KITABU CHA PILI CHA WAFALME
1 Baada ya kifo cha Ahabu, Wamoabu+ waliwaasi Waisraeli.
2 Huo ndio wakati ambapo Ahazia alianguka chini kupitia kiunzi kilichokuwa katika chumba chake cha darini kule Samaria, akajeruhiwa. Kwa hiyo akawatuma wajumbe, akawaambia: “Nendeni mkamuulize Baal-zebubu mungu wa Ekroni+ ikiwa nitapona jeraha hili.”+ 3 Lakini malaika wa Yehova akamwambia Eliya*+ Mtishbi: “Ondoka, nenda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, mnaenda kutafuta ushauri kutoka kwa Baal-zebubu mungu wa Ekroni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli?+ 4 Kwa hiyo Yehova anasema hivi: “Hutatoka katika kitanda unacholalia, kwa maana hakika utakufa.”’” Kisha Eliya akaenda zake.
5 Wajumbe hao waliporudi kwake, mara moja akawauliza: “Kwa nini mmerudi?” 6 Wakamjibu: “Kuna mtu aliyekuja kukutana nasi, akatuambia, ‘Nendeni, rudini kwa mfalme aliyewatuma mkamwambie, “Yehova anauliza hivi: ‘Je, unawatuma wajumbe waende kutafuta ushauri kutoka kwa Baal-zebubu mungu wa Ekroni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli? Kwa hiyo, hutatoka katika kitanda unacholalia, kwa maana hakika utakufa.’”’”+ 7 Ndipo mfalme akawauliza: “Mtu aliyekuja kukutana nanyi na kusema maneno hayo alikuwaje?” 8 Wakamwambia: “Alikuwa mwanamume aliyevaa vazi la manyoya+ na mshipi wa ngozi kiunoni.”+ Mara moja akasema: “Ni Eliya Mtishbi.”
9 Kisha mfalme akamtuma mkuu wa 50 na wanaume wake 50 kwa Eliya. Mkuu huyo alipanda kwenda kumwona, akamkuta ameketi kwenye kilele cha mlima. Akamwambia: “Mtu wa Mungu wa kweli,+ mfalme anasema, ‘Shuka chini.’” 10 Lakini Eliya akamjibu mkuu huyo wa 50: “Ikiwa kwa kweli mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni,+ ukuteketeze wewe na wanaume wako 50.” Basi moto ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza pamoja na wanaume wake 50.
11 Kwa hiyo mfalme akamtuma tena mkuu mwingine wa 50 na wanaume wake 50 kwenda kwa Eliya. Akaenda na kumwambia: “Mtu wa Mungu wa kweli, mfalme anasema, ‘Shuka chini haraka.’” 12 Lakini Eliya akawajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu wa kweli, moto na ushuke kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na wanaume wako 50.” Basi moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza pamoja na wanaume wake 50.
13 Kisha mfalme akamtuma tena mkuu wa tatu wa 50 na wanaume wake 50. Lakini yule mkuu wa tatu wa 50 akapanda, akainama na kupiga magoti mbele ya Eliya, akaanza kumsihi apate kibali mbele yake na kumwambia, “Mtu wa Mungu wa kweli, tafadhali, acha uhai wangu na uhai wa watumishi hawa wako 50 uwe* na thamani machoni pako. 14 Tayari moto umeshuka kutoka mbinguni ukawateketeza wale wakuu wawili wa kwanza wa 50 na makundi yao ya 50, lakini sasa acha uhai wangu uwe* na thamani machoni pako.”
15 Ndipo malaika wa Yehova akamwambia Eliya: “Shuka pamoja naye. Usimwogope.” Basi akainuka, akashuka na kwenda pamoja naye kwa mfalme. 16 Kisha Eliya akamwambia mfalme: “Yehova anasema hivi: ‘Uliwatuma wajumbe kutafuta ushauri kutoka kwa Baal-zebubu mungu wa Ekroni.+ Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli?+ Kwa nini hukutafuta neno lake? Basi hutatoka katika kitanda unacholalia, kwa maana hakika utakufa.’” 17 Kwa hiyo akafa, kulingana na neno la Yehova ambalo Eliya alikuwa amesema; na kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yehoramu*+ akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu+ mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
18 Na mambo mengine katika historia ya Ahazia,+ mambo aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli?
2 Yehova alipokuwa karibu kumchukua Eliya+ kuelekea mbinguni* katika dhoruba ya upepo,+ Eliya na Elisha+ wakaondoka Gilgali.+ 2 Eliya akamwambia Elisha: “Kaa hapa, tafadhali, kwa sababu Yehova amenituma Betheli.” Lakini Elisha akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi na kama unavyoishi,* sitakuacha.” Basi wakashuka kwenda Betheli.+ 3 Kisha wana wa manabii* huko Betheli wakaja kwa Elisha na kumuuliza: “Je, unajua kwamba leo Yehova anamchukua bwana wako asiwe kiongozi wako?”+ Ndipo akajibu: “Tayari najua. Nyamazeni.”
4 Sasa Eliya akamwambia: “Elisha, tafadhali kaa hapa, kwa sababu Yehova amenituma Yeriko.”+ Lakini Elisha akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi na kama unavyoishi,* sitakuacha.” Basi wakaenda Yeriko. 5 Kisha wana wa manabii waliokuwa Yeriko wakaenda kwa Elisha na kumuuliza: “Je, unajua kwamba leo Yehova anamchukua bwana wako asiwe kiongozi juu yako?” Ndipo akajibu: “Tayari najua. Nyamazeni.”
6 Sasa Eliya akamwambia: “Kaa hapa, tafadhali, kwa sababu Yehova amenituma Yordani.” Lakini Elisha akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi na kama unavyoishi,* sitakuacha.” Basi wote wawili wakaendelea na safari. 7 Na wana 50 wa manabii wakaenda pia, wakasimama na kuwatazama kwa mbali wote wawili wakiwa wamesimama kando ya Mto Yordani. 8 Kisha Eliya akachukua vazi lake rasmi,+ akaliviringa na kuyapiga maji, nayo yakagawanyika kushoto na kulia, basi wote wawili wakavuka ng’ambo kupitia nchi kavu.+
9 Mara tu walipovuka, Eliya akamwambia Elisha: “Omba jambo unalotaka nikutendee kabla sijachukuliwa na kukuacha.” Basi Elisha akamuuliza: “Tafadhali, naweza kupata mafungu mawili+ ya* roho yako?”+ 10 Eliya akajibu: “Umeomba jambo gumu. Ikiwa utaniona nitakapochukuliwa na kukuacha, itakuwa hivyo kwako; lakini usiponiona, jambo hilo halitatokea.”
11 Walipokuwa wakitembea, huku wakizungumza, kwa ghafla gari la moto na farasi wa moto+ wakawatenganisha, na Eliya akapanda kuelekea mbinguni* katika dhoruba ya upepo.+ 12 Elisha alitazama huku akipaza sauti, “Baba yangu, baba yangu! Gari la Israeli na wapanda farasi wake!”+ Alipotoweka kabisa machoni pake, akashika mavazi yake mwenyewe na kuyararua vipande viwili.+ 13 Ndipo akaliokota vazi rasmi+ la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, akarudi na kusimama kwenye ukingo wa Yordani. 14 Kisha akachukua vazi rasmi la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwake, akayapiga maji na kuuliza: “Yuko wapi Yehova, Mungu wa Eliya?” Alipoyapiga maji, yaligawanyika kushoto na kulia, Elisha akavuka ng’ambo.+
15 Wana wa manabii waliokuwa Yeriko walipomwona kwa mbali, wakasema: “Roho ya Eliya imetua juu ya Elisha.”+ Basi wakaenda kukutana naye na kumwinamia mpaka ardhini. 16 Wakamwambia: “Hapa sisi watumishi wako tuna wanaume mashujaa 50. Tafadhali, waruhusu waende kumtafuta bwana wako. Labda roho ya* Yehova imemwinua juu na kumtupa juu ya mojawapo ya milima au katika mojawapo ya mabonde.”+ Lakini akawaambia: “Msiwatume.” 17 Hata hivyo, waliendelea kumsihi mpaka akaona aibu, kwa hiyo akasema: “Watumeni.” Wakawatuma wanaume 50, nao wakaendelea kumtafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata. 18 Waliporudi kwake, alikuwa anakaa Yeriko.+ Kisha akawauliza: “Je, sikuwaambia msiende?”
19 Baada ya muda watu wa jiji hilo wakamwambia Elisha: “Bwana wetu, unaona kwamba jiji hili liko mahali pazuri;+ lakini maji ni mabaya, na wakaaji wa nchi ni tasa.”* 20 Akawaambia: “Nileteeni bakuli dogo jipya, mweke chumvi ndani yake.” Basi wakamletea. 21 Kisha akatoka na kwenda kwenye chemchemi ya maji hayo, akatupa chumvi ndani yake+ na kusema: “Yehova anasema hivi: ‘Nimeyaponya maji haya. Hayatasababisha tena kifo wala utasa.’”* 22 Na maji hayo yameponywa mpaka leo hii, kulingana na neno alilosema Elisha.
23 Akapanda kutoka huko na kwenda Betheli. Alipokuwa akitembea njiani, wavulana fulani walitoka jijini na kuanza kumdhihaki,+ wakaendelea kumwambia: “Panda juu, wewe mwenye upara! Panda juu, wewe mwenye upara!” 24 Hatimaye akageuka na kuwatazama, akawalaani katika jina la Yehova. Ndipo dubu jike wawili+ wakatoka msituni na kuwararua vipandevipande watoto 42.+ 25 Kutoka huko, akaendelea na safari mpaka Mlima Karmeli,+ na kutoka huko akarudi Samaria.
3 Yehoramu+ mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli kule Samaria katika mwaka wa 18 wa utawala wa Mfalme Yehoshafati wa Yuda, naye alitawala kwa miaka 12. 2 Akaendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, lakini si kwa kadiri aliyotenda baba yake au mama yake, kwa maana aliondoa nguzo takatifu ya Baali ambayo baba yake alikuwa ametengeneza.+ 3 Hata hivyo, alishikamana na dhambi ambazo Yeroboamu mwana wa Nebati alikuwa amesababisha Waisraeli watende.+ Hakuziacha.
4 Mesha mfalme wa Moabu alikuwa mfugaji wa kondoo, naye alikuwa akilipa wanakondoo 100,000 na kondoo dume 100,000 ambao hawajakatwa manyoya kama ushuru kwa mfalme wa Israeli. 5 Mara tu Ahabu alipokufa,+ mfalme wa Moabu akamwasi mfalme wa Israeli.+ 6 Basi Mfalme Yehoramu akaondoka Samaria siku hiyo na kuwakusanya Waisraeli wote. 7 Akamtumia pia ujumbe Mfalme Yehoshafati wa Yuda, akisema: “Mfalme wa Moabu ameniasi. Je, utaenda pamoja nami kupigana vita dhidi ya Moabu?” Akasema: “Nitaenda.+ Mimi ni kama wewe. Watu wangu ni kama watu wako. Farasi wangu ni kama farasi wako.”+ 8 Kisha akamuuliza: “Tupande kupitia njia gani?” Akajibu: “Kupitia njia ya nyika ya Edomu.”
9 Basi mfalme wa Israeli akaondoka pamoja na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu.+ Baada ya kuzunguka kwa siku saba, jeshi na wanyama wa kufugwa waliokuwa wakiwafuata hawakuwa na maji. 10 Mfalme wa Israeli akasema: “Inasikitisha sana! Yehova ametuita sisi wafalme watatu ili tu atutie mikononi mwa Moabu!” 11 Ndipo Yehoshafati akauliza: “Je, hakuna nabii wa Yehova mahali hapa ambaye tunaweza kumwomba ushauri kutoka kwa Yehova?+ Basi mmoja wa watumishi wa mfalme wa Israeli akajibu: “Yupo Elisha+ mwana wa Shafati, aliyekuwa akimmiminia Eliya maji mikononi.”*+ 12 Kisha Yehoshafati akasema: “Neno la Yehova liko pamoja naye.” Basi mfalme wa Israeli na pia Yehoshafati na mfalme wa Edomu wakashuka kwenda kumwona.
13 Elisha akamwambia mfalme wa Israeli: “Kwa nini umekuja kuniona?*+ Nenda kwa manabii wa baba yako na kwa manabii wa mama yako.”+ Lakini mfalme wa Israeli akamwambia: “Sitaenda, kwa maana ni Yehova aliyetuita sisi wafalme watatu ili atutie mikononi mwa Moabu.” 14 Elisha akamwambia: “Kwa hakika kama anavyoishi Yehova wa majeshi ambaye ninamtumikia,* kama singekuwa ninamheshimu Mfalme Yehoshafati+ wa Yuda, singekutazama wala kukutilia maanani.+ 15 Sasa niletee mpiga kinubi.”*+ Mara tu mpiga kinubi huyo alipoanza kupiga kinubi, mkono wa Yehova ukaja juu ya Elisha.+ 16 Akasema, “Yehova anasema hivi: ‘Chimbeni mitaro katika bonde* hili, 17 kwa maana Yehova anasema hivi: “Hamtaona upepo, wala hamtaona mvua; hata hivyo bonde* hili litajaa maji,+ nanyi mtakunywa maji yake, ninyi, ng’ombe wenu, na wanyama wenu wengine.”’ 18 Lakini hili ni jambo dogo sana machoni pa Yehova,+ kwa maana ataitia pia Moabu mikononi mwenu.+ 19 Mnapaswa kuangamiza kila jiji lenye ngome+ na kila jiji bora, mnapaswa kuukata kila mti mzuri, mnapaswa kuziba chemchemi zote za maji, nanyi mnapaswa kuharibu kila shamba zuri kwa kutupa mawe humo.”+
20 Na asubuhi, wakati ambapo toleo la nafaka la asubuhi hutolewa,+ maji yakaanza kuja kwa ghafla kutoka upande wa Edomu, na nchi ikajaa maji.
21 Wamoabu wote wakasikia kwamba wafalme hao walikuwa wamekuja kupigana nao, basi wakawakusanya pamoja wanaume wote walioweza kubeba silaha,* nao wakasimama mpakani. 22 Walipoamka asubuhi na mapema, jua lilikuwa likiangaza juu ya maji, na Wamoabu waliokuwa upande wa pili waliona maji yakiwa mekundu kama damu. 23 Wakasema: “Hii ni damu! Hakika wafalme wamechinjana wenyewe kwa upanga. Haya basi, enyi Wamoabu, twendeni tukachukue nyara!”+ 24 Walipoingia katika kambi ya Israeli, Waisraeli wakatoka na kuanza kuwaua Wamoabu, nao wakawakimbia.+ Waisraeli wakazidi kuingia Moabu, wakawaua Wamoabu kadiri walivyosonga. 25 Wakabomoa majiji, na kila mtu akatupa jiwe katika kila shamba zuri, na kulijaza mawe; wakaziba kila chemchemi ya maji+ na kuukata kila mti mzuri.+ Mwishowe ni kuta za mawe za jiji la Kir-haresethi+ pekee zilizobaki, na watu wenye makombeo wakalizunguka na kuliangamiza.
26 Mfalme wa Moabu alipoona kwamba ameshindwa vitani, akachukua wanaume 700 waliojihami kwa mapanga ili wapenye na kuingia kwa mfalme wa Edomu;+ lakini hawakuweza. 27 Basi akamchukua mwana wake mzaliwa wa kwanza ambaye angetawala baada yake akamtoa kuwa dhabihu ya kuteketezwa+ juu ya ukuta. Wamoabu wakawa na ghadhabu kali dhidi ya Waisraeli, kwa hiyo Waisraeli wakaacha kumshambulia mfalme huyo na kurudi katika nchi yao.
4 Basi mke wa mmoja wa wana wa manabii+ akamlilia Elisha akisema: “Mume wangu ambaye ni mtumishi wako amekufa, nawe unajua vizuri kwamba mtumishi wako alimwogopa Yehova sikuzote.+ Sasa mtu fulani aliyemdai mume wangu deni fulani amekuja kuwachukua watoto wangu wawili wawe watumwa wake.” 2 Kwa hiyo Elisha akamuuliza: “Nikusaidieje? Niambie, una nini nyumbani?” Akajibu: “Mimi kijakazi wako sina chochote nyumbani ila mtungi wa mafuta.”*+ 3 Basi Elisha akamwambia: “Nenda nje, waombe majirani wako wote vyombo, vyombo vitupu. Usiombe vyombo vichache. 4 Kisha uingie nyumbani mwako pamoja na wanao na kufunga mlango. Jaza vyombo hivyo vyote, na uweke kando vilivyojaa.” 5 Basi mwanamke huyo akaenda zake.
Alipoingia nyumbani pamoja na wanawe na kufunga mlango, wakamletea vyombo, naye akaendelea kuvijaza mafuta.+ 6 Vyombo hivyo vilipojaa, akamwambia hivi mmoja wa wanawe: “Niletee chombo kingine.”+ Lakini mwana huyo akamwambia: “Hakuna vyombo vingine.” Basi mafuta yakakoma.+ 7 Kwa hiyo mwanamke huyo akaenda kwa yule mtu wa Mungu wa kweli, mtu huyo akamwambia: “Nenda, yauze mafuta hayo ulipe madeni yako, nawe pamoja na wanao mnaweza kuishi kwa kile kinachobaki.”
8 Siku moja Elisha alienda Shunemu,+ na huko kulikuwa na mwanamke mmoja maarufu, mwanamke huyo akamsihi sana ale chakula huko.+ Na kila mara alipopita mahali hapo, alikuwa akiingia mahali hapo kula chakula. 9 Basi mwanamke huyo akamwambia mume wake: “Najua kwamba mtu huyu anayepitia hapa kila mara ni mtu mtakatifu wa Mungu. 10 Tafadhali, acha tutengeneze chumba kidogo juu ya paa,+ tumwekee humo kitanda, meza, kiti, na kinara cha taa. Kisha, wakati wowote anapotutembelea, anaweza kukaa humo.”+
11 Siku moja Elisha alifika huko, akaingia katika chumba hicho kilichokuwa paani ili alale. 12 Basi akamwambia Gehazi+ mtumishi wake: “Mwite huyo mwanamke Mshunamu.”+ Kwa hiyo akamwita, basi akaja na kusimama mbele yake. 13 Kisha Elisha akamwambia Gehazi: “Tafadhali mwambie mwanamke huyu, ‘Umejitaabisha sana kwa ajili yetu.+ Tukufanyie nini?+ Je, ninaweza kuzungumza na mfalme+ au mkuu wa jeshi kwa niaba yako?’” Lakini mwanamke huyo akasema: “Ninaishi miongoni mwa watu wangu mwenyewe.” 14 Kwa hiyo Elisha akauliza: “Basi tumfanyie nini mwanamke huyu?” Gehazi akasema: “Kwa kweli, hana mwana,+ na mume wake ni mzee.” 15 Mara moja akasema: “Mwite.” Basi akamwita, akaja na kusimama mlangoni. 16 Kisha Elisha akasema: “Wakati huu, mwaka ujao, utakuwa ukimkumbatia mwana.”+ Lakini mwanamke huyo akasema: “La hasha, bwana wangu, mtu wa Mungu wa kweli! Usinidanganye mimi kijakazi wako.”
17 Hata hivyo, mwanamke huyo akapata mimba na kuzaa mwana wakati huohuo mwaka uliofuata, kama Elisha alivyomwambia. 18 Mtoto huyo akakua, na siku moja alitoka kwenda kwa baba yake aliyekuwa na wavunaji. 19 Alikuwa akimwambia baba yake: “Kichwa changu kinauma, jamani kichwa changu kinauma!” Ndipo baba yake akamwambia mtumishi: “Mbebe umpeleke kwa mama yake.” 20 Basi akambeba na kumrudisha kwa mama yake, naye akakaa kwenye mapaja ya mama yake mpaka adhuhuri, kisha akafa.+ 21 Basi akapanda na kumlaza kwenye kitanda cha mtu wa Mungu wa kweli,+ akafunga mlango na kuondoka. 22 Sasa akamwita mume wake na kumwambia: “Tafadhali, mwagize mtumishi mmoja aje kwangu na punda mmoja, ili niende haraka kwa yule mtu wa Mungu wa kweli na kurudi.” 23 Lakini mume wake akasema: “Kwa nini unaenda kumwona leo? Si mwezi mpya+ wala sabato.” Hata hivyo, mwanamke huyo akasema: “Mambo yote yako sawa.” 24 Basi akaweka matandiko juu ya punda na kumwambia mtumishi wake: “Kaza mwendo. Usipunguze mwendo mpaka nitakapokwambia.”
25 Basi akaenda kwa mtu wa Mungu wa kweli kwenye Mlima Karmeli. Mara tu mtu wa Mungu wa kweli alipomwona kutoka mbali, akamwambia Gehazi mtumishi wake: “Tazama! Ndiye yule mwanamke Mshunamu anakuja. 26 Tafadhali, kimbia ukakutane naye na kumuuliza, ‘Je, u mzima? Je, mume wako ni mzima? Je, mtoto wako ni mzima?’” Mwanamke huyo akasema: “Mambo yote yako sawa.” 27 Mwanamke huyo alipofika kwa mtu wa Mungu wa kweli mlimani, mara moja akamshika miguu.+ Ndipo Gehazi akamkaribia ili amsukume mbali, lakini mtu wa Mungu wa kweli akasema: “Mwache, kwa maana ana* uchungu mwingi sana, na Yehova amenificha jambo hilo na hajaniambia.” 28 Ndipo mwanamke huyo akasema: “Bwana wangu, je, nilikuomba mwana? Je, sikusema, ‘Usinipe tumaini la uwongo’?”+
29 Mara moja akamwambia Gehazi: “Jifunge mavazi yako kiunoni,+ chukua fimbo yangu mkononi mwako, uende. Ukikutana na yeyote, usimsalimu; na yeyote akikusalimu, usimjibu. Nenda uiweke fimbo yangu juu ya uso wa mvulana huyo.” 30 Ndipo mama ya mvulana huyo akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi na kama wewe mwenyewe unavyoishi,* sitakuacha.”+ Kwa hiyo Gehazi akaondoka na kwenda pamoja na mwanamke huyo. 31 Gehazi akawatangulia, akaiweka ile fimbo juu ya uso wa mvulana huyo, lakini hapakuwa na sauti yoyote wala dalili yoyote.+ Basi akarudi kukutana na Elisha na kumwambia: “Mvulana hakuamka.”
32 Elisha alipoingia katika nyumba hiyo, mvulana huyo alikuwa amelala kwenye kitanda chake akiwa mfu.+ 33 Aliingia ndani, akajifungia humo pamoja na mvulana huyo na kuanza kusali kwa Yehova.+ 34 Kisha akapanda kitandani na kumlalia mtoto huyo, kinywa chake kikiwa juu ya kinywa cha mvulana huyo, macho yake juu ya macho yake, na viganja vyake juu ya viganja vyake, akaendelea kumlalia, na mwili wa mtoto huyo ukaanza kupata joto.+ 35 Kisha Elisha akatembea huku na kule chumbani, akapanda kitandani na kumlalia tena. Mvulana huyo akapiga chafya mara saba, kisha akafungua macho.+ 36 Sasa akamwita Gehazi na kumwambia: “Mwite yule mwanamke Mshunamu.” Basi akamwita, naye akaja. Ndipo Elisha akamwambia: “Mchukue mwanao.”+ 37 Mwanamke huyo akaingia ndani, akaanguka miguuni pa Elisha na kuinama mbele yake mpaka ardhini, kisha akamchukua mwanawe na kutoka nje.
38 Elisha aliporudi Gilgali, kulikuwa na njaa kali nchini.+ Wana wa manabii+ walikuwa wameketi mbele yake, akamwambia mtumishi wake:+ “Weka kile chungu kikubwa motoni uwachemshie mchuzi wana wa manabii.” 39 Basi mmoja wao akaenda shambani kuchuma miholi, akapata mzabibu wa mwituni na kuchuma maboga ya mwituni kutoka kwenye mzabibu huo, akajaza vazi lake. Kisha akarudi na kuyakata vipandevipande ndani ya chungu cha mchuzi, bila kujua yalikuwa nini. 40 Baadaye wakawapakulia wanaume hao ili wale, lakini mara tu walipokunywa mchuzi huo, wakalia wakisema: “Kuna kifo ndani ya chungu hiki, Ee mtu wa Mungu wa kweli.” Nao hawakuweza kuunywa. 41 Kwa hiyo Elisha akasema: “Leteni unga kidogo.” Baada ya kuutupa ndani ya chungu hicho, akasema: “Wapakulieni watu.” Na hakukuwa tena na kitu chochote chenye kudhuru ndani ya chungu hicho.+
42 Mtu fulani alikuja kutoka Baal-shalisha,+ akamletea mtu wa Mungu wa kweli mikate 20 ya shayiri+ iliyookwa kwa shayiri iliyokomaa kwanza, pamoja na mfuko wa nafaka iliyotoka kuvunwa.+ Kisha Elisha akasema: “Wape watu ili wale.” 43 Hata hivyo, mtumishi wake akamuuliza: “Nitawezaje kuwapa wanaume 100 chakula hiki?”+ Elisha akasema: “Wape watu ili wale, kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Watakula na kingine kitabaki.’”+ 44 Basi akawapa, nao wakala na kingine kikabaki,+ kama Yehova alivyosema.
5 Sasa Naamani, mkuu wa jeshi la mfalme wa Siria, alikuwa mtu maarufu aliyeheshimiwa na bwana wake, kwa sababu Yehova alikuwa amewapa Wasiria ushindi* kupitia yeye. Alikuwa shujaa hodari, ingawa alikuwa na ukoma.* 2 Pindi moja Wasiria walipovamia Israeli, walimchukua mateka msichana mdogo kutoka katika nchi ya Israeli, akawa kijakazi wa mke wa Naamani. 3 Msichana huyo alimwambia hivi bimkubwa wake: “Laiti bwana wangu angemtembelea nabii+ aliye kule Samaria! Angemponya ukoma wake.”+ 4 Basi akaenda* na kumwambia bwana wake mambo aliyosema msichana huyo kutoka Israeli.
5 Kisha mfalme wa Siria akasema: “Nenda sasa! Nami nitamtumia barua mfalme wa Israeli.” Basi akaenda, akaondoka akiwa amebeba talanta kumi* za fedha, vipande 6,000 vya dhahabu, na mavazi kumi. 6 Akampelekea mfalme wa Israeli barua hiyo ambayo ilisema hivi: “Pamoja na barua hii, ninamtuma mtumishi wangu Naamani ili umponye ukoma wake.” 7 Mara tu mfalme wa Israeli aliposoma barua hiyo, aliyararua mavazi yake na kusema: “Je, mimi ni Mungu, ninaweza kuua na kumfanya mtu aendelee kuwa hai?+ Kwa maana anamtuma mtu huyu kwangu na kuniambia nimponye ukoma wake! Mnaona wenyewe kwamba anatafuta ugomvi nami.”
8 Lakini Elisha mtu wa Mungu wa kweli aliposikia kwamba mfalme wa Israeli ameyararua mavazi yake, mara moja akamtumia mfalme ujumbe huu: “Kwa nini uliyararua mavazi yako? Tafadhali, mruhusu aje kwangu ili ajue kwamba kuna nabii katika Israeli.”+ 9 Basi Naamani akaja na farasi wake na magari yake ya vita, akasimama katika mlango wa nyumba ya Elisha. 10 Hata hivyo, Elisha akamtuma mjumbe amwambie: “Nenda ukaoge mara saba+ katika Mto Yordani,+ na mwili wako utaponywa, nawe utakuwa safi.” 11 Ndipo Naamani akakasirika, akaanza kuondoka akisema: “Nilisema moyoni mwangu, ‘Atatoka na kunijia na kusimama hapa na kuliita jina la Yehova Mungu wake, akitikisa mkono wake kwenda mbele na nyuma juu ya ukoma ili auponye.’ 12 Je, Abana na Farpari, mito ya Damasko,+ si bora kuliko maji yote ya Israeli? Je, siwezi kuoga humo na kuwa safi?” Ndipo akageuka na kwenda zake kwa hasira kali.
13 Basi watumishi wake wakamkaribia na kumwambia: “Baba yangu, kama nabii huyo angekwambia ufanye jambo fulani lisilo la kawaida, je, hungefanya? Je, wakati huu hupaswi kufanya zaidi, kwa kuwa amekuambia tu, ‘Oga, uwe safi’?” 14 Ndipo akashuka mtoni na kujitumbukiza* mara saba katika Mto Yordani, kama alivyosema mtu wa Mungu wa kweli.+ Kisha mwili wake ukaponywa ukawa kama mwili wa mvulana mdogo,+ akawa safi.+
15 Kisha akarudi kwa yule mtu wa Mungu wa kweli,+ yeye na msafara wake wote,* akasimama mbele yake na kusema: “Sasa najua kwamba hakuna Mungu mahali pengine popote duniani isipokuwa Israeli.+ Sasa, tafadhali, pokea zawadi* kutoka kwangu mimi mtumishi wako.” 16 Hata hivyo, Elisha akasema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi ambaye ninamtumikia,* sitaipokea.”+ Akamsihi sana aipokee, lakini akazidi kukataa. 17 Hatimaye Naamani akasema: “Ikiwa hutaipokea, tafadhali, mimi mtumishi wako ninaomba udongo wa nchi hii, kiasi kinachoweza kubebwa na nyumbu wawili, kwa sababu mimi mtumishi wako sitaendelea kutoa dhabihu ya kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine yoyote isipokuwa kwa Yehova. 18 Lakini Yehova anisamehe mimi mtumishi wako kwa jambo hili moja: Bwana wangu anapoingia katika nyumba ya* Rimoni ili kusujudu humo, yeye huegemea mkono wangu, kwa hiyo ninalazimika kusujudu katika nyumba ya Rimoni. Nitakapokuwa nikisujudu katika nyumba ya Rimoni, tafadhali, naomba Yehova anisamehe mimi mtumishi wako kwa kufanya jambo hilo.” 19 Basi Elisha akamwambia: “Nenda kwa amani.” Baada ya kuondoka na kusafiri umbali fulani, 20 Gehazi+ mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu wa kweli+ akasema moyoni mwake: ‘Tazama, Bwana wangu amemwacha huyu Naamani Msiria+ aende zake kwa kukataa kupokea vitu alivyoleta. Kwa hakika kama Yehova anavyoishi, nitakimbia na kumfuata, nichukue kitu fulani kutoka kwake.’ 21 Kwa hiyo Gehazi akamfuata mbio Naamani. Naamani alipoona mtu fulani akimfuata mbio, akashuka kutoka kwenye gari lake na kwenda kumpokea, akamuuliza: “Je, mambo yote yako sawa?” 22 Akasema: “Mambo yote yako sawa. Bwana wangu amenituma nikwambie, ‘Tazama! Sasa hivi vijana wawili kutoka kwa wana wa manabii wamekuja kwangu kutoka katika eneo lenye milima la Efraimu. Tafadhali, wape talanta moja ya fedha na mavazi mawili.’”+ 23 Naamani akasema: “Haya, chukua talanta mbili.” Naye akamsihi sana azipokee,+ akafunga talanta mbili za fedha katika mifuko miwili, pamoja na mavazi mawili, akawapa watumishi wake wawili, wakambebea vitu hivyo.
24 Alipofika Ofeli,* akavichukua kutoka mikononi mwao, akaviweka nyumbani, na kuwaruhusu watu hao waende zao. Walipoondoka, 25 akaingia na kusimama karibu na bwana wake. Sasa Elisha akamuuliza: “Umetoka wapi, Gehazi?” Lakini akajibu: “Mimi mtumishi wako sikwenda mahali popote.”+ 26 Ndipo akamwambia: “Je, moyo wangu haukuwa pamoja nawe wakati yule mtu aliposhuka kutoka kwenye gari lake ili kukupokea? Je, huu ni wakati wa kupokea fedha au kupokea mavazi au mashamba ya mizeituni au mashamba ya mizabibu au kondoo au ng’ombe au watumishi wa kiume au watumishi wa kike?+ 27 Sasa ukoma wa Naamani+ utashikamana nawe pamoja na wazao wako milele.” Mara moja akaondoka mbele yake akiwa na ukoma, mweupe kama theluji.+
6 Wana wa manabii+ wakamwambia Elisha: “Tazama! Mahali tunapokaa pamoja nawe ni padogo sana kwetu. 2 Tafadhali, acha twende Yordani. Kila mmoja wetu achukue gogo kutoka sehemu hiyo na kujenga huko mahali tunapoweza kukaa.” Akawaambia: “Nendeni.” 3 Mmoja wao akamwambia: “Tafadhali, unaweza kwenda pamoja nasi watumishi wako?” Basi akasema: “Nitakwenda.” 4 Kwa hiyo akaenda pamoja nao, wakafika Yordani na kuanza kukata miti. 5 Mmoja wao alipokuwa akikata mti, shoka likaanguka majini, akasema kwa sauti: “Ole wangu, bwana wangu, liliazimwa!” 6 Mtu wa Mungu wa kweli akauliza: “Limeanguka wapi?” Basi akamwonyesha mahali hapo. Ndipo Elisha akakata kipande cha mti na kukitupa hapo, akalifanya shoka lielee. 7 Akasema: “Lichukue.” Akaunyoosha mkono wake na kulichukua.
8 Sasa mfalme wa Siria alienda kupigana vita na Waisraeli.+ Akashauriana na watumishi wake na kuwaambia: “Nitapiga kambi pamoja nanyi mahali fulani na fulani.” 9 Kisha mtu wa Mungu wa kweli+ akamtumia mfalme wa Israeli ujumbe huu: “Jihadhari usipitie mahali hapa, kwa sababu hapa ndipo Wasiria wanaposhukia.” 10 Basi mfalme wa Israeli akatuma ujumbe mahali ambapo mtu wa Mungu wa kweli alikuwa amemwonya kupahusu. Mtu wa Mungu wa kweli akaendelea kumwonya, naye mfalme akaepuka mahali hapo mara kadhaa.*+
11 Jambo hilo likamkasirisha sana mfalme* wa Siria, kwa hiyo akawaita watumishi wake na kuwauliza: “Niambieni! Ni nani miongoni mwetu aliye upande wa mfalme wa Israeli?” 12 Kisha mmoja wa watumishi wake akajibu: “Hakuna yeyote miongoni mwetu, bwana wangu mfalme! Nabii Elisha aliye Israeli ndiye humwambia mfalme wa Israeli mambo unayosema katika chumba chako mwenyewe cha kulala.”+ 13 Mfalme akasema: “Nendeni mkatafute mahali alipo, ili niwatume watu wamkamate.” Baadaye mfalme akaambiwa, “Yuko Dothani.”+ 14 Mara moja akapeleka huko farasi na magari ya vita, na pia jeshi kubwa; likaja usiku na kulizunguka jiji hilo.
15 Mtumishi* wa mtu wa Mungu wa kweli alipoamka asubuhi na mapema na kutoka nje, aliona jeshi lenye farasi na magari ya vita yakiwa yamezunguka jiji. Mara moja mtumishi huyo akamwambia: “Ole wetu, bwana wangu! Tutafanya nini?” 16 Lakini Elisha akamwambia: “Usiogope!+ Kwa maana wale walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.”+ 17 Ndipo Elisha akaanza kusali na kusema: “Ee Yehova, tafadhali, mfungue macho yake, ili aone.”+ Mara moja Yehova akamfungua macho mtumishi huyo naye akaona, na tazama! eneo lenye milima lilikuwa limejaa farasi na magari ya vita ya moto+ kumzunguka Elisha pande zote.+
18 Wasiria waliposhuka kuelekea mahali alipokuwa, Elisha akasali kwa Yehova na kusema: “Tafadhali, lipige kwa upofu taifa hili.”+ Basi akawapiga kwa upofu kama Elisha alivyoomba. 19 Sasa Elisha akawaambia: “Njia yenyewe si hii, na jiji lenyewe si hili. Nifuateni, nami nitawapeleka kwa mtu mnayemtafuta.” Hata hivyo, aliwapeleka Samaria.+
20 Walipofika Samaria, Elisha akasema: “Ee Yehova, wafungue macho ili waone.” Kwa hiyo, Yehova akawafungua macho, nao wakaona kwamba walikuwa katikati ya Samaria. 21 Mfalme wa Israeli alipowaona, alimuuliza Elisha, “Je, niwaue, baba yangu, niwaue?” 22 Lakini Elisha akajibu: “Usiwaue. Je, unawaua wale ambao umewachukua mateka kwa upanga wako na kwa upinde wako? Wape mikate na maji ili wale na kunywa+ na kurudi kwa bwana wao.” 23 Basi akawaandalia karamu kubwa, nao wakala na kunywa, kisha akawaruhusu warudi kwa bwana wao. Makundi ya wavamizi ya Wasiria+ hayakurudi tena katika nchi ya Israeli.
24 Baadaye Ben-hadadi mfalme wa Siria akalikusanya pamoja jeshi lake lote* na kupanda kwenda kulizingira jiji la Samaria.+ 25 Kwa hiyo kukawa na njaa kali+ sana huko Samaria, nao wakalizingira jiji hilo mpaka kichwa cha punda+ kikawa na thamani ya vipande 80 vya fedha, na robo ya kipimo cha kabi* cha mavi ya njiwa ikawa na thamani ya vipande vitano vya fedha. 26 Mfalme wa Israeli alipokuwa akipita juu ya ukuta, mwanamke fulani akamwambia hivi kwa sauti: “Tusaidie, Ee bwana wangu mfalme!” 27 Mfalme akasema: “Yehova asipokusaidia, nitakupa msaada kutoka wapi? Kutoka kwenye uwanja wa kupuria? Au kutoka katika shinikizo la divai au mafuta?” 28 Mfalme akamuuliza: “Una shida gani?” Akamjibu: “Mwanamke huyu aliniambia, ‘Mtoe mwana wako tumle leo, na mwanangu tutamla kesho.’+ 29 Basi tukamchemsha mwanangu na kumla.+ Siku iliyofuata nikamwambia, ‘Mlete mwana wako tumle.’ Lakini akamficha mwanawe.”
30 Mara tu mfalme aliposikia maneno ya mwanamke huyo, akayararua mavazi yake.+ Alipokuwa akipita juu ya ukuta, watu wakaona kwamba alikuwa amevaa nguo za magunia ndani ya nguo zake. 31 Mfalme akasema: “Mungu na aniadhibu, tena vikali, ikiwa Elisha mwana wa Shafati hatakatwa kichwa leo!”+
32 Elisha alikuwa ameketi nyumbani kwake pamoja na wazee. Mfalme akamtuma mtu amtangulie, lakini kabla ya mjumbe huyo kufika, Elisha akawaambia wazee hao: “Je, mmeona jinsi ambavyo mwana huyu wa muuaji+ amemtuma mtu aje kunikata kichwa? Mjumbe huyo atakapofika, fungeni mlango, nanyi muusukume ili asiingie. Je, bwana wake hayuko nyuma yake akimfuata?” 33 Alipokuwa akizungumza nao, mjumbe huyo akaja kwake, mfalme akasema: “Msiba huu unatoka kwa Yehova. Kwa nini niendelee kumngojea Yehova?”
7 Sasa Elisha akasema: “Sikiliza neno la Yehova. Yehova anasema hivi: ‘Kesho karibu wakati kama huu sea moja* ya unga laini itakuwa na thamani ya shekeli moja, na sea mbili za shayiri zitakuwa na thamani ya shekeli moja* katika lango la* Samaria.’”+ 2 Ndipo kamanda msaidizi ambaye mfalme alimtegemea akamwambia hivi mtu wa Mungu wa kweli: “Hata Yehova akiyafungua malango ya mbinguni ya mafuriko, je, kweli jambo hilo linaweza kutokea?”*+ Ndipo Elisha akamwambia, “Utaona kwa macho yako mwenyewe,+ lakini hutakula vyakula hivyo.”+
3 Kulikuwa na watu wanne wenye ukoma kwenye lango la jiji,+ nao wakaambiana: “Kwa nini tuketi hapa mpaka tufe? 4 Tukisema, ‘Acheni tuingie jijini,’ na bado kuna njaa kali jijini,+ tutafia humo. Nasi tukiketi hapa, bado tutakufa. Basi sasa twende zetu kwenye kambi ya Wasiria. Wakituruhusu tuishi, tutaishi; lakini wakituua, basi tutakufa.” 5 Kwa hiyo wakaondoka jioni giza lilipoanza kuingia, wakaingia kwenye kambi ya Wasiria. Walipofika kandokando ya kambi ya Wasiria, hakukuwa na mtu yeyote.
6 Kwa maana Yehova alikuwa amesababisha kambi ya Wasiria isikie sauti ya magari ya vita na farasi, sauti ya jeshi kubwa.+ Basi wakaambiana: “Tazama! Mfalme wa Israeli amekodi wafalme wa Wahiti na wafalme wa Misri watushambulie!” 7 Mara moja wakaondoka na kukimbia katika giza la jioni, wakaacha mahema yao, farasi wao, punda wao, na kambi yote kama ilivyokuwa, wakakimbia ili kuokoa maisha yao.*
8 Watu hao wenye ukoma walipokaribia kambi hiyo, wakaingia ndani ya hema moja na kuanza kula na kunywa. Wakachukua fedha, dhahabu, na mavazi kutoka humo, wakaenda na kuficha vitu hivyo. Kisha wakarudi na kuingia katika hema lingine, wakachukua vitu kutoka humo na kwenda kuvificha.
9 Mwishowe wakaambiana: “Jambo tunalofanya si sawa. Leo ni siku ya habari njema! Tukisitasita na kusubiri mpaka mapambazuko, tutastahili kuadhibiwa. Twendeni sasa tukaiambie nyumba ya mfalme habari hizi.” 10 Basi wakaenda na kuwaita kwa sauti walinzi wa malango ya jiji na kuwaambia: “Tulienda kwenye kambi ya Wasiria, lakini hakukuwa na mtu yeyote huko—hatukusikia sauti ya yeyote. Kulikuwa tu na farasi na punda waliofungwa na mahema yaliyoachwa kama yalivyokuwa.” 11 Mara moja walinzi hao wa malango wakatangaza habari hizo, nazo zikafika nyumbani kwa mfalme.
12 Mara moja mfalme akaamka usiku na kuwaambia watumishi wake: “Acheni niwaambie yale ambayo Wasiria wametutendea. Wanajua kwamba tuna njaa,+ kwa hiyo walitoka kambini na kujificha shambani, wakisema, ‘Watatoka jijini, nasi tutawakamata wakiwa hai na kuingia jijini.’”+ 13 Ndipo mmoja wa watumishi wake akasema: “Tafadhali, waruhusu baadhi ya wanaume wachukue farasi watano kati ya wale waliobaki jijini. Hali itakayowapata itakuwa sawa na hali itakayoupata umati wa Waisraeli unaobaki hapa. Hali yao itakuwa sawa na ya umati wa Waisraeli ambao waliangamia. Basi na tuwatume waende tuone hali itakavyokuwa.” 14 Wakachukua magari mawili pamoja na farasi, na mfalme akawatuma kwenye kambi ya Wasiria na kuwaambia: “Nendeni mwone hali ilivyo.” 15 Wakawafuata mpaka Yordani, na mavazi na vyombo ambavyo Wasiria walikuwa wametupa walipokuwa wakikimbia kwa hofu vilikuwa vimetapakaa njia yote. Kisha wajumbe hao wakarudi na kumletea mfalme habari.
16 Ndipo watu wakatoka na kuipora kambi ya Wasiria, hivi kwamba sea moja ya unga laini ikawa na thamani ya shekeli moja, na sea mbili ya shayiri ikawa na thamani ya shekeli moja, kulingana na neno la Yehova.+ 17 Mfalme alimweka yule kamanda msaidizi awe msimamizi wa lango, kamanda ambaye mfalme alimtegemea, lakini watu wakamkanyaga-kanyaga langoni hadi akafa, kama yule mtu wa Mungu wa kweli alivyokuwa amemwambia mfalme alipokwenda kumwona. 18 Ilitendeka kama mtu wa Mungu wa kweli alivyokuwa amemwambia mfalme: “Kesho wakati kama huu, sea mbili za shayiri zitakuwa na thamani ya shekeli moja, na sea moja ya unga laini itakuwa na thamani ya shekeli moja katika lango la Samaria.”+ 19 Lakini yule kamanda msaidizi alikuwa amemwambia mtu wa Mungu wa kweli: “Hata Yehova akiyafungua malango ya mbinguni ya mafuriko, je, kweli jambo hilo linaweza kutokea?”* Elisha akamjibu: “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini hutakula vyakula hivyo.” 20 Hivyo ndivyo ilivyotokea kwake, kwa maana watu walimkanyaga-kanyaga langoni hadi akafa.
8 Elisha alimwambia hivi yule mwanamke ambaye alikuwa amemfufua mwanawe:+ “Ondoka uende, wewe pamoja na familia yako, uishi kama mgeni mahali popote unapoweza kuishi, kwa maana Yehova ametangaza kwamba kutakuwa na njaa kali+ nchini kwa miaka saba.” 2 Basi yule mwanamke akaondoka na kufanya kama mtu wa Mungu wa kweli alivyomwambia. Akaenda pamoja na familia yake kuishi katika nchi ya Wafilisti+ kwa miaka saba.
3 Baada ya miaka saba, mwanamke huyo akarudi kutoka katika nchi ya Wafilisti, akaenda kumsihi mfalme ili arudishiwe nyumba yake na shamba lake. 4 Sasa mfalme alikuwa akizungumza na Gehazi mtumishi wa yule mtu wa Mungu wa kweli, akamwambia: “Tafadhali, nisimulie mambo yote makuu ambayo Elisha amefanya.”+ 5 Alipokuwa akimsimulia mfalme jinsi Elisha alivyomfufua mtoto aliyekufa,+ yule mwanamke ambaye mwana wake alikuwa amefufuliwa akaja kwa mfalme akimsihi arudishiwe nyumba yake na shamba lake.+ Mara moja Gehazi akasema: “Bwana wangu mfalme, huyu ndiye yule mwanamke, na huyu ndiye mwana wake ambaye Elisha alimfufua.” 6 Ndipo mfalme akamuuliza mwanamke huyo, naye akamsimulia kisa chote. Kisha mfalme akamkabidhi mwanamke huyo kwa ofisa wa makao ya mfalme, akamwambia hivi ofisa huyo: “Rudisha mali yote ya mwanamke huyu na mazao yote ya shamba lake tangu siku alipotoka nchini hadi sasa.”
7 Elisha alienda Damasko+ wakati Ben-hadadi+ mfalme wa Siria alipokuwa mgonjwa. Ben-hadadi akaambiwa hivi: “Yule mtu wa Mungu wa kweli+ amekuja.” 8 Ndipo mfalme akamwambia Hazaeli:+ “Chukua zawadi, ukakutane na mtu wa Mungu wa kweli.+ Muulize Yehova kupitia kwake, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’” 9 Hazaeli akachukua zawadi na kwenda kukutana naye, alichukua vitu vizuri vya kila aina kutoka Damasko, mizigo iliyoweza kubebwa na ngamia 40. Akaja na kusimama mbele yake na kumwambia: “Mwana wako, Ben-hadadi, mfalme wa Siria amenituma kwako nikuulize, ‘Je, nitapona ugonjwa huu?’” 10 Elisha akamjibu: “Nenda ukamwambie, ‘Hakika utapona,’ lakini Yehova amenionyesha kwamba hakika atakufa.”+ 11 Elisha akamkazia macho sana Hazaeli mpaka akaona aibu. Kisha yule mtu wa Mungu wa kweli akaanza kulia. 12 Hazaeli akamuuliza: “Bwana wangu, kwa nini unalia?” Akamjibu: “Kwa sababu ninajua madhara utakayowatendea Waisraeli.+ Utateketeza ngome zao, utawaua kwa upanga wanaume wao mashujaa, utawapondaponda watoto wao, na kuwapasua tumbo wanawake wao wenye mimba.”+ 13 Hazaeli akasema: “Mimi mtumishi wako, ambaye ni mbwa tu, ninawezaje kufanya jambo kama hilo?” Lakini Elisha akasema: “Yehova amenionyesha kwamba wewe utakuwa mfalme wa Siria.”+
14 Kisha Hazaeli akamwacha Elisha na kurudi kwa bwana wake, Ben-hadadi akamuuliza: “Elisha alikwambia nini?” Akamjibu: “Aliniambia kwamba hakika utapona.”+ 15 Lakini siku iliyofuata, Hazaeli akachukua tandiko, akalitumbukiza ndani ya maji, na kumfunika nalo usoni mpaka akafa.+ Kisha Hazaeli akawa mfalme baada yake.+
16 Katika mwaka wa tano wa utawala wa Yehoramu+ mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Yehoshafati alipokuwa mfalme wa Yuda, Yehoramu+ mwana wa Mfalme Yehoshafati wa Yuda akawa mfalme. 17 Alikuwa na umri wa miaka 32 alipoanza kutawala, naye alitawala huko Yerusalemu kwa miaka minane. 18 Alitembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ kama walivyofanya watu wa nyumba ya Ahabu,+ kwa maana alikuwa amemwoa binti ya Ahabu;+ naye aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova.+ 19 Lakini Yehova hakutaka kuangamiza Yuda kwa sababu ya Daudi mtumishi wake,+ kwa maana alikuwa amemwahidi atampa yeye na wanawe taa sikuzote.+
20 Katika siku za Yehoramu, Waedomu waliasi dhidi ya Yuda,+ nao wakajichagulia mfalme wao wenyewe.+ 21 Basi Yehoramu akavuka kwenda Sairi na magari yake yote ya vita, akaondoka usiku na kuwashinda Waedomu waliokuwa wamemzingira yeye na makamanda wa magari ya vita; na wanajeshi wakakimbilia katika mahema yao. 22 Lakini tangu siku hiyo Waedomu wameendelea kuiasi nchi ya Yuda. Watu wa Libna+ waliasi pia wakati huo.
23 Na mambo mengine katika historia ya Yehoramu, mambo yote aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 24 Kisha Yehoramu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ Na Ahazia+ mwana wake akawa mfalme baada yake.
25 Katika mwaka wa 12 wa utawala wa Yehoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli, Ahazia mwana wa Mfalme Yehoramu wa Yuda akawa mfalme.+ 26 Ahazia alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa mwaka mmoja huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Athalia,+ mjukuu wa* Mfalme Omri+ wa Israeli. 27 Alitembea katika njia ya nyumba ya Ahabu+ na kuendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, kama nyumba ya Ahabu, kwa maana alikuwa ameoa kutoka katika nyumba ya Ahabu.+ 28 Basi Ahazia alienda pamoja na Yehoramu mwana wa Ahabu kupigana vita na Mfalme Hazaeli wa Siria kule Ramothi-gileadi,+ lakini Wasiria wakamjeruhi Yehoramu.+ 29 Kwa hiyo Mfalme Yehoramu akarudi Yezreeli+ ili apone majeraha aliyopata kutoka kwa Wasiria huko Rama alipopigana na Mfalme Hazaeli wa Siria.+ Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akashuka kwenda Yezreeli kumwona Yehoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.*
9 Kisha nabii Elisha akamwita mmoja wa wana wa manabii na kumwambia: “Jifunge mavazi yako kiunoni, na uchukue haraka chupa hii ya mafuta uende Ramothi-gileadi.+ 2 Utakapofika huko, mtafute Yehu+ mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi; ingia ndani, umchukue kutoka miongoni mwa ndugu zake, na kumpeleka katika chumba cha ndani zaidi. 3 Kisha chukua chupa ya mafuta, uyamimine juu ya kichwa chake na kusema, ‘Yehova anasema hivi: “Ninakutia mafuta uwe mfalme wa Israeli.”’+ Halafu ufungue mlango na kukimbia bila kukawia.”
4 Basi yule mtumishi wa nabii akaenda Ramothi-gileadi. 5 Alipofika, aliwakuta wakuu wa majeshi wakiwa wameketi pamoja. Akasema: “Nina ujumbe wako, ewe mkuu.” Yehu akamuuliza: “Ni ujumbe wa nani kati yetu?” Akasema: “Ujumbe wako, ewe mkuu.” 6 Basi Yehu akainuka na kuingia ndani ya nyumba; mtumishi huyo akammiminia yale mafuta juu ya kichwa na kumwambia, “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Ninakutia mafuta uwe mfalme wa watu wa Yehova, uwe mfalme wa Israeli.+ 7 Unapaswa kuiangamiza nyumba ya Ahabu bwana wako, nami nitailipizia kisasi damu ya watumishi wangu manabii na watumishi wote wa Yehova ambao Yezebeli aliwaua.*+ 8 Na nyumba yote ya Ahabu itaangamia; nami nitamwangamiza kila mwanamume* wa Ahabu, kutia ndani wasio na uwezo na walio dhaifu katika Israeli.+ 9 Nami nitaifanya nyumba ya Ahabu kuwa kama nyumba ya Yeroboamu+ mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha+ mwana wa Ahiya. 10 Kuhusu Yezebeli, mbwa watamla katika shamba kule Yezreeli,+ na hakuna yeyote atakayemzika.’” Kisha mtumishi huyo akafungua mlango na kukimbia.+
11 Yehu aliporudi kwa watumishi wa bwana wake, wakamuuliza: “Je, mambo yote yako sawa? Kwa nini mwendawazimu huyu alikuja kwako?” Akawajibu: “Ninyi mnajua huyu ni mtu wa aina gani na mambo anayosema.” 12 Lakini wakasema: “Hilo si kweli! Tafadhali tuambie.” Ndipo akasema: “Aliniambia hivi, halafu akasema, ‘Yehova anasema hivi: “Ninakutia mafuta uwe mfalme wa Israeli.”’”+ 13 Ndipo kila mmoja wao akavua vazi lake haraka na kulitandika chini ya Yehu kwenye ngazi zilizo wazi,+ nao wakapiga pembe na kusema: “Yehu amekuwa mfalme!”+ 14 Kisha Yehu+ mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi akapanga njama dhidi ya Yehoramu.
Yehoramu alikuwa akilinda huko Ramothi-gileadi,+ yeye na Waisraeli wote, kwa sababu ya Mfalme Hazaeli+ wa Siria. 15 Baadaye Mfalme Yehoramu akarudi Yezreeli+ ili kuuguza majeraha aliyokuwa amepata kutoka kwa Wasiria alipopigana na Mfalme Hazaeli wa Siria.+
Sasa Yehu akasema: “Mkikubaliana nami, msimwache yeyote atoroke kutoka jijini na kupeleka habari hii Yezreeli.” 16 Kisha Yehu akapanda gari lake na kwenda Yezreeli, kwa maana Yehoramu alikuwa amelala huko akiwa amejeruhiwa, na Mfalme Ahazia wa Yuda alikuwa ameshuka kwenda kumwona Yehoramu. 17 Mlinzi aliyekuwa amesimama juu ya mnara huko Yezreeli aliona kundi kubwa la wanaume wa Yehu likija. Mara moja akasema: “Ninaona kundi kubwa la wanaume.” Yehoramu akasema: “Chukua mpanda farasi mmoja umtume akutane nao, awaulize, ‘Je, mmekuja kwa amani?’” 18 Basi mpanda farasi akaenda kukutana naye, akasema: “Mfalme anauliza, ‘Je, mmekuja kwa amani?’” Lakini Yehu akasema: “Kwa nini unauliza kuhusu ‘amani’? Nifuate!”
Basi yule mlinzi akasema: “Mjumbe aliwafikia, lakini hajarudi.” 19 Kwa hiyo akatuma mpanda farasi wa pili, akawaambia hivi alipowafikia: “Mfalme anauliza hivi: ‘Je, mmekuja kwa amani?’” Lakini Yehu akasema: “Kwa nini unauliza kuhusu ‘amani’? Nifuate!”
20 Basi yule mlinzi akasema: “Aliwafikia, lakini hajarudi, na uendeshaji wa gari ni kama wa Yehu mjukuu* wa Nimshi, kwa maana yeye huendesha gari kama mwendawazimu.” 21 Yehoramu akasema: “Fungeni farasi kwenye gari!” Basi farasi wakafungwa kwenye gari lake la vita, na Yehoramu mfalme wa Israeli na Ahazia+ mfalme wa Yuda wakaondoka kila mmoja kwenye gari lake la vita ili kukutana na Yehu. Wakakutana naye katika shamba la Nabothi,+ Myezreeli.
22 Mara tu Yehoramu alipomwona Yehu, akamuuliza: “Yehu, umekuja kwa amani?” Lakini akamjibu: “Kunawezaje kuwa na amani wakati kuna ukahaba wa Yezebeli+ mama yako na ulozi wake mwingi?”+ 23 Mara moja Yehoramu akageuza gari lake ili akimbie, akamwambia Ahazia: “Tumedanganywa, Ahazia!” 24 Yehu akachukua upinde wake na kumpiga mshale Yehoramu katikati ya mabega, na mshale huo ukatokea moyoni mwake, naye akaanguka ndani ya gari lake la vita. 25 Kisha akamwambia Bidkari kamanda wake msaidizi: “Mwinue na umtupe katika shamba la Nabothi, Myezreeli.+ Kumbuka kwamba mimi na wewe tulipokuwa tukiendesha magari ya farasi* tukimfuata Ahabu baba yake, Yehova mwenyewe alitangaza hivi dhidi yake:+ 26 ‘“Kwa hakika kama nilivyoona damu ya Nabothi+ na damu ya wanawe jana,” asema Yehova, “nitakulipa+ wewe katika shamba hilihili,” asema Yehova.’ Basi sasa mwinue na umtupe katika shamba hili, kulingana na neno la Yehova.”+
27 Mfalme Ahazia wa Yuda+ alipoona hayo, alikimbia kupitia njia ya nyumba ya bustani. (Baadaye Yehu akamfuatia na kusema: “Muueni yeye pia!” Kwa hiyo wakampiga ndani ya gari akipanda kuelekea Guri, karibu na mji wa Ibleamu.+ Lakini akaendelea kukimbia mpaka Megido, akafia huko. 28 Kisha watumishi wake wakambeba ndani ya gari mpaka Yerusalemu, wakamzika katika kaburi lake pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ 29 Mfalme Ahazia alianza kutawala Yuda katika mwaka wa 11 wa utawala wa Yehoramu mwana wa Ahabu.)+
30 Yehu alipofika Yezreeli,+ Yezebeli+ akasikia habari hizo. Basi akapaka macho yake wanja na kupamba nywele zake, akatazama chini kupitia dirishani. 31 Yehu alipokuwa akiingia langoni, Yezebeli akasema: “Je, mambo yalimwendea sawa Zimri, aliyemuua bwana wake?”+ 32 Yehu akatazama juu dirishani na kuuliza: “Ni nani aliye upande wangu? Ni nani?”+ Mara moja maofisa wawili au watatu wa makao ya mfalme wakamtazama wakiwa dirishani. 33 Yehu akasema: “Mtupeni chini mwanamke huyo!” Kwa hiyo wakamtupa chini, na kiasi fulani cha damu yake kikatapakaa kwenye ukuta na farasi, kisha Yehu akamkanyaga-kanyaga. 34 Baada ya hayo akaingia ndani, akala na kunywa. Halafu akasema: “Tafadhali, mchukueni mwanamke huyu aliyelaaniwa mkamzike. Kwa maana yeye ni binti ya mfalme.”+ 35 Lakini walipoenda kumzika, hawakupata chochote isipokuwa fuvu la kichwa na miguu na viganja vya mikono.+ 36 Waliporudi na kumwambia Yehu, akasema: “Jambo hilo linatimiza neno hili la Yehova+ alilosema kupitia mtumishi wake Eliya, Mtishbi: ‘Katika shamba la Yezreeli, mbwa wataula mwili wa Yezebeli.+ 37 Na maiti ya Yezebeli itakuwa kama mbolea katika shamba la Yezreeli, ili watu wasiseme: “Huyu ni Yezebeli.”’”
10 Sasa Ahabu+ alikuwa na wana 70 kule Samaria. Kwa hiyo Yehu akaandika barua, akazituma Samaria kwa wakuu wa Yezreeli, wazee,+ na walezi wa watoto wa Ahabu,* akisema: 2 “Sasa barua hii itakapowafikia ninyi, wana wa bwana wenu watakuwa pamoja nanyi, na pia mtakuwa na magari ya vita, farasi, jiji lenye ngome, na silaha. 3 Chagueni mwana bora na anayefaa* kabisa kati ya wana wa bwana wenu na mumweke kwenye kiti cha ufalme cha baba yake. Kisha mpigane vita kwa ajili ya nyumba ya bwana wenu.”
4 Lakini wakaogopa sana na kusema: “Tazama! Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupigana naye,+ sisi tutawezaje kupigana naye?” 5 Basi msimamizi wa jumba la mfalme,* gavana wa jiji, wazee, na wale walezi wakamtumia Yehu ujumbe huu: “Sisi ni watumishi wako, nasi tutafanya mambo yote utakayotuambia. Hatutamweka yeyote kuwa mfalme. Fanya jambo lolote unaloona ni jema machoni pako.”
6 Ndipo Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema: “Ikiwa mko upande wangu na mko tayari kunitii, leteni vichwa vya wana wa bwana wenu na mje kwangu kesho wakati kama huu kule Yezreeli.”
Wana 70 wa mfalme walikuwa pamoja na wanaume mashuhuri wa jiji waliokuwa wakiwalea. 7 Mara tu barua hiyo ilipowafikia, wakawachukua wana wa mfalme, wanaume 70,+ na kuwachinja, kisha wakaweka vichwa vyao ndani ya vikapu, wakampelekea kule Yezreeli. 8 Mjumbe akaenda kwa Yehu na kumwambia: “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Kwa hiyo akasema: “Viwekeni katika marundo mawili kwenye lango la jiji mpaka asubuhi.” 9 Yehu alipotoka asubuhi, alisimama mbele ya watu wote na kuwaambia: “Ninyi hamna hatia.* Naam, nilipanga njama dhidi ya bwana wangu, nikamuua,+ lakini ni nani aliyewaua hawa wote? 10 Basi jueni kwamba hakuna neno hata moja la Yehova ambalo Yehova amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu litakalokosa kutimia,*+ na Yehova amefanya yale aliyosema kupitia mtumishi wake Eliya.”+ 11 Basi Yehu akawaua watu wote waliobaki wa nyumba ya Ahabu kule Yezreeli, na pia watu wake wote mashuhuri, marafiki zake, na makuhani wake,+ hakumwacha mtu yeyote wa nyumba yake akiwa hai.+
12 Kisha akaondoka na kuelekea Samaria. Njiani kulikuwa na nyumba ya kuwakatia kondoo manyoya. 13 Huko Yehu akakutana na ndugu za Mfalme Ahazia+ wa Yuda, naye akawauliza, “Ninyi ni nani?” Wakasema: “Sisi ni ndugu za Ahazia, nasi tunashuka kwenda kuwajulia hali wana wa mfalme na wana wa mama malkia.” 14 Mara moja akasema: “Wakamateni wakiwa hai!” Basi wakawakamata wanaume 42 wakiwa hai na kuwachinja kando ya tangi la maji la nyumba ya kuwakatia kondoo manyoya. Hakumwacha yeyote kati yao akiwa hai.+
15 Alipokuwa akiondoka mahali hapo, alikutana na Yehonadabu+ mwana wa Rekabu+ akija kumpokea. Yehu akamsalimia* na kumuuliza: “Je, moyo wako ni kamili* kunielekea, kama moyo wangu ulivyo kamili kukuelekea?”
Yehonadabu akajibu: “Ndiyo.”
“Ikiwa ndivyo, nipe mkono wako.”
Kwa hiyo akampa mkono wake, na Yehu akamvuta na kumpandisha kwenye gari lake. 16 Kisha akasema: “Twende pamoja, uone kwamba sivumilii ushindani wowote kumwelekea* Yehova.”+ Basi wakaenda pamoja naye katika gari lake la vita. 17 Kisha Yehu akafika Samaria na kuwaua watu wote waliobaki wa nyumba ya Ahabu huko Samaria mpaka alipowaangamiza wote,+ kulingana na neno la Yehova alilomwambia Eliya.+
18 Tena Yehu akawakusanya watu wote na kuwaambia: “Ahabu alimwabudu Baali kwa kiwango kidogo tu,+ lakini Yehu atamwabudu kwa kiwango kikubwa zaidi. 19 Basi wakusanyeni manabii wote wa Baali,+ waabudu wake wote, na makuhani wake wote+ waje kwangu. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosa kufika, kwa sababu nina dhabihu kubwa kwa ajili ya Baali. Yeyote atakayekosa kufika hataishi.” Lakini Yehu alikuwa akitenda kwa ujanja ili awaangamize waabudu wa Baali.
20 Yehu akaendelea kusema: “Tangazeni* kusanyiko takatifu kwa ajili ya Baali.” Basi wakalitangaza. 21 Kisha Yehu akatuma ujumbe kotekote katika Israeli, na waabudu wote wa Baali wakaja. Hakuna hata mmoja wao ambaye hakuja. Wakaingia katika nyumba ya* Baali,+ na nyumba ya Baali ikajaa kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine. 22 Akamwambia msimamizi wa chumba cha mavazi: “Leta mavazi kwa ajili ya waabudu wote wa Baali.” Basi akawaletea mavazi. 23 Halafu Yehu na Yehonadabu+ mwana wa Rekabu wakaingia katika nyumba ya Baali. Yehu akawaambia waabudu wa Baali: “Tafuteni kwa uangalifu mhakikishe kwamba hakuna mwabudu yeyote wa Yehova humu ndani isipokuwa waabudu wa Baali.” 24 Mwishowe wakaingia ndani ili kutoa dhabihu mbalimbali na dhabihu za kuteketezwa. Yehu alikuwa ameweka wanaume wake 80 nje na kuwaambia, “Yeyote kati ya wanaume ninaowatia mikononi mwenu akiponyoka, mtalipia uhai wake kwa uhai wenu.”*
25 Mara tu alipomaliza kutoa dhabihu ya kuteketezwa, Yehu akawaambia hivi walinzi* na makamanda wasaidizi: “Ingieni ndani na kuwaua! Msimwache yeyote aponyoke!”+ Basi walinzi na makamanda wasaidizi wakawaua kwa upanga na kuwatupa nje, wakaingia mpaka kwenye chumba kitakatifu cha ndani cha* nyumba hiyo ya Baali. 26 Kisha wakatoa nje nguzo takatifu+ za nyumba ya Baali na kuiteketeza kila nguzo.+ 27 Wakabomoa nguzo takatifu+ ya Baali na kuibomoa nyumba ya Baali,+ na kuigeuza kuwa vyoo, na hivyo ndivyo ilivyo mpaka leo.
28 Kwa hiyo Yehu akakomesha kabisa ibada ya Baali katika Israeli. 29 Hata hivyo, Yehu hakugeuka na kuacha dhambi ambazo Yeroboamu mwana wa Nebati alisababisha Waisraeli kutenda kuhusiana na wale ndama wa dhahabu waliokuwa Betheli na Dani.+ 30 Basi Yehova akamwambia Yehu: “Kwa kuwa umetenda vema na umefanya yaliyo sawa machoni pangu kwa kutenda mambo yote yaliyokuwa moyoni mwangu niliyokusudia kuitendea nyumba ya Ahabu,+ vizazi vinne vya wana wako vitaketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.”+ 31 Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kutembea katika Sheria ya Yehova Mungu wa Israeli kwa moyo wake wote.+ Hakugeuka na kuacha dhambi ambazo Yeroboamu alisababisha Waisraeli kutenda.+
32 Siku hizo Yehova alianza kupunguza* eneo la Israeli, eneo moja baada ya lingine. Hazaeli akaendelea kuwashambulia kotekote katika eneo la Israeli,+ 33 kuanzia Yordani kuelekea mashariki, nchi yote ya Gileadi—ya watu wa kabila la Gadi, Rubeni, na Manase+—kutoka Aroeri, jiji lililo kando ya Bonde la Arnoni,* mpaka Gileadi na Bashani.+
34 Na mambo mengine katika historia ya Yehu, mambo yote aliyofanya na ukuu wake, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 35 Kisha Yehu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake huko Samaria; na Yehoahazi mwana wake+ akawa mfalme baada yake. 36 Yehu alitawala Israeli kwa miaka 28 akiwa Samaria.
11 Basi Athalia+ mama ya Ahazia alipoona kwamba mwanawe amekufa,+ alitoka na kuangamiza uzao wote wa kifalme.*+ 2 Hata hivyo, Yehosheba binti ya Mfalme Yehoramu, dada ya Ahazia, akamchukua Yehoashi+ mwana wa Ahazia, akamwiba kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliopaswa kuuawa na kumweka yeye pamoja na mlezi wake katika chumba cha ndani cha kulala. Wakafanikiwa kumficha ili Athalia asimwone, kwa hiyo hakuuawa. 3 Akakaa pamoja naye kwa miaka sita akiwa amefichwa katika nyumba ya Yehova, Athalia alipokuwa akitawala nchi.
4 Katika mwaka wa saba, Yehoyada aliagiza wakuu wa mamia wa walinzi walioitwa Wakari na wa walinzi* wa jumba la mfalme+ waitwe, wakaja kwake katika nyumba ya Yehova. Akafanya mapatano* pamoja nao na kuwaapisha kuhusu mapatano hayo katika nyumba ya Yehova, kisha akawaonyesha mwana wa mfalme.+ 5 Akawapa agizo hili: “Hivi ndivyo mtakavyofanya: Theluthi moja watashika zamu siku ya Sabato, na kuweka ulinzi mkali katika nyumba ya* mfalme,+ 6 theluthi nyingine watakuwa katika Lango la Msingi, na theluthi nyingine watakuwa katika lango lililo nyuma ya walinzi wa jumba la mfalme. Mtalinda nyumba hiyo kwa zamu. 7 Vikundi vyenu viwili ambavyo havipaswi kuwa na zamu siku ya Sabato vinapaswa kuweka ulinzi mkali katika nyumba ya Yehova ili kumlinda mfalme. 8 Mnapaswa kumzunguka mfalme pande zote, kila mmoja akiwa na silaha zake mikononi mwake. Yeyote atakayekaribia kikosi hicho atauawa. Mfuateni mfalme popote aendapo.”*
9 Wakuu wa mamia+ wakafanya sawasawa na alivyoamuru kuhani Yehoyada. Basi kila mmoja wao akachukua wanaume wake waliokuwa na zamu siku ya Sabato, pamoja na wale ambao hawakuwa na zamu siku ya Sabato, wakaja kwa kuhani Yehoyada.+ 10 Kisha kuhani akawapa wakuu wa mamia mikuki na ngao za mviringo zilizokuwa za Mfalme Daudi, ambazo zilikuwa katika nyumba ya Yehova. 11 Na walinzi wa jumba la mfalme+ wakasimama mahali pao, kila mmoja akiwa na silaha zake mikononi, kuanzia upande wa kulia wa nyumba mpaka upande wa kushoto wa nyumba, kando ya madhabahu,+ na kando ya nyumba hiyo, kumzunguka mfalme pande zote. 12 Kisha Yehoyada akamtoa nje mwana wa mfalme+ na kumvika taji na Ushahidi,*+ wakamweka kuwa mfalme na kumtia mafuta. Wakaanza kupiga makofi na kusema: “Mfalme na aishi muda mrefu!”+
13 Athalia aliposikia sauti ya watu wakikimbia, mara moja akaja na kujiunga na watu katika nyumba ya Yehova.+ 14 Kisha akamwona mfalme akiwa amesimama hapo kando ya nguzo kama ilivyokuwa desturi.+ Wakuu na wapiga tarumbeta+ walikuwa pamoja na mfalme, na watu wote nchini walikuwa wakishangilia na kupiga tarumbeta. Ndipo Athalia akayararua mavazi yake na kupaza sauti: “Ni njama! Ni njama!” 15 Lakini kuhani Yehoyada akawaamuru hivi wakuu wa mamia,+ wale waliowekwa kulisimamia jeshi: “Mwondoeni miongoni mwa vikosi, na yeyote akimfuata, muueni kwa upanga!” Kwa maana kuhani alikuwa amesema: “Msimuue ndani ya nyumba ya Yehova.” 16 Basi wakamkamata, na alipofika mahali ambapo farasi huingia katika nyumba ya* mfalme,+ akauawa hapo.
17 Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yehova na mfalme na watu,+ kwamba wataendelea kuwa watu wa Yehova, pia akafanya agano kati ya mfalme na watu.+ 18 Baada ya hayo, watu wote nchini wakaenda kwenye nyumba ya* Baali na kubomoa madhabahu zake,+ nao wakazivunja kabisa sanamu zake,+ na kumuua Matani kuhani wa Baali+ mbele ya madhabahu.
Halafu kuhani akawaweka waangalizi wa nyumba ya Yehova.+ 19 Tena, akawachukua wakuu wa mamia,+ walinzi walioitwa Wakari, walinzi wa jumba la mfalme,+ na watu wote nchini ili wamsindikize mfalme kushuka kutoka katika nyumba ya Yehova, wakaja katika jumba la mfalme kupitia lango la walinzi wa jumba la mfalme. Kisha mfalme akaketi kwenye kiti cha wafalme.+ 20 Basi watu wote nchini wakashangilia na jiji likatulia, kwa maana walikuwa wamemuua Athalia kwa upanga katika jumba la mfalme.
21 Yehoashi+ alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala.+
12 Katika mwaka wa 7 wa utawala wa Yehu,+ Yehoashi+ akawa mfalme, naye akatawala kwa miaka 40 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Sibia kutoka Beer-sheba.+ 2 Yehoashi akaendelea kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova sikuzote ambazo kuhani Yehoyada alimfundisha. 3 Hata hivyo, mahali pa juu+ hapakuondolewa, na bado watu walikuwa wakitoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu.
4 Yehoashi akawaambia makuhani: “Chukueni pesa zote zinazoletwa katika nyumba ya Yehova kwa ajili ya matoleo matakatifu,+ pesa ambazo kila mtu amekadiriwa kutoa,+ pesa zilizotolewa kama thamani iliyokadiriwa ya mtu,* na pesa zote ambazo moyo wa kila mtu umemchochea kuleta katika nyumba ya Yehova.+ 5 Makuhani wenyewe watachukua pesa hizo kutoka kwa wale wanaozitoa* na kuzitumia kurekebisha nyumba hiyo, sehemu yoyote iliyoharibika.”*+
6 Kufikia mwaka wa 23 wa utawala wa Mfalme Yehoashi, makuhani walikuwa bado hawajairekebisha nyumba hiyo.+ 7 Kwa hiyo Mfalme Yehoashi akamwita kuhani+ Yehoyada na makuhani wengine na kuwauliza: “Kwa nini hamwirekebishi nyumba? Kwa hiyo msichukue pesa zaidi kutoka kwa watu ikiwa hazitumiwi kurekebisha nyumba.”+ 8 Basi makuhani wakakubali kwamba hawatachukua pesa zaidi kutoka kwa watu na kwamba hawatakuwa na wajibu wa kurekebisha nyumba hiyo.
9 Kisha kuhani Yehoyada akachukua sanduku,+ akatoboa tundu kwenye kifuniko chake, akaliweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia ndani ya nyumba ya Yehova. Makuhani waliolinda mlangoni waliweka pesa zote zilizoletwa katika nyumba ya Yehova katika sanduku hilo.+ 10 Kila mara walipoona kwamba sanduku hilo lina pesa nyingi, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja na kuzikusanya* na kuzihesabu pesa hizo zilizoletwa katika nyumba ya Yehova.+ 11 Waliwapa wale waliowekwa kusimamia kazi katika nyumba ya Yehova pesa zilizokuwa zimehesabiwa. Nao wakawalipa maseremala na wajenzi waliokuwa wakifanya kazi katika nyumba ya Yehova,+ 12 na pia waashi na watu waliokata mawe. Pia walinunua mbao na mawe yaliyochongwa kwa ajili ya kurekebisha sehemu zilizoharibika za nyumba ya Yehova na kutumia pesa hizo kulipia gharama nyingine zote za kurekebisha nyumba hiyo.
13 Hata hivyo, hawakutumia pesa zozote zilizoletwa katika nyumba ya Yehova kutengeneza mabeseni ya fedha, mikasi ya kukatia tambi za taa, mabakuli, tarumbeta,+ au kitu chochote cha dhahabu au fedha kwa ajili ya nyumba ya Yehova.+ 14 Waliwapa pesa hizo wale tu waliofanya kazi hiyo, nao walizitumia kurekebisha nyumba ya Yehova. 15 Hawakudai hesabu ya matumizi ya pesa hizo kutoka kwa wanaume waliowapa pesa za kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu wanaume hao walikuwa waaminifu.+ 16 Hata hivyo, pesa za dhabihu za hatia+ na pesa za dhabihu za dhambi hazikuletwa katika nyumba ya Yehova; zilikuwa za makuhani.+
17 Wakati huo ndipo Hazaeli+ mfalme wa Siria alipanda kwenda kupigana na jiji la Gathi,+ naye akaliteka, kisha akaamua kulishambulia* jiji la Yerusalemu.+ 18 Ndipo Mfalme Yehoashi wa Yuda akachukua matoleo yote matakatifu ambayo mababu zake Yehoshafati, Yehoramu, na Ahazia, wafalme wa Yuda, walikuwa wameyatakasa na pia matoleo yake mwenyewe matakatifu na dhahabu yote iliyokuwa katika hazina za nyumba ya Yehova na katika nyumba ya mfalme,* akampelekea Hazaeli mfalme wa Siria.+ Kwa hiyo Hazaeli akaondoka Yerusalemu.
19 Na mambo mengine katika historia ya Yehoashi, mambo yote aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha nyakati za wafalme wa Yuda? 20 Hata hivyo, watumishi wake walipanga njama dhidi ya Yehoashi+ na kumuua katika nyumba ya Kilima,*+ katika njia inayoshuka kwenda Sila. 21 Yozakari mwana wa Shimeathi na Yehozabadi mwana wa Shomeri, watumishi wake, ndio waliompiga na kumuua.+ Wakamzika pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi, na Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.+
13 Katika mwaka wa 23 wa utawala wa Yehoashi+ mwana wa Ahazia+ mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu+ akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 17. 2 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, na kuendelea kutenda dhambi ya Yeroboamu mwana wa Nebati aliyosababisha Waisraeli kutenda.+ Hakugeuka na kuiacha. 3 Kwa hiyo hasira ya Yehova+ ikawaka dhidi ya Waisraeli,+ akawatia mikononi mwa Mfalme Hazaeli+ wa Siria na mikononi mwa Ben-hadadi+ mwana wa Hazaeli siku zao zote.
4 Baada ya muda Yehoahazi akamsihi Yehova amwonyeshe kibali,* naye Yehova akamsikiliza, kwa maana alikuwa ameona jinsi mfalme wa Siria alivyowakandamiza Waisraeli.+ 5 Basi Yehova akawapa Waisraeli mwokozi+ ili awaokoe kutoka mikononi mwa Wasiria, na Waisraeli wakakaa katika nyumba zao kama awali.* 6 (Hata hivyo, hawakuacha dhambi ya nyumba ya Yeroboamu aliyosababisha Waisraeli kutenda.+ Waliendelea kutenda* dhambi hiyo, na mti mtakatifu*+ ukaendelea kusimama huko Samaria.) 7 Yehoahazi akabaki tu na jeshi lenye wapanda farasi 50, magari 10 ya vita, na wanajeshi 10,000 wanaotembea kwa miguu kwa sababu mfalme wa Siria alikuwa amewaangamiza,+ aliwakanyaga-kanyaga kama mavumbi wakati wa kupura.+
8 Na mambo mengine katika historia ya Yehoahazi, mambo yote aliyofanya na ukuu wake, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 9 Kisha Yehoahazi akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake huko Samaria;+ na Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
10 Katika mwaka wa 37 wa utawala wa Mfalme Yehoashi wa Yuda, Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 16. 11 Akaendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, hakuacha kutenda dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati alizosababisha Waisraeli kutenda.+ Aliendelea kutenda* dhambi hizo.
12 Na mambo mengine katika historia ya Yehoashi, mambo yote aliyofanya na ukuu wake na jinsi alivyopigana na Mfalme Amazia wa Yuda,+ je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 13 Kisha Yehoashi akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake, na Yeroboamu*+ akaketi kwenye kiti chake cha ufalme. Naye Yehoashi akazikwa huko Samaria pamoja na wafalme wa Israeli.+
14 Sasa Elisha+ alipougua ugonjwa ambao hatimaye ulisababisha kifo chake, Yehoashi mfalme wa Israeli alishuka kwenda kwake na kumlilia akisema: “Baba yangu, baba yangu! Gari la vita la Israeli na wapanda farasi wake!”+ 15 Ndipo Elisha akamwambia: “Chukua upinde na mishale.” Basi akachukua upinde na mishale. 16 Kisha akamwambia mfalme wa Israeli: “Shika upinde wako.” Basi akashika upinde wake, halafu Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme. 17 Kisha akasema: “Fungua dirisha la upande wa mashariki.” Basi akalifungua. Elisha akasema: “Piga mshale!” Basi akapiga mshale. Sasa akasema: “Mshale wa ushindi* wa Yehova, mshale wa ushindi* dhidi ya Siria! Utapiga* Siria huko Afeki+ mpaka uiangamize kabisa.”
18 Akaendelea kusema: “Chukua mishale,” naye akaichukua. Kisha Elisha akamwambia mfalme wa Israeli: “Piga ardhi.” Basi akapiga ardhi mara tatu halafu akaacha. 19 Ndipo yule mtu wa Mungu wa kweli akamkasirikia sana na kumwambia: “Ulipaswa kuipiga ardhi mara tano au mara sita! Kama ungefanya hivyo, ungeipiga Siria mpaka uiangamize, lakini sasa utaipiga Siria mara tatu tu.”+
20 Baada ya hayo, Elisha akafa na kuzikwa. Kulikuwa na makundi ya wavamizi+ ya Wamoabu yaliyokuwa yakija nchini mwanzoni mwa mwaka.* 21 Wanaume fulani walipokuwa wakimzika mtu, waliona kundi la wavamizi, kwa hiyo wakamtupa mara moja mtu huyo ndani ya kaburi la Elisha na kukimbia. Mtu huyo alipogusa mifupa ya Elisha, akafufuka+ na kusimama.
22 Sasa Mfalme Hazaeli+ wa Siria aliwakandamiza Waisraeli+ sikuzote za utawala wa Yehoahazi. 23 Hata hivyo, Yehova akawaonyesha kibali na rehema+ na kuwajali kwa sababu ya agano lake na Abrahamu,+ Isaka,+ na Yakobo.+ Hakutaka kuwaangamiza, naye hajawatupa mbali kutoka mbele zake* mpaka leo. 24 Mfalme Hazaeli wa Siria alipokufa, Ben-hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake. 25 Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akayachukua tena majiji ambayo Ben-hadadi mwana wa Hazaeli alikuwa ameyachukua vitani kutoka kwa Yehoahazi baba yake. Yehoashi alimshinda Ben-hadadi mara tatu,+ naye akayakomboa majiji ya Israeli.
14 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Mfalme Yehoashi wa Yuda akawa mfalme. 2 Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 29 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Yehoadini wa Yerusalemu.+ 3 Aliendelea kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, lakini si kama Daudi+ babu yake. Alifanya mambo yote kama Yehoashi baba yake.+ 4 Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa,+ na watu bado walikuwa wakitoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu.+ 5 Mara tu ufalme ulipoimarika kabisa mikononi mwake, aliwaua watumishi wake waliomuua mfalme, baba yake.+ 6 Lakini hakuwaua wana wa wauaji hao, kulingana na amri hii ya Yehova iliyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa: “Akina baba hawapaswi kuuawa kwa sababu ya wana wao, na wana hawapaswi kuuawa kwa sababu ya baba zao; lakini kila mtu anapaswa kuuawa kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe.”+ 7 Akawaua Waedomu+ katika Bonde la Chumvi,+ wanaume 10,000, akaliteka jiji la Sela katika vita hivyo,+ na tangu wakati huo jiji hilo likaitwa Yoktheeli.
8 Kisha Amazia akawatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli, akisema: “Njoo, tupambane vitani.”*+ 9 Mfalme Yehoashi wa Israeli akatuma ujumbe huu kwa Mfalme Amazia wa Yuda: “Gugu lenye miiba kule Lebanoni lilituma ujumbe huu kwa mwerezi huko Lebanoni, ‘Mpe mwanangu binti yako awe mke wake.’ Hata hivyo, mnyama wa mwituni wa Lebanoni akapita karibu na kulikanyaga-kanyaga gugu hilo lenye miiba. 10 Ni kweli kwamba uliwaangamiza Waedomu,+ kwa hiyo moyo wako umekuwa na kiburi. Furahia utukufu wako, lakini kaa katika nyumba yako mwenyewe.* Kwa nini utafute msiba kisha uanguke, na kuwaangusha pia watu wa Yuda?” 11 Lakini Amazia hakusikiliza.+
Basi Mfalme Yehoashi wa Israeli akapanda kwenda huko, naye akapambana vitani na Mfalme Amazia wa Yuda huko Beth-shemeshi,+ jiji la Yuda.+ 12 Watu wa Yuda wakashindwa na Waisraeli, kwa hiyo kila mmoja akakimbilia nyumbani kwake.* 13 Mfalme Yehoashi wa Israeli akamkamata Mfalme Amazia wa Yuda, mwana wa Yehoashi mwana wa Ahazia, huko Beth-shemeshi. Kisha wakaja Yerusalemu, naye akabomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu+ mpaka Lango la Pembeni,+ urefu wa mikono 400.* 14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vitu vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Yehova na katika hazina za nyumba ya mfalme,* na pia akachukua mateka. Kisha akarudi Samaria.
15 Na mambo mengine katika historia ya Yehoashi, mambo aliyofanya na ukuu wake na jinsi alivyopigana na Mfalme Amazia wa Yuda, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 16 Kisha Yehoashi akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake huko Samaria+ pamoja na wafalme wa Israeli; na Yeroboamu mwana wake*+ akawa mfalme baada yake.
17 Amazia+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda aliendelea kuishi kwa miaka 15 baada ya kifo cha Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.+ 18 Na mambo mengine katika historia ya Amazia, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 19 Baadaye njama ikapangwa dhidi yake+ huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatie huko Lakishi, nao wakamuua huko. 20 Kwa hiyo wakambeba juu ya farasi, naye akazikwa Yerusalemu pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi.+ 21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria,*+ aliyekuwa na umri wa miaka 16,+ wakamweka kuwa mfalme baada ya Amazia baba yake.+ 22 Alijenga upya jiji la Elathi+ na kulirudisha kwa Yuda baada ya mfalme* kuzikwa pamoja na mababu zake.+
23 Katika mwaka wa 15 wa utawala wa Amazia mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu+ mwana wa Mfalme Yehoashi wa Israeli akawa mfalme huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 41. 24 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova. Hakuacha dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Waisraeli kutenda.+ 25 Alirudisha mpaka wa Israeli kuanzia Lebo-hamathi*+ hadi kwenye Bahari ya Araba,*+ kulingana na neno ambalo Yehova Mungu wa Israeli alisema kupitia Yona+ mtumishi wake, mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-heferi.+ 26 Kwa maana Yehova alikuwa ameyaona mateso makali sana ya Waisraeli.+ Hakukuwa na yeyote aliyebaki wa kuwasaidia Waisraeli, hata watu wasio na uwezo au walio dhaifu hawakuwepo. 27 Lakini Yehova alikuwa ameahidi kwamba hatafutilia mbali jina la Israeli kutoka chini ya mbingu.+ Kwa hiyo akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.+
28 Na mambo mengine katika historia ya Yeroboamu, mambo yote aliyofanya na ukuu wake, jinsi alivyopigana na jinsi alivyorudisha jiji la Damasko+ na Hamathi+ ili yamilikiwe tena na Yuda nchini Israeli, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 29 Kisha Yeroboamu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake, pamoja na wafalme wa Israeli; na Zekaria+ mwanawe akawa mfalme baada yake.
15 Katika mwaka wa 27 wa utawala wa Mfalme Yeroboamu* wa Israeli, Azaria*+ mwana wa Mfalme Amazia+ wa Yuda akawa mfalme.+ 2 Alikuwa na umri wa miaka 16 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 52 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu. 3 Aliendelea kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, kama alivyotenda Amazia baba yake.+ 4 Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa,+ na watu bado walikuwa wakitoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu.+ 5 Yehova alimletea mfalme pigo, naye aliendelea kuwa na ukoma+ mpaka siku aliyokufa; alikaa katika nyumba iliyotengwa,+ huku Yothamu mwana wa mfalme+ akiisimamia nyumba ya mfalme,* akiwahukumu watu nchini.+ 6 Na mambo mengine katika historia ya Azaria,+ mambo yote aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 7 Kisha Azaria akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake+ katika Jiji la Daudi; na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
8 Katika mwaka wa 38 wa utawala wa Mfalme Azaria+ wa Yuda, Zekaria+ mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miezi sita. 9 Alitenda maovu machoni pa Yehova, kama walivyotenda mababu zake. Hakuacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati alizosababisha Waisraeli kutenda.+ 10 Kisha Shalumu mwana wa Yabeshi akapanga njama dhidi yake na kumuua+ huko Ibleamu.+ Baada ya kumuua, Shalumu akawa mfalme. 11 Na mambo mengine katika historia ya Zekaria yameandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli. 12 Hilo lilitimiza neno hili la Yehova alilokuwa amemwambia Yehu: “Vizazi vinne vya wana wako+ vitaketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.”+ Na ikawa hivyo.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa 39 wa utawala wa Mfalme Uzia+ wa Yuda, naye alitawala kwa mwezi mmoja kamili huko Samaria. 14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akapanda kutoka Tirsa+ na kuja Samaria, akamuua Shalumu+ mwana wa Yabeshi huko Samaria. Baada ya kumuua, akawa mfalme. 15 Mambo mengine katika historia ya Shalumu na njama aliyopanga, yameandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli. 16 Wakati huo ndipo Menahemu alipokuja kutoka Tirsa na kuliangamiza jiji la Tifsa na wote waliokuwa katika jiji hilo na katika eneo lake, kwa sababu hawakumfungulia malango ya jiji hilo. Aliliangamiza na kuwapasua tumbo wanawake wenye mimba wa jiji hilo.
17 Katika mwaka wa 39 wa utawala wa Mfalme Azaria wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, naye alitawala kwa miaka kumi huko Samaria. 18 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova. Na sikuzote za utawala wake hakuacha dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati alizosababisha Waisraeli kutenda.+ 19 Mfalme Pulu+ wa Ashuru aliingia nchini, na Menahemu akampa Pulu talanta 1,000 za fedha* ili amsaidie kuimarisha mamlaka yake katika ufalme huo.+ 20 Kwa hiyo Menahemu alikusanya fedha hizo kwa kuwatoza ushuru wanaume mashuhuri na matajiri wa Israeli.+ Akampa mfalme wa Ashuru shekeli 50 za fedha* kwa kila mwanamume. Kisha mfalme wa Ashuru akarudi, hakukaa nchini. 21 Na mambo mengine katika historia ya Menahemu,+ mambo yote aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 22 Kisha Menahemu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake; na Pekahia mwana wake akawa mfalme baada yake.
23 Katika mwaka wa 50 wa utawala wa Mfalme Azaria wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miaka miwili. 24 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova. Hakuacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati alizosababisha Waisraeli kutenda.+ 25 Kisha Peka+ mwana wa Remalia kamanda wake msaidizi akapanga njama dhidi yake na kumuua huko Samaria katika mnara wenye ngome wa nyumba ya mfalme* pamoja na Argobu na Arie. Alikuwa pamoja na wanaume 50 wa Gileadi; na baada ya kumuua, akawa mfalme. 26 Na mambo mengine katika historia ya Pekahia, mambo yote aliyofanya, yameandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli.
27 Katika mwaka wa 52 wa utawala wa Mfalme Azaria wa Yuda, Peka+ mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 20. 28 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, naye hakuacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati alizosababisha Waisraeli kutenda.+ 29 Katika siku za utawala wa Mfalme Peka wa Israeli, Mfalme Tiglath-pileseri+ wa Ashuru alivamia na kuteka Iyoni, Abel-beth-maaka,+ Yanoa, Kedeshi, Hasori, Gileadi,+ na Galilaya,+ nchi yote ya Naftali,+ akawapeleka wakaaji wa maeneo hayo uhamishoni kule Ashuru.+ 30 Kisha Hoshea+ mwana wa Ela akapanga njama dhidi ya Peka mwana wa Remalia, akampiga na kumuua; naye akawa mfalme baada yake katika mwaka wa 20 wa utawala wa Yothamu+ mwana wa Uzia. 31 Na mambo mengine katika historia ya Peka, mambo yote aliyofanya, yameandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu+ mwana wa Mfalme Uzia+ wa Yuda akawa mfalme. 33 Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 16 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Yerusha binti ya Sadoki.+ 34 Aliendelea kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, kama alivyofanya Uzia baba yake.+ 35 Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa, na watu bado walikuwa wakitoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu.+ Yeye ndiye aliyejenga lango la juu la nyumba ya Yehova.+ 36 Na mambo mengine katika historia ya Yothamu, mambo aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 37 Siku hizo Yehova alianza kumtuma Resini mfalme wa Siria na Peka+ mwana wa Remalia kushambulia Yuda.+ 38 Kisha Yothamu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi babu yake. Na Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
16 Katika mwaka wa 17 wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, Ahazi+ mwana wa Mfalme Yothamu wa Yuda akawa mfalme. 2 Ahazi alikuwa na umri wa miaka 20 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 16 huko Yerusalemu. Hakutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova Mungu wake, kama alivyotenda Daudi babu yake.+ 3 Badala yake, alitembea katika njia ya wafalme wa Israeli,+ na hata alimteketeza* motoni mwana wake mwenyewe,+ akifuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli. 4 Aliendelea pia kutoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu,+ kwenye vilima, na chini ya kila mti wenye majani mengi.+
5 Wakati huo ndipo Mfalme Resini wa Siria na Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli walipopanda ili kuja kupigana vita dhidi ya Yerusalemu.+ Wakamzingira Ahazi lakini hawakuweza kuliteka jiji. 6 Wakati huo Mfalme Resini wa Siria akarudisha Elathi+ kwa Edomu, kisha akawafukuza Wayahudi* kutoka Elathi. Na Waedomu wakaingia Elathi, nao wamekuwa wakiishi humo tangu wakati huo. 7 Kwa hiyo Ahazi akatuma wajumbe kwa Mfalme Tiglath-pileseri+ wa Ashuru, akisema: “Mimi ni mtumishi wako na mwanao. Njoo uniokoe kutoka mikononi mwa mfalme wa Siria na kutoka mikononi mwa mfalme wa Israeli, wanaonishambulia.” 8 Kisha Ahazi akachukua fedha na dhahabu iliyokuwa katika nyumba ya Yehova na katika hazina za nyumba ya mfalme,* akampelekea mfalme wa Ashuru kama rushwa.+ 9 Mfalme wa Ashuru akakubali ombi lake, naye akapanda kwenda Damasko na kuliteka jiji hilo na kuwapeleka watu wake uhamishoni huko Kiri,+ akamuua Resini.+
10 Ndipo Mfalme Ahazi akaenda kukutana na Mfalme Tiglath-pileseri wa Ashuru kule Damasko. Alipoona madhabahu iliyokuwa Damasko, Mfalme Ahazi akamtumia kuhani Uriya ramani ya madhabahu hiyo, akamwonyesha mfano wake na jinsi ilivyojengwa.+ 11 Kuhani Uriya+ akajenga madhabahu+ kulingana na maagizo yote ambayo Mfalme Ahazi alikuwa ametuma kutoka Damasko. Kuhani Uriya akamaliza kuijenga kabla ya Mfalme Ahazi kurudi kutoka Damasko. 12 Mfalme aliporudi kutoka Damasko na kuiona madhabahu hiyo, aliikaribia na kutoa dhabihu juu yake.+ 13 Akaendelea kufukizia moshi wa dhabihu zake za kuteketezwa na matoleo yake ya nafaka juu ya madhabahu hiyo; pia aliimiminia madhabahu hiyo matoleo yake ya kinywaji na kuinyunyizia damu ya dhabihu zake za ushirika. 14 Kisha akaiondoa madhabahu ya shaba+ iliyokuwa mbele za Yehova, kutoka mahali ilipokuwa mbele ya nyumba, katikati ya madhabahu yake na nyumba ya Yehova, akaiweka upande wa kaskazini wa madhabahu yake. 15 Mfalme Ahazi akamwamuru hivi kuhani Uriya:+ “Fukiza moshi wa dhabihu ya asubuhi kwenye madhabahu hiyo kubwa,+ pia toleo la nafaka la jioni,+ dhabihu ya kuteketezwa ya mfalme, na toleo lake la nafaka, na pia dhabihu za kuteketezwa, matoleo ya nafaka, na matoleo ya kinywaji ya watu wote. Unapaswa pia kuinyunyizia madhabahu hiyo damu yote ya dhabihu za kuteketezwa na damu yote ya dhabihu nyingine. Nitaamua nitakalofanya na madhabahu ya shaba.” 16 Kuhani Uriya akafanya mambo yote ambayo Mfalme Ahazi aliamuru.+
17 Zaidi ya hayo, Mfalme Ahazi akazikata vipandevipande kuta za pembeni za yale magari+ na kuondoa mabeseni yaliyokuwa juu yake,+ akaiondoa ile Bahari kutoka juu ya wale ng’ombe dume wa shaba+ na kuiweka kwenye sakafu ya mawe.+ 18 Pia, alihamisha kutoka katika nyumba ya Yehova sehemu iliyofunikwa ambayo ilikuwa imejengwa katika nyumba hiyo kwa ajili ya Sabato na pia njia ya nje aliyotumia mfalme kuingia katika nyumba hiyo; alifanya hivyo kwa sababu ya mfalme wa Ashuru.
19 Na mambo mengine katika historia ya Ahazi, mambo aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda?+ 20 Kisha Ahazi akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake katika Jiji la Daudi; na Hezekia*+ mwanawe akawa mfalme baada yake.
17 Katika mwaka wa 12 wa utawala wa Mfalme Ahazi wa Yuda, Hoshea+ mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli huko Samaria; alitawala kwa miaka tisa. 2 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, lakini si kwa kiwango ambacho wafalme wa Israeli waliomtangulia walitenda. 3 Mfalme Shalmanesa wa Ashuru alipanda kuja kumshambulia,+ na Hoshea akawa mtumishi wake, akaanza kumlipa ushuru.+ 4 Hata hivyo, mfalme wa Ashuru alipata habari kwamba Hoshea alishiriki kupanga njama fulani, kwa maana alikuwa amewatuma wajumbe kwa Mfalme So wa Misri+ na hakuleta ushuru kwa mfalme wa Ashuru kama alivyofanya miaka iliyotangulia. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akamfunga na kumtia gerezani.
5 Mfalme wa Ashuru aliivamia nchi nzima, naye akaja Samaria na kulizingira kwa miaka mitatu. 6 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mfalme wa Ashuru aliliteka jiji la Samaria.+ Kisha akawapeleka Waisraeli uhamishoni+ kule Ashuru na kuwaweka katika eneo la Hala na Habori kando ya mto Gozani+ na katika majiji ya Wamedi ili waishi humo.+
7 Hilo lilitendeka kwa sababu Waisraeli walimtendea dhambi Yehova Mungu wao, aliyewatoa nchini Misri kutoka mikononi mwa Farao mfalme wa Misri.+ Waliabudu* miungu mingine,+ 8 wakafuata desturi za mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli, nao wakafuata desturi zilizoanzishwa na wafalme wa Israeli.
9 Waisraeli walikuwa wakifuatia mambo ambayo hayakuwa sawa machoni pa Yehova Mungu wao. Wakaendelea kujenga mahali pa juu katika majiji yao yote,+ kuanzia mnara wa walinzi mpaka jiji lenye ngome.* 10 Wakaendelea kujisimamishia nguzo takatifu na miti mitakatifu*+ juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi;+ 11 nao walikuwa wakifukiza moshi wa dhabihu mahali pote pa juu kama yalivyofanya mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyapeleka uhamishoni kutoka mbele yao.+ Waliendelea kutenda maovu na kumkasirisha Yehova.
12 Waliendelea kuabudu sanamu zenye kuchukiza,*+ ambazo Yehova alikuwa amewaambia hivi kuzihusu: “Msifanye hivyo!”+ 13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.” 14 Lakini hawakusikiliza, nao wakaendelea kuwa wakaidi kama* mababu zao ambao hawakudhihirisha imani katika Yehova Mungu wao.+ 15 Waliendelea kukataa masharti yake na agano lake+ alilofanya na mababu zao na vikumbusho vyake alivyowapa ili kuwaonya,+ nao wakaendelea kufuata sanamu za ubatili,+ na wao wenyewe wakawa ubatili,+ wakiiga mataifa yaliyowazunguka pande zote ambayo Yehova alikuwa amewaamuru wasiyaige.+
16 Waliendelea kuacha amri zote za Yehova Mungu wao, nao wakatengeneza sanamu za chuma* za ndama wawili+ na kutengeneza mti mtakatifu,*+ nao wakaliinamia jeshi lote la mbinguni+ na kumwabudu Baali.+ 17 Pia waliwateketeza* motoni wana wao na mabinti wao,+ wakafanya uaguzi,*+ wakatafuta ishara za ubashiri, na wakaendelea kujitoa* wenyewe kutenda maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.
18 Kwa hiyo Yehova akawakasirikia sana Waisraeli hivi kwamba akawaondoa mbele zake.+ Hakumwacha yeyote abaki isipokuwa watu wa kabila la Yuda peke yao.
19 Hata watu wa kabila la Yuda hawakushika amri za Yehova Mungu wao;+ walifuata pia desturi zilizofuatwa na Waisraeli.+ 20 Yehova aliwakataa wazao wote wa Israeli, akawaaibisha na kuwatia mikononi mwa waporaji, mpaka alipowatupa mbali kutoka mbele zake. 21 Aliwararua Waisraeli kutoka katika nyumba ya Daudi, nao wakamweka Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme.+ Lakini Yeroboamu akasababisha Waisraeli wapotoke na kuacha kumfuata Yehova, naye akasababisha watende dhambi kubwa. 22 Na Waisraeli wakaendelea kufuata dhambi zote ambazo Yeroboamu alitenda.+ Hawakuziacha 23 mpaka Yehova alipowaondoa Waisraeli kutoka mbele zake, kama alivyokuwa amesema kupitia watumishi wake wote manabii.+ Kwa hiyo Waisraeli wakaondolewa katika nchi yao na kupelekwa uhamishoni kule Ashuru,+ nao wangali huko hadi leo.
24 Kisha mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babiloni, Kutha, Ava, Hamathi, na Sefarvaimu+ na kuwaweka katika majiji ya Samaria ili waishi humo badala ya Waisraeli; nao wakamiliki Samaria na kuishi katika majiji yake. 25 Walipoanza kuishi humo, hawakumwogopa* Yehova. Kwa hiyo Yehova akawatuma simba waje miongoni mwao,+ nao wakawaua baadhi ya watu. 26 Mfalme wa Ashuru akapata habari hii: “Mataifa uliyoyapeleka uhamishoni na kuyaweka katika majiji ya Samaria ili yaishi humo hayajui dini* ya Mungu wa nchi hiyo. Kwa hiyo anaendelea kuwatuma simba miongoni mwao; na simba hao wanawaua, kwa sababu hakuna yeyote kati yao anayejua dini ya Mungu wa nchi hiyo.”
27 Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mrudisheni huko mmoja wa makuhani mliowaleta uhamishoni, aishi huko na kuwafundisha watu hao dini ya Mungu wa nchi hiyo.” 28 Basi mmoja wa makuhani ambao walikuwa wamepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akarudi na kuishi Betheli,+ naye akaanza kuwafundisha jinsi wanavyopaswa kumwogopa* Yehova.+
29 Hata hivyo, kila taifa likajitengenezea mungu wake na kumweka* katika nyumba za ibada mahali pa juu ambapo Wasamaria walikuwa wamejenga; kila taifa lilifanya hivyo katika majiji walimokuwa wakiishi. 30 Basi wanaume wa Babiloni wakatengeneza Sukoth-benothi, na wanaume wa Kuthi wakatengeneza Nergali, na wanaume wa Hamathi+ wakatengeneza Ashima, 31 na Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki. Wasefarvaimu walikuwa wakiwateketeza wana wao motoni kwa ajili ya Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.+ 32 Ingawa walimwogopa Yehova, waliwachagua makuhani kutoka kwa watu wa kawaida ili wahudumu mahali pa juu, na makuhani hao walihudumu kwa niaba yao mahali pa juu katika nyumba za ibada.+ 33 Kwa hiyo walimwogopa Yehova, lakini waliabudu miungu yao wenyewe kulingana na dini* ya mataifa ambamo walitolewa.+
34 Mpaka leo wanafuata dini* zao za awali. Hakuna yeyote kati yao anayemwabudu* Yehova, na hakuna yeyote anayefuata maagizo yake, hukumu zake, na Sheria, na amri ambayo Yehova aliwapa wana wa Yakobo, ambaye alibadili jina lake na kumwita Israeli.+ 35 Yehova alipofanya agano pamoja nao,+ aliwaamuru hivi: “Msiogope miungu mingine, wala msiiinamie wala kuiabudu wala kuitolea dhabihu.+ 36 Lakini mnapaswa kumwogopa Yehova, aliyewatoa nchini Misri kwa nguvu nyingi na kwa mkono ulionyooshwa,+ Yeye ndiye mnayepaswa kumwogopa,+ nanyi mnapaswa kumwinamia yeye, nanyi mnapaswa kumtolea yeye dhabihu. 37 Nanyi mnapaswa sikuzote kufuata kwa uangalifu masharti, maamuzi, Sheria, na amri aliyowaandikia,+ na hampaswi kuogopa miungu mingine. 38 Na hampaswi kusahau agano nililofanya pamoja nanyi,+ na hampaswi kuogopa miungu mingine. 39 Lakini mnapaswa kumwogopa Yehova Mungu wenu, kwa kuwa yeye ndiye atakayewaokoa kutoka mikononi mwa maadui wenu wote.”
40 Lakini hawakutii, nao wakafuata dini* yao ya awali.+ 41 Kwa hiyo mataifa hayo yakamwogopa Yehova,+ lakini yalikuwa pia yakiabudu sanamu zao za kuchongwa. Wana wao na wajukuu wao wamekuwa wakitenda kama mababu zao mpaka leo hii.
18 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea+ mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia+ mwana wa Mfalme Ahazi+ wa Yuda akawa mfalme. 2 Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 29 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Abi* binti ya Zekaria.+ 3 Aliendelea kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova,+ kama alivyofanya Daudi babu yake.+ 4 Yeye ndiye aliyeondoa mahali pa juu,+ akazivunjavunja nguzo takatifu, na kuukata ule mti mtakatifu.*+ Pia alimpondaponda yule nyoka wa shaba aliyetengenezwa na Musa;+ kwa maana mpaka wakati huo Waisraeli walikuwa wakimfukizia moshi wa dhabihu, na nyoka huyo alikuwa akiitwa sanamu ya nyoka wa shaba.* 5 Alimtumaini Yehova+ Mungu wa Israeli; na hakuna mfalme yeyote kati ya wafalme wote wa Yuda aliyekuwa kama yeye, kabla yake wala baada yake. 6 Alishikamana kabisa na Yehova.+ Hakugeuka na kuacha kumfuata; aliendelea kushika amri ambazo Yehova alimpa Musa. 7 Na Yehova alikuwa pamoja naye. Popote alipoenda, alitenda kwa hekima. Alimwasi mfalme wa Ashuru na kukataa kumtumikia.+ 8 Aliwashinda pia Wafilisti+ mpaka Gaza na maeneo yake, kuanzia mnara wa walinzi mpaka jiji lenye ngome.*
9 Katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, yaani, mwaka wa saba wa Hoshea+ mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Mfalme Shalmanesa wa Ashuru alikuja kushambulia Samaria, akaanza kulizingira.+ 10 Nao wakaliteka+ baada ya miaka mitatu; Samaria lilitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Hoshea wa Israeli. 11 Kisha mfalme wa Ashuru akawapeleka Waisraeli uhamishoni+ kule Ashuru na kuwaweka katika eneo la Hala na Habori kando ya mto Gozani na katika majiji ya Wamedi ili waishi humo.+ 12 Walipelekwa huko kwa sababu hawakuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wao, badala yake waliendelea kuvunja agano lake, mambo yote ambayo Musa mtumishi wa Yehova aliamuru.+ Hawakusikiliza wala kutii.
13 Katika mwaka wa 14 wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru+ alipanda kuja kuyashambulia majiji yote yenye ngome ya Yuda na kuyateka.+ 14 Kwa hiyo Mfalme Hezekia wa Yuda akatuma ujumbe huu kwa mfalme wa Ashuru kule Lakishi: “Nimekosea. Ondokeni, msinishambulie, nami nitalipa chochote mtakachonitoza.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Mfalme Hezekia wa Yuda faini ya talanta 300 za fedha* na talanta 30 za dhahabu. 15 Basi Hezekia akawapa fedha yote iliyokuwa katika nyumba ya Yehova na katika hazina za nyumba ya mfalme.*+ 16 Wakati huo Hezekia aling’oa* milango ya hekalu+ la Yehova na miimo ambayo yeye mwenyewe, Mfalme Hezekia wa Yuda, alikuwa ameifunika kwa dhahabu,+ naye akampa mfalme wa Ashuru.
17 Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma Tartani,* Rabsarisi,* na Rabshake* pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi+ kwenda kwa Mfalme Hezekia kule Yerusalemu.+ Wakapanda kwenda Yerusalemu na kujipanga karibu na mfereji wa kidimbwi cha juu, kwenye barabara kuu ya uwanja wa mfuaji wa nguo.+ 18 Walipomwita mfalme atoke nje, Eliakimu+ mwana wa Hilkia, aliyekuwa msimamizi wa nyumba,* Shebna+ aliyekuwa mwandishi, na Yoa mwana wa Asafu aliyefanya kazi ya kuweka kumbukumbu, wakaenda nje kukutana nao.
19 Basi Rabshake akawaambia: “Tafadhali, mwambieni hivi Hezekia: ‘Mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru, anauliza, “Ujasiri wako unategemea msingi gani?+ 20 Unasema, ‘Nina mbinu na nguvu za kupigana vita,’ lakini hayo ni maneno matupu. Unamtumaini nani, hivi kwamba unathubutu kuniasi mimi?+ 21 Tazama! Unautumaini msaada wa utete huu uliopondeka, Misri,+ ambao mtu yeyote akiuegemea utamchoma kiganja na kukitoboa. Hivyo ndivyo Farao mfalme wa Misri alivyo kwa wote wanaomtumaini. 22 Nawe ukiniambia, ‘Tunamtumaini Yehova Mungu wetu,’+ je, si yeye ndiye ambaye mahali pake pa juu na madhabahu zake zimeondolewa na Hezekia,+ huku akiwaambia watu wa Yuda na Yerusalemu, ‘Mnapaswa kuinama mbele ya madhabahu hii hapa Yerusalemu’?”’+ 23 Basi sasa, tafadhali, fanya mkataba huu pamoja na bwana wangu mfalme wa Ashuru: nitakupa farasi 2,000 ikiwa unaweza kupata wapanda farasi wa kutosha idadi hiyo.+ 24 Basi, unawezaje kumzuia hata gavana mmoja aliye mdogo zaidi kati ya watumishi wa bwana wangu, huku ukiitumaini nchi ya Misri ili upate magari ya vita na wapanda farasi? 25 Sasa je, nimepanda kuja kushambulia mahali hapa ili kupaharibu bila kupewa idhini na Yehova? Yehova mwenyewe aliniambia, ‘Panda uende kuishambulia nchi hii na kuiharibu.’”
26 Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, na Shebna+ na Yoa wakamwambia Rabshake:+ “Tafadhali, zungumza nasi watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu,*+ kwa maana tunaweza kuielewa; usizungumze nasi kwa lugha ya Wayahudi huku watu walio ukutani wakisikia.”+ 27 Lakini Rabshake akawaambia: “Je, bwana wangu amenituma niwaambie ninyi na bwana wenu tu maneno haya? Je, sipaswi kuwaambia pia wanaume wanaoketi ukutani, wale watakaokula kinyesi chao wenyewe na kunywa mkojo wao wenyewe pamoja nanyi?”
28 Kisha Rabshake akasimama na kusema hivi kwa sauti kubwa kwa lugha ya Wayahudi: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru.+ 29 Mfalme anasema hivi: ‘Msikubali Hezekia awadanganye, kwa maana hawezi kuwaokoa kutoka mikononi mwangu.+ 30 Na msikubali Hezekia awafanye mumtumaini Yehova mkisema: “Kwa hakika Yehova atatuokoa, na jiji hili halitatiwa mikononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 31 Msimsikilize Hezekia, kwa maana mfalme wa Ashuru anasema hivi: “Fanyeni amani pamoja nami na mjisalimishe,* na kila mmoja wenu atakula matunda ya mzabibu wake mwenyewe na matunda ya mtini wake mwenyewe na kunywa maji kutoka katika tangi lake mwenyewe, 32 mpaka nitakapokuja na kuwapeleka katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe,+ nchi yenye nafaka na divai mpya, nchi yenye mikate na mashamba ya mizabibu, nchi yenye mizeituni na asali. Ndipo mtakapoishi, nanyi hamtakufa. Msimsikilize Hezekia, kwa maana anawapotosha kwa kusema, ‘Yehova atatuokoa.’ 33 Je, kuna mungu yeyote kati ya miungu ya mataifa ambaye amewahi kuiokoa nchi yake kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru? 34 Iko wapi miungu ya Hamathi+ na Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu,+ Hena, na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mikononi mwangu?+ 35 Ni mungu yupi kati ya miungu yote ya nchi mbalimbali ambaye ameokoa nchi yake kutoka mikononi mwangu, hivi kwamba Yehova aokoe Yerusalemu kutoka mikononi mwangu?”’”+
36 Lakini watu walikaa kimya, hawakumjibu neno lolote, kwa maana mfalme alikuwa amewaagiza hivi: “Msimjibu.”+ 37 Lakini Eliakimu mwana wa Hilkia, aliyekuwa msimamizi wa nyumba,* Shebna aliyekuwa mwandishi, na Yoa mwana wa Asafu aliyekuwa akifanya kazi ya kuweka kumbukumbu wakaja kwa Hezekia mavazi yao yakiwa yameraruliwa, wakamwambia maneno ya Rabshake.
19 Mara tu Mfalme Hezekia aliposikia hilo, akayararua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia na kuingia katika nyumba ya Yehova.+ 2 Kisha akamtuma Eliakimu, aliyekuwa msimamizi wa nyumba,* Shebna aliyekuwa mwandishi, na wazee miongoni mwa makuhani, wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya,+ mwana wa Amozi. 3 Wakamwambia: “Hezekia anasema hivi: ‘Leo ni siku ya taabu, ya kemeo,* na ya aibu; kwa maana watoto wako tayari kuzaliwa,* lakini hakuna nguvu za kuwazaa.+ 4 Huenda Yehova Mungu wako atayasikia maneno yote ya Rabshake, aliyetumwa na bwana wake mfalme wa Ashuru ili amdhihaki Mungu aliye hai,+ naye atamfanya awajibike kwa sababu ya maneno ambayo Yehova Mungu wako amesikia. Basi toa sala+ kwa niaba ya watu waliobaki ambao wameokoka.’”
5 Kwa hiyo watumishi wa Mfalme Hezekia wakaenda kwa Isaya,+ 6 naye Isaya akawaambia: “Mwambieni hivi bwana wenu, ‘Yehova anasema hivi: “Usiogope+ kwa sababu ya maneno uliyosikia, maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru waliyasema na kunikufuru.+ 7 Sasa ninatia wazo fulani akilini mwake,* naye atasikia habari na kurudi katika nchi yake mwenyewe; nami nitamuua kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.”’”+
8 Baada ya Rabshake kusikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi,+ alirudi na kumkuta akipigana vita na Libna.+ 9 Ndipo mfalme akasikia maneno haya yakisemwa kumhusu Tirhaka mfalme wa Ethiopia: “Ametoka ili kuja kupigana nawe.” Kwa hiyo akawatuma tena wajumbe+ kwa Hezekia, akisema: 10 “Mwambieni hivi Mfalme Hezekia wa Yuda: ‘Usikubali Mungu wako unayemtumaini akudanganye akisema: “Yerusalemu halitatiwa mikononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 11 Tazama! Umesikia mambo ambayo wafalme wa Ashuru walizitendea nchi zote kwa kuziangamiza.+ Je, ni wewe peke yako utakayeokolewa? 12 Je, miungu ya mataifa yaliyoangamizwa na mababu zangu iliyaokoa mataifa hayo? Gozani, Harani,+ Resefu, na watu wa Edeni waliokuwa Tel-asari wako wapi? 13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, na mfalme wa majiji ya Sefarvaimu, na wa Hena, na wa Iva?’”+
14 Hezekia akachukua barua hizo kutoka mikononi mwa wajumbe na kuzisoma. Kisha Hezekia akapanda kwenda katika nyumba ya Yehova, akazitandaza mbele za Yehova.+ 15 Hezekia akaanza kusali+ mbele za Yehova akisema: “Ee Yehova Mungu wa Israeli, unayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi,+ wewe peke yako ndiye Mungu wa kweli wa falme zote za dunia.+ Uliumba mbingu na dunia. 16 Tega sikio lako, Ee Yehova, usikie!+ Fungua macho yako,+ Ee Yehova, uone! Sikia maneno ambayo Senakeribu amesema ili kukudhihaki wewe Mungu uliye hai. 17 Ee Yehova, ni kweli kwamba wafalme wa Ashuru wameharibu mataifa na nchi zao.+ 18 Nao wameitupa miungu yao motoni, kwa sababu haikuwa miungu+ bali kazi ya mikono ya wanadamu,+ miti na mawe. Ndiyo sababu waliweza kuiangamiza. 19 Lakini sasa, Ee Yehova Mungu wetu, tafadhali tuokoe kutoka mikononi mwake, ili falme zote duniani zijue kwamba wewe peke yako ndiye Mungu, Ee Yehova.”+
20 Kisha Isaya mwana wa Amozi akatuma ujumbe huu kwa Hezekia: “Yehova Mungu wa Israeli anasema, ‘Nimesikia sala yako+ ambayo umenitolea kumhusu Mfalme Senakeribu wa Ashuru.+ 21 Hili ndilo neno ambalo Yehova amesema dhidi yake:
“Binti bikira wa Sayuni anakudharau, anakudhihaki.
Binti ya Yerusalemu anakutikisia kichwa.
22 Umemdhihaki na kumkufuru nani?+
Umepaza sauti yako dhidi ya nani+
Na kuinua macho yako yenye kiburi?
Ni dhidi ya Mtakatifu wa Israeli!+
23 Kupitia wajumbe wako+ umemdhihaki Yehova+ ukisema,
‘Kwa wingi wa magari yangu ya vita
Nitapanda vilele vya milima,
Sehemu za mbali sana za Lebanoni.
Nitakata mierezi yake mirefu sana, miberoshi yake iliyo bora.
Nitaingia mahali pake palipo ndani kabisa, misitu yake yenye miti mingi sana.
24 Nitachimba visima na kunywa maji mageni;
Nitavikausha vijito vyote vya* Misri kwa nyayo za miguu yangu.’
25 Je, hujasikia? Tangu zamani za kale liliamuliwa.*+
Tangu siku zilizopita nimelitayarisha.*+
Sasa nitalitimiza.+
Utayabadili majiji yenye ngome yawe marundo ya magofu yenye ukiwa.+
26 Wakaaji wake hawatakuwa na uwezo;
Wataogopeshwa na kuaibishwa.
Watakuwa kama mimea ya shambani na nyasi mbichi,+
Kama nyasi zilizo kwenye paa zinazokaushwa na upepo wa mashariki.
27 Lakini ninajua vizuri unapoketi, unapotoka nje, unapoingia,+
Na unapokuwa na ghadhabu dhidi yangu,+
28 Kwa sababu ghadhabu yako dhidi yangu+ na mngurumo wako umefika masikioni mwangu.+
Basi nitatia kulabu yangu puani mwako na lijamu yangu+ katikati ya midomo yako,
Nami nitakurudisha kupitia njia uliyoitumia kuja.”+
29 “‘Na hii ndiyo itakayokuwa ishara kwako:* Mwaka huu utakula mimea inayoota yenyewe;* na katika mwaka wa pili utakula nafaka inayochipuka kutoka katika mimea hiyo;+ lakini katika mwaka wa tatu utapanda mbegu na kuvuna, nawe utapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.+ 30 Watu wa nyumba ya Yuda watakaoponyoka, wale wanaobaki,+ watatia mizizi chini na kuzaa matunda kwenda juu. 31 Kwa maana waliobaki watatoka Yerusalemu na waokokaji watatoka katika Mlima Sayuni. Bidii ya Yehova wa majeshi itatenda hayo.+
32 “‘Kwa hiyo Yehova anasema hivi kuhusu mfalme wa Ashuru:+
“Hataingia katika jiji hili+
Wala hatapiga mshale humo
Wala kulikabili kwa ngao
Wala kujenga boma la kulizingira.+
33 Atarudi kupitia njia aliyotumia kuja;
Hataingia katika jiji hili,” asema Yehova.
34 “Nitalilinda jiji hili+ na kuliokoa kwa ajili yangu mwenyewe+
Na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”’”+
35 Usiku huohuo malaika wa Yehova alienda na kuwaua wanaume 185,000 katika kambi ya Waashuru.+ Watu walipoamka asubuhi na mapema, waliona maiti zote hizo.+ 36 Kwa hiyo Mfalme Senakeribu wa Ashuru akaondoka, akarudi Ninawi+ na kukaa huko.+ 37 Alipokuwa akiinama chini katika nyumba ya* Nisroki mungu wake, watoto wake mwenyewe wa kiume Adrameleki na Shareza walimuua kwa upanga+ na kutorokea nchi ya Ararati.+ Na Esar-hadoni+ mwanawe akawa mfalme baada yake.
20 Siku hizo Hezekia akawa mgonjwa karibu afe.+ Nabii Isaya mwana wa Amozi akaja na kumwambia, “Yehova anasema hivi: ‘Wape maagizo watu wa nyumba yako, kwa maana utakufa; hutapona.’”+ 2 Ndipo akaugeuza uso wake kuelekea ukutani, akaanza kusali hivi kwa Yehova: 3 “Nakusihi, Ee Yehova, tafadhali, kumbuka jinsi ambavyo nimetembea mbele zako kwa uaminifu na kwa moyo kamili, nami nimetenda mambo mema machoni pako.”+ Kisha Hezekia akaanza kulia sana na kububujikwa na machozi.
4 Isaya hakuwa amefika katika ua wa katikati, neno la Yehova lilipomjia likisema:+ 5 “Rudi ukamwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, ‘Yehova Mungu wa Daudi babu yako anasema hivi: “Nimesikia sala yako. Nimeona machozi yako.+ Tazama, ninakuponya.+ Siku ya tatu utapanda kwenda katika nyumba ya Yehova.+ 6 Nitakuongezea miaka 15 ya kuishi,* nami nitakuokoa wewe na jiji hili kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru,+ nami nitalilinda jiji hili kwa ajili yangu mwenyewe na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”’”+
7 Ndipo Isaya akasema: “Leteni keki ya tini kavu zilizoshinikizwa.” Basi wakaileta na kuipaka kwenye jipu hilo, kisha akapona hatua kwa hatua.+
8 Hezekia alikuwa amemuuliza hivi Isaya: “Ni ishara gani+ itakayonionyesha kwamba Yehova ataniponya na kwamba nitapanda kwenda katika nyumba ya Yehova siku ya tatu?” 9 Isaya akajibu: “Hii ndiyo ishara kutoka kwa Yehova itakayokuonyesha kwamba Yehova atatimiza neno alilosema: Je, unataka kivuli kilicho kwenye ngazi* kiende mbele hatua kumi au kirudi nyuma hatua kumi?”+ 10 Hezekia akasema: “Ni rahisi kivuli kwenda mbele hatua kumi lakini si rahisi kirudi nyuma hatua kumi.” 11 Kwa hiyo nabii Isaya akamwomba Yehova, Naye akafanya kivuli kilichokuwa kwenye ngazi ya Ahazi kirudi nyuma hatua kumi na tayari kilikuwa kimeshuka ngazi.+
12 Wakati huo mfalme wa Babiloni, Berodak-baladani mwana wa Baladani, akamtumia Hezekia barua na zawadi, kwa maana alisikia kwamba Hezekia alikuwa mgonjwa.+ 13 Hezekia akawakaribisha* na kuwaonyesha nyumba yake yote yenye hazina+—fedha, dhahabu, mafuta ya zeri na mafuta mengine yenye thamani, ghala lake la silaha, na kila kitu kilichokuwa katika hazina zake. Hakuna kitu chochote ambacho Hezekia hakuwaonyesha katika nyumba yake mwenyewe* na katika milki yake yote.
14 Kisha nabii Isaya akaenda kwa Mfalme Hezekia na kumuuliza: “Watu hawa walisema nini, nao walitoka wapi?” Hezekia akajibu: “Walitoka katika nchi ya mbali, kutoka Babiloni.”+ 15 Kisha akauliza: “Waliona nini katika nyumba yako?”* Hezekia akajibu: “Waliona kila kitu katika nyumba yangu.* Hakuna chochote ambacho sikuwaonyesha katika hazina zangu.”
16 Sasa Isaya akamwambia Hezekia: “Sikia neno la Yehova,+ 17 ‘Tazama! Siku zinakuja, na vitu vyote vilivyo katika nyumba yako* na vitu vyote ambavyo mababu zako wamehifadhi mpaka leo hii vitapelekwa Babiloni.+ Hakuna chochote kitakachobaki,” asema Yehova. 18 ‘Na baadhi ya wana wako mwenyewe utakaowazaa watachukuliwa+ na kuwa maofisa wa makao ya mfalme katika jumba la mfalme wa Babiloni.’”+
19 Ndipo Hezekia akamwambia Isaya: “Neno la Yehova ambalo umesema ni jema.”+ Kisha akasema: “Ni jema ikiwa kutakuwa na amani na utulivu* wakati wa maisha yangu.”*+
20 Na mambo mengine katika historia ya Hezekia, ukuu wake wote na jinsi alivyotengeneza kile kidimbwi+ na ule mfereji na kuleta maji jijini,+ je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 21 Kisha Hezekia akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake;+ na Manase mwanawe+ akawa mfalme baada yake.+
21 Manase+ alikuwa na umri wa miaka 12 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 55 huko Yerusalemu.+ Mama yake aliitwa Hefziba. 2 Manase alitenda maovu machoni pa Yehova, akafuata mazoea yenye kuchukiza ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyafukuza kutoka mbele ya Waisraeli.+ 3 Alijenga upya mahali pa juu ambapo Hezekia baba yake alikuwa amebomoa,+ akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali na kutengeneza mti mtakatifu,*+ kama alivyofanya Ahabu mfalme wa Israeli.+ Naye akaliinamia jeshi lote la mbinguni na kuliabudu.+ 4 Alijenga pia madhabahu katika nyumba ya Yehova,+ ambayo Yehova alikuwa amesema hivi kuihusu: “Nitaweka jina langu Yerusalemu.”+ 5 Naye alijenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni+ katika nyua mbili za nyumba ya Yehova.+ 6 Naye alimteketeza* motoni mwana wake mwenyewe; alifanya uchawi, alitafuta ishara za ubashiri,+ na kuwaweka rasmi watu wanaowasiliana na roho na wabashiri.+ Alitenda kwa kiwango kikubwa sana mambo maovu machoni pa Yehova, na kumkasirisha.
7 Akachukua sanamu ya kuchongwa ya mti mtakatifu*+ aliyokuwa ametengeneza na kuiweka ndani ya nyumba ambayo Yehova alikuwa amemwambia hivi Daudi na Sulemani mwanawe kuihusu: “Nitaweka jina langu milele katika nyumba hii na katika jiji la Yerusalemu, ambalo nimelichagua kati ya makabila yote ya Israeli.+ 8 Nami sitaifanya tena miguu ya Waisraeli itangetange kutoka katika nchi niliyowapa mababu zao+ ikiwa watashika kwa uangalifu mambo yote niliyowaamuru,+ Sheria yote ambayo Musa mtumishi wangu aliwaagiza wafuate.” 9 Lakini hawakutii, na Manase aliendelea kuwapotosha, akasababisha watende uovu mkubwa zaidi kuliko uliofanywa na mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyaangamiza kutoka mbele ya Waisraeli.+
10 Yehova aliendelea kusema hivi kupitia watumishi wake manabii:+ 11 “Manase mfalme wa Yuda amefanya mambo haya yote yenye kuchukiza; ametenda mambo maovu zaidi kuliko Waamori wote+ waliomtangulia,+ naye amesababisha watu wa Yuda watende dhambi kwa sanamu zake zenye kuchukiza.* 12 Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Tazama, ninaleta msiba mkubwa sana Yerusalemu+ na Yuda hivi kwamba masikio yote mawili ya yeyote atakayesikia habari zake yatawasha.+ 13 Nami nitanyoosha kamba ya kupimia juu ya Yerusalemu,+ kamba iliyotumika kupima Samaria+ na kutumia timazi iliyotumiwa kupima nyumba ya Ahabu,+ nami nitalifuta kabisa Yerusalemu liwe safi kama mtu anavyofuta bakuli liwe safi, akilifuta na kulipindua.+ 14 Nitawaacha watu waliobaki wa urithi wangu+ na kuwatia mikononi mwa maadui wao, nao wataporwa na kuchukuliwa nyara na maadui wao wote,+ 15 kwa sababu walitenda maovu machoni pangu nao waliendelea kunikasirisha tangu siku ambayo mababu zao walitoka Misri mpaka leo hii.’”+
16 Manase pia alimwaga damu nyingi sana isiyo na hatia mpaka alipojaza Yerusalemu damu hiyo kutoka mwisho mmoja hadi mwingine,+ mbali na dhambi yake aliyosababisha Yuda kutenda kwa kufanya maovu machoni pa Yehova. 17 Na mambo mengine katika historia ya Manase na yote aliyofanya na dhambi alizotenda, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 18 Kisha Manase akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake katika bustani ya nyumba yake, katika bustani ya Uza;+ na Amoni mwanawe akawa mfalme baada yake.
19 Amoni+ alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka miwili huko Yerusalemu.+ Mama yake aliitwa Meshulemethi binti ya Haruzi kutoka Yotba. 20 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, kama alivyofanya Manase baba yake.+ 21 Aliendelea kutembea katika njia zote ambazo baba yake alitembea, akaendelea kuziabudu na kuziinamia sanamu zenye kuchukiza ambazo baba yake aliabudu.+ 22 Kwa hiyo akamwacha Yehova Mungu wa mababu zake, naye hakutembea katika njia ya Yehova.+ 23 Hatimaye watumishi wa Amoni wakapanga njama dhidi yake na kumuua mfalme Amoni ndani ya nyumba yake mwenyewe. 24 Lakini watu wa nchi hiyo wakawaua wale wote waliopanga njama dhidi ya Mfalme Amoni, nao wakamweka Yosia mwanawe kuwa mfalme baada yake.+ 25 Na mambo mengine katika historia ya Amoni, mambo aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 26 Kwa hiyo wakamzika katika kaburi lake katika bustani ya Uza,+ na Yosia mwanawe+ akawa mfalme baada yake.
22 Yosia+ alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 31 huko Yerusalemu.+ Mama yake aliitwa Yedida binti ya Adaya kutoka Boskathi.+ 2 Alitenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova na kutembea katika njia zote za Daudi babu yake,+ naye hakugeuka na kwenda kulia au kushoto.
3 Katika mwaka wa 18 wa Mfalme Yosia, mfalme huyo alimtuma mwandishi Shafani, mwana wa Azalia mwana wa Meshulamu, kwenye nyumba ya Yehova,+ akisema: 4 “Panda uende kwa kuhani mkuu Hilkia+ umwambie akusanye pesa zote zinazoletwa katika nyumba ya Yehova+ ambazo walinzi wa malango wanakusanya kutoka kwa watu.+ 5 Waagize wawape wale waliowekwa kusimamia kazi katika nyumba ya Yehova, ili nao wawape wafanyakazi walio katika nyumba ya Yehova wanaopaswa kurekebisha sehemu zilizoharibika za* nyumba hiyo,+ 6 yaani, wawape mafundi, wajenzi, na waashi, ambao watazitumia kununua mbao na mawe yaliyochongwa ili kurekebisha nyumba hiyo.+ 7 Lakini hawapaswi kudaiwa hesabu yoyote ya matumizi ya pesa wanazopewa, kwa sababu ni waaminifu.”+
8 Baadaye kuhani mkuu Hilkia akamwambia mwandishi Shafani:+ “Nimepata kitabu cha Sheria+ katika nyumba ya Yehova.” Basi Hilkia akampa Shafani kitabu hicho, naye akaanza kukisoma.+ 9 Kisha mwandishi Shafani akaenda kwa mfalme na kumwambia: “Watumishi wako wamekusanya* pesa zilizopatikana katika nyumba hiyo, nao wamewapa wale wanaosimamia kazi katika nyumba ya Yehova.”+ 10 Pia, mwandishi Shafani akamwambia mfalme: “Kuna kitabu+ ambacho kuhani Hilkia amenipa.” Kisha Shafani akaanza kukisoma mbele ya mfalme.
11 Mara tu mfalme aliposikia maneno ya kitabu hicho cha Sheria, akayararua mavazi yake.+ 12 Halafu mfalme akamwagiza hivi kuhani Hilkia, Ahikamu+ mwana wa Shafani, Akbori mwana wa Mikaya, mwandishi Shafani, na Asaya mtumishi wa mfalme: 13 “Nendeni mkatafute ushauri wa Yehova kwa niaba yangu, kwa niaba ya watu, na kwa niaba ya watu wote wa Yuda kuhusu maneno ya kitabu hiki ambacho kimepatikana; kwa maana ghadhabu ya Yehova iliyowaka dhidi yetu ni kali,+ kwa sababu mababu zetu hawakutii maneno ya kitabu hiki kwa kuyashika mambo yote yaliyoandikwa kutuhusu.”
14 Basi kuhani Hilkia, Ahikamu, Akbori, Shafani, na Asaya wakaenda kwa nabii wa kike anayeitwa Hulda.+ Alikuwa mke wa Shalumu mwana wa Tikva mwana wa Harhasi, mtunzaji wa chumba cha mavazi, naye alikuwa akiishi katika Wilaya ya Pili ya Yerusalemu; wakazungumza naye huko.+ 15 Hulda akawaambia, “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Mwambieni hivi mtu aliyewatuma kwangu: 16 “Yehova anasema, ‘Nitaleta msiba mahali hapa na kwa wakaaji wake, maneno yote ya kitabu ambacho mfalme wa Yuda amesoma.+ 17 Kwa sababu wameniacha na wanaifukizia miungu mingine+ moshi wa dhabihu ili kunikasirisha kwa kazi zote za mikono yao,+ ghadhabu yangu itawaka dhidi ya mahali hapa nayo haitazimwa.’”+ 18 Lakini mwambieni hivi mfalme wa Yuda aliyewatuma kutafuta ushauri wa Yehova: “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kuhusu maneno ambayo umesikia, 19 kwa sababu moyo wako ulikuwa msikivu,* nawe ukajinyenyekeza+ mbele za Yehova uliposikia mambo niliyosema dhidi ya mahali hapa na wakaaji wake—kwamba watakuwa kitu cha kutisha na laana—nawe ukayararua mavazi yako+ na kulia mbele zangu, mimi pia nimekusikia, asema Yehova. 20 Ndiyo sababu nitakuzika pamoja na mababu zako,* nawe utalazwa kwa amani katika kaburi lako, na macho yako hayataona msiba wote nitakaoleta mahali hapa.’”’” Kisha wakampelekea mfalme jibu hilo.
23 Basi mfalme akatuma ujumbe, na wazee wote wa Yuda na Yerusalemu wakakusanywa.+ 2 Baada ya hayo mfalme akapanda kwenda katika nyumba ya Yehova pamoja na wanaume wote wa Yuda, wakaaji wote wa Yerusalemu, makuhani, na manabii—watu wote, kuanzia mdogo mpaka mkubwa. Akasoma, watu wote wakisikia, maneno yote ya kitabu+ cha agano+ kilichokuwa kimepatikana katika nyumba ya Yehova.+ 3 Mfalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano* mbele za Yehova,+ kwamba atamfuata Yehova na kushika amri zake, vikumbusho vyake, na sheria zake kwa moyo wake wote na kwa nafsi* yake yote kwa kutekeleza maneno ya agano hilo yaliyoandikwa katika kitabu hicho. Watu wote wakakubali agano hilo.+
4 Halafu mfalme akamwagiza kuhani mkuu Hilkia,+ makuhani wa daraja la pili, na walinzi wa milango waondoe kutoka katika hekalu la Yehova vyombo vyote vilivyotengenezwa kwa ajili ya Baali, kwa ajili ya mti mtakatifu,*+ na kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni. Kisha akaviteketeza nje ya Yerusalemu kwenye matuta ya Kidroni, akapeleka majivu yake Betheli.+ 5 Basi akawaondoa kabisa makuhani wa miungu ya kigeni, waliochaguliwa na wafalme wa Yuda kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu katika majiji ya Yuda na maeneo yanayozunguka Yerusalemu, na pia wale waliofukiza moshi wa dhabihu kwa Baali, kwa jua, kwa mwezi, kwa makundi ya nyota za unajimu, na kwa jeshi lote la mbinguni.+ 6 Akauondoa mti mtakatifu*+ katika nyumba ya Yehova na kuupeleka nje ya Yerusalemu, katika Bonde la Kidroni, akauteketeza+ katika Bonde la Kidroni, akausaga mpaka ukawa mavumbi na kuyatawanya mavumbi hayo juu ya makaburi ya watu wa kawaida.+ 7 Akabomoa pia nyumba za wanaume makahaba wa hekaluni+ zilizokuwa katika nyumba ya Yehova, mahali ambapo wanawake walikuwa wakifuma mahema ya ibada ya mti mtakatifu.*
8 Kisha akawaondoa makuhani wote katika majiji ya Yuda, naye akafanya mahali pa juu ambapo makuhani walifukizia moshi wa dhabihu pasifae kwa ibada, kuanzia Geba+ mpaka Beer-sheba.+ Alibomoa pia mahali pa juu palipokuwa kwenye malango yaliyokuwa katika njia ya kuingia kwenye lango la Yoshua mkuu wa jiji, malango yaliyokuwa upande wa kushoto mtu anapoingia katika lango la jiji. 9 Makuhani wa mahali pa juu hawakuhudumu kwenye madhabahu ya Yehova kule Yerusalemu,+ lakini walikula mikate isiyo na chachu pamoja na ndugu zao. 10 Pia alipafanya Tofethi,+ palipokuwa katika Bonde la Wana wa Hinomu*+ pasifae kwa ibada, ili mtu yeyote asimteketeze* motoni mwana wake au binti yake kwa ajili ya Moleki.+ 11 Pia farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu* kwa jua aliwazuia wasiingie katika nyumba ya Yehova kupitia chumba* cha Nathan-meleki ofisa wa makao ya mfalme, chumba kilichokuwa barazani; naye akayateketeza motoni magari yaliyowekwa wakfu kwa jua.+ 12 Mfalme alibomoa pia madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walijenga kwenye paa+ la chumba cha juu cha Ahazi, na pia madhabahu ambazo Manase alijenga katika nyua mbili za nyumba ya Yehova.+ Alizivunjavunja na kutawanya mavumbi yake katika Bonde la Kidroni. 13 Na mahali pa juu palipokuwa mbele ya Yerusalemu upande wa kusini* wa Mlima wa Uharibifu,* mahali ambapo Sulemani mfalme wa Israeli alijenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu wa kike mwenye kuchukiza wa Wasidoni; kwa ajili ya Kemoshi mungu mwenye kuchukiza wa Moabu; na kwa ajili ya Milkomu+ mungu mwenye kuchukiza wa Waamoni,+ mfalme alipafanya pasifae kwa ibada. 14 Naye akavunjavunja nguzo takatifu, akaikata miti mitakatifu*+ na kujaza mahali pake mifupa ya binadamu. 15 Alibomoa pia madhabahu iliyokuwa Betheli, mahali pa juu ambapo Yeroboamu mwana wa Nebati alijenga na ambapo palisababisha Waisraeli watende dhambi.+ Baada ya kuibomoa madhabahu hiyo na mahali pa juu, aliteketeza mahali hapo pa juu, akapasagasaga pakawa mavumbi, na kuuteketeza mti mtakatifu.*+
16 Yosia alipogeuka na kuona makaburi yaliyokuwa mlimani, aliagiza mifupa itolewe katika makaburi hayo na kuteketezwa kwenye madhabahu, akaifanya madhabahu hiyo isifae kwa ibada, kulingana na neno la Yehova lililokuwa limesemwa na mtu wa Mungu wa kweli aliyetabiri kwamba mambo hayo yangetukia.+ 17 Kisha akauliza: “Lile jiwe la kaburi ninaloona pale ni la nani?” Ndipo watu wa jiji hilo wakamjibu: “Ni kaburi la mtu wa Mungu wa kweli kutoka Yuda+ aliyetabiri mambo haya uliyoitendea madhabahu ya Betheli.” 18 Kwa hiyo akasema: “Acheni apumzike. Mtu yeyote asiiguse mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria.+
19 Yosia pia aliondoa nyumba zote za ibada zilizokuwa mahali pa juu katika majiji ya Samaria,+ ambazo wafalme wa Israeli walijenga na kumkasirisha Mungu, akazitendea kama alivyozitendea zile zilizokuwa Betheli.+ 20 Basi makuhani wote wa mahali pa juu waliokuwa mahali hapo akawatoa dhabihu juu ya madhabahu hizo, naye akateketeza mifupa ya wanadamu juu yake.+ Kisha akarudi Yerusalemu.
21 Kisha mfalme akawaamuru hivi watu wote: “Fanyeni Pasaka+ ya Yehova Mungu wenu kama ilivyoandikwa katika kitabu hiki cha agano.”+ 22 Pasaka kama hiyo haikuwa imewahi kufanywa tangu siku ambazo waamuzi walikuwa wakiongoza Israeli wala sikuzote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.+ 23 Lakini katika mwaka wa 18 wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hiyo ya Yehova ilifanywa Yerusalemu.
24 Yosia pia aliwaondoa kabisa watu wote waliowasiliana na roho, wabashiri,+ sanamu za terafimu,*+ sanamu zenye kuchukiza,* na vitu vyote vyenye kuchukiza vilivyokuwa katika nchi ya Yuda na Yerusalemu, ili atekeleze maneno ya Sheria+ yaliyoandikwa katika kitabu ambacho kuhani Hilkia alipata katika nyumba ya Yehova.+ 25 Kabla ya Yosia hakukuwa na mfalme yeyote aliyekuwa kama yeye, ambaye alimrudia Yehova kwa moyo wake wote na kwa nafsi yake yote+ na kwa nguvu zake zote, kulingana na Sheria yote ya Musa, na baada yake hakutokea yeyote aliyekuwa kama yeye.
26 Hata hivyo, Yehova hakuacha hasira yake kali iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya mambo yote yenye kuchukiza ambayo Manase alifanya na kumkasirisha Mungu.+ 27 Yehova akasema: “Nitaliondoa Yuda pia mbele za macho yangu,+ kama nilivyoliondoa Israeli;+ nami nitalikataa jiji hili nililochagua, Yerusalemu, na nyumba ambayo nilisema hivi kuihusu: ‘Jina langu litaendelea kukaa humo.’”+
28 Na mambo mengine katika historia ya Yosia, mambo yote aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? 29 Katika siku zake Farao Neko mfalme wa Misri alikuja kukutana na mfalme wa Ashuru karibu na Mto Efrati, kisha Mfalme Yosia akaenda kukabiliana naye; lakini Neko alipomwona, alimuua huko Megido.+ 30 Basi watumishi wake wakasafirisha maiti yake katika gari la vita kutoka Megido, wakamleta Yerusalemu na kumzika katika kaburi lake. Kisha watu nchini wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia wakamtia mafuta na kumweka kuwa mfalme baada ya baba yake.+
31 Yehoahazi+ alikuwa na umri wa miaka 23 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miezi mitatu huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 32 Yehoahazi alianza kutenda maovu machoni pa Yehova, alitenda mambo yote ambayo mababu zake walitenda.+ 33 Farao Neko+ alimtia gerezani kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi, ili kumzuia asitawale Yerusalemu, kisha akaitoza nchi faini ya talanta 100 za fedha* na talanta moja ya dhahabu.+ 34 Isitoshe, Farao Neko alimweka Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme baada ya Yosia baba yake na kubadili jina lake kuwa Yehoyakimu; lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri,+ ambako alifia hatimaye.+ 35 Yehoyakimu alimpa Farao fedha na dhahabu, lakini alilazimika kuitoza nchi kodi ili ampe Farao fedha alizodai. Alimtoza kila mtu nchini kiasi kilichokadiriwa cha fedha na dhahabu cha kumpa Farao Neko.
36 Yehoyakimu+ alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 11 huko Yerusalemu.+ Mama yake aliitwa Zebida binti ya Pedaya kutoka Ruma. 37 Yehoyakimu aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova,+ alitenda mambo yote ambayo mababu zake walitenda.+
24 Katika siku za utawala wa Yehoyakimu, Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni alikuja kumshambulia, Yehoyakimu akawa mtumishi wake kwa miaka mitatu. Hata hivyo, alimgeuka na kumwasi. 2 Kisha Yehova akaanza kutuma makundi ya wavamizi ya Wakaldayo,+ Wasiria, Wamoabu, na Waamoni yaende kumshambulia. Aliendelea kutuma makundi hayo yawavamie watu wa Yuda ili kuwaangamiza, kulingana na neno la Yehova+ alilosema kupitia watumishi wake manabii. 3 Hakika watu wa Yuda walipatwa na mambo hayo kwa agizo la Yehova, ili kuwaondoa mbele za macho yake+ kwa sababu ya dhambi zote ambazo Manase alitenda,+ 4 na pia kwa sababu ya damu isiyo na hatia aliyomwaga,+ kwa maana alijaza Yerusalemu damu isiyo na hatia na Yehova hakutaka kumsamehe.+
5 Na mambo mengine katika historia ya Yehoyakimu, mambo yote aliyotenda, je, hayajaandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda?+ 6 Kisha Yehoyakimu akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake;+ na Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 Mfalme wa Misri hakutoka tena kamwe katika nchi yake, kwa maana mfalme wa Babiloni alichukua vitu vyote vilivyokuwa vya mfalme wa Misri,+ kuanzia Korongo* la Misri+ mpaka Mto Efrati.+
8 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka 18 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miezi mitatu huko Yerusalemu.+ Mama yake aliitwa Nehushta binti ya Elnathani wa Yerusalemu. 9 Yehoyakini aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, alitenda mambo yote ambayo baba yake alitenda. 10 Wakati huo watumishi wa Mfalme Nebukadneza wa Babiloni walipanda kwenda kushambulia Yerusalemu, wakalizingira jiji hilo.+ 11 Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alikuja wakati watumishi wake walipokuwa wakilizingira jiji hilo.
12 Mfalme Yehoyakini wa Yuda akatoka nje kwenda kukutana na mfalme wa Babiloni,+ akiwa pamoja na mama yake, watumishi wake, wakuu wake, na maofisa wa makao yake;+ na mfalme wa Babiloni akamchukua mateka katika mwaka wa nane wa utawala wake.+ 13 Kisha akachukua hazina zote za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mfalme.*+ Alivikata vipandevipande vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Sulemani mfalme wa Israeli alitengeneza katika hekalu la Yehova.+ Hilo lilitendeka kama Yehova alivyokuwa ametabiri. 14 Akawapeleka uhamishoni watu wote wa Yerusalemu, wakuu wote,+ mashujaa wote hodari, na kila fundi na mfua chuma*+—aliwapeleka uhamishoni watu 10,000. Hakuna yeyote aliyebaki isipokuwa watu maskini kabisa nchini.+ 15 Basi akampeleka Yehoyakini+ uhamishoni Babiloni;+ alimpeleka pia mama ya mfalme, wake za mfalme, maofisa wa makao yake, na viongozi wa nchi, akawapeleka uhamishoni Babiloni kutoka Yerusalemu. 16 Pia mfalme wa Babiloni aliwapeleka uhamishoni Babiloni mashujaa wote, 7,000, na vilevile mafundi na wahunzi* 1,000, wote walikuwa wanaume mashujaa waliozoezwa kupigana vita. 17 Mfalme wa Babiloni alimweka Matania, mjomba wa Yehoyakini,+ kuwa mfalme baada yake na kubadili jina lake kuwa Sedekia.+
18 Sedekia alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 11 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 19 Sedekia aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, alitenda mambo yote ambayo Yehoyakimu alitenda.+ 20 Mambo hayo yalitukia Yerusalemu na Yuda kwa sababu ya hasira ya Yehova, mpaka alipowatupa mbali kutoka mbele zake.+ Na Sedekia akamwasi mfalme wa Babiloni.+
25 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika mwezi wa kumi, siku ya kumi ya mwezi huo, Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni alikuja na jeshi lake lote kushambulia Yerusalemu.+ Akapiga kambi na kujenga ukuta kulizingira jiji hilo pande zote,+ 2 naye akalizingira jiji hilo mpaka mwaka wa 11 wa utawala wa Mfalme Sedekia. 3 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne njaa ilikuwa kali sana+ jijini, na watu waliokuwemo hawakuwa na chakula.+ 4 Sehemu ya ukuta wa jiji ilibomolewa,+ na wanajeshi wote wakakimbia wakati wa usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, wakati Wakaldayo walipokuwa wakilizingira jiji; naye mfalme akafuata njia inayoelekea Araba.+ 5 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia mfalme, nalo likamfikia katika jangwa tambarare la Yeriko, na wanajeshi wake wote wakatawanyika na kumwacha. 6 Kisha wakamkamata mfalme+ na kumpeleka mpaka kwa mfalme wa Babiloni kule Ribla, nao wakamhukumu. 7 Wakawachinja wana wa Sedekia huku akitazama; kisha Nebukadneza akampofusha macho Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba, na kumpeleka Babiloni.+
8 Katika mwezi wa tano, siku ya saba ya mwezi huo, yaani, mwaka wa 19 wa utawala wa Mfalme Nebukadneza wa Babiloni, Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi, mtumishi wa mfalme wa Babiloni, alikuja Yerusalemu.+ 9 Akateketeza kabisa nyumba ya Yehova,+ nyumba ya mfalme,*+ na nyumba zote Yerusalemu;+ aliteketeza pia nyumba ya kila mtu maarufu.+ 10 Na jeshi lote la Wakaldayo lililokuwa pamoja na mkuu wa walinzi lilibomoa kuta zilizozunguka Yerusalemu.+ 11 Nebuzaradani mkuu wa walinzi aliwapeleka uhamishoni watu wote waliobaki jijini, watu waliojisalimisha kwa mfalme wa Babiloni, na watu wengine.+ 12 Lakini mkuu wa walinzi aliwaacha baadhi ya watu maskini kabisa nchini ili watunze mashamba ya mizabibu na kufanya kazi za kulazimishwa.+ 13 Pia Wakaldayo walivunja vipandevipande nguzo za shaba+ za nyumba ya Yehova na magari+ na Bahari ya shaba,+ vitu vilivyokuwa katika nyumba ya Yehova, nao wakaipeleka shaba hiyo Babiloni.+ 14 Walichukua pia ndoo za kuondolea majivu, sepetu, mikasi ya kukatia tambi za taa, vikombe, na vyombo vyote vya shaba vilivyotumiwa katika utumishi wa hekaluni. 15 Mkuu wa walinzi alichukua vyetezo na mabakuli yaliyotengenezwa kwa dhahabu+ na fedha halisi.+ 16 Shaba yote iliyotumiwa kutengeneza zile nguzo mbili, ile Bahari, na yale magari ambayo Sulemani alitengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yehova, haingeweza kupimwa uzito.+ 17 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa mikono 18,*+ na kifuniko chake kilikuwa cha shaba; na urefu wa kifuniko hicho ulikuwa mikono mitatu, na wavu pamoja na makomamanga yote yaliyozunguka kifuniko yalitengenezwa kwa shaba.+ Nguzo ya pili pamoja na wavu wake ilifanana na ya kwanza.
18 Mkuu wa walinzi alimchukua pia kuhani mkuu Seraya,+ Sefania+ kuhani wa pili, na walinzi watatu wa milango.+ 19 Pia alimchukua kutoka jijini ofisa mmoja wa makao ya mfalme aliyekuwa msimamizi wa wanajeshi, watu watano waliopatikana jijini walioshirikiana kwa ukaribu na mfalme, na pia mwandishi wa mkuu wa jeshi, aliyewaandikisha watu jeshini, na wanaume 60 kutoka miongoni mwa watu wa kawaida waliokuwa bado jijini. 20 Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi aliwachukua na kuwapeleka kwa mfalme wa Babiloni kule Ribla.+ 21 Mfalme wa Babiloni aliwaua na kuwaangamiza huko Ribla katika nchi ya Hamathi.+ Hivyo watu wa Yuda wakaenda uhamishoni kutoka katika nchi yao.+
22 Mfalme Nebukadneza wa Babiloni akamchagua Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani+ awasimamie watu aliowaacha katika nchi ya Yuda.+ 23 Wakuu wote wa jeshi na wanajeshi wao waliposikia kwamba mfalme wa Babiloni amemchagua Gedalia, mara moja wakaenda kwa Gedalia huko Mispa. Wakuu hao ni Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofa, na Yaazania mwana wa Mmaakathi, pamoja na wanajeshi wao.+ 24 Gedalia akawaapia hivi pamoja na wanajeshi wao: “Msiogope kuwa watumishi wa Wakaldayo. Kaeni katika nchi hii na kumtumikia mfalme wa Babiloni, na mambo yatawaendea vyema.”+
25 Na katika mwezi wa saba, Ishmaeli+ mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa kifalme,* akaja na wanaume wengine kumi, nao wakampiga na kumuua Gedalia pamoja na Wayahudi na Wakaldayo waliokuwa pamoja naye huko Mispa.+ 26 Kisha watu wote, kuanzia mdogo mpaka mkubwa, pamoja na wakuu wa jeshi, wakaondoka na kwenda Misri,+ kwa sababu waliwaogopa Wakaldayo.+
27 Na katika mwaka wa 37 tangu Mfalme Yehoyakini+ wa Yuda alipopelekwa uhamishoni, katika mwezi wa 12, siku ya 27 ya mwezi huo, Mfalme Evil-merodaki wa Babiloni, katika mwaka alioanza kutawala, alimwachilia huru Mfalme Yehoyakini wa Yuda kutoka gerezani.+ 28 Alizungumza naye kwa fadhili na kukikweza kiti chake cha ufalme juu zaidi kuliko viti vya wafalme wengine waliokuwa pamoja naye Babiloni. 29 Basi Yehoyakini akavua mavazi yake ya gerezani, na sikuzote za maisha yake alikuwa akila kwenye meza ya mfalme. 30 Naye alipewa chakula kwa ukawaida kutoka kwa mfalme, siku baada ya siku, siku zote za maisha yake.
Maana yake “Mungu Wangu Ni Yehova.”
Au “nafsi yangu na nafsi ya watumishi hawa wako 50 iwe.”
Au “nafsi yangu iwe.”
Yaani, ndugu ya Ahazia.
Au “angani.”
Au “nafsi yako inavyoishi.”
Inaonekana maneno “wana wa manabii” yanarejelea shule ya kuwafundisha manabii au chama cha manabii.
Au “nafsi yako inavyoishi.”
Au “nafsi yako inavyoishi.”
Au “sehemu mbili za.”
Au “angani.”
Au “upepo wa.”
Au labda, “yanaharibu mimba.”
Au labda, “kuharibu mimba.”
Au “aliyekuwa mtumishi wa Eliya.”
Tnn., “Kuna nini kati yangu nawe?”
Tnn., “ambaye ninasimama mbele zake.”
Au “mwanamuziki.”
Au “korongo.”
Au “korongo.”
Au “wote waliojifunga mshipi.”
Au “mtungi wa mafuta wenye mdomo wa birika.”
Au “nafsi yake ina.”
Au “kama nafsi yako mwenyewe inavyoishi.”
Au “wokovu.”
Au “alikuwa na ugonjwa wa ngozi.”
Inawezekana ni Naamani.
Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Au “kujizamisha.”
Tnn., “kambi yake yote.”
Tnn., “baraka.”
Tnn., “ninasimama mbele zake.”
Au “hekalu la.”
Eneo fulani kule Samaria, inawezekana ni kilima au ngome.
Au “zaidi ya mara moja au mbili.”
Tnn., “lilikasirisha sana moyo wa mfalme.”
Au “Mhudumu.”
Tnn., “akaikusanya pamoja kambi yake yote.”
Kabi moja ilikuwa sawa na lita 1.22. Angalia Nyongeza B14.
Sea moja ilikuwa sawa na lita 7.33 (vibaba 6.66). Angalia Nyongeza B14.
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Au “masoko ya.”
Tnn., “kweli neno hilo linaweza kutimia?”
Au “nafsi zao.”
Tnn., “kweli neno hilo linaweza kutimia?”
Tnn., “binti ya.”
Au “mgonjwa.”
Tnn., “waliofia mikononi mwa Yezebeli.”
Tnn., “mtu yeyote anayekojoa ukutani.” Huu ni msemo wa Kiebrania wa kuwadharau wanaume.
Tnn., “mwana.”
Tnn., “makundi ya magari ya farasi.”
Tnn., “walezi wa Ahabu.”
Au “mnyoofu.”
Tnn., “nyumba.”
Au “Ninyi ni waadilifu.”
Tnn., “litakaloanguka ardhini.”
Au “akambariki.”
Tnn., “mnyoofu.”
Au “uone bidii yangu kwa ajili ya.”
Tnn., “Takaseni.”
Au “hekalu la.”
Au “mtalipia nafsi yake kwa nafsi yenu.”
Tnn., “wakimbiaji.”
Tnn., “kwenye jiji la,” labda ni jengo lililokuwa kama ngome.
Tnn., “kukata.”
Au “Korongo la Arnoni.”
Tnn., “mbegu yote ya ufalme.”
Tnn., “wakimbiaji.”
Au “agano.”
Au “jumba la.”
Tnn., “anapotoka nje na anapoingia ndani.”
Labda ni kitabu cha kukunjwa kilichokuwa na Sheria ya Mungu.
Au “jumba la.”
Au “hekalu la.”
Au “nafsi.”
Au “wale wanaowajua.”
Au “yenye nyufa.”
Au “kuziweka ndani ya mifuko.” Tnn., “kuzifunga.”
Tnn., “Hazaeli akauelekeza uso wake dhidi ya.”
Au “jumba la mfalme.”
Au “Beth-milo.”
Au “akautuliza uso wa Yehova.”
Yaani, kwa amani na usalama.
Tnn., “Aliendelea kutembea katika.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “Alitembea katika.”
Yaani, Yeroboamu wa Pili.
Au “wokovu.”
Au “wokovu.”
Au “Utaishinda.”
Tnn., “mwaka unapoingia,” inawezekana ni wakati wa masika.
Tnn., “kutoka kwenye uwepo wake.”
Au “tukutane uso kwa uso.”
Au “jumba lako la mfalme.”
Tnn., “katika hema lake.”
Karibu mita 178 (futi 584). Angalia Nyongeza B14.
Au “jumba la mfalme.”
Yaani, Yeroboamu wa Pili.
Maana yake “Yehova Amesaidia.” Anaitwa Uzia katika 2Fa 15:13; 2Nya 26:1-23; Isa 6:1; na Zek 14:5.
Yaani, Amazia baba yake.
Au “njia ya kuingia Hamathi.”
Yaani, Bahari ya Chumvi.
Yaani, Yeroboamu wa Pili.
Maana yake “Yehova Amesaidia.” Anaitwa Uzia katika 2Fa 15:13; 2Nya 26:1-23; Isa 6:1; na Zek 14:5.
Au “jumba la mfalme.”
Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Au “jumba la mfalme.”
Tnn., “alimpitisha.”
Au “watu wa Yuda.”
Au “jumba la mfalme.”
Maana yake “Yehova Huimarisha.”
Tnn., “Waliogopa.”
Yaani, kila mahali, penye watu wengi au wachache.
Angalia Kamusi.
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Tnn., “kufanya shingo zao kuwa ngumu kama shingo za.”
Tnn., “za kuyeyushwa.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “waliwapitisha.”
Au “wakabashiri.”
Tnn., “kujiuza.”
Au “hawakumwabudu.”
Au “hayajui desturi za dini.”
Au “kumwabudu.”
Au “miungu yake na kuiweka.”
Au “desturi za dini.”
Au “desturi za dini.”
Tnn., “anayemwogopa.”
Au “desturi za dini.”
Ufupisho wa jina Abiya.
Angalia Kamusi.
Au “akiitwa Nehushtani.”
Yaani, kila mahali, penye watu wengi au wachache.
Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Au “jumba la.”
Tnn., “alikata na kuondoa.”
Au “kamanda.”
Au “ofisa mkuu wa makao ya mfalme.”
Au “msimamizi mkuu wa vinywaji vya mfalme.”
Au “jumba la mfalme.”
Au “Kisiria.”
Tnn., “Fanyeni baraka pamoja nami na mtoke nje na kuja kwangu.”
Au “jumba la mfalme.”
Au “jumba la mfalme.”
Au “matusi.”
Tnn., “wamefika kwenye mlango wa tumbo la uzazi.”
Tnn., “ninatia roho fulani ndani yake.”
Au labda, “katikati ya.”
Au “Nitaikausha mifereji yote ya Nile ya.”
Tnn., “lilifanywa.”
Au “nimelitengeneza.”
Yaani, Hezekia.
Au “nafaka zilizoanguka na kuota zenyewe.”
Au “hekalu la.”
Tnn., “katika siku zako.”
Huenda ngazi hizo zilitumiwa kuonyesha wakati, kama saa ya kivuli inavyoonyesha wakati kwa kufuata mwendo wa jua.
Au “akawasikiliza.”
Au “jumba lake la kifalme.”
Au “jumba lako la mfalme?”
Au “jumba langu la mfalme.”
Au “jumba lako la mfalme.”
Au “ukweli.”
Tnn., “katika siku zangu.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “alimpitisha.”
Angalia Kamusi.
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Au “kurekebisha nyufa zilizo katika.”
Tnn., “wamemimina.”
Tnn., “laini.”
Tnn., “nitakukusanya kwa watu wako.” Huu ni msemo wa kishairi unaorejelea kifo.
Au “kufanya upya lile agano.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi, “Gehena.”
Tnn., “asimpitishe.”
Tnn., “wamewatoa.”
Au “chumba cha kulia chakula.”
Tnn., “kulia.” Yaani, kusini, mtu anapotazama mashariki.
Yaani, Mlima wa Mizeituni, hasa upande wa kusini ulio mbali zaidi unaojulikana pia kama Mlima wa Kosa.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “miungu ya familia; sanamu.”
Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.
Talanta moja ilikuwa na uzito wa kilogramu 34.2. Angalia Nyongeza B14.
Angalia Kamusi.
Au “jumba la mfalme.”
Au labda, “mjenzi wa maboma ya ulinzi.”
Au labda, “wajenzi wa maboma ya ulinzi.”
Au “jumba la mfalme.”
Mkono mmoja ulilingana na sentimita 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “mbegu ya ufalme.”