Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • nwt Ayubu 1:1-42:17
  • Yobu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yobu
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Yobu

YOBU

1 Katika inchi ya Usi kulikuwa mutu mumoja mwenye jina lake lilikuwa Yobu.*+ Alikuwa mutu munyoofu na muaminifu-mushikamanifu;*+ alikuwa anamuogopa Mungu na kuepuka mambo ya mubaya.+ 2 Alizaa watoto wanaume saba (7) na watoto wanamuke tatu (3). 3 Mifugo yake ilikuwa kondoo elfu saba (7 000), ngamia elfu tatu (3 000), ngombe elfu moja (1 000), punda mia tano (500), na alikuwa na watumishi wengi sana, kwa hiyo akakuwa mukubwa kuliko watu wote wa Mashariki.

4 Kila mumoja wa wana wake alikuwa anafanya karamu kwenye nyumba yake katika siku yake mwenyewe yenye ilipangwa.* Na walikuwa wanaalika dada zao watatu (3) ili kula na kunywa pamoja nao. 5 Wakati siku za karamu zilikuwa zinamalizika, Yobu alikuwa anawaita kusudi awatakase. Kwa hiyo alikuwa anaamuka asubui sana na kutoa zabihu za kuteketezwa+ kwa ajili ya kila mumoja wao. Kwa maana Yobu alikuwa anasema: “Pengine wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu katika moyo wao.” Ni vile Yobu alikuwa anafanya sikuzote.+

6 Basi siku ikafika yenye wana wa Mungu* wa kweli+ waliingia ili kusimama mbele ya Yehova,+ na Shetani+ pia akaingia kati yao.+

7 Kisha Yehova akamuambia Shetani: “Unatoka wapi?” Shetani akamujibu Yehova: “Ninatoka kuzunguka-zunguka katika dunia na kutembea-tembea ndani yake.”+ 8 Na Yehova akamuambia Shetani: “Je, umemuona* mutumishi wangu Yobu? Hakuna mutu kama yeye juu ya dunia. Yeye ni mutu munyoofu na muaminifu-mushikamanifu,*+ mwenye kumuogopa Mungu na kuepuka mambo ya mubaya.” 9 Kwa hiyo Shetani akamujibu Yehova: “Je, Yobu anamuogopa Mungu bure?+ 10 Je, haukutia ukuta wa ulinzi kumuzunguka yeye+ na nyumba yake na kila kitu chenye iko* nacho? Umebariki kazi ya mikono yake,+ na mifugo yake imeenea katika inchi yote. 11 Lakini, ili mambo yabadilike, unyooshe mukono wako na upige kila kitu chenye iko* nacho, na hakika atakulaani mbele ya uso wako.” 12 Basi Yehova akamuambia Shetani: “Angalia! Kila kitu chenye iko* nacho kiko katika mukono wako. Lakini tu usiweke mukono wako juu ya mutu huyo!” Kwa hiyo Shetani akatoka mbele ya* Yehova.+

13 Sasa siku moja yenye watoto wake wanaume na watoto wake wanamuke walikuwa wanakula na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mukubwa,+ 14 mujumbe mumoja akakuja kwa Yobu na kusema: “Ngombe walikuwa wanalima na punda walikuwa wanakula majani pembeni yao 15 wakati Wasabea waliwashambulia na kuwakamata, na wakaua watumishi kwa upanga. Mimi tu ndiye niliponyoka ili kukuletea habari.”

16 Wakati alikuwa angali anasema, mwingine akakuja na kusema: “Moto kutoka kwa Mungu* ulianguka kutoka mbinguni na kuwaka kati ya kondoo na watumishi na kuwateketeza! Mimi tu ndiye niliponyoka ili kukuletea habari.”

17 Wakati alikuwa angali anasema, mwingine akakuja na kusema: “Wakaldayo+ walifanya vikundi tatu (3) na wakavamia ngamia na kuwakamata, na kuua watumishi kwa upanga. Mimi tu ndiye niliponyoka ili kukuletea habari.”

18 Wakati alikuwa angali anasema, mwingine tena akakuja na kusema: “Watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke walikuwa wanakula na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mukubwa. 19 Upepo mukali ukakuja kwa kushitukia kutoka katika jangwa, na ukapiga pembe ine (4) za nyumba, na nyumba hiyo ikaangukia vijana hao na wakakufa. Mimi tu ndiye niliponyoka ili kukuletea habari.”

20 Basi Yobu akasimama na kupasua nguo yake na akanyoa nywele za kichwa chake; kisha akaanguka chini na kuinama 21 na kusema:

“Nilitoka katika tumbo la uzazi la mama yangu nikiwa uchi,

Na nitarudia nikiwa uchi.+

Yehova ametoa,+ na Yehova amenyanganya.

Jina la Yehova liendelee kusifiwa.”

22 Katika mambo haya yote, Yobu hakutenda zambi wala kumulaumu Mungu kwa jambo lolote la mubaya.*

2 Kisha siku ikafika yenye wana wa Mungu wa kweli*+ waliingia ili kusimama mbele ya Yehova,+ na Shetani pia akaingia kati yao ili kusimama mbele ya Yehova.+

2 Kisha Yehova akamuambia Shetani: “Unatoka wapi?” Shetani akamujibu Yehova: “Ninatoka kuzunguka-zunguka katika dunia na kutembea-tembea ndani yake.”+ 3 Na Yehova akamuambia Shetani: “Je, umemuona* mutumishi wangu Yobu? Hakuna mutu kama yeye juu ya dunia. Yeye ni mutu munyoofu na muaminifu-mushikamanifu,*+ mwenye kumuogopa Mungu na kuepuka mambo ya mubaya. Mupaka sasa angali anashika sana uaminifu-mushikamanifu wake,+ hata kama unajaribu kunichochea+ nimuharibu* pasipo sababu.” 4 Lakini Shetani akamujibu Yehova: “Ngozi kwa ngozi. Mutu atatoa kila kitu chenye iko* nacho ili aokoe uzima wake.* 5 Lakini, ili mambo yabadilike, unyooshe mukono wako na upige mufupa wake na nyama yake, na hakika atakulaani mbele ya uso wako.”+

6 Basi Yehova akamuambia Shetani: “Angalia! Yeye iko* katika mukono wako! Lakini tu usiondoe uzima wake!”* 7 Kwa hiyo Shetani akatoka mbele ya* Yehova na akamupiga Yobu kwa majipu yenye maumivu makali*+ kuanzia kikanyangio cha muguu wake mupaka sehemu ya juu ya katikati ya kichwa chake. 8 Na Yobu akakamata kipande cha chombo cha udongo ili kujipalula, na akakaa katika majivu.+

9 Mwishowe bibi yake akamuambia: “Ungali unashikilia sana uaminifu-mushikamanifu wako? Laani Mungu na ukufe!” 10 Lakini yeye akamuambia: “Unazungumuza kama mumoja wa wanamuke wenye hawana akili. Tukubali tu mambo ya muzuri kutoka kwa Mungu wa kweli na tusikubali pia mambo ya mubaya?”+ Katika mambo haya yote, Yobu hakutenda zambi kwa midomo yake.+

11 Marafiki watatu (3) wa Yobu wakasikia juu ya misiba yote yenye ilimupata, na kila mumoja akatoka mahali pake⁠—Elifazi+ Mutemani, Bildadi+ Mushua,+ na Sofari+ Munaamati. Basi wakasikilizana kukutana ili waende kumupatia Yobu pole na kumufariji. 12 Wakati walimuona kwa mbali, hawakumutambua. Wakaanza kulia kwa sauti kubwa na kupasua nguo zao, na wakatupa mavumbi katika hewa na juu ya vichwa vyao.+ 13 Kisha wakakaa chini pamoja naye kwa siku saba (7), muchana na usiku. Hakuna mwenye alimuambia neno fulani, kwa sababu waliona kwamba maumivu yake yalikuwa makali sana.+

3 Kisha mambo hayo Yobu akaanza kusema na kulaani siku yenye alizaliwa.*+ 2 Yobu akasema:

 3 “Iangamie ile siku yenye nilizaliwa,+

Pia ule usiku wenye mutu fulani alisema: ‘Mwanaume amechukuliwa mimba!’

 4 Siku hiyo ikuwe giza.

Mungu mwenye kuwa juu asifikirie siku hiyo;

Mwangaza wowote usiiangazie.

 5 Giza nzito lifunike* siku hiyo.

Wingu la mvua likae juu yake.

Jambo lolote lenye kuleta giza wakati wa muchana liogopeshe sana siku hiyo.

 6 Usiku huo⁠—​utawaliwe na giza;+

Usikuwe na furaha kati ya siku za mwaka,

Na usiingie kati ya hesabu ya miezi.

 7 Ndiyo! Usiku huo ukuwe tasa;*

Vigelegele vya shangwe visisikiwe usiku huo.

 8 Wenye kulaani siku hiyo wailaani,

Wale wenye wanaweza kuamusha Leviatani.*+

 9 Nyota za ile mangaribi wakati giza linaanza zikuwe na giza;

Usiku huo ungojee mwangaza lakini usiupate,

Na usione miali ya mapambazuko.*

10 Kwa maana usiku huo haukufunga milango ya tumbo la uzazi la mama yangu;+

Wala haukuzuia macho yangu yasione taabu.

11 Sababu gani sikukufa wakati nilizaliwa?

Sababu gani sikukata pumuzi wakati nilitoka katika tumbo la uzazi?+

12 Sababu gani magoti yalikuwa pale ili kunipokea

Na maziwa ili kuninyonyesha?

13 Kwa maana kwa sasa ningekuwa nimelala pasipo kusumbuliwa;+

Ningekuwa nimelala usingizi na kupumuzika+

14 Pamoja na wafalme wa dunia na washauri wao,

Wenye walijijengea mahali kwenye sasa ni mabomoko,*

15 Ao pamoja na wakubwa wenye walikuwa na zahabu,

Wenye nyumba zao zilikuwa zimejaa feza.

16 Ao sababu gani sikukuwa kama mimba yenye iliharibika kwa uficho,

Kama watoto wenye hawajaona mwangaza hata siku moja?

17 Kule hata waovu wameacha kusumbua;

Kule wenye kuchoka wanapumuzika.+

18 Kule wafungwa ni wenye kutulia pamoja;

Hawasikie sauti ya mutu mwenye anawalazimisha kufanya kazi.

19 Wadogo na wakubwa wako sawasawa kule,+

Na mutumwa anapata uhuru, haiko tena chini ya mamlaka ya bwana wake.

20 Sababu gani anapatia mwangaza mutu mwenye kuteseka

Na uzima kwa wale wenye uchungu mwingi?*+

21 Sababu gani wanatamani sana kifo, lakini hakifike?+

Wanakitafuta sana kuliko namna wanatafuta hazina zenye kufichwa,

22 Wale wenye kushangilia sana,

Wenye kufurahi wakati wanapata kaburi.

23 Sababu gani anapatia mwangaza mwanaume mwenye amepotea njia,

Mwenye Mungu ametia ukuta kumuzunguka pande zote?+

24 Kwa maana kuliko kula chakula changu ninalia kwa maumivu,+

Na kilio changu cha maumivu+ kinamwangika kama maji.

25 Kwa maana kile ninaogopa kimenifikia,

Na kile ninaogopa kimenipata.

26 Sina amani, sina utulivu, sina pumuziko,

Lakini taabu inaendelea kuja.”

4 Kisha Elifazi+ Mutemani akajibu:

 2 “Kama mutu anajaribu kusema na wewe, utashindwa kuvumilia?

Kwa maana ni nani anaweza kujizuia kusema?

 3 Kwa kweli, umerekebisha watu wengi,

Na ulikuwa unatia nguvu mikono yenye kuwa zaifu.

 4 Maneno yako yalikuwa yanamuinua mutu mwenye kujikwaa,

Na ulikuwa unatia nguvu wale wenye magoti yenye kukunjama.

 5 Lakini sasa yamekupata wewe, na umelemewa;*

Yamekugusa wewe, na umevurugika.

 6 Je, heshima yako kwa Mungu haikupatie uhakika?

Je, njia yako ya uaminifu-mushikamanifu+ haikupatie tumaini?

 7 Tafazali, kumbuka: Ni mutu gani mwenye hana kosa mwenye amekwisha kuangamia?

Ni wakati gani watu wanyoofu wamepata kuharibiwa?

 8 Kile nimeona ni kwamba wale wenye kulima* ubaya

Na wale wenye kupanda taabu watavuna mambo yaleyale.

 9 Kwa pumuzi ya Mungu wanakufa,

Na kwa mulipuko wa kasirani yake wanafikia mwisho.

10 Simba ananguruma, na mwana-simba anatoa sauti,

Lakini hata meno ya simba wenye nguvu* yanavunjika.

11 Simba anakufa kwa sababu ya kukosa mawindo,

Na vitoto vya simba vinasambazwa.

12 Sasa nililetewa neno kwa siri,

Na sauti yake ya chini-chini ilifika katika sikio langu.

13 Katika mawazo yenye kuvuruga akili wakati wa maono ya usiku,

Wakati usingizi muzito unaanguka juu ya wanadamu,

14 Mutetemeko mukubwa ulikuja juu yangu,

Ukajaza woga katika mifupa yangu yote.

15 Roho fulani akapita mbele ya uso wangu;

Nywele za mwili wangu zikasimama.

16 Kisha akasimama bila kutikisika,

Lakini sikutambua sura yake.

Umbo fulani ilikuwa mbele ya macho yangu;

Kulikuwa utulivu, na kisha nikasikia sauti:

17 ‘Mwanadamu mwenye anaweza kufa anaweza kuwa mwenye haki kuliko Mungu?

Mutu anaweza kuwa safi kuliko Mutengenezaji wake mwenyewe?’

18 Angalia! Hana imani katika watumishi wake,

Na anapata makosa ndani ya malaika* wake.

19 Namna gani basi wale wenye kukaa katika nyumba za udongo,

Wenye musingi wao uko katika mavumbi,+

Wenye wanapondwa upesi kama nondo!*

20 Wanapondwa-pondwa kuanzia asubui mupaka mangaribi;

Wanakufa milele, na hakuna mwenye kutambua.

21 Je, hawako kama hema yenye kamba yake imengolewa?

Wanakufa bila kuwa na hekima.

5 “Ita, tafazali! Je, kuko mutu mwenye anakujibu?

Utamuendea nani kati ya watakatifu?

 2 Kwa maana kinyongo kitamuua mupumbavu,

Na wivu utamuua mujinga.

 3 Nimeona mupumbavu akitia mizizi,

Lakini bila kutazamia makao yake yakalaaniwa.

 4 Wana wake wanakosa kabisa usalama,

Na wanapondwa kwenye mulango mukubwa wa muji,+ na hawana mutu wa kuwaokoa.

 5 Mutu mwenye njaa anakula kile anavuna,

Anakikamata hata kati ya miiba,

Na mali zao zinakamatwa katika mutego.

 6 Kwa maana mambo ya mubaya hayaote kutoka katika mavumbi,

Na taabu haichipuke kutoka katika udongo.

 7 Kwa maana mwanadamu anazaliwa kwa ajili ya taabu,

Kama vile hakika cheche za moto zinaruka juu.

 8 Lakini mimi ningemupelekea Mungu ombi langu,

Na ningemupelekea Mungu kesi yangu ya hukumu,

 9 Yeye mwenye anatenda mambo makubwa na yenye hayawezi kuchunguzwa,

Mambo ya ajabu yenye hayana hesabu.

10 Anapatia dunia mvua

Na anatuma maji juu ya maeneo ya mashamba.

11 Anasimamisha watu wa hali ya chini,

Na wale wenye huzuni anawapandisha kwenye wokovu.

12 Anavunja mipango mibaya ya wadanganyifu,

Ili kazi ya mikono yao isikuwe na matokeo ya muzuri.

13 Yeye anakamata wenye hekima katika ujanja wao wenyewe,+

Ili mipango ya watu werevu ivunjwe.

14 Wanakutana na giza wakati wa muchana,

Na wanapapasa-papasa katikati ya muchana kama vile ni usiku.

15 Anaokoa kutokana na upanga wa kinywa chao,

Anaokoa maskini katika mukono wa mwenye nguvu,

16 Ili kukuwe tumaini kwa ajili ya mutu wa hali ya chini,

Lakini kinywa cha ukosefu wa haki kinafungwa.

17 Angalia! Mwenye furaha ni ule mwenye Mungu anakaripia;

Kwa hiyo usikatae nizamu ya Mweza-Yote!

18 Kwa maana yeye anatokeza maumivu, lakini anafunga kidonda;

Anavunja, lakini anaponyesha kwa mikono yake mwenyewe.

19 Atakuokoa katika taabu sita (6),

Hata ya saba (7) haitakuumiza.

20 Wakati wa njaa atakukomboa katika kifo,

Na wakati wa vita atakuepusha na nguvu ya upanga.

21 Utalindwa ili usiumizwe na mashambulizi ya ulimi,+

Na hautaogopa wakati uharibifu utakuja.

22 Utachekelea uharibifu na njaa,

Na hautaogopa wanyama wa pori wa dunia.

23 Kwa maana majiwe ya shamba hayatakuumiza,*

Na wanyama wa pori wataishi kwa amani pamoja na wewe.

24 Utajua kwamba hema yako iko salama,*

Na hakuna kitu kitakosekana wakati utachunguza malisho yako.

25 Utakuwa na watoto wengi,

Na wazao wako watakuwa wengi kama majani ya dunia.

26 Utakuwa ungali na nguvu wakati utaingia ndani ya kaburi,

Kama mafungu ya nafaka yenye kukusanywa wakati wake.

27 Angalia! Tumechunguza mambo hayo, na yako vile.

Sikiliza na uyakubali.”

6 Kisha Yobu akajibu:

 2 “Ingekuwa muzuri kama uchungu wangu+ ungepimwa kabisa

Na kutiwa kwenye mizani* pamoja na musiba wangu!

 3 Kwa maana sasa ni muzito kuliko muchanga wa bahari.

Ndiyo sababu maneno yangu yamekuwa mazungumuzo ya ovyoovyo.*+

 4 Kwa maana mishale ya Mweza-Yote imenitoboa,

Na roho yangu inakunywa sumu yake;+

Vitu vya kuogopesha kutoka kwa Mungu vinajipanga ili kunishambulia.

 5 Je, punda wa pori+ atalia wakati iko* na majani,

Ao ngombe-dume atalia wakati iko na chakula?

 6 Chakula chenye hakina utamu* kinakuliwa bila chumvi,

Ao kuko utamu katika maji ya mumea* wa muholi?

 7 Nimekataa* kugusa vitu hivyo.

Vitu hivyo viko kama kitu cha kuambukiza katika chakula changu.

 8 Aa! kama ombi langu lingetimizwa

Na kama Mungu angenipatia kile ninatamani!

 9 Kama Mungu angefurahia kuniponda,

Na kama angenyoosha mukono wake na kuniharibu!+

10 Kwa maana hata jambo hilo lingenifariji;

Ningeruka kwa furaha ijapokuwa maumivu yangu yenye kuendelea,

Kwa maana sijakataa maneno ya Mutakatifu.+

11 Je, niko na nguvu za kuendelea kungojea?+

Na ni mwisho wa namna gani unaningojea, ili niendelee kuishi?*

12 Je, niko na nguvu kama mwamba?

Ao je, mwili wangu ni wa shaba?

13 Je, kuko jambo lolote lenye ninaweza kufanya ili nijisaidie

Wakati vitu vyangu vyote vyenye vilikuwa vinanisaidia vimepotea?

14 Kila mutu mwenye anakataa kumutendea mwanadamu mwenzake kwa upendo mushikamanifu+

Atakuwa ameacha kumuogopa Mweza-Yote.+

15 Ndugu zangu ni wajanja+ kama muto mudogo wa kipindi cha baridi,

Kama maji yenye kukauka ya mito midogo ya kipindi cha baridi.

16 Imekuwa nyeusi kwa sababu ya barafu,

Na teluji* yenye kuyeyuka imefichwa ndani yake.

17 Lakini kwa wakati wake mito hiyo midogo inakosa maji na inapotea;

Wakati wa jua kali, inakauka.

18 Njia ya mito hiyo midogo inaelekezwa mahali pengine;

Na inateremuka mupaka katika jangwa na kupotea.

19 Misururu ya wasafiri wa Tema+ inaitafuta;

Wasafiri wenye kutoka Sheba*+ wanaingojea.

20 Wamepata haya kwa sababu ya tegemeo lao la uongo;

Wanakuja pale ili tu kupoteza tumaini.

21 Kwa maana ni vile mumekuwa mbele ya macho yangu;+

Mumeona kuogopesha kwa musiba wangu, na mumeogopa.+

22 Je, nimekwisha kusema, ‘Munipatie kitu fulani,’

Ao kuwaomba munipatie zawadi yoyote katika mali zenu?

23 Je, nimekwisha kuwaomba munikomboe katika mukono wa adui

Ao muniokoe katika mikono ya wakandamizaji?

24 Munifundishe, na mimi nitanyamaza;+

Munisaidie nielewe kosa langu.

25 Maneno ya kweli hayaumize!+

Lakini karipio lenu linaweza kuwa na faida gani?+

26 Je, munafanya mupango wa kukaripia maneno yangu,

Maneno ya mutu mwenye amepoteza tumaini,+ yenye upepo unapeperusha mbali?

27 Munaweza vilevile kupiga kura juu ya yatima+

Na kumuuzisha* rafiki yenu!+

28 Sasa muniangalie,

Kwa maana sitasema uongo mbele ya nyuso zenu.

29 Mubadilike, tafazali⁠—​musinihukumu mubaya⁠—​

Ndiyo, mubadilike, kwa maana haki yangu ingali yote.

30 Je, ulimi wangu unasema mambo yenye hayafae?

Je, kaakaa* langu halitambue jambo la mubaya?

7 “Katika dunia, je, maisha ya mwanadamu mwenye anaweza kufa hayako kama kazi ya kulazimishwa,

Na siku zake kama siku za mufanyakazi wa kulipwa?+

 2 Kama vile mutumwa, yeye anatamani sana kivuli,

Na kama vile mufanyakazi wa kulipwa, yeye anangojea malipo yake.+

 3 Kwa hiyo nimepewa miezi yenye haina mafaa yoyote*

Na nimehesabiwa mateso kila usiku.+

 4 Wakati ninalala, ninajiuliza, ‘Nitaamuka wakati gani?’+

Lakini wakati usiku unakuwa murefu, ninaendelea kujigeuza-geuza mupaka wakati wa gizagiza la asubui.

 5 Mwili wangu umejaa funza* na madonge ya uchafu;+

Ngozi yangu imejaa vigaga* na usaha.+

 6 Siku zangu zinapita mbio kuliko chombo cha kusuka cha musukaji wa nguo,+

Na zinaisha bila tumaini.+

 7 Kumbuka kwamba maisha yangu ni upepo,+

Kwamba hakuna siku jicho langu litaona tena furaha.*

 8 Jicho lenye linaniona sasa halitaniona tena;

Macho yenu yatanitafuta, lakini sitakuwa tena.+

 9 Kama vile wingu lenye kufifia na kupotea,

Mutu mwenye kushuka ndani ya Kaburi* hapande juu tena.+

10 Hatarudia tena katika nyumba yake,

Na mahali pake hapatamutambua tena.+

11 Kwa hiyo, sitazuia kinywa changu.

Nitasema kwa sababu ya uchungu wa roho yangu;

Nitalalamika kwa sababu ya mateso yangu makali!*+

12 Je, mimi ni bahari ao munyama mukubwa wa bahari,

Ili uweke mulinzi juu yangu?

13 Wakati ninasema, ‘Kiti changu kitanifariji;

Kitanda changu kitapunguza mateso yangu,’

14 Kisha unaniogopesha sana na ndoto

Na kunitia woga kupitia maono,

15 Ili nichague* kufa kwa sababu ya kukosa pumuzi,

Ndiyo, kifo pa nafasi ya huu mwili wangu.*+

16 Ninachukia maisha yangu;+ sitaki kuendelea kuishi.

Uniache, kwa maana siku zangu ziko kama pumuzi.+

17 Mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umuhangaikie

Na kukaza uangalifu* wako juu yake?+

18 Sababu gani unamuchunguza kila asubui

Na kumujaribu kila wakati?+

19 Je, hautaacha kuniangalia

Na kuniacha kwa muda wa kutosha ili nimeze mate yangu?+

20 Kama nimefanya zambi, namna gani ninaweza kukuumiza wewe, Muchunguzaji wa wanadamu?+

Sababu gani umenifanya kuwa shabaha yako?

Je, nimekuwa muzigo kwako?

21 Sababu gani hausamehe zambi yangu

Na kusamehe kosa langu?

Kwa maana hivi karibuni nitalala katika mavumbi,+

Na utanitafuta, lakini sitakuwa tena.”

8 Kisha Bildadi+ Mushua+ akajibu:

 2 “Utaendelea kusema hivi mupaka wakati gani?+

Maneno ya kinywa chako ni kama tu upepo wenye nguvu!

 3 Je, Mungu atapotosha haki,

Ao Mweza-Yote atapotosha uadilifu?*

 4 Kama wana wako wamemutendea zambi,

Anawaacha wapewe azabu kwa sababu ya uasi wao;*

 5 Lakini kama tu unamutafuta Mungu+

Na kumulilia Mweza-Yote ili akuonyeshe wema,

 6 Na kama kwa kweli ungekuwa safi na munyoofu,+

Angekukazia uangalifu*

Na kukurudisha mahali pako penye kustahili.

 7 Na hata kama mwanzo wako ulikuwa mudogo,

Wakati wako wenye kuja ungekuwa mukubwa.+

 8 Tafazali, uliza kizazi chenye kilitangulia,

Na ukazie uangalifu mambo yenye baba zao walijionea.+

 9 Kwa maana tulizaliwa jana tu, na hatujue kitu,

Kwa sababu siku zetu katika dunia ziko kama kivuli.

10 Je, hawatakufundisha

Na kukuambia mambo yenye wanajua?*

11 Je, mumea wa mafunjo* utakuwa murefu mahali kwenye hakuna tingitingi?

Je, matete yatakuwa ya murefu bila maji?

12 Wakati majani yake yangali yanafungana, mbele hayajakatwa,

Yatakauka mbele ya mumea mwingine wowote.

13 Huo ndio mwisho wa* wale wote wenye kumusahau Mungu,

Kwa maana tumaini la mwenye hamuogope Mungu* litapotea,

14 Mwenye tegemeo lake ni la bure

Na mwenye tegemeo lake liko zaifu kama vile utando wa* buibui.

15 Ataegemea nyumba yake, lakini haitaendelea kusimama;

Atajaribu kuishikilia, lakini haitadumu.

16 Yeye ni mumea wenye majimaji katika mwangaza wa jua,

Na matawi yake yanaenea katika bustani.+

17 Mizizi yake inasukana-sukana katika rundo la majiwe;

Anatafuta nyumba kati ya majiwe.*

18 Lakini wakati atangolewa* mahali pake,

Mahali pale patamukana na kusema, ‘Sijakuonaka hata siku moja.’+

19 Ndiyo, ni vile atapotea;*+

Kisha wengine watachipuka kutoka katika mavumbi.

20 Kwa kweli Mungu hatakataa watu wenye kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu;*

Wala hataunga* mukono watu waovu,

21 Kwa maana atajaza tena kinywa chako kicheko

Na midomo yako sauti za furaha.

22 Wenye kukuchukia watafunikwa na haya,

Na hema ya watu waovu haitakuwa tena.”

9 Yobu akajibu:

 2 “Kwa kweli ninajua kwamba ni vile.

Lakini namna gani mwanadamu mwenye anaweza kufa anaweza kuwa na haki katika kesi ya hukumu pamoja na Mungu?+

 3 Kama mutu anataka kubishana Naye,*+

Mutu huyo hawezi kujibu ulizo moja kati ya maulizo Yake elfu moja (1 000).

 4 Yeye ni mwenye hekima katika moyo na mwenye nguvu nyingi sana.*+

Ni nani anaweza kumupinga na akose kuumia?+

 5 Anahamisha* milima bila mutu kujua;

Anaipindua katika kasirani yake.

 6 Anatikisa dunia itoke mahali pake,

Na hivyo nguzo zake zinatetemeka.+

 7 Anaamuru jua lisitoe mwangaza

Na anazuia mwangaza wa nyota;+

 8 Anatandika mbingu yeye peke yake,+

Na anakanyanga juu ya mawimbi makubwa ya bahari.+

 9 Alifanya kundi la nyota la Ashi,* Kesili,* na Kima,*+

Na makundi ya nyota ya anga la kusini;*

10 Anafanya mambo makubwa na yenye hayawezi kuchunguzwa,+

Mambo ya ajabu yenye hayawezi kuhesabiwa.+

11 Anapita pembeni yangu, lakini siwezi kumuona;

Anapita karibu na mimi, lakini simutambue.

12 Wakati anakamata kitu kwa nguvu, ni nani anaweza kushindana naye?

Ni nani anaweza kumuuliza, ‘Unafanya nini?’+

13 Mungu hatazuia kasirani yake;+

Hata wale wenye kumusaidia Rahabu*+ watainama mbele ya Mungu.

14 Namna gani basi wakati ninamujibu

Ninapaswa kuchagua kwa uangalifu maneno yangu ili kubishana naye!

15 Hata kama ningekuwa na haki, singemujibu.+

Ningemulilia tu muamuzi* wangu anionyeshe rehema.

16 Nikimuita, atanijibu?

Siamini kama atasikiliza sauti yangu,

17 Kwa maana ananiponda kwa zoruba

Na anaongeza vidonda vyangu bila sababu.+

18 Haniache nipumue;

Anaendelea kunijaza mambo machungu.

19 Kama ni nguvu, ni yeye mwenye kuwa na nguvu.+

Kama ni haki, anasema: ‘Ni nani anaweza kunishitaki?’

20 Kama ningekuwa na haki, kinywa changu mwenyewe kingenihukumu;

Hata kama ninaendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu,* atasema niko na hatia.*

21 Hata kama ninaendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu,* sijiamini mimi mwenyewe;*

Ninakataa* maisha yangu.

22 Yote ni sawa. Ndiyo sababu ninasema,

‘Anaharibu wenye hawana kosa* na pia waovu.’

23 Kama mafuriko yanatokeza kifo cha kushitukia,

Atachekelea hali ya kupoteza tumaini ya watu wenye hawana kosa.

24 Dunia imetiwa katika mukono wa muovu;+

Anafunika macho ya* waamuzi wake.

Kama haiko yeye, ni nani basi?

25 Siku zangu zinakimbia mbio kuliko mukimbiaji;+

Zinakimbia bila kuona mema.

26 Zinapita haraka kama mashua* ya matete,

Kama tai wenye kushuka mbio ili kukamata mawindo.

27 Kama ninasema, ‘Nitasahau malalamiko yangu,

Nitabadilisha sura yangu na kufurahi,’

28 Ningeendelea kuogopa kwa sababu ya maumivu yangu yote,+

Na ninajua ungenipata na kosa.

29 Ningeonwa kuwa na hatia.*

Basi sababu gani nijisumbue bure?+

30 Nikinawa na teluji* yenye kuyeyuka,

Na kusafisha mikono yangu na sabuni,*+

31 Basi, ungenitupa ndani ya shimo,

Na hata nguo zangu zingenichukia.

32 Kwa maana yeye haiko mwanadamu kama mimi ili niweze kumujibu,

Ili tuende naye kwenye tribinali.+

33 Hakuna mutu wa kuamua* kati yetu,

Mwenye anaweza kuwa muamuzi wetu.*

34 Kama angeacha kunipiga*

Na kuacha kunitisha kupitia mambo yake yenye kuogopesha,+

35 Halafu ningesema naye bila kuogopa,

Kwa maana sina tabia ya kusema kwa woga.

10 “Ninachukia* maisha yangu.+

Nitaonyesha malalamiko yangu.

Nitasema kwa sababu ya uchungu wangu mwingi!*

 2 Nitamuambia Mungu: ‘Usinitangaze kuwa na hatia.

Uniambie sababu gani unashindana na mimi.

 3 Je, unapata faida kwa kunikandamiza,

Kwa kuzarau kazi ya mikono yako+

Na kupendelea mashauri ya waovu?

 4 Je, uko na macho ya kimwili,

Ao je, unaonaka kama vile mwanadamu mwenye anaweza kufa anaonaka?

 5 Je, siku zako ni kama siku za wanadamu wenye wanaweza kufa,

Ao miaka yako ni kama ya mwanadamu,+

 6 Ili utafute kosa langu

Na kuendelea kutafuta zambi yangu?+

 7 Unajua kwamba sina hatia;+

Na hakuna mwenye anaweza kuniokoa katika mukono wako.+

 8 Mikono yako mwenyewe ilinitengeneza na kunifanya,+

Lakini sasa unataka kuniharibu kabisa.

 9 Tafazali, kumbuka kwamba ulinifanya kwa udongo,+

Lakini sasa unanirudisha katika mavumbi.+

10 Haukunimwanga kama maziwa

Na kunigandisha kama jibini?*

11 Ulinivalisha ngozi na nyama,

Ukanisuka kwa mifupa na mishipa.+

12 Umenipatia uzima na upendo mushikamanifu;

Umelinda roho yangu* na kuitunza.+

13 Lakini ulikusudia kwa siri kufanya mambo haya.*

Ninajua kwamba mambo haya yametoka kwako.

14 Kama nilifanya zambi, ungeniangalia,+

Na ungekataa kunisamehe kosa langu.

15 Kama niko na hatia, ole wangu!

Na hata kama sina kosa, siwezi kuinua kichwa changu,+

Kwa sababu nimejaa haya na mateso.+

16 Kama ninainua kichwa changu, unaniwinda kama simba+

Na tena unaonyesha nguvu zako ili kuniumiza.

17 Unaleta mashahidi wapya ili kunipinga

Na kuongeza kasirani yako juu yangu,

Wakati magumu juu ya magumu yanakuja juu yangu.

18 Basi sababu gani ulinitosha ndani ya tumbo la uzazi?+

Afazali ningekufa mbele jicho lolote linione.

19 Ingekuwa kama vile sijapata kuwa hata siku moja;

Ningekamatwa kutoka katika tumbo la uzazi na kupelekewa moja kwa moja ndani ya kaburi.’

20 Je, siku zangu haziko kidogo?+ Basi aniache;

Ageuzie macho yake mbali na mimi, ili nipumuzike kidogo*+

21 Mbele ya mimi kuenda⁠—​na sitarudia+⁠—

Kwenye inchi ya giza kubwa,+

22 Kwenye inchi ya giza nzito,

Inchi ya kivuli kizito na muvurugo,

Kwenye hata mwangaza unafanana na giza.”

11 Sofari+ Munaamati akajibu:

 2 “Je, maneno haya yote yatakosa kujibiwa,

Ao je, kusema mingi kutafanya mutu akuwe na haki?*

 3 Je, maneno yako yenye hayana maana yatanyamazisha watu?

Je, utakosa kukaripiwa na mutu kwa sababu ya maneno yako ya muzaha?+

 4 Kwa maana unasema, ‘Mafundisho yangu ni safi,+

Na niko safi mbele ya macho yako.’+

 5 Lakini ingekuwa muzuri kama Mungu angesema

Na kukufungulia midomo yake!+

 6 Halafu angekufunulia siri za hekima,

Kwa maana hekima yenye kutenda inatia ndani mambo mengi.

Basi ungetambua kwamba Mungu anaruhusu sehemu fulani ya kosa lako isahauliwe.

 7 Je, unaweza kuvumbua mambo mazito ya Mungu

Ao kuvumbua kila kitu juu ya* Mweza-Yote?

 8 Hekima yake iko juu kuliko mbingu. Wewe unaweza kufanya nini?

Inashuka chini sana kuliko Kaburi.* Wewe unaweza kujua nini?

 9 Ni ya murefu kuliko dunia

Na kubwa kuliko bahari.

10 Akipita na kumukamata mutu fulani na kuitisha tribinali,

Ni nani anaweza kumupinga?

11 Kwa maana anajua wakati watu wanatenda kwa udanganyifu.

Wakati anaona mambo maovu, je, hatayakazia uangalifu?

12 Lakini mupumbavu ataelewa

Wakati tu punda wa pori ataweza kuzaa mwanadamu.*

13 Ingekuwa muzuri kama ungetayarisha moyo wako

Na kumuinulia mikono yako.

14 Kama mukono wako unatenda mambo ya mubaya, uutupe mbali,

Na usiruhusu ukosefu wa haki ukae katika mahema yako.

15 Halafu utaweza kuinua uso wako bila kasoro;

Na utaweza kusimama imara, bila kuogopa.

16 Halafu utasahau taabu yako;

Utaikumbuka kama maji yenye yameteremuka na kukupita.

17 Maisha yako yatangaa kuliko katikati ya muchana;

Hata giza lake litakuwa kama asubui.

18 Utakuwa na uhakika kwa sababu kuko tumaini,

Na utaangalia huku na huku na kulala kwa usalama.

19 Utalala, bila mutu wa kukuogopesha,

Na watu wengi watatafuta wema wako.

20 Lakini macho ya waovu yatakuwa zaifu;

Na hawatapata mahali pa kukimbilia,

Na tumaini lao litakuwa tu kifo.”+

12 Kisha Yobu akajibu:

 2 “Kwa kweli ninyi ndio watu wenye kujua mambo,*

Na hekima itakufa pamoja na ninyi!

 3 Lakini mimi pia niko na uelewaji.*

Mimi siko mudogo kuliko ninyi.

Ni nani mwenye hajue mambo haya?

 4 Nimekuwa kitu cha kuchekwa na marafiki wangu,+

Mutu mwenye kumuita Mungu ili amujibu.+

Mwenye haki na mwenye hana lawama ni kitu cha kuchekwa.

 5 Mutu mwenye hana mahangaiko anazarau musiba,

Anafikiri kwamba musiba unafikia tu watu wenye miguu ya kuyumba-yumba.*

 6 Mahema ya wanyanganyi yako na amani,+

Na wale wenye kumuchokoza Mungu wako salama,+

Wale wenye kuwa na mungu wao katika mikono yao.

 7 Lakini, tafazali, uliza wanyama, nao watakufundisha;

Pia ndege wa anga, nao watakuambia.

 8 Ao uchunguze* dunia, nayo itakufundisha;

Na samaki wa bahari watakutangazia jambo hilo.

 9 Ni nani kati yao mwenye hajue

Kwamba mukono wa Yehova umefanya hayo?

10 Uzima wa kila kitu chenye uzima uko* katika mukono wake

Na roho* ya kila mwanadamu.*+

11 Je, sikio halipime maneno

Kama vile ulimi* unaonja chakula?+

12 Je, haiko wazee ndio wenye kuwa na hekima,+

Na je, uelewaji haukuje kwa sababu ya kuishi siku nyingi?

13 Yeye iko* na hekima na nguvu;+

Iko* na mashauri na uelewaji.+

14 Akibomoa kitu, hakiwezi kujengwa tena;+

Kile amefunga, hakuna mutu anaweza kufungua.

15 Akizuia maji, kila kitu kinakauka;+

Akiyaachilia, yanalemea dunia.+

16 Yeye iko* na nguvu na hekima yenye kutenda;+

Mwenye kudanganywa na mwenye kudanganya wote ni wake;

17 Anafanya washauri watembee miguu wazi,*

Na anafanya waamuzi kuwa wapumbavu.+

18 Anafungua minyororo yenye kufungwa na wafalme,+

Na anafunga mukaba* kuzunguka viuno vyao.

19 Anafanya makuhani watembee miguu wazi,+

Na anapindua wale wenye kuwa imara kabisa katika mamlaka;+

20 Ananyamazisha washauri wenye kutumainiwa

Na anaondoa hekima ya wazee;

21 Anamwanga zarau juu ya watu wenye vyeo,+

Na kufanya wenye nguvu kuwa wazaifu;*

22 Anafunua mambo mazito yenye kuwa katika giza,+

Na anafanya giza nzito kuwa mwangaza;

23 Anafanya mataifa yakuwe na nguvu ili ayaharibu;

Anafanya mataifa yakuwe makubwa ili ayapeleke katika uhamisho.

24 Anaondoa uelewaji* wa viongozi wa watu

Na kuwafanya watange-tange kwenye hakuna njia katika maeneo yenye yameachwa.+

25 Wanapapasa-papasa katika giza,+ kwenye hakuna mwangaza;

Anawafanya watange-tange kama walevi.+

13 “Ndiyo, jicho langu limeona mambo hayo yote,

Sikio langu limeyasikia na kuyaelewa.

 2 Mambo yenye munajua, mimi pia ninayajua;

Mimi siko mudogo kuliko ninyi.

 3 Kwa upande wangu, ingekuwa muzuri kama ningesema mimi mwenyewe na Mweza-Yote;

Ninatamani kutetea kesi yangu ya hukumu mbele ya Mungu.+

 4 Lakini munanipakaa uongo;

Ninyi wote ni wanganga wenye hawana faida yoyote.+

 5 Ingekuwa muzuri kama mungenyamaza kabisa,

Hilo lingeonyesha kwamba muko na hekima.+

 6 Tafazali, musikilize mawazo yangu,

Na mukazie uangalifu maombi ya midomo yangu.

 7 Je, mutamusemea Mungu maneno yenye hayako ya haki,

Na je, mutasema kwa udanganyifu kwa ajili yake?

 8 Je, mutakuwa upande wake,*

Je, mutajaribu kutetea kesi ya hukumu ya Mungu wa kweli?

 9 Je, mutapona kama anawachunguza?+

Je, mutamudanganya kama vile mungemudanganya mwanadamu mwenye anaweza kufa?

10 Hakika atawakaripia

Kama munajaribu kuonyesha upendeleo kwa siri.+

11 Je, utukufu wake mwenyewe hautawaogopesha sana

Na woga wake hautawaangukia?

12 Maneno yenu ya hekima ni mezali za majivu;

Maneno yenu ya kujitetea ni zaifu kama vile ngao za udongo.

13 Munyamaze mbele yangu, ili mimi pia niseme.

Kisha muache kile kitanipata kinipate!

14 Sababu gani ninajiweka katika hatari*

Na kuweka uzima wangu* katika mikono yangu?

15 Hata kama angeniua, ningeendelea kungojea;+

Ningetetea kesi yangu ya hukumu mbele ya uso wake.

16 Halafu angekuwa wokovu wangu,+

Kwa maana mutu mwenye hamuogope Mungu* hawezi kuingia mbele yake.+

17 Musikilize kwa uangalifu maneno yangu;

Mukazie uangalifu mambo yenye ninasema.

18 Muone, sasa, nimetayarisha kesi yangu ya hukumu;

Ninajua kwamba niko na haki.

19 Ni nani atashindana na mimi?

Ningekufa kama ningenyamaza!*

20 Ee Mungu, ninakuomba tu mambo mbili,

Ili nisijifiche mbele yako:

21 Ondoa mukono wako muzito juu yangu,

Na usiache woga wako uniogopeshe.+

22 Ao uite na mimi nitajibu,

Ao uniache niseme, na wewe unijibu.

23 Nimefanya makosa na zambi gani?

Unionyeshe kosa langu na zambi yangu.

24 Sababu gani unaficha uso wako+

Na kuniona kuwa adui yako?+

25 Je, utajaribu kuogopesha jani lenye kupeperushwa na upepo

Ao kufuatilia majani yenye kukauka?

26 Kwa maana unaendelea kuandika mashitaka makali juu yangu,

Na unanifanya nipate matokeo ya zambi za ujana wangu.

27 Umetia miguu yangu katika mikatale,

Unachunguza njia zangu zote,

Na unafuata kila alama ya miguu yangu.

28 Kwa hiyo mwanadamu* anaharibika kama kitu chenye kuoza,

Kama nguo yenye imekuliwa na nondo.*

14 “Mwanadamu, mwenye kuzaliwa na mwanamuke,

Anaishi siku kidogo+ na zenye kujaa taabu.*+

 2 Anatokea kama ua na kisha anakauka;*+

Anakimbia kama kivuli na kupotea.+

 3 Ndiyo, umekaza macho yako juu yake,

Na kumuhukumu.*+

 4 Ni nani anaweza kutosha mutu safi ndani ya mutu mwenye haiko safi?+

Hakuna mwenye anaweza!

 5 Kama siku zake zimeamuliwa,

Unajua hesabu ya miezi yake;

Umemuwekea mupaka ili asiweze kuvuka.+

 6 Geuza macho yako usimuangalie ili apumuzike,

Mupaka wakati atamaliza siku yake, kama mufanyakazi wa kulipwa.+

 7 Kwa maana kuko tumaini hata kwa ajili ya muti.

Kama unakatwa, utaota tena,

Na matawi yake yataendelea kukomaa.

 8 Kama muzizi wake unazeeka katika udongo

Na kama kisiki chake kinakufa ndani ya udongo,

 9 Kwa harufu ya maji utaota tena;

Na utatokeza matawi kama mumea mupya.

10 Lakini mwanadamu anakufa na analala bila nguvu yoyote;

Wakati mwanadamu anakufa, iko* wapi?+

11 Maji yanakauka katika bahari,

Na muto unateremuka na kukauka.

12 Mwanadamu pia analala na haamuke.+

Hawataamuka mupaka wakati mbingu haitakuwa tena,

Wala hawataamushwa katika usingizi wao.+

13 Ingekuwa muzuri kama ungenificha katika Kaburi,*+

Ungenificha mupaka kasirani yako ipite,

Ungeniwekea kipindi cha wakati na kunikumbuka!+

14 Kama mutu anakufa, je, anaweza kuishi tena?+

Nitangojea siku zote za kazi yangu ya kulazimishwa

Mupaka wakati kitulizo changu kitakuja.+

15 Utaita, na mimi nitakujibu.+

Utatamani sana kazi ya mikono yako.

16 Lakini sasa, unaendelea kuhesabu kila hatua yangu;

Unaangalia tu zambi yangu.

17 Zambi yangu imefungwa ndani ya mufuko na kutiwa muhuri,

Na unatia muhuri juu ya kosa langu kwa gundi.*

18 Kama vile mulima unaanguka na kuporomoka

Na mwamba unaondolewa mahali pake,

19 Kama vile maji yanakula majiwe

Na maji yake mengi yanateremusha udongo wa dunia,

Ni vile umeharibu tumaini la mwanadamu mwenye anaweza kufa.

20 Unaendelea kumupita nguvu mupaka wakati anakufa;+

Unabadilisha uso wake, na unamufukuza.

21 Wana wake wanaheshimiwa, lakini yeye hajue;

Wanazarauliwa, lakini yeye hatambue jambo hilo.+

22 Anasikia maumivu wakati tu angali muzima;

Anaomboleza* wakati tu angali anaishi.”

15 Elifazi+ Mutemani akajibu:

 2 “Mutu mwenye hekima atajibu kwa maneno yenye hayana maana,*

Ao atajaza tumbo lake kwa upepo wa mashariki?

 3 Kukaripia kwa maneno ya bure-bure hakuna faida,

Na kusema-sema tu hakuna maana yoyote.

 4 Kwa maana wewe unapunguza nguvu za woga wa Mungu,

Na unapunguza nia yoyote ya kumuhangaikia Mungu.

 5 Kwa maana kosa lako linakufanya useme mambo yenye unasema,*

Na unachagua maneno ya ujanja.

 6 Kinywa chako mwenyewe kinakuhukumu, wala haiko mimi;

Midomo yako mwenyewe inatoa ushuhuda wenye unakupinga.+

 7 Je, ni wewe ulikuwa mwanadamu wa kwanza kuzaliwa,

Ao je, ulizaliwa mbele ya vilima kuzaliwa?

 8 Je, wewe unasikilizaka mazungumuzo ya siri ya Mungu,

Ao je, unawaza kama wewe tu ndiye uko na hekima?

 9 Unajua nini yenye sisi hatujue?+

Unaelewa nini yenye sisi hatuelewe?

10 Watu wenye imvi na wazee wako kati yetu,+

Watu wenye miaka mingi kuliko baba yako.

11 Je, hautosheke na faraja za Mungu,

Ao maneno ya upole yenye unaambiwa?

12 Sababu gani moyo wako unakupeleka mbali,

Na sababu gani macho yako yanawaka kasirani?

13 Kwa maana unafanya roho yako imukasirikie Mungu,

Na unaacha maneno kama hayo yatoke katika kinywa chako mwenyewe.

14 Je, mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nani ili akuwe safi,

Ao mutu mwenye alizaliwa na mwanamuke ni nani ili akuwe mwenye haki?+

15 Angalia! Hana imani katika watakatifu wake,

Hata mbingu haziko safi mbele ya macho yake.+

16 Namna gani basi mutu mwenye kuchukiza na mwenye kupotoka,+

Mwanadamu mwenye anakunywa ukosefu wa haki kama vile maji!

17 Nitakuelezea; unisikilize!

Nitaeleza mambo yenye nimeona,

18 Mambo yenye watu wenye hekima wamejifunza kutoka kwa baba zao,+

Mambo yenye hawakuficha.

19 Wao peke yao ndio walipewa inchi,

Na hakuna mugeni mwenye alipita kati yao.

20 Mutu muovu anateseka siku zake zote,

Katika miaka yote yenye imewekwa kwa ajili ya mutesaji.

21 Sauti zenye kuogopesha sana ziko katika masikio yake;+

Wakati wa amani, wanyanganyi wanamushambulia.

22 Haamini kwamba ataponyoka giza;+

Amewekwa ili kuuawa kwa upanga.

23 Anatanga-tanga ili kutafuta chakula*⁠—​kiko wapi?

Anajua muzuri kwamba siku ya giza inakaribia.

24 Taabu na uchungu vinaendelea kumuogopesha sana;

Vinamushinda nguvu kama mufalme mwenye kuwa tayari kushambulia.

25 Kwa maana ananyoosha mukono wake ili kumupinga Mungu

Na anajaribu kumupinga* Mweza-Yote;

26 Kwa kichwa-nguvu anakimbia ili kumushambulia,

Akiwa na ngao ya munene, yenye kuwa ngumu;*

27 Uso wake unafunikwa na mafuta,

Na viuno vyake vinajaa mafuta;

28 Anakaa katika miji yenye itaharibiwa,

Katika nyumba zenye hakuna mutu atakaa ndani,

Zenye zitakuwa marundo ya majiwe.

29 Hatakuwa tajiri na mali yake haitaongezeka,

Wala vitu vyake havitaenea katika inchi.

30 Hataponyoka giza;

Mwali wa moto utakausha tawi lake,*

Na atakufa kwa mulipuko wa pumuzi ya kinywa cha Mungu.*+

31 Hapaswe kupotoka na kutegemea mambo yenye hayana mafaa yoyote,

Kwa maana kile anapata kwa kubadilishana na kitu kingine hakitakuwa na mafaa yoyote;

32 Jambo hilo litatendeka mbele ya siku yake kufika,

Na matawi yake hayatakuwa katika hali ya muzuri hata siku moja.+

33 Atakuwa kama muzabibu wenye unaangusha zabibu za mubichi,

Na kama muzeituni wenye unaangusha maua yake.

34 Kwa maana mukusanyiko wa watu wenye hawamuogope Mungu* hautazaa kitu,+

Na moto utateketeza mahema ya rushwa.*

35 Wanabeba mimba ya ubaya na kuzaa uovu,

Na tumbo lao la uzazi linazaa udanganyifu.”

16 Yobu akajibu:

 2 “Nimesikia mambo mengi kama hayo zamani.

Ninyi wote ni wafariji wenye kusumbua!+

 3 Je, maneno yenye hayana maana yatakuwa na mwisho?

Ni nini inawachochea kujibu hivi?

 4 Mimi pia ningeweza kusema kama ninyi.

Kama mungekuwa katika hali yangu,*

Ningesema maneno yenye kusadikisha ili kuwashambulia

Na ningetikisa kichwa changu juu yenu.+

 5 Lakini, kuliko kufanya vile, ningewatia nguvu kwa maneno ya kinywa changu,

Na faraja ya midomo yangu ingewatuliza.+

 6 Hata nikisema, maumivu yangu hayatulie,+

Na nikiacha kusema, maumivu yangu yanapunguka kwa kadiri gani?

 7 Lakini sasa amenichokesha;+

Ameharibu watu wote wa nyumba yangu.*

 8 Pia unanikamata, na huo umekuwa ushahidi,

Na hivyo kukonda kwangu kunaonekana na kunatoa ushahidi mbele ya uso wangu.

 9 Kasirani yake imenipasua vipande-vipande, na ananiwekea kinyongo.+

Ananisagia meno yake.

Adui yangu ananitoboa na macho yake.+

10 Wamefungua kinywa chao wazi juu yangu,+

Na wamepiga machafu yangu kwa zarau;

Wanakusanyika kwa wingi ili kunishambulia.+

11 Mungu ananiweka katika mikono ya vijana wadogo wanaume,

Na ananitupa kwa nguvu katika mikono ya waovu.+

12 Nilikuwa nimekaa bila wasiwasi, lakini akanivunja-vunja;+

Alinikamata nyuma ya shingo na kuniponda-ponda;

Kisha akanifanya kuwa shabaha yake.

13 Wapiga-mishale wake wananizunguka;+

Anatoboa figo zangu+ na hasikie huruma;

Anamwanga nyongo* yangu juu ya udongo.

14 Ananitoboa matundu-matundu;

Ananishambulia kama mupiganaji-vita.

15 Nimeshona nguo ya gunia ili kufunika ngozi yangu,+

Na nimezika heshima* yangu katika mavumbi.+

16 Uso wangu ni mwekundu kwa sababu ya kulia,+

Na kuko kivuli kizito* juu ya kope za macho yangu,

17 Hata kama mikono yangu haijafanya jeuri yoyote

Na sala yangu iko safi.

18 Ee dunia, usifunike damu yangu!+

Na acha kilio changu kisikuwe na mahali pa kupumuzikia!

19 Hata sasa, shahidi wangu iko* mbinguni;

Mwenye anaweza kunitetea iko katika nafasi za juu.

20 Marafiki wangu wananichekelea+

Wakati jicho langu linamumwangia Mungu machozi.*+

21 Acha mutu akuwe muamuzi kati ya mwanadamu na Mungu,

Kama vile mutu anaweza kufanya kati ya mwanadamu na mwenzake.+

22 Kwa maana miaka yenye imebakia ni kidogo,

Na nitaenda katika njia yenye hakuna kurudia tena.+

17 “Roho yangu imevunjika, siku zangu zimezimishwa;

Kaburi linaningojea.+

 2 Watu wenye kufanya zihaka wananizunguka,+

Na macho yangu yanalazimika kutazama* mwenendo wao wa uasi.

 3 Tafazali, kubali kitu chenye ninakuwekesha, na ukiweke.

Ni nani mwingine atanishika mukono na kutoa ahadi kwa ajili yangu?+

 4 Kwa sababu umeficha utambuzi mbali na moyo wao;+

Ndiyo maana hauwainue.

 5 Anaweza kuamua kufurahia vitu vyake pamoja na marafiki wake,

Lakini wakati uleule macho ya watoto wake yako zaifu.

 6 Amenifanya kuwa kitu cha kuzarauliwa* kati ya vikundi vya watu,+

Na hivyo nimekuwa mutu wa kutemewa mate kwenye uso.+

 7 Macho yangu yanafifia kwa sababu ya uchungu,+

Na viungo vyote vya mwili wangu viko kama kivuli.

 8 Watu wanyoofu wanashangaa kwa sababu ya jambo hilo,

Na mutu mwenye hana kosa anasumbuka kwa sababu ya mutu mwenye hamuogope Mungu.*

 9 Mwenye haki anaendelea kufuata njia yake,+

Na mwenye mikono safi anaendelea kuwa na nguvu.+

10 Lakini, ninyi wote munaweza kuja na kusema tena mawazo yenu,

Kwa maana sikuona mutu mwenye hekima kati yenu.+

11 Siku zangu zimeisha;+

Mipango yangu, tamaa za moyo wangu, zimevunjwa.+

12 Wanaendelea kugeuza usiku kuwa muchana,

Wanasema, ‘Mwangaza unapaswa kuwa karibu kwa sababu kuko giza.’

13 Nikiendelea kungojea, Kaburi* litakuwa nyumba yangu;+

Nitatandika kitanda changu katika giza.+

14 Nitaambia shimo* kwa sauti kubwa,+ ‘Wewe ni baba yangu!’

Na funza,* ‘Wewe ni mama yangu na dada yangu!’

15 Basi, tumaini langu liko wapi?+

Ni nani anaweza kuona tumaini langu?

16 Hilo* litashuka kwenye milango mikubwa ya Kaburi* yenye mapingo*

Wakati sisi wote tutashuka pamoja katika mavumbi.”+

18 Bildadi+ Mushua akajibu:

 2 “Mutaacha kusema maneno kama haya wakati gani?

Mujaribu kuelewa ili na sisi tuseme.

 3 Sababu gani tuonekane kuwa wanyama+

Na kuonekana kuwa wajinga* mbele ya macho yenu?

 4 Hata kama unajipasua mwenyewe* vipande-vipande katika kasirani yako,

Je, dunia itaachwa kwa sababu yako,

Ao je, mwamba utaondoka mahali pake?

 5 Ndiyo, mwangaza wa muovu utazimishwa,

Na mwali wake wa moto hautangaa.+

 6 Mwangaza katika hema yake utakuwa giza,

Na taa yenye kuwa juu yake itazimishwa.

 7 Hatua zake zenye nguvu zimefupishwa,

Na shauri lake mwenyewe litamwangusha.+

 8 Kwa maana miguu yake itamuingiza ndani ya wavu,*

Na atatanga-tanga kwenye kamba za wavu.

 9 Mutego utamunasa kwenye kisigino;

Na mutego utamukamata.+

10 Kamba imefichwa katika udongo kwa ajili yake,

Na mutego uko katika njia yake.

11 Vitu vyenye kuogopesha vinamutisha pande zote,+

Na vinamufuatilia karibu na miguu yake.

12 Nguvu zake zimepunguka,

Na musiba+ utamufanya ayumbe-yumbe.*

13 Ngozi yake imekuliwa;

Ugonjwa hatari sana unakula* viungo vya mwili wake.

14 Ameondolewa katika usalama wa hema yake+

Na kuenda kwa mufalme mwenye kuogopesha sana.*

15 Wageni watakaa katika hema yake;

Kiberiti kitasambazwa juu ya makao yake.+

16 Mizizi yake itakauka chini yake,

Na matawi yake yatakauka juu yake.

17 Hakuna mwenye atamukumbuka katika dunia,

Na jina lake halitajulikana* katika barabara.

18 Atatoshwa kwenye mwangaza na kupelekwa katika giza

Na atafukuzwa mbali na inchi yenye kuzaa.

19 Hatakuwa na mutoto wala wazao kati ya watu wake,

Na hatakuwa na mutu mwenye ataokoka mahali kwenye anaishi.*

20 Wakati siku yake itafika, watu wa Mangaribi watashituka

Na watu wa Mashariki wataogopa sana.

21 Hayo ndiyo mambo yenye yanatokea kwenye mahema ya mukosaji

Na kwenye makao ya mutu mwenye hamujue Mungu.”

19 Yobu akajibu:

 2 “Mutaendelea kukasirisha nafsi yangu* mupaka wakati gani,+

Na kuniponda na maneno?+

 3 Hii ni mara ya kumi munanikemea;*

Hamusikie haya kunitendea kwa ukali.+

 4 Na kama kwa kweli nimefanya kosa,

Ni kosa langu mimi mwenyewe.

 5 Kama munaendelea kujiinua juu yangu,

Na kuonyesha kwamba ninastahili kulaumiwa,

 6 Basi, mujue kama Mungu ndiye amenidanganya,

Na kunikamata katika wavu wake wa* kuwinda.

 7 Angalia! Ninaendelea kuita kwa sauti kubwa, ‘Jeuri!’ lakini sipate jibu;+

Ninaendelea kuomba musaada, lakini hakuna haki.+

 8 Amefunga njia yangu kwa ukuta wa majiwe, na siwezi kupita;

Amefunika njia zangu kwa giza.+

 9 Ameondoa utukufu wangu

Na kuvua taji juu ya kichwa changu.

10 Amenibomoa kila upande mupaka niangamie;

Anangoa tumaini langu kama muti.

11 Kasirani yake inawaka juu yangu,

Na ananiona kuwa adui yake.+

12 Majeshi yake yanakuja pamoja na kunizunguka kwa ajili ya vita,

Na yanapiga kambi kuzunguka hema yangu.

13 Amefukuza ndugu zangu mbali na mimi,

Na wale wenye kunijua wamegeuka na kuniacha.+

14 Marafiki wangu wa karibu* wameenda,

Na wale wenye nilijua muzuri wamenisahau.+

15 Wageni katika nyumba yangu+ na watumishi wangu wanamuke wananiona kama mugeni;

Nimekuwa mugeni mbele ya macho yao.

16 Ninamuita mutumishi wangu, lakini hajibu;

Ninamulilia kwa kinywa changu ili anisikilie huruma.

17 Harufu ya pumuzi yangu inamuchukiza sana bibi yangu,+

Na ninanuka mubaya mbele ya ndugu zangu.*

18 Hata watoto wadogo wananizarau;

Wakati ninasimama, wanaanza kunicheka.

19 Marafiki wangu wote wa karibu wananichukia,+

Na wale wenye nilipenda wamenigeukia.+

20 Mifupa yangu inakamatana na ngozi na nyama ya mwili wangu,+

Na nimeponyoka na ngozi ya meno yangu.

21 Munionyeshe rehema, marafiki wangu, munionyeshe rehema,

Kwa maana mukono wa Mungu mwenyewe umenigusa.+

22 Sababu gani munaendelea kunitesa kama vile Mungu ananitesa,+

Kwa kunishambulia bila kuacha?*+

23 Ingekuwa muzuri kama maneno yangu yangeandikwa,

Kama yangeandikwa katika kitabu!

24 Kama tu yangeandikwa milele katika mwamba,

Kwa kalamu ya chuma na risasi!

25 Kwa maana ninajua muzuri kwamba mukombozi wangu+ anaishi;

Kisha wakati fulani atakuja na kusimama juu ya dunia.*

26 Kisha ngozi yangu kuharibiwa hivi,

Wakati ningali katika mwili wangu, nitamuona Mungu,

27 Mimi mwenyewe nitamuona,

Macho yangu mwenyewe yatamuona, hapana macho ya mutu mwingine.+

Lakini ndani yangu kabisa ninajisikia mwenye kulemewa!*

28 Kwa maana munasema, ‘Tunamutesa namna gani?’+

Kwa kuwa mimi ndiye chanzo cha lile tatizo.

29 Muogope upanga,+

Kwa maana upanga unaleta azabu juu ya makosa;

Munapaswa kujua kwamba kuko muamuzi.”+

20 Sofari+ Munaamati akajibu:

 2 “Ndiyo sababu mawazo yangu yenye kuhangaisha yananisukuma kujibu

Kwa sababu ya wasiwasi wenye ninasikia.

 3 Nimesikia karipio lenye linanitukana;

Na uelewaji* wangu unanisukuma kujibu.

 4 Hakika unapaswa kuwa umejua jambo hili tangu zamani,

Kwa maana imekuwa vile tangu mwanadamu alitiwa* juu ya dunia,+

 5 Kwamba makelele ya furaha ya waovu ni ya muda tu

Na shangwe ya mutu mwenye hamuogope Mungu* ni ya wakati mufupi.+

 6 Hata kama ukubwa wake unapanda mupaka mbinguni

Na kichwa chake kinafika kwenye mawingu,

 7 Ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe;

Wale wenye walizoea kumuona watasema, ‘Iko* wapi?’

 8 Ataruka mbali kama ndoto, na hawatamupata;

Atafukuzwa mbali kama maono ya usiku.

 9 Jicho lenye lilimuona halitamuona tena,

Na mahali pake hapatamuona tena.+

10 Watoto wake watatafuta maskini ili wawaonyeshe wema,

Na mikono yake mwenyewe itarudisha mali yake.+

11 Mifupa yake ilikuwa na nguvu nyingi za ujana,

Lakini hizo* zitalala pamoja naye katika mavumbi tu.

12 Kama mambo ya mubaya ni matamu katika kinywa chake,

Kama anayaficha chini ya ulimi wake,

13 Kama anayaonja na hataki kuyatema

Lakini anaendelea kuyaacha katika kinywa chake,

14 Chakula chake kitageuka kuwa kichungu ndani ya tumbo lake;

Kitakuwa kama sumu* ya nyoka-kobra ndani yake.

15 Amemeza mali, lakini ataitapika;

Mungu ataiondoa katika tumbo lake.

16 Atanyonya sumu ya nyoka-kobra;

Meno ya nyoka-kipiri yatamuua.*

17 Hakuna siku ataona mito midogo ya maji,

Mito ya asali na siagi.

18 Atarudisha vitu vyake bila kuvitumia;*

Hatafurahia utajiri wa biashara yake.+

19 Kwa maana ameponda-ponda na kuacha maskini;

Amenyanganya nyumba yenye hakujenga.

20 Lakini hatakuwa na amani ndani yake mwenyewe;

Utajiri wake hautamusaidia kuponyoka.

21 Hakuna kitu chenye kitabakia ili akimeze;

Ndiyo sababu hali yake ya muzuri haitaendelea.

22 Wakati mali yake itakuwa mingi sana, atapatwa na mahangaiko;

Nguvu zote za taabu zitakuja kumushambulia.

23 Wakati atakuwa anajaza tumbo lake,

Mungu* atamumwangia kasirani yake yenye kuwaka,

Atamunyeshea kasirani hiyo mupaka ndani ya matumbo yake.

24 Wakati atakimbia silaha za chuma,

Mishale ya upinde wa shaba itamutoboa.

25 Anachomoa mushale kwenye mugongo wake,

Silaha yenye kungaa katika nyongo* yake,

Na woga mukubwa unamukamata.+

26 Giza kubwa litafunika hazina zake;

Moto wenye hakuna mwenye aliuchochea utamuteketeza;

Musiba unamungojea mutu yeyote mwenye ataponyoka mwenye anapatikana katika hema yake.

27 Mbingu itafunua kosa lake;

Dunia itasimama ili kumupinga.

28 Mafuriko yatafagilia mbali nyumba yake;

Yatakuwa muto wenye nguvu katika siku ya kasirani ya Mungu.*

29 Hilo ndilo fungu lenye Mungu anapatia mutu muovu,

Uriti wenye Mungu amemuamulia.”

21 Yobu akajibu:

 2 “Musikilize kwa uangalifu mambo yenye ninasema;

Na hiyo ikuwe ndiyo faraja yenye munanipatia.

 3 Munivumilie wakati ninasema;

Kisha mimi kusema, munaweza sasa kunichekelea.+

 4 Je, malalamiko yangu ninayapeleka kwa mwanadamu?

Kama ni vile, ningekosa uvumilivu, haiko vile?

 5 Muniangalie na muendelee kushangaa;

Mutie mukono wenu juu ya kinywa chenu.

 6 Wakati ninafikiria jambo hilo, ninavurugika,

Na mwili wangu wote unatetemeka.

 7 Sababu gani waovu wanaendelea kuishi,+

Wanazeeka, na kuwa matajiri?*+

 8 Kila siku watoto wao wako mbele yao,

Na wanaishi na kuona wazao wao.

 9 Nyumba zao ziko na usalama, hawaogope kitu,+

Na Mungu hawapatie azabu kwa fimbo yake.

10 Ngombe-dume wao wanaingiza mimba bila tatizo;

Ngombe-dike wao wanazaa na mimba zao hazitokake.

11 Vijana wao wanaume wanakimbia inje kama vile kundi,

Na watoto wao wanaruka huku na huku.

12 Wanaimba kwa ngoma ya kidogo* na kinubi

Na wanafurahi wakati wanasikia sauti ya filimbi.*+

13 Wanapitisha siku zao katika maisha ya furaha

Na wanashuka kwa amani* katika Kaburi.*

14 Lakini wanamuambia Mungu wa kweli, ‘Utuache!

Hatutaki kujua njia zako.+

15 Mweza-Yote ni nani ili tumutumikie?+

Tutapata faida gani tukimujua?’+

16 Lakini ninajua kwamba hawana uwezo wa kujiletea hali ya muzuri.+

Mawazo* ya waovu yako mbali na mimi.+

17 Ni mara ngapi taa ya waovu inazimishwa?+

Ni mara ngapi wanapatwa na musiba?

Ni mara ngapi Mungu anawaharibu kwa kasirani yake?

18 Je, kuko siku wamekuwa kama majani yenye kukauka mbele ya upepo

Na kama maganda ya mbegu yenye kupeperushwa na zoruba?

19 Mungu ataweka akiba ya azabu ya mutu kwa ajili ya wana wake mwenyewe.

Lakini acha Mungu amulipe ili ajue jambo hilo.+

20 Na macho yake mwenyewe yaone kuharibiwa kwake,

Na akunywe kasirani kali ya Mweza-Yote.+

21 Sababu gani ahangaikie kile chenye kitapata nyumba yake kisha kifo chake

Kama hesabu ya miezi yake imefupishwa?+

22 Je, kuko mutu mwenye anaweza kumufundisha Mungu ujuzi,*+

Wakati Yeye ndiye anahukumu hata wenye kuwa juu zaidi?+

23 Mutu mumoja anakufa wakati angali na nguvu zake zote+

Wakati hana wasiwasi kabisa na hana mahangaiko,+

24 Wakati mapaja yake yamenenepa kwa mafuta

Na mifupa yake ikiwa yenye nguvu.*

25 Lakini mutu mwingine anakufa kisha kuteseka sana,*

Akiwa hajaonja hata siku moja mambo ya muzuri.

26 Wote watalala katika mavumbi,+

Na funza* watawafunika wote wawili.+

27 Angalia! Ninajua hakika mawazo yenu

Na mipango yenye munafanya ili kunifanya mubaya.*+

28 Kwa maana munasema, ‘Iko wapi nyumba ya ule mutu wa maana,

Na iko wapi hema yenye muovu aliishi ndani yake?’+

29 Je, hamukuuliza watu wenye kusafiri?

Je, hamukujifunza kwa uangalifu mawazo yao,*

30 Kwamba mutu muovu analindwa katika siku ya musiba,

Na kuokolewa katika siku ya kasirani kali?

31 Ni nani mwenye atamukemea kuhusu njia yake,

Na ni nani atamulipa kwa sababu ya mambo yenye amefanya?

32 Wakati anapelekwa kwenye makaburi,

Watakesha kwenye kaburi lake.

33 Madonge ya udongo wa bonde* yatakuwa matamu kwake,+

Na wanadamu wote watamufuata*+

Kama vile wengi wenye hawana hesabu wenye walimutangulia.

34 Kwa hiyo sababu gani munanifariji na maneno yenye hayana maana?+

Katika majibu yenu hamuna kitu kingine isipokuwa tu udanganyifu!”

22 Elifazi+ Mutemani akajibu:

 2 “Je, mwanadamu anaweza kuwa na faida kwa Mungu?

Je, mutu mwenye ufahamu anaweza kuwa na faida kwake?+

 3 Je, Mweza-Yote anahangaika* kwamba wewe ni mwenye haki,

Ao je, anapata faida yoyote kwa sababu unafuata njia ya uaminifu-mushikamanifu?+

 4 Je, atakupatia azabu

Na kuingia katika hukumu pamoja na wewe kwa sababu unamuheshimia?

 5 Je, haiko kwa sababu ya uovu wako mwingi sana

Na makosa yako hayana mwisho?+

 6 Kwa maana wewe unanyanganya ndugu zako bila sababu kitu chenye kiliwekeshwa kwa ajili ya mukopo,

Na unavua watu nguo zao, na kuwaacha uchi.*+

 7 Haupatie mwenye kuchoka maji ya kunywa,

Na unakataa kumupatia chakula mutu mwenye njaa.+

 8 Inchi ni ya mutu mwenye nguvu,+

Na mutu mwenye kupendelewa anakaa ndani yake.

 9 Lakini ulifukuza wajane mikono wazi,

Na uliponda-ponda mikono ya watoto wenye hawana baba.*

10 Ndiyo sababu umezungukwa na mitego,*+

Na woga mukubwa wa bila kutazamia unakuletea wasiwasi;

11 Ndiyo sababu kuko giza kubwa lenye linafanya usione,

Na mafuriko ya maji yamekufunika.

12 Je, Mungu haiko katika nafasi za juu za mbingu?

Na angalia namna nyota zote ziko juu sana.

13 Lakini umesema: ‘Kwa kweli Mungu anajua nini?

Je, anaweza kuhukumu katika giza nzito?

14 Mawingu yanamuzuia ili asione

Wakati anatembea kwenye muviringo wa mbingu.’

15 Utafuata njia ya zamani

Yenye watu waovu wamefuata,

16 Watu wenye walichukuliwa* mbele ya wakati wao kufika,

Wenye musingi wao ulifagiliwa mbali na mafuriko?*+

17 Walikuwa wanamuambia Mungu wa kweli: ‘Utuache!’

Na ‘Mweza-Yote anaweza kutufanya nini?’

18 Lakini, Yeye ndiye alijaza nyumba zao vitu vya muzuri.

(Mawazo maovu kama hayo hayako ndani yangu.)

19 Wenye haki wataona jambo hilo na kushangilia,

Na wenye hawana kosa watawachekelea na kusema:

20 ‘Wapinzani wetu wameharibiwa,

Na moto utateketeza mambo yao yenye yalibakia.’

21 Ujikaze umujue, na utakuwa na amani;

Halafu mambo ya muzuri yatakujia.

22 Kubali sheria ya kinywa chake,

Na uweke maneno yake katika moyo wako.+

23 Ukimurudilia Mweza-Yote, utarudishwa katika hali ya muzuri;+

Ukiondoa ukosefu wa haki katika hema yako,

24 Ukitupa zahabu yako* katika mavumbi

Na zahabu ya Ofiri+ katika mabonde yenye miamba,

25 Halafu Mweza-Yote atakuwa zahabu yako,

Na atakuwa feza yako ya muzuri kabisa.

26 Kisha utafurahi kwa sababu ya Mweza-Yote,

Na utamuinulia Mungu uso wako.

27 Utamulilia, na atakusikia;

Na utatimiza naziri zako.

28 Kila kitu chenye utaamua kufanya kitakuwa na matokeo ya muzuri,

Na mwangaza utaangazia njia yako.

29 Kwa maana utapatishwa haya wakati utaongea kwa kiburi,

Lakini ataokoa munyenyekevu.*

30 Ataokoa watu wenye hawana kosa;

Kwa hiyo kama mikono yako iko safi, hakika utaokolewa.”

23 Yobu akajibu:

 2 “Hata leo nitatoa malalamiko yangu kwa kichwa-nguvu;*+

Nguvu zangu zimeisha juu ya kulia kwa sababu ya maumivu.

 3 Ingekuwa muzuri kama ningejua mahali kwenye ningemupata Mungu!+

Ningeenda mahali pake kwenye anakaa.+

 4 Ningepeleka kesi yangu ya hukumu mbele yake

Na kujaza kinywa changu mawazo ya kujitetea;

 5 Ningejua namna angenijibu

Na ningefikiria mambo yenye angeniambia.

 6 Je, angeshindana na mimi kwa nguvu zake nyingi?

Hapana, hakika angenisikia.+

 7 Pale mutu munyoofu angenyoosha mambo pamoja naye,

Na Muamuzi wangu angetangaza kuwa sina kosa milele.

 8 Lakini nikienda upande wa mashariki, haiko kule;

Na nikirudia, simupate.

 9 Wakati anafanya kazi upande wa kushoto, siwezi kumuangalia;

Kisha anageukia upande wa kuume, lakini tu simuone.

10 Lakini anajua njia yenye nimefuata.+

Akiisha kunijaribu, nitatoka nikiwa safi kama vile zahabu.+

11 Miguu yangu imefuata karibu-karibu alama za miguu yake;

Nimefuata njia yake bila kugeukia upande mwingine.+

12 Sijaacha amri ya midomo yake.

Nimeweka maneno yake kama hazina+ kuliko hata mambo yenye niliombwa kufanya.*

13 Wakati amekusudia kufanya jambo fulani, ni nani anaweza kumupinga?+

Wakati anataka* kufanya jambo fulani, yeye analifanya.+

14 Kwa maana atatenda mambo yote yenye amekusudia kunitendea,

Na ametayarisha mambo mengi kama hayo.

15 Ndiyo maana nimekuwa na wasiwasi kwa sababu yake;

Wakati ninawaza juu yake, woga wangu unaongezeka.

16 Mungu amenifanya nikuwe na moyo wa woga,

Na Mweza-Yote ameniogopesha.

17 Lakini bado sijanyamazishwa na giza

Ao na giza nzito lenye limefunika uso wangu.

24 “Sababu gani Mweza-Yote haweke wakati?+

Sababu gani wale wenye kumujua hawaone siku yake?*

 2 Watu wanasogeza alama za mipaka;+

Wanaiba makundi kwa ajili ya malisho yao.

 3 Wanafukuzia mbali punda wa watoto wenye hawana baba

Na wananyanganya ngombe-dume wa mujane kusudi akuwe kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo.+

 4 Wanasukuma maskini waondoke katika barabara;

Watu wazaifu wa dunia wanalazimika kujificha mbali nao.+

 5 Maskini wanatafuta chakula kama punda wa pori+ katika jangwa;

Wanatafutia watoto wao chakula katika jangwa.

 6 Wanalazimika kuvuna katika mashamba ya wengine*

Na kuokota masalio katika shamba la mizabibu la waovu.

 7 Wanalala usiku wakiwa uchi, bila nguo;+

Hawana kitu cha kujifunika wakati wa baridi.

 8 Wanalowanishwa na mvua ya milima;

Wanashikamana sana na miamba kwa sababu ya kukosa mahali pa kujificha.

 9 Mutoto mwenye hana baba anaondolewa kwa nguvu kwenye maziwa ya mama yake;+

Na nguo za maskini zinakamatwa ili zikuwe kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo,+

10 Wanawalazimisha kutembea uchi, bila nguo,

Na wakiwa na njaa, wakati wanabeba mafungu ya nafaka.

11 Wanafanya kazi ya jasho kati ya kuta za matuta wakati wa joto;*

Wanakanyanga vikamulio vya divai, lakini wanabakia na kiu.+

12 Wenye kuwa karibu kufa wanaendelea kulia kwa maumivu katika muji;

Wenye waliumizwa sana wanalilia* musaada,+

Lakini Mungu haone kama hilo ni kosa.*

13 Kuko wale wenye wanakataa mwangaza;+

Hawatambue njia zake,

Na hawafuate barabara zake.

14 Muuaji anaamuka asubui sana;

Anaua watu wenye hawana uwezo na maskini,+

Na wakati wa usiku anafanya kazi ya kuiba.

15 Jicho la muzinifu linangojea mangaribi wakati giza linaanza,+

Anasema, ‘Hakuna mwenye ataniona!’+

Na anafunika uso wake.

16 Wanavunja* nyumba wakati wa giza;

Muchana wanajifungia ndani.

Hawajue mwangaza ni nini.+

17 Kwa maana wanaona asubui kuwa sawa na giza nzito;

Wanajua vitu vyenye kuogopesha vya giza nzito.

18 Lakini wanabebwa kwa vyepesi na maji.*

Sehemu yao ya inchi italaaniwa.+

Hawatarudia kwenye mashamba yao ya mizabibu.

19 Kama vile ukame na joto vinakausha teluji* yenye kuyeyuka,

Ni vile pia Kaburi* linachukua wenye wametenda zambi!+

20 Mama yake atamusahau;* na funza* atafanya karamu juu yake.

Hatakumbukwa tena.+

Na ukosefu wa haki utavunjwa kama vile muti.

21 Anatesa mwanamuke tasa,

Na anamutendea mubaya mujane.

22 Mungu* atatumia nguvu zake ili kuharibu wenye nguvu;

Hata wakisimama, hawana uhakika wa kuishi.

23 Mungu* anawaacha wajitumainie na kujisikia salama,+

Lakini macho yake yako juu ya matendo yao yote.*+

24 Wanatukuzwa kwa wakati mufupi, kisha hawako tena.+

Wanashushwa chini+ na kukusanywa kama watu wengine;

Wanakatwa kama vichwa vya nafaka.

25 Sasa ni nani anaweza kuonyesha kama mimi niko muongo

Ao kupinga maneno yangu?”

25 Bildadi+ Mushua akajibu:

 2 “Utawala na uwezo wenye kuogopesha ni vyake;

Anaweka amani mbinguni.*

 3 Je, majeshi yake yanaweza kuhesabiwa?

Ni nani mwenye haangaziwe na mwangaza wake?

 4 Basi namna gani mwanadamu mwenye anaweza kufa anaweza kuwa mwenye haki mbele ya Mungu,+

Ao namna gani mutu mwenye alizaliwa na mwanamuke anaweza kuwa bila kosa?*+

 5 Hata mwezi haungae

Na nyota haziko safi mbele ya macho yake,

 6 Namna gani basi mwanadamu mwenye anaweza kufa, ambaye ni funza,*

Na mwana wa binadamu, ambaye ni munyoo!”

26 Yobu akajibu:

 2 “Mumesaidia mutu mwenye hana nguvu kabisa!

Mumeokoa mukono wenye hauna nguvu kabisa!+

 3 Kwa kweli mumemupatia mutu mwenye hana hekima mashauri ya muzuri sana!+

Na mumefunua kwa wingi hekima yenu yenye kutenda!*

 4 Munajaribu kusema na nani,

Na ni nani aliwaongoza kusema mambo kama hayo?*

 5 Wale wenye hawana uwezo katika kifo wanatetemeka;

Wako chini hata kuliko maji na viumbe vyenye kukaa ndani yake.

 6 Kaburi* liko uchi mbele ya Mungu,*+

Na mahali pa uharibifu hapajafunikwa.*

 7 Anatandika anga la kaskazini* mahali kwenye hakuna kitu,*+

Ananinginiza dunia mahali kwenye hakuna kitu;

 8 Anafunga maji katika mawingu yake,+

Ili mawingu yasipasuke kwa sababu ya uzito wa maji;

 9 Anafunika kiti chake cha ufalme kisionekane,

Na anatandika wingu lake juu yake.*+

10 Anachora mwisho* kwenye uso wa maji;+

Anaweka mupaka kati ya mwangaza na giza.

11 Nguzo za mbingu zinatikisika;

Na zinashangaa sana kwa sababu ya kukemea kwake.

12 Anavuruga bahari kwa nguvu zake,+

Na kwa uelewaji wake anavunja vipande-vipande munyama mukubwa wa bahari.*+

13 Kwa pumuzi yake* anasafisha anga;

Mukono wake unatoboa nyoka mwenye kuenda mbio kwa kutereza.

14 Angalia! Hizo ni sehemu za pembeni-pembeni tu za njia zake;+

Ni sauti ya chini-chini tu ndiyo tumesikia juu yake!

Basi ni nani anaweza kuelewa mungurumo wake wenye nguvu?”+

27 Yobu akaendelea na hotuba* yake, kwa kusema:

 2 “Kama vile hakika Mungu anaishi, yeye mwenye ameniima haki,+

Na kama vile Mweza-Yote anaishi, yeye mwenye amenitia uchungu,+

 3 Kwa wakati wote wenye pumuzi yangu itakuwa ndani yangu

Na roho ya Mungu ndani ya matundu ya pua yangu,+

 4 Midomo yangu haitasema ukosefu wa haki;

Wala ulimi wangu hautasema udanganyifu!

 5 Ni jambo lenye siwezi kuwazia kuwatangaza ninyi kuwa wenye haki!

Mupaka wakati nitakufa, sitaacha* uaminifu-mushikamanifu wangu!+

 6 Nitaendelea kutenda haki na sitaiacha hata kidogo;+

Moyo wangu hautanihukumu* wakati wote wenye nitakuwa muzima.*

 7 Adui yangu akuwe kama mutu muovu,

Na wale wenye kunishambulia wakuwe kama wenye hawako wenye haki.

 8 Kwa maana mutu mwenye hamuogope Mungu* iko* na tumaini gani wakati anaharibiwa,+

Wakati Mungu anaondoa uzima wake?*

 9 Mungu atasikia kilio chake

Wakati anapatwa na taabu?+

10 Ao atapata furaha kwa sababu ya Mweza-Yote?

Je, ataitia Mungu nyakati zote?

11 Nitawafundisha juu ya uwezo* wa Mungu;

Sitaficha jambo lolote juu ya Mweza-Yote.

12 Angalia! Kama ninyi wote mumeona maono,

Sababu gani munasema mambo yenye hayana maana kabisa?

13 Hilo ndilo fungu lenye Mungu anamupatia mutu muovu,+

Uriti wenye watesaji wanapokea kutoka kwa Mweza-Yote.

14 Kama wana wake wanakuwa wengi, watauawa kwa upanga,+

Na wazao wake hawatakuwa na chakula cha kuenea.

15 Wale wenye watabakia kisha yeye kufa watazikwa kwa pigo,

Na wajane wao hawatawalia.

16 Hata kama anarundika feza kama mavumbi

Na kuweka nguo za muzuri kama udongo,

17 Hata akiikusanya,

Mwenye haki ndiye atazivaa,+

Na mwenye hana kosa atagawanya feza yake.

18 Nyumba yenye anajenga ni zaifu kama nyumba ya nondo,*

Na kama kibanda+ chenye kujengwa na mulinzi.

19 Atalala akiwa tajiri lakini hatakusanya kitu;

Wakati atafungua macho yake, hakutakuwa kitu chochote.

20 Kitu chenye kuogopesha kitamuangukia kama vile mafuriko;

Zoruba itamubeba kwa nguvu usiku.+

21 Upepo wa mashariki utamupeperusha, naye atapotea;

Utamufagilia mbali kutoka mahali pake.+

22 Utajitupa juu yake bila huruma+

Wakati atakuwa anajaribu bila tumaini kukimbia nguvu zake.+

23 Unamupigia mikono

Na kumupigia muluzi+ ukiwa mahali pake.*

28 “Kuko mahali pa kuchimba feza

Na mahali pa zahabu yenye wanasafisha;+

 2 Chuma kinatoshwa katika udongo,

Na shaba inayeyushwa* kutoka katika miamba.+

 3 Mwanadamu anashinda giza;

Anachunguza sana ndani ya weusi na giza,

Akitafuta jiwe lenye samani.*

 4 Anachimba shimo mbali na makao ya watu,

Mahali kwenye kumesahauliwa, mbali na mahali kwenye watu wanatembea;

Watu fulani wanashuka ndani ya shimo na wanayumba-yumba wakiwa wenye kuninginia.

 5 Chakula kinakomaa juu ya udongo;

Lakini kule chini, kuko musukosuko kama wa moto.*

 6 Katika majiwe hayo kuko yakuti,

Na mavumbi yake yako na zahabu.

 7 Hakuna ndege mwenye kuwinda mwenye anajua njia ya kuenda kule;

Jicho la mwewe mweusi halijaiona.

 8 Wanyama wa pori wenye nguvu hawajakanyanga juu yake;

Mwana-simba hajatembea kule kwa kuvizia-vizia.

 9 Mwanadamu anagonga mwamba mugumu kwa mukono wake;

Anapindua milima kwenye misingi yake.

10 Anachimba mifereji ya maji+ ndani ya mwamba;

Macho yake yanaona kila kitu chenye samani.

11 Anafunga chemchemi za mito

Na analeta kwenye mwangaza kitu chenye kufichwa.

12 Lakini hekima⁠—​inaweza kupatikana wapi,+

Na chanzo cha uelewaji kiko wapi?+

13 Hakuna mwanadamu mwenye anajua samani yake,+

Na haipatikane katika inchi ya wazima.

14 Maji yenye kuenda chini sana yanasema, ‘Haiko ndani yangu!’

Na bahari inasema, ‘Haiko ndani yangu!’+

15 Haiwezi kununuliwa kwa zahabu safi;

Wala feza haiwezi kupimwa kuwa bei yake.+

16 Haiwezi kununuliwa kwa zahabu ya Ofiri+

Wala kwa majiwe ya shohamu na yakuti yenye kuwa vigumu kupatikana.

17 Zahabu na kioo haviwezi kulinganishwa nayo;

Wala chombo chochote cha zahabu safi* hakiwezi kubadilishwa nayo.+

18 Marijani na fuwele havistahili kutajwa,+

Kwa maana mufuko wenye kujaa hekima ni wenye samani kubwa kuliko mufuko wenye kujaa lulu.

19 Topazi+ ya Kushi haiwezi kulinganishwa nayo;

Haiwezi kununuliwa hata kwa zahabu safi.

20 Lakini hekima inatoka wapi,

Na ni nini chanzo cha uelewaji?+

21 Imefichwa mbali na macho ya kila kiumbe chenye uzima+

Na kufichwa mbali na ndege wa mbinguni.

22 Uharibifu na kifo vinasema,

‘Masikio yetu yamesikia tu habari zake.’

23 Mungu anaelewa njia ya kuipata;

Yeye peke yake ndiye anajua kwenye inakaa,+

24 Kwa maana yeye anaangalia mupaka kwenye miisho ya dunia,

Na anaona kila kitu chini ya mbingu.+

25 Wakati aliweka nguvu* ya upepo+

Na kupima maji,+

26 Wakati aliweka sheria kwa ajili ya mvua+

Na kuweka njia kwa ajili ya wingu la zoruba yenye kunguruma,+

27 Kisha aliona hekima na kuifasiria;

Aliisimamisha na kuipima.

28 Na alimuambia mwanadamu:

‘Angalia! Kumuogopa Yehova⁠—​ndiyo hekima,+

Na kuacha ubaya ni uelewaji.’”+

29 Yobu akaendelea na hotuba* yake, kwa kusema:

 2 “Ingekuwa muzuri kama ningekuwa kama vile nilikuwa katika ile miezi ya zamani,

Katika siku zenye Mungu alikuwa ananilinda,

 3 Wakati alifanya taa yake iangaze juu ya kichwa changu,

Wakati nilitembea katika giza kwa musaada wa mwangaza wake,+

 4 Wakati nilikuwa na* nguvu za ujana,

Wakati urafiki pamoja na Mungu ulikuwa wazi katika hema yangu,+

 5 Wakati Mweza-Yote alikuwa angali pamoja na mimi,

Wakati watoto* wangu wote walikuwa wananizunguka pande zote,

 6 Wakati miguu yangu ilinawishwa katika siagi,

Na miamba ilinimwangia mito midogo ya mafuta.+

 7 Wakati nilizoea kuenda kwenye mulango mukubwa wa muji+

Na kukaa kwenye kiti changu katika kiwanja cha watu wote,+

 8 Vijana wanaume walikuwa wananiona na kuenda pembeni,*

Na hata wazee walikuwa wanasimama na kubakia wima.+

 9 Wakubwa walijizuia kusema;

Walikuwa wanatia mukono wao kwenye kinywa chao.

10 Sauti za watu wa maana zilinyamazishwa;

Ulimi wao ulishikamana na sehemu ya juu ya kinywa chao.

11 Kila mutu mwenye alinisikia alikuwa ananisifu,

Na wale wenye waliniona walikuwa wanashuhudia kwa ajili yangu.

12 Kwa maana nilikuwa ninaokoa maskini mwenye kulilia musaada,+

Na mutoto mwenye hana baba na mutu yeyote mwenye hakukuwa na mutu wa kumusaidia.+

13 Mutu mwenye alikuwa karibu kufa alikuwa ananibariki,+

Na nilifurahisha moyo wa mwanamuke mujane.+

14 Nilivaa haki kama nguo;

Haki yangu ilikuwa kama kanzu* na kilemba.

15 Nilikuwa macho kwa vipofu

Na miguu kwa vilema.

16 Nilikuwa baba kwa maskini;+

Nilikuwa ninachunguza kesi ya hukumu ya watu wenye sijue.+

17 Nilikuwa ninavunja mataya* ya muovu+

Na kuondoa mawindo katika meno yake.

18 Nilizoea kusema, ‘Nitakufia ndani ya nyumba yangu mwenyewe,*+

Na siku zangu zitakuwa nyingi kama chembe za muchanga.

19 Mizizi yangu itaenea ndani ya maji,

Na umande utakaa usiku wote kwenye matawi yangu.

20 Utukufu wangu unafanywa kuwa mupya kila wakati,

Na upinde katika mukono wangu utaendelea kurusha mishale.’

21 Watu walikuwa wananisikiliza kwa hamu,

Walingojea kimya mashauri yangu.+

22 Wakati nilimaliza kusema, hawakukuwa na neno lingine la kusema;

Maneno yangu yalikuwa yanaanguka polepole* katika masikio yao.

23 Waliningojea kama vile wanangojea mvua;

Walifungua kinywa chao wazi kama vile wanangojea mvua ya kipindi cha mvua ya mwisho.+

24 Wakati niliwaonyesha sura yenye kicheko, hawakuamini jambo hilo;

Mwangaza wa sura yangu ulikuwa unawapatia tena tumaini.*

25 Niliwapatia muongozo nikiwa kichwa chao,

Na niliishi kama mufalme kati ya majeshi yake,+

Kama mutu mwenye kufariji watu wenye kuomboleza.+

30 “Sasa wananichekelea+

⁠—​Wanaume wenye miaka kidogo kuliko mimi,

Wenye baba zao ningekataa

Kuwaweka pamoja na imbwa wenye kulinda kundi langu.

 2 Uwezo wa mikono yao ulikuwa na faida gani kwangu?

Nguvu zao zimekwisha.

 3 Wamechoka sana kwa sababu ya uhitaji na njaa;

Wanatafuna udongo wenye kukauka

Wenye ulikuwa tayari umeharibiwa na kuachwa ukiwa.

 4 Wanakusanya mumea wa chumvi kutoka katika miti midogo-midogo;

Chakula chao ni muzizi wa miti ya miretemu.

 5 Wanafukuzwa watoke katikati ya watu;+

Watu wanawalalamikia kama vile wangemufanyia mwizi.

 6 Wanaishi kwenye miteremuko ya mabonde,

Katika mashimo ya udongo na ya miamba.

 7 Wanalia katika miti midogo-midogo

Na wanajikusanya kati ya mimea yenye kuwasha.

 8 Kama wana wa wenye hawana akili na wenye hawana jina,

Wamefukuzwa* watoke katika inchi.

 9 Lakini sasa wananichekelea hata katika nyimbo zao;+

Nimekuwa kwao kitu cha kuzarauliwa.*+

10 Wananichukia na kujitenga na mimi;+

Hawasite kunitemea mate kwenye uso wangu.+

11 Kwa sababu Mungu ameniondolea nguvu zangu* na kuninyenyekeza,

Hawajizuie kufanya jambo lolote mbele yangu.*

12 Kwenye mukono wangu wa kuume wanasimama kama kikundi cha watu wenye kasirani;

Wananifukuza

Na wanatia vizuizi vya uharibifu katika njia yangu.

13 Wanaharibu barabara zangu

Na kufanya taabu yangu ikuwe mubaya zaidi,+

Bila mutu wa kuwazuia.*

14 Wanakuja kama vile watu wenye kupita katika tundu kubwa la ukuta;

Wanakuja kwa wingi katikati ya uharibifu.

15 Woga mukubwa umenilemea;

Heshima yangu imepeperushwa mbali kama upepo,

Na wokovu wangu umepotea kama wingu.

16 Na sasa uzima wangu* unapunguka ndani yangu;+

Siku za mateso+ zinanikamata.

17 Maumivu yanatoboa* mifupa yangu usiku;+

Maumivu yenye kunitafuna hayamalizike hata kidogo.+

18 Nguvu nyingi zinaharibu nguo yangu;*

Inanibana kama shingo ya nguo yangu.

19 Mungu ameniangusha chini ndani ya matope;

Nimefanywa kuwa mavumbi na majivu.

20 Ninakulilia unisaidie, lakini haunijibu;+

Ninasimama, lakini wewe unaniangalia tu.

21 Umenitendea bila huruma;+

Kwa nguvu zote za mukono wako, unanishambulia.

22 Unaniinua na kunipeperusha kwa upepo;

Kisha unanitupa huku na huku katika zoruba.*

23 Kwa maana ninajua kwamba utanishusha mupaka kwenye kifo,

Nyumba kwenye kila mutu mwenye uzima ataenda.

24 Lakini hakuna mwenye angepiga mutu mwenye kuvunjika moyo*+

Wakati analilia musaada akiwa katika taabu.

25 Je, sikutoa machozi kwa ajili ya wale wenye walikuwa katika magumu?

Je, sikuhuzunika* kwa ajili ya maskini?+

26 Hata kama nilitumainia mema, mabaya yalikuja;

Nilitazamia mwangaza, lakini giza likakuja.

27 Tumbo langu lilinguruma bila kuacha;

Siku za mateso zilinishambulia.

28 Ninatembea-tembea kwa huzuni;+ hakuna mwangaza wa jua.

Katika mukusanyiko wa watu, ninasimama na kulilia musaada.

29 Nimekuwa ndugu ya mbweha

Na rafiki ya mabinti wa mbuni.+

30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inaanguka;+

Mifupa yangu inateketea kwa sababu ya joto.*

31 Kinubi changu kinatumiwa tu kwa ajili ya maombolezo,

Na filimbi* yangu kwa ajili ya sauti ya kilio.

31 “Nimefanya agano pamoja na macho yangu.+

Basi namna gani ninaweza kumukazia bikira uangalifu kwa njia yenye haifae?+

 2 Nitapata fungu gani kutoka kwa Mungu, kule juu,

Nitapata uriti gani kutoka kwa Mweza-Yote, kule juu?

 3 Je, musiba haungojee mukosaji

Na je, taabu haingojee wale wenye kufanya mambo ya kuumiza?+

 4 Je, yeye haone njia zangu+

Na kuhesabu hatua zangu zote?

 5 Je, kuko siku nimetembea katika njia yenye haiko ya kweli?*

Je, muguu wangu umekimbilia udanganyifu?+

 6 Acha Mungu anipime kwa mizani* yenye kuwa sawa;+

Halafu atajua uaminifu-mushikamanifu wangu.+

 7 Kama hatua zangu zimeacha kufuata njia+

Ao moyo wangu umefuata macho yangu+

Ao mikono yangu imechafuliwa,

 8 Basi acha nipande mbegu na mwingine akule,+

Na acha kile ninapanda kingolewe.*

 9 Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamuke+

Na kama nimevizia+ kwenye mulango wa jirani yangu,

10 Basi acha bibi yangu asagie mwanaume mwingine nafaka,

Na wanaume wengine wafanye ngono naye.*+

11 Kwa maana huo ungekuwa mwenendo wa haya,

Kosa lenye kustahili azabu ya waamuzi.+

12 Huo ungekuwa moto wenye kuteketeza na kuharibu,*+

Wenye kuteketeza* hata mizizi ya mazao yangu yote.

13 Kama nilikosa kupatia watumishi wangu wanaume ao watumishi wanamuke haki yao

Wakati walikuwa na malalamiko* juu yangu,

14 Nitafanya nini wakati Mungu atapambana na mimi?*

Nitamujibu nini wakati ataniomba nitoe hesabu?+

15 Je, Mwenye alinifanya katika tumbo la uzazi, hakuwafanya wao pia?+

Je, haiko uleule Mwenye alitufanya mbele tuzaliwe?*+

16 Kama nilikataa kupatia maskini kile walitamani+

Ao kuhuzunisha macho ya mwanamuke mujane;*+

17 Kama nilikula chakula changu peke yangu

Bila kupatia mayatima;+

18 (Kwa maana tangu ujana wangu yatima amekomaa pamoja na mimi kama vile nilikuwa baba yake,

Na tangu utoto wangu* nimekuwa kiongozi wa mwanamuke mujane.)

19 Kama nilimuona mutu akikufa kwa sababu ya kukosa nguo

Ao maskini mwenye hana kitu cha kujifunika;+

20 Kama hakunibariki*+

Wakati alikuwa anajitia joto na manyoya ya kondoo wangu;

21 Kama niliinua mukono wangu ili kutesa yatima+

Wakati alihitaji musaada wangu kwenye mulango mukubwa wa muji;*+

22 Basi acha mukono wangu uanguke kutoka kwenye bega langu,

Na acha mukono wangu uvunjike kwenye kiko* chake.

23 Kwa maana niliogopa musiba kutoka kwa Mungu,

Na sikuweza kusimama mbele ya utukufu wake.

24 Kama nilitia tumaini langu katika zahabu

Ao kuambia zahabu safi, ‘Wewe ni tegemeo langu!’+

25 Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu ilikuwa nyingi+

Kwa sababu ya vitu vingi vyenye nilipata;+

26 Kama niliona jua likingaa,*

Ao mwezi ukipita katika utukufu wake;+

27 Na moyo wangu ukashawishiwa kwa uficho,

Na kinywa changu kikabusu mukono wangu ili kuviabudu;+

28 Basi hilo lingekuwa kosa lenye kustahili azabu ya waamuzi,

Kwa maana ningekuwa nimemukana Mungu wa kweli kule juu.

29 Je, kuko siku nimeshangilia kwa sababu ya kuharibiwa kwa adui yangu+

Ao kufurahi kwa sababu amepatwa na jambo la mubaya?

30 Hakuna siku niliruhusu kinywa changu kitende zambi

Kwa kuomba uzima wake* katika kiapo.+

31 Je, watu wa hema yangu hawajasema,

‘Ni nani anaweza kupata mutu mwenye hajashiba chakula chake?’*+

32 Hakuna mugeni* mwenye alilazimika kulala inje usiku;+

Niliacha milango yangu wazi kwa ajili ya wasafiri.

33 Je, kuko siku nimejaribu kufunika zambi zangu kama vile watu wengine,+

Kwa kuficha kosa langu ndani ya mufuko wa nguo yangu?

34 Je, nimekwisha kuogopa mawazo ao matendo ya watu wengi,

Ao nimekwisha kuogopa sana kuzarauliwa na familia zingine,

Na hivyo nimenyamaza na kuogopa kuenda inje?

35 Ingekuwa muzuri kama mutu fulani angenisikiliza!+

Ningeandika jina langu juu ya mambo yenye nimesema!*

Acha Mweza-Yote anijibu!+

Ingekuwa muzuri kama mushitaki wangu angekuwa ameandika mashitaka kwenye karatasi!*

36 Ningeibeba kwenye bega langu,

Na ningeifunga kuzunguka kichwa changu kama vile taji.

37 Ningemupatia hesabu ya kila hatua yenye ninafanya;

Ningemukaribia bila kuogopa, kama vile mukubwa.

38 Kama inchi yangu mwenyewe ingenilaumu

Na mifereji yake ingelia pamoja;

39 Kama nimekula mazao yake bila kulipa,+

Ao kama nimefanya wenye inchi* hiyo wapoteze tumaini;+

40 Basi acha miiba iote kwa ajili yangu pahali pa ngano

Na magugu yenye harufu mubaya pahali pa shayiri.”

Maneno ya Yobu yanaishia hapa.

32 Basi wanaume hao watatu (3) wakaacha kujaribu kumujibu Yobu, kwa sababu alijiona kuwa mwenye haki.*+ 2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli ule Mubuzi+ wa familia ya Ramu, alikuwa amekasirika sana. Kasirani yake iliwaka juu ya Yobu kwa sababu alijaribu kujionyesha kuwa mutu mwenye kufanya mambo yenye kuwa sawa pa nafasi ya Mungu.+ 3 Pia, alikasirikia sana marafiki watatu (3) wa Yobu kwa sababu hawakupata jibu lakini walikuwa wamemutangaza Mungu kuwa muovu.+ 4 Elihu alikuwa amengojea mbele ya kumujibu Yobu, kwa sababu walikuwa na miaka mingi kuliko yeye.+ 5 Wakati Elihu aliona kwamba wale wanaume watatu (3) hawakukuwa na neno la kujibu, kasirani yake ikawaka. 6 Kwa hiyo Elihu mwana wa Barakeli ule Mubuzi, akaanza kuzungumuza, na kusema:

“Mimi ni kijana*

Na ninyi ni wazee.+

Kwa hiyo, kwa heshima, nilijizuia,+

Na sikupima kuwaambia mambo yenye ninajua.

 7 Niliwaza, ‘Acha miaka iseme,*

Na acha wingi wa miaka utangaze hekima.’

 8 Lakini ni roho yenye kuwa ndani ya watu,

Pumuzi ya Mweza-Yote, ndiyo inawapatia uelewaji.+

 9 Haiko kuishi miaka mingi tu ndiko kunamufanya* mutu akuwe na hekima,

Na haiko wazee peke yao ndio wanaelewa mambo yenye kuwa sawa.+

10 Kwa hiyo ninasema, ‘Munisikilize,

Na mimi pia nitawaambia mambo yenye ninajua.’

11 Muangalie! Nilingojea maneno yenu;

Niliendelea kusikiliza mawazo yenu+

Wakati mulikuwa munatafuta mambo ya kusema.+

12 Niliwasikiliza kwa uangalifu,

Lakini hakuna mutu katikati yenu mwenye aliweza kumuonyesha Yobu kosa lake*

Ao kujibu mawazo yake.

13 Kwa hiyo musiseme, ‘Tumepata hekima;

Mungu ndiye anamupinga, hapana mwanadamu.’

14 Yobu hakuelekeza maneno yake kwangu,

Kwa hiyo sitamujibu kwa kutumia mawazo yenu.

15 Wamekuwa na wasiwasi, hawana tena majibu;

Hawana tena neno la kusema.

16 Nimengojea, lakini hawaendelee kusema;

Wamesimama pale tu, bila neno lingine la kujibu.

17 Kwa hiyo mimi pia nitatoa jibu;

Mimi pia nitasema mambo yenye ninajua,

18 Kwa maana niko na maneno mengi;

Roho yenye kuwa ndani yangu inanisukuma.

19 Sehemu zangu za ndani ziko kama divai yenye haina nafasi ya kupitisha hewa,

Kama chupa mupya za ngozi za kuwekea divai zenye zinakaribia kupasuka.+

20 Acha niseme ili nipate kitulizo!

Nitafungua midomo yangu na kutoa jibu.

21 Sitapendelea mutu yeyote;+

Wala sitasifu-sifu mwanadamu yeyote,*

22 Kwa maana sijue kusifu-sifu watu;

Kama nilifanya vile, Mutengenezaji wangu angeniharibu mara moja.

33 “Lakini sasa, Yobu, tafazali sikia maneno yangu;

Sikiliza kila kitu chenye ninasema.

 2 Angalia, tafazali! Ninapaswa kufungua kinywa changu;

Ulimi wangu unapaswa* kusema.

 3 Maneno yangu yanatangaza unyoofu wa moyo wangu,+

Na midomo yangu inasema kwa uaminifu mambo yenye ninajua.

 4 Roho ya Mungu iliniumba,+

Na pumuzi ya Mweza-Yote ilinileta kwenye uzima.+

 5 Unijibu basi kama unaweza;

Toa mawazo yako mbele yangu; ukuwe tayari kujitetea.

 6 Angalia! Mimi niko tu kama wewe mbele ya Mungu wa kweli;

Mimi pia niliumbwa kwa udongo.+

 7 Kwa hiyo woga wangu usikuogopeshe

Na mukazo wowote kutoka kwangu usikulemee.

 8 Lakini ulisema katika masikio yangu,

Ndiyo, niliendelea kusikia maneno haya,

 9 ‘Niko safi, sina zambi;+

Niko safi, sina kosa.+

10 Lakini Mungu anapata sababu za kunipinga;

Ananiona kuwa adui yake.+

11 Anatia miguu yangu katika mikatale;

Anachunguza njia zangu zote.’+

12 Lakini unakosea kwa kusema vile, kwa hiyo nitakujibu;

Mungu ni mukubwa kuliko mwanadamu mwenye anaweza kufa.+

13 Sababu gani unamulaumu Yeye?+

Je, ni sababu hajajibu maneno yako yote?+

14 Kwa maana Mungu anasema mara moja na mara ya pili,

Lakini hakuna mutu mwenye anasikiliza,

15 Katika ndoto, maono ya usiku,+

Wakati wanadamu wanashikwa na usingizi muzito

Wakati wanalala kwenye vitanda vyao.

16 Kisha anafungua masikio yao+

Na anaingiza* maagizo yake ndani yao,

17 Ili kumuepusha mutu asifanye zambi+

Na kulinda mwanadamu ili asikuwe na kiburi.+

18 Mungu anaepusha nafsi yake isiingie ndani ya shimo,*+

Na uzima wake usiharibiwe kwa upanga.*

19 Mutu anakaripiwa pia kupitia maumivu kwenye kitanda chake

Na kupitia maumivu yenye kuendelea ya mifupa yake,

20 Kwa hiyo nafsi yake inachukia* sana mukate,

Na anakataa* hata chakula kizuri.+

21 Nyama ya mwili wake inakonda hata haitambuliwe,

Na mifupa yake yenye ilikuwa haionekane inatoka sasa inje.*

22 Nafsi yake inakaribia* shimo;*

Uzima wake unakaribia wale wenye kuleta kifo.

23 Kama kuko mujumbe* kwa ajili yake,

Muteteaji mumoja kati ya elfu moja (1 000),

Ili amuambie mwanadamu mambo yenye kunyooka,

24 Kisha Mungu anamuonyesha wema na kusema,

‘Musiache aingie ndani ya shimo!*+

Nimepata bei ya ukombozi!+

25 Mwili wake ukuwe teketeke* kuliko wakati wa ujana;+

Akuwe tena na nguvu za siku za ujana wake.’+

26 Atamulilia Mungu,+ mwenye atamukubali,

Na ataona uso Wake na kupiga vigelegele vya shangwe,

Na Yeye atamurudishia mwanadamu mwenye anaweza kufa haki Yake.

27 Mutu huyo ataambia* watu,

‘Nimefanya zambi+ na kupotosha mambo yenye kuwa sawa,

Lakini sikupokea kile chenye nilistahili.*

28 Amekomboa nafsi yangu isiingie* ndani ya shimo,*+

Na uzima wangu utaona mwangaza.’

29 Kwa kweli, Mungu anafanya mambo yote haya

Mara mbili, mara tatu (3), kwa ajili ya mwanadamu,

30 Ili kumutosha* katika shimo,*

Kusudi aweze kuangaziwa na mwangaza wa uzima.+

31 Kaza uangalifu, Yobu! Unisikilize!

Nyamaza, na mimi nitaendelea kusema.

32 Kama uko na jambo la kusema, unijibu.

Sema, kwa maana ninataka kukutetea.

33 Kama hauna jambo la kusema, unisikilize;

Nyamaza, na mimi nitakufundisha hekima.”

34 Kwa hiyo Elihu akaendelea kusema:

 2 “Musikilize maneno yangu, ninyi wenye hekima;

Munisikie, ninyi wenye kujua mambo mengi sana.

 3 Kwa sababu sikio linapima maneno

Kama vile ulimi* unaonja chakula.

 4 Tuchunguze kwa ajili yetu wenyewe mambo yenye kuwa sawa;

Tuamue kati yetu wenyewe mambo mema.

 5 Kwa maana Yobu amesema, ‘Niko na haki,+

Lakini Mungu ameniima haki.+

 6 Je, niseme uongo juu ya namna hukumu yangu inapaswa kuwa?

Kidonda changu hakipone, hata kama sina kosa.’+

 7 Ni mwanaume gani mwingine mwenye iko* kama Yobu,

Mwenye kunywa zarau kama maji?

 8 Yeye ni rafiki ya wakosaji

Na anashirikiana na watu waovu.+

 9 Kwa maana amesema, ‘Mwanadamu hapate faida

Kwa kujaribu kumupendeza Mungu.’+

10 Kwa hiyo munisikilize, ninyi watu wenye uelewaji:*

Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwamba Mungu wa kweli atende uovu,+

Na Mweza-Yote afanye makosa!+

11 Kwa maana atamupatia mwanadamu zawabu kulingana na matendo yake+

Na ataleta juu yake matokeo ya njia zake.

12 Kwa kweli, Mungu hawezi kutenda uovu;+

Mweza-Yote hawezi kupotosha haki.+

13 Ni nani alimupatia daraka la kusimamia dunia,

Na ni nani alimuweka juu ya ulimwengu wote?*

14 Kama angeelekeza uangalifu* wake juu yao,

Kama angejikusanyia roho yao na pumuzi yao,+

15 Wanadamu wote wangeangamia pamoja,

Na wanadamu wangerudia katika mavumbi.+

16 Basi kama muko na uelewaji, mukaze uangalifu juu ya jambo hili;

Musikilize kwa uangalifu mambo yenye ninasema.

17 Je, mutu mwenye kuchukia haki anapaswa kuongoza,

Ao je, ungemuhukumu mutu mwenye nguvu ambaye ni mwenye haki?

18 Je, unaweza kumuambia mufalme, ‘Wewe hauko wa maana,’

Ao watu wenye vyeo, ‘Ninyi muko watu waovu’?+

19 Kuko Mutu mwenye haonyeshe wakubwa upendeleo

Mwenye haonyeshe upendeleo kwa matajiri na kuzarau maskini,*+

Kwa maana wote hao ni kazi ya mikono yake.+

20 Wanaweza kufa bila kutazamia,+ katikati ya usiku;+

Wanatetemeka sana na kufa;

Hata wenye nguvu wanaondolewa, lakini hapana kwa mikono ya mwanadamu.+

21 Kwa maana macho ya Mungu yako juu ya njia za mwanadamu,+

Na Yeye anaona hatua zake zote.

22 Hakuna giza ao kivuli kizito

Mahali waovu wanaweza kujificha.+

23 Kwa maana Mungu hajaweka wakati fulani kwa ajili ya kila mwanadamu

Ili aonekane mbele ya Mungu katika hukumu.

24 Anavunja-vunja wenye nguvu bila kufanya uchunguzi wowote

Na anatia wengine mahali pao.+

25 Kwa maana anajua mambo yenye wako wanafanya;+

Anawapindua wakati wa usiku, nao wanapondwa-pondwa.+

26 Anawapiga kwa sababu ya uovu wao,

Mahali kila mutu anaweza kuona,+

27 Kwa sababu wamegeuka na kuacha kumufuata+

Na wamezarau njia zake zote;+

28 Wanafanya maskini wamulilie Mungu,

Kwa hiyo anasikia kilio cha wenye hawana uwezo.+

29 Wakati Mungu ananyamaza, ni nani anaweza kumuhukumu?

Wakati anaficha uso wake, ni nani anaweza kumuona?

Ikuwe kuelekea taifa ao mutu mumoja, matokeo ni sawasawa,

30 Ili mutu mwenye hamuogope Mungu* asitawale+

Ao kutegea watu mitego.

31 Kwa maana, je, kuko mutu mwenye anaweza kumuambia Mungu,

‘Nimepewa azabu, hata kama sikufanya kosa lolote;+

32 Unifundishe jambo lenye sikuona;

Kama nimefanya kosa lolote, sitalifanya tena’?

33 Je, Mungu akupatie zawabu kwa sababu ya maneno yako wakati unakataa hukumu yake?

Unapaswa kuamua, hapana mimi.

Basi uniambie mambo yenye unajua muzuri.

34 Watu wenye uelewaji* wataniambia

⁠—​Kila mutu mwenye hekima mwenye ananisikia⁠—​

35 ‘Yobu anazungumuza bila ujuzi,+

Na maneno yake yanakosa utambuzi.’

36 Acha Yobu ajaribiwe* mupaka mwisho

Kwa sababu majibu yake ni kama ya watu waovu!

37 Anaongeza uasi juu ya zambi yake;+

Anapiga mikono kwa zarau mbele yetu

Na anasema maneno mengi ya kumushitaki Mungu wa kweli!”+

35 Elihu akaendelea kujibu:

 2 “Je, uko kabisa hakika kwamba uko na haki ya kusema,

‘Niko mwenye haki kuliko Mungu’?+

 3 Kwa maana unasema, ‘Haki yangu iko na faida gani kwako?*

Je, hali yangu iko muzuri kuliko vile ingekuwa kama ningefanya zambi?+

 4 Nitakujibu

Wewe pamoja na marafiki wako.+

 5 Angalia juu mbinguni na uone,

Ona mawingu,+ yenye kuwa mbali juu yako.

 6 Kama unatenda zambi, hilo linamuumiza namna gani?+

Kama makosa yako yanaongezeka, hilo linamufanya nini?+

 7 Kama uko mwenye haki, unamupatia nini;

Anapokea nini kutoka kwako?+

 8 Uovu wako uko na matokeo juu ya mwanadamu tu kama wewe,

Na haki yako juu ya mwana wa binadamu.

 9 Watu wanalia wakati wanakandamizwa sana;

Wanalia ili wapate kitulizo kwa sababu ya utawala* wa watu wenye nguvu.+

10 Lakini hakuna mwenye kusema, ‘Iko* wapi Mungu, Mutengenezaji wangu Mukubwa,+

Yeye mwenye kufanya nyimbo ziimbwe usiku?’+

11 Anatufundisha+ kuliko wanyama wa dunia,+

Na anatufanya tukuwe na hekima kuliko ndege wa mbinguni.

12 Watu wanalia, lakini yeye hawajibu,+

Kwa sababu ya kiburi cha waovu.+

13 Kwa kweli Mungu hasikie kilio chenye hakina maana;*+

Mweza-Yote hakikazie uangalifu.

14 Namna gani basi, wakati unalalamika kwamba haumuone!+

Kesi yako ya hukumu iko mbele yake, kwa hiyo unapaswa kumungojea kwa hamu.+

15 Kwa maana hajakuomba kwa kasirani utoe hesabu;

Wala hajakazia uangalifu maneno yako makali sana.+

16 Yobu anafungua wazi kinywa chake bure;

Anasema maneno mengi bila ujuzi.”+

36 Elihu akaendelea kusema:

 2 “Univumilie kidogo wakati ninaendelea kueleza,

Kwa maana ningali na maneno ya kusema kwa ajili ya Mungu.

 3 Nitasema mingi juu ya mambo yenye ninajua,

Na nitamutangaza Mutengenezaji wangu kuwa mwenye haki.+

 4 Kwa kweli maneno yangu hayako ya uongo;

Ule Mwenye kuwa mukamilifu katika ujuzi+ iko* hapa mbele yako.

 5 Kwa kweli, Mungu ni mwenye nguvu+ na hakatae mutu yeyote;

Yeye ni mukubwa katika nguvu zake za uelewaji;*

 6 Hatalinda uzima wa watu waovu,+

Lakini anapatia watu wenye kuteseka haki.+

 7 Yeye haondoe macho yake juu ya watu wenye haki;+

Anawaweka juu ya viti vya ufalme pamoja na wafalme,*+ nao wanatukuzwa milele.

 8 Lakini kama wamefungwa kwa pingu

Na kukamatwa katika kamba za mateso,

 9 Anawafunulia mambo yenye wamefanya,

Makosa yenye walitenda kwa sababu ya kiburi chao.

10 Anafungua masikio yao ili yasikie karipio

Na anawaambia waache kutenda maovu.+

11 Kama wanatii na kumutumikia yeye,

Wataishi siku zao zote katika hali ya muzuri,

Na miaka yao itakuwa yenye kupendeza.+

12 Lakini kama hawatii, wataharibiwa kwa upanga*+

Na watakufa bila ujuzi.

13 Watu wenye hawamuogope Mungu* katika moyo wao wataweka kinyongo.

Hawalilie musaada hata wakati anawafunga.

14 Wanakufa* wakati wangali vijana,+

Wanapitisha* maisha yao kati ya makahaba wanaume wa hekalu.+

15 Lakini Mungu* anaokoa watu wenye kuteseka katika mateso yao;

Anafungua sikio lao wakati wanakandamizwa.

16 Anakuokoa wakati unakaribia kuingia katika taabu+

Na kukupeleka mahali kwenye nafasi kubwa, kwenye hakuna kizuizi,+

Kwenye meza yenye chakula kingi kizuri ili kukufariji.+

17 Kisha utatosheka na hukumu yenye itapata watu waovu,+

Wakati hukumu itatolewa na haki kutetewa.

18 Lakini ukuwe muangalifu ili kasirani isikufanye ukuwe na chuki,*+

Na usiruhusu rushwa* kubwa ikupotoshe.

19 Je, kilio chako cha kuomba musaada

Ao bidii yako nyingi inaweza kukuzuia usipatwe na taabu?+

20 Usitamani usiku,

Wakati watu wanaangamia kutoka mahali pao.

21 Ukuwe muangalifu kwamba usigeuke ili kufanya maovu,

Kwa kuchagua maovu pahali pa mateso.+

22 Angalia! Mungu ni mwenye kuinuliwa katika nguvu zake;

Ni mufundishaji gani iko* kama yeye?

23 Ni nani ameongoza* njia yake+

Ao kumuambia, ‘Jambo lenye umefanya ni kosa’?+

24 Usisahau kutukuza matendo yake,+

Yenye wanadamu wameimba.+

25 Wanadamu wote wameyaona,

Mwanadamu mwenye anaweza kufa ameyaangalia kwa mbali.

26 Ndiyo, Mungu ni mukubwa kuliko namna tunaweza kujua;+

Hatuwezi hata kidogo kuelewa* hesabu ya miaka yake.+

27 Anakusanya juu matone ya maji;+

Yanagandamana katika kunguku yake na kufanyiza mvua;

28 Kisha mawingu yanamwanga maji hayo chini;+

Yananyesha kwa wingi juu ya wanadamu.

29 Je, mutu anaweza kuelewa namna mawingu yametandikwa,*

Mungurumo wa radi kutoka katika hema yake?*+

30 Ona namna anasambaza juu yake umeme wake wa radi*+

Na kufunika sehemu za chini kabisa za* bahari.

31 Kupitia njia hizo anatunza* vikundi vya watu;

Na kuwapatia chakula kwa wingi.+

32 Anafunika umeme wa radi kwa mikono yake,

Na anaiongoza ili ipige shabaha yake.+

33 Mungurumo wa radi yake unaeleza habari juu yake,

Hata mifugo inaeleza mwenye anakuja.*

37 “Kwa sababu hiyo moyo wangu unapiga-piga

Na kuruka-ruka mahali pake.

 2 Musikilize kwa uangalifu mungurumo wa sauti yake

Na mungurumo wenye unatoka katika kinywa chake.

 3 Anaeneza mungurumo huo chini ya mbingu yote

Na anatuma umeme wake wa radi+ mupaka kwenye miisho ya dunia.

 4 Kisha hilo kuko sauti ya mungurumo;

Ananguruma kwa sauti kubwa sana,+

Na hazuie radi yake wakati sauti yake inasikiwa.

 5 Mungu ananguruma kwa sauti yake+ kwa njia ya ajabu;

Anafanya mambo makubwa yenye hatuwezi kuelewa.+

 6 Kwa maana anaambia teluji,* ‘Anguka juu ya dunia,’+

Na mvua kubwa, ‘Nyesha kwa nguvu.’+

 7 Mungu anasimamisha kazi zote za wanadamu*

Ili kila mwanadamu mwenye anaweza kufa atambue kazi Yake.

 8 Wanyama wa pori wanaingia katika mapango yao

Na wanabakia ndani ya mashimo yao.

 9 Zoruba inavuma kutoka katika chumba chake,+

Na baridi inatoka katika pepo za kaskazini.+

10 Kwa pumuzi ya Mungu, barafu inatengenezwa,+

Na eneo kubwa la maji linagandamana kabisa.+

11 Ndiyo, anabebesha mawingu muzigo wa majimaji;

Anasambaza umeme wake wa radi+ katika mawingu;

12 Yanaenda kwa kuzunguka-zunguka mahali kwenye anayaelekeza;

Yanatimiza kila kitu chenye anaamuru+ juu ya uso wa dunia yenye kuikaliwa na watu.*

13 Ikuwe kwa ajili ya azabu*+ ao kwa ajili ya inchi

Ao kwa ajili ya upendo mushikamanifu, anafanya hilo litokee.+

14 Sikiliza jambo hili, Yobu;

Tulia na ufikiri sana juu ya kazi za ajabu za Mungu.+

15 Je, unajua namna Mungu anaongoza* mawingu

Na namna anafanya umeme wa radi uangaze kutoka katika wingu lake?

16 Je, unajua namna mawingu yanaelea?+

Hizo ni kazi za ajabu za Ule mwenye kuwa mukamilifu katika ujuzi.+

17 Sababu gani nguo zako zinakuwa na moto

Wakati dunia imetulia kwa sababu ya upepo wa kusini?+

18 Je, unaweza, pamoja naye, kutandika* anga+

Zenye kuwa ngumu kama vile kioo cha metali?

19 Utuambie kile tunapaswa kumuelezea;

Hatuwezi kujibu kwa sababu tuko katika giza.

20 Je, anapaswa kujulishwa kwamba ninataka kusema?

Ao mutu yeyote amesema jambo lenye anapaswa kujulishwa?+

21 Hawawezi hata kuona mwangaza,*

Hata kama unangaa katika anga,

Mupaka upepo upite na kuondoa mawingu.

22 Kungaa kama vile zahabu kunatoka kaskazini;

Utukufu wa Mungu+ ni wenye kuogopesha sana.

23 Hatuwezi kumuelewa kabisa Mweza-Yote;+

Iko* na nguvu nyingi sana,+

Na hawezi hata siku moja kuvunja haki+ na uadilifu* wake mwingi.+

24 Kwa hiyo, watu wanapaswa kumuogopa.+

Kwa sababu yeye hafurahie mutu yeyote kati ya wale wenye wanawaza kwamba wako na hekima.”*+

38 Kisha Yehova akamujibu Yobu katika zoruba yenye upepo mukali:+

 2 “Ni nani huyu mwenye kutia giza mashauri yangu

Na kuzungumuza bila ujuzi?+

 3 Tafazali, ujitayarishe kama mwanaume;

Nitakuuliza maulizo, na wewe uniambie.

 4 Ulikuwa wapi wakati niliweka misingi ya dunia?+

Uniambie, ikiwa unawaza kama unajua.

 5 Ni nani aliweka vipimo vyake, kama unajua,

Ao ni nani mwenye alinyoosha kamba ya kupimia kutoka upande wake mumoja mupaka upande wake mwingine?

 6 Vikalio vyake vimeingizwa ndani ya nini,

Ao ni nani aliweka jiwe lake la pembe,+

 7 Wakati nyota za asubui+ zilipiga pamoja vigelele vya shangwe,

Na wana wote wa Mungu*+ walianza kupandisha sauti za shangwe?

 8 Na ni nani alifungia bahari nyuma ya milango+

Wakati ilitoka kwa nguvu katika tumbo la uzazi,

 9 Wakati niliivalisha mawingu

Na kuifunika* katika giza nzito,

10 Wakati niliiwekea mupaka wangu

Na kutia mapingo* yake na milango mahali pake,+

11 Na nilisema, ‘Unaweza kufika mupaka hapa, na usiende mbali na hapa;

Ni hapa mawimbi yako yenye majivuno yatasimamia’?+

12 Je, kuko siku umepatia asubui amri

Ao kuonyesha mapambazuko* mahali pake,+

13 Ili yashike miisho ya dunia

Na kutikisa watu waovu watoke ndani yake?+

14 Dunia inabadilishwa kama vile udongo wa mufinyanzi* chini ya muhuri,

Na vitu vyenye kuwa ndani yake vinangaa kama vile mapambo ya nguo.

15 Lakini mwangaza wa watu waovu unaondolewa juu yao,

Na mukono wao wenye kuinuliwa unavunjwa.

16 Je, umeshuka kwenye chemchemi za bahari

Ao umechunguza maji yenye kuenda chini sana?+

17 Je, umeonyeshwa milango mikubwa ya kifo,+

Ao umeona milango mikubwa ya giza nzito?*+

18 Je, umeelewa ukubwa wa eneo la dunia?+

Uniambie, kama unajua mambo hayo yote.

19 Mwangaza unakaa upande gani?+

Na mahali giza linakaa ni wapi,

20 Ili ulipeleke kwenye eneo lake

Na kuelewa njia zenye kuenda kwenye nyumba yake?

21 Je, unajua mambo hayo kwa sababu ulikuwa umekwisha kuzaliwa

Na kwa sababu hesabu ya miaka yako* ni kubwa?

22 Je, umeingia ndani ya madepo ya teluji,*+

Ao umeona madepo ya mvua ya majiwe,+

23 Yenye nimeweka kwa ajili ya siku ya taabu,

Kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?+

24 Mwangaza* unasambazwa kutoka upande gani,

Na upepo wa mashariki unavuma juu ya dunia kutoka wapi?+

25 Ni nani ametengeneza mufereji kwa ajili ya mafuriko

Na kutengeneza njia kwa ajili ya wingu la zoruba yenye kunguruma,+

26 Ili kufanya mvua inyeshe mahali kwenye mwanadamu haishi,

Juu ya jangwa kwenye hakuna watu,+

27 Ili kushibisha maeneo yenye yameharibiwa ambayo yameachwa

Na kufanya majani yaote tena?+

28 Je, mvua iko na baba,+

Ao ni nani alizaa matone ya umande?+

29 Barafu ilitoka katika tumbo la uzazi la nani,

Na ni nani alizaa barafu nyembamba ya mbinguni+

30 Wakati maji yanakuwa kama vile yamefunikwa na jiwe,

Na uso wa maji yenye kuenda chini sana unagandamana?+

31 Unaweza kufunga kamba za kundi la nyota la Kima*

Ao kufungua kamba za kundi la nyota la Kesili?*+

32 Je, unaweza kuleta kundi la nyota* katika wakati wake

Ao kuongoza kundi la nyota la Ashi* pamoja na wana wake?

33 Je, unajua sheria zenye zinaongoza mbingu,+

Ao unaweza kuzilazimisha zikuwe na mamlaka juu ya dunia?

34 Je, unaweza kupandisha sauti yako mupaka kwenye mawingu

Ili kufanya mafuriko ya maji yakufunike?+

35 Je, unaweza kutuma miali ya umeme wa radi?

Je, itakuja na kukuambia, ‘Sisi tuko hapa!’?

36 Ni nani alitia hekima ndani ya mawingu*+

Ao kupatia maajabu ya anga* uelewaji?+

37 Ni nani mwenye kuwa na hekima ya kutosha ili kuhesabia mawingu,

Ao nani mwenye anaweza kumwanga mitungi ya maji ya mbinguni+

38 Wakati mavumbi yanakuwa rundo la udongo wenye kugandamana

Na madonge ya udongo yanakamatana pamoja?

39 Je, unaweza kumuwindia simba mawindo

Ao kutosheleza hamu ya kula ya wana-simba+

40 Wakati wanashutama katika mashimo yao

Ao kuvizia katika mapango yao?

41 Ni nani mwenye anatayarisha chakula kwa ajili ya kunguru+

Wakati watoto wake wanamulilia Mungu awasaidie

Na kutanga-tanga kwa sababu hakuna chakula?

39 “Je, unajua ni wakati gani mbuzi wa milima wanazaa?+

Je, umekwisha kuona wakati paa wanazaa vitoto vyao?+

 2 Je, unahesabia miezi yenye wanapaswa kutimiza wakiwa na mimba?

Je, unajua ni wakati gani wanazaa?

 3 Wanashutama wakati wanazaa vitoto vyao,

Na maumivu yao ya kuzaa yanaisha.

 4 Vitoto vyao vinapata nguvu na kukomalia katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba;

Vinaenda na havirudie tena kwa mama zao.

 5 Ni nani alimuachilia punda wa pori akuwe huru,+

Na ni nani alifungua kamba za punda wa pori?

 6 Nimefanya jangwa kuwa makao yake

Na inchi yenye chumvi kuwa mahali pake pa kuishi.

 7 Yeye anazarau fujo za muji;

Na hasikie makelele za muendeshaji.

 8 Anatanga-tanga kwenye milima, akitafuta malisho,

Akitafuta kila mumea wenye majani ya mubichi.

 9 Je, ngombe-dume wa pori iko* tayari kukutumikia?+

Je, atalala usiku katika kibanda chako?*

10 Je, utafunga ngombe-dume wa pori kwa kamba katika mufereji,

Ao atakufuata nyuma ili alime* bonde?

11 Je, utategemea nguvu zake nyingi

Na kumuacha afanye kazi yako ya nguvu?

12 Je, utamutegemea akuletee mavuno* yako,

Na atayakusanya kwenye kiwanja chako cha kupigia-pigia nafaka?

13 Mabawa ya mbuni yanapiga-piga kwa furaha,

Lakini, je, mabawa na manyoya yake yanaweza kulinganishwa na ya korongo?+

14 Kwa maana yeye anaacha mayai yake juu ya udongo,

Na anayatia joto katika mavumbi.

15 Yeye anasahau kwamba muguu fulani unaweza kuyavunja

Ao kwamba munyama wa pori anaweza kuyakanyanga.

16 Anatendea wana wake kwa ukali, kama vile hawako wake;+

Haogope kwamba kazi yake inaweza kuwa ya bure.

17 Kwa maana Mungu amemuima* hekima

Na hakumupatia fungu la uelewaji.

18 Lakini wakati anasimama na kupiga-piga mabawa yake,

Yeye anachekelea farasi na mupandaji wake.

19 Je, ni wewe unapatia farasi nguvu yake?+

Je, ni wewe unavalisha shingo yake manyoya ya murefu yenye kutetemeka?

20 Je, unaweza kumufanya aruke kama nzige?

Mulio wake mukubwa wa kungoroma unaogopesha sana.+

21 Anakwaruza-kwaruza udongo katika bonde na kufurahia sana nguvu yake;+

Anakimbia kuenda kwenye mapigano.*+

22 Anachekelea woga na haogope kitu.+

Harudie nyuma kwa sababu ya upanga.

23 Mufuko wa mishale unafanya makelele juu yake,

Mukuki mukubwa na mukuki mudogo vinangaa.

24 Anasonga mbele* akitetemeka kwa musisimuko,

Hawezi kusimama wakati anasikia* sauti ya baragumu.

25 Wakati baragumu inalia, yeye anasema, ‘Aha!’

Anasikia harufu ya mapigano akiwa mbali

Na anasikia sauti ya makamanda na makelele ya vita.+

26 Je, ni uelewaji wako ndio unawezesha kipanga kuruka,

Na kukunjua mabawa yake kuelekea kusini?

27 Ao je, tai anapanda juu kwa amri yako+

Na kujenga chicha yake* juu sana,+

28 Na kukaa usiku muzima kwenye muteremuko mukali,

Akiishi katika ngome yake juu ya mwamba mukubwa wenye kuchongoka-chongoka?*

29 Akiwa pale anatafuta chakula;+

Macho yake yanaona mbali sana.

30 Vitoto vyake vinanyonya damu;

Na kila mahali kwenye kuko maiti za watu wenye waliuawa, yeye iko* pale.”+

40 Yehova akaendelea kumujibu Yobu:

 2 “Je, mutu mwenye kutafuta-tafuta makosa anapaswa kushindana na Mweza-Yote?+

Mwenye anataka kumukaripia Mungu ajibu.”+

 3 Yobu akamujibu Yehova:

 4 “Angalia! Mimi niko mutu wa bure kabisa.+

Nitakujibu nini?

Ninatia mukono wangu juu ya kinywa changu.+

 5 Niliongea mara moja, lakini sitajibu tena;

Mara mbili, lakini sitasema neno lingine.”

 6 Kisha Yehova akamujibu Yobu katika zoruba yenye upepo mukali:+

 7 “Tafazali, ujitayarishe kama mwanaume;

Nitakuuliza maulizo, na wewe uniambie.+

 8 Je, utatilia mashaka haki yangu?*

Je, utanihukumu kuwa muovu ili wewe ukuwe na haki?+

 9 Je, uko na mukono wenye nguvu kama wa Mungu wa kweli,+

Ao je, sauti yako inaweza kunguruma kama yake?+

10 Tafazali, ujipambe, kwa utukufu na ukubwa;

Ujivalishe heshima na uzuri.

11 Mwanga kasirani yako kali;

Angalia kila mutu mwenye majivuno, na umushushe chini.

12 Angalia kila mutu mwenye majivuno, na umunyenyekeze,

Na ukanyange waovu kwenye wanasimama.

13 Ufiche wote katika mavumbi;

Uwafungie* katika mahali kwenye kufichwa,

14 Halafu hata mimi nitakubali mbele yako*

Kwamba mukono wako wa kuume unaweza kukuokoa.

15 Angalia sasa, huyu ni Behemoti,* mwenye niliumba kama vile nilikuumba wewe.

Yeye anakula majani kama ngombe-dume.

16 Angalia nguvu zenye kuwa katika viuno vyake

Na nguvu zenye kuwa katika mishipa ya tumbo lake!

17 Anakaza mukia wake kama mwerezi;

Mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.

18 Mifupa yake ni kama mianzi* ya shaba;

Miguu yake ni fito za chuma.

19 Yeye ni wa kwanza kati ya* kazi za Mungu;

Ni Muumbaji wake tu ndiye mwenye anaweza kumukaribia na upanga wake.

20 Kwa maana milima inazaa chakula kwa ajili yake,

Mahali wanyama wote wa pori wanacheza.

21 Analala chini ya miti ya yungiyungi,

Katika maficho ya matete ya tingitingi.

22 Miti ya yungiyungi inamufunika kwa kivuli,

Na mierebi ya bonde* inamuzunguka.

23 Kama muto unakuwa na musukosuko, yeye hashituke.

Haogope, hata kama maji ya Yordani+ yanajimwanga kwenye kinywa chake.

24 Je, kuko mutu mwenye anaweza kumukamata akiwa macho,

Ao kumutoboa pua kwa ndoano?*

41 “Je, unaweza kuvua Leviatani*+ kwa ndoano

Ao kufunga ulimi wake kwa kamba?

 2 Je, unaweza kupitisha kamba* katika matundu ya pua yake

Ao kutoboa mataya* yake kwa ndoano?*

 3 Je, atakulilia ili umusikilie huruma,

Ao atazungumuza na wewe kwa upole?

 4 Atafanya mapatano pamoja na wewe,

Ili umufanye kuwa mutumwa wako maisha yake yote?

 5 Je, utacheza naye kama vile unacheza na ndege

Ao kumufunga kamba kwa ajili ya watoto wako wadogo wanamuke?

 6 Je, wafanyabiashara watamutumia ili kubadilishana vitu?

Je, watamugawanya kati ya wafanyabiashara?

 7 Je, utajaza mikuki kwenye ngozi yake+

Ao mikuki ya kuvua samaki kwenye kichwa chake?

 8 Tia mukono wako juu yake;

Utakumbuka pigano hilo na hautafanya tena vile hata siku moja!

 9 Ni bure* kujaribu kumukamata.

Kumuona tu kutakufanya ushituke.*

10 Hakuna mwenye anapima kumuchokoza.

Basi ni nani anaweza kusimama ili kunipinga?+

11 Ni nani mwenye amekuwa wa kwanza kunipatia kitu fulani ili nimulipe?+

Kila kitu chenye kuwa chini ya mbingu ni changu.+

12 Sitaacha kusema kuhusu miguu yake,

Kuhusu nguvu zake na mwili wake wenye umeumbwa muzuri.

13 Ni nani ameondoa nguo yake ya inje?

Ni nani ataingia katika mataya* yake yenye kuwa wazi?

14 Ni nani anaweza kufungua kwa nguvu milango ya kinywa chake?*

Meno yake kuzunguka pande zote yanaogopesha sana.

15 Mugongo wake uko na mistari ya magamba*

Yenye kufungana sana pamoja.

16 Kila gamba linakamatana sana na lingine

Na hivyo hewa haiwezi kuingia katikati ya magamba hayo.

17 Yanafungana pamoja;

Yanakamatana na hayawezi kutenganishwa.

18 Chafya yake inatoa mwangaza,

Na macho yake ni kama miali ya mapambazuko.*

19 Miangaza ya umeme wa radi inatoka katika kinywa chake;

Cheche za moto zinatoka inje.

20 Moshi unatoka katika matundu ya pua yake,

Kama tanuru yenye kuwashwa moto kwa matete.

21 Pumuzi yake inawasha makaa,

Na mwali wa moto unatoka katika kinywa chake.

22 Kuko nguvu nyingi katika shingo yake,

Na woga mukubwa unatembea mbele yake.

23 Mikunjo ya ngozi yake inakamatana;

Iko imara, kama vile metali yenye imemwangwa juu yake na kukauka, na haitikisike.

24 Moyo wake uko mugumu kama vile jiwe,

Ndiyo, mugumu kama jiwe la chini la kusagia.

25 Wakati anasimama, hata watu wenye nguvu wanaogopa;

Kishindo chake kinaleta wasiwasi.

26 Upanga wenye utamufikia hautamuweza;

Wala mukuki, mushale, ao kichwa cha mushale.+

27 Anaona chuma kama nyasi tu,

Na shaba kama muti wenye kuoza.

28 Mushale hauwezi kumufanya akimbie;

Kwake majiwe ya kombeo yako kama nyasi yenye kukauka.

29 Anaona gongo* kama vile nyasi yenye kukauka,

Na anachekelea muvumo wa mukuki mudogo.

30 Upande wake wa chini uko kama vipande vyenye kuchongoka vya vyombo vya udongo;

Anajinyoosha katika matope kama kifaa cha kupiga-piga nafaka.+

31 Anafanya mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana kutokote kama vile chungu;

Anakoroga bahari kama chungu cha mafuta yenye marashi.

32 Wakati anapita, anaacha njia imengaa.

Mutu atawaza kwamba mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana kuko na nywele nyeupe.

33 Hakuna mwenye kuwa kama yeye juu ya dunia,

Kiumbe chenye kiliumbwa ili kisiweze kuogopa.

34 Anaangalia kila kitu chenye majivuno.

Yeye ni mufalme juu ya wanyama wote wa pori wenye nguvu.”

42 Kisha Yobu akamujibu Yehova:

 2 “Sasa ninajua kwamba unaweza kufanya mambo yote

Na hauwezi kushindwa kutimiza kila jambo lenye unafikiria kufanya.+

 3 Ulisema, ‘Ni nani huyu mwenye kutia giza mashauri yangu bila ujuzi?’+

Basi nilisema, lakini bila kuelewa

Kuhusu mambo ya ajabu sana kwangu, yenye sijue.+

 4 Ulisema, ‘Tafazali sikiliza, na mimi nitasema.

Nitakuuliza maulizo, na wewe uniambie.’+

 5 Masikio yangu yalisikia habari juu yako,

Lakini sasa ninakuona na macho yangu.

 6 Ndiyo sababu ninaondoa* mambo yenye nilisema,+

Na ninatubu katika mavumbi na majivu.”+

7 Kisha Yehova kumuambia Yobu maneno hayo, Yehova akamuambia Elifazi Mutemani:

“Kasirani yangu inawaka juu yako na juu ya marafiki wako wawili,+ kwa sababu hamukusema kweli juu yangu+ kama vile mutumishi wangu Yobu amefanya. 8 Sasa mukamate ngombe-dume saba (7) na kondoo-dume saba kisha muende kwa mutumishi wangu Yobu, na mutoe zabihu ya kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Na mutumishi wangu Yobu atasali kwa ajili yenu.+ Hakika nitakubali ombi* lake na sitawatendea kulingana na upumbavu wenu, kwa kuwa hamukusema kweli juu yangu kama vile mutumishi wangu Yobu amefanya.”

9 Kwa hiyo Elifazi Mutemani, Bildadi Mushua, na Sofari Munaamati wakaenda na kufanya kama vile Yehova alikuwa amewaambia wafanye. Na Yehova akakubali sala ya Yobu.

10 Kisha Yobu kusali kwa ajili ya marafiki wake,+ Yehova akaondoa mateso ya Yobu+ na kumurudishia tena hali yake ya muzuri.* Yehova akamupatia mara mbili ya vitu vyenye alikuwa navyo zamani.+ 11 Ndugu na dada zake wote pamoja na marafiki wake wote wa zamani+ wakamutembelea na wakakula chakula pamoja naye. Wakamupatia pole na kumufariji kwa sababu ya mateso yote yenye Yehova alikuwa ameruhusu yamupate. Kila mumoja wao akamupatia kipande cha feza na pete ya zahabu.

12 Basi Yehova akabariki miaka ya mwisho ya maisha ya Yobu kuliko mwanzo,+ na Yobu akakuwa na kondoo elfu kumi na ine (14 000), ngamia elfu sita (6 000), ngombe elfu mbili (2 000) wenye kufungwa wawili-wawili, na punda-dike elfu moja (1 000).+ 13 Pia akakuwa na watoto wanaume saba (7) na watoto wanamuke watatu (3).+ 14 Mutoto wake wa kwanza mwanamuke alimuita jina Yemima, wa pili Kezia, na wa tatu (3) Kerene-hapuku. 15 Katika inchi yote hapakukuwa wanamuke wenye sura na umbo ya muzuri kama watoto wanamuke wa Yobu, na baba yao akawapatia uriti pamoja na ndugu zao.

16 Kisha pale Yobu akaishi miaka mia moja makumi ine (140), na akaona watoto wake na wajukuu wake⁠—vizazi ine (4). 17 Mwishowe Yobu akakufa, kisha kuishi maisha ya murefu na yenye kupendeza.*

Inawezekana jina hilo linamaanisha “Kitu Chenye Kuchukiwa.”

Ao “mutu mwenye hana lawama na munyoofu.”

Ao “kwenye nyumba ya kila mumoja wao kwa zamu yake.”

Huu ni usemi wa Kiebrania wenye kumaaanisha wana wa Mungu ambao ni malaika.

Tnn., “umeweka moyo wako juu ya.”

Ao “mutu mwenye hana lawama na munyoofu.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Tnn., “mbele ya uso wa.”

Ao pengine, “Umeme wa radi.”

Ao “kusema kwamba Mungu amefanya jambo lolote la mubaya.”

Huu ni usemi wa Kiebrania wenye kumaanisha wana wa Mungu ambao ni malaika.

Tnn., “umeweka moyo wako juu ya.”

Ao “mutu mwenye hana lawama na munyoofu.”

Tnn., “nimumeze.”

Ao “eko.”

Ao “nafsi yake.”

Ao “eko.”

Ao “nafsi yake.”

Tnn., “mbele ya uso wa.”

Ao “vidonda vibaya sana.”

Tnn., “kulaani siku yake.”

Ao “Giza na kivuli cha kifo vifunike.”

Ao “Ingekuwa muzuri mutu asizaliwe usiku huo.”

Inaeleweka kwamba maneno haya yanahusu mamba ao munyama mwingine mukubwa mwenye nguvu mwenye anaishi ndani ya maji.

Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.

Ao pengine, “wenye walijijengea mahali kwenye kuwa ukiwa.”

Ao “wenye uchungu wa nafsi.”

Tnn., “umechoka”

Ao “kupanga, kutunga.”

Ao “wana-simba wenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”

Ao “wajumbe.”

Nondo ni kidudu fulani cha kuruka chenye kinakula nguo.

Ao “yatafanya agano (mapatano) pamoja na wewe.”

Tnn., “iko na amani.”

Ao “kilo.”

Ao “ya bure-bure; yenye hayana maana.”

Ao “eko.”

Ao “laza.”

Ao “muti mudogo.”

Ao “Nafsi yangu imekataa.”

Ao “ili nirefushe maisha (nafsi) yangu.”

Ao “neige.”

Ao “Kikundi cha wasafiri Wasabea.”

Ao “kumutoa rafiki yenu ili mupate mali.”

Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.

Ao “miezi ya ubatili.”

Ao “mivunyu.”

Kigaga ni ngozi ngumu juu ya kidonda chenye kinakaribia kupona.

Tnn., “litaona tena mema.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao ”kwa sababu ya uchungu wa nafsi yangu!”

Ao “nafsi yangu ichague.”

Tnn., “pa nafasi ya mifupa yangu.”

Tnn., “kuweka moyo.”

Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “Anawatuma waingie katika mukono wa uasi wao.”

Ao “Angeanza kutenda kwa ajili yako.”

Tnn., “Na kutoa maneno yenye kuwa katika mioyo yao?”

Ao “papyrus.” Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “Hizo ndizo njia za.”

Ao “muasi-imani.”

Tnn., “nyumba ya.”

Ao “Anaangalia nyumba ya majiwe.”

Ao “atamezwa.”

Ao “ni vile njia yake itayeyuka.”

Ao “wenye hawana lawama.”

Tnn., “hatashika mukono wa.”

Ao “kumupeleka kwenye tribinali.”

Ao “mwenye uwezo katika nguvu.”

Ao “Anaondoa.”

Pengine ni kundi la nyota la Dubu Mukubwa (Kundi Kubwa la Ursa).

Pengine ni kundi la nyota la Orioni.

Pengine ni nyota zenye kuitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, ao Ngombe.

Tnn., “vyumba vya ndani vya kusini.”

Pengine ni munyama mukubwa wa bahari.

Ao pengine, “mushitaki.”

Ao “Hata kama sina kosa.”

Tnn., “mimi ni mupotovu.”

Ao “bila kosa.”

Ao “sijue nafsi yangu.”

Ao “Ninazarau.”

Ao “wenye kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu.”

Tnn., “nyuso za.”

Ao “mashua ya maji; bateau.”

Tnn., “muovu.”

Ao “neige.”

Ao “potashi.”

Ao “mupatanishi.”

Tnn., “kuweka mukono wake juu yetu sisi wawili.”

Tnn., “angeondoa fimbo yake juu yangu.”

Ao “Nafsi yangu inachukia.”

Ao “kwa uchungu wa nafsi yangu.”

Ao “fromage.”

Ao “pumuzi yangu; uzima wangu.”

Tnn., “Na mambo haya umeyaficha katika moyo wako.”

Ao “nifurahi kidogo.”

Ao “mutu mwenye kujisifu atakuwa na haki?”

Ao “kutambua mipaka ya.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “Wakati punda wa pori atazaliwa mwanadamu.”

Tnn., “ninyi ndio watu.”

Tnn., “moyo.”

Ao “yenye kutereza.”

Ao pengine, “uzungumuze na.”

Ao “Nafsi ya kila mutu mwenye kuishi iko.”

Ao “pumuzi.”

Tnn., “kila mwili wa mwanadamu.”

Tnn., “kaakaa.” Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.

Ao “eko.”

Ao “Eko.”

Ao “eko.”

Ao “bila kitu chochote.”

Ao “mushipi.”

Tnn., “kuregeza mukaba wa wenye nguvu.”

Tnn., “moyo.”

Ao “mutamupendelea.”

Tnn., “Sababu gani ninabeba nyama yangu katika meno yangu?”

Ao “nafsi yangu.”

Ao “muasi-imani.”

Ao pengine, “Mutu akiweza, nitanyamaza na kufa.”

Tnn., “yeye,” pengine mwanadamu mwenye kutajwa ni Yobu.

Nondo ni kidudu fulani cha kuruka chenye kinakula nguo.

Ao “zenye kujaa musukosuko.”

Ao pengine, “anakatwa.”

Tnn., “kunihukumu.”

Ao “eko.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “colle.”

Ao “Nafsi yake inaomboleza.”

Ao “ujuzi wenye ni upepo mutupu.”

Ao “kosa lako linazoeza kinywa chako.”

Tnn., “mukate.”

Ao “anajaribu kumushinda.”

Tnn., “ngao yenye mafundo makubwa.”

Ni kusema, tumaini lolote la kupona.

Tnn., “chake.”

Ao “waasi-imani.”

Ao “kata-midomo.”

Ao “Kama nafsi yenu ingekuwa pahali pa nafsi yangu.”

Ao “wale wenye kukusanyika pamoja na mimi.”

Nyongo ni maji machungu yenye kutengenezwa na maini yenye yanasaidia kuyeyusha chakula katika tumbo.

Ao “nguvu.” Tnn., “pembe.”

Ao “kivuli cha kifo.”

Ao “eko.”

Ao pengine, “halina usingizi.”

Ao “kukazia uangalifu.”

Tnn., “mezali.”

Ao “muasi-imani.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “kaburi.”

Ao “muvunyu.”

Ni kusema, tumaini langu.

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.

Ao pengine, “wachafu.”

Ao “unapasua nafsi yako.”

Ao “makila.”

Ao “achechemee.”

Tnn., “Muzaliwa wa kwanza wa kifo anakula.”

Ao “kifo chenye kuogopesha sana.”

Tnn., “hatakuwa na jina.”

Ao “kwenye makao yake ya muda.”

Ao “kunikasirisha.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “munanitukana.”

Ao “makila yake ya.”

Ao “Watu wa jamaa yangu.”

Tnn., “wana wa tumbo langu la uzazi,” ni kusema, tumbo lenye lilinibeba (tumbo la uzazi la mama yangu).

Tnn., “Na mbona hamutosheke na mwili wangu?”

Tnn., “juu ya (kwenye) mavumbi.”

Ao “Figo zangu zimechoka ndani yangu.”

Tnn., “roho ya uelewaji wangu.”

Ao “wanadamu walitiwa; Adamu alitiwa.”

Ao “muasi-imani.”

Ao “Eko.”

Ni kusema, nguvu zake.

Ao “nyongo.”

Tnn., “Ulimi wa nyoka-kipiri utamuua.”

Tnn., “na hatavimeza.”

Tnn., “Yeye.”

Nyongo ni maji machungu yenye kutengenezwa na maini yenye yanasaidia kuyeyusha chakula katika tumbo.

Tnn., “kasirani yake.”

Ao “kuwa na nguvu.”

Ao “tari.”

Ao “zumari.”

Ao “kwa wakati mufupi,” ni kusema, kifo cha haraka na cha bila maumivu.

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mashauri; mipango.”

Ao “kumufundisha Mungu jambo lolote.”

Ao “mafuta ya ndani ya mifupa yake hayajakauka.”

Ao “akiwa na nafsi yenye huzuni.”

Ao “mivunyu.”

Ao pengine, “kunitendea kwa jeuri.”

Tnn., “alama zao.”

Ao “bonde la muto.”

Tnn., “Na atakokota wanadamu wote wamufuate.”

Ao “Je, inamufurahisha Mweza-Yote.”

Tnn., “unavua nguo za wenye kuwa uchi.”

Ao “mayatima.”

Tnn., “mitego ya ndege.”

Ao “wenye maisha yao yalifupishwa.”

Tnn., “muto.”

Ao “vipande vyako vya zahabu.”

Ao “mutu mwenye macho ya haya.”

Ao “malalamiko yangu ni ya uasi.”

Ao “yenye niliamuriwa kufanya.”

Ao “nafsi yake inataka.”

Ni kusema, siku yake ya hukumu.

Ao pengine, “wanavuna chakula cha mifugo katika shamba.”

Ao pengine, “Wanakamua mafuta kati ya kuta za matuta.”

Ao “Nafsi za wenye waliumizwa sana zinalilia.”

Ao pengine, “Mungu halaumu mutu yeyote kuwa muovu.”

Tnn., “Wanatoboa.”

Tnn., “Yeye ni mwepesi juu ya uso wa maji.”

Ao “neige.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “Tumbo la uzazi litamusahau.”

Ao “muvunyu.”

Tnn., “Yeye.”

Tnn., “Yeye.”

Tnn., “juu ya njia zao.”

Tnn., “katika nafasi zake za juu.”

Ao “safi.”

Ao “muvunyu.”

Ao “akili.”

Tnn., “Na ni pumuzi (roho) ya nani yenye imetoka ndani yenu?”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “yeye.”

Ao “Na Abadoni hajafunikwa.”

Tnn., “kaskazini.”

Tnn., “eneo tupu.”

Ni kusema, juu ya kiti chake cha ufalme.

Tnn., “muviringo.”

Tnn., “Rahabu.”

Tnn., “upepo wake.”

Tnn., “mezali.”

Ao “sitajiondolea; nitalinda.”

Ao “hautanizihaki.”

Ao “kwa ajili ya siku yoyote kati ya siku zangu.”

Ao “muasi-imani.”

Ao “eko.”

Ao “nafsi yake.”

Ao pengine, “kupitia mukono.”

Nondo ni kidudu fulani cha kuruka chenye kinakula nguo.

Ao pengine, “Wanamupigia mikono na kumupigia muluzi wakiwa mahali pao.”

Tnn., “inamwangwa.”

Tnn., “jiwe.”

Inaonekana kwamba maneno haya yanahusu uchimbaji wa majiwe yenye samani.

Ao “yenye ilisafishwa.”

Tnn., “uzito.”

Tnn., “mezali.”

Tnn., “katika siku za.”

Ao “watumishi.”

Tnn., “kujificha.”

Ao “koti yenye haina mikono.”

Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.

Tnn., “ndani ya chicha yangu.”

Tnn., “yalikuwa yanaanguka matone-matone.”

Ao pengine, “Hawakukuwa wanatia giza katika mwangaza wa sura yangu.”

Tnn., “Wamepigwa mijeledi.”

Tnn., “mezali.”

Tnn., “ameregeza upinde wangu.”

Ao “Wanaondoa lijamu.” Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.

Ao pengine, “Bila mutu wa kuwasaidia.”

Ao “nafsi yangu.”

Tnn., “Mifupa yangu imetobolewa usiku.”

Ao pengine, “Nimeharibika kwa sababu ya ukali wa mateso yangu.”

Ao pengine, “unaniharibu kwa kishindo.”

Tnn., “rundo la mabomoko.”

Ao “nafsi yangu haikuhuzunika.”

Ao pengine, “homa.”

Ao “zumari.”

Ao pengine, “pamoja na watu wenye hawapendi kweli?”

Ao “kilo.”

Ao “acha wazao wangu wangolewe.”

Tnn., “acha wanaume wengine wainame juu yake.”

Tnn., “kula (kumeza) mupaka uharibifu.”

Ao “kungoa.”

Ao “kesi ya hukumu.”

Tnn., “wakati atasimama?”

Tnn., “katika tumbo la uzazi.”

Tnn., “nilifanya macho ya mwanamuke mujane yakuwe zaifu.”

Tnn., “kuanzia ndani ya tumbo la uzazi la mama yangu.”

Tnn., “Kama viuno vyake havikunibariki.”

Ao pengine, “Wakati niliona kwamba nilikuwa na musaada kwenye mulango mukubwa wa muji.”

Ao “kutoka kwenye mufupa wake wa juu.” Kiko ni kiungo chenye kuwa kati ya kiwiko cha mukono na bega.

Tnn., “mwangaza ukingaa.”

Ao “nafsi yake.”

Tnn., “nyama yake.”

Ao “mukaaji mugeni.”

Ao “Hii ndiyo sahihi yangu.”

Ao “hati.”

Ao “nafsi ya wenye inchi.”

Ao “kwa sababu alikuwa mwenye haki katika macho yake mwenyewe.”

Tnn., “niko na siku kidogo.”

Tnn., “siku ziseme.”

Ao “Haiko siku nyingi ndizo zinamufanya.”

Ao “mwenye alimukaripia Yobu.”

Ao “sitapatia mwanadamu yeyote jina la cheo.”

Tnn., “Ulimi wangu pamoja na kaakaa langu vinapaswa.” Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.

Tnn., “anatia muhuri juu ya.”

Ao “kaburi.”

Ao “kwa silaha.”

Tnn., “uzima wake unachukia.”

Ao “nafsi yake inakataa.”

Ao “inaonekana waziwazi.”

Ao “Uzima wake unakaribia.”

Ao “kaburi.”

Ao “malaika.”

Ao “kaburi.”

Ao “wenye afya ya muzuri zaidi.”

Tnn., “ataimbia.”

Ao pengine, “Haikuniletea faida.”

Ao “uzima wangu usiingie.”

Ao “kaburi.”

Ao “kutosha nafsi yake.”

Ao “kaburi.”

Tnn., “kaakaa.” Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.

Ao “eko.”

Tnn., “moyo.”

Ao “dunia yote yenye kuikaliwa na watu.”

Tnn., “moyo wake.”

Ao “watu wenye vyeo na kuzarau watu wa hali ya chini.”

Ao “muasi-imani.”

Tnn., “moyo.”

Ao pengine, “Baba yangu, acha Yobu ajaribiwe.”

Pengine inahusu Mungu.

Tnn., “mukono.”

Ao “Eko.”

Ao “cha uongo.”

Ao “eko.”

Tnn., “moyo wake.”

Ao pengine, “Anaweka wafalme juu ya viti vya ufalme.”

Ao “kwa silaha.”

Ao “Waasi-imani.”

Ao “Nafsi zao zinakufa.”

Ao pengine, “Wanamalizia.”

Tnn., “Yeye.”

Ao “upige mikono kwa zarau.”

Ao “kata-midomo.”

Ao “eko.”

Ao pengine, “amemulaumu; amemuomba atoe hesabu kuhusu.”

Ao “kuchunguza.”

Ao “tabaka za mawingu.”

Tnn., “kibanda chake.”

Tnn., “mwangaza wake.”

Tnn., “mizizi ya.”

Ao pengine, “anatetea kesi ya hukumu ya.”

Ao pengine, “kitu chenye kinakuja.”

Ao “neige.”

Tnn., “anatia muhuri kwenye mukono wa kila mwanadamu.”

Ao “udongo wenye kuzaa wa dunia.”

Tnn., “fimbo.”

Ao “anaamuru.”

Ao “kukunjua.”

Ni kusema, wa jua.

Ao “Eko.”

Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “watu wenye kuwa na hekima katika moyo wao.”

Huu ni usemi wa Kiebrania wenye kumaanisha wana wa Mungu ambao ni malaika.

Ao “kuifunga kwa kitambaa.”

Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.

Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “kivuli cha kifo.”

Tnn., “siku zako.”

Ao “neige.”

Ao pengine, “Umeme wa radi.”

Pengine ni nyota zenye kuitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, ao Ngombe.

Pengine ni kundi la nyota la Orioni.

Tnn., “Mazaroti.” Kwenye 2Fa 23:5, neno hilo linatumiwa ili kuzungumuzia makundi ya nyota ya zodiaki.

Pengine ni kundi la nyota la Dubu Mukubwa (Kundi Kubwa la Ursa).

Ao pengine, “ndani ya mwanadamu.”

Ao pengine, “akili.”

Ao “eko.”

Ao “chombo chako cha kukulishia wanyama.”

Ao “apitishe jembe la kukokota lenye meno mengi katika.”

Tnn., “mbegu.”

Tnn., “amemufanya asahau.”

Tnn., “Anatoka ili kukutana na silaha.”

Tnn., “Anameza udongo (dunia).”

Ao pengine, “Haamini.”

Ao “nyumba yake; kiota chake.”

Tnn., “kwenye jino la mwamba mukubwa.”

Ao “eko.”

Ao “Je, utafanya haki yangu kuwa bure?”

Tnn., “Ufunge nyuso zao.”

Ao “nitakupongeza.”

Pengine ni kiboko.

Ao “mabomba, mirija.”

Tnn., “Yeye ni mwanzo wa.”

Ao “bonde la muto.”

Tnn., “mutego.”

Pengine ni mamba.

Tnn., “nyasi.”

Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.

Tnn., “mwiba.”

Ao “ubatili.”

Ao “uanguke chini.”

Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.

Tnn., “uso wake.”

Ao pengine, “Anajivunia mistari yake ya magamba.”

Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.

Gongo ni fimbo yenye kuvimba kwenye mwisho wake mumoja.

Ao “ninafuta.”

Tnn., “Hakika, nitainua uso wake.”

Tnn., “Yehova akageuza utekwa wa Yobu.”

Tnn., “akiwa amezeeka na kujaa siku.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine