo alifanya ukahaba katika nchi ya Misri.+ 20 Naye akaendelea kuwa na uchu kama masuria wa wale ambao kiungo chao ni kama kiungo cha punda-dume na ambao kiungo chao cha uzazi ni kama kiungo cha uzazi cha farasi-dume.+ 21 Nawe ukaendelea kuukazia fikira mwenendo mpotovu wa ujana wako kwa kufinywa kwa vifua vyako kutoka Misri+ na kuendelea, kwa ajili ya maziwa ya ujana wako.+

22 “Kwa hiyo, Ee Oholiba, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninawaamsha juu yako wale wanaokupenda kwa tamaa,+ wale ambao nafsi yako imegeukia mbali kutoka kwao ikiwa imechukizwa, nami nitawaleta juu yako pande zote,+ 23 wana wa Babiloni+ na Wakaldayo+ wote, Pekodi+ na Shoa na Koa, wana wote wa Ashuru pamoja nao, vijana wenye kupendeza, magavana na watawala-wasaidizi wote, mashujaa wa vita na walioitwa, wote wakiwa wamepanda farasi. 24 Nao lazima wataingia ndani juu yako pamoja na kelele za magari ya vita na za magurudumu,+ na pamoja na kutaniko la vikundi vya watu, pamoja na ngao kubwa na ngao ndogo na kofia. Watajipanga juu yako pande zote, nami nitawapa hukumu, nao watakuhukumu wewe kwa hukumu zao.+ 25 Nami nitaonyesha ukali wangu juu yako,+ nao watakuchukulia hatua katika ghadhabu.+ Wataondoa pua yako na masikio yako, na sehemu yako inayobaki itaanguka kwa upanga. Wao wenyewe watawachukua wana wako na binti zako,+ na sehemu yako inayobaki itateketezwa kwa moto.+ 26 Nao hakika watakuvua mavazi+ yako na kuvichukua vyombo vyako vinavyopendeza.+ 27 Nami hakika nitaufanya mwenendo wako mpotovu ukome kutoka kwako,+ na ukahaba wako kutoka nchi ya Misri;+ nawe hutainua macho yako kuwaelekea, nawe hutakumbuka Misri tena.’

28 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninakutia mkononi mwa wale ambao umewachukia, mkononi mwa wale ambao kutoka kwao nafsi yako imegeukia mbali ikiwa imechukizwa.+ 29 Nao watakuchukulia hatua kwa chuki na kuchukua mali zako zote ulizofanyia kazi na kukuacha ukiwa uchi na tupu;+ nao utupu wa matendo yako ya uasherati na mwenendo wako mpotovu na matendo yako ya ukahaba utafunuliwa.+ 30 Utafanyiwa mambo hayo kwa sababu uliyafuata mataifa kama kahaba,+ kwa sababu ulijitia unajisi kwa sanamu zao za mavi.+ 31 Umetembea katika njia ya dada yako;+ nami nitalazimika kukitia kikombe chake mkononi mwako.’+

32 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kikombe cha dada yako utakinywa, kile chenye kina na kipana.+ Utakuwa kitu cha kuchekwa na kudhihakiwa, kikombe kilicho na mengi.+ 33 Utajaa ulevi na huzuni, kwa kikombe cha mshangao na cha ukiwa, kikombe cha dada yako Samaria. 34 Nawe utalazimika kukinywa na kukimaliza,+ na vigae vyake utavitafuna, na maziwa yako utayang’oa.+ “Kwa maana mimi mwenyewe nimesema,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’

35 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu umenisahau+ nawe ulinitupa nyuma ya mgongo wako,+ basi wewe mwenyewe pia chukua mwenendo wako mpotovu na matendo yako ya ukahaba.’ ”

36 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, je, utawahukumu+ Ohola na Oholiba+ na kuwaambia machukizo yao?+ 37 Kwa maana wamefanya uzinzi+ na damu imo mikononi mwao,+ nao wamefanya uzinzi na sanamu zao za mavi.+ Na, mbali na hayo, waliwafanya wana wao waliokuwa wamenizalia wapite motoni kama chakula kwao.+ 38 Tena, hili ndilo wamenifanyia: Wamepatia unajisi+ patakatifu+ pangu katika siku hiyo, nazo sabato zangu wamezitia unajisi.+ 39 Nao walipokuwa wamewachinja wana wao kwa ajili ya sanamu zao za mavi+ waliingia ndani ya patakatifu pangu katika siku hiyo ili kupatia unajisi,+ na, tazama! hivyo ndivyo wamefanya katikati ya nyumba yangu.+ 40 Tena, walipoanza kuwaita wanaume kutoka mbali, ambao walitumiwa mjumbe,+ kisha, tazama! wao wakaja,+ kwa ajili ya yule ambaye ulikuwa umejiosha+ kwa ajili yake, ukapaka rangi macho+ yako na kujipamba kwa mapambo.+ 41 Nawe ukaketi juu ya kitanda chenye utukufu,+ pamoja na meza iliyowekwa kwa utaratibu mbele yake,+ nawe ukaweka juu yake uvumba+ wangu na mafuta+ yangu. 42 Na sauti ya umati uliostarehe ilikuwa ndani yake,+ na kwa wanaume kutoka katika umati wa wanadamu kulikuwa na walevi+ wakiletwa kutoka nyikani, nao wakaweka vikuku mikononi mwa wanawake na mataji yenye kupendeza juu ya vichwa vyao.+

43 “Ndipo nikasema kuhusu yule ambaye uzinzi+ umemfanya achakae, ‘Sasa ataendelea kufanya ukahaba wake, naam, yeye mwenyewe.’+ 44 Nao wakaendelea kuingia kwake, kama vile mtu anavyokuja kwa mwanamke kahaba; hivyo ndivyo walivyoingia kwa Ohola na kwa Oholiba wakiwa wanawake wa mwenendo mpotovu.+ 45 Lakini watu waadilifu,+ hao ndio watakaomhukumu kwa hukumu ya wanawake wazinzi+ na kwa hukumu ya wanawake wanaomwaga damu;+ kwa maana wao ni wanawake wazinzi, na damu imo mikononi mwao.+

46 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kutaniko litaletwa juu yao+ nao watafanywa kuwa kitu chenye kutisha na kitu cha kuporwa.+ 47 Nalo kutaniko litawapiga kwa mawe,+ nao watakatwa kwa panga zao. Watawaua wana wao na binti zao,+ nao wataziteketeza nyumba zao kwa moto.+ 48 Nami hakika nitafanya mwenendo mpotovu+ ukome nchini,+ nao wanawake wote watalazimika kukubali kurekebishwa, hivi kwamba wasifanye kulingana na mwenendo wenu mpotovu.+ 49 Nao watauleta mwenendo wenu mpotovu juu yenu,+ nanyi mtazichukua dhambi za sanamu zenu za mavi; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’ ”+

24 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia katika mwaka wa tisa, katika mwezi wa kumi, siku ya kumi ya mwezi huo, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, jiandikie jina la siku hii, siku hii ya leo. Mfalme wa Babiloni amejitupa juu ya Yerusalemu siku hii ya leo.+ 3 Na utunge neno la kimethali kuhusu nyumba hii yenye kuasi,+ nawe utasema kuwahusu,

“ ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tia motoni chungu cha kupikia chenye mdomo mpana; kitie motoni, na pia umimine maji ndani yake.+ 4 Kusanya vipande ndani yake,+ kila kipande chema, paja na bega; kijaze mifupa bora zaidi. 5 Kondoo bora zaidi na achukuliwe,+ na pia urundike kuni zikiwa katika mviringo chini yake. Tokosa vipande vyake, pia upike mifupa yake katikati yake.” ’ ”+

6 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Ole wake jiji lenye matendo ya kumwaga damu,+ kile chungu cha kupikia chenye mdomo mpana, ambacho kutu yake iko ndani yake, na ambacho kutu yake haikukitoka! Kipande kwa kipande chake, kitoe nje;+ kura yoyote isipigwe juu yake.+ 7 Kwa maana damu yake imekuwa katikati yake kabisa.+ Aliiweka juu ya uso ulio wazi na wenye kung’aa, wa mwamba. Hakuimimina chini, ili kuifunika kwa mavumbi.+ 8 Ili kuleta ghadhabu kwa ajili ya kulipiza kisasi,+ nimeiweka damu yake juu ya uso ulio wazi na wenye kung’aa, wa mwamba, ili isipate kufunikwa.’+

9 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Ole wake jiji lenye matendo ya kumwaga damu!+ Mimi mwenyewe pia nitalifanya fungu hilo liwe kubwa.+ 10 Zifanye kuni ziwe nyingi. Uwashe moto. Itokose nyama kabisa. Na uumwage mchuzi mzito, na uiache mifupa iwe moto sana. 11 Kisimamishe juu ya makaa yake ili kiwe moto; na shaba yake itakuwa moto, nao uchafu wake utayeyushwa katikati yake.+ Kutu yake na iteketee.+ 12 Taabu! Zimemfanya mtu achoke, lakini kiasi kikubwa cha kutu yake hakitoki kwake.+ Kutu yake na itiwe motoni!’

13 “ ‘Kulikuwa na mwenendo mpotovu katika uchafu wako.+ Kwa sababu hiyo nililazimika kukusafisha, lakini hukuwa safi kutokana na uchafu wako.+ Hutakuwa safi tena mpaka nitakapoituliza ghadhabu yangu kwako.+ 14 Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.+ Lazima ije,+ nami nitatenda. Sitapuuza,+ wala sitasikitika + wala kujuta.+ Kulingana na njia zako na kulingana na matendo yako hakika watakuhukumu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

15 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, kusema: 16 “Mwana wa binadamu, tazama, ninaondolea mbali kutoka kwako kitu chenye kutamanika+ machoni pako kwa pigo moja,+ nawe usijipige kifua, wala usilie, wala machozi yako yasitoke.+ 17 Ugua pasipo maneno. Usiwaombolezee hata kidogo waliokufa.+ Jifunge kitambaa chako cha kichwani,+ na uvae viatu vyako miguuni+ pako. Nawe usifunike masharubu,+ wala usile mkate wa wanadamu.”+

18 Nami nikasema na watu asubuhi, naye mke wangu mwishowe akafa jioni. Kwa hiyo nilifanya asubuhi vile ambavyo nilikuwa nimeamriwa. 19 Nao watu wakaendelea kuniambia: “Je, hutatuambia ni jinsi gani mambo haya yanatuhusu, mambo unayoyafanya?”+ 20 Ndipo nikawaambia: “Neno la Yehova limenijia, na kusema, 21 ‘Iambie nyumba ya Israeli: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama, mimi ninapatia unajisi patakatifu pangu,+ fahari ya nguvu zenu,+ kitu chenye kutamanika machoni penu+ na kitu ambacho nafsi yenu hukihurumia, nao wana wenu na binti zenu ambao mmewaacha nyuma—wataanguka kwa upanga.+ 22 Nanyi mtalazimika kufanya kama nilivyofanya. Hamtafunika masharubu,+ wala kula mkate wa wanadamu.+ 23 Nacho kitambaa chenu cha kichwa kitakuwa vichwani mwenu, navyo viatu vyenu vitakuwa miguuni penu. Hamtajipiga-piga wala hamtalia,+ nanyi mtalazimika kuoza katika makosa yenu,+ nanyi hakika mtaugua kila mtu pamoja na mwenzake.+ 24 Na Ezekieli amekuwa ishara kwa ajili yenu.+ Mtatenda kulingana na yote ambayo ametenda. Litakapokuja jambo hili,+ ninyi pia mtalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’ ” ’ ”+

25 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, je, haitakuwa katika siku ambayo nitachukulia mbali ngome zao, kile kitu kizuri cha furaha yao, kitu chenye kutamanika machoni pao+ na tamaa ya nafsi yao, wana wao na binti zao,+ kwamba 26 katika siku hiyo mwenye kuponyoka atakujia ili kuyafanya masikio yasikie jambo hili?+ 27 Katika siku hiyo kinywa chako kitafunguliwa kuelekea aliyeponyoka,+ nawe utasema nawe hutakuwa bubu tena;+ nawe hakika utakuwa ishara kwao,+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”+

25 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako kwa wana wa Amoni na kutoa unabii juu yao.+ 3 Nawe utasema hivi kuwahusu wana wa Amoni, ‘Sikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Kwa sababu umesema Aha! Juu ya patakatifu pangu, kwa sababu pametiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli, kwa sababu imefanywa kuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda, kwa sababu wameenda uhamishoni,+ 4 kwa hiyo tazama, ninakutia wewe mkononi mwa Watu wa Mashariki uwe kitu cha kumilikiwa,+ nao wataweka kambi zao zenye kuta ndani yako nao hakika wataweka ndani yako maskani zao. Wao wenyewe watakula matunda yako, nao wenyewe watakunywa maziwa yako.+ 5 Nami nitafanya Raba+ pawe kiwanja cha malisho cha ngamia na wana wa Amoni wawe mahali pa kupumzika kwa ajili ya kundi;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” ’ ”+

6 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu ulipiga makofi+ na kupiga vishindo kwa miguu, nawe uliendelea kushangilia kwa dhihaka zote ulizokuwa nazo katika nafsi yako juu ya nchi ya Israeli,+ 7 kwa hiyo tazama mimi hapa; nimekunyooshea mkono wangu,+ nami nitakutoa uporwe na mataifa; nami nitakukatilia mbali kutoka katikati ya vikundi vya watu na kukuharibu kutoka katika nchi hizi.+ Nitakuangamiza wewe,+ nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’

8 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu Moabu+ na Seiri+ wamesema: “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama mataifa mengine yote,”+ 9 kwa hiyo tazama, ninafungua mteremko wa Moabu katika majiji, katika majiji yake hadi kwenye mipaka yake, pambo la nchi hiyo, Beth-yeshimothi,+ Baal-meoni,+ Kiriathaimu,+ 10 kwa Watu wa Mashariki,+ pamoja na wana wa Amoni;+ nami nitaifanya kuwa kitu cha kumilikiwa, ili isikumbukwe,+ yaani, wana wa Amoni, katikati ya mataifa. 11 Nami nitafanya matendo ya hukumu katika Moabu;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+

12 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu Edomu ametenda kwa kulipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda nao waliendelea kufanya kosa kwa kadiri kubwa na kujilipizia kisasi juu yao,+ 13 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Pia nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu+ na kukatilia mbali kutoka kwake mwanadamu na mnyama wa kufugwa,+ nami nitapafanya kuwa ukiwa kutoka Temani,+ mpaka Dedani.+ Wataanguka kwa upanga. 14 ‘Nami nitaleta kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli;+ nao watafanya katika Edomu kulingana na hasira yangu na kulingana na ghadhabu yangu; nao watalazimika kujua kisasi changu ni nini,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” ’

15 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu Wafilisti wametenda kwa kulipiza kisasi+ nao waliendelea kujilipizia kisasi wenyewe wakiwa na kisasi chenye dhihaka katika nafsi, ili kusababisha uharibifu,+ wakiwa na uadui unaodumu mpaka wakati usio na kipimo,+ 16 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninaunyoosha mkono wangu juu ya Wafilisti,+ nami nitawakatilia mbali Wakerethi+ na kuiangamiza pwani ya bahari inayobaki.+ 17 Nami nitafanya katikati yao matendo makubwa ya kisasi, kwa makaripio yenye ghadhabu;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoleta kisasi changu juu yao.” ’ ”+

26 Na ikawa kwamba katika mwaka wa kumi na moja, katika siku ya kwanza ya mwezi, neno la Yehova lilinijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, kwa sababu Tiro+ amesema juu ya Yerusalemu,+ ‘Aha! Amevunjwa,+ milango ya vikundi vya watu!+ Hakika mwelekeo wa mambo utageuka uwe kwangu. Nitajazwa—ameharibiwa,’+ 3 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama niko juu yako, Ee Tiro, nami nitainua mataifa mengi juu yako,+ kama vile bahari inavyoinua mawimbi yake.+ 4 Na hakika wao wataziharibu kuta za Tiro+ na kuibomoa minara yake,+ nami nitakwangua mavumbi yake kutoka kwake na kumfanya kuwa uso ulio wazi na wenye kung’aa wa mwamba. 5 Atakuwa uwanja wa kukaushia nyavu za kukokota+ katikati ya bahari.’+

“ ‘Kwa maana mimi mwenyewe nimesema,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘naye lazima atakuwa kitu cha kuporwa na mataifa. 6 Na miji yake ya kandokando iliyoko shambani—watauawa kwa upanga, na watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+

7 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama, juu ya Tiro ninamleta Nebukadreza mfalme wa Babiloni kutoka kaskazini,+ mfalme wa wafalme,+ pamoja na farasi+ na magari ya vita+ na askari wapanda-farasi na kutaniko,+ naam, umati wa watu. 8 Ataua, naam, kwa upanga, miji yako ya kandokando iliyoko shambani, naye atajenga ukuta wa kukuzingira na kujenga juu yako boma la kuzingira+ na kuinua juu yako ngao kubwa; 9 na shambulio la mtambo wake wa kushambulia atalielekeza juu ya kuta zako, naye ataibomoa minara yako, kwa panga zake. 10 Kwa sababu ya umati unaosukasuka wa farasi zake mavumbi yao yatakufunika.+ Kwa sababu ya sauti ya askari wapanda-farasi na gurudumu na gari la vita kuta zako zitatikisika, atakapoingia katika malango yako, kama ilivyo nyakati za kuingia katika jiji lililofunguliwa kwa matundu yaliyotobolewa. 11 Kwa kwato za farasi zake atakanyaga-kanyaga barabara zako zote.+ Watu wako atawaua, naam, kwa upanga, nazo nguzo zako zenye nguvu zitaanguka chini. 12 Nao hakika watateka nyara mali+ zako na kupora mali zako za mauzo,+ na kubomoa kuta zako, nazo nyumba zako zenye kutamanika watazibomoa. Nao wataweka mawe yako na mbao zako na mavumbi yako katikati ya maji.’

13 “‘Nami nitafanya kelele za kuimba kwako zikome,+ na sauti ya vinubi vyako haitasikiwa tena.+ 14 Nami nitakufanya kuwa uso ulio wazi na wenye kung’aa, wa mwamba.+ Utakuwa uwanja wa kukaushia nyavu za kukokota.+ Wewe hutajengwa tena kamwe; kwa maana mimi mwenyewe, Yehova, nimesema,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+

15 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amemwambia Tiro hivi, ‘Inapotokea sauti ya kuanguka kwako, wakati ambapo aliyetiwa majeraha ya kufisha atakapougua, wakati ambapo kutakuwapo mauaji yenye machinjo katikati yako, je, visiwa havitatikisika?+ 16 Nao wakuu wote wa bahari hakika watashuka kutoka katika viti vyao vya ufalme+ na kuvua makoti yao yasiyo na mikono, nao watayavua mavazi yao wenyewe yenye mapambo. Watavaa mavazi ya kutetemeka. Wataketi chini,+ nao hakika watatetemeka kila pindi+ na kukukazia macho kwa mshangao. 17 Nao wataimba wimbo wa huzuni juu yako+ na kukuambia:

“ ‘ “Lo! Jinsi umeangamia, wewe uliyekuwa ukikaliwa kutoka baharini,+ wewe jiji lililosifiwa, uliyekuwa mwenye nguvu katika bahari,+ yeye na wale wanaokaa ndani yake, wale waliowatia wakaaji wote wa dunia woga wao! 18 Sasa visiwa vitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako. Na visiwa vilivyomo baharini vitaingiwa na wasiwasi kwa sababu ya kuondoka kwako.” ’+

19 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Nitakapokufanya wewe uwe jiji lililoharibiwa, kama majiji ambayo kwa kweli hayakaliwi, nitakapoleta juu yako kilindi cha maji, na maji mengi yawe yamekufunika,+ 20 pia nitakushusha chini pamoja na wale wanaoshuka kuingia shimoni kwa watu wa zamani za kale,+ nami nitakufanya ukae katika nchi ya chini zaidi,+ kama mahali palipoharibiwa kwa muda mrefu, pamoja na wale wanaoshuka kuingia shimoni,+ ili usipate kukaliwa; nami nitaweka pambo katika nchi ya wale walio hai.+

21 “ ‘Nitakufanya kuwa vitisho vya ghafula,+ nawe hutakuwapo; nawe utatafutwa,+ lakini hutapatikana tena kamwe mpaka wakati usio na kipimo,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

27 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, mfanyie Tiro wimbo wa huzuni,+ 3 nawe utamwambia Tiro,

“ ‘Wewe unayekaa katika malango ya bahari,+ mwanamke mfanya-biashara wa vikundi vya watu wa visiwa vingi,+ Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Ee Tiro, wewe mwenyewe umesema, ‘Mimi ni mkamilifu wa uzuri.’+ 4 Maeneo yako yamo katika moyo wa bahari.+ Wajenzi wako mwenyewe wameukamilisha uzuri wako.+ 5 Walikutengenezea kutokana na miberoshi kutoka Seniri+ mbao zote. Waliuchukua mwerezi kutoka Lebanoni+ na kufanya mlingoti juu yako. 6 Waliyafanya makasia yako kutokana na miti mikubwa sana ya Bashani. Waliifanya omo yako kwa pembe za tembo katika mbao za mvinje, kutoka katika visiwa vya Kitimu.+ 7 Mtando wako wa nguo ulikuwa kitani cha rangi mbalimbali kutoka Misri,+ ili kuwa tanga yako. Uzi wa bluu+ na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau+ kutoka katika visiwa vya Elisha+ ndivyo vilivyofunika sitaha yako.

8 “ ‘ “Wakaaji wa Sidoni+ na Arvadi+ wenyewe wakawa wapiga-makasia wako. Watu wako wenye ustadi,+ Ee Tiro, walikuwa ndani yako; walikuwa mabaharia+ wako. 9 Hata wanaume wazee wa Gebali+ na watu wake wenye ustadi walikuwa ndani yako wakiwa wenye kutia kalafati mipasuko+ yako. Meli zote za baharini na wanamaji wake wenyewe walikuwa ndani yako, ili kufanya biashara. 10 Waajemi+ na Waludimu+ na watu wa Putu+—walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita. Walitundika ngao na kofia kwako.+ Wao ndio walioisababisha fahari yako. 11 Wana wa Arvadi,+ hata jeshi lako, walikuwa juu ya kuta zako pande zote, na watu mashujaa ndio waliokuwa katika minara yako mwenyewe. Walizitundika ngao zao za mviringo juu ya kuta zako kuzunguka pande zote.+ Wao wenyewe waliukamilisha uzuri wako.

12 “ ‘ “Tarshishi+ alikuwa mwanabiashara wako kwa sababu ya wingi wa namna zote za vitu vyenye thamani.+ Kwa ajili ya fedha yake, chuma, bati na risasi, maghala yake yalitolewa.+ 13 Yavani,+ Tubali+ na Mesheki+ walikuwa wafanya-biashara wako. Vitu vyako vya biashara vilitolewa kwa ajili ya nafsi za wanadamu+ na vitu vya shaba. 14 Kutoka katika nyumba ya Togarma+ kulikuwa na farasi na farasi wa vita na nyumbu, ambao kwa ajili yao maghala yako yalitolewa. 15 Wana wa Dedani+ walikuwa wafanya-biashara wako; visiwa vingi vilikuwa wanabiashara uliowaajiri; wamekulipa pembe za tembo+ na mpingo kama zawadi. 16 Edomu alikuwa mwanabiashara wako kwa sababu ya wingi wa kazi zako. Maghala yako yalitolewa kwa ajili ya feruzi,+ sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na vitambaa vya rangi mbalimbali na kitambaa bora na marijani na zabarijadi.

17 “ ‘ “Yuda na nchi ya Israeli walikuwa wafanya-biashara wako. Vitu vyako vya biashara vilitolewa+ kwa ajili ya ngano+ ya Minithi+ na vyakula vya pekee na asali+ na mafuta na zeri.+

18 “ ‘ “Damasko+ alikuwa mwanabiashara wako katika wingi wa kazi zako, kwa sababu ya wingi wa vitu vyako vyote vyenye thamani, pamoja na divai+ ya Helboni na sufu ya rangi ya kijivu. 19 Vedani na Yavani kutoka Uzali—walitoa kwa ajili ya maghala yako. Chuma katika kazi ya kufua madini, kida na kane+—vilikuwa kwa ajili ya vitu vyako vya biashara. 20 Dedani+ alikuwa mfanya-biashara wako katika mavazi ya vitambaa vilivyofumwa vya kupandia farasi. 21 Waarabu+ na wakuu wote wa Kedari+ wenyewe walikuwa wanabiashara uliowaajiri. Katika wana-kondoo na kondoo-dume na mbuzi-dume+—walikuwa wanabiashara katika hao. 22 Wafanya-biashara wa Sheba+ na Raama+ wenyewe walikuwa wafanya-biashara wako; kwa ajili ya namna zote za manukato yaliyo bora zaidi na kwa ajili ya namna zote za mawe ya thamani na dhahabu, maghala yako yalitolewa.+ 23 Harani+ na Kane na Edeni,+ wafanya-biashara wa Sheba,+ Asihuru+ na Kilmadi walikuwa wafanya-biashara wako. 24 Walikuwa wafanya-biashara wako katika mavazi ya fahari, katika mitandio ya kitambaa cha bluu na kitambaa cha rangi mbalimbali na katika mazulia ya nguo za rangi mbili, katika kamba zilizosokotwa na kufanywa kuwa thabiti, katika kituo chako cha kufanyia biashara.

25 “ ‘ “Meli za Tarshishi+ zilikuwa misafara yako ya vitu vyako vya biashara, hivi kwamba unajazwa na kuwa na utukufu sana katika moyo wa bahari kuu.+

26 “ ‘ “Wale wanaokupigia makasia wamekuleta katika maji makuu.+ Upepo wa mashariki umekuvunja katika moyo wa bahari kuu.+ 27 Vitu vyako vyenye thamani na maghala yako,+ vitu vyako vya biashara,+ wanamaji wako na mabaharia+ wako, wenye kutia kalafati mipasuko+ yako na wale wanaofanya biashara na watu wako wote wa vita,+ walio ndani yako na katika kutaniko lako lote, walio katikati yako,—wataanguka katika moyo wa bahari kuu katika siku ya kuanguka kwako.+

28 “ ‘ “Nchi iliyo wazi itatikisika itakaposikia sauti ya kilio cha mabaharia wako.+ 29 Na wale wote wanaotumia kasia, wanamaji, mabaharia wote wa baharini, hakika watashuka kutoka katika meli zao; watasimama juu ya nchi.+ 30 Nao hakika watajiacha wasikiwe juu yako kwa sauti yao nao watapaaza kilio kwa uchungu.+ Nao watatia mavumbi juu ya vichwa vyao.+ Watagaagaa katika majivu.+ 31 Nao watajitia upara kwa ajili yako,+ na kujifunga nguo za magunia+ na kukulilia wewe kwa uchungu wa nafsi, kwa kuomboleza kwa uchungu.+ 32 Nao katika maombolezo yao watakuimbia wimbo wa huzuni,+

“ ‘ “ ‘Ni nani aliye kama Tiro,+ kama yeye ambaye amenyamazishwa katikati ya bahari?+ 33 Maghala+ yako yalipotoka katika bahari kuu,+ uliwashibisha watu wengi.+ Kwa wingi wa vitu vyako vyenye thamani na vitu vyako vya biashara uliwatajirisha wafalme wa dunia.+ 34 Sasa umevunjwa na bahari kuu, katika vilindi vya maji.+ Navyo vitu vyako vya biashara na kutaniko lako lote,+ vimeanguka katikati yako. 35 Wakaaji wote wa visiwa+—hakika watakukazia macho kwa mshangao, nao wafalme wao wenyewe watalazimika kutetemeka kwa hofu.+ Nyuso zitaingiwa na wasiwasi.+ 36 Nao wanabiashara kati ya vikundi vya watu, hakika watapiga mluzi juu yako.+ Utakuwa vitisho vya ghafula, nawe hutakuwapo tena mpaka wakati usio na kipimo.’ ” ’ ”+

28 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, mwambie kiongozi wa Tiro, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi:

“ ‘ “Kwa sababu moyo wako umekuwa na majivuno,+ nawe unaendelea kusema, ‘Mimi ni mungu.+ Katika kiti cha mungu nimejiketisha mwenyewe,+ katika moyo wa bahari kuu,’+ wakati ambapo wewe ni mtu wa udongo,+ wala si mungu,+ nawe unaendelea kuufanya moyo wako kama moyo wa mungu— 3 tazama! wewe una hekima kuliko Danieli.+ Hakuna siri ambazo zimelingana na wewe.+ 4 Kwa hekima yako na kwa utambuzi wako umejipatia mali, nawe unaendelea kupata dhahabu na fedha katika maghala yako.+ 5 Kwa wingi wa hekima yako,+ kwa mali zako za mauzo,+ umefanya utajiri wako uwe mwingi,+ nao moyo wako ukaanza kuwa na majivuno kwa sababu ya utajiri wako.” ’+

6 “ ‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Kwa sababu unaufanya moyo wako kama moyo wa mungu,+ 7 kwa hiyo tazama, ninaleta juu yako wageni,+ waonevu wa mataifa,+ nao hakika watachomoa panga zao juu ya uzuri wa hekima yako na kutia unajisi fahari yako inayong’aa.+ 8 Watakushusha chini mpaka shimoni,+ nawe utakufa kifo cha mtu aliyeuawa katika moyo wa bahari kuu.+ 9 Je, kwa hakika utasema, ‘Mimi ni mungu,’ mbele yake yeye anayekuua,+ wakati ambapo wewe ni mtu wa udongo tu, wala si mungu,+ mkononi mwa wale wanaokutia unajisi?” ’

10 “ ‘Kwa mkono wa wageni utakufa vifo vya watu ambao hawajatahiriwa,+ kwa maana mimi mwenyewe nimesema,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

11 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 12 “Mwana wa binadamu, mfanyie mfalme wa Tiro wimbo wa huzuni,+ nawe umwambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi:

“ ‘ “Unafunga kielelezo kwa muhuri, kinachojaa hekima+ na kikamilifu katika uzuri.+ 13 Ulikuwa katika Edeni, bustani ya Mungu.+ Kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, zabarijadi, topazi na yaspi; krisolito, shohamu+ na yashefi; yakuti, feruzi+ na zumaridi; nao ufundi wa viwekeo na wa vitundu vyako ulikuwa wa dhahabu ndani yako. Vilitayarishwa katika siku ya kuumbwa kwako. 14 Wewe ndiye kerubi aliyetiwa mafuta anayefunika, nami nimekuweka wewe. Ulikuwa katika mlima mtakatifu wa Mungu.+ Ulitembea katikati ya mawe yenye moto. 15 Hukuwa na kosa katika njia zako tangu siku ya kuumbwa+ kwako mpaka ukosefu wa uadilifu ulipoonekana ndani yako.+

16 “ ‘ “Kwa sababu ya wingi wa mali zako za mauzo+ walikujaza jeuri katikati yako, nawe ukaanza kutenda dhambi.+ Nami nitakufukuza kama uliye najisi kutoka katika mlima wa Mungu, nami nitakuharibu wewe,+ Ee kerubi unayefunika, kutoka katikati ya mawe yenye moto.

17 “ ‘ “Moyo wako ulikuwa na majivuno kwa sababu ya urembo wako.+ Uliiharibu hekima yako kwa sababu ya fahari yako inayong’aa.+ Nitakutupa chini.+ Nitakuweka mbele ya wafalme, ili wakutazame.+

18 “ ‘ “Kwa sababu ya wingi wa makosa yako,+ kwa sababu ya ukosefu wa haki wa mali zako za mauzo,+ umepatia unajisi patakatifu pako. Nami nitatokeza moto kutoka katikati yako. Huo ndio utakaokuteketeza.+ Nami nitakufanya kuwa majivu juu ya dunia mbele ya macho ya wale wanaokuona.+ 19 Nao wale wote wanaokujua wewe katikati ya vikundi vya watu, hakika watakukazia macho kwa mshangao.+ Utakuwa vitisho vya ghafula, nawe hutaendelea kuwapo tena mpaka wakati usio na kipimo.” ’ ”+

20 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 21 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako Sidoni,+ na utoe unabii juu yake. 22 Nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, niko juu yako,+ Ee Sidoni, nami hakika nitatukuzwa katikati yako;+ nao watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapofanya matendo ya hukumu+ ndani yake nami kwa kweli nitakaswe ndani yake.+ 23 Nami nitatuma tauni ndani yake na damu katika barabara zake.+ Na aliyeuawa ataanguka katikati yake kwa upanga juu yake kila upande;+ nao watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 24 Na katika nyumba ya Israeli hakutakuwa tena na mchongoma hatari+ au mwiba wenye kuumiza kutoka kwa wote hao wanaowazunguka pande zote, wale wanaowatendea kwa dhihaka; na watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” ’

25 “ ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Nitakapokusanya pamoja nyumba ya Israeli kutoka kwa vikundi vya watu ambao kati yao wametawanyika,+ mimi pia nitatakaswa kati yao machoni pa mataifa.+ Nao hakika watakaa kwenye nchi+ yao niliyompa mtumishi wangu, Yakobo.+ 26 Nao kwa kweli watakaa juu yake kwa usalama+ na kujenga nyumba+ na kupanda mashamba ya mizabibu,+ nao watakaa kwa usalama+ ninapofanya matendo ya hukumu juu ya wale wote wanaowatendea kwa dhihaka kuwazunguka pande zote;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao.” ’ ”

29 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili ya mwezi huo, neno la Yehova lilinijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako kwa Farao mfalme wa Misri+ na utoe unabii juu yake na juu ya Misri yote.+ 3 Ongea, nawe useme, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama niko juu yako, Ee Farao, mfalme wa Misri,+ yule mnyama mkubwa wa baharini+ anayelala akiwa amejinyoosha katikati ya mifereji yake ya Nile,+ ambaye amesema, ‘Mto wangu wa Nile ni wangu, na mimi—mimi nimeufanya kwa ajili yangu mwenyewe.’+ 4 Nami nitaweka kulabu katika mataya yako+ na kufanya samaki wa mifereji yako ya Nile washikamane na magamba yako. Nami nitakutoa kutoka katikati ya mifereji yako ya Nile na samaki wote wa mifereji yako ya Nile wanaoshikamana na magamba yako. 5 Nami nitakuacha nyikani, wewe na samaki wote wa mifereji yako ya Nile.+ Utaanguka juu ya uso wa nchi.+ Hutaokotwa wala kukusanywa pamoja. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama-mwitu wa dunia na kwa viumbe vinavyoruka vya mbinguni.+ 6 Na wakaaji wote wa Misri watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ kwa sababu walikuwa, kama kitegemeo, utete kwa nyumba ya Israeli.+ 7 Walipokushika mkono, ulipondwa,+ nawe ulifanya bega lao lote lipasuke. Na walipojitegemeza juu yako, ulivunjika,+ nawe ulifanya viuno vyao vyote vitetemeke.”+

8 “ ‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninaleta upanga juu yako,+ nami nitakatilia mbali kutoka kwako mtu wa udongo na mnyama wa kufugwa.+ 9 Nayo nchi ya Misri itakuwa mahame yenye ukiwa na mahali palipoharibiwa;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, kwa sababu amesema, ‘Mto Nile ni wangu, na mimi mwenyewe nimeufanya.’+ 10 Kwa hiyo tazama, niko juu yako na juu ya mifereji yako ya Nile,+ nami nitaifanya nchi ya Misri iwe mahali palipoharibiwa, ukavu, mahame yaliyotiwa ukiwa,+ kutoka Migdoli+ hadi Sewene+ na hadi mpaka wa Ethiopia. 11 Mguu wa mtu wa udongo hautapita katikati yake,+ wala mguu wa mnyama wa kufugwa hautapita katikati yake,+ na kwa miaka 40 haitakaliwa.+ 12 Nami nitaifanya nchi ya Misri iwe mahame yenye ukiwa katikati ya nchi zilizofanywa ukiwa;+ na majiji yake yatakuwa mahame yenye ukiwa katikati ya majiji yaliyoharibiwa kwa miaka 40;+ nami nitawatawanya Wamisri katikati ya mataifa na kuwatapanya katika nchi mbalimbali.”+

13 “ ‘Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Mwishoni mwa miaka 40+ nitawakusanya Wamisri pamoja kutoka kati ya vikundi vya watu ambamo watakuwa wametawanywa,+ 14 nami nitarudisha kundi la mateka ya Wamisri; nami nitawarudisha katika nchi ya Pathrosi,+ katika nchi ya asili yao, nao huko watakuwa ufalme wa hali ya chini. 15 Itakuwa chini kuliko zile falme nyingine, nayo haitajiinua yenyewe tena juu ya mataifa mengine,+ nami nitawafanya kuwa wachache sana ili wasiweze kuyatiisha mataifa mengine.+ 16 Haitakuwa tena uhakika wa nyumba ya Israeli,+ kufanya kosa likumbukwe kwa wao kugeuka na kuwafuatilia.+ Nao watalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” ’ ”

17 Sasa ikawa kwamba katika mwaka wa 27, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova likanijia, na kusema: 18 “Mwana wa binadamu, Nebukadreza mwenyewe,+ mfalme wa Babiloni, alitumikisha jeshi lake utumishi mkubwa juu ya Tiro.+ Kila kichwa kilitiwa upara, na kila bega lilikwaruzwa.+ Lakini kuhusu malipo,+ hapakuwa na malipo yoyote kwa ajili yake na jeshi lake kutoka Tiro kwa ajili ya utumishi aliokuwa amefanya juu yake.

19 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninampa Nebukadreza mfalme wa Babiloni nchi ya Misri,+ naye atauchukua utajiri wake na kuteka nyara kubwa kutokana nayo+ na kuipora kwa wingi sana; nayo itakuwa malipo kwa ajili ya jeshi lake.’

20 “ ‘Nami nimempa nchi ya Misri iwe malipo yake kwa ajili ya utumishi ambao alifanya juu yake, kwa sababu walitenda kwa ajili yangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

21 “Katika siku hiyo nitafanya pembe ichipuke kwa ajili ya nyumba ya Israeli,+ nami nitakupa sababu ya kufungua kinywa katikati yao;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”

30 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, toa unabii, nawe useme,+ ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Pigeni mayowe, ‘Ole wa siku ile!’+ 3 kwa maana siku iko karibu, naam, siku ya Yehova iko karibu.+ Siku ya mawingu,+ itakuwa wakati uliowekwa wa mataifa.+ 4 Na hakika upanga utaingia Misri,+ na maumivu makali yatatukia Ethiopia wakati ambapo mtu ataanguka akiwa ameuawa katika Misri nao kwa kweli wachukue mali yake nayo misingi yake kwa kweli ibomolewe.+ 5 Ethiopia+ na Putu+na Ludi na jamii yote iliyochangamana+ na Kubu na wana wa nchi ya agano—pamoja nao wataanguka kwa upanga.” ’+

6 “Yehova amesema hivi, ‘Wanaounga mkono Misri lazima waanguke pia, na fahari ya nguvu zake lazima ishuke chini.’+

“ ‘Kutoka Migdoli+ mpaka Sewene+ wataanguka ndani yake kwa upanga,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 7 ‘Lazima pia wafanywe kuwa ukiwa katikati ya nchi zilizofanywa ukiwa, na majiji yake yatakuwa katikati kabisa ya majiji yaliyoharibiwa.+ 8 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapowasha moto katika Misri na wasaidizi wake wote kwa kweli wavunjwe.+ 9 Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele zangu katika meli, ili kuifanya Ethiopia yenye kujitumaini ianze kutetemeka.+ Na maumivu makali yatatukia kati yao katika siku ya Misri, kwa maana, tazama! lazima ije.’+

10 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Nitaufanya pia umati wa Misri ukome kwa mkono wa Nebukadreza mfalme wa Babiloni.+ 11 Yeye na watu wake pamoja naye, watu wa mataifa wenye kuonea,+ wanaletwa ndani ili kuiharibu nchi. Nao watachomoa panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi kwa waliouawa.+ 12 Nami nitaifanya mifereji ya Nile+ iwe nchi kavu na kuiuza nchi mkononi mwa watu wabaya,+ nami nitaifanya nchi na vyote vinavyoijaza ifanywe ukiwa kwa mkono wa wageni.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’+

13 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Nitaangamiza pia sanamu za mavi+ na kufanya miungu isiyo na thamani ikome katika Nofu,+ na hakutakuwa tena na mkuu kutoka katika nchi ya Misri; nami hakika nitatia hofu katika nchi ya Misri.+ 14 Nami nitafanya Pathrosi+ kuwa ukiwa na kuwasha moto katika Soani+ na kufanya matendo ya hukumu katika No.+ 15 Nami nitaimwaga ghadhabu yangu+ juu ya Sini, ngome ya Misri, na kuukatilia mbali umati wa No.+ 16 Nami nitawasha moto katika Misri. Hakika Sini itakuwa katika maumivu makali, na No yenyewe itatekwa kwa kutobolewa matundu; na kwa habari ya Nofu—kutakuwa na wapinzani wakati wa mchana! 17 Nao vijana wa Oni+ na Pibesethi, wataanguka kwa upanga, na majiji yataenda utekwani. 18 Na katika Tehafnehesi+ siku itakuwa na giza, nitakapovunja huko nira za Misri.+ Na katika yeye fahari ya nguvu zake kwa kweli itakomeshwa.+ Na kwa habari yake, mawingu yatamfunika,+ na miji yake mwenyewe ya kandokando itaenda utekwani.+ 19 Nami nitafanya matendo ya hukumu katika Misri;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”

20 Na ikazidi kuwa kwamba katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, siku ya saba ya mwezi huo, neno la Yehova likanijia, na kusema: 21 “Mwana wa binadamu, hakika nitauvunja mkono wa Farao mfalme wa Misri,+ na, tazama! hautafungwa hata kidogo ili kuufanya upone kwa kutia kitambaa ili kuufunga,+ ili uwe na nguvu za kushika upanga.”

22 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama, mimi niko dhidi ya Farao mfalme wa Misri,+ nami nitaivunja mikono yake,+ ule wenye nguvu na ule uliovunjika,+ nami nitaufanya upanga uanguke kutoka mkononi mwake.+ 23 Nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa na kuwatapanya kati ya nchi mbalimbali.+ 24 Nami nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babiloni+ na kuutia upanga wangu mkononi mwake,+ nami nitaivunja mikono ya Farao, naye ataugua kwelikweli mbele yake kama mwenye majeraha ya kufisha.+ 25 Nami nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babiloni, na mikono yenyewe ya Farao itaanguka; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babiloni naye kwa kweli aunyooshe juu ya nchi ya Misri.+ 26 Nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa+ na kuwatapanya kati ya nchi mbalimbali; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”

31 Na ikazidi kutukia kwamba katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa tatu, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova likanijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, mwambie Farao mfalme wa Misri na umati wake,+

“ ‘Umefanana na nani katika ukuu wako? 3 Tazama! Mwashuru, mwerezi katika Lebanoni,+ wenye matawi ya kupendeza,+ wenye kifuniko chenye majani mengi kinachotoa kivuli, na wenye kimo kirefu,+ hivi kwamba kilele chake kilikuwa kati ya mawingu.+ 4 Ni maji yaliyoufanya uwe mkubwa;+ kilindi cha maji kiliufanya urefuke. Pamoja na vijito vyake kilikuwa kikienda kuzunguka pande zote mahali ulipopandwa; nacho kiliipeleka mifereji yake kwenye miti yote ya shambani. 5 Ndiyo sababu ulikuwa mrefu zaidi kwa kimo kuliko miti mingine yote ya shambani.+

“ ‘Na matawi yake yalizidi kuongezeka, na matawi yake yaliendelea kuwa marefu zaidi kwa sababu ya maji mengi kwenye mifereji ya maji.+ 6 Viumbe vyote vinavyoruka vya mbinguni vilifanya viota+ vyao kwenye matawi yake, na wanyama wote wa mwituni walizaa chini ya matawi yake,+ na mataifa yote yenye hesabu kubwa ya watu yalikuwa yakikaa katika kivuli chake. 7 Nao ukawa wenye kupendeza katika ukuu wake,+ katika urefu wa majani yake, kwa maana mizizi yake ilikuwa juu ya maji mengi. 8 Mierezi mingine haikulingana nao katika bustani ya Mungu.+ Nayo miberoshi, haikufanana nao kwa habari ya matawi yake. Na miaramoni yenyewe haikuwa kama huo katika matawi yake. Hakuna mti mwingine wowote katika bustani ya Mungu uliofanana nao katika uzuri wake.+ 9 Niliufanya kuwa mzuri katika wingi wa majani yake,+ na miti mingine yote ya Edeni iliyokuwa katika bustani ya Mungu wa kweli ikawa ikiuonea wivu.’+

10 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu wewe ulikuwa na kimo kirefu, hivi kwamba huo ukaweka kilele chake kati ya mawingu+ na moyo wake ukainuliwa kwa sababu ya kimo chake,+ 11 mimi nitautia pia mkononi mwa mdhalimu wa mataifa.+ Hakika atauchukulia hatua. Nitaufukuza huo kulingana na uovu wake.+ 12 Na wageni, watu wa mataifa wenye kuonea, wataukata, na watu watauacha milimani; na katika mabonde yote majani yake hakika yataanguka, na matawi yake yatavunjwa katikati ya sakafu zote za vijito vya dunia.+ Na vikundi vyote vya watu wa dunia watashuka kutoka katika kivuli chake na kuuacha.+ 13 Viumbe vyote vinavyoruka vya mbinguni vitakaa juu ya shina lake lililoanguka, na wanyama wote wa mwituni hakika watakuwa juu ya matawi yake;+ 14 ili wowote kati ya miti iliyonyweshwa maji vizuri usipate kuwa na kimo kirefu, au kuweka vilele vyake kati ya mawingu, na ili wowote ule unaokunywa maji usiweze kusimama juu yake kwa kimo, kwa maana yote hiyo hakika itatolewa ife,+ kwenda kwa nchi iliyo chini,+ katikati ya wana wa binadamu, kwa wale wanaoshuka kuingia shimoni.’

15 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Hakika nitasababisha maombolezo katika siku yake ya kushuka kuingia katika Kaburi.*+ Nitakifunika kilindi cha maji kwa sababu yake, nipate kuvizuia vijito vyake na ili yale maji mengi yazuiliwe; na kwa sababu yake nitatia giza Lebanoni, na kwa sababu yake miti yote ya shambani itazimia. 16 Wakati wa sauti ya kuanguka kwake hakika nitasababisha mataifa yatikisike wakati nitakapoishusha chini mpaka katika Kaburi* pamoja na wale wanaoshuka kuingia shimoni,+ na katika nchi iliyo chini miti yote ya Edeni,+ iliyo bora na iliyo mizuri kabisa ya Lebanoni, yote ile inayokunywa maji, itafarijiwa.+ 17 Pamoja naye wao wenyewe pia wameshuka mpaka katika Kaburi,*+ kwa wale waliouawa kwa upanga, na wale ambao kama mbegu yake wamekaa katika kivuli chake katikati ya mataifa.’+

18 “ ‘Umefanana na nani hivyo katika utukufu+ na ukuu katikati ya miti ya Edeni?+ Lakini hakika utashushwa pamoja na miti ya Edeni mpaka nchi iliyo chini.+ Utalala chini pamoja na wale waliouawa kwa upanga katikati ya watu ambao hawajatahiriwa. Huyu ni Farao na umati wake wote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

32 Na ikazidi kutukia kwamba katika mwaka wa kumi na mbili, katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova likanijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, mfanyie wimbo wa huzuni Farao mfalme wa Misri, nawe utamwambia, ‘Umenyamazishwa kama mwana-simba wa mataifa mwenye manyoya shingoni.+

“ ‘Nawe umekuwa kama mnyama mkubwa wa majini katika bahari,+ nawe uliendelea kufoka katika mito yako, nawe ukaendelea kutibua maji kwa miguu yako na kuichafua mito yao.’

3 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Pia nitatandaza juu yako wavu+ wangu kwa kutumia kutaniko la vikundi vingi vya watu, nao hakika watakuleta katika wavu wangu wa kukokota.+ 4 Nami nitakuacha juu ya nchi. Nitakutupa juu ya uso wa shamba.+ Nami nitavifanya viumbe vyote vinavyoruka vya mbinguni vikae juu yako, nami nitawashibisha wanyama-mwitu wa dunia nzima kutokana nawe.+ 5 Nami nitaiweka nyama yako juu ya milima na kuyajaza mabonde kwa takataka zako.+ 6 Nami nitaifanya nchi inywe kilichokutoka, damu yako,+ juu ya milima; na vijito vitajazwa kutokana nawe.’

7 “ ‘Na wakati utakapozimwa nitazifunika mbingu na kuzitia giza nyota zake. Nalo jua, nitalifunika kwa mawingu, na mwezi wenyewe hautaacha nuru yake iangaze.+ 8 Mianga yote ya nuru mbinguni—nitaitia giza kwa sababu yako, nami nitatia giza juu ya nchi yako,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

9 “ ‘Nami nitaitia uchungu mioyo ya vikundi vingi vya watu nitakapoleta mateka kutoka kwako katikati ya mataifa mpaka nchi ambazo hukuzijua.+ 10 Nami nitafanya vikundi vingi vya watu waingiwe na hofu+ kwa sababu yako, na wafalme wao watatetemeka kwa hofu kwa sababu yako wakati nitakapoutikisa upanga wangu usoni pao,+ nao watatetemeka kila dakika, kila mmoja kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, katika siku ya kuanguka kwako.’+

11 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Upanga wa mfalme wa Babiloni utakuja juu yako.+ 12 Nitaufanya umati wako uanguke kwa panga za wenye nguvu, watu wa mataifa wenye kuonea, hao wote;+ nao kwa kweli wataipora fahari ya Misri, na umati wake wote lazima uangamizwe.+ 13 Nami nitaangamiza wanyama wake wote wa kufugwa kutoka kando ya maji mengi,+ na mguu wa mtu wa udongo hautayatibua+ tena, wala hata kwato za mnyama wa kufugwa hazitayatibua.’

14 “ ‘Wakati huo nitayafanya maji yao yawe safi, na mito yao nitaifanya iende kama mafuta,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

15 “ ‘Nitakapoifanya nchi ya Misri iwe mahame yenye ukiwa nayo nchi ifanywe ukiwa, isiwe na vitu vinavyoijaza,+ nitakapowaua wakaaji wote waliomo ndani yake, pia watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+

16 “ ‘Huu ni wimbo wa huzuni, na hakika watu watauimba. Hata binti za mataifa watauimba; watauimba juu ya Misri na juu ya umati wake wote,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

17 Na ikazidi kutukia kwamba katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya kumi na tano ya mwezi huo, neno la Yehova likanijia, na kusema: 18 “Mwana wa binadamu, ombolezea umati wa Misri na kuushusha chini,+ yeye na binti za mataifa makuu, mpaka nchi iliyo chini,+ pamoja na wale wanaoshuka kuingia shimoni.+

19 “ ‘Wewe unapendeza zaidi kwa kulinganishwa na nani?+ Shuka, nawe lazima ulazwe pamoja na watu ambao hawajatahiriwa!’+

20 “ ‘Wataanguka katikati ya wale waliouawa kwa upanga.+ Yeye ametiwa mkononi mwa upanga. Mkokoteeni mbali pamoja na umati wake wote.

21 “ ‘Watu wa kwanza kabisa kati ya wenye nguvu watasema naye katikati ya Kaburi,* pamoja na wasaidizi wake.+ Hakika watashuka chini;+ watalala kama wale ambao hawajatahiriwa, waliouawa kwa upanga. 22 Huko ndiko aliko Ashuru pamoja na kutaniko lake lote.+ Makaburi yake yanamzunguka pande zote. Hao wote wameuawa, wale wanaoanguka kwa upanga.+ 23 Kwa maana makaburi yake yamewekwa katika sehemu za ndani kabisa za shimo,+ na kutaniko lake linazunguka kaburi lake pande zote, hao wote wakiwa wameuawa, wakianguka kwa upanga, kwa sababu walikuwa wamesababisha hofu katika nchi ya walio hai.

24 “ ‘Kuna Elamu+ na umati wake wote kulizunguka kaburi lake pande zote, hao wote wakiwa wameuawa, wale wanaoanguka kwa upanga, ambao wameshuka chini wakiwa hawajatahiriwa mpaka nchi iliyo chini, wale ambao wamesababisha hofu yao katika nchi ya wale walio hai; nao watachukua fedheha yao pamoja na wale wanaoshuka kuingia katika shimo.+ 25 Katikati ya waliouawa wameweka kitanda+ kwa ajili yake katikati ya umati wake wote. Makaburi yake yanakizunguka pande zote. Hao wote hawajatahiriwa, wakiwa wameuawa kwa upanga,+ kwa sababu hofu yao ilisababishwa katika nchi ya wale walio hai; nao watachukua fedheha yao pamoja na wale wanaoshuka kuingia katika shimo. Yeye amewekwa katikati ya waliouawa.

26 “ ‘Mesheki+ na Tubali+ na umati wake wote wako huko. Makaburi yake yanamzunguka pande zote. Hao wote hawajatahiriwa, wakiwa wamechomwa kwa upanga, kwa sababu wamesababisha hofu yao katika nchi ya wale walio hai. 27 Nao je, hawatalala pamoja na wenye nguvu,+ wanaoanguka kutoka kati ya watu ambao hawajatahiriwa, ambao wameshuka kuingia katika Kaburi* wakiwa na silaha zao za vita? Nao wataweka panga zao chini ya vichwa vyao, nayo makosa yao yatakuwa juu ya mifupa yao,+ kwa sababu wenye nguvu walisababisha hofu katika nchi ya wale walio hai.+ 28 Na wewe, utavunjwa katikati ya watu ambao hawajatahiriwa, nawe utalala chini pamoja na wale waliouawa kwa upanga.

29 “‘Edomu,+ wafalme wake na wakuu wake wote wako huko, ambao, katika nguvu zao, waliwekwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga;+ wao wenyewe watalala pamoja na watu ambao hawajatahiriwa+ na pamoja na wale wanaoshuka kuingia katika shimo.

30 “ ‘Watawala wadogo wa kaskazini wako huko, hao wote, na Wasidoni+ wote, ambao wameshuka chini pamoja na wale waliouawa, katika utishaji wao kwa sababu ya nguvu zao, wakiwa wameona aibu. Nao watalala wakiwa hawajatahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga nao watachukua fedheha yao pamoja na wale wanaoshuka kuingia katika shimo.+

31 “ ‘Hao ndio atakaowaona Farao, naye atafarijiwa juu ya umati wake wote.+ Farao na jeshi lake lote watakuwa watu waliouawa kwa upanga,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

32 “ ‘Kwa maana amesababisha hofu yake katika nchi ya walio hai,+ naye atalazwa katikati ya watu ambao hawajatahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, yeye Farao na umati wake wote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

33 Nalo neno la Yehova likanijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, sema na wana wa watu wako,+ nawe uwaambie,

“‘Kwa habari ya nchi, ikiwa nitauleta upanga+ juu yake na watu wa nchi, kila mmoja, wamchukue mtu na kumweka kuwa mlinzi wao,+ 3 naye kwa kweli aone upanga ukija juu ya nchi, naye apige baragumu na kuwaonya watu,+ 4 na msikiaji kwa kweli asikie sauti ya baragumu lakini asitii onyo hata kidogo,+ nao upanga uje na kumchukua, damu yake mwenyewe itakuwa juu ya kichwa chake.+ 5 Aliisikia sauti ya baragumu, lakini hakutii onyo. Damu yake mwenyewe itakuwa juu yake binafsi. Na kama angetii onyo, nafsi yake ingeponyoka.+

6 “ ‘Basi kwa habari ya mlinzi, kama akiuona upanga ukija naye kwa kweli asipige baragumu+ na watu wasipate onyo lolote nao upanga uje na kuichukua nafsi kutoka kwao, hiyo itachukuliwa kwa sababu ya kosa lake yenyewe,+ lakini damu yake nitaidai kutoka mkononi mwa mlinzi.’+

7 “Basi kwa habari yako wewe, Ee mwana wa binadamu, nimekufanya kuwa mlinzi kwa nyumba ya Israeli,+ na kutoka katika kinywa changu lazima usikie neno na kuwapa onyo kutoka kwangu.+ 8 Mimi ninapomwambia mtu mwovu, ‘Wewe mwovu, hakika utakufa!’+ lakini kwa kweli wewe usiseme ili kumwonya mwovu aiache njia yake,+ yeye mwenyewe kwa kuwa ni mwovu atakufa katika kosa lake,+ lakini damu yake nitaidai katika mkono wako. 9 Lakini kwa habari yako wewe, ikiwa kwa kweli utamwonya mwovu aiache njia yake ili ageuke na kuiacha lakini kwa kweli asigeuke na kuiacha njia yake, yeye mwenyewe atakufa katika kosa lake,+ lakini wewe hakika utaiokoa nafsi yako.+

10 “Basi kwa habari yako wewe, Ee mwana wa binadamu, iambie nyumba ya Israeli, ‘Ninyi mmesema hivi: “Kwa sababu maasi yetu na dhambi zetu ziko juu yetu nasi tunaozea humo,+ basi tutawezaje kuendelea kuishi?” ’+ 11 Waambie, ‘ “Kama ninavyoishi,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “Ninapendezwa, si na kifo cha mwovu,+ bali kwamba mtu mwovu ageuke na kuiacha+ njia yake na kwa kweli aendelee kuishi.+ Geukeni, geukeni mziache njia zenu mbaya,+ maana kwa nini mfe, Ee nyumba ya Israeli?” ’+

12 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, waambie wana wa watu wako, ‘Uadilifu wenyewe wa mwadilifu hautamkomboa katika siku ya maasi yake.+ Lakini kwa habari ya uovu wa mwovu, hautamtikisa katika siku atakapogeuka na kuuacha uovu wake.+ Wala hata mtu yeyote mwenye uadilifu hataweza kuendelea kuishi kwa sababu ya huo siku ile atakapotenda dhambi.+ 13 Ninapomwambia mwadilifu: “Hakika utaendelea kuishi,” na yeye mwenyewe kwa kweli autegemee uadilifu wake mwenyewe na kutenda ukosefu wa haki,+ matendo yake yote ya uadilifu hayatakumbukwa, lakini kwa ukosefu wake wa haki ambao ameutenda—atakufa kwa sababu ya huo.+

14 “ ‘Ninapomwambia mwovu: “Hakika utakufa,”+ naye kwa kweli ageuke na kuiacha dhambi yake+ na kuendelea kutenda haki na uadilifu,+ 15 naye mwovu arudishe kitu kile kilichowekwa rehani,+ alipe vitu vile vilivyochukuliwa kwa unyang’anyi,+ naye kwa kweli atembee katika sheria za uzima kwa kutotenda ukosefu wa haki,+ hakika ataendelea kuishi.+ Yeye hatakufa. 16 Hakuna yoyote kati ya dhambi zake alizozitenda itakayokumbukwa juu yake.+ Yeye ameendelea kutenda haki na uadilifu. Hakika ataendelea kuishi.’+

17 “Nao wana wa watu wako wamesema, ‘Njia ya Yehova si sawa,’+ lakini, wao, njia yao ndiyo ambayo si sawa.

18 “Mtu mwadilifu anapogeuka na kuuacha uadilifu wake na kwa kweli atende kwa njia isiyo ya haki, lazima pia afe kwa sababu hiyo.+ 19 Na mwovu anapogeuka na kuuacha uovu wake na kuendelea kutenda haki na uadilifu, yeye ataendelea kuishi kwa sababu ya hayo.+

20 “Nanyi mmesema, ‘Njia ya Yehova si sawa.’+ Nitawahukumu ninyi kila mmoja wenu kulingana na njia zake,+ Ee nyumba ya Israeli.”

21 Mwishowe ikatukia kwamba katika mwaka wa kumi na mbili, katika mwezi wa kumi, siku ya tano ya mwezi wa uhamisho wetu, mtu aliyeponyoka kutoka Yerusalemu akanijia,+ akisema: “Jiji limepigwa na kuangushwa!”+

22 Basi mkono wa Yehova ulikuwa juu yangu wakati wa jioni kabla ya kuja kwa huyo aliyeponyoka,+ na Yeye akakifungua kinywa changu kabla ya huyo kunijia wakati wa asubuhi, nacho kinywa changu kilikuwa kimefunguliwa nami sikuwa bubu tena.+

23 Nalo neno la Yehova likaanza kunijia, likisema: 24 “Mwana wa binadamu, wakaaji wa mahali hapa palipoharibiwa+ wanasema hata juu ya udongo wa Israeli, ‘Abrahamu alikuwa mmoja tu, hata hivyo aliitwaa nchi hii.+ Na sisi ni wengi; tumepewa nchi hii iwe mali yetu.’+

25 “Kwa hiyo waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Mnaendelea kula pamoja na damu,+ nayo macho yenu mnaendelea kuyainua kuelekea sanamu zenu za mavi,+ nanyi mnaendelea kuimwaga damu.+ Kwa hiyo je, mnapaswa kuimiliki nchi hii?+ 26 Mmeutegemea upanga wenu.+ Mmefanya chukizo,+ na kila mmoja wenu amemtia unajisi mke wa mwenzake.+ Kwa hiyo je, mnapaswa kuimiliki nchi hii?” ’+

27 “Unapaswa kuwaambia hivi, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Kama ninavyoishi, hakika wale walio katika mahali palipoharibiwa wataanguka kwa upanga;+ na yule aliye katika shamba, hakika nitamfanya awe chakula cha mnyama-mwitu;+ na wale walio katika mahali imara na katika mapango+ watakufa kwa tauni. 28 Nami kwa kweli nitaifanya nchi iwe mahame yenye ukiwa,+ naam, ukiwa, na fahari ya nguvu zake itakomeshwa+ na milima ya Israeli itafanywa ukiwa,+ pasipo mtu anayepita katikati. 29 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoifanya nchi iwe mahame yenye ukiwa,+ naam, ukiwa, kwa sababu ya machukizo yote ambayo wamefanya.” ’+

30 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, wana wa watu wako wanasemezana juu yako kando ya kuta na katika miingilio ya nyumba,+ na mmoja amesema na mwingine, kila mmoja na ndugu yake, na kusema, ‘Njooni, tafadhali, msikie ni neno gani linalotoka kwa Yehova.’+ 31 Nao wataingia ndani kwako, kama wanavyoingia watu, na kuketi mbele yako kama watu wangu;+ nao hakika watayasikia maneno yako lakini hawatayatenda,+ kwa maana wanaonyesha tamaa zenye uchu kwa kinywa chao nao moyo wao unafuatilia pato lao lisilo la haki.+ 32 Na, tazama! kwao wewe ni kama wimbo wa mapendo yenye hisia, kama mtu mwenye sauti nzuri na mwenye kupiga kinanda vizuri.+ Nao hakika watayasikia maneno yako, lakini hakuna yeyote anayeyatenda.+ 33 Na yatakapotimia—tazama! lazima yatatimia+—wao pia watalazimika kujua kwamba nabii alikuwa katikati yao.”+

34 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli. Toa unabii, nawe uwaambie hao wachungaji, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Ole wao wachungaji wa Israeli,+ ambao wamekuwa watu wanaojilisha wenyewe!+ Je, wachungaji hawapaswi kulisha kundi?+ 3 Mnakula mafuta,+ na kujivika sufu ninyi wenyewe. Mnamchinja mnyama aliyenona.+ Hamlishi kundi lenyewe. 4 Walio wagonjwa hamkuwatia nguvu,+ na anayeugua hamkumponya, na aliyevunjika hamkumfunga, na aliyefukuzwa hamkumrudisha, na aliyepotea hamkumtafuta apatikane,+ lakini mmewatawala kwa ukali, naam, kwa uonevu.+ 5 Nao wakatawanyika hatua kwa hatua kwa sababu hapakuwa na mchungaji,+ hivi kwamba wakawa chakula cha kila mnyama wa mwituni, nao wakaendelea kutawanyika.+ 6 Kondoo zangu waliendelea kupotea kwenye milima yote na juu ya kila kilima kirefu;+ na juu ya uso wote wa dunia kondoo zangu+ walitawanyika, pasipo mtu wa kutafuta wala mtu anayejitahidi kupata.

7 “ ‘ “Kwa hiyo, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Yehova, 8 ‘ “Kama ninavyoishi,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “hakika kwa sababu kondoo zangu walikuwa kitu cha kuporwa na kondoo zangu waliendelea kuwa chakula kwa ajili ya kila mnyama wa mwituni, kwa sababu hapakuwa na mchungaji yeyote, nao wachungaji wangu hawakuwatafuta kondoo zangu, bali wachungaji waliendelea kujilisha wenyewe,+ nao hawakuwalisha kondoo zangu,” ’ 9 kwa hiyo, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Yehova. 10 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama niko dhidi ya wachungaji,+ na hakika mimi nitadai kondoo zangu kutoka mkononi mwao na kuwafanya waache kuwalisha kondoo zangu,+ nao wachungaji hawatajilisha tena kamwe;+ nami nitawakomboa kondoo zangu kutoka kinywani mwao, nao hawatakuwa chakula chao.’ ”+

11 “ ‘Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Mimi nipo hapa, mimi mwenyewe, nami nitawatafuta kondoo zangu na kuwatunza.+ 12 Kulingana na utunzaji wa mtu anayelisha kundi+ lake katika siku ya kuja kwake kuwa katikati ya kondoo zake ambao wametawanyika kotekote,+ hivyo ndivyo nitakavyowatunza kondoo zangu; nami nitawakomboa kutoka mahali pote ambapo wametawanyika katika siku ya mawingu na giza zito.+ 13 Nami nitawatoa+ kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya pamoja kutoka katika zile nchi na kuwaleta kwenye nchi yao+ na kuwalisha kwenye milima ya Israeli, kando ya vijito na kando ya makao yote ya nchi.+ 14 Katika malisho mazuri nitawalisha wao, na makao yao yatakuwa katika milima mirefu ya Israeli.+ Huko watalala katika makao mazuri,+ na kwenye malisho manono watajilisha juu ya milima ya Israeli.”

15 “ ‘ “Mimi mwenyewe nitawalisha kondoo zangu,+ na mimi mwenyewe nitawalaza,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 16 “Aliyepotea nitamtafuta, na aliyefukuzwa nitamrudisha,+ na aliyevunjika nitamfunga na anayeugua nitamtia nguvu, lakini aliyenona+ na aliye na nguvu nitamwangamiza. Huyo nitamlisha hukumu.”+

17 “ ‘Nanyi kondoo zangu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninahukumu kati ya kondoo na kondoo, kati ya kondoo-dume na mbuzi-dume.+ 18 Je, ni jambo dogo kwenu kwamba ninyi mnajilisha malisho yaliyo bora zaidi+ lakini yale malisho mengine yenu mnayakanyaga-kanyaga kwa miguu yenu, na kwamba maji safi mnayanywa lakini yaliyobaki mnayachafua kwa kuyakanyaga-kanyaga kwa miguu yenu? 19 Nao kondoo zangu, je, wajilishe kwenye malisho mliyokanyaga-kanyaga kwa miguu yenu na kunywa maji yaliyochafuliwa kwa kukanyagwa-kanyagwa kwa miguu yenu?”

20 “ ‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amewaambia hivi: “Tazama mimi nipo hapa, mimi mwenyewe, nami nitahukumu kati ya kondoo aliyenona na kondoo aliyekonda, 21 kwa sababu kwa ubavu na kwa bega mliendelea kusukuma na kwa pembe zenu mliendelea kuwasukuma wote waliofanywa kuwa wagonjwa mpaka mkawa mmewatawanya nje.+ 22 Nami nitawaokoa kondoo zangu, nao hawataendelea kuwa tena kitu cha kuporwa;+ nami nitahukumu kati ya kondoo na kondoo. 23 Nami nitasimamisha juu yao mchungaji mmoja,+ naye atawalisha, naam, mtumishi wangu Daudi.+ Yeye mwenyewe atawalisha, na yeye mwenyewe atakuwa mchungaji wao.+ 24 Na mimi mwenyewe, Yehova, nitakuwa Mungu wao,+ na mtumishi wangu Daudi atakuwa mkuu katikati yao.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.

25 “ ‘ “Nami nitafanya agano la amani pamoja nao,+ na hakika mimi nitamkomesha katika nchi mnyama-mwitu mwenye kudhuru,+ nao kwa kweli watakaa nyikani kwa usalama na kulala katika misitu.+ 26 Nami nitawafanya wao na mazingira ya kilima changu kuwa baraka,+ nami nitaifanya mvua inayomwagika ishuke kwa wakati wake. Kutakuwa na mvua inayomwagika ya baraka.+ 27 Na mti wa shambani utatoa matunda+ yake, na nchi yenyewe itatoa mazao+ yake, nao kwa kweli watakuwa katika nchi yao kwa usalama.+ Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapovunja nira+ zao na kuwakomboa kutoka katika mkono wa wale waliokuwa wakiwatumia kama watumwa.+ 28 Nao hawataendelea kuwa kitu cha kuporwa na mataifa;+ na kwa habari ya mnyama-mwitu wa dunia, yeye hatawararua, nao kwa kweli watakaa katika usalama, pasipo mtu yeyote wa kuwatetemesha.+

29 “ ‘ “Nami nitawainulia mmea ili kujifanyia jina,+ nao hawatakuwa tena wale walioondolewa na njaa katika nchi,+ nao hawatachukua fedheha tena kamwe kutoka kwa mataifa.+ 30 ‘Nao watalazimika kujua kwamba mimi, Yehova Mungu wao, niko pamoja nao+ na kwamba wao ni watu wangu, nyumba ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” ’+

31 “ ‘Na kwa habari yenu ninyi kondoo zangu,+ kondoo wa malisho yangu, ninyi ni watu wa udongo. Mimi ni Mungu wenu,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

35 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, elekeza uso+ wako kwenye eneo lenye milima la Seiri+ na utoe unabii juu yake.+ 3 Nawe utaliambia, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Mimi hapa niko dhidi yako, Ee eneo lenye milima la Seiri,+ nami nitaunyoosha mkono wangu juu yako+ na kukufanya uwe mahame, naam, kuwa ukiwa.+ 4 Majiji yako nitayafanya kuwa mahali palipoharibiwa, na wewe mwenyewe utakuwa mahame yenye ukiwa;+ nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ 5 kwa sababu ulikuwa na uadui wenye kudumu mpaka wakati usio na kipimo+ nawe uliendelea kuwatia wana wa Israeli kwenye nguvu za upanga,+ wakati wa maafa yao,+ wakati wa kosa lao la mwisho.” ’+

6 “ ‘Kwa hiyo kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘kwa sababu nilikuwa nikikutayarisha kwa ajili ya damu, damu yenyewe pia itakufuatilia wewe.+ Hakika damu ndiyo uliyoichukia, na damu yenyewe ndiyo itakayokufuatilia.+ 7 Nami hakika nitalifanya eneo lenye milima la Seiri kuwa mahame, naam, kuwa ukiwa,+ nami nitamkatilia mbali kutoka hilo mtu yeyote anayepita katikati na mtu anayerudi.+ 8 Nami nitaijaza milima yake kwa watu wake waliouawa; na katika vilima vyako na mabonde yako na vijito vyako vyote, wale waliouawa kwa upanga wataanguka humo.+ 9 Nitakufanya kuwa mahame yenye ukiwa yanayodumu mpaka wakati usio na kipimo, nayo majiji yako mwenyewe hayatakaliwa;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+

10 “Kwa sababu ulisema, ‘Mataifa haya mawili na nchi hizi mbili—zitakuwa zangu mwenyewe, nasi hakika tutaitwaa kila nchi,’+ ijapokuwa Yehova mwenyewe alikuwa hapo,+ 11 ‘kwa hiyo kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitatenda pia kulingana na hasira yako na kulingana na wivu wako ambao umeonyesha kwa sababu ya hisia zako za chuki kuwaelekea;+ nami nitajijulisha mwenyewe katikati yao nitakapokuhukumu.+ 12 Nawe utalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesikia mambo yako yote yasiyo ya heshima ambayo umesema kuhusu milima ya Israeli,+ ukisema: “Imefanywa ukiwa. Imetiwa mkononi mwetu iwe chakula chetu.”+ 13 Nanyi mliendelea kutenda kwa majivuno makubwa juu yangu kwa vinywa vyenu,+ nanyi mmezidisha maneno yenu juu yangu.+ Mimi mwenyewe nimeyasikia.’+

14 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Wakati uleule ambao dunia yote inashangilia, nitakufanya wewe kuwa mahame yenye ukiwa. 15 Kama vile tu ulivyoshangilia urithi wa nyumba ya Israeli kwa sababu ilifanywa ukiwa, nitakutendea jambo hilohilo.+ Utakuwa mahame yenye ukiwa, Ee eneo lenye milima la Seiri, naam, Edomu yote, naam, yote pia;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”+

36 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, toa unabii juu ya milima ya Israeli, nawe utasema, ‘Ee milima ya Israeli,+ lisikieni neno la Yehova. 2 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Kwa sababu adui amesema juu yenu,+ ‘Aha! Hata mahali pa juu pa wakati wa kale+—pamekuwa mali yetu!’ ” ’+

3 “Kwa hiyo toa unabii, nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Kwa sababu, naam, kwa sababu kumekuwa na kufanywa ukiwa+ na kuumwa kutoka pande zote,+ ili muwe mali ya mabaki ya mataifa+ nanyi mnaendelea kusemwa kwa midomo+ na kati ya watu kuna habari mbaya,+ 4 kwa hiyo, enyi milima ya Israeli,+ lisikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Ni hivi Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameambia milima na vilima, vijito na mabonde na mahali palipoharibiwa+ na kufanywa ukiwa na majiji yaliyoachwa ambayo yameporwa na kudhihakiwa na mabaki ya mataifa yanayozunguka pande zote;+ 5 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Hakika katika moto wa bidii yangu nitasema+ juu ya mabaki ya mataifa na juu ya Edomu yote,+ wale ambao wamejipatia wenyewe nchi yangu iwe mali yao kwa kushangilia kwa moyo wote,+ kwa dharau katika nafsi yao,+ kwa ajili ya kiwanja chake cha malisho na ili kuipora.’ ” ’+

6 “Kwa hiyo toa unabii kuhusu udongo wa Israeli, nawe utaambia milima na vilima, vijito na mabonde, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama! mimi mwenyewe katika bidii yangu na katika ghadhabu yangu lazima nitasema, kwa sababu mmechukua fedheha ya mataifa.” ’+

7 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Mimi mwenyewe nimeuinua mkono wangu katika kiapo+ ili mataifa yanayowazunguka pande zote—hayo yatachukua fedheha yao yenyewe.+ 8 Na ninyi wenyewe, enyi milima ya Israeli, mtatoa matawi yenu wenyewe na kuzaa matunda yenu wenyewe kwa ajili ya watu wangu Israeli,+ kwa maana wamekaribia hatua ya kuingia ndani.+ 9 Kwa maana tazama, nimewapa ninyi kibali changu, nami hakika nitageuka kuwaelekea ninyi,+ na kwa kweli ninyi mtalimwa na kupandwa mbegu.+ 10 Nami nitazidisha binadamu juu yenu, nyumba yote ya Israeli, naam, nyumba yote,+ na majiji yatakaliwa,+ na mahali palipoharibiwa penyewe patajengwa upya.+ 11 Naam, nitawazidisha binadamu na wanyama juu yenu,+ nao hakika wataongezeka na kuzaa, nami kwa kweli nitawafanya ninyi mkaliwe kama ilivyokuwa hali yenu ya zamani+ nami nitafanya mema zaidi kuliko ilivyokuwa hali yenu ya zamani;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 12 Na juu yenu nitawafanya binadamu watembee, naam, watu wangu Israeli, nao watawamiliki ninyi,+ nanyi mtakuwa fungu lao la urithi,+ nanyi hamtawaua+ watoto wao tena.’ ”

13 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu kuna wale wanaowaambia ninyi: “Wewe ni mmezaji wa binadamu, nawe umekuwa nchi inayowaua watoto wa mataifa yako,” ’+ 14 ‘kwa hiyo hutawameza binadamu tena,+ nawe hutawaua watoto wa mataifa yako tena,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 15 ‘Nami sitasababisha tena mazungumzo zaidi yenye kufedhehesha ya mataifa yasikiwe juu yako,+ nawe hutachukua tena shutuma ya watu,+ nayo mataifa yako hutayafanya yajikwae tena,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

16 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 17 “Mwana wa binadamu, nyumba ya Israeli walikuwa wakikaa katika nchi yao, nao wakaendelea kuichafua kwa njia yao na kwa matendo yao.+ Njia yao imekuwa mbele zangu kama uchafu wa hedhi.+ 18 Nami nikamwaga ghadhabu yangu juu yao kwa sababu ya damu waliyokuwa wameimwaga juu ya nchi,+ nchi ambayo walikuwa wameichafua kwa sanamu zao za mavi.+ 19 Nami nikawatawanya katikati ya mataifa, hivi kwamba wakasambaa katika nchi mbalimbali.+ Niliwahukumu kulingana na njia yao na kulingana na matendo yao.+ 20 Kwa hiyo wakaingia kwa mataifa ambamo waliingia, na watu wakatia unajisi jina langu takatifu+ kwa kusema hivi juu yao, ‘Hawa ndio watu wa Yehova, nao wametoka katika nchi yake.’+ 21 Nami nitalihurumia jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli imelitia unajisi katikati ya mataifa ambamo wameingia.”+

22 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Sifanyi jambo hili kwa ajili yenu, Ee nyumba ya Israeli, bali kwa ajili ya jina langu takatifu, ambalo ninyi mmelitia unajisi katikati ya mataifa ambamo mmeingia.” ’+ 23 ‘Nami hakika nitalitakasa jina langu kuu,+ ambalo lilikuwa likitiwa unajisi katikati ya mataifa, ambalo ninyi mlilitia unajisi katikati yao; nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘wakati nitakapotakaswa katikati yenu mbele ya macho yao.+ 24 Nami nitawatoa ninyi kutoka kwa mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi zote na kuwaingiza katika nchi yenu.+ 25 Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi;+ nami nitawasafisha ninyi kutokana na uchafu+ wenu wote na kutokana na sanamu zenu zote za mavi.+ 26 Nami nitawapa ninyi moyo mpya,+ na nitatia ndani yenu roho mpya,+ nami nitauondoa moyo wa jiwe kutoka mwilini mwenu na kuwapa ninyi moyo wa nyama.+ 27 Nami nitaitia roho yangu ndani yenu,+ nami nitachukua hatua ili mtembee katika masharti yangu,+ nayo maamuzi yangu ya hukumu mtayashika na kuyafanya kikweli.+ 28 Nanyi hakika mtakaa katika nchi niliyowapa mababu zenu,+ nanyi mtakuwa watu wangu na mimi mwenyewe nitakuwa Mungu wenu.’+

29 “ ‘Nami nitawaokoa ninyi kutoka kwenye uchafu+ wenu wote na kuiita nafaka na kuifanya iwe tele, nami sitaweka juu yenu njaa yoyote.+ 30 Nami hakika nitafanya matunda ya mti yawe tele, na mazao ya shamba, ili msishutumiwe tena na mataifa kwa sababu ya njaa.+ 31 Nanyi mtakumbuka njia zenu mbaya na matendo yenu ambayo hayakuwa mazuri,+ nanyi mtachukizwa na nafsi zenu wenyewe kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ya machukizo yenu.+ 32 Sifanyi jambo hili kwa ajili yenu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘na ijulikane kwenu. Mwone aibu na kufedheheka kwa sababu ya njia zenu, Ee nyumba ya Israeli.’+

33 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Siku nitakayowasafisha ninyi kutokana na makosa yenu yote nitayafanya pia majiji yakaliwe,+ na mahali palipoharibiwa patajengwa upya.+ 34 Nayo nchi iliyofanywa ukiwa italimwa, ingawa ilikuwa imekuwa mahame yenye ukiwa machoni pa kila mpita-njia.+ 35 Na hakika watu watasema: “Ile nchi kule ambayo ilifanywa ukiwa imekuwa kama bustani ya Edeni,+ nayo majiji yaliyokuwa ukiwa na ambayo yalikuwa yamebomolewa yametiwa ngome; yamekaliwa.”+ 36 Nayo mataifa yatakayokuwa yamebaki kuwazunguka ninyi pande zote yatalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimejenga vitu vilivyobomolewa,+ nimepanda kilichofanywa ukiwa. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nimelitenda.’+

37 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Hili ndilo bado nitajiacha niulizwe na nyumba ya Israeli ili niwafanyie:+ Mimi nitawazidisha kwa watu kama kundi.+ 38 Kama kundi la watu watakatifu, kama kundi la Yerusalemu katika majira yake ya sherehe,+ hivyo ndivyo majiji yaliyokuwa yamefanywa ukiwa yatakavyojaa kundi la watu;+ nao watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”

37 Mkono wa Yehova ulikuwa juu yangu,+ hivi kwamba akanichukua katika roho ya Yehova+ na kuniweka chini katikati ya nchi tambarare ya bondeni, nayo ilikuwa imejaa mifupa.+ 2 Naye akanipitisha kando yake pande zote, na, tazama! ilikuwa mingi sana kwenye uso wa hiyo nchi tambarare ya bondeni na, tazama! ilikuwa mikavu sana.+ 3 Naye akaanza kuniambia: “Mwana wa binadamu, je, mifupa hii inaweza kuwa hai?” Nikajibu: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, wewe mwenyewe unajua vema.”+ 4 Naye akaendelea kuniambia: “Toa unabii juu ya mifupa hii, nawe uiambie, ‘Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Yehova:

5 “ ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameiambia mifupa hii hivi: “Tazama, ninaleta ndani yenu pumzi, nanyi lazima muwe hai.+ 6 Nami nitaweka juu yenu kano na kufanya nyama ije juu yenu, nami nitaitandaza ngozi juu yenu na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtakuwa hai;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” ’ ”+

7 Nami nikatoa unabii kama nilivyoamriwa.+ Na sauti ikaanza kutokea mara tu nilipotoa unabii, na tazama, kulikuwa na sauti ya kugongana, nayo mifupa ikaanza kukaribiana, mfupa kwa mfupa wake. 8 Nami nikaona, na, tazama! kano na nyama zikaja juu yake na ngozi ikaanza kutandazwa juu yake. Lakini kwa habari ya pumzi, hamkuwa na yoyote ndani yake.

9 Naye akaendelea kuniambia: “Tolea upepo unabii. Toa unabii, Ee mwana wa binadamu, nawe utauambia upepo, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Ingia kutoka kwenye zile pepo nne, Ee upepo, na upulize juu ya watu hawa waliouawa,+ ili wawe hai.” ’ ”+

10 Nami nikatoa unabii kama vile alivyokuwa ameniamuru, nayo pumzi ikaanza kuingia ndani yao, nao wakaanza kuishi na kusimama kwa miguu yao,+ jeshi kubwa, naam, kubwa sana.

11 Naye akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, kwa habari ya mifupa hii, hii ni nyumba nzima ya Israeli.+ Tazama, wanasema, ‘Mifupa yetu imekauka, nalo tumaini letu limeangamia.+ Tumekatiliwa mbali, tukabaki peke yetu.’ 12 Kwa hiyo toa unabii, nawe utawaambia, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama ninayafungua makaburi yenu,+ nami nitawatoa kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, na kuwaingiza katika nchi ya Israeli.+ 13 Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova nitakapoyafungua makaburi yenu na nitakapowatoa ninyi kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu.” ’+ 14 ‘Nami nitaitia roho yangu ndani yenu, nanyi mtakuwa hai,+ nami nitawakalisha katika nchi yenu; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nimelifanya,’ asema Yehova.”+

15 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 16 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, jichukulie kijiti+ na uandike juu yake, ‘Kwa Yuda na kwa wenzake, wana wa Israeli.’+ Na uchukue kijiti kingine na kuandika juu yake, ‘Kwa Yosefu, kijiti cha Efraimu,+ na wenzake, nyumba yote ya Israeli.’+ 17 Na uvifanye vikaribiane viwe kijiti kimoja kwa ajili yako mwenyewe, navyo kwa kweli vitakuwa kimoja tu mkononi mwako.+ 18 Na wana wa watu wako watakapoanza kukuambia, ‘Je, hutatuambia mambo haya yana maana gani kwako?’+ 19 waambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninakichukua kijiti cha Yosefu, kilicho mkononi mwa Efraimu, na wenzake, makabila ya Israeli, nami nitawaweka juu yake, yaani, kijiti cha Yuda, nami kwa kweli nitavifanya kuwa kijiti kimoja,+ navyo vitakuwa kimoja mkononi mwangu.” ’ 20 Navyo vijiti utakavyoandika juu yake vitakuwa mkononi mwako mbele ya macho yao.+

21 “Nawe uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninawachukua wana wa Israeli kutoka katikati ya mataifa ambako wameenda, nami nitawakusanya kutoka pande zote na kuwaleta katika nchi yao.+ 22 Nami kwa kweli nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo,+ kwenye milima ya Israeli, na mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote,+ nao hawataendelea tena kuwa mataifa mawili, wala hawataendelea tena kugawanyika katika falme mbili.+ 23 Nao hawatajitia unajisi tena kwa sanamu zao za mavi na kwa machukizo yao na kwa makosa yao yote;+ nami hakika nitawaokoa kutoka katika makao yao yote ambamo wametenda dhambi ndani yake, nami nitawasafisha,+ nao watakuwa watu wangu, na mimi mwenyewe nitakuwa Mungu wao.+

24 “ ‘ “Na mtumishi wangu Daudi atakuwa mfalme juu yao,+ nao wote watakuwa na mchungaji mmoja;+ nao watatembea katika maamuzi yangu ya hukumu,+ na sheria zangu watazishika,+ nao hakika watazifanya.+ 25 Nao kwa kweli watakaa juu ya nchi niliyompa mtumishi wangu, Yakobo, ambamo mababu zenu walikaa,+ nao kwa kweli watakaa juu yake,+ wao na wana wao na wana wa wana wao mpaka wakati usio na kipimo,+ na Daudi mtumishi wangu atakuwa mkuu wao mpaka wakati usio na kipimo.+

26 “ ‘ “Nami nitafanya agano la amani+ pamoja nao; watakuwa na agano lenye kudumu mpaka wakati usio na kipimo.+ Nami nitawaweka na kuwazidisha+ na kuweka patakatifu pangu katikati yao mpaka wakati usio na kipimo.+ 27 Na maskani yangu kwa kweli itakuwa juu yao,+ nami hakika nitakuwa Mungu wao, na wao wenyewe watakuwa watu wangu.+ 28 Na mataifa watalazimika kujua kwamba mimi, Yehova,+ ninawatakasa Israeli wakati patakatifu pangu patakapokuwa katikati yao mpaka wakati usio na kipimo.” ’ ”+

38 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu,+ elekeza uso wako juu ya Gogu wa nchi ya Magogu,+ mkuu wa wakuu wa Mesheki+ na Tubali,+ na utoe unabii juu yake. 3 Nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, niko dhidi yako, Ee Gogu, wewe mkuu wa wakuu wa Mesheki na Tubali. 4 Nami hakika nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako+ na kukutoa pamoja na jeshi lako lote,+ farasi na wapanda-farasi, wote wakiwa wamevaa mavazi yenye kupendeza,+ kutaniko kubwa sana, lenye ngao kubwa na ngao ndogo, wote wakiwa na panga;+ 5 Uajemi,+ Ethiopia+ na Putu+ pamoja nao, wote wakiwa na ngao ndogo na kofia; 6 Gomeri+ na vikosi vyake vyote, nyumba ya Togarma,+ wa sehemu za mbali zaidi za kaskazini, na vikosi vyake vyote, vikundi vingi vya watu pamoja nawe.+

7 “ ‘ “Uwe tayari, nawe ujitayarishe, wewe pamoja na kutaniko lako lote,+ wale waliokutanika kando yako, nawe utakuwa mlinzi wao.

8 “ ‘ “Baada ya siku nyingi utakaziwa fikira. Katika miaka ya mwisho utakuja katika nchi+ ya watu waliorudishwa kutoka kwenye upanga, waliokusanywa kutoka kwa vikundi vingi vya watu,+ na kuletwa kwenye milima ya Israeli, ambayo imekuwa mahali palipoharibika daima; naam, nchi ambayo imerudishwa kutoka kwa vikundi vya watu, ambamo wamekaa kwa usalama, hao wote.+ 9 Nawe lazima utapanda. Utaingia kama dhoruba.+ Utakuwa kama mawingu ya kuifunika nchi,+ wewe na vikosi vyako vyote na vikundi vingi vya watu pamoja nawe.” ’

10 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Na itatukia katika siku hiyo kwamba mambo yataingia moyoni mwako,+ nawe hakika utapanga hila yenye madhara;+ 11 nawe utasema: “Nitapanda juu ya nchi iliyo wazi ya mashambani.+ Nitawaingilia wale wasio na usumbufu, wanaokaa kwa usalama, wote wanaokaa bila ukuta,+ nao hawana hata mapingo na milango.” 12 Ili kuteka nyara kubwa na kupora kwa wingi,+ ili kuugeuzia mkono wako kuelekea mahali palipoharibiwa panapokaliwa tena+ na juu ya kikundi cha watu waliokusanywa pamoja kutoka katika mataifa,+ wanaokusanya utajiri na mali,+ wale wanaokaa katikati+ ya dunia.

13 “ ‘Sheba+ na Dedani+ na wanabiashara wa Tarshishi+ na wana-simba wake wote wenye manyoya shingoni+—hao watakuambia: “Je, unakuja kuteka nyara kubwa? Je, umekutanisha kutaniko lako ili kupora kwa wingi, ili kuchukua fedha na dhahabu, kuchukua utajiri na mali, ili kuteka nyara kubwa sana?” ’

14 “Kwa hiyo toa unabii, Ee mwana wa binadamu, nawe umwambie Gogu, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Je, haitakuwa katika siku ile wakati watu wangu Israeli wanapokaa kwa usalama kwamba utajua hilo?+ 15 Nawe hakika utakuja kutoka mahali pako, kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini,+ wewe na vikundi vingi vya watu pamoja nawe, hao wote wakiwa wamepanda farasi, kutaniko kubwa, naam, jeshi kubwa sana.+ 16 Nawe utalazimika kupanda na kuja juu ya watu wangu Israeli, kama mawingu ili kuifunika nchi.+ Itatukia katika siku za mwisho, nami hakika nitakuleta wewe juu ya nchi yangu,+ kusudi mataifa yanijue mimi wakati ninapojitakasa mwenyewe kupitia kwako mbele ya macho yao, Ee Gogu.” ’+

17 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Je, wewe ndiye+ yuleyule niliyesema juu yake katika siku za zamani kwa mkono wa watumishi wangu hao manabii wa Israeli, waliokuwa wakitoa unabii katika siku hizo—miaka—juu ya kukuleta wewe juu yao?’+

18 “ ‘Na itatukia katika siku hiyo, katika siku ambayo Gogu atakuja juu ya nchi ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘kwamba ghadhabu yangu itapanda puani mwangu.+ 19 Na katika ukali wangu,+ katika moto wa ghadhabu yangu, nitalazimika kusema.+ Kwa kweli katika siku hiyo tetemeko kubwa litatukia katika nchi ya Israeli.+ 20 Na kwa sababu yangu samaki wa baharini na viumbe vinavyoruka vya mbinguni na wanyama wa mwituni na vitu vyote vinavyotambaa juu ya nchi na wanadamu wote walio katika uso wa nchi watalazimika kutetemeka,+ nayo milima kwa kweli itaangushwa chini+ na njia zenye mwinuko mkali zitaanguka, na kila ukuta utaanguka chini.’

21 “ ‘Nami nitaita upanga juu yake kotekote katika eneo langu lote lenye milima,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ ‘Upanga wa kila mmoja utakuwa juu ya ndugu yake.+ 22 Nami nitajiingiza mwenyewe katika hukumu+ pamoja naye, kwa tauni+ na kwa damu;+ nami nitanyesha mvua kubwa yenye kufurika na mawe,+ moto+ na kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya vikundi vingi vya watu vitakavyokuwa pamoja naye.+ 23 Nami hakika nitajitukuza mwenyewe na kujitakasa mwenyewe+ na kujijulisha mwenyewe mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+

39 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, toa unabii juu ya Gogu,+ nawe useme, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama niko dhidi yako, Ee Gogu, ewe mkuu wa wakuu wa Mesheki+ na Tubali.+ 2 Nami nitakugeuza na kukuongoza+ na kukufanya uje kutoka katika sehemu za mbali zaidi za kaskazini+ na kukuingiza kwenye milima ya Israeli. 3 Nami nitaupiga upinde wako utoke katika mkono wako wa kushoto, nayo mishale yako nitaiangusha kutoka katika mkono wako mwenyewe wa kuume. 4 Utaanguka juu ya milima ya Israeli,+ wewe na vikosi vyako vyote na vikundi vya watu vitakavyokuwa pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wenye kuwinda, na ndege wa kila namna ya bawa, na wanyama wa mwituni.” ’+

5 “ ‘Utaanguka juu ya uso wa nchi,+ kwa maana mimi mwenyewe nimesema,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

6 “ ‘Nami nitatuma moto juu ya Magogu+ na juu ya wale wanaokaa visiwani kwa usalama;+ na watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova. 7 Na jina langu takatifu nitalijulisha katikati ya watu wangu Israeli, wala sitaliacha tena jina langu litiwe unajisi;+ na mataifa watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ Mtakatifu katika Israeli.’+

8 “ ‘Tazama! itakuwa na lazima itatendeka,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. ‘Hii ndiyo siku ambayo nimesema juu yake.+ 9 Na wakaaji wa majiji ya Israeli hakika wataenda na kuteketeza na kuwasha mioto kwa silaha na ngao ndogo na ngao kubwa,—kwa pinde na kwa mishale na kwa fimbo na kwa mikuki; nao watazitumia kuwasha mioto+ kwa miaka saba. 10 Nao hawatachukua vijiti shambani, wala hawatakusanya kuni misituni, kwa maana watatumia silaha kuwasha mioto.’

“ ‘Nao hakika watawateka nyara wale waliokuwa wakiwateka nyara,+ na kuwapora wale waliokuwa wakiwapora,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

11 “ ‘Na itatukia kwamba katika siku hiyo, nitampa Gogu+ mahali huko, kaburi katika Israeli, bonde la wale wanaopita katikati upande wa mashariki wa bahari, nalo litakuwa likiwazuia wale wanaopita katikati. Nao watalazimika kumzika Gogu na umati wake wote huko, nao hakika wataliita, Bonde la Umati wa Gogu.+ 12 Na wale wa nyumba ya Israeli watalazimika kuwazika hao ili kuisafisha nchi, kwa miezi saba.+ 13 Na watu wote wa nchi watalazimika kuzika, na hakika kwao hilo litakuwa jambo lenye sifa katika siku ambayo nitajitukuza mwenyewe,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

14 “ ‘Na kutakuwa na watu kwa ajili ya kazi ya kuajiriwa yenye kuendelea ambao watawatenga, wakipita katikati ya nchi, wakizika, na wale wanaopita katikati, wale waliobaki kwenye uso wa dunia, ili kuisafisha. Mpaka mwisho wa miezi saba wataendelea kutafuta. 15 Na wale wanaopita katikati lazima wapite nchini, na mtu akiuona mfupa wa mwanadamu ataweka pia alama kando yake, mpaka wale wanaozika watakapokuwa wameuzika katika Bonde la Umati wa Gogu.+ 16 Nalo jina la jiji hilo litakuwa pia Hamona. Nao watalazimika kuitakasa nchi.’+

17 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Sema na ndege wa kila namna ya bawa na wanyama wote wa mwituni:+ “Kusanyikeni pamoja na mje. Jikusanyeni pamoja pande zote kwenye dhabihu yangu, ambayo ninatoa kwa ajili yenu, dhabihu kubwa juu ya milima ya Israeli.+ Nanyi hakika mtakula nyama na kunywa damu.+ 18 Mtakula nyama ya wenye nguvu, nanyi mtakunywa damu ya wakuu wa dunia,+ kondoo-dume, na wana-kondoo,+ na mbuzi-dume, ngombe-dume wachanga,+ vinono wote wa Bashani.+ 19 Nanyi hakika mtakula mafuta mpaka mshibe+ na kunywa damu mpaka mlewe, kutokana na dhabihu yangu nitakayotoa kwa ajili yenu.” ’

20 “ ‘Nanyi mtashiba mezani pangu kwa farasi na waendesha-gari, watu wenye nguvu na mashujaa wa vita wa namna zote,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+

21 “ ‘Nami nitaweka utukufu wangu kati ya mataifa; na mataifa yote yatalazimika kuiona hukumu yangu ambayo nimeitenda+ na mkono wangu ambao nimeuweka katikati yao.+ 22 Na wale wa nyumba ya Israeli watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao kuanzia siku hiyo na kuendelea.+ 23 Nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba ilikuwa kwa sababu ya kosa lao kwamba wao, nyumba ya Israeli, walienda uhamishoni,+ kwa sababu walijiendesha kwa kukosa uaminifu kunielekea mimi, hivi kwamba nikawaficha wao uso wangu+ na kuwatia mkononi mwa wapinzani wao, nao wakawa wakianguka, wote hao, kwa upanga.+ 24 Niliwatendea kulingana na uchafu wao na kulingana na ukosaji wao,+ nami nikaendelea kuwaficha uso wangu.’

25 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Sasa nitawarudisha mateka wa Yakobo+ na kwa kweli niwe na rehema juu ya nyumba yote ya Israeli;+ nami nitajitoa kikamili kwa ajili ya jina langu takatifu.+ 26 Nao watakuwa wamechukua fedheha+ yao na ukosefu wao wote wa uaminifu ambao wamenitendea,+ wakati watakapokaa katika nchi yao kwa usalama,+ pasipo mtu yeyote wa kuwatetemesha.+ 27 Nitakapowarudisha kutoka katika vikundi vya watu nami kwa kweli niwakusanye pamoja kutoka katika nchi za adui zao,+ mimi pia nitajitakasa mwenyewe katikati yao mbele ya macho ya mataifa mengi.’+

28 “ ‘Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao, nitakapowapeleka uhamishoni kwa mataifa na kwa kweli niwarudishe pamoja kwenye nchi yao,+ hivi kwamba sitamwacha yeyote kati yao abaki huko.+ 29 Nami sitaendelea tena kuwaficha uso wangu,+ kwa sababu nitaimimina roho yangu juu ya nyumba ya Israeli,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

40 Katika mwaka wa 25 wa uhamisho+ wetu, mwanzoni mwa mwaka, siku ya 10 ya mwezi, katika mwaka wa 14 baada ya jiji kupigwa na kuangushwa,+ siku hiyohiyo mkono wa Yehova ukawa juu yangu,+ hivi kwamba akanileta mahali hapo.+ 2 Katika maono ya Mungu alinileta katika nchi ya Israeli na hatua kwa hatua akaniweka juu ya mlima mrefu sana,+ ambao juu yake palikuwa na kitu kama muundo wa jiji kuelekea kusini.+

3 Naye akanileta huko, na, tazama! alikuwapo mtu fulani. Sura yake ilikuwa kama shaba,+ naye alikuwa na kamba ya kitani mkononi mwake, na utete wa kupimia,+ naye alikuwa amesimama langoni. 4 Naye mtu huyo akaanza kuniambia: “Mwana wa binadamu,+ ona kwa macho yako, na kwa masikio yako usikie, na uweke moyo wako juu ya yote ninayokuonyesha, kwa sababu umeletwa hapa nipate kukuonyesha. Itangazie nyumba ya Israeli kila kitu unachokiona.”+

5 Na, tazama! kulikuwa na ukuta nje ya nyumba kuizunguka pande zote. Na katika mkono wa mtu huyo kulikuwa na utete wa kupimia wenye urefu wa mikono sita, na wenye kipimo cha mkono mmoja na cha upana wa kiganja kimoja. Naye akaanza kupima upana wa kitu kilichojengwa, utete mmoja; na kimo chake, utete mmoja.

6 Kisha akaja katika lango, ambalo upande wake wa mbele unaelekea mashariki,+ akapanda juu kwa kutumia ngazi zake. Naye akaanza kupima kizingiti cha lango hilo,+ upana wa utete mmoja, na kile kizingiti kingine, upana wa utete mmoja. 7 Na chumba cha walinzi kilikuwa na urefu wa utete mmoja na upana wa utete mmoja, na kati ya vyumba vya walinzi+ kulikuwa na kipimo cha mikono mitano; na kizingiti cha lango kando ya ukumbi wa lango kuelekea upande wa ndani kilikuwa utete mmoja.

8 Naye akapima ukumbi wa lango kuelekea upande wa ndani, utete mmoja.+ 9 Kwa hiyo akapima ukumbi wa lango, mikono minane; na nguzo zake za kando, mikono miwili; na ukumbi wa lango ulielekea upande wa ndani.

10 Na vyumba vya walinzi vya lango kuelekea mashariki vilikuwa vitatu upande huu na vitatu upande ule. Hivyo vitatu vilikuwa na kipimo kilekile, nazo nguzo za kando zilikuwa na kipimo kilekile, upande huu na upande ule.

11 Kisha akapima upana wa mwingilio wa lango, mikono kumi; urefu wa lango, mikono kumi na mitatu.

12 Na eneo lililozungushiwa ua mbele ya vyumba vya walinzi lilikuwa mkono mmoja, na kulikuwa na eneo la mkono mmoja kila upande lililozungushiwa ua. Na chumba cha mlinzi kilikuwa mikono sita upande huu na mikono sita upande ule.

13 Naye akapima lango kutoka kwenye dari ya chumba kimoja cha mlinzi mpaka kwenye dari ya kile kingine, upana wa mikono 25;+ mwingilio mmoja ulielekeana na mwingilio mwingine. 14 Kisha akafanya nguzo za kando za mikono 60, pia nguzo za kando za ua katika malango kuzunguka pande zote. 15 Na upande wa mbele wa lango la njia ya kuingilia mpaka upande wa mbele wa ukumbi wa lango la ndani ulikuwa mikono 50.

16 Na palikuwa na madirisha yenye viunzi vyenye upana tofauti+ kwa ajili ya vyumba vya walinzi na kwa ajili ya nguzo zao za kando kuelekea upande wa ndani wa lango kuzunguka pande zote, na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa ajili ya zile kumbi. Nayo madirisha yalikuwa yenye kuzunguka pande zote kuelekea upande wa ndani, na kwenye nguzo za kando palikuwa na maumbo ya mitende.+

17 Naye akanileta hatua kwa hatua ndani ya ua wa nje, na, tazama! palikuwa na vyumba vya kulia chakula,+ na sakafu ya mawe iliyofanywa kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote. Palikuwa na vyumba 30 vya kulia chakula juu ya ile sakafu ya mawe.+ 18 Nayo sakafu ya mawe kando ya malango ilikuwa sawa kabisa na urefu wa malango—ile sakafu ya chini ya mawe.

19 Naye akapima upana kutoka upande wa mbele wa lango la chini mpaka mbele ya ua wa ndani. Upande wake wa nje ulikuwa mikono mia moja, upande wa mashariki na upande wa kaskazini.

20 Na ua wa nje ulikuwa na lango ambalo upande wake wa mbele ulielekea kaskazini. Akapima urefu wake na upana wake. 21 Navyo vyumba vyake vya walinzi vilikuwa vitatu upande huu na vitatu upande ule. Na nguzo zake za kando na ukumbi wake zilikuwa kulingana na kipimo cha lango la kwanza. Urefu wake mikono 50, na upana wake mikono 25. 22 Na kipimo cha madirisha yake na ukumbi wake na maumbo yake ya mitende+ kilikuwa sawa na kipimo cha lango ambalo upande wake wa mbele unaelekea mashariki. Na kwa kutumia vipandio saba watu wangeweza kupanda kuingia ndani yake, na ukumbi wake ulikuwa mbele yake.

23 Na lango la ua wa ndani lilielekeana na lango la upande wa kaskazini; pia lile la upande wa mashariki. Naye akapima kutoka lango moja mpaka lango lingine mikono mia moja.

24 Naye akanileta hatua kwa hatua upande wa kusini,+ na, tazama! kulikuwa na lango upande wa kusini, naye akapima nguzo zake za kando na ukumbi wake kwa vipimo sawa na hivi. 25 Na palikuwa na madirisha kuzunguka pande zote juu yake na juu ya ukumbi wake, kama madirisha hayo. Urefu wake mikono 50, na upana wake mikono 25. 26 Na palikuwa na ngazi saba za kulipandia, na ukumbi wake ulikuwa mbele yake.+ Nalo lilikuwa na maumbo ya mitende, moja upande huu na lingine upande ule juu ya nguzo zake za kando.

27 Na ua wa ndani ulikuwa na lango upande wa kusini. Naye akapima kutoka lango mpaka lango upande wa kusini mikono mia moja. 28 Naye akanileta hatua kwa hatua mpaka ndani ya ua wa ndani kupitia lango la kusini. Naye akalipima lango la kusini kwa vipimo sawa na hivi. 29 Navyo vyumba vyake vya walinzi na nguzo zake za kando na ukumbi wake vilikuwa na vipimo sawa na hivi. Na palikuwa na madirisha kuzunguka pande zote juu yake na juu ya ukumbi wake. Urefu wake mikono 50, na upana wake mikono 25.+ 30 Na palikuwa na kumbi kuzunguka pande zote; urefu wake mikono 25, na upana wake mikono 5. 31 Na ukumbi wake ulielekea ua wa nje, na maumbo ya mitende yalikuwa kwenye nguzo zake za kando,+ na mpando wake ulikuwa vipandio vinane.+

32 Naye akanileta hatua kwa hatua ndani ya ua wa ndani kupitia njia ya mashariki, naye akapima lango kwa vipimo sawa na hivi. 33 Navyo vyumba vyake vya walinzi na nguzo zake za kando na ukumbi wake vilikuwa na vipimo sawa na hivi, hilo na ukumbi wake lilikuwa na madirisha kuzunguka pande zote juu. Urefu wake mikono 50, na upana wake mikono 25. 34 Na ukumbi wake ulielekea ua wa nje, na maumbo ya mitende yalikuwa kwenye nguzo zake za kando upande huu na upande ule. Na mpando wake ulikuwa vipandio vinane.

35 Naye akanileta ndani ya lango la kaskazini,+ naye akapima, kwa vipimo sawa na hivi,+ 36 vyumba vyake vya walinzi, nguzo zake za kando na ukumbi wake. Nalo lilikuwa na madirisha kuzunguka pande zote. Urefu wake mikono 50, na upana wake mikono 25. 37 Na kuelekea ua wake wa nje palikuwa na nguzo zake za kando, na maumbo ya mitende yalikuwa juu ya nguzo zake za kando upande huu na upande ule.+ Na mpando wake ulikuwa vipandio vinane.

38 Na chumba cha kulia chakula pamoja na mwingilio wake kilikuwa kando ya nguzo za kando za malango. Hapo ndipo walipokuwa wakioshea toleo zima la kuteketezwa.+

39 Na katika ukumbi wa lango palikuwa na meza mbili upande huu na meza mbili upande ule, za kuchinjia juu yake lile toleo zima la kuteketezwa+ na lile toleo la dhambi+ na lile toleo la hatia.+ 40 Na upande wa nje, mtu anapopanda mpaka kwenye mwingilio wa lango la kaskazini, palikuwa na meza mbili. Na ule upande mwingine wa ukumbi wa lango palikuwa na meza mbili. 41 Palikuwa na meza nne hapa na meza nne pale kando ya lango—meza nane, ambazo walikuwa wakichinjia juu yake. 42 Na zile meza nne kwa ajili ya toleo zima la kuteketezwa zilikuwa za mawe yaliyochongwa. Urefu wake mkono mmoja na nusu, na upana wake mkono mmoja na nusu, na kimo kilikuwa mkono mmoja. Juu yake pia walikuwa wakiweka vifaa ambavyo walikuwa wakitumia kuchinjia toleo zima la kuteketezwa na ile dhabihu. 43 Na rafu za kuwekea vitu zilikuwa na upana wa kiganja kimoja, zikiwa zimefungwa kwa uthabiti upande wa ndani, kuzunguka pande zote; na juu ya meza walikuwa wakiweka nyama ya toleo la zawadi.+

44 Na upande wa nje wa lango la ndani palikuwa na vyumba vya kulia chakula vya waimbaji,+ katika ua wa ndani, ulio upande wa lango la kaskazini. Na upande wake wa mbele ulielekea kusini. Palikuwa na kimoja upande wa lango la mashariki. Upande wake wa mbele ulielekea kaskazini.

45 Naye akaniambia: “Hiki, chumba cha kulia chakula ambacho upande wake wa mbele unaelekea kusini, ni cha makuhani wanaotimiza wajibu wa nyumba.+ 46 Na chumba cha kulia chakula ambacho upande wake wa mbele unaelekea kaskazini ni cha makuhani wanaotimiza wajibu wa madhabahu.+ Hao ni wana wa Sadoki,+ ambao, kutoka kwa wana wa Lawi, wanamkaribia Yehova ili kumhudumia.”+

47 Naye akapima ua wa ndani. Urefu wake ulikuwa mikono 100, na upana mikono 100, mraba. Nayo madhabahu ilikuwa mbele ya nyumba.

48 Naye akanileta ndani ya ukumbi wa nyumba, naye akapima nguzo ya kando ya ukumbi,+ mikono 5 upande huu na mikono 5 upande ule. Na upana wa lango ulikuwa mikono 3 upande huu na mikono 3 upande ule.

49 Urefu wa ukumbi ulikuwa mikono 20, na upana wake mikono 11. Nao walikuwa wakiupanda kwa kutumia ngazi. Na palikuwa na nguzo kando ya miimo ya kando, mmoja hapa na mmoja pale.+

41 Naye akanileta hekaluni, akapima zile nguzo za kando, mikono 6 upana wake hapa na mikono 6 upana wake pale, upana wa nguzo ya kando. 2 Nao upana wa mwingilio ulikuwa mikono 10, na sehemu za kando za mwingilio zilikuwa mikono 5 hapa na mikono mitano pale. Naye akapima urefu wake, mikono 40; na upana, mikono 20.

3 Naye akaingia ndani na kupima nguzo ya kando ya mwingilio, mikono 2; na mwingilio, mikono 6; na upana wa mwingilio ulikuwa mikono 7. 4 Naye akapima urefu wake, mikono 20; na upana wake, mikono 20,+ mbele ya hekalu. Kisha akaniambia: “Hapa ndipo Patakatifu Zaidi.”+

5 Naye akapima ukuta wa nyumba, mikono sita. Na upana wa chumba cha kando ulikuwa mikono minne, kuzunguka pande zote; uliizunguka nyumba yote pande zote.+ 6 Navyo vyumba vya kando vilikuwa chumba cha kando juu ya chumba cha kando, ghorofa tatu, na kila sehemu ikiwa na 30; navyo viliingia ndani ya ukuta wa nyumba, yaani, vyumba vya kando kuzunguka pande zote, ili vipate kushikiliwa, lakini havikushikiliwa katika ukuta wa nyumba.+ 7 Navyo vilipanuka kuelekea upande wa nje na kugeuka kuelekea sehemu ya juu na ile iliyo juu yake mpaka kwenye vile vyumba vya kando, kwa maana njia inayopinda-pinda ya nyumba ile ilienda juu na juu kuizunguka nyumba pande zote.+ Kwa hiyo nyumba ilipanuka kuelekea juu, na kutoka ghorofa ya chini kabisa mtu angeweza kupanda mpaka ghorofa ya juu kabisa,+ kupitia ghorofa ya katikati.

8 Nami nikaona kwamba kulikuwa na jukwaa refu kwa ajili ya nyumba kuizunguka pande zote. Nayo misingi ya nguzo za kando, ilikuwa utete mzima wa mikono sita mpaka kwenye mahali pa kuungania.+ 9 Upana wa ukuta uliokuwa wa chumba cha kando, upande wa nje, ulikuwa mikono mitano. Na kulikuwa na nafasi iliyoachwa wazi kwa ujenzi wa vyumba vya kando vilivyokuwa vya nyumba hiyo.

10 Na kati ya vile vyumba vya kulia chakula+ upana ulikuwa mikono 20 kuizunguka nyumba, pande zote. 11 Nao mwingilio wa chumba cha kando ulikuwa katika upande wa ile nafasi iliyoachwa wazi, mwingilio mmoja ukielekea kaskazini na mwingilio mmoja upande wa kusini; nao upana wa eneo la nafasi iliyoachwa wazi ulikuwa mikono mitano, kuzunguka pande zote.

12 Nalo jengo lililokuwa mbele ya eneo lililotengwa, ambalo upande wake wa kando ulielekea magharibi, lilikuwa na upana wa mikono 70. Nao ukuta wa jengo ulikuwa na upana wa mikono 5, kuzunguka pande zote; nao urefu wake ulikuwa mikono 90.

13 Naye akaipima nyumba, mikono mia moja urefu wake; na lile eneo lililotengwa na jengo na kuta zake, mikono mia moja urefu wake. 14 Nao upana wa upande wa mbele wa nyumba na lile eneo lililotengwa katika upande wa mashariki ulikuwa mikono mia moja.

15 Naye akapima urefu wa jengo mbele ya lile eneo lililotengwa lililokuwa nyuma yake na mabaraza yake upande huu na upande ule, mikono mia moja.

Pia hekalu na mahali pa ndani zaidi+ na zile kumbi za ua; 16 vizingiti, na madirisha yenye viunzi vyenye upana tofauti,+ na mabaraza yalizunguka hizo tatu pande zote. Mbele ya kizingiti kulikuwa na mbao zilizofunika kuzunguka pande zote,+ na kutoka kwenye sakafu mpaka madirishani; nayo madirisha yalikuwa yamefunikwa. 17 Mpaka juu ya mwingilio na kufikia nyumba ya ndani na upande wa nje na juu ya ukuta wote kuzunguka pande zote, kwenye nyumba ya ndani na nje, kulikuwa na vipimo, 18 hata makerubi+ waliochongwa na maumbo ya mitende,+ pakiwa umbo la mtende katikati ya kerubi na kerubi, naye kerubi alikuwa na nyuso mbili.+ 19 Nao uso wa mwanadamu ulielekea umbo la mtende upande huu, na uso wa mwana-simba mwenye manyoya shingoni ulielekea umbo la mtende upande ule,+ wakiwa wamechongwa juu ya nyumba yote kuizunguka pande zote. 20 Kutoka sakafuni mpaka juu ya mwingilio kulikuwa na makerubi waliochongwa na maumbo ya mitende, kwenye ukuta wa hekalu.

21 Kwa habari ya hekalu, miimo ya mlango ilikuwa mraba;+ na mbele ya mahali patakatifu kulikuwa na sura kama sura ifuatayo: 22 ile madhabahu ya mbao ilikuwa na kimo cha mikono mitatu, nao urefu wake ulikuwa mikono miwili, nayo ilikuwa na miimo yake ya pembeni.+ Nao urefu wake na kuta zake zilikuwa za mbao. Naye akaniambia: “Hii ndiyo meza iliyo mbele za Yehova.”+

23 Nalo hekalu na mahali patakatifu palikuwa na milango miwili.+ 24 Na sehemu mbili za mlango zilikuwa kwenye milango, hizo mbili zikiwa zenye kukunjika. Mlango mmoja ulikuwa na sehemu mbili za mlango zenye kukunjika, na ule mlango mwingine ulikuwa na sehemu mbili za mlango zenye kukunjika. 25 Na juu yake, juu ya milango ya hekalu, palifanyizwa makerubi na maumbo ya mitende,+ kama ilivyofanywa juu ya kuta, na kulikuwa na kipaa cha mbao juu ya upande wa mbele wa ukumbi upande wa nje. 26 Na kulikuwa na madirisha yenye kiunzi chenye upana tofauti+ na maumbo ya mitende upande huu na upande ule kandokando ya kumbi za kando na vyumba vya kando vya nyumba na vile vipaa.

42 Naye akanileta hatua kwa hatua+ mpaka kwenye ua wa nje katika njia inayoelekea kaskazini.+ Naye akanileta kwenye jengo la chumba cha kulia chakula+ lililokuwa mbele ya eneo lililotengwa+ na ambalo lilikuwa mbele ya jengo lililoelekea kaskazini. 2 Mbele ya urefu wa mikono 100 kulikuwa na mwingilio wa kaskazini, nao upana ulikuwa mikono 50. 3 Mbele ya ile mikono 20 iliyokuwa ya ua wa ndani+ na mbele ya sakafu ya mawe+ iliyokuwa ya ua wa nje kulikuwa na baraza+ lenye kuangaliana na baraza katika ghorofa tatu. 4 Na mbele ya vyumba vya kulia chakula palikuwa na njia yenye upana wa mikono kumi kuelekea ndani,+ njia ya mkono mmoja, nayo miingilio yake ilielekea kaskazini. 5 Na kwa habari ya vyumba vya kulia chakula, vya juu zaidi vilikuwa vifupi, kwa maana yale mabaraza yalivipunguza, kuliko yalivyopunguza vile vya chini zaidi na kuliko yalivyopunguza vile vya katikati, katika jengo hilo. 6 Kwa maana yalikuwa katika ghorofa tatu,+ nayo hayakuwa na nguzo kama nguzo za zile nyua. Ndiyo sababu sehemu kubwa zaidi ilipunguzwa katika vile vya chini zaidi na katika vile vya katikati kutoka ukutani.

7 Nao ukuta wa mawe uliokuwa nje ulikuwa karibu na vyumba vya kulia chakula kuelekea ua wa nje mbele ya vile vyumba vingine vya kulia chakula. Urefu wake ulikuwa mikono 50. 8 Kwa maana urefu wa vyumba vya kulia chakula vilivyokuwa vikielekea ua wa nje ulikuwa mikono 50, na, tazama! mbele ya hekalu mikono 100. 9 Na kutoka upande wa chini wa vyumba hivyo vya kulia chakula njia ya kuingilia ilielekea mashariki, mtu anapoingia akitoka ua wa nje.

10 Katika upana wa ule ukuta wa mawe kuelekea mashariki, mbele ya lile eneo lililotengwa+ na mbele ya jengo, kulikuwa na vyumba vya kulia chakula.+ 11 Na kulikuwa na njia mbele yake inayofanana na vile vyumba vya kulia chakula vilivyokuwa vikielekea kaskazini,+ hivyo ndivyo urefu wake ulivyokuwa na ndivyo upana wake ulivyokuwa; na milango yake yote ya kutokea ilifanana, nazo ramani zake zilifanana na miingilio yake ilifanana. 12 Na kama ilivyokuwa ile miingilio ya vyumba vya kulia chakula iliyoelekea kusini ndivyo ulivyokuwa ule mwingilio mbele ya njia, njia iliyo mbele ya ukuta unaolingana wa mawe kuelekea mashariki, mtu anapoiingia.+

13 Naye akaniambia: “Vyumba vya kulia chakula vya kaskazini na vyumba vya kulia chakula vya kusini ambavyo viko mbele ya eneo lililotengwa,+ hivyo ndivyo vyumba vya kulia chakula vilivyo vitakatifu, ambamo makuhani wanaomkaribia+ Yehova hula vitu vitakatifu zaidi.+ Humo wao huweka vitu vilivyo vitakatifu zaidi na toleo la nafaka na toleo la dhambi na toleo la hatia, kwa sababu mahali hapo ni patakatifu.+ 14 Wakati hao, makuhani, wakiisha kuingia, wao pia hawatatoka nje kutoka katika mahali patakatifu mpaka kwenye ua wa nje, lakini humo watayaweka mavazi yao ambayo wao huyavaa kwa ukawaida wakihudumu,+ kwa maana hayo ni kitu kitakatifu. Watavaa mavazi mengine,+ nao watakikaribia kile kinachohusiana na watu.”

15 Naye akamaliza vipimo vya nyumba ya ndani, naye akanitoa nje kupitia lango ambalo upande wake wa mbele ulielekea mashariki,+ naye akalipima kuzunguka pande zote.

16 Akapima upande wa mashariki kwa ule utete wa kupimia. Ulikuwa tete mia tano, kwa utete wa kupimia,+ kuzunguka pande zote.

17 Akapima upande wa kaskazini, tete mia tano, kwa utete wa kupimia, kuzunguka pande zote.

18 Upande wa kusini akaupima, tete mia tano, kwa utete wa kupimia.

19 Akazunguka upande wa magharibi. Akapima tete mia tano, kwa utete wa kupimia.

20 Akazipima zile pande nne. Kulikuwa na ukuta kuzunguka pande zote,+ wenye urefu wa tete mia tano na upana wa tete mia tano,+ ili kutenganisha kilicho kitakatifu na kilicho najisi.+

43 Kisha akanifanya niende kwenye lango, lango linaloelekea mashariki.+ 2 Na, tazama! utukufu+ wa Mungu wa Israeli ulikuwa ukija kutoka upande wa mashariki,+ nayo sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi;+ nayo dunia yenyewe ikang’aa kwa sababu ya utukufu wake.+ 3 Nayo ilionekana kama maono niliyokuwa nimeona,+ kama maono niliyoona nilipokuja kuliharibu jiji;+ pia kulionekana vitu kama nilivyoona kando ya mto Kebari,+ nami nikaanguka kifudifudi.

4 Na utukufu+ wa Yehova ukaingia ndani ya Nyumba kupitia lango ambalo upande wake wa mbele ulielekea mashariki.+ 5 Na roho ikaniinua+ na kuniingiza ndani ya ua wa ndani, na, tazama! Nyumba hiyo ilikuwa imejaa utukufu wa Yehova.+ 6 Nami nikaanza kusikia mtu akisema nami kutoka katika Nyumba+ hiyo, naye mtu huyo akaja kusimama kando yangu.+ 7 Naye akaniambia:

“Mwana wa binadamu, hapa ndipo mahali pa kiti changu cha ufalme+ na mahali pa nyayo za miguu yangu,+ ambapo nitakaa katikati ya wana wa Israeli mpaka wakati usio na kipimo;+ nao, nyumba ya Israeli, hawataendelea tena kulitia unajisi jina langu takatifu,+ wao na wafalme wao,+ kwa uasherati wao na kwa mizoga+ ya wafalme wao wakati wanapokufa, 8 kwa kuweka kwao kizingiti chao pamoja na kizingiti changu na mwimo wa mlango wao kando ya mwimo wa mlango wangu, kukiwa na ukuta kati yangu na wao.+ Nao walilitia unajisi jina langu takatifu kwa machukizo yao ambayo walifanya,+ hivi kwamba nikawaangamiza katika hasira yangu.+ 9 Sasa na wauondolee mbali nami uasherati+ wao na mizoga ya wafalme wao,+ nami hakika nitakaa katikati yao mpaka wakati usio na kipimo.+

10 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, iambie nyumba ya Israeli kuhusu ile Nyumba,+ ili wafedheheke kwa sababu ya makosa yao,+ nao lazima wapime kielelezo hicho. 11 Na ikiwa kwa kweli watafedheheka kwa sababu ya mambo yote ambayo wamefanya, ramani ya ile Nyumba,+ na mpangilio wake na njia zake za kutokea na za kuingilia, na ramani zake zote na vipimo vyake vyote, na ramani zake zote na sheria zake zote uwajulishe na kuziandika machoni pao, ili wapate kuona ramani zake zote na vipimo vyake vyote nao kwa kweli wafanye hivyo.+ 12 Hii ndiyo sheria ya Nyumba hiyo. Juu ya mlima eneo lake lote kuzunguka pande zote ni kitu kitakatifu zaidi.+ Tazama! Hii ndiyo sheria ya Nyumba hiyo.

13 “Na hivi ndivyo vipimo vya madhabahu kwa kipimo cha mikono,+ mkono mmoja ukiwa ni mkono mmoja na upana wa kiganja+ kimoja. Nayo sehemu yake ya chini ni mkono mmoja. Na mkono mmoja upana wake. Na mpaka wake uko juu ya mdomo wake kuzunguka pande zote, shubiri moja. Na huo ndio msingi wa madhabahu. 14 Na kutoka sehemu ya chini kwenye sakafu mpaka kwenye rafu ya chini inayozunguka kuna mikono miwili, nao upana ni mkono mmoja. Na kutoka ile rafu ndogo mpaka kwenye ile rafu kubwa inayozunguka kuna mikono minne, nao upana wake ni mkono mmoja. 15 Nayo majiko ya madhabahu ni mikono minne, na kutoka kwenye majiko ya madhabahu kuelekea juu kuna zile pembe nne.+ 16 Nayo majiko ya madhabahu yana urefu wa mikono kumi na miwili, na upana wa mikono kumi na miwili,+ mraba pande zake nne.+ 17 Nayo rafu inayozunguka ina urefu wa mikono kumi na minne, na upana wa mikono kumi na minne, pande zake nne; nao mpaka unaoizunguka ni nusu mkono, nayo sehemu yake ya chini ni mkono mmoja kuzunguka pande zote.

“Nazo ngazi zake zinaelekea mashariki.”

18 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Hizi ndizo sheria za madhabahu katika siku ile ya kuifanya, ili kutoa juu yake matoleo mazima ya kuteketezwa+ na kunyunyiza damu juu yake.’+

19 “ ‘Nawe utawapa makuhani Walawi,+ ambao ni uzao wa Sadoki,+ wale wanaonikaribia mimi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘ili kunihudumia, ng’ombe-dume mchanga, mwana wa mifugo, awe toleo la dhambi.+ 20 Nawe utachukua sehemu ya damu yake na kuitia kwenye zile pembe zake nne na juu ya ncha nne za rafu inayozunguka na juu ya mpaka unaozunguka pande zote na kuitakasa kutokana na dhambi+ na kufanya upatanisho kwa ajili yake.+ 21 Nawe utamchukua yule ng’ombe-dume mchanga, lile toleo la dhambi, na lazima mtu aliteketeze katika mahali palipochaguliwa pa ile Nyumba, nje ya patakatifu.+ 22 Na siku ya pili utaleta karibu dume la mbuzi, ambaye hana kasoro, awe toleo la dhambi; nao wataitakasa madhabahu kutokana na dhambi kama vile walivyoitakasa kutokana na dhambi kwa yule ng’ombe-dume mchanga.’

23 “ ‘Wakati utakapomaliza kutakasa kutokana na dhambi utamleta karibu ng’ombe-dume mchanga, mwana wa mifugo, ambaye hana kasoro, na kondoo-dume kutoka katika kundi, ambaye hana kasoro. 24 Nawe utawaleta karibu mbele za Yehova, nao makuhani watatupa chumvi juu yao na kuwatoa+ kwa Yehova wakiwa toleo zima la kuteketezwa. 25 Kwa siku saba utamtoa mbuzi-dume akiwa toleo la dhambi kila siku;+ na ng’ombe-dume mchanga, mwana wa mifugo, na kondoo-dume kutoka katika kundi, ambao hawana kasoro, watawatoa. 26 Kwa siku saba watafanya upatanisho+ kwa ajili ya madhabahu, nao wataitakasa na kuiweka rasmi. 27 Nao watamaliza siku hizo. Na itakuwa kwamba katika siku ya nane+ na kuanzia hapo na kuendelea makuhani watatoa juu ya madhabahu matoleo yenu mazima ya kuteketezwa na dhabihu zenu za ushirika; nami hakika nitapendezwa nanyi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

44 Naye akanirudisha kupitia lango la patakatifu, lile la nje linaloelekea mashariki,+ nalo lilikuwa limefungwa.+ 2 Ndipo Yehova akaniambia: “Lango hili, litakaa likiwa limefungwa. Halitafunguliwa, na hakuna mtu wa vivi hivi tu atakayeliingilia; kwa maana Yehova mwenyewe, Mungu wa Israeli,+ ameliingilia, nalo litakaa likiwa limefungwa. 3 Hata hivyo, mkuu+—kwa kuwa yeye ni mkuu ataketi humo, ili ale mkate mbele za Yehova.+ Ataingia kupitia ukumbi wa lango, na kupitia hapo atatoka.”+

4 Naye sasa akanileta kupitia lango la kaskazini mpaka mbele ya ile Nyumba, nipate kuona, na, tazama! utukufu wa Yehova ulikuwa umeijaza nyumba ya Yehova.+ Nami nikaanguka kifudifudi.+ 5 Ndipo Yehova akaniambia: “Mwana wa binadamu, weka moyoni mwako+ na uone kwa macho yako, na kwa masikio yako usikie yote ninayokuambia kuhusu kanuni zote za nyumba ya Yehova na kuhusu sheria zake zote, nawe utauweka moyo wako juu ya njia ya kuingilia ya ile Nyumba pamoja na mahali pote pa kutokea pa patakatifu. 6 Nawe utamwambia Uasi,+ nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Inatosha, kwa sababu ya machukizo yenu yote, Ee nyumba ya Israeli,+ 7 mnapowaingiza ndani wageni ambao hawajatahiriwa moyoni na ambao hawajatahiriwa katika mwili,+ ili wawe ndani ya patakatifu pangu na kupatia unajisi, naam, nyumba yangu; mnapotoa mkate+ wangu, mafuta+ na damu,+ huku wakiendelea kuvunja agano langu kwa sababu ya machukizo yenu yote.+ 8 Wala hamjautunza wajibu wa vitu vyangu vitakatifu,+ wala hamkuwaweka wengine kwa ajili yenu wawe watunzaji wa wajibu wangu katika patakatifu pangu.” ’+

9 “ ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Hakuna mgeni yeyote, ambaye hajatahiriwa moyoni na ambaye hajatahiriwa katika mwili, atakayeingia ndani ya patakatifu pangu, yaani, mgeni yeyote aliye katikati ya wana wa Israeli.” ’+

10 “ ‘Lakini Walawi walioenda mbali nami+ wakati ambapo Israeli, aliyeondoka akaenda mbali nami, alienda kufuatilia sanamu zao za mavi, wao pia lazima wachukue kosa lao.+ 11 Na katika patakatifu pangu watakuwa wahudumu katika vyeo vya uangalizi juu ya malango ya ile Nyumba na wahudumu kwenye ile Nyumba.+ Wao wenyewe watachinja toleo zima la kuteketezwa na dhabihu kwa ajili ya watu,+ na wao wenyewe watasimama mbele yao ili kuwahudumia.+ 12 Kwa sababu waliendelea kuwahudumia mbele ya sanamu zao za mavi+ na kuwa kikwazo cha kuingiza ndani ya dhambi kwa nyumba ya Israeli,+ ndiyo sababu nimeuinua mkono wangu juu yao,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nao watalichukua kosa lao. 13 Nao hawatanikaribia ili kutenda kama kuhani kwangu au kukaribia chochote kati ya vitu vyangu vilivyo vitakatifu,+ vilivyo vitakatifu zaidi, nao watachukua fedheha yao na machukizo yao waliyoyafanya.+ 14 Nami hakika nitawafanya wao kuwa watunzaji wa wajibu wa ile Nyumba, kuhusu utumishi wake wote na kuhusu yote ambayo yanapasa kufanywa ndani yake.’+

15 “ ‘Nao makuhani Walawi,+ wana wa Sadoki,+ ambao walitunza wajibu wa patakatifu pangu wakati ambapo wana wa Israeli waliondoka wakaenda mbali nami,+ wao wenyewe watanikaribia na kunihudumia, nao watasimama mbele zangu+ na kunitolea mafuta+ na damu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 16 ‘Hao ndio watakaoingia katika patakatifu pangu,+ na wao wenyewe wataikaribia meza yangu ili kunihudumia,+ nao watauangalia wajibu wangu.+

17 “ ‘Na itatukia kwamba watakapoingia ndani ya malango ya ua wa ndani, wanapaswa kuvaa mavazi ya kitani, na wasivae sufu yoyote wanapohudumu katika malango ya ua wa ndani na wakiwa ndani.+ 18 Vitambaa vya kichwa vya kitani ndivyo vitakavyokuwa kichwani pao,+ na suruali za kitani ndizo zitakazokuwa viunoni mwao.+ Wasijifunge chochote ambacho husababisha jasho. 19 Na wanapoenda kwenye ua wa nje, hata kwenye ua wa nje kwa watu, wanapaswa kuyavua mavazi yao waliyokuwa wameyavaa wakihudumu,+ nao watayaweka kwenye vyumba vitakatifu vya kulia chakula+ na kuvaa mavazi mengine, ili wasije wakawatakasa watu kwa mavazi yao.+ 20 Nao hawapaswi kuvinyoa vichwa vyao,+ na nywele za kichwa hawapaswi kuziacha ziwe ndefu. Kwa vyovyote vile wanapaswa wazikate nywele za kichwa chao.+ 21 Wala makuhani wowote wasinywe divai yoyote wanapoingia ndani ya ua wa ndani.+ 22 Nao hawatamwoa mjane au mwanamke yeyote aliyetalikiwa,+ lakini wanaweza kuoa mabikira wa uzao wa nyumba ya Israeli+ au mjane ambaye ni mjane wa kuhani.’

23 “ ‘Nao watawafundisha watu wangu tofauti kati ya kitu kitakatifu na kitu najisi; nao watawajulisha watu tofauti kati ya kitu ambacho si safi na kitu safi.+ 24 Na katika kesi wao wenyewe watasimama ili kuhukumu;+ wataihukumu pia kwa maamuzi yangu ya hukumu.+ Nazo sheria zangu na kanuni zangu kuhusiana na majira yangu yote ya sherehe+ watazishika, nazo sabato zangu watazitakasa.+ 25 Wala asiingie kwa mtu aliyekufa ajitie uchafu, lakini kwa ajili ya baba au mama au mwana au binti au ndugu au dada ambaye hajaolewa wanaweza kujitia uchafu.+ 26 Na baada ya yeye kutakaswa, wanapaswa kumhesabia siku saba.+ 27 Na katika siku atakayoingia ndani ya patakatifu, ndani ya ua wa ndani, ili kuhudumu ndani ya patakatifu, anapaswa kutoa toleo lake la dhambi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

28 “ ‘Nao utakuwa urithi wao: Mimi ndiye urithi wao.+ Nanyi msiwape mali yoyote katika Israeli: Mimi ndiye mali yao. 29 Toleo la nafaka na toleo la dhambi na toleo la hatia—hao ndio watakaokula hayo.+ Na kila kitu kilichotolewa katika Israeli—kitakuwa chao.+ 30 Na ya kwanza kati ya matunda ya kwanza yaliyoiva ya kila kitu na kila mchango wa kila kitu kutoka katika michango yenu yote—yatakuwa ni ya makuhani;+ na matunda ya kwanza ya unga wenu wenye chenga-chenga mtawapa makuhani,+ ili kufanya baraka ikae juu ya nyumba yako.+ 31 Makuhani wasile mnyama yeyote aliyekufa tayari wala kiumbe chochote kilichoraruliwa vipande-vipande kati ya viumbe vinavyoruka au kati ya wanyama.’+

45 “ ‘Na wakati ninyi mtakapoigawa nchi iwe urithi,+ mtamtolea Yehova mchango,+ fungu takatifu kutoka katika nchi;+ urefu wake utakuwa mikono 25,000, nao upana wake 10,000.+ Litakuwa fungu takatifu katika mipaka yake yote kuzunguka pande zote. 2 Kutoka katika hilo kutakuwako kwa ajili ya mahali patakatifu fungu la urefu wa 500 kwa upana wa 500, likiwa mraba kuzunguka pande zote;+ nalo litakuwa na kiwanja cha malisho cha mikono 50 kila upande.+ 3 Na kutoka katika kipimo hicho utapima urefu wa 25,000 na upana wa 10,000, na patakatifu patakuwa ndani yake, kitu kitakatifu zaidi.+ 4 Litakuwa fungu takatifu kutoka katika nchi kwa ajili ya makuhani wenyewe,+ wahudumu wa patakatifu, wale wanaokaribia ili kumhudumia Yehova.+ Na hapo patakuwa mahali pa nyumba kwa ajili yao, na mahali patakatifu kwa ajili ya patakatifu.

5 “ ‘Urefu utakuwa 25,000 nao upana wake utakuwa 10,000.+ Patakuwa pa Walawi, wahudumu wa ile Nyumba. Nao watamiliki vyumba 20 vya kulia chakula.+

6 “ ‘Na miliki ya jiji, mtatoa upana wa 5,000 na urefu wa 25,000, sawasawa na mchango mtakatifu.+ Itakuwa ya nyumba yote ya Israeli.

7 “ ‘Na kwa ajili ya mkuu kutakuwako upande huu na upande ule wa mchango mtakatifu na wa miliki ya jiji, mbali na ule mchango mtakatifu+ na ile miliki ya jiji, kitu fulani upande wa magharibi kuelekea magharibi na kitu upande wa mashariki kuelekea mashariki. Nao urefu utakuwa sawasawa na moja kati ya yale mafungu, kutoka mpaka wa magharibi hadi mpaka wa mashariki.+ 8 Nayo nchi, itakuwa mali yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataendelea kuwatendea vibaya tena watu wangu,+ nao wataipa nyumba ya Israeli nchi hiyo kulingana na makabila yao.’+

9 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Imetosha, enyi wakuu wa Israeli!’+

“ ‘Ondoeni jeuri na uporaji,+ na mfanye haki na uadilifu.+ Acheni kutumia uwezo vibaya kuchukua vitu vya watu wangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 10 ‘Mnapaswa kuwa na mizani sahihi na efa sahihi na kipimo sahihi cha bathi.+ 11 Na kuhusu efa na kipimo cha bathi, kutakuwa na kiwango kimoja kamili, ili kipimo cha bathi kichukue sehemu ya kumi ya homeri na sehemu ya kumi ya homeri ichukue efa;+ kuhusiana na homeri, kiwango chake kinachohitajiwa kinapaswa kuwa hicho. 12 Nayo shekeli+ ni gera 20.+ Shekeli 20, shekeli 25, shekeli 15 ndizo zitakazokuwa mane moja kwako.’

13 “ ‘Huu ndio mchango ambao utautoa, sehemu ya sita ya efa kutoka katika homeri ya ngano, na sehemu ya sita ya efa kutoka katika homeri ya shayiri; 14 na kuhusu posho la mafuta, kuna kipimo cha bathi cha mafuta. Bathi ni sehemu ya kumi ya kori. Bathi kumi ni homeri moja; kwa sababu bathi kumi ni homeri moja. 15 Na kondoo mmoja kutoka katika kundi, kutoka katika mifugo mia mbili ya Israeli,+ kwa ajili ya toleo la nafaka+ na kwa ajili ya toleo zima la kuteketezwa+ na kwa ajili ya dhabihu za ushirika,+ ili kufanya upatanisho kwa ajili yao,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

16 “ ‘Nao watu wote wa nchi, watakuwa na wajibu wa kutoa mchango+ huu kwa mkuu katika Israeli.+ 17 Naye mkuu+ atakuwa na wajibu juu ya matoleo mazima ya kuteketezwa+ na toleo la nafaka+ na toleo la kinywaji+ wakati wa sherehe+ na wakati wa miezi mipya+ na wakati wa sabato,+ wakati wa majira yote ya sherehe ya nyumba ya Israeli.+ Yeye ndiye atakayetoa toleo la dhambi na toleo la nafaka na toleo zima la kuteketezwa na dhabihu za ushirika, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.’

18 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi huo, utamchukua ng’ombe-dume mchanga, mwana wa mifugo, ambaye hana kasoro,+ nawe utapatakasa patakatifu kutokana na dhambi.+ 19 Naye kuhani atachukua sehemu ya damu ya toleo la dhambi na kuiweka kwenye mwimo wa mlango+ wa ile Nyumba na juu ya zile pembe nne za rafu ya madhabahu+ inayozunguka na juu ya mwimo wa lango la ua wa ndani. 20 Na hivyo ndivyo utakavyofanya katika siku ya saba ya mwezi kwa sababu ya mtu yeyote anayefanya kosa+ na kwa sababu ya mtu yeyote ambaye hana uzoefu; nanyi mtafanya upatanisho kwa ajili ya ile Nyumba.+

21 “ ‘Katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi huo, mtafanya pasaka.+ Hiyo ikiwa ni sherehe ya siku saba, keki zisizo na chachu ndizo zitakazoliwa.+ 22 Na katika siku hiyo, kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi, mkuu atatoa ng’ombe-dume mchanga kuwa toleo la dhambi.+ 23 Na kwa siku hizo saba za sherehe+ atamtolea Yehova toleo zima la kuteketezwa la ng’ombe-dume saba wachanga na kondoo-dume saba, ambao hawana kasoro, kila siku kwa siku saba,+ na kuwa toleo la dhambi atatoa dume la mbuzi kila siku.+ 24 Naye atatoa toleo la nafaka la efa kwa ajili ya yule ng’ombe-dume mchanga na efa kwa ajili ya yule kondoo-dume, na, kwa habari ya mafuta, hini moja kwa efa.+

25 “ ‘Katika mwezi wa saba, katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo, wakati wa sherehe,+ atatoa vitu vivyo hivyo kwa siku saba,+ vivyo hivyo kwa habari ya toleo la dhambi, toleo zima la kuteketezwa, na toleo la nafaka na mafuta.’ ”

46 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa habari ya lango la ua wa ndani linaloelekea mashariki,+ litakaa likiwa limefungwa+ kwa siku sita za kazi,+ na katika siku ya sabato litafunguliwa, na katika siku ya mwezi mpya litafunguliwa.+ 2 Naye mkuu ataingia kupitia kwenye ukumbi wa lango,+ kutoka nje, na kusimama kando ya mwimo wa lango;+ nao makuhani watatoa toleo lake zima la kuteketezwa na dhabihu zake za ushirika, naye atainama penye kizingiti cha lango,+ naye atatoka nje, lakini lango lenyewe halitafungwa mpaka jioni. 3 Nao watu wa nchi watainama kwenye kizingiti cha lango hilo katika siku za sabato na katika miezi mipya, mbele za Yehova.+

4 “ ‘Nalo toleo zima la kuteketezwa ambalo mkuu atamtolea Yehova katika siku ya sabato litakuwa wana-kondoo sita ambao hawana kasoro na kondoo-dume mmoja ambaye hana kasoro;+ 5 na toleo la nafaka la efa moja kwa ajili ya yule kondoo-dume,+ na kwa ajili ya wale wana-kondoo toleo la nafaka kulingana na uwezo wake wa kutoa,+ na, kwa habari ya mafuta, hini moja kwa efa.+ 6 Na siku ya mwezi mpya+ kutakuwa na ng’ombe-dume mchanga, mwana wa mifugo, ambaye hana kasoro, na wana-kondoo sita na kondoo-dume mmoja; hawapaswi kuwa na kasoro.+ 7 Naye atatoa toleo la nafaka la efa moja kwa ajili ya yule ng’ombe-dume mchanga na efa moja kwa ajili ya yule kondoo-dume, na kwa ajili ya wale wana-kondoo atatoa kulingana na uwezo wake; na, kwa habari ya mafuta, hini moja kwa efa.+

8 “ ‘Naye mkuu+ anapoingia ndani, ataingia kupitia njia ya ukumbi wa lango, naye atatoka nje kupitia njia hiyo.+ 9 Na watu wa nchi hiyo wanapoingia ndani mbele za Yehova katika majira ya sherehe,+ yeye anayeingia kupitia njia ya lango la kaskazini+ ili kuinama atatoka nje kupitia njia ya lango la kusini;+ na yule anayeingia kupitia njia ya lango la kusini atatoka nje kupitia njia ya lango la kaskazini. Mtu yeyote asirudi kupitia njia ya lango aliloingilia, kwa maana anapaswa kutoka nje moja kwa moja mbele yake. 10 Na kwa habari ya mkuu aliye katikati yao, wakati wao wanapoingia ndani, yeye ataingia ndani; na wakati wao wanapotoka nje, yeye atatoka nje.+ 11 Na katika sherehe+ na katika majira ya sherehe toleo la nafaka litakuwa efa moja kwa ajili ya yule ng’ombe-dume mchanga na efa moja kwa ajili ya yule kondoo-dume, na kwa ajili ya wale wana-kondoo kulingana na uwezo wake wa kutoa; na, kwa habari ya mafuta, hini moja kwa efa.+

12 “ ‘Na ikiwa mkuu atatoa toleo la hiari ili liwe toleo zima la kuteketezwa,+ au dhabihu za ushirika ziwe toleo la hiari kwa Yehova, mtu atamfungulia pia lango linaloelekea mashariki,+ naye atatoa toleo lake zima la kuteketezwa na dhabihu zake za ushirika kama vile anavyofanya siku ya sabato.+ Naye atatoka nje, na mtu atalifunga lango baada ya yeye kutoka nje.+

13 “ ‘Na mwana-kondoo dume ambaye hana kasoro, aliye katika mwaka wake wa kwanza, utamtoa awe toleo zima la kuteketezwa kila siku kwa Yehova.+ Utamtoa asubuhi baada ya asubuhi. 14 Na utatoa toleo la nafaka pamoja naye asubuhi baada ya asubuhi sehemu ya sita ya efa na, kwa habari ya mafuta, sehemu ya tatu ya hini ya kuunyunyizia unga laini.+ Toleo la nafaka kwa Yehova ni sheria ya kudumu mpaka wakati usio na kipimo, daima. 15 Nao wataandaa mwana-kondoo dume na toleo la nafaka na mafuta asubuhi baada ya asubuhi kuwa toleo zima la kuteketezwa la daima.’

16 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Mkuu akimpa zawadi kila mmoja wa wanawe iwe urithi wake, huo wenyewe utakuwa mali ya wanawe wenyewe. Hiyo ndiyo miliki yao kulingana na urithi wao. 17 Na akimpa mmoja wa watumishi wake zawadi kutoka katika urithi wake, huo pia utakuwa wake mpaka ule mwaka wa uhuru;+ nao utarudi kwa mkuu. Ni urithi wake tu—kwa habari ya wanawe—ndio utakaoendelea kuwa wao wenyewe. 18 Naye mkuu hatachukua urithi wowote wa watu ili kuwalazimisha waondoke katika miliki yao.+ Atawapa wanawe urithi kutoka kwenye miliki yake mwenyewe, ili watu wangu wasitawanyike kila mmoja mbali na miliki yake.’ ”+

19 Naye akaniingiza ndani kupitia njia ya kuingilia+ iliyokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vya kulia chakula, vile vya makuhani, vilivyoelekea kaskazini,+ na, tazama! hapo palikuwa na mahali, pande zote mbili za nyuma kuelekea magharibi. 20 Naye akaniambia: “Hapa ndipo mahali ambapo makuhani watatokosea toleo la hatia+ na toleo la dhambi,+ na ambapo wataokea toleo la nafaka,+ ili wasitoe chochote na kukipeleka kwenye ua wa nje ili kuwatakasa watu.”+

21 Naye akanitoa nje mpaka kwenye ua wa nje na kunipitisha kwenye ile miimo minne ya pembeni ya ule ua, na, tazama! kulikuwa na ua karibu na mwimo huu wa pembeni wa ule ua, ua ulio karibu na mwimo ule wa pembeni wa ua. 22 Katika ile miimo minne ya ua kulikuwa na nyua ndogo, zenye urefu wa mikono 40 na mikono 30 upana wake. Zote nne zikiwa zina miundo ya pembeni zilikuwa na kipimo kilekile. 23 Na kulikuwa na mstari kuzizunguka pande zote, kuzizunguka zote nne pande zote, na kulikuwa na mahali pa kutokosea+ palipofanywa chini ya mistari hiyo kuzunguka pande zote. 24 Kisha akaniambia: “Hizi ni nyumba za wale wanaotokosa ambapo wahudumu wa ile Nyumba hutokosea dhabihu ya watu.”+

47 Naye akanirudisha hatua kwa hatua mpaka kwenye mlango wa ile Nyumba,+ na, tazama! kulikuwa na maji+ yaliyokuwa yakitoka chini ya kizingiti cha Nyumba hiyo upande wa mashariki,+ kwa maana upande wa mbele wa Nyumba ulikuwa mashariki. Nayo maji hayo yalikuwa yakishuka kutoka chini, kutoka upande wa kuume wa Nyumba hiyo, upande wa kusini wa madhabahu.

2 Naye akanileta hatua kwa hatua kupitia lango la kaskazini+ na kunizungusha kupitia njia ya nje kwenda kwenye lango la nje linaloelekea mashariki,+ na, tazama! maji+ yalikuwa yanatiririka kutoka upande wa mkono wa kuume.

3 Mtu huyo alipotoka kwenda mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake,+ alipima pia mikono elfu moja na kunipitisha katikati ya maji yale, maji yanayofika kwenye vifundo vya miguu.

4 Naye akaendelea kupima elfu moja kisha akanipitisha katikati ya maji yale, maji yanayofika kwenye magoti.

Naye akaendelea kupima elfu moja na sasa akanipitisha katikati—maji yanayofika kiunoni.

5 Naye akaendelea kupima elfu moja. Kilikuwa kijito ambacho sikuweza kupita katikati, kwa maana maji hayo yalikuwa yameinuka juu, maji ya mtu kuweza kuogelea, kijito ambacho hakingeweza kupitwa katikati.

6 Ndipo akaniambia: “Je, umeona hili, Ee mwana wa binadamu?”

Kisha akanitembeza na kunirudisha kwenye ukingo wa kijito hicho. 7 Niliporudi, kumbe, tazama! kwenye ukingo wa kijito hicho kulikuwa na miti mingi sana, upande huu na upande ule.+ 8 Naye akaendelea kuniambia: “Maji haya yanaenda eneo la mashariki nayo yatakwenda chini kupitia Araba.+ Nayo yatakuja baharini.+ Yanapoletwa katika bahari yenyewe,+ maji yake kwa kweli huponywa pia. 9 Na itakuwa kwamba kila nafsi hai ambayo huzaana kwa wingi,+ kila mahali ambapo huja kijito hicho kilichoongezeka ukubwa wake mara mbili, itapata uzima. Na itatukia kwamba kutakuwako samaki wengi sana, kwa sababu hapo ndipo maji hayo hakika yataingia, nayo maji ya bahari yataponywa,+ na kila kitu kitakuwa hai mahali ambapo kijito hicho kitafika.

10 “Na itatukia kwamba wavuvi watasimama kando yake kutoka En-gedi+ mpaka En-eglaimu. Kutakuwa na uwanja wa kukaushia nyavu za kukokota. Kulingana na aina zake, samaki wao watakuwa wengi sana, kama samaki wa ile Bahari Kuu.+

11 “Kuna mahali pake penye majimaji na penye matope, napo hapataponywa.+ Hakika pataachiwa chumvi.+

12 “Na kando ya kijito hicho, kando ya ukingo upande huu na upande ule, kutatokea kila namna ya miti kwa ajili ya chakula.+ Majani yake hayatakauka,+ wala matunda yake hayataharibiwa.+ Kila mwezi itazaa matunda mapya, kwa sababu maji yake—yanatoka katika patakatifu penyewe.+ Nayo matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa maponyo.”+

13 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Hili ndilo eneo ambalo mtajigawia kuwa urithi wa nchi ya makabila kumi na mawili ya Israeli, kukiwa na mafungu mawili ya shamba kwa Yosefu.+ 14 Nanyi mtairithi, kila mmoja sawa na ndugu yake, nchi ambayo niliinua mkono wangu katika kiapo+ kwamba nitawapa mababu zenu;+ na nchi hiyo itawaangukia ninyi kwa kura ili kuwa urithi.+

15 “Na huu ndio mpaka wa nchi kuelekea upande wa kaskazini, kutoka Bahari Kuu kupitia njia ya kwenda Hethloni,+ mtu anapoingia Sedadi,+ 16 Hamathi,+ Berotha,+ Sibraimu, ulio katikati ya mpaka wa Damasko+ na mpaka wa Hamathi; Haser-hatikoni, ulio kuelekea upande wa mpaka wa Haurani.+ 17 Nao mpaka kutoka baharini utakuwa Hasar-enoni,+ mpaka wa Damasko na kaskazini—kuelekea kaskazini, na mpaka wa Hamathi.+ Huo ndio upande wa kaskazini.

18 “Na upande wa mashariki ni kutoka katikati ya Haurani+ na Damasko+ na katikati ya Gileadi+ na nchi ya Israeli; Yordani,+ kutoka katika mpaka wa bahari upande wa mashariki mtapima. Huo ndio upande wa mashariki.

19 “Na upande wa kusini ni kuelekea kusini, kutoka Tamari+ mpaka maji ya Meribath-kadeshi,+ bonde la mto+ mpaka ile Bahari Kuu. Huo ndio upande wa kusini, kuelekea Negebu.

20 “Na upande wa magharibi ni ile Bahari Kuu, kutoka katika mpaka ulio mbele moja kwa moja hadi kuingia ndani huko Hamathi.+ Huo ndio upande wa magharibi.”

21 “Nanyi mtajigawia nchi hii, yale makabila kumi na mawili ya Israeli. 22 Na itatukia kwamba mtajigawia wenyewe iwe urithi+ kwenu na kwa wakaaji wageni wanaokaa wakiwa wageni katikati yenu,+ ambao wamezaa wana katikati yenu. Nao watakuwa kwenu kama mwenyeji katikati ya wana wa Israeli. Pamoja nanyi wataanguka katika urithi kwa kura katikati ya makabila ya Israeli.+ 23 Na itatukia kwamba katika kabila ambalo mkaaji mgeni anakaa akiwa mgeni, hapo ndipo mtakapompa urithi wake,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

48 “Na haya ndiyo majina ya makabila hayo. Kutoka upande wa kaskazini, upande wa njia ya Hethloni+ hadi kuingia ndani huko Hamathi,+ Hasar-enani,+ mpaka wa Damasko kuelekea kaskazini, upande wa Hamathi; nayo itakuwa na mpaka wa mashariki na wa magharibi, Dani+ fungu moja. 2 Na kwenye mpaka wa Dani, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Asheri+ moja. 3 Na kwenye mpaka wa Asheri, kutoka mpaka wa mashariki hata kwenye mpaka wa magharibi, Naftali+ moja. 4 Na kwenye mpaka wa Naftali, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Manase+ moja. 5 Na kwenye mpaka wa Manase, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Efraimu+ moja. 6 Na kwenye mpaka wa Efraimu, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Rubeni+ moja. 7 Na kwenye mpaka wa Rubeni, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Yuda+ moja. 8 Na kwenye mpaka wa Yuda, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, mchango ambao ninyi mnapaswa kutoa unapaswa kuwa na upana wa mikono 25,000,+ na urefu kulingana na moja la yale mafungu kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi. Napo patakatifu patakuwa katikati yake.+

9 “Kwa habari ya mchango ambao mnapaswa kumtolea Yehova, urefu utakuwa mikono 25,000 na upana mikono 10,000. 10 Na kwa habari yake kutakuwako mchango mtakatifu kwa ajili ya makuhani,+ upande wa kaskazini mikono 25,000, na upande wa magharibi upana wa mikono 10,000, na upande wa mashariki upana wa mikono 10,000, na upande wa kusini urefu wa mikono 25,000. Na patakatifu pa Yehova patakuwa katikati yake.+ 11 Patakuwa kwa ajili ya makuhani, waliotakaswa kutoka kwa wana wa Sadoki,+ ambao waliutunza wajibu kunielekea mimi, ambao hawakuenda mbali wakati ambapo wana wa Israeli walienda huku na huku, kama vile Walawi walivyoenda huku na huku.+ 12 Nao watakuwa na mchango kutoka katika mchango wa hiyo nchi ukiwa kitu kitakatifu zaidi, kwenye mpaka wa Walawi.+

13 “Na Walawi watakuwa na fungu,+ karibu kabisa na eneo la makuhani, lenye urefu wa mikono 25,000, na upana wa mikono 10,000; urefu wote ukiwa 25,000, na upana ukiwa 10,000.+ 14 Nao hawapaswi kuuza sehemu yoyote kati ya hiyo, wala mtu hapaswi kubadilishana, wala mtu hapaswi kuacha sehemu bora zaidi ya nchi itoke kwao; kwa maana hicho ni kitu kitakatifu kwa Yehova.+

15 “Kwa habari ya ile mikono 5,000 inayobaki katika upana kandokando ya ile mikono 25,000, ni kitu najisi cha jiji,+ kiwe makao na kiwe uwanja wa malisho. Nalo jiji litakuwa katikati yake.+ 16 Na hivi ndivyo vipimo vya jiji: mpaka wa kaskazini mikono 4,500, na mpaka wa kusini 4,500, na mpaka wa mashariki 4,500, na mpaka wa magharibi 4,500. 17 Na jiji litakuwa na uwanja wa malisho,+ upande wa kaskazini mikono 250, na upande wa kusini 250, na upande wa mashariki 250, na upande wa magharibi 250.

18 “Na kitakachobaki katika urefu kitalingana kabisa na mchango mtakatifu,+ mikono 10,000 upande wa mashariki, na 10,000 upande wa magharibi; napo patalingana kabisa na mchango mtakatifu, na mazao yake yatakuwa kwa ajili ya mkate wa wale wanaotumikia jiji.+ 19 Na wale wanaotumikia jiji kutoka katika makabila yote ya Israeli watapalima.+

20 “Mchango mzima ni mikono 25,000 urefu kwa 25,000 upana. Mtachanga sehemu iliyo mraba iwe mchango mtakatifu pamoja na miliki ya jiji.

21 “Na sehemu iliyobaki itakuwa ya mkuu,+ upande huu na upande ule wa mchango mtakatifu na wa miliki ya jiji,+ kando ya mikono 25,000 ya mchango mtakatifu kuelekea mpaka wa mashariki; na upande wa magharibi kando ya mikono 25,000 kuelekea mpaka wa magharibi.+ Kama yalivyo mafungu hayo, ndivyo itakavyokuwa kwa ajili ya mkuu. Na mchango mtakatifu na patakatifu pa ile Nyumba patakuwa katikati yake.

22 “Nayo miliki ya Walawi na miliki ya jiji, itakuwa katikati ya miliki ya mkuu. Katikati ya mpaka wa Yuda+ na mpaka wa Benyamini itakuwa ya mkuu.

23 “Nayo yale makabila mengine, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Benyamini+ fungu moja. 24 Na kando ya mpaka wa Benyamini, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Simeoni+ moja. 25 Na kando ya mpaka wa Simeoni, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Isakari+ moja. 26 Na kando ya mpaka wa Isakari, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Zabuloni+ moja. 27 Na kando ya mpaka wa Zabuloni, kutoka mpaka wa mashariki hadi mpaka wa magharibi, Gadi+ moja. 28 Na kando ya mpaka wa Gadi, hadi mpaka wa kusini, litakuwa kuelekea kusini; nao mpaka utakuwa kutoka Tamari+ hadi maji ya Meribath-kadeshi,+ hadi kwenye bonde la mto,+ hadi kwenye ile Bahari Kuu.+

29 “Hii itakuwa nchi ambayo mtafanya iangukie makabila ya Israeli kwa kura iwe urithi,+ na hayo yatakuwa mafungu yao,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.

30 “Na haya yatakuwa malango ya kutokea ya jiji: Kwenye mpaka wa kaskazini, kipimo kitakuwa mikono 4,500.+

31 “Na malango ya jiji yatakuwa kulingana na makabila ya Israeli, malango matatu yakiwa upande wa kaskazini, lango la Rubeni, moja; lango la Yuda, moja; lango la Lawi, moja.

32 “Na kwenye mpaka wa mashariki kutakuwa mikono 4,500, na malango matatu, naam, lango la Yosefu, moja; lango la Benyamini, moja; lango la Dani, moja.

33 “Na mpaka wa kusini utakuwa mikono 4,500 kipimo chake, ukiwa na malango matatu, lango la Simeoni, moja; lango la Isakari, moja; lango la Zabuloni, moja.

34 “Mpaka wa magharibi utakuwa mikono 4,500, kukiwa na malango matatu, lango la Gadi, moja; lango la Asheri, moja; lango la Naftali, moja.

35 “Kuzunguka pande zote kutakuwa mikono 18,000; na jina la jiji kutoka siku hiyo na kuendelea litakuwa, Yehova Mwenyewe Yupo Hapo.”+

[Maelezo ya Chini]

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki